Amini unashinda
Amini kuwa unashinda na wewe utashinda. Hata vita wanashinda wale wanaoamini katika ushindi. Kutokujiamini ni sawa na kushindwa tayari.
Amini kuwa unashinda na wewe utashinda. Hata vita wanashinda wale wanaoamini katika ushindi. Kutokujiamini ni sawa na kushindwa tayari.
Hakuna uwezo bila fursa. Huwezi kusema unauwezo wa kitu kama hauna fursa ya kukifanya.
Usimpe mtu ushauri ambao unahisi ataukubali sana, mpe mtu ushauri wenye manufaa kwake japo ni mgumu kuukubali.
Uwe mzuri kwenye kufanya kama ulivyo kwenye kufikiri. Matendo yako yafanane na maneno na maneno na matendo.
Ukitaka kufanya biashara kwa ufanisi; wakati wa kununua nunua ukiwa na mtazamo wa muuzaji kwa kufikiri kama wewe ungekua ndio unauza ungeuzaje, na Wakati wa kuuza uza ukiwa na mtazamo wa mnunuzi kwa kufikiri kama ungekua wewe ndiye mnunuzi ungenunuaje.
Maisha ya ujana ni kufanya mema au mabaya, kushinda au kushindwa. Uzee ni sherehe au majuto ya ujana.
Kujaribu kufanya jambo kubwa la kipekee ni kushinda hata kama halijafanikiwa.
Siri kuu ya kuishinda hasira yako ni kusubiri kabla ya kutenda unapokuwa na hasira.
Tunatakiwa tujenge uhodari na uwezo utakaotusaidia kutumia fursa zilizo wazi mbele yetu.
Jarbu Mambo mengi kadiri uwezavyo kwani kwa kujaribu ndivyo tunajua tunaweza au hatuwezi. Kamwe usiseme huwezi jambo kabla ya kujaribu.
Kushindwa jambo sio Makosa, bali kuacha kufanya jambo kabisa ni makosa makubwa.
Kama vile moto unavyozimwa na maji ndivyo vivyo hivyo hasira inamalizwa na maneno ya upole.
Kwenye dunia hii vitu haviwezi kusimama kama havijasimamishwa.
Biashara ya maisha ni kusonga mbele tuu. Maisha hayarudi nyuma wala hayafai kurudisha nyuma. Maisha yanasonga mbele.
Uwezo wa kuwa makini katika jambo bila kuyumbishwa na kitu chochote ni ishara kuu ya mtu mwenye akili na mwenye mafanikio.
Recent Comments