Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya

Mapishi ya Wali Wa Tambi Na Kuku Wa Sosi Ya Mtindi

Vipimo Vya Wali

Mchele – 3 vikombe

Tambi – 2 vikombe

Mafuta – ยผ kikombe

Chumvi

Vipimo Vya Kuku

Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande – 1 Kilo

Kitunguu maji kilichokatwa katwa – 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa – 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa – 1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Paprika – 1 kijiko cha supu

Masala ya kuku (tanduri au yoyote) – 1 kijiko cha supu

Ndimu – 2 vijiko vya supu

Mtindi (yoghurt) au malai (cream) – 1 kikombe

Mafuta – ยผ kikombe

Majani ya kotmiri (coriander) – ยฝ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali:

Osha Mchele, uroweke.
Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zigeuke rangi kuwa nyekundu.
Tia mchele endelea kukaanga kidogo.
Tia maji kiasi cha wali kupikika kama unavyopika pilau. Kiasi cha maji kinategemea aina ya mchele
Funika katika moto mdogo mdogo hadi uive ukiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu.
Tia mafuta katika karai, kisha tia kitunguu ukaange muda mdogo tu, usikiache kugeuka rangi.
Tia kuku na masala yake, endelea kukaanga, kisha tia mtindi au malai ufunike apikike na kuiva vizuri.
Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa ikiwa tayari kuliwa na wali wa tambi.

Mapishi ya Ndizi za nazi na utumbo

Mahitaji

Ndizi mshale 10
Utumbo wa ng’ombe 1/2 kilo
Nazi ya kopo 1
Nyanya 1
Kitunguu kikubwa 1
Tangawizi/ swaum 1 kijiko cha chakula
Olive oil kiasi
Limao 1
Chumvi
Curry powder 1 kijiko cha chai
Turmaric 1/2 kijiko cha chai
Coriander ya powder 1/2 kijiko cha chai
Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai
Pilipili kali nzima (usiipasue)

Matayarisho

Safisha utumbo kisha uweke ktk pressure cooker pamoja na chumvi kiasi, limao, tangawizi, swaum na maji kiasi kisha uchemshe kwa muda wa nusu saa. Baada ya hapo menya ndizi kisha zikate vipande vidogo kiasi ili ziwahi kuiva, kisha ktk sufuria ya kupikia tia vitunguu na nyanya kisha ndizi kwa juu yake na supu ya utumbo kiasi chumvi kidogo na mafuta kiasi kisha bandika jikoni na uchemshe mpaka ndizi zikaribie kuiva. Zikisha karibia kuiva tia utumbo na spice zote, pilipili nzima na tui la nazi kisha changanya vizuri na uache vichemke mpaka ndizi na tui la nazi vitakapoiva na rojo ibaki kiasi. Baada ya hapo Ndizi zako zitakuwa tayari kwa kuliwa.

Mapishi ya Ndizi na Nyama Ya Ngโ€™ombe

Mahitaji

Ndizi mbichi – 10-12

Nyama ngโ€™ombe – 1 kilo moja

Kitunguu maji – 2

Nyanya/tungule – 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 7

Tangawizi mbichi – 1 kipande

Ndimu – 2 kamua

Chumvi – kiasi

Mafuta – 3 vijiko vya supu

Tui la nazi – 3 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Saga kitunguu thomu na tangawiz mbichi.
Weka nyama katika sufuria tia kijiko kimoja cha kitunguu thomu na tangawizi, chumvi na ndimu kisha chemsha hadi iive.
Menya ndizi ukatekate
Weka mafuta katika sufuria tia kitunguu maji kilokatwakatwa ukaange kidogo tu kisha tia nyanya/tungule uendelea kukaanga.
Tia tangawizi na thomu ilobakia.
Tia ndizi, kaanga kidogo kisha tia supu ya nyama na nyama yake.
Ziache ndizi ziive zikiwa tayari tia tui la nazi zikiwa tayari.

Mapishi ya Biriani la nyama ya ng’ombe

Mahitaji

Nyama ya ng’ombe (beef 1/2 kilo)
Mchele (rice 1/2 kilo)
Vitunguu (onion 2)
Viazi (potato 2)
Vitunguu swaum (garlic 3 cloves)
Tangawizi (ginger)
Nyanya ya kopo (tomato 1/2 ya tin)
Curry powder (1/2 kijiko cha chai)
Binzari nyembamba ya kusaga (cumin 1/2 kijiko cha chai)
Binzari manjano (tarmaric 1/2 kijiko cha chai)
Mafuta (vegetable oil)
Chumvi (salt)
Rangi ya chakula (food colour)
Giligilani (fresh coriander)
Maziwa ya mgando (yogurt kikombe 1 cha chai)
Hiliki nzima (cardamon 3cloves)
Karafuu (clove 3)
Pilipili mtama nzima (black pepper 5)
Amdalasini (cinamon stick 1)

Matayarisho

Katakata nyama kisha ioshe na uiweke kwenye sufuria kisha tia kitunguu swaum, tangawizi, nyanya, curry powder, binzari zote, chumvi na maziwa ya mgando kisha bandika jikoni ichemke mpaka nyama iive na mchuzi ubakie kidogo.Baada ya hapo kaanga viazi na uweke pembeni, kisha kaanga vitunguu na mafuta mpaka viwe ya brown na kisha uvitie viazi vitunguu, na mafuta yake katika nyama. Koroga na uache uchemke kidogo kisha ipua na utie fresh coriander iliyokatwa na hapo mchuzi wako utakuwa tayari.
Baada ya hapo loweka mchele wako kwa muda wa dakika 10, kisha chemsha maji yatie chumvi, hiliki, karafuu, pilipili mtama na abdalasin na mafuta. Yakisha chemka tia mchele na uache uchemke mpaka ukauke maji yakisha kauka tia rangi ya chakula na uanze kugeuza ili ichanganyike na wali wote. Baada ya hapo ufunike na uache mpaka uive. Na baada ya hapo biriani litakuwa tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kupika Visheti

Viamba upishi

Unga 2 Vikombe

Samli au shortening ya mboga 2 Vijiko vya supu

Maziwa ยพ Kikombe

Iliki Kiasi

Mafuta ya kukarangia Kiasi

Shira

Sukari 1 Kikombe

Maji ยพ Kikombe

Vanila ยฝ Kijiko cha chai

Zafarani (ukipenda) Kiasi

Jinsi ya kupika na kuandaa

Katika kisufuria pasha moto maziwa na wakati huo huo chemsha Samli katika kisufuria kengine.
Tia unga katika bakuli na iliki, kisha mimina samli iliyochemka na huku unachanganya, kisha tia maziwa na uwendele kuchanganya vizuri isiwe na madonge, ikiwa maziwa haitoshi ongeza maji kidogo.
Kisha uwache unga ukae mahali pa joto kwa muda wa dakika 10 hivi.
Halafu fanya viduara vidogo vidogo, kisha finyiza kwenye greta yenye vishimo vidogo ili upate umbo kama kwenye picha.
Kisha karanga kwenye mafuta yaliyopata moto hadi vibadilike rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta.
Chemsha shira, ikiwa tayari mimina visheti na upepete na kuzichanganya zipate shira kote.
Weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa na kahawa.

Mawazo ya Chakula cha Mchana cha Dakika 20 kwa Siku zenye Shughuli Nyingi

Mawazo ya Chakula cha Mchana cha Dakika 20 kwa Siku zenye Shughuli Nyingi

Leo, nataka kuzungumzia kuhusu mawazo ya chakula cha mchana cha dakika 20 kwa siku zenye shughuli nyingi. Kama AckySHINE, ninaelewa jinsi wakati unavyoweza kuwa mdogo sana wakati wa mchana, hasa ikiwa una shughuli nyingi za kufanya. Lakini hii haimaanishi kuwa unapaswa kusahau kuhusu lishe bora na kupendeza kwenye chakula chako cha mchana. Hapa nitakupa mawazo kadhaa ya chakula cha mchana cha dakika 20 ambacho kitakufanya uhisi kuridhika na kuwa na nguvu kwa shughuli zako zote.

  1. ๐Ÿฅ— Saladi yenye afya: Andaa saladi yenye mboga mbalimbali kama vile letusi, nyanya, pilipili, karoti, na matango. Ongeza kuku wa kuchoma uliyebaki kutoka kwenye chakula cha jioni cha jana ili kuongeza protini. Pamba na vijiko vichache vya dressing ya saladi.

  2. ๐Ÿฒ Supu ya mboga: Pika supu ya mboga kwa kutumia mboga uliyopenda kama vile karoti, viazi, na kabichi. Ongeza viungo kama vile vitunguu, nyanya, na pilipili kwa ladha zaidi. Supu ya mboga ni njia nzuri ya kupata virutubisho vyote muhimu kwa haraka.

  3. ๐Ÿฑ Sushi ya kujitengenezea: Andaa sushi ya kujitengenezea kwa kutumia mchele uliopikwa, tangawizi, na mchuzi wa soya. Weka mboga ulizopenda kama vile karoti, matango, au avokado kwenye sushi yako. Hii ni chaguo nzuri kwa watu ambao wanapenda vyakula vya Kijapani.

  4. ๐Ÿฅช Sandwich ya kujitengenezea: Tengeneza sandwich yako mwenyewe kwa kutumia mkate kamili, nyama ya kukaanga, na mboga kama vile lettuce na nyanya. Unaweza pia kuongeza viungo vingine kama vile mayonnaise au mchuzi wa haradali kwa ladha zaidi.

  5. ๐Ÿ› Nafaka na mboga: Pika nafaka ya haraka kama vile quinoa au mchele mweupe. Ongeza mboga uliyopenda kama vile maharage ya kijani, karoti, au pilipili. Hii ni chaguo nzuri kwa watu ambao wanapenda chakula cha kitamu na cha kusitawisha.

  6. ๐Ÿ Pasta isiyo na nyama: Pika pasta isiyo na nyama kwa kutumia spageti au tagliatelle. Ongeza mboga kama vile broccoli, nyanya, na vitunguu kwa ladha zaidi. Pamba na mchuzi wa nyanya na viungo vingine kama vile bizari au pilipili kwa ladha zaidi.

  7. ๐ŸŒฎ Tacos za mboga: Tengeneza tacos za mboga kwa kutumia nyanya, pilipili, na vitunguu vilivyosonga. Ongeza mboga uliyopenda kama vile avokado au maharage. Pamba na mchuzi wa guacamole na juisi ya limao kwa ladha zaidi.

  8. ๐Ÿฅฆ Stir-fry ya mboga: Pika stir-fry ya mboga kwa kutumia mboga kama vile kabichi, karoti, na pilipili. Ongeza viungo kama vile vitunguu na tangawizi kwa ladha zaidi. Pamba na mchuzi wa soya na kitunguu saumu kwa ladha zaidi.

  9. ๐Ÿ  Mkate wa viazi: Pika viazi vitamu na utumie kama mkate badala ya mkate wa kawaida. Ongeza nyama ya kukaanga au mboga kama vile avocado na nyanya kwenye mkate wako wa viazi. Hii ni chaguo nzuri kwa watu ambao wanataka chakula cha mchana chenye afya na ladha ya kipekee.

  10. ๐Ÿฒ Chapati ya mboga: Pika chapati ya mboga kwa kutumia unga wa ngano, mboga iliyosagwa, na viungo kama vile pilipili na kitunguu. Tumia chapati hizi kama msingi wa sahani yako ya mboga kwa ladha na mlo kamili.

  11. ๐Ÿฅ• Mchanganyiko wa mboga: Kata mboga uliyopenda kama vile karoti, pilipili, na vitunguu katika vipande vidogo. Changanya na mchuzi wa soya au mchuzi mwingine wa ladha na pika kwa muda mfupi. Tumia mchanganyiko huu kama msingi wa sahani yako ya mboga.

  12. ๐ŸŒฏ Burrito ya mboga: Tengeneza burrito ya mboga kwa kutumia tortilla, mboga uliyosonga, na mchuzi wa nyanya. Ongeza viungo vingine kama vile pilipili na tangawizi kwa ladha zaidi. Hii ni chaguo nzuri kwa watu ambao wanapenda vyakula vya Mexiko.

  13. ๐Ÿฅฃ Mchuzi wa maharage: Pika mchuzi wa maharage kwa kutumia maharage ya kijani na viungo kama vile vitunguu na nyanya. Tumia mchuzi huu kama msingi wa chakula chako cha mchana kwa ladha na lishe.

  14. ๐Ÿฅฆ Saladi ya kijani: Tengeneza saladi ya kijani kwa kutumia mboga mbalimbali za majani kama vile spinachi, kale, na letusi. Ongeza viungo kama vile avokado, quinoa, na karanga kwa ladha zaidi. Pamba na mchuzi wa limao na mafuta ya zeituni kwa ladha zaidi.

  15. ๐Ÿฑ Bento ya mboga: Andaa bento ya mboga kwa kuweka mboga mbalimbali kama vile nyanya, karoti, na kabichi kwenye sehemu tofauti za sanduku la chakula. Ongeza protini kama tofu au tempeh kwa ladha zaidi. Pamba na mchuzi wa soya au mchuzi mwingine wa ladha kwa ladha zaidi.

Hizi ni baadhi tu ya mawazo ya chakula cha mchana cha dakika 20 kwa siku zenye shughuli nyingi. Kumbuka kuwa unaweza kubadilisha viungo au kuongeza viungo vyovyote unavyopenda ili kufanya chakula chako cha mchana kiwe cha kipekee na chenye ladha. Hakikisha unazingatia lishe na kula chakula kilichojaa virutubisho ili uwe na nguvu na kufanya vizuri siku nzima. Je, una mawazo yoyote mengine ya chakula cha mchana cha dakika 20? Nipatie maoni yako!

MAPISHI YA LADU

VIAMBAUPISHI

Unga – 6 vikombe

Samli – ยฝkikombe

Baking Powder – ยฝkijiko cha chai

Maziwa- 1 kikombe

Maji -Kisia kiasi kama unga bado mzito

VIAMBAUPISHI VYA SHIRA

Sukari – 5 vikombe

Maji – 2ย 1/2 vikombe

Vanilla – 2 vijiko vya chai

Rangi ya orange – 1 kijiko cha chai

Iliki ya unga – 1 Kijiko cha chai

MAANDALIZI

Changanya unga wa dengu, samli, baking powder pamoja na maziwa katika mashine ya keki (cake mixer).
Ukisha changanya angalia kama mchanganyiko wako umekua mwepesi kidogo kuliko wa keki, kama bado mzito basi ongeza maji kiasi.
Kisha weka mafuta kiasi kwenye karai,weka na samli kikombe kimoja, weka kwenye moto wa kiasi.
Mafuta yakisha pata moto, chukua kijiko kikubwa cha matundu chota mchanganyiko wako na kijiko cha kawaida tia kwenye kijiko cha matundu. Hakikisha kijiko cha matundu kiwe juu ya karai ili mchanganyiko wako uchuruzike ndani ya mafuta yalio pata moto.
Pika ndani ya mafuta mpaka iwive, ila usiache ikawa brown.
Toa mchanganyiko ulowiva tia ndani ya shira uliyo pika. Hakikisha shira iwe imepoa kabla ya kutia mchanganyiko huo.
Endelea kupika mchanganyiko wako mpaka uishe, kila ukitoa katika mafuta hakikisha unatia ndani ya shira.
Ukishamaliza wote kanda huo mchanganyiko ulokua ndani ya shira mpaka uone shira yote imekauka (yaani iwe imeingia ndani ya mchanganyiko).
Tupia zabibu kavu na lozi zilizo katwa, changanya na mkono.
Wacha mchanganyiko katika bakuli, funika na foil mpaka siku ya pili.
Siku ya pili chukua mchanganyiko kiasi katika mkono tengeneza mviringo (round).

MAANDALIZI YA SHIRA

Katika sufuria, tia sukari, maji, iliki, vanilla na rangi.
weka kwenye moto wacha ichemke mpaka itowe povu (bubbles) juu.
Kisha toa povu, wacha shira kwenye moto kama dakika 3.
Hakikisha shira yako iwe inanata kiasi kwenye vidole, lakini iwe nyepesi kidogo kuliko shira ya kaimati.

Mapishi ya Biriani

Mahitaji

Mchele (rice 1/2 kilo)
Nyama (beef 1/2 kilo)
Vitunguu (onion 2)
Kitunguu swaum (garlic 1 kijiko cha chai)
Tangawizi (ginger 1 kijiko cha chai)
Maziwa mgando (yogurt 1 kikombe cha chai)
Hiliki nzima (cardamon 6)
Amdalasini nzima (cinamon stick 2)
Karafuu nzima (cloves 6)
Pilipili mtama nzima (black pepper 8)
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Binzari manjano (turmaric 1/2 kijiko cha chai)
Binzari nyembamba nzima (cumin 1/4 kijiko cha chai)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)

Matayarisho

Kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia nyama na uikaange kwa muda wa dakika 10. baada ya hapo tia tangawizi, kitunguu swaum, hiliki(4), amdalasini (1), karafuu (4), pilipili mtama (5), Curry powder, binzari manjano, binzari nyembamba na chumvi. Kisha koroga. Baada ya hapo tia yogurt na uipike mpaka ikauke kisha tia maji kidogo, funika na upunguze moto na uache ichemke kwa muda wa nusu saa.Baada ya hapo nyama itakuwa imeiva na mchuzi kubakia kidogo.Kwahiyo itatakiwa kuiipua.
Loweka mchele kwa dakika 10. kisha chemsha maji mengi kidogo katika sufuria kubwa. baada ya hapo tia hiliki (2) amdalamsini (1) karafuu(2) pilipili mtama (3) chumvi na mafuta kiasi. acha ichemke kidogo kisha tia mchele.Hakikisha maji yameufunika mchele kabisa na uuache uchemke kwa muda wa dakika 8 tu (kwani hautakiwi kuiva kabisa) kisha uipue na uchuje maji yote katika chujio. baada ya hapo chukua sufuria ya kuokea (baking pot kama unayoiona kweye picha) Kisha weka wali nusu na uusambaze sawia kisha weka mchuzi nyama na mchuzi wake pia utandaze na umalizie kwa kuweka leya ya wali uliobakia. Baada ya hapo ufunike na uweke kwenye oven kwenye moto wa 200ยฐC kwa muda wa nusu saa.na baada ya hapo biriani litakuwa tayari kwa kuliwa.

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kuku Na Mboga Mchanganyiko

Vipimo

Mchele wa basmati/pishori – 4 vikombe vikubwa (mugs)

Kuku – 2

Vitnguu vya kijani (sprin onions) katakata – 5 miche

Maharage machanga (spring beans) katakata – kiasi kujaza mug moja

Pilipili boga la (capsicum) katakata – 1

Karoti katakata vipande virefu – 1

Kitunguu thomu (garlic) kuna (grate) – 1 kubwa

Tangawizi mbichi kuna (grate) – 1 kubwa

Sosi ya soya (soy sauce) – 2 vijiko vya supu

Kidonge cha supu – 1

Mafuta ya kupikia – ยผ kikombe cha chai

Chumvi – kiasi

Pilipili manga – 1 kijiko cha supu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha kuku vizuri, katakata vipande, weka katika sufuria, tia chumvi, pilipili manga, mfunike, umkaushe motoni huku ukimgeuza geuza.

Roweka mchele kisha uchemshe uive nusu. Chuja maji, tia siagi kidogo ili usigandane.

Weka karai ya kupika mboga (wok) au sufuria kisha tia mafuta yashite moto.

Tia kitunguu thomu, tangawizi, kaanga kidogo.

Tia mboga zote, ulizokatakata.

kaanga kidogo, kisha tia sosi ya soya na kidonge cha supu. Usizipike sana mboga mpaka zikalainika mno. Sababu zitaiva katika mchele

Changanya kuku na mboga kisha changanya vyote katika mchele, urudishe katika moto.

Funika upike hadi uive kamilifu.

Pakua kwenye sahani.

LISHE BORA KWA WATU WENYE AFYA NZURI

โ€ข Kula chakula bora kunamaanisha kula vyakula aina tofauti ya vyakula kila siku kama vile matunda, mboga, maziwa na aina ya vyakula vyenye asili ya nyama wa kufuga kama kuku, mbuzi, ngombe, samaki na na vyakula vya nafaka.

โ€ข Lishe bora linamaanisha pia kula chakula ambacho hakina mafuta mengi, sukari au chumvi nyingi

โ€ข Zingatia angalau vyakula vya nafaka kama vile mtama, mahindi, mchele, ngano, wimbi, ndegu, njegere. n.k

โ€ข Ni bora kula matunda mengi kama โ€˜maembe, ndizimbivu, papai, pera, chungwa, ubuyu, nanasi, pesheni, zambarauโ€ na mbogamboga kama vile โ€œmchicha, majani ya mboga, karoti, nyanya chungu, nyanya, mkunde, biringanyaโ€ mara tano kwa siku.

โ€ข Kama mboga na matunda hazipatikani ni bora kununua zile ambazo zimehifadhiwa tayari kwenye mikebe au zile ziko kwenye jokofu (friji).

โ€ข Punguza kula vyakula ambavyo vinapikwa kwa mafuta mengi na chumvi nyingi

โ€ข Lishe bora hukusaidia wewe na jamii yako kuishi vyema, kuwa na afya bora, kufanya kazi vizuri na kwa bidii, shuleni na hata kucheza.

Jinsi ya kupika Biryani ya mbogamboga

Biriani ni miongoni mwa vyakula ambavyo ni nadra sana kupikwa katika familia nyingi tofauti na vyakula vingine. Inawezekana ni kutokana na watu wengi kutoelewa namna ya kuoika chakula hiki kutokana na kuhitaji viungo vingi ambavyo huwapa usumbufu wapishi.
Kuna aina mbalimbali za upishi wa biriani ambapo mara nyingi hutofautiana kutokana na viungo vinavyotumika katika upishi.
Biriani la mbogamboga ni miongoni mwa aina hizo za upishi. Chakula hiki kinaweza kuliwa na kila mtu hususan wale wasiotumia nyama wala samaki.

Mahitaji:

ยฝ kg mchele wa basmati
Kitunguu maji kikubwa 1
Nyanya 1 kubwa
Karoti 1 kubwa
Njegere robo kikombe
Kiazi ulaya 1 kikubwa
Tangawizi za kusaga kijiko 1
Kitunguu swaumu cha kusaga kijiko 1
Karafuu kijiko 1
Majani ya kotimili fungu 1
Maziwa ya mtingi ยผ kikombe
Chumvi na pilipili kiasi
Unga wa dhani kijiko 1 cha mezani
Juisi ya limao kijiko 1 cha mezani
Mafua ยผ lita

Maandalizi:

Chemsha mchele na kisha weka pembeni
Osha mbogamboga zote isipokuwa vitunguu na nyanya
Changanya mtindi na tangawizi pamoja na kitunguu swaumu viache vikae kwa muda wa saa moja
Chukua sufuria weka mafuta na kisha kaanga vitunguu maji, weka nyanya, chumvi, kotimili na limao halafu weka karafuu na kanga hadi vichanganyike vizuri
Miminia mchanganyiko wa mtindi na baadaye weka pilipili na baadaye weka unga wa dhania
Chukua mchele uliochemshwa changanya na mchanganyiko huo
Palia moto juu ya chakula chako na acha kwa muda wa dakika 30
Baada ya hapo chakula chako cha biriani kitakuwa tayari kwa kuliwa

Mapishi ya Wali Mweupe Kwa Mchuzi Wa Kuku Wa Balti

Vipimo

Kuku 1 mkate vipande vipande

Vitunguu 3 katakata (chopped)

Nyanya 5 zikatekate (chopped)

Tangawizi mbichi ilokunwa au ilosagwa 1 kijiko cha kulia

Thomu (kitunguu saumu) kilosagwa kijiko 1 cha kulia

Bizari mchanganyiko (garam masala) kijiko 1 cha chai

Jira/bizari ya pilau (cummin powder) kijiko 1 cha chai

Dania/gilgilani ilosagwa (coriander powder) kijiko 1 cha chai

Mtindi/maziwa lala (yoghurt) vijiko vya kulia 4 mjazo au paketi moja ndogo.

Malai ya kupikia (cooking cream) kikombe 1

Kasuri methi (majani makavu ya uwatu/dried fenugreek leaves) 1 kijiko cha kulia

Mafuta ya kupikia ยฝ kikombe

Chumvi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha kuku vizuri mwache achuje maji.
Weka mafuta katika sufuria kaanga vitunguu mpaka vianze kugeuka rangi ya brown hafifu. Kisha tia tangawizi na thomu ukaange.
Tia kuku ukaange mpaka ageuke mweupe kisha tia nyanya endelea kukaanga ziwive.
Piga mtindi vizuri katika kibakuli uwe nyororo.
Epua sufuria weka kando kisha tia mtindi uchanganye vizuri pamoja na kuku.
Rudisha katika moto acha uchanganyike na kuku kidogo kisha mwagia malai ya kupikia (cooking cream)
Tia kasuri methi/majani makavu ya uwatu yaliyovurugwa. Acha katika moto dakika 1 tu.
Epua umimine katika chombo na nyunyizia ikiwa tayari kuliwa na wali mweupe.

Jinsi ya kupika vizuri Wali Wa Karoti Na Nyama

MAHITAJI YA WALI

Mchele – 3 Magi

Mafuta – 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu – 3

Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa – 1 kikubwa

Pilipli manga – 1/2 kijicho chai

Hiliki – 1/2 kijiko chai

Karafuu ya unga – 1/4 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga – 1/2 kijiko cha chai

Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji – 1 kijiko cha chai

Zabibu kavu (ukipenda) – 1/4 kikombe

Chumvi kiasi

KUPIKA WALI

Kwenye sufuria tia mafuta na kaanga karoti kidogo.
Tia vitunguu kisha tia bizari zote.
Tia maji kiasi (kutegemea aina ya mchele) na chumvi
Tia mchele upike uwive.
Karibu na kuwvia tia zabibu ukipenda.
Funika endelea kuupika hadi uwive.

MAHITAJI KWA NYAMA

Nyama – 2 Ratili (LB)

Chumvi – Kiasi

Mafuta – 1/4 kikombe

Kitunguu (kata virefu virefu) – 1 Kikubwa

Pilipili mboga kubwa – 2 ukipenda moja nyekundu moja kijani unazikata vipande virefu virefu.

Figili mwitu (celery) kata vipande virefu virefu- Miche miwili.

KUPIKA NYAMA

Chemsha nyama hadi iwive
Ikaange kwa mafuta hadi iwe nyekundu
Weka vitunguu, pilipili mboga na figili mwitu
Kaanga kidogo tu kama dakika moja.
Tayari kuliwa na wali.

Mapishi ya Maharage na spinach

Mahitaji

Maharage yaliyochemshwa kiasi
Spinach zilizokatwa kiasi
Vitunguu maji 2
Nyanya 1/2 kopo
Swaum/Tangawizi 1 kijiko cha chakula
Curry powder 1 kijiko cha chai
Olive oil
Chumvi

Matayarisho

Kaanga vitunguu vikianza kuwa vya brown tia tangawizi/swaum kisha nyanya. Pika mpaka nyanya ziive kisha tia curry powder na chumvi. Vipike kiasi kisha tia maharage na maji kidogo kisha funika na uache vichemke. Baada ya muda tia spinach vipike pamoja na maharage mpaka ziive kisha ziipue. Baada ya hapo mboga yako itakuwa tayari kwa kuseviwa.

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

๐ŸŒ™๐Ÿฅ˜

Usiku wa Juma ni wakati mzuri wa kujumuika na familia na marafiki, na ni wakati ambapo tunaweza kufurahia chakula kitamu na kitamu. Lakini kwa wengi wetu, maandalizi ya chakula cha jioni inaweza kuwa changamoto kubwa, haswa baada ya siku ndefu ya kazi. Ili kuhakikisha tunapata chakula cha afya na kitamu kila usiku wa Juma, ni muhimu kuwa na mpango mzuri wa vyakula vya kutayarishwa mapema. Kama AckySHINE, ningependa kukushauri juu ya vyakula vinavyofaa kwa usiku wa Juma ambavyo unaweza kuandaa mapema na kufurahia na familia yako.

  1. Mboga za Kuchemsha: ๐Ÿฅฆ๐Ÿ†

Mboga za kuchemsha ni chaguo bora la afya kwa usiku wa Juma. Unaweza kutayarisha mboga kama brokoli, bamia, au mchicha mapema na kuhifadhi kwenye jokofu. Wakati wa chakula cha jioni, unaweza kuwachemsha kwa muda mfupi au kuwachoma kidogo kwenye sufuria. Pamoja na mboga hizi, unaweza kuongeza viungo kama vile kitunguu saumu na pilipili kuongeza ladha.

  1. Maharagwe ya Kukaanga: ๐Ÿ›๐ŸŒถ๏ธ

Maharagwe ya kukaanga ni chakula kingine cha kitamu na chenye afya ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kuwachemsha maharagwe mapema na kisha kukaanga katika mafuta kidogo pamoja na viungo kama vile vitunguu na nyanya. Pamoja na chapati au wali, maharagwe ya kukaanga huunda mlo kamili na wenye lishe.

  1. Saladi ya Matunda: ๐Ÿ“๐Ÿ‰

Saladi ya matunda ni chakula kitamu na kinga ambacho kinaweza kuongeza ladha kwa usiku wa Juma. Unaweza kukata matunda kama vile tufaha, ndizi, na maembe mapema na kuhifadhi kwenye friji. Wakati wa chakula cha jioni, unaweza kuongeza limau au juisi ya machungwa kwa ladha zaidi. Saladi ya matunda ni kitamu, yenye afya, na rahisi kuandaa.

  1. Pilau ya Tofu: ๐Ÿš๐Ÿฅ•

Pilau ya tofu ni chakula kingine cha kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema na kufurahia na familia yako. Unaweza kuandaa pilau ya mchele na tofu, mboga kama karoti na bizari, na viungo kama vile vitunguu na tangawizi. Pamoja na saladi ya mboga, pilau ya tofu ni mlo kamili na wenye lishe.

  1. Wali wa Nazi: ๐Ÿš๐Ÿฅฅ

Wali wa nazi ni chakula rahisi na kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kupika mchele katika maziwa ya nazi na kuongeza viungo kama vile mdalasini na karafuu. Pamoja na curry ya mboga, wali wa nazi huunda mchanganyiko mzuri na wenye ladha.

  1. Chapati za Kusukuma: ๐Ÿฅ™๐Ÿ›

Chapati za kusukuma ni chakula kitamu na cha kuridhisha ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kupika mkate wa unga mapema na kuzihifadhi kwenye friji. Wakati wa chakula cha jioni, unaweza kuzitoa na kuzikaanga kidogo kwenye sufuria bila mafuta au mafuta kidogo. Pamoja na mboga za kuchemsha au maharagwe ya kukaanga, chapati za kusukuma ni chakula kamili na kitamu.

  1. Supu ya Nyanya: ๐Ÿ…๐Ÿฒ

Supu ya nyanya ni chakula rahisi na cha kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kuwachemsha nyanya na kuziponda kuwa supu laini. Pamoja na vitunguu, pilipili, na viungo vingine, supu ya nyanya ni chakula cha joto na kinachowasha moyo.

  1. Samaki wa Kukaanga: ๐ŸŸ๐Ÿฝ๏ธ

Samaki wa kukaanga ni chakula cha afya na kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kuvuta samaki mapema na kuhifadhi kwenye friji. Wakati wa chakula cha jioni, unaweza kuwakaanga na kuongeza viungo kama vile pilipili na chumvi. Pamoja na ugali au wali, samaki wa kukaanga huunda mlo kamili na wenye ladha.

  1. Kuku wa Kuchoma: ๐Ÿ—๐Ÿ”ฅ

Kuku wa kuchoma ni chakula kingine cha kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kuandaa kuku kwa kutumia viungo vya kuchoma kama vile tangawizi, vitunguu, pilipili, na mdalasini. Pamoja na mihogo ya kuchoma au viazi vya kuchoma, kuku wa kuchoma ni chakula chenye ladha na chenye lishe.

  1. Nyama ya Ng’ombe ya Kukaanga: ๐Ÿ„๐Ÿฝ๏ธ

Nyama ya ng’ombe ya kukaanga ni chakula cha kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kuikaanga nyama ya ng’ombe pamoja na viungo kama vile pilipili, tangawizi, na vitunguu. Pamoja na mchele wa mnazi au chapati, nyama ya ng’ombe ya kukaanga huunda mlo kamili na wenye ladha.

  1. Kachumbari: ๐Ÿฅ’๐Ÿ…

Kachumbari ni saladi rahisi na yenye ladha ambayo unaweza kuandaa mapema. Unaweza kukata nyanya, tango, vitunguu, na pilipili kisha kuchanganya na viungo kama vile chumvi, pilipili, na limau. Pamoja na chapati au viazi vya kuchoma, kachumbari huongeza ladha kwa chakula cha jioni.

  1. Mihogo ya Kuchoma: ๐Ÿ ๐Ÿ”ฅ

Mihogo ya kuchoma ni chakula rahisi na kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kukata mihogo kwa umbo la vipande na kuiweka kwenye tanuri moto. Pamoja na samaki wa kukaanga au kuku wa kuchoma, mihogo ya kuchoma ni chakula kamili na cha kuridhisha.

  1. Chapati za Mchuzi: ๐Ÿฅ™๐Ÿ›

Chapati za mchuzi ni chakula kingine cha kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kuandaa mkate wa unga mapema na kuoka kwenye oveni. Pamoja na mchuzi wa nyama au mboga, chapati za mchuzi huunda mchanganyiko mzuri na wenye ladha.

  1. Saladi ya Nyama ya Kusokotwa: ๐Ÿฅ—๐Ÿ–

Saladi ya nyama ya kusokotwa ni chakula kingine cha kitamu ambacho unaweza kuandaa mapema. Unaweza kupika nyama ya ng’ombe au kuku na kuiweka kwenye friji. Wakati wa chakula cha jioni, unaweza kukatakata nyama na kuichanganya na mboga kama karoti na pilipili. Pamoja na mkate wa unga au wali, saladi ya nyama ya kusokotwa ni chakula cha afya na cha kuridhisha.

  1. Keki ya Chokoleti: ๐Ÿฐ๐Ÿซ

Keki ya chokoleti ni chakula tamu ambacho unaweza kuandaa mapema kwa usiku wa Juma. Unaweza kuoka keki ya choko

Mapishi ya Pilau Ya Adesi Za Brown Karoti Na Mchicha Kwa Samaki Wa Salmon

Vipimo

Mchele vikombe 3

Karoti 1 ikune (grate)

Mchicha katakata kiasi

Adesi za brown

Kitunguu katakata (chopped)

Supu ya kitoweo chochote upendayo au vidonge vya supu 2

Garama masala (bizari mchanganyiko) kijiko 1 cha kulia

Samli ยผ kikombe

Chumvi kiasi

Vipimo Vya Samaki Wa Salmon

Samaki wa Salmon vipande 4 vikubwa

Tangawizi mbichi ilosagwa kijiko 1 cha kulia

Thomu (garlic/saumu) kijiko 1 cha kulia

Chumvi kiasi

Bizari ya mchuzi kijiko 1 cha kulia

Ndimu 1 kamua

Nyanya 2 kata slice kubwa kubwa

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Samaki wa Salmon

Changanya viungo vyote upake katika samaki.
Weka katika treya na panga slice za nyanya juu yake.
Oka (grill/choma) katika oven umgeuze samaki upande wa pili.
Akiwa tayari epua.

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali

Roweka mchele kiasi kutegemea aina ya mchele. Tumia basmati (pishori)
Roweka adesi kisha zichemshe katika maji ya kiasi. Chuja maji adesi na maji yatakayobakia tumia katika kupikia pilau hii.
Kaanga vitunguu katika samli iliyoshika moto kwenye sufuria ya kupikia.
Vikianza kugeuka rangi tia karoti, mchicha, adesi, bizari mchanganyiko kisha kaanga kidogo.
Tia mchele ukaange kidogo kisha tia supu au maji pamoja na kidonge cha supu.
Tia chumvi ukoroge funika upike kama pilau.
Epua upakue katika sahani utolee kwa samaki wa salmon

Jinsi ya kupika Pilau Ya Nyama Ya Ng’ombe Na Nyanya

Viambaupishi

Mchele (Basmati) 3 vikombe

Nyama ya ngoโ€™mbe 1 kg

Pilipili boga 1 kubwa

Nyanya 2 kubwa

Vitunguu maji 2 vikubwa

Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa 1 kijiko cha supu

Tangawizi 1 kijiko cha chai

Ndimu 1

Mafuta ya kupikia ยฝ kikombe

Mdalasini ยฝ kijiko cha chai

Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai

Pilipili manga ยฝ Kijiko cha chai

Hiliki ยฝ Kijiko cha chai

Jinsi ya kuandaa na kupika

Loweka mchele wako katika chombo

Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi

Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi

katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni

Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia

Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto

Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya

Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi

Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke

Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza

Funika na punguza moto na uache uive taratibu

Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.

Jinsi ya kupika Mkate

Mahitaji

Unga wa ngano ( self risen flour) kikombe 1 na 1/2
Hamira (yeast) 1 kijiko cha chai
Sukari (sugar) 1 kijiko cha chakula
Chumvi (salt) 1/2 kijiko cha chai
Siagi iliyoyeyushwa (melted butter) 1 kijiko cha chakula
Maji ya uvuguvugu ( warm water) kiasi

Matayarisho

Changanya vitu vyote katika bakuli kubwa kisha aanza kukanda mpaka upate donge laini.Baada ya hapo liweke hilo donge kwenye bakuli la plastic na weke katika sehemu yenye joto ili unga uumuke. Hakikisha unga unaumuka zaidi (yani unaji double size) unaweza kuchukua kama saa 1 na nusu hivi. Baada ya hapo ukande tena na uache uumuke tena kwa mara ya pili, Ukisha umuka pakaza butter katika baking tin (chombo cha kuokea) na upakaze mkate butter kwa juu,kisha uoke katika oven kwa muda wa dakika 30 (katika moto wa 200C) (hakikisha juu na chini unakuwa wa brown Na hapo mkate wako utakuwa tayari

Mapishi โ€“ Mayai Mchanganyiko, Tosti na Soseji

Karibu tena jikoni, leo tunaandaa vitafunwa kwa ajili ya kifungua kinywa asubuhi.

Mahitaji

Mayai 3
Soseji 2
Mkate slesi 2
Mafuta ya kupikia vijiko 2
Chumvi

Matayarisho

Piga piga mayai vizuri kwenye bakuli na weka chumvi kidogo kisha weka kikaango kwenye moto na mafuta kidogo.

Kikisha pata moto miminia mchanganyiko wa mayai na uanze kukorogo pale tu unapomiminia, endelea kukoroga hadi uone yanakuwa magumu na kuanza kuiva. Pika kwa kiwango unachopendelea na kusha epua na weka kwenye sahani.

Weka mafuta kijiko kimoja kwenye kikaango na kisha weka soseji zako na uzipike kiasi pande zote kisha epua na weka pembeni.

Weka slesi za mikate kwenye toster na zikiwa tayari unaweza weka siagi ili kuongeza ladha na mvuto.
Andaa mlo wako pamoja na juice, maziwa au chai.

Mapishi ya Boga La Nazi

Vipimo

Boga la kiasi – nusu yake

Tui zito la nazi 1 ยฝ gilasi

Sukari ยฝ kikombe

Hiliki ยฝ kijiko cha chai

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Menya boga kisha katakata vipande vya kiasi.
Weka katika sufuri tia maji kiasi ya kuchemshia na kuwiva bila ya kubakia maji mengi.
Changanya tui na sukari na hiliki kisha mimina juu ya boga wacha katika moto dakika chache tu bila ya kufunika.
Epua mimina katika chombo likiwa tayari.

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About