Mambo ya mke na mume haya, chezea mchepuko!?
Mume akamwambia mke wake:
“Funga macho yako tufanye maombi”
Akaanza kwa Kimombo:-
“… Lord I pray for Grace, I pray for Mercy, I pray 4 Joy, I pray 4 Love, I pray 4 Hope, I pray 4 GLORY, I pray 4 Faith, I pray 4….”
Mke akadakia, “Unadhani mimi sina ee” akaanza:-
I pray 4 Felix, I pray 4 Temu, I pray 4 Rweyemamu, I pray 4 Masawe, I pray 4 Benson, I pray 4 Onyango, I pray 4 Swai, I pray kwa wote niliowasahau!!
Chezea mchepuko…!!
Soma huyu mtoto anachosema sasa, Ndoto za watoto bwana! Kazi ipo!
Mwalimu aliingia darasani na kuwauliza wanafunzi juu ya ndoto zao za baadae.
MWAL: John we unataka ukiwa mkubwa uwe nani?
JOHN: Nataka niwe daktari wa moyo niwasaidie watanzania wanaougua magonjwa ya moyo.
MWAL: vizuri. Na wewe Rose unataka kuwa nani?
ROSE: Nataka kuwa rubani, niweze kusaidia watu wanapenda kusafiri kw anga.
MWAL: Safi sana Rose. Utakua utakua mfano kwa wasichana wenzio kuwa na bidii kwenye masomo ya sayansi.
MWAL: Na wewe Nehemiah ??
Nehemiah : mimi nataka kuwa tajiri mkubwa sana. Niwe na nyumba Tanzania, S.Africa, Marekani na Dubai. Niwe na gari 7 za kutembelea. Kila siku nabadilisha. Leo nikipanda hii, siirudii hadi week iishe. Nataka niwe namiliki viwanda, Makampuni, ndege binafsi na mashamba makubwa. Nataka niwe na nguvu serikalini ya kuamua nani awe Rais na nani asiwe……”
Akameza mate kisha akaendelea….
“Nataka kuwa na walinzi 20 wenye silaha nzito wakinizunguka, na watumishi wakininyenyekea. Nataka kuwa bilionea ninayeogopwa. Lakini pia nataka kuwa na mke mzuuuri sana ambaye nitakuwa natembea nae kila mahali.”
MWAL: ndoto nzuri sn lakini unahitaji bidii sana kutimiza. Haya na wewe Jenny tueleze unataka kuwa nani??
JENNY: Nataka kuwa mke wa Nehemiah .!!
SMS nzuri ya mapenzi ya kimahaba ya kutuma kwa mpenzi wako umpendaye
Fikra hutawala mtima wangu, Kwa madhila yalojaa duniani, Kwa muhali wa yanayojiri, Kwa machweo na mawio, Kwa totoro ama nuruni, Nao moyo hukosa ukamilifu, Kwa utashi wa zake hisia, Zinipazo sababu kuu, Ya upendo juu yako, Ya kukufanya daima uwe, Mawazoni mwangu. Mawazoni ama ndotoni, Daima wewe hutawala, Kila asubuhi niamkapo, Nao usiku nilalapo, U chakula changu akilini, Nalo tulizo langu moyoni, Daima huuwaza upekee, Wewe uliojaaliwa, Na hivyo naihisi furaha, Daima wewe uwapo, Mawazoni mwangu.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ujumbe wa kimahaba kwa mpenzi wako
Nitaenda mbali Zaidi ya maono yako
Safarini nitajenga hekalu la pendo letu
Nitapuliza filimbi kama ishara ya utambulisho wako
Na mwanzo wa sherehe ya ndoa yetu
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Meseji ya kumtumia mpenzi wako kumwambia kuwa yeye ndiye chaguo lako
Nafsi yangu inafurahia ya kwamba
wewe ndio chaguo langu, ubavu wangu
tabasamu usoni mwangu ndio siri ya
pendo lako kwangu
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
SMS ya kumtumia mpenzi wako kumwambia kuwa unamjali na kumpenda milele
Tambua kuwa nakujali
Furahia kwamba nitakuwa na wewe
Katika siku zote za maisha yangu
Nitakupenda bila kikomo milele
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ujumbe wa mapenzi kwa umpendaye kwa dhati
Nakupenda usiku na mchana Nakuwaza siku zote za maisha yangu
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Meseji nzuri ya kumtumia mpenzi umpendaye kwa moyo
Katika nyuso za dunia, na kati ya miamba ya jangwani, Kuna SAUTI! Neno la pendo lako liotapo karibu yangu. Ni zaidi ya roho iendayo safarini.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
SMS ya kuahidi kumpenda mpenzi wako milele
Niliumbwa kwa ajili yako, mbele yako nitakushika mkono, nikuonyesha sayari yangu, pendo langu la undani, na NITAKUHESHIMU milele mpenzi wangu.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
SMS ya kumwambia mpenzi wako kuwa bado unampenda na hujabadilika
“Japokuwa”
“Kuku” “Haogi” “Yai” “Lake” “Litabaki” “Kuwa” “Jeupe” “Tu” “Namaanisha”
“Kuwa”
“Hata” “Kama” “Ukiona”
“Nipo” “”KIMYA”” Muda”
“Mrefu” “”UPENDO”” “Wangu” “Kwako”
“””Bado”””
“Uko” Pale pale!!!!!
Usijali
“Tupo Pamoja” “Kwa” “Asilimia 100%”.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Mungu Anakuita Na Kukupa Nafasi Ya Kutubu Na Kumrudia Yeye Ili Akusamehe na Kukubariki
Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! Msifanye migumu mioyo yenu. Zab 95:7-8
Tunaalikwa kutubu na kumrudia Mungu kwa Mioyo yetu yote na kwa nia dhabiti. Mungu ni mwaminifu, atatusamehe dhambi zetu na kutufanya kuwa wapya.
Dawa ya dhambi ni kutubu na kusamehewa.
Kutubu sio kusema tuu “Ninatubu” au “Ninaomba msamaha”. Kutubu ni kuona uchungu kweli rohoni kwa dhambi tulizotenda, tukizikataa na kunuia kutokuzitenda tena.
12“Lakini hata sasa,”
nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
“Nirudieni kwa moyo wote,
kwa kufunga, kulia na kuomboleza.
13Msirarue mavazi yenu kuonesha huzuni
bali nirudieni kwa moyo wa toba.”
Mrudieni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu;
yeye amejaa neema na huruma;
hakasiriki upesi, ni mwingi wa fadhili;
daima yu tayari kuacha kuadhibu.
14Huenda Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atabadili nia
na kuwapeni baraka ya mazao,
mkamtolea sadaka za nafaka na kinywaji.
15Pigeni tarumbeta huko Siyoni!
Toeni amri watu wafunge;
itisheni mkutano wa kidini.
16Wakusanyeni watu wote,
wawekeni watu wakfu.
Waleteni wazee,
wakusanyeni watoto,
hata watoto wanyonyao.
Bwana arusi na bibi arusi
na watoke vyumbani mwao.
17Kati ya madhabahu na lango la hekalu,
makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu,
walie na kuomba wakisema:
“Wahurumie watu wako, ee Mwenyezi-Mungu.
Usiyaache mataifa mengine yatudharau
na kutudhihaki yakisema,
‘Yuko wapi basi Mungu wao?’” Yoeli 2:12-17
Uzuri wa Mungu ni kwamba anasamehe na kusahau, tunapotubu dhambi zetu Mungu anatufutia makosa yetu, anaponya majeraha au madhara yaliyoletwa na dhambi hiyo na kisha antubariki kwa Neema na Vipawa vya kusonga Mbele.
Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena dhambi zao.” Yeremia 31:34
Mungu anatambua kwamba Binadamu ni dhaifu na anaweza kuanguka dhambini ndio maana anatupa nafasi ya Kutubu na Kumrudia yeye.
13Afichaye makosa yake hatafanikiwa;
lakini anayeungama na kuyaacha atapata rehema. Methali 28:13
Mungu anazifahamu juhudi zetu katika kutafuta kutenda mema ndio maana anakubali toba ya kweli na anatupa matumaini ya kusonga mbele.
“Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”. Isaya 1:18
Biblia inatuambia kuwa anaheri yule atubuye na kusamehewa kosa lake kwa sababu hana hatia mbele ya Mungu.
1 Heri yake mtu aliyesamehewa kosa lake,
mtu ambaye dhambi yake imeondolewa kabisa.
2Heri mtu ambaye Mwenyezi-Mungu hamwekei hatia,
mtu ambaye hana hila moyoni mwake. Zaburi 32:1-2
Tunapaswa kukumbuka kuwa toba ya kweli ya kutupa msamamaha inaambatana na kuwasamehe wengine na kuondoa kinyongo kwa wengine waliotukosea. Yesu anatufundisha kuwa inatupasa tusamehe ili na sisi tusamehewe.
14“Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe nyinyi pia. 15Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe nyinyi makosa yenu. Mathayo 6:14-15
Tena, Mungu anatusamehe Makosa Yetu bila kujali tunakosea Mara nagpi na tunarudi kwake mara ngapi. Ndio maana Yesu alitufundisha kuwa tunapokosewa na wenzetu ni lazima tuwasamehe haijalishi wametukosea mara ngapi.
3Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe. 4Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema, ‘Nimetubu,’ lazima umsamehe.” Luka 17:3-4
Unapotubu na kuomba msamaha ni sharti uwasamehe pia wale waliokukosea ili na wewe usamehewe. Kusameheana na wenzetu ndio tabia ya Kimungu ambayo yatupasa kujifunza na kuiishi ili na sisi tuwe watoto wema wa Mungu.
12Nyinyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo, basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe nyinyi. Wakolosai 3:12-13
Tumuombe Mungu atujalie Moyo wa toba na kujirudi kwake Kila tunapokosea. Na tumuombe pia atupe nguvu na uwezo wa kuwasamehe wale wanaotukosea.
KUMBUKA: Unapotubu dhambi zako na kusamehewa ndipo inapokuwa rahisi kwa sala zako kujibiwa. Mungu ni rafiki ya waliosafi Moyoni, na ndio anaowasikiliza na kuwaonyesha nguvu na uwezo wake.
Nakualika kwa Sala ya Toba, uweze kurudi kwa Mungu. Sali kutoka moyoni, kwa kujua kuwa unapendwa na Mungu, Kwa Imani na Matumaini Kwake.
Sala ya Toba
Mungu wangu, Baba wa mbinguni, nakuja mbele zako nikiwa na moyo uliovunjika na toba ya kweli. Nakiri kuwa mimi ni mwenye dhambi, na nimekosa mbele zako kwa njia nyingi. Nimefanya mambo ambayo hayakupendeza, na nimeshindwa kutenda yale uliyoniagiza. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Kwa maana wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu” (Warumi 3:23).
Ee Bwana, naomba unisamehe dhambi zangu zote. Nimetenda dhambi kwa mawazo, kwa maneno, na kwa matendo. Ninatubu kwa dhati na kwa kweli kutoka moyoni mwangu. Naomba unioshe kwa damu ya Yesu Kristo, Mwanao mpendwa, ambaye alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu. Kama unavyosema katika Neno lako, “Lakini ikiwa tutatembea katika nuru kama Yeye alivyo katika nuru, tu ushirika sisi kwa sisi, na damu yake Yesu Kristo, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote” (1 Yohana 1:7).
Ninakiri kuwa mimi ni mnyonge bila wewe, na siwezi kufanya lolote bila msaada wako. Naomba unijaze na Roho Mtakatifu, aniongoze na kunipa nguvu ya kushinda majaribu na dhambi. Ee Mungu, niongoze katika njia zako za haki, na unisaidie kuishi maisha yanayokupendeza. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Basi kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu” (Wakolosai 3:1).
Ninakuja mbele zako nikiwa na unyenyekevu na moyo wa toba. Naomba unirehemu na unifanye kuwa kiumbe kipya ndani ya Kristo. Kama unavyosema katika Neno lako, “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama! yamekuwa mapya” (2 Wakorintho 5:17). Asante kwa upendo wako usio na kikomo, na kwa neema yako inayotosha kila siku. Naomba haya yote kwa jina la Yesu Kristo, aliye Mwokozi wangu.
Bwana, naomba unifundishe kuwa mtiifu na kuwa na moyo wa shukrani kwa kila jambo. Acha neno lako likae kwa wingi ndani yangu, na linibadilishe kutoka ndani hadi nje. Nisaidie kuacha njia zote za dhambi, na kuwa mwaminifu kwako katika kila hali. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Neno lako nimeliweka moyoni mwangu, nisije nikakutenda dhambi” (Zaburi 119:11).
Ninakubali kuwa mimi ni mnyonge na ninahitaji msaada wako kila siku. Nakiri dhambi zangu na naomba unisamehe. Naomba unipatie moyo safi, na kunifufua kiroho. Kama unavyosema katika Neno lako, “Ee Mungu, uniumbie moyo safi, unirejeshee roho iliyotulia ndani yangu” (Zaburi 51:10). Naomba unifanye kuwa mwanga na chumvi duniani, ili niweze kuonyesha upendo wako kwa wengine. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima” (Mathayo 5:14).
Asante, Bwana, kwa kusikia sala yangu. Naamini kuwa umesikia na kujibu ombi langu. Ninatangaza kuwa mimi ni wa Kristo, na ninakubaliana na mapenzi yako maishani mwangu. Kama unavyosema katika Neno lako, “Ninaweza kufanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu” (Wafilipi 4:13). Kwa jina la Yesu, Amina.
Umakini katika kuwaza
Kuwa makini sana na mawazo yako, Yanaweza kukupeleka Mbinguni au motoni.
Kumbuka vile unavyowaza ndivyo utakavyovitenda.
Amua kuwaza mema kutoka ndani ya moyo wako kisha utatenda mema katika maisha yako
Kumbuka Mungu humhukumu mtu kwa mawazo yake maana mawazo ya mtu ndiyo mtu mwenyewe
Tuwaze mema wapenzi ili tuwe wema
Kuwa Makini na Mawazo Yako
Kuwa makini sana na mawazo yako, yanaweza kukupeleka Mbinguni au motoni. Mawazo ni nguvu inayoweza kuelekeza maisha yako kwa njia ya heri au shari, na ni muhimu kuyadhibiti na kuyatumia kwa njia inayofaa.
“Ndivyo aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.” (Mithali 23:7)
“Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema; na mtu mwovu katika hazina mbaya hutoa yaliyo mabaya; kwa kuwa wingi wa moyo huongea kinywa chake.” (Luka 6:45)
“Tena mkiwaza hayo, yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema, ikiwepo wema wowote, ikiwa na sifa njema yoyote, mawazeni hayo.” (Wafilipi 4:8)
Mawazo Yanaelekeza Matendo
Kumbuka vile unavyowaza ndivyo utakavyovitenda. Mawazo yako yanaathiri moja kwa moja matendo yako. Unapowaza mema, utatenda mema; unapowaza mabaya, utatenda mabaya. Hivyo, ni muhimu kuzingatia na kuimarisha mawazo yako kuwa chanya na yenye kujenga.
“Kwa maana nimemwita Bwana siku zote; heshima na utukufu una mpata.” (Zaburi 19:14) “Mkishika maagizo yangu, mtapata uzima; tena msifanye mfano wa matendo ya nchi ya Misri mliyokaa, wala msifanye mfano wa matendo ya nchi ya Kanaani niliyowaleta; wala msizifuate sheria zao.”_ (Mambo ya Walawi 18:3-4)
“Jishughulisheni na mawazo yaliyo juu, wala siyo ya chini.” (Wakolosai 3:2)
Amua Kuwaza Mema
Amua kuwaza mema kutoka ndani ya moyo wako kisha utatenda mema katika maisha yako. Uamuzi wa kuwaza mema unatokana na kujitolea kuwa na moyo safi na mwenye nia njema. Jenga tabia ya kusoma na kutafakari Neno la Mungu ili moyo wako uweze kujazwa na mawazo mema yanayokuza tabia njema.
“Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.” (Zaburi 119:105)
“Nitalificha neno lako moyoni mwangu, nisije nikakutenda dhambi.” (Zaburi 119:11)
“Mwenye hekima ana moyo wa busara, neno la Mungu ni ngao kwake.” (Mithali 14:33)
Hukumu ya Mungu kwa Mawazo
Kumbuka Mungu humhukumu mtu kwa mawazo yake maana mawazo ya mtu ndiyo mtu mwenyewe. Mungu anaangalia moyo wa mtu na mawazo yanayotoka ndani yake. Ni muhimu kujitahidi kuwa na mawazo yanayoendana na mapenzi ya Mungu ili tuweze kumpendeza.
“Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina makali kuliko upanga wowote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake, tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” (Waebrania 4:12)
“Kila njia ya mtu ni safi machoni pake mwenyewe, lakini Bwana huzipima roho.” (Mithali 16:2)
“Kwa maana mimi, Bwana, nachunguza mioyo, nakijaribu viuno, nimpe kila mtu kwa kadiri ya njia zake, kwa kadiri ya matunda ya matendo yake.” (Yeremia 17:10)
Mawazo Mema Yanaweza Kutupeleka Kwa Wema
Tuwaze mema wapenzi ili tuwe wema. Mawazo mema hujenga tabia nzuri na matendo mema. Ni jukumu letu kujitahidi kuwaza na kutenda mema kila wakati, kwani kwa kufanya hivyo, tunakuwa vyombo vya amani na upendo wa Mungu duniani.
“Wenye amani hawatafutwa kwa bure, bali watapata furaha ya Bwana.” (Isaya 32:17)
“Kwa hiyo, wote mnaoamini, muwe na nia moja, wenye huruma, wenye kupendana kama ndugu, wenye huruma nyingi, wanyenyekevu.” (1 Petro 3:8)
“Na Bwana mwenyewe awafanye ninyi mzidi sana na kuongezeka katika upendo ninyi kwa ninyi na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu.” (1 Wathesalonike 3:12)
Kwa hivyo, tuwe makini na mawazo yetu, tuwe na nia ya kuwaza mema, na tuishi kwa kutenda matendo mema yanayotokana na mawazo hayo. Mungu anapenda watu wenye moyo safi na wenye nia njema, na atawabariki kwa wingi wa rehema na neema zake.
Amri ya Saba ya Mungu: Usiibe – Tambua mali ya mtu na kuheshimu
Je, Amri ya Saba ya Mungu inafundisha nini?
Amri ya saba ya Mungu inafundisha kuitambua mali ya mtu na kuiheshimu.
Mali ya mtu ni ipi?
Mali ya mtu ni ile aliyoipata kwa njia halali yaani kwa haki.
Lengo la mali ya binafsi ni lipi?
Kutosheleza mahitaji yake mtu binafsi, ya familia, ya wenye shida na ya kanisa.
Mtu awatendeje wanyama?
Mtu anatakiwa kuwatendea wanyama kwa wema kama viumbe wa Mungu
Amri ya saba ya Mungu inakataza nini?
Inakataza haya;
1. Wizi
2. Kulangua
3. Kutapeli
4. Kughushi
5. Kufuja mali
6. Kutoa au kupokea rushwa
7. Ufisadi
8. Kuharibu mali ya mtu au jamii
Anayejipatia mali kwa njia isiyo ya halali yampasa kufanya nini?
Anayejipatia mali kwa njia isiyo ya halali yampasa kurudisha gharama yake kwa mwenye mali
Anayeharibu mali ya mwingine lazima afanye nini?
Anayeharibu mali ya mwingine lazima alipe hasara aliyosababisha. (Lk 19:8)
Je yatupasa kufanya kazi?
Ndiyo, kwa sababu:
1. Kazi inampa mwanadamu heshima
2. Kufanya kazi ni wajibu wa haki. (Mwa 1:28)
Je ni lazima kuwasaidia masikini na fukara?
Ndiyo, Kuwatendea Masikini mema ni kumtendea Yesu mwenyewe. (Mt 25:40)
ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema “Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, “Tusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.
Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”
Au;
“Utuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..” Au;
“Salamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi.
Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.
Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.
Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Maria…, “Atukuzwe..”, “Ee Yesu wangu…” na “Tuwasifu milele…” kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.
MATENDO YA ROZARI TAKATIFU
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utusikie
- Kristo utusikilize
- Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
- Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
- Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
- Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie
- Maria Mtakatifu ………. utuombee
- Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
- Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee
- Mama wa Kristo ……… utuombee
- Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
- Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
- Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
- Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
- Mama usiye na doa ……….. utuombee
- Mama mpendelevu ………. utuombee
- Mama mstajabivu ………. utuombee
- Mama wa Muumba ………. utuombee
- Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
- Mama wa Kanisa……….. utuombee
- Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
- Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
- Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
- Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
- Bikra mweye huruma ………….. utuombee
- Bikra mwaminifu………….. utuombee
- Kioo cha haki ………….. utuombee
- Kikao cha hekima ………….. utuombee
- Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
- Chombo cha neema ………….. utuombee
- Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
- Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
- Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
- Mnara wa Daudi ………….. utuombee
- Mnara wa pembe ………….. utuombee
- Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
- Sanduku la Agano ………….. utuombee
- Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
- Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
- Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
- Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
- Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
- Msaada wa waKristo ………….. utuombee
- Malkia wa Malaika ………….. utuombee
- Malkia wa Mababu ………….. utuombee
- Malkia wa Manabii ………….. utuombee
- Malkia wa Mitume ………….. utuombee
- Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
- Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
- Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
- Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
- Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
- Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
- Malkia wa amani ………….. utuombee
- Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusamehe ee Bwana.
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusikilize ee Bwana
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utuhurumie.
- Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
Karibu Vitatabu vya Kikatoliki
-
Vitabu Vya Dini
KITABU CHA SALA ZA KILA SIKU ASUBUHI NA JIONI
Original price was: Sh4,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Mwongozo wa Sala na Nyimbo za Ibada ya Njia ya Msalaba
Original price was: Sh6,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Biblia Takatifu Agano la Kale
Original price was: Sh7,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Novena Ya Huruma ya Mungu
Original price was: Sh2,500.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Mwongozo wa kusali Rozari Takatifu ya Mama Bikira Maria
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Novena ya Roho Mtakatifu
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
📕Kitabu cha Sala Muhimu: Mkusanyiko wa SALA, LITANIA NA NOVENA
Original price was: Sh12,500.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Biblia Takatifu Agano Jipya
Original price was: Sh3,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Kitabu cha Tafakari kwa Mkristu Mkatoliki (Sehemu ya I)
Original price was: Sh3,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
Kwa nini Wakatoliki wanaweka Sanamu Kanisani?
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now -
Vitabu Vya Dini
KITABU CHA NOVENA KWA MTAKATIFU RITA WA KASHIA
Original price was: Sh5,000.Sh0Current price is: Sh0. Download Now
Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania
Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kusheherekea tarehe 28 Agosti, Sikukuu ya Mtk. Augustino wa Hippo.
SIKU YA KWANZA – kutafuta ukweli – kweli ni nini?
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina
Tafakari
Pamoja na Mtakatifu Augustino tunasema “ Umetuumba kwa ajili yako ee Bwana, kwani ni wewe peke yako ndie Mungu wetu, na nyoyo zetu hazitapumzika, hadi tupumzike ndani mwako.”
Tunapoanza Novena yetu kwa Mtakatifu Augustino tunamwomba Mungu neema ya kuwa na roho kama yake katika safari yetu katika kuzitambua nafsi zetu. Tunatafakari sisi ni nani na tunaelekea wapi kama wafuasi wa Mtakatifu Augustino katika dunia ya leo. Kama Mt Augustino alivyoutafuta ukweli bila kuchoka, nasi tutulie na kuruhusu maswali haya yaguse ufahamu wetu. Ni nini kinachonisababisha niendelee kumtafuta Mungu? Baada ya kumpata Mungu, ninamfanyaje awe hai kwa watu wale ninaoishi nao?
Kama kuna jambo moja Mt Augustino anasisitiza tena na tena kuhusu kumtafuta Mungu, ni kuwa lazima tuanze kumtafuta ndani mwetu. Huko ndiko tutakuta ukweli, mwanga na furaha katika Kristu mwenyewe. Ndani ya nafsi zetu ndiko tutasikilizwa tunaposali, katika nafsi zetu ndiko tutampenda Mungu na kumwabudu.
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristu utuhurumie Kristu utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristu utusikie Kristu utusikilize
Baba wa mbinguni Mungu utuhurumie
Mwana Mkombozi wa dunia Mungu utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu mmoja utuhurumie
Maria Mama wa Yesu utuombee
Maria Mama wa faraja utuombee
Maria Mama wa shauri jema utuombee
Mt. Augustimo nyota angavu ya Kanisa utuombee
Mt Augustino uliyejawa bidii kwa ajili ya kuutafuta utukufu wa Mungu utuombee
Mt. Augustino mtetezi jasiri wa Ukweli utuombee
Mt Augustino ushindi wa neema ya Mungu utuombee
Mt Augustino uliyewaka mapendo kwa Mungu utuombee
Mt Augustino mkuu sana na mnyenyekevu sana utuombee
Mt Augustino mfalme wa maaskofu na wanateolojia utuombee
Mt Augustino baba wa maisha ya kitawa utuombee
Mt Augustino mtakatifu kati ya wenye hekima na mwenye hekima kati ya watakatifu utuombee
Utuombee Mtakatifu Augustino – ili tustahili maagano ya Kristu.
Tuombe: Umetuumba kwa ajili yako ee Bwana, na nyoyo zetu hazitapumzika kamwe, hadi tutakapopumzika ndani mwako. Tunakuomba utubariki katika mahangaiko yetu ya kukutafuta wewe na utusaidie tunapokutana na makwazo. Tunapokupata, tunaomba utujalie neema ya kuwa waaminifu kwako ee Mungu wa historia, tuwe waaminifu kwa Yesu Kristu Mkombozi wetu, kwa Kanisa letu na mafundisho yake, na tuwe waaminifu katika wito wetu tuliouchagua katika kukutumikia wewe. Tunaomba hayo kwako wewe Baba mwema, kwa njia ya Kristu Bwana wetu na kwa maombezi ya Mtakatifu Augustino Msimamizi wa Jumuiya yetu, Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya pili – Utulivu
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina
Tafakari
“Ingia sasa, ndani ya moyo wako (Isaya 46:8) na uwe na imani, utamkuta Kristu humo. Humo anaongea na wewe, mimi, mwalimu, napaaza tu sauti yake lakini Yeye ndiye anayekufunza wewe kwa ufanisi zaidi katika utulivu wako”
Je tunapenda maisha ya utulivu ambapo tunapata muda wa kumtafakari Mungu na mambo anayotutendea katika maisha yetu? Kwa vile Yesu anaongea nasi katika utulivu, inatupasa tujifunze namna ya kuutunza utulivu ndani ya nafsi zetu licha ya mahangaiko na misukosuko ya maisha. Tutenge muda katika siku yetu ambapo tunaweza kutulia na Kristu na kumsikiliza, na wala sio sisi kuongea nae tu bila kumsikiliza naye pia. Soma Neno la Mungu kwa utulivu na kwa tafakari, na uone kama kuna kitu gani Mungu anakuaombia leo. Lazima tusafishe macho ya nyoyo zetu, ili tuweze kumwona Mungu ndani mwetu. Tunafanya hivyo kwa njia ya toba na maungamo. Kusafishwa vizuri ni jambo linaloweza kuambatana na maumivu, lakini tunahitaji usafi wa nafsi ili tuweze kuwa wasikivu zaidi kwa sauti ya Mungu ndani mwetu.
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Ee Baba mwema, tunataka kumfuata Mwanao Yesu kwa ukaribu zaidi. Utuwezeshe kuumbika upya nawe kwa mfano wa Mtakatifu Augustino katika maisha yake ya utulivu. Utusaidie kuacha mambo ya dunia hii yanayopita ili tupate hamu kubwa zaidi ya kukufuata. Imarisha imani yetu ili tusikie sauti yako katika maandiko: ili tuweze kukuona Wewe katika matukio ya maisha yetu. Tunaomba haya kwa njia ya Kristu Bwana wetu, anayeishi na kutawala nawe na Roho Mtakatifu, Mungu mmoja milele na milele. Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya tatu – matendo-tafakari na matendo
Katika wito wetu uwao wote wa maisha yetu, tunaalikwa na Yesu tutafakari jinsi Martha alivyolalamika kuwa dada yake Maria alitumia muda wote katika kumsikiliza Yesu badala ya kusaidia kazi. Mt. Augustino akiwa kama mtawa aliuchukua mfano wa Martha na Maria kwa kushiriki kwa ukamilifu pia katika ujenzi wa uhai wa Kanisa kwa njia ya maandishi na kazi zake njema. Je mimi ninaoanishaje kati ya kutenda, kusali na tafakari takatifu?
Mt. Augustino anatufundisha kuwa tuwe tayari kuwatumikia wengine. Asiwepo mtu anayedhani kuwa anaweza kusali tu muda wote bila matendo, na wala asiwepo anayedhani atafaidika kwa matendo mengi yasiyosindikizwa na wingi wa sala. Tunapozigundua karama zetu Mungu alizotupa, tuwe tayari kuzishirikisha kwa wengine, kwani siku ya mwisho tutahukumiwa kwa namna ambavyo tuliwajali wengine. Kwa hiyo baada ya kumpata Mungu ndani mwako, usibaki humo, bali mgeukia yeye aliyekuumba. “Tupande mlimani lakini tusijenge vibanda, tushuke tuwatumikie wengine”
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Mungu Baba yetu, tunakutukuza na kukushukuru kwa kulijalia Kanisa lako mtakatifu mkuu namna hii. Tunapojitahidi kuishi roho na karama zake, utujalie neema za kukua katika utumishi wetu kwa wengine kwa njia ya matendo mema na pia katika maisha yetu ya sala, kwa mfano wa Mt. Augustino. Tunaomba hayo kwa Jina la Mwanao, Bwana na Mwokozi wetu. Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya nne – umaskini wa kiinjili – maisha ya kujitoa
Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina.
Kuna wakati Mt. Augustino alikosa kitu chochote cha kuwapatia wasiojiweza, kwa sababu alikuwa anagawa kila alichoweza kwa wenye shida. Alipoishiwa kabisa, aliuza baadhi ya vitu alivyokuwa navyo ili kupata pesa iliyohitajika kwa ajili ya wenye shida.
Je, mimi pamoja na karama zote alizonijalia Mungu na vipaji vyote nilivyo navyo, ninajitahidi kuiga mfano wa Mt. Augustino katika kujitoa kwa wengine?
Umaskini wa kiinjili ni tofauti na umaskini wa kukosa mali au pesa. Ni namna moyo wa mtu anavyopenda kujitoa hata nje ya Jumuiya yake. Yesu Kristu alijitoa kabisa kwetu kwa kuuacha Umungu wake na kujitwalia ufukara wetu ili aweze kututajirisha. Hii ni changamoto kwetu kuwa tuwe tayari kujitoa kwa ajili ya wale wanaotuhitaji na Augustino ni mfano katika hilo. Tujitolee kufanya kazi za huruma, kwani mtu hataishi kwa mkate tu. Je tunawasaidiaje maskini walioko katika eneo letu? Ufalme wa Mungu utawafikiaje wengine kupitia kwetu. Mt Augustino anatupa changamoto leo kuwa tukubali kwa moyo mmoja kutoa vitu tulivyo navyo kwa ajili ya wengine, na tumfuate Kristu kwa moyo mpya na wa dhati.
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Tunakutukuza ee Bwana kwa kila unatupowezesha kushirikisha vile ulivyotujalia kwa ajili ya wahitaji, na kushikama katika upendo wako. Tunakuomba utujalie neema ya kudumu katika kushirikiana na kupendana ili tuwe mashahidi wa ukarimu wako mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristu, anayeishi na kutawala pamoja nawe na Roho Mtakatifu, Mungu mmoja daima na milele, Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya tano – urafiki katika jumuiya yetu
Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina.
Mt. Augustino anashuhudia kuwa kitu kilichomweka karibu na marafiki zake kaka na dada zake ni kulekuongea na kucheka pamoja, kusaidiana, kusoma vitabu vinavyofanana vyenye mambo ya kujenga, kutaniana, kutofautiana mara kwa mara bila kukasirikiana, na alama za urafiki wetu zilijionyesha katika nyuso zetu, sauti zetu, macho yetu, na namna nyingi nyingine”. Je mimi nafurahia mahusiano yaliyoko katika Jumuiya yetu? Kuna jambo gani naweza kufanya ili kuboresha mahusiano na wanajumuiya wenzangu?
Ushahidi wa mapendo ya kweli unakuja pale tunapokuwa tayari kubebeana mizigo yetu. Tunapojitahidi kuboresha mambo yanayohusu Jumuiya, ukweli ni kuwa tunaboresha mambo yetu binafsi pia. Tumwombe Mungu ili tuweze kuona namna ambavyo Jumuiya yetu inatutegema katika hali na namna mbalimbali na tuweze kuboresha mahusiano ili kukuza urafiki kati yetu kama anavyotufundisha Kristu.
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Bwana Mungu wetu, ulimfunulia Mt. Augustino uzuri ulioko katika urafiki uliojengwa katika misingi yako. Utujalie sisi tunaosimamiwa naye hapa duniani, tukue katika urafiki mtakatifu wa kijumuiya. Utujalie tufikie ukamilifu wa urafiki huo katika makao yetu ya mbinguni unakoishi na kutawala daima na milele, Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya sita – augustino mfano wa unyenyekevu
Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina.
Unyenyekevu unapatikana tu katika vita vya kiroho. Umuhimu wa majaribu katika maisha yako ya kiroho ni kuwa ni kwa kupitia tu majaribu hayo unajipatia unyenyekevu. Hapo ndio unauona umuhimu wa kumpokea yesu kuwa Mwokozi wako. Ukiwa na kiburi itakuwa ni kikwazo kikubwa kumpokea Mwokozi.
Kwa Augustino, unyenyekevu sio kujidharau, bali ni kujitahidi kufahamu karama alizotujalia Mungu na kuziendeleza. Ili kuwa mtu mnyenyekevu, jifahamu kuwa u mdhambi, na kuwa Mungu ndie anayeweza kukuweka huru. Fanya maungamo ya dhambi zako ili uwe wa kundi lake Mungu. Je, kama unyenyekevu ndio ukweli, ninajitahidije kuushirikisha ukweli huu kwa wengine katika Jumuiya yetu?
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Tuelekezee nyoyo zetu katika wema wako ee bwana, na geuza macho yetu mbali na kiburi na puuzi za dunia ili tuwe wafuasi wa maneno yako: Jifunzeni kwangu kwani mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo. Utujalie tukue kila siku katika unyenyekevu ambao unampendeza sana moyo wa Msimamizi wetu mt. Augustino. Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya saba – uangalizi wa imani yetu
Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina.
Na tumpende Bwana wetu, tulipende kanisa lake. Tunampokea Roho Mtakatifu kadri tunavyolipenda Kanisa lake, kama tukiunganika pamoja kwa upendo, kama tukilifurahia jina katoliki na Imani yake. Tuamini kuwa tutakuwa na Roho Mtakatifu kwa kipimo cha upendo wetu kwa Kanisa lake. Tunalipenda Kanisa kama tulisimama imara katika ushirika na upendo.
Je ninalipenda Kanisa Katoliki? Ninajitahidi kujifunza imani hii na kuwashirikisha wengine au ninafuata mkumbo tu? Tunaalikwa kuishi kwa mfano wa Mt. Augustino ambaye alijielimisha kuhusu imani ya Kanisa Katoliki na kuikumbatia, kuitetea na kuishirikisha kwa wengine. Tusisite kujitoa katika dunia yetu ya leo pale tunapohitajika katika kueneza imani yetu. Tumwombe Mungu atujalie kwa mfano wa Mt. Augustino, moyo wa kusukumwa kuwashirikisha wengine imani iliyo hai kwa njia ya maneno, na matendo yetu, na hivyo kulitetea Kanisa la Bwana wetu Yesu Kristu kila wakati kwa injili iliyo hai.
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Baba mwenye upendo, tunakushukuru kwa zawadi ya Mt. Augustino uliyolipatia Kanisa lako. Kwa maombezi yake, sisi tunakuomba mwanga na ujasiri wa kujitoa bila masharti kwa unyenyekevu na daima katika huduma kwa wengine hasa wenye shida mbalimbali katika mahitaji ya mwili na ya roho. Tunaomba hayo, kwa njia ya Kristu Bwana wetu, Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya nane – utayari katika kulisaidia kanisa letu
Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina.
Jumuiya ni kiini cha Kanisa la leo, kama ilivyokuwa wakati wa mitume, wakifundishwa na mitume. Kama Jumuiya za kwanza za wakristu, tunaalikwa nasi leo tuwe na utayari katika kulisaidia Kanisa letu kwa njia mbalimbali hasa kwa kutoa zaka kwa wakati. Wakati huohuo pia tuelewe kuwa Roho Mtakatifu anatupatia vipaji na karama kuendana na mahitaji ya Kanisa lake, na hivyo tusisahau kushirikisha karama na vipaji hivyo kanisani kwetu ili kuujenga mwili wa Kristu. Kwa njia hiyohiyo, kazi zetu za kitume ziendane na mahitaji ya Kanisa letu leo hii kwani yote tunapewa na Roho wa Mungu kwa ajili ya utumishi kwa wengine. Je, shughuli zetu kama Jumuiya zinaendana na mahitaji ya Kanisa la Mungu kwa wakati huu? Ni mabadiliko gani tunaitwa kuyafanya kama Jumuiya na kama mtu mmoja mmoja ili kuboresha Kanisa kupitia Jumuiya yetu?
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Baba mwema, tunakuheshimu na kukutukuza kwa kutupatia Mt. Augustino. Tukiwa tumejiweka chini ya mafundisho yake, tunaomba neema na maongozi yako ili tuweze daima kuwa na utayari wa kulisaidia Kanisa letu kwa njia ya zaka na majitoleo kadri ya mahitaji, na utujalie neema tunazokuomba kwa njia ya Yesu Kristu, Bwana na Mwokozi wetu. Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
Siku ya tisa – utayari wa kuwasaidia wenzetu
Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina.
Mt. Augustine daima alikuwa tayari kuwasaidia wahitaji. Alitoa kila alichoweza vikiwemo vile vitu alivyotengewa kwa ajili ya matumizi yake yeye mwenyewe, na alipokosa kitu zaidi cha kutoa, aliyeyusha baadhi ya vyombo vya dhahabu vilivyokuwa vimewekwa wakfu kwa ajili ya kuuza na kisha aliwagawia maskini pesa iliyopatikana. Nasi mara nyingine inawezekana hatuna pesa mfukoni za kuwapa wale wanaohitaji tuwasaidie, lakini bila shaka tuna vitu. Mazao ya mashambani, mifugo, na vitu aina mbalimbali alivyotujalia Mungu. Kwa hiyo kila mmoja wetu ana kitu anachoweza kumpa mwenzake, pengine kama sina chochote zaidi angalau nina muda wa kusali na kuwaombea wengine kuendana na mahitaji ya Jumuiya yetu, au kuwatembelea wapweke, wenye majonzi na kuwafariji wengine. Cha msingi ni kumtazama Kristu, ambaye ana njaa na anateseka, ndani ya wenzetu.
Tunafanya vyema kushikamana na maskini. Sio maskini wa mali na pesa tu tunazungumzia hapa, bali pia maskini wa kiroho, wale wanaohitaji kuelekezwa, wenye mashaka, wapweke, wagonjwa, na wanaoteseka na dhambi. Tumwombe Mungu ili tuimarike kiroho, maana tutaweza kuwasaidia hao maskini tu pale ambapo sisi wenyewe tuna utajiri wa kiroho, yaani tunaye Kristu ndani mwetu.
Tunapomalizia Novena yetu ya siku tisa, tutafakari kuwa, kama Mt. Augustino angekuwa hai leo, angewajibika namna gani, angewasaidiaje maskini walioko katika Jumuiya yetu, mahali petu pa kazi na hata katika familia zetu?
Litania kwa heshima ya Mtakatifu Augustino
(Angalia siku ya kwanza)
Tuombe: Bwana, tunakuomba urejeshe upya katika Kanisa lako roho kama ile uliyompa Mt. Augustino. Kwa mfano wake, tujazwe na kiu ya kukupata wewe peke yako kama chemchem ya hekima na chanzo cha upendo wa milele ili tuwe na utayari wa kuwasaidia wenzetu wote wenye shida za aina mbalimbali. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina.
Baba yetu……, Salamu Maria….., Atukuzwe Baba……
SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI
Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yesu./ Jina la yule msaliti aliyemwuza Yesu/ limewafanya wengi wakusahau./ Walakini Kanisa zima linakuheshimu/ na kukuomba kama Msaidizi katika mashaka makubwa,/ na katika mambo yasiyo na matumaini tena./
Uniombee mimi mnyonge./ Ninaomba utumie uwezo ule uliojaliwa/ wa kuleta upesi msaada kwa watu walioukosa./ Unisaidie sasa katika mahitaji yangu,/ ili nipate kitulizo na msaada wa mbinguni/ katika lazima zangu,/ masumbuko na mateso,/ hasa/ (taja shida yako)./ Pia ili niweze kumsifu Mungu nawe na wateule wote milele./
Mtakatifu Yuda Tadei,/ utuombee,/ na uwaombee watu wote wanaokuheshimu na kukuomba msaada./
Moyo Mtakatifu wa Yesu,/ Rafiki mpenzi wa Yuda Tadei,/ nakutumainia./
(Mwisho Sali: Baba yetu (x3), Salamu Maria (x3) na Atukuzwe(x3).
Sala ya Baba Yetu: Sala ya Bwana
Baba Yetu uliye mbinguni,
jina lako litukuzwe;
ufalme wako ufike,
utakalo lifanyike
duniani kama mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku,
utusamehe makosa yetu,
kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika kishawishi,
lakini utuopoe maovuni.
Amina
SMS nzuri ya kumtakia umpendaye mchana mwema
Mpenzi kila tunapokuwa chumbani huwa napenda kuwa mbunifu, huwa najitahidi kuepuka udhaifu, ili mapenzi yangu yasikukifu, ENDELEA KUFURAHIA MAPENZI YANGU. Mchana mwema
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
MAFUNDISHO MUHIMU KUHUSU MWILI NA DAMU YA YESU KRISTU | BIBLIA INAVYOELEZA KUHUSU EKARISTI
Yesu alituambia nini kuhusu Mwili wake na damu yake?
Damu na Mwili aliotupa Yesu ni nini? Ekaristi ni nini hasa?
Fundisho hili la mwili na damu ya Yesu (Ekaristi) lilikua Agizo tunalopaswa kulitii mpaka leo?
Mitume walitii Fundisho la Ekaristi na waliliishi?
Je mkate na divai vilichukuliwa na Mitume kama nini hasa? walichukulia Ekaristi kama nini?
16Je, kikombe cha Baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? 17(Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja) (1 Wakorinto 10:16)
Je ni lazima Kwa Mkristu kupokea Mwili na damu ya Yesu (Ekaristi)?
Je ni kwa nini madhehebu mengine hawakubali mafundisho haya ya Ekaristi Takatifu, Je ni mara ya kwanza watu kukataa?
Hata wakati Yesu akiyasema maneno haya Wafuasi Wengi Walimwacha kama Biblia inavyosema; 60Wengi wa wafuasi Wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?’’ (Yohana 6:60). Haishangazi hata leo weni hawaamini mafundisho haya japokua ndio msingi wa Imani ya Kikristo.
Mitume walifundisha nini kuhusu Mwili na Damu ya Kristu (Ekaristi)?
Je, Divai iliyotumiwa na Yesu na mitume pamoja na Wakristu wa Kwanza ilikua na Kilevi (pombe)?
Kwa hiyo hata Mitume na Wakristu wa kwanza walitumia divai yenye kilevi ndio maana kuna waliolewa na walionywa kuhusu hilo.
Je Yesu Yupo Mzima katika Ekaristi Takatifu? Na kwa nini Tunaabudu Ekaristi?
Ukisoma Yoh 6:51-57 inasema hivi;
51Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu ye yote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’’ 52Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?’’ 53Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin, nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu Yake, hamna uzima ndani yenu. 54Mtu ye yote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. 55Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 56Ye yote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake. 57Kama vile Baba aliye hai alivyonituma Mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
Mstari wa 51 Yesu alisema wazi Mkate huo ni Mwili wake.
Thamani na Uwepo wa Yesu Mwenyewe unaonekana katika Mstari wa 53 na wa 56. Kumbuka hapa amesema “Mimi nitakaa ndani yake” Hakusema Mwili wangu utakaa ndani yake. Kwa maana nyingine ni kwamba Ekaristi ni Yesu Mzima na Sio Mwili tuu.
54Mtu ye yote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. 55Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 56Ye yote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
Wale Wanaopinga fundisho la Ekaristi wanafikiri Yesu alivyosema Mimi ni Chakula Kutoka Mbinguni hakumaanisha Mwili bali Maneno na Imani Kwake lakini Tukisoma 51 Yesu alisema wazi kuwa Mwili wake ndio Mkate wenyewe.
51Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu ye yote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’’
Mitume wa Yesu walielewa hivi fundisho hili ndio Maana walishiriki Meza ya Bwana kila walipokutana na waliheshimu kama Mwili na Damu ya Kristo.
7Siku ya kwanza ya juma tulikutana pamoja kwa ajili ya kumega mkate. (Mdo 20:7)
Ili kujua kuwa Mitume waliheshimu Mwili na Damu ya Yesu Biblia inatuambia hivi;
23Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule alipotolewa, alitwaa mkate, 24naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema “Huu ndio mwili Wangu, ambao ni kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho Wangu.” 25Vivi hivi baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu Yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo kwa ukumbusho Wangu.” 26Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo. 27Kwa hiyo, mtu ye yote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana. 28Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe. 29Kwa maana mtu ye yote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, anajiletea hukumu juu yake mwenyewe. 30Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa. (1 Wakorinto 11:23-30)
Kwa hiyo Mitume walisisitiza kuhusu Mwili na Damu ya Kristu kuwa ni Mtakatifu.
51Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu ye yote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’’
Yesu alisema Mimi ni Mkate wa Uzima ambao alimaanisha upo katika Mwili wake. Mwili tuu hauna uzima kama hauna Yesu ndani yake. Kwa sababu Mwili ni Mzima na Unaye Yesu ndani yake ndiyo maana unaweza kuleta uzima kwa Wengine.
Tunaelewa kwamba Yesu alijitoa Msalabani Mwili Wake na Damu yake na ndicho alichotupa ktk Ekaristi. Na Mwili wake huo Ulikua umembeba yeye aliye Mungu ndiyo maana tunaabudu Ekaristi alipo Yesu aliye Mungu.
Kwa kuwa Yesu ni Mungu Kama tunavyosoma katika Yoh 1:1-12
1 Hapo mwanzo, kabla ya kuwapo kitu kingine cho chote, aliku wapo Neno. Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye alikuwa Mungu. 2 Tangu mwanzo Neno amekuwa na Mungu. 3 Vitu vyote viliumbwa na yeye, wala hakuna cho chote kilichoumbwa ambacho hakukiumba. 4 Uzima ulikuwa ndani yake na uzima huo ndio ulikuwa nuru ya watu……..14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.
Kwa hiyo Neno huyo huyo Ndiye aliyetukomboa kwa kuutoa mwili wake sadaka Msalabani na ndiye Aliyetupa Mwili Wake na Damu yake ktk Ekaristi na anaabudiwa kwa kuwa yupo katika mwili huo.
“Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili Wangu unaotolewa kwa ajili yenu, fanyeni hivi kwa ukumbusho Wangu.” (Luka 22: 19). Kwa namna hii alitupa mwili wake.
Alisema fanyeni kwa ukumbusho wangu na Sio wa mwili wangu.
Hivyo Ekaristi ni Yesu Mwenyewe aliye Mungu. Ndiyo sababu tunaabudu Ekaristi Takatifu.
Recent Comments