Vihoja Vya Kuwaadisia
Wadada lenu hili. Mimi sipo
Wadada kama una sura mbaya subiri NEEMA YA BWANA..Sio kutuambia mna uzuri wa Ndani usioonekana..Sisi ni Wanaume,Sio MINYOO
๐๐๐๐
Cheki masifa yalivyomponza huyu, Sifa nyingine ni mbaya jamani
Mbongo, Mganda, na Mkenya walikamatwa na makosa Uchina.
Wakaambiwa adhabu ni ama kifo cha moja kwa moja au adhabu nyingine ambayo atakayeifaulu atakuwa huru, atakayeshindwa atauawa.
Basi wao wakaomba wapewe hiyo adhabu nyingine wajaribu bahati yao.
Wakapelekwa msituni wakaambiwa kila mmoja aende kwa njia yake halafu arudi na matunda kumi ya kufanana.
Wakaingia msituni kila mtu njia yake.
โฆ Mganda akarudi wa kwanza na machungwa kumi. Akaambiwa adhabu yake ni kumeza moja moja likiwa zima bila kufumba macho bila kulia wala kucheka wala kujitikisa mpaka yote kumi yaishe. Akameza la kwanza. Safi. Kumeza la pili, akashindwa kuvumilia akafumba macho. Akapigiwa risasi akafa.
Mkenya akaja. Ana vitunda vidogo vidogo kama pili vilaini. Akasomewa masharti. Akaanza kumeza bila kufumba macho wala kulia, wala niniโฆ alipofika cha tisa akashindwa kuvumilia akaangua kicheko! Akapigwa risasi pia akafa.
Wakiwa kuzimu Mganda akamwuliza Mkenya, โVipi, mbona ulishindwa kuvumilia wakati kilibaki kitunda kimoja tu?โ
Mkenya akamjibu: โMkuu, nilishindwa kuzuia kicheko maana nilimwona Mbongo anakuja na matikiti maji!โ
Cheki huyu kiherehere alivyojibiwa
Za asubuhi?
Nzur sjui huko?
Huku kwema tuu
VP si ulimaliza chuo ww?
Ndio kwani vp?
Mbona hatuoni matunda yake?
Kwani mi nlienda na miche ya mipapai au miembe au umeambiwa TIA, IFM na IAA wanakodisha Mashamba ya nyanya ????????
Hamna sio hvyo umeenda mbali kaka
Kama kilomita ngapi?
Haya yaishe bhanaโฆ
Ukome kwa kiherehere
Nitukane tuu unakumbuka kuna SKU nlkupa buku ya nauli?
Nitajie namba yako ya tgo pesa nkuwekee hyo buku
Kwani mi nimesema unilipe
Utajua mwenyewe ila nakutumia kwenye namba uliyonitext wee si umefanya ujinga mi nafanya upumbavu
Simple lyke dat Viherehere huwa tunawajbu HVOโฆโฆ๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Angalia nilivyoingizwa mjini na ujanja wangu wote
Ndio nilikuwa nimeshuka kwenye basi la SAI BABA pale Ubungo, nina Begi kubwa Mgongoni na begi Dogo la Lap Top mkononi, sura inatazama Mbele Very Serious kama nipo kwenye Gwaride la Uhuru!..Mabega juu yanafanya Cheers na Mawingu!, natembea kwa madoidoโฆ..leo nimetoka Likizo Moshi,
“Brother Simu ya ukweli hii..kitu cha Tecno C9 bei poa” hii ilikuwa sauti ya Teja mmoja hivi!
Yaani huyu Teja Bwege kweli,anataka kumuuzia nani sabuni? mimi sio wa kuja!โฆkamwe Siwezi kuibiwa hapa Town,hakuna wizi au utapeli nisioujua!, Mimi nimezaliwa Mwananyamala kwa Manjunju, nikalelewa Tandale kwa Mtogole, Shule ya msingi nimesoma Turiani Magomeni, Hivi Mbwa gani aniibie?โฆkwa Style ipi?
Sipendi kabisa Upuuzi!, Wajinga ndio wataibiwa, sio Mimi!โฆsasa Kwa mwendo wa haraka nikatoka nje kabisa ya Stendi ya Ubungo straight mpaka Stendi ya dala dala za Kariakoo, hapo ndipo nikakutana na Vijana wawili wadogo wakiwa na mzani wa kupimia uzito,โฆhakika napenda sana vijana wanaojituma kama hawa na sio ile Mijizi ya kule ndani Stendi!!,โฆ.hapa sasa nikapata wazo!
“Dogo mnapima uzito kwa shilingi ngapi?”
“Mia mbili tu Kaka!”
”Ok”
Kwa mwendo wa kikakamavu nikapanda juu ya mzani,lengo hapa ni kujua uzito wangu, Mtori niliokula mwezi mzima kule kwa Mshekuu sio mchezo, hapa nahisi nacheza kwenye kg za John Cena,
“Mama wee! Dogo mzani mzima huu kweli? Mbona nina kilo 134?” (Nilihamaki)
“Aaah! Brother huoni umepanda na Mabegi juu ya mzani?”’
Hahaha! kweli nimechanganyikiwa!โฆSasa nikatoa mabegi yote mawili na kurudi juu ya Mzani, hapa ndipo Uzito ukashuka kutoka kg 134 mpaka kg 56!โฆMy God kweli Body la “One Pack ” haliongopi! thats means mabegi yaliniongezea kg 78! duh hii ni hatari!
“Yaani we Dogo kitambi chote hiki kg 56? huu Mzani Mzima kweli?”
Kimyaโฆ
“Dogo huu Mzani vipi?”
Kimyaโฆ
Dogo ana dharau huyu!โฆSasa ndio nikabandua macho yangu toka kwenye kioo cha mzani ili nimtazame huyu dogo asiyejibu!โฆ.ndipo macho yangu yakakutana na Kigoda tupu kilichochongwa Mvomero!โฆDogo hakuwepo!โฆ.na Mabegi pia hayapo!โฆlap top haipo!โฆ.NIMEPIGWA!
Ni dhahiri watoto wa Mjini walikuwa wameniacha juu ya Mzani, wamechukua Lap top ya Milioni na wameniachia Mzani chakavu wa elfu 40, what a stress!โฆ.sasa nilirudisha macho kwenye kioo cha uzito na sasa kilisoma KG 38!โฆyaani dakika hii hii nimepungua kilo zingine 18, Hakiyamama nahisi hata utumbo wangu wamebeba!โฆniitieni Ambulance!
๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ
Njia 3 rahisi za kuondoa kitambi
JE, una KITAMBI na unataka kukiondoa?
FANYA HAYA;
1. Kopa mkopo mkubwa benki
2. Nunua gari bovu la biashara
3.Oana na mke mwenye kelele.
Ukiona miezi mitatu hakijaisha basi ujue umevimba BANDAMA sio kitambi..
Huyu jamaa amekomeshwa, majambazi ni shida!
CHEKA KIDOGO
Majambaz waliliteka gar moja lililokua limeshehen abiria
Baada ya abiria kusachiwa na majambaz hao na kukutwa hawana pesa, majambaz wakasema kila m2 atapigwa viboko (bakora) kutokana na namba ya shati alilovaa
Aliyekua hana namba atasalimika
Kaz ikaanza, jamaa alievaa jez ya ROONEY wa Man U akapigwa fimbo 10, mwengine alievaa nguo ya 50cent akapigwa 50, n.k, sasa kwa pemben kulikua na jamaa analia sn yaani kila akijiangalia, kumbe alikua amevaa fulana limeandikwa LOWASA 2015 duuuh! Unajua kilichotokea ngoja niweke cm chaji kwanza.
Angalia huyu mwanafunzi anachomjibu huyu mwalimu wake
1. Ticha:”Punda ni mnyama anaefugwa nyumbani,lakini akiwa mwituni anaitwa pundamiliaโฆ.Je sungura anayeishi mwituni anaitwaje?”
ZUZU:”Sunguramilia.”
2.Ticha:”Rais wa kwanza wa kenya aliitwa KENYATTAโฆJe rais wa kwanza wa
Tanzania aliitwaje?”
ZUZU:”TANZANIATTA.”
3. Ticha:”Kuku yuko katika jamii ya NDEGEโฆJe samaki yuko katika jamii ya nini?”
ZUZU:”MELI.”
4. Ticha:”Coach wa Arsenal anaitwa ARSENE,wa Man-city anaitwa MANCINIโฆ.Je wa
Liverpool anaitwaje?
ZUZU:”LIVER.”
5 Ticha:”Ukiwa na mbuzi 10,wezi waje waibe 5,utabaki na nini?”
ZUZU:”Hasira nyingi sana!”
Duh. Chezeya kuhama!
Pale imebaki siku moja uhame kwenye nyumba ya kupanga af unakuta umebakiza unit 60 za umeme, inabidi tu uchemshe maji hadi yale ya kuflashia choo
๐ก๐ก๐ก๐ก๐ก
Staili nyingine za michepuko ni shida
Mtu na mkewe walikuwa bado wamelala asubuhi, mtu akapiga hodi mke akaenda kufungua mlango, si akakuta mchepuko wake,
MKE: Unataka nini we mpumbavu?
MUME: Nani huyo unamtukana?
MKE: Kuna mtu hapa anakichwa kama nenda urudi badae
MCHEPUKO:Nawewe pua kama poa
MKE:Miguu kama masaa mawili
MCHEPUKO:Masikio kama sichelewi
MKE: Ondoka hapa mjinga we. โฆโฆ Akafunga mlango
MUME: mwambie ana macho kama sitoki leo ng’oo
SIPENDI UJINGA MM nikiwa na my love pr
Ukimuona mbwa kwenye harusi hii ndiyo maana yake
Hili nalo neneo.
Ukimuona mbwa๐ถ harusini usimpige mawe wala kumfukuza inawezekana kilichomleta pale ndicho kilichokupeleka na wewe hapo
Angalia pombe ilichomfanya huyu jamaa, kweli pombe haimuachi mtu salama
Leo nimeiogopa pombe.
Nimetokea kuiogopa pombe baada ya kumwona jirani yangu akicheza muziki kwa sauti ya jenereta langu, akidhani yuko clubโฆ..nkamsikia anasema “wee dj noomaaaa”
Baada ya kuzima jenereta akaniuliza uo mziki kaimba nan?
Nlivyokuwa na roho mbaya Nikamwambia iyo ni collabo ya Yamaha na Petrol
๐๐๐๐๐
Ameniomba nimfungulie akaunt facebook cheki nilichomjibu
Leo nimechoka zangu alafu shangazi amekuja anataka nimuunganishe facebook. Imebidi nimwambie
lazima awe na picha passport size 4 kwaajili ya kuweka profile picture, barua kutoka kwa afisa mtendaji na Atm card ya nmb bank. Alafu awe na marefa wanne ambao wamekuwa facebook for more than 3 years. Amesema
hataki tena kujiunga fb!
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Saa ivi niko zangu nimelala naendelea kupunguza uchovu
Angalia huyu Jamaa alivyomuweza huyu mrembo
Nipo kwenye daladala siti ya nyuma kabisa nimekaa na mrembo mzurii.sasa nikawa namtongoza kwa sauti ya chini sana watu wengine wasiskie,akawa hanijibu kitu,mala gafra akapayuka kwanguvu na kwa sauti ya juu iliyomshtua kila mtu.โ
โ”Nimesema stakii,stakii tena unikome”โ๐ณ๐ณ
โNami nikamjibu kwa sauti ya juu vile vileโ
โ”Kama umejamba nisikwambie bhanaa,kwani ww nani?”โโน
๐๐๐๐๐๐๐๐๐
โโMIMI SIO MTU WA MCHEZO MCHEZOโ
Sipendag ujuinga mim
Unakumbuka hizi enzi za utoto?
Kitambo tukiwa watoto ulikuwa unaitwa uje ule kwa lugha tofauti kulingana na chakula kilichopikwa siku na muda husika
1. UGALI NA KUNDE
Mwitaji : ๐ฃJoniiiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Uje ukule
2. UGALI NA SAMAKI
Mwitaji: ๐ฃ we Joniiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Unaitwa na Mama
3. WALI NA NYAMA/KUKU
Mwitaji: ๐ฃ Joniiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Shauri yako!
๐๐๐๐๐๐
Angalia huyu mke wa mtu anavyojichanganya hadi kwa mme wake
MUME: “Mke wangu nasikia John katembea na wake za watu wooote hapa mtaani kasoro mmoja tu!”
MKE: “Mmmh! basi huyo aliebaki atakuwa MAMA MBILINGE KISIKI, maana yule mama ndo ANAJIFANYAGA MGUMU sanaaa.!!”
Je, huyu mama angekuwa mkeo ungekuwa na swali lingine la kumuuliza?
Wachaga kweli kiboko: Mcheki huyu mchaga na mbuzi!!!
Mchaga alinunua mbuzi akamwambia mpishi Nyama nusu ipike pilau na ingine itie kwenye friza. Kichwa fanya supu, miguu fanya mchuzi chukuchuku. Ngozi usitupe tutafanya mswala, utumbo pikia ndizi na mifupa tutawauzia wenye mbwa. Kinyesi kihifadhi kwa mbolea ya bustani.
Mpishi akamuuliza Hutaki na sauti ya mbuzi tufanye ring tone kwenye simu yako? Mchaga akajibu Yesuu! hivi inawezekana? bac fanya hivyo tuwauzie na wengine hiyo ringtone. ๐๐
Nilichokifanya wakati naangalia taarifa ya habari
Jana wakati naangalia taarifa ya habar mtangazaji akasema “mpenz mtazamaji nataka nikupeleke moja kwa moja had marekani” nikazima TV kwa haraka nikaenda kuvaa viatu. Hadi sahv bado nmekaa hapa seblen nahisi bado wanaihangaikia Visa yangu
๐๐๐๐๐๐
Huyu mama mkwe kazidi sasa
Eti kuna mkaka alitembelewa na mama yake mzazi. Wakiwa sebuleni yeye, mama na mke wake, mke wake akaanza kuonekana tofauti kama vile anajiskia vibaya. Akaenda chumbani. Baada ya muda mfupi yule mkaka akamfuata. Wakakaa sana huko kisha mkaka akarudi sebuleni kuendelea kuongea na mama yake. Lakini zipu ya suruali yake ilikuwa wazi. Mama akamuuliza, mkeo anaendeleaje? Akamuambia, anajisikia vzr sasa. Nimempa panadol. Mama akatabasamu na kumwambia mwanaye, sawa. Lakini siku nyingine ukishatoa panadol ukumbuke kufunga pharmacy๐๐
Recent Comments