Vichekesho Vya Katikati Ya Wiki
Angalia hawa vichaa walichokifanya, Vichaa bwana, ni noma!
Vichaa walipanga kutoroka, wakakubaliana wamnyonge mlinzi watoroke!
Walipofika getini wakakuta geti lipo wazi na hakuna mlinzi, wakasema “Turudi mipango yote imevurugika…
Soma hii, kama wewe ndio mzazi wa huyu msichana ungefanyaje?
Wewe ni mzazi mwanao anasoma kidato cha tatu mkoani umemsafirisha leo kwenda shule baada ya masaa matano ukasikia gari alilo panda mwanao limepata ajali wamekufa watu wote upo ktk harakati za kuandaa msiba,
mwanao anakupigia simu baba/mama mimi mzima sijafa mpenzi wangu ABDUL aliniambia nishuke Chalinze ili niwe nae kwa siku mbili alafu niende shule je, wewe mzazi unge mfanyaje mwanao?
Angalia anachojibu huyu babu. Wazee wengine bwana
Babu: Mjukuu wangu ngoja nikusimulie hadithi ya mimi babu yako kwenye vita ya kagera
Mjukuu: Niambie babu
Babu: Kwenye vita ya kagera tulienda sehemu tukakamatwa wote askari na maadui wakatuambia chagueni kuuliwa au kubakwa.
Mjukuu: Sasa babu wewe ulichagua nn?
Babu: Niliuliwa!!!
Mzunguko wa elimu kiafrikaafrika
01.👉 Wale wanafunzi walioongoza Mashuleni, wanaenda kwenye Engineering na Medical school.
02.👉 Wale waliokuwa wa pili, wanachukua MBA na LLB na kuja kuwa Mameneja wa wanafunzi walioshika nafasi ya kwanza.
03.👉 Wale waliokuwa wa tatu, wanageukia Siasa na kuwaongoza wote hapo juu. Yaani wa kwanza na wa pili.
04.👉 Wale waliofeli, wanaenda Jeshi, hawa wakigoma, basi hao wa juu wote hawana raha.
05.👉 Wale waliopata Zero na waliokataa shule wanakuwa waganga wa kienyeji, wote hapo juu watamtafuta huyu, pale mambo yao yanapokwenda kombo. Tuache kudharauliana, kila mtu ni boss akiwa kwenye nafasi yake. 😂😂😂😂😉😆😆😆🏃🏃😜😜😜😜😜
Hakuna mtu mwenye mbio duniani kama huyu
HAKUNA MTU MWENYE MBIO, KAMA MSICHANA ALIYEPAKA MAKE UP ALAFU MVUA INYESHE….. 😂😂
Makonda wana mambo, Kila mtu ni ndugu yao
Hakuna m2 mwenye ndugu wengi kama konda wa daladala.
Utasikia,
“HAYA, DADA HAPO MBELE, MJOMBA KULE MWISHO.
MA-MDOGO UNAENDA?,
NGOJA ASHUKE BIBI.
HAYA SHEMEJI UMEIKUTA YA KUWAH.
Babu njoo ukae!
Baba angu hapo tusogee kidogo,
Shangazi maliza ngazi,
Swaiba geukia mbele,
Kaka hapo shika upande wa pili,
Mdogo wangu mpishe Ma Mkwe akae.
Subiri Shemeji yako apande…
Duh… makonda noma…!!
Madhara ya kwenda baa na mke ndo kama haya
Jamaa alienda Bar na mke wake wa ndoa wakakaa kwenye viti, wakati wanasubiri vinywaji akapita binti mmoja anayejiuza akamsogelea yule mke wa jamaa
akamnong’oneza:- “AKULIPE KABISA KABLA HUJALALA NAYE, NI MGUMU KULIPA HUYOO!!.
HALAFU HUWA HATUMII KONDOMU…”
Unajua ni nini kilitokea?
Misemo 10 bora ya kuchekesha itakayokuacha mdomo wazi
1. Mwanaume hata awe bahili vipi, hawezi kumpa mwanamke mimba nusu.
2. Hata uwe na magari mangapi chooni utaenda kwa miguu.
3. Kama ubinadamu kazi mbona hatupewi mishahara?
4. Ukichanganya wali na choroko unapata mseto, lakini hautibu malaria.
5. Hata njiwa nae ana makinda, lakini hawezi kuwa spika wa Bunge.
6. Hata uwe na haraka vipi kwenda Zenj, huwezi kupanda Jahazi ya Yusuph Mzee.
7. Umeme hauna kiuno lakini unaongoza kwa kukatika.
8. Hata uwe kauzu vipi, huwezi kujamba wakati unatongoza.
9. Hata uwe na imani kali vipi, huwezi kusali wakati unafanya mapenzi.
10. Hata kizibo ni mfuniko lakini hauwezi
kufunika sufuria.
Huu ndio uchawi unaweza kufanyika siku mpenzi wako akikutambulisha kwao
😂😂😂😂😂
*UCHAWI* ni nini?
`Uchawi ni pale mpenzi wako anapokupeleka kwao kufika tyu ghafla unakutana na dada yake getini ambaye alikuwa ni mpenzi wako wa zamani, ile kuingia ndani unamuona kaka yake ambaye mlipigana baada ya kukufumania na mke wake, hujakaa vizuri unamuona mama yake ambaye ndiye jimama shangingi lako anayekuweka mjini akupaye jeuri ya kutamba ambapo hata gari unalolitumia alikupa yeye na hataki upajue anapoishi, wakati unataka kuondoka unakutana uso kwa uso na baba yake ambaye alikuwaga wakili wako kwenye kesi ya ubakaji`
🤣😂😂😂😂🤣
SMS Mafua ndiyo hii
JE UMESHAWAHI KUONA SMS MAFUA?
Cheki hii hapa……..
“Mabo dugu yagu mziba? Bwada nasubuliwa sada na bafua baka dashindwa kuadika beseji do hayo dugu yagu.
Diobeeni dipone
😂😂😂😂😂😂😂😂
Hapana Chezea
Bafua
Kilichotokea nikiiwa namsaidia mtoto home work
Kusaidia Mtoto wa Nursery Homework ni Ngumu. Unamuuliza “Nina Pipi Tano, nikiwagawia Watoto Watatu, kila mmoja Pipi Mojamoja nabakiwa na ngapi? Anakwambia, “toa Kwanza nizione..”😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Jambo la kufanya kama binti alikuachaga zamani na sahizi anakutaka
Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana
..unaenda kuoga, unakumbuka kuwa umesahau sabuni…unaenda kuchukua sabuni kurudi bafuni, unakuta ng’ombe amekunywa maji yote..unaamua kufuata mengne,unarudi unakuta mbuzi kala sabuni…😂😂😂😂
Huu mchezo hautaki makeup
Mama mwenye nyumba anajipodoa anashinda saloon kujipodoa lakini house girl hata mafuta usoni hapaki lakini akipita na khanga yake moja tuu nyumba inatetemeka😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂 huu mchezo hautaki mekapu
Raha ya kuoa kijijini
Kuoa vijijini raha sana Hata ukiulizwa unafanya kazi gani ukiwaambia mimi ni admin basi daaaah wanaona wewe ni bonge la boss😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Baada ya mwanamke kukataa kufungua mlango angalia kilichomkuta
MUME: Fungua mlango!
MKE: Leo sifungui! Nimechoshwa na ulevi wako.
MUME: kama hufungui najitupa kwenye hili shimo nife kabisa.
MKE. Kufa huna faida yoyote duniani!
MUME kachukua jiwe kubwa kalitupa kwenye shimo chubwiiiiiii!
MKE kajifunga kanga, kafungua mlango. Ghafla mume kaingia ndani na kumfungia mke nje.
MKE: Nifungulie la sivyo nitapiga kelele majirani waje.
MUME: Piga kelele na wakija uwambie unakotoka usiku huu na khanga moja.
Huyu Baba ni noma, Cheki anachomjibu huyu mtoto wake
Mtoto: baba eti Botwasna ipo wap?
Baba: angalia itakuwa humo humo kabatini maana mama yako nae kwa kuficha kuficha vitu hajambo…
Mapenzi Stress tupu
Stress Tupu
Unapokea Sms kwa mpenzi wako anakuambia
“Kuanzia Leo Mimi Na wewe Basi! ????”
Unashtuka ??…. Una muuliza kulikoni? ????
Anakujibu: “Sorry Sio Sms yako?”
Hapo Ndo utajua Kwanini Hakuna Mmasai Albino??????
Angalia kilichomkuta huyu msanii wa mziki na mashabiki wake
Msanii mmoja anaitwa ”KINYA” alikuwa ana perfom jukwaan..!!!
Kawaida kila msanii lazima ajitambulishe, mfano:-
”YEAH NI TEMBA hapa au
YEAH NI CHEGE hapa…!!!
Yeye akasema: “YEAH NIKINYA HAPA…!!!”
Watu wakapiga kelele ”UTAZOAAA” mwenyewe bwenge wee
JE, WEWE UNGEJITAMBULISHAJE NAITAJI JIBU LAKO TUONE♥
Ukata wa January
Boss;- kwa nini umechelewa kazini
Juma;- kuna mtu njiani alidondosha elfu1
Boss;- ohhoh kwa hiyo ulikuwaunamsaidia kuitafuta
Juma;- hapana nilikuwa nimeikanyaga
😃😃😃😃😃😃😃😂😂😂😂😂😂😂
Recent Comments