SMS Nzuri: Meseji za Visa Vya Desemba
Angalia Kiingereza kilivyoniponza
Shikamoo kingereza..!
Baada ya kufika Kempiski nikaona menu imeandikwa:
Sauteed white corn, rare lucy beans, garnished with rift potatoes & topped with organic unprocessed guacamole!
Price: TSH 44,000/=
Nikaagiza!
Nilipoletewa ndio nagundua kwamba: ni makande na parachichi ..🤔
hapo ndo unagundua mwalimu wa kiingereza alikuwa sio mtu wa mchezo mchezo🤒💨
Huyu panya wa tatu ni noma
🐀 🐀 🐀 Panya watatu walikua wakibishana nani Ni noma zaidi
Panya 1: jamani mimi ni noma Wiki hii nimekula rat rat(sumu ya panya) mara tatu na sijadedi !!!
Panya 2 Wewe unasema nini, mimi nimekula nyama ikiwa
kwa mtego mara 5 nasijawahi dakwa
RAT 3 Mmemaliza? Mie hata sijui mnabishana nini? Mimi hii mimba niliyo nayo ni ya paka !!!
Panya WA 1 na 2 wakazimia😆😆😆😆😆
Panya wa 3 huwa hapendi ujinga kabisa
Madenge hakosi visa. Soma hii
MADENGE
HAKOSI
VISA
baada ya kumaliza form four baba akamwambia achague zawadi yoyote aipendayo
MADENGE: naomba pesa nikamuoe bibi maana siku nyingi amekuwa akiniita mchumba wake.
BABA: Shenzi, yule ni mama yangu mzazi huwezi kumuoa.
MADENGE: Mbona wewe umemuoa mama yangu mzazi sijasema kitu ww inakuuma? lazima nilipize kisasi ikikuuma muache mama yangu kila mtu akae na mamayake. 😂😂😂
Namna wazazi wanavyoongea na mabinti katika umri tofauti
Miaka 13: Usipende wavulana ni wabaya.
Miaka 18: Sitaki nikuone na yule mvulana tena!
Miaka 23: Lini utatuletea mchumba wako?
Miaka 26: Wenzio wanaolewa.
Miaka 30: Tumekuambia kwamba acha
kuchagua sana wanaume, hutaki kusikia!
Miaka 33: Kuna mtu wa Mungu yupo kule
anaombea unaweza kupata mchumba
Miaka 36: At least pata mtoto mmoja.
Miaka 39: We will take care of all the wedding
bills…yeyote ni sawa sisi tutagharamia kila kitu mwanetu wee mlete tu .
Miaka 45: hivi kweli nani alikuroga.?
😂😂😂 changamkia fulsa umri ukifika
Utoto raha..! Angalia hawa watoto wanachokifanya sasa
Leo nimepulizia Air Fresh yenye Harufu ya Pilau nyumbani kwangu sasa watoto wa Jirani wamehamia Mlangoni kwangu ndio wanacheza hapo. Kila nikitoka wananisalimia. Mama yao ndio kanimaliza kabisa nimetoka akaniambia
“Kumbe wewe ni Mpishi mzuri, Hongera”
Imebidi nisirudi nyumbani maana wale watoto wanaweza kuingia ndani kabisa na pilau hakuna.
#UTOTO RAHA 😂
😂😂😂😂👆🏻👆🏻👆🏻
Angalia walichofanyiana hawa wanadoa, Kati ya huyu mme na mke nani zaidi?
MUME wakati anakata roho huku mkewe akiwa amemshikilia alisema mke wangu, mi natubu kwako, kwani nilifanya mapenzi na dada yako, mdogo wako, rafiki yako na mama yako
MKE akamnong’oneza mume wake na kumwambia mbona mimi nayafahamu yote, ndio maana nimekupa sumu ili na wewe ujue uchungu wake. JE NANI ZAIDI?
Angalia huyu ticha wa Hesabu alichofanyiwa
Looku Looku* 👀👀
*Ama Kweli Mkuki Kwa Nguruwe kwa Binadamu Mchungu Skia Hii….!!*
*Ishawahi kutokea Pale nilipokutana njiani na mwalimu aliyekufundisha MATHS secondary afu akaniambia nimuelekeze njia ya kwenda sehemu fulani.*
*_Nenda mbele kama 2KM hivi kisha kata kushoto,ila hakikisha ANGLE inakuwa ni 30.5 KUSINI MASHARIKI.Kisha tumia PYTHAGORAS na hakikisha una FOUR FIGURE ili kupata thamani ya ANGLE._*
*Mwalimu alisonya na kuondoka.*😏😏😏😒😒
*Stakagi ujinga kabisa mimi, wakati ananichapa alifikiri sifa*😂😂
😅🙌🏽🙌🏽 *Mniache Tuu Mimi Sio Kwa Bifu Ilo Aiseee*🏃🏾
Cheki nilichomfanyia boss wangu
Bosi wangu karudi safari yake kutoka serengeti..! Si akanitumia picha, lakini ilikuwa network yenyewe tabu.. kwahio picha haikufunguka na kwa vile niliona itachelewa kufunguka na ataona sikumjibu basi nami..
Nikampelekea msg nikamuandikia umependeza saana bosi mashaallah…!!
sasa baada tu ya kumfika msg.. na huku picha ikafunguka kumbe picha ya Sokwe..!!
Basi Kaniambia kesho niende ofsini kwake kuna barua yangu..
Nahisi hyo barua ina pesa, hapa cjalala, nmekosa usingizi kabisa,nawaza ninunulie nn hyo pesa.Na kesho asubuhi sa 12 asubuhi atanikuta ofisini kwake naisubiri barua, sipendagi ujinga mimi.
Nani Mkali Hapa kati ya DEMU na MSHIKAJI?
“MAENEO FLANI ya KISHUA”
-Mshikaji kamwona demu mkali
anakatiza kitaa akamkubali akaamua
amfuate amtemee cheche
MSHIKAJI- mambo dada?
DEMU- pouwa
MSHIKAJI-
umependezaa!!!
DEMU- asante.
MSHIKAJI- unaweza ukanisaidia
namba
yako ya simu……..
maana duh
nmekukubali
kinyama.
Demu baada ya kuambiwa vile
akazama kwenye pochi lake akatoa
noti ya
sh.10000 akaandika namba yake
kwenye
noti akampa mshikaji.
Mshikaji kapokea ile noti kachana
sehem
iliyoandikwa namba halafu
kamrudishia
Demu noti yake..!!!
NANI ANA DHARAU
NA NANI JEURI..
DEMU AU MSHIKAJI??!
Haya ndiyo madhara ya kulala kanisani
Tukiwa kanisani mdada alikuwa amelala , akaamka akasikia Pastor anasema
” SIMAMA”
Yule dada akasimama akashangaaa kanisa zima linamtizima kwa mshangao akiwemo mumewe, akaangalia kanisa zima akashtuka kujiona yeye peke yake ndiye aliesimama
Pastor akaendelea vizur endelea kusimama, tumepata mmoja hadi sasa aliyesimama narudia kwa mara ya mwisho kama hujasikia vizuri
” kama wew umewahi kumsaliti au bado unasaliti ndoa yako SIMAMA”
Binti akazimia
Duh! Wanaume jamani…
Lakini sisi wanaume hatuko fair … Yani demu anang’ng’ana kujipodoa uso na sisi tunaangalia matako. 😆😆😆mungu anatuona jaman😆😆😆😆😆😆Makeup ya matako iletwe
Angalia nilichokifanya baada ya kuumwa na meno
Baada ya kuumwa na Meno nikaamua hivi.
mimi sipeñdagi ujinga,,,Nmeumwa na jino moja la chini..nimeng’oa meno yote ya chini ili iwe funzo kwa meno ya juu😡😡
Mshahara usiobadilika
PAMOJA NA HALI NGUMU YA UCHUMI NCHINI HUWEZI AMINI MSHAHARA WA DHAMBI HAUJABADILIKA HATA KIDOGO…BADO NI MAUTI VILEVILE
😊😊😊😊
Mkwe kazua mpya, Hii dunia ina mambo sana
Mama mkwe alimuuliza mkwewe “binti” samahani mbona mtoto hajafanana na mwanangu kabisa?
Binti akajibu, “bila samahani mama huku chini nina njia ya uzazi sio mashine ya photocopy”
mama mkwe hoii!! Chezea Wakwe Wa Bongo wewe.
Ndoa zina mambo, cheki haya mambo ya mtu na mke wake
Mke: mume wangu leo 2badilishe stail kwani nimechoka kla siku hiyo hiyo tu
Mme: kwel mke wang hata mimi nilikuwa nataka nikuambie hivyo hivyo
Mke: sasa stail ya leo wewe utaosha vyombo mimo nitaangalia tv
Mme: huna haya wala hujui baya…!!!
we unadhani ni xtail gani mume aldhani???
MAMBO KUMI YA KUFURAHISHA NA HUWEZI KUYAFANYA
1. Huwezi kuosha Macho kwa Sabuni;
2. Huwezi kuhesabu Nywele zako;
3. Huwezi kupumua kwa Pua na huku umetoa Ulimi;
4. Unajaribu kufanya namba 3
6. Umeona inawezekana, sanasana unakuwa Kama Jibwa;
7. Unatabasamu kwa kuwa umejiona Mjinga!
8. Umeruka namba 5;
9. Unahakikisha Kama kweli 5 haipo.
10. Unacheka kwa kuwa nimekubamba!
Angalia sababu ya mke Mtarajiwa kuzimia kabla ya harusi
*Jihadharini* na wachapaji wa kadi za harusi. Hakikisha unasoma maandishi yaliyochapwa kabla ya kadi kuchapwa na kusambazwa!
Mchapaji aliombwa aweke 1 Yohana 4:18 katika kadi ya harusi lakini mchapaji kwa makosa aliweka Yohana 4:18.
1 Yohana 4:18 panasema, “Katika pendo hakuna hofu, lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu…”
Lakini Yohana 4:18 tunasoma, “Kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako.”
🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃😂😂😂😂_MKE MTARAJIWA AKAZIMIA HAPA, TUNAMPEPEA_
Ungekua wewe ni mwalimu ungemshauri nini huyu mwanafunzi?
Mwalimu aliingia darasani na kuwauliza wanafunzi juu ya ndoto zao za baadae.
MWAL: John we unataka ukiwa mkubwa uwe nani?
JOHN: Nataka niwe daktari wa moyo niwasaidie watanzania wanaougua magonjwa ya moyo.
MWAL: vizuri. Na wewe Rose unataka kuwa nani?
ROSE: Nataka kuwa rubani, niweze kusaidia watu wanapenda kusafiri kw anga.
MWAL: Safi sana Rose. Utakua utakua mfano kwa wasichana wenzio kuwa na bidii kwenye masomo ya sayansi.
MWAL: Na wewe James??
JAMES: mimi nataka kuwa tajiri mkubwa sana. Niwe na nyumba Tanzania, S.Africa, Marekani na Dubai. Niwe na gari 7 za kutembelea. Kila siku nabadilisha. Leo nikipanda hii, siirudii hadi week iishe. Nataka niwe namiliki viwanda, Makampuni, ndege binafsi na mashamba makubwa. Nataka niwe na nguvu serikalini ya kuamua nani awe Rais na nani asiwe……”
Akameza mate kisha akaendelea….
“Nataka kuwa na walinzi 20 wenye silaha nzito wakinizunguka, na watumishi wakininyenyekea. Nataka kuwa bilionea ninayeogopwa. Lakini pia nataka kuwa na mke mzuuuri sana ambaye nitakuwa natembea nae kila mahali.”
MWAL: ndoto nzuri sn lakini unahitaji bidii sana kutimiza. Haya na wewe Jenny tueleze unataka kuwa nani??
JENNY: Nataka kuwa mke wa James.!!
Ungekua wewe ndio baba wa Huyu mtoto ungemjibu nini?
MTOTO: Hivi Baba wewe umezaliwa wapi?????
BABA: Mbeya
MTOTO: Mama nae kazaliwa wapi????
BABA: Tanga
MTOTO: Mimi jee?????
BABA: Dar
MTOTO: Sasa tulikutanaje????
😂😂 hapo wee kama baba ungemjibuje mwanao😳😳😳
Recent Comments