SMS Nzuri: Meseji za Vihoja Vya Vijana
Kapresha kakiamua kuja kanakujaga tuu, cheki kilichompata huyu mme wa mtu mpenda michepuko
Kimchepuko chako kinakuandikia meseji kama hii…
…Samahani baby kama unavyojua nimeokoka ,nimetubu kanisani lakini nabii kaniambia niwaombe msamaha wote niliowakosea.
Nimemkosea sana mkeo kwa kumwibia mumewe na nimepanga kuja kumwomba msamaha kesho ntakuja na nabii na Mchumba wangu mpya nilie mpata kanisani.
Samahani kwa usumbufu uliojitokeza lakini hilo ni kwa ajili ya utukufu wa bwana!!!
Wako Manka wa Magorofani😅😅
Angalia huyu mtoto anachomjibu baba yake baada ya kutoka kwenye mtihani
BABA: mwanangu kwenye huu mtihani uliofanya natumaini utafanya vizuri.
DOGO: ndio baba nitapata mia kwa mia.
BABA: kwanini unasema hivyo?.
DOGO: kwasababu jana kanisani tulifundishwa “Yesu ni jibu” kwahiyo kote nimejaza Yesu.
BABA: kwel kazi ipo
JE UNGEKUWA WEWE HUYO NDO MWANAO UNGEMFANYAJE?
Mjini shule. Soma hii
Kuna mdada nilimkopesha pesa kwa ahadi kuwa baada ya wiki moja atanirejeshea pesa zangu.
Baada ya wiki moja nampigia simu hapokei simu zangu, nimempigia zaidi ya mara kumi (10) bila ya mafanikio!
Kila nikimpigia simu hajibu simu zangu, nikahamua kumwandikia message kwa WhatsApp…!
_Hello Mamu, Nakupigia simu sio kukudai pesa zangu, ila nataka kukwambia kuwa hapa Ubungo Plaza kuna wadada wawili walikuwa wanapigana kumgombea Mumeo (Baba Nang’oto). Ilikuwa vuta nikuvute na mumeo alikuwa kasimama tu anawaangalia akitabasamu. Baada ugomvi kwisha akaondoka na mmoja wao na kumwacha yule mwingine akitukana matusi kama ana akili nzuri._
—
_*Kisha nikaituma ile message*_
Baada ya dakika kama mbili hivi, akanipigia simu nami wala sikupokea simu yake… Akapiga tena na tena kama mara ishirini hivi wala sikupokea.
*Akatuma message akiniuliza…*
_Hao wanawake unawajuwa, …mume wangu na huyo mwanamke wameelekea wapi, wewe unawajuwa hao wanawake waliopigana, yaani hapa nimechanganyikiwa kwa kweli…!_
Nikaisoma message yake wala sikuijibu, nikamchunia kimyaaa…!
Akanipigia tena simu mara tano, sikupokea simu zake, kimyaaa…! Akaniandikia message nyingine….
*…Nakupigia jamani pokea simu basi nina pesa zako nataka nikupe… Naomba basi tukutane mjini unihadithie vizuri…!*
Nami nikamjibu…
_Nitumie hizo pesa kwenye Namba yangu ya Mpesa, ili nipitie sheli kujaza mafuta nije mjini kukupitia nikupeleke mahala walipo…!_
Baada ya dakika 2 message ikaingia, kuangalia balance yangu ya Mpesa, nikakuta kaingiza pesa zangu zote ninazo mdai…!
Nikazima simu nikajilalia zangu kimyaaa…. Kama sio mie!
Angalia sababu ya mke Mtarajiwa kuzimia kabla ya harusi
*Jihadharini* na wachapaji wa kadi za harusi. Hakikisha unasoma maandishi yaliyochapwa kabla ya kadi kuchapwa na kusambazwa!
Mchapaji aliombwa aweke 1 Yohana 4:18 katika kadi ya harusi lakini mchapaji kwa makosa aliweka Yohana 4:18.
1 Yohana 4:18 panasema, “Katika pendo hakuna hofu, lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu…”
Lakini Yohana 4:18 tunasoma, “Kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako.”
🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃😂😂😂😂_MKE MTARAJIWA AKAZIMIA HAPA, TUNAMPEPEA_
Angalia huyu polisi kitu alichonijibu
Nimefika hapa Polisi Station nimefarijika sana na Kustuka baada ya kumkuta Askari hapa Kaunta anasoma Biblia nikajisikia fahari kuona anasoma neno kituo cha Polisi. Nikamuukiza Afande ni Nani alimuua Goliathi? Akasema Muulize Afande Mwita mlango namba 2 ndo anausika na Kesi za Mauaji.😂😂
Ufugaji wa nguruwe kazi, Cheki jamaa hawa wake walivyompa mtihani
MWANAHARAKATI: Hawa nguruwe unawalishanini?
.
MFUGAJI: Nawalisha mabaki ya chakula toka migahawa mbalimbali
.
MWANAHARAKATI: Hayo ni makosa unawatesawanyama kwa kuwalisha chakula kichafu. Akapigwa faini… Baada ya siku chache wakaja wanaharakati toka Umoja wa Mataifa
.
MWANAHARAKATI: Hawa nguruwe unawalisha nini?
.
MFUGAJI: Huwa nawaanzia siku na uji wa ulezi, halafu mikate, mchana ugali kwa kabeji na usiku viazi
.
MWANAHARAKATI: Loh watu wanakufa kwa njaa wewe unalisha nguruwe, akapigwa faini….siku chache baadae wakaja wanaharakati wa Mazingira
.
MWANAHARAKATI: Hawa nguruwe unawalisha nini?
.
MFUGAJI: (Kwanza akasita kidogo) Hawa huwa nawapa shilingi alfu tano kila mmoja kila siku halafu wao wenyewe wanaenda kununua chakula wanachokitaka.. .
Ndege ya Tanzania
Kuna maprofesa 40 walipanda AIR TANZANIA ili wasafari. Kabla ndege haijaanza kuondoka, Lilipita tangazo kama ifuatavyo:
Ndugu wasafiri wote, ndege unayotarajia kusafiri nayo imetengenezwa na wanafunzi wa Kitanzania.
Baada ya tangazo maprofesa wote waliteremka isipokuwa mmoja alibaki kwenye kiti chake
Walipomuuliza ni kwanini hakuondoka akajibu kwa haraka na furaha kuwa:
Kama ndege hii imetengenezwa na watanzania, hata kuwaka haitawaka!
Angalia huyu bibi alichotufanyia kwenye gari
tulikua kwenye gari kibao ad wengne mlangon likasmimama kituo kimoja kulikua kuna bibi anataka kupanda
Konda- bibi twende sit kibao ata utalala
Bibi – oooh sawa mjukuu
Konda – simama tu apo wanashuka mbele
Bibi – akacheka sana tu
Konda- mbona unacheka bibi
Bibi – mjukuu hawa wote hawashuki wanakufa apo mbele
Watu- simamisha gar
Saiv bibi kabaki mwenyewe amelala sit ya nyuma😆😆😅😂😂
Lugha za namba ni noma
Leo kuna mdogo wangu nimemtumia meseji nimemuomba aniazime chaja yake ya simu. Akanijibu 21002 Nikawa mkali nikamuambia kuchajia mara moja tu ndio HELA yote hio si bora nikanunue Chaja yangu mpya. Akaniambia nimesema TUMIA TU 😂😂mtatuua na lugha zenu😜
Unakumbuka haya enzi za shule?
Kama umesoma st Kayumba utakuwa una aidia na haya…
1.Unaenda shule umechelewa unakuta mwalim anakamata wachelewaj unaamua urudi nyumbani
2.unachukua kimbegu cha ubuyu unasugua sakafuni af unamuunguza mwenzio
3.mkiruhusiwa tu unakimbia unataka uwe wa kwanza kwenye njia yenu y kurudia nyumban
4.MTU akikukera unamfungia shule (mnapigana baada ya kufunga shule)
5.MTU akikunyima kitu chake unamwambia “Ahaa eeh utaona sa nne”
6.wadada wembamba ndo wanaongoza kwa kusuta wenzao
7.ukiibiwa daftar jipya unalia kuliko hata uliloandika
8.unajaza mapeni kwenye mkebe(compass) na mengine hayaandiki
9.vifaa vingine kwenye mkebe hujawahi hata kuvitumia mfano bikari labda utolee mwiba😂
10.hakuna habari nzur kama kuambiwa Leo hamna shule mwalim haupo
11.habari mbaya zaidi n kurud nyumban kutoka shule una njaa af unaambiwa chakula mgeni kaja tumempa
12.mtoto wa mwalim utamgundua tu kwanzia sweta begi na viatu vyake
13.usiombee umpige mtoto wa mwalim utataman uache shule
14.unatengeneza kifutio cha ndala af unatishia eti kinafuta hadi peni😂
15.ukaguzi na huna ufagio.. unaomba chelewa kwa watu af unaongeza kijiti katikati
16.siku ukienda na ufagio wanakagua maji, ukienda na naji wanakagua kuni au mbolea😆
😂
Dah shule zetu hizi kiboko!!
Ipi umeipitia wewe
Share na wengine
Hyuyu daktari ni noma, cheki anachokisema
Kuna Daktari wa Moyo alifariki wakamchongeaa jeneza lenye umbo la Moyo. Ghafla Daktari mwingine akaanza kucheka, watu wakamuuliza “kwanini unacheka unafurahia mwenzako kufariki?” Daktari yule akajibu “hapana mimi ni Daktari wa kutahiri nafikilia nikifa mtanichongea jeneza lenye umbo la ….”
Angalia huyu mgeni anachokifanya, wageni wengine ni hatari
Hata kama ni Mgeni this is too much.
Mwenyeji: Karibu mgeni karibu ukae,utapenda chai au soda?
Mgeni: Nipe nianze na soda wakati chai inachemka.
Mwenyeji: Utakunywa fanta au sprite?
Mgeni: Nipe fanta wakati sprite inapoa.
Mwenyeji: Utakunywa na keki au mkate?
Mgeni: Nipe keki mkate nitanywea chai ikishachemka.
Mwenyeji: Utapendelea ndiz au machungwa,
Mgeni: Nipe machungwa ndizi ntakula na wali
mchana.
Chezea mgeni ww.!!!
Cheki tabia za kuandika vimaneno vya ajabuajabu kwenye pikipiki na bodaboda ilivyomponza huyu
Jamaa mmoja dereva wa bajaji alianguka, sasa bajaji ikawa imem’bana akawa anafurukuta bila mafanikio Cha ajabu watu wakawa wanampita bila kumsaidia, Kumbe Nyuma ya Bajaji yake alikua Kaandika “NIACHENI KAMA NILIVYO, HII NDIO STYLE YANGU” 😂😂😂 Mpaka sasa nimemwacha bado yuko hapo *Sipendagi Ujinga mimi* 🚶🏽🚶🏽🚶🏽🚶🏽🚶🏽
Angalia kilichojiri katika semina ya wanandoa kuhusu upendo
Kulikuwa na semina ya wanawake kuhusu namna ya kuishi kwa upendo katika ndoa.
Mwalimu aliwauliza ni wangapi wanawapenda waume zao? Wote wakanyoosha mikono kama ishara ya kuwa wanawapenda waume zao.
Mwalimu akauliza tena, “Ni lini mara ya mwisho umemwambia mumeo “Nakupenda Mpenzi”?
Majibu yalikuwa kama ifuatavyo:
Wengine wakisema Asubuhi ya leo,
Wengine jana,
Wengine wiki iliyopita
Wengine mwezi uliopita
Na wengine wakasema hawakumbuki!
Mwalimu aliwapa kazi kila mwanasemina achukue simu yake na kumtumia mume wake meseji yenye neno “NAKUPENDA MPENZI”
Baada ya meseji kwenda aliwaamuru kubadilishana simu kila mtu na jirani yake.
Kila mwanasemina aliambiwa kusoma meseji za majibu kwenye simu aliyoshika
Simu ya 1 – “Samahani, nani mwenzangu”!
Simu ya 2 – “Samahani, wrong number”!
Simu ya 3 – “Si nimekuambia usinitumie messages kwenye namba hii”!
Simu ya 4 – “Mh! leo mvua itanyesha”!
Simu ya 5 – “Nikija tutaongea zaidi”!
Simu ya 6 – “……Imedhibitishwa umepokea Tsh300,000 kutoka kwa ……”!
Simu ya 7 – “Me too”!
Simu ya 6 – “Huu ujumbe ndio ulikuwa unamtumia huyo hawara yako ee, leo utanikoma”!
Huyu Baba ni noma, Cheki anachomjibu huyu mtoto wake
Mtoto: baba eti Botwasna ipo wap?
Baba: angalia itakuwa humo humo kabatini maana mama yako nae kwa kuficha kuficha vitu hajambo…
Haya ndiyo madhara ya kutowapeleka watoto kanisani ⛪
MTOTO aliibiwa yeboyebo KANISANI akawa analia sana kwa uchungu mpaka MCHUNGAJI akamwambia usilie mwachie MUNGU. MTOTO akajibu Mungu hazimtoshi zile yebo ni ndogo! Usicheke,
Huu ni Mtihani Tuwapeleke Watoto KANISANI Wamjue MUNGU.
Majibu ya mkato ya kuchekesha Kutoka Kenya
Njeri: Roysambu ni ngapi?
Makanga: Roysambu ni moja tu. Pengine kama Chinese wamejenga ingine.
Odhis: Hii gari haina watu bana.
Makanga: Kwani hao wawili wenye wamekaa hapo ndani ni ng’ombe?
Man: Wekeni nyimbo za Yesu tafadhali.
Makanga: Yesu bado hajatoa album. Akitoa tutaeka.
Mwikali: Excuse me conda…gari za Mwingi zinapandiwa wapi?
Makanga: Ziliacha kupandwa juu hazimei.
Man: Kwani mwisho wa gari ni wapi?
Makanga: Mwisho ni hapo penye number plate iko.
Karis: Ruaka ni how much?
Makanga: Sijaskia Ruaka ikiuzwa. But nikiskia nitakwambia.
Passenger: Shukisha dere.
Makanga: Tukishukisha dere utaendesha gari?
Johnny: Maze, hii gari iko na joto sana.
Makanga: Basi shuka upande fridge
Recent Comments