Hapa itakuaje?
NAJISIKIA NIMEBOEKA…
SIJUI NIENDE KAMBI YOYOTE YA JESHI NITEREMSHE BENDERA
ALAFU NITOKE MBIO…..
😜😜😜😜😜🏃🏾🏃🏾🏃🏾🏃🏾🏃🏾🏃🏾
NAJISIKIA NIMEBOEKA…
SIJUI NIENDE KAMBI YOYOTE YA JESHI NITEREMSHE BENDERA
ALAFU NITOKE MBIO…..
😜😜😜😜😜🏃🏾🏃🏾🏃🏾🏃🏾🏃🏾🏃🏾
MLEVI mmoja aliingia baa akavuta kiti na kukaa mhudumu akatokea kumsikiliza.
MHUDUMU: Nikusaidie nini?
MLEVI: Eeh! nipe bia ya baridi kisaha wasikilize wote waliokaa hapa, wape bia na wao maana sipendi kunywa pombe wengine wananiangalia
Akaja mhudumu wa jikoni “nikusaidie nini?”
MLEVI: Niletee supu kisha wasikilize wote waliokaa hapa na wao wape supu sipendi kunywa supu watu wananiangalia
Safari hii watu wakapiga makofi
Baadae akamuita mhudumu
MLEVI: Niandikie bili zangu kisha waandikie wote bili zao sipendi kulipa huku watu wananiangalia
Wale wateja wakamvaa na kumshushia kichapo… teh teh teh teh teh hii kali hakuna cha bure mjini hahahaha na jasho la mtu haliliwi wandugu
Mwili wa binadamu unafanya mambo
mengi ya kibaiolojia ambayo mara
nyingi ni vigumu kuyaelewa. Mwili una mifumo mbalimbali ya ulinzi ambayo inatulinda na hatari zinazoweza kutudhuru. Mifumo hiyo
inatulinda masaa 24 ya siku, Siku zote 7 za wiki, katika mambo yote
yanayoweza kuhatarisha maisha yetu.
Yafuatayo ni mambo yanayofanywa
na mwili ambayo ni kati ya hiyo
mifumo ya ulinzi wa mwili wa
binadamu.
1. KUPIGA MIAYO (YAWNING)
Lengo kubwa la kupiga muayo ni
kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi
kwenye ubongo au baada ya ubongo
kuchoka kufanya kazi.
Vile vile kama ukiwa umechoka au una
njaa husabababisha oxygen
kupungua kwenye damu na kwenye
mapafu, hii hupelekea tatizo la
kupumua, hivyo kupiga miayo
husaidia kuingiza oxygen ya ziada
mwilini ili irudishe mwili katika hali
yake ya kawaida.
2. KUPIGA CHAFYA (SNEEZING)
Mara nyingi tunapiga chafya pale pua
zetu zinapokua zimejaa bakteria wa
magonjwa ambao hawahitajiki
mwilini, Vumbi pamoja na takataka
mbali mbali zilizoingia kupitia pua.
Hivyo kupiga chafya ni kitenda cha
mwili kujisafisha kwa kuyatoa hayo
matakataka nje yaliyoingia mwilini.
3. KUJINYOOSHA (STRETCHING)
Kuninyoosha mwili ni kitendo kisicho
cha hiari ambacho lengo lake ni
kuuandaa mwili kwa ajili ya kazi
mbalimbali za kutumia nguvu
utakazokabiliana nazo kwa siku nzima.
Lakini pia kujinyoosha kunaipa misuli
ya mwili mazoezi na kuiweka sawa
vilevile kunarudisha mzunguko wa
damu katika hali yake ya kawaida na
kumtoa mtu katika uchovu.
4. KWIKWI (HICCUPING)
Najua umewahi kupata kwikwi, na
mara nyingi mara baada ya kumaliza
kula chakula. Je umeshawahi kujiuliza
ile sauti ya ajabu ya kwikwi
inasababishwa na nini au kwa
sabababu gani watu hushikwa na
kwikwi?
Hiyo yote husababishwa na
DIAPHRAGM (tamka DAYA – FRAM)
kiungo kinachopatikana ndani ya
mwili wa binadamu chini kabisa ya
kifua baada ya mapafu(lungs). Kazi
kubwa ya diaphragm ni kusaidia katika
upumuaji, (inhale) na (exhale). Pale
unapoingiza hewa ndani (inhale)
diaphragm hushuka chini ili kusaidia
kuivuta hewa ifike kwenye mapafu. Na
unapotoa hewa nje (exhale)
diaphragm hutulia kwa kubakia
sehem yake ili kuwezesha hewa chafu
kutoka nje kupitia pua na mdomo.
Sasa basi, kuna wakati diaphragm
kubugudhiwa na kuisababisha
kushuka chini kwa kasi sana jambo
linalosababisha wewe kuvuta hewa
(inhale) kwa kasi isiyo ya kawaida
kupitia koromeo la sauti, hewa ikifika
kwenye box la sauti (larynx), sehem
hiyo hujifunga kwa haraka sana ili
kuzuia hewa isipite huko na ndipo
KWIKWI hutokea.
Mambo mengine yanayoweza
kuibugudhi diaphragm na
kuisababisha kufanya kazi vibaya
mpaka kupelekea kwikwi ni kitendo
cha kula haraka haraka au
kuvimbewa.
5. KUJIKUNJA KWA NGOZI YA VIDOLE
VYA MIKONO BAADA YA KULOWA AU
KUKAA MUDA MREFU KWENYE MAJI.
Je umewahi shuhudia jinsi ngozi ya
vidole vyako inavyojikunja baada ya
kufua nguo muda mrefu au kushika
maji muda mrefu? Unajua ni kwa
sababu gani ngozi hujikunja kama ya
mtu aliyezeeka angali yu kijana mara
baada ya kukaa sana kwenye maji?
Watu wengi kabla walizani kwamba
kujikunja kwa ngozi hiyo hutokana na
maji kuingia kwenye ngozi na hivyo
ngozi hujikunja baada ya kulowa.
Lakini wanasayansi baada ya kufanya
utafiti kwa muda merefu juu ya nini
hasa hupelekea ngozi kujikunja?
Walisema HAPANA si kwa sababu ya
ngozi kulowana. Na walikuja na
majibu haya.
Mwili unapokutana na majimaji mara
moja hupeleka taarifa na kutafsiri
kwamba mazingira hayo yana UTELEZI
(Slippery) hivyo kutasababisha mikono
kushindwa kushika (Grip) au kukamata
vitu kwa urahisi kutokana na utelezi
huo. Hapo mwili huchukua hatua ya
haraka kuikunja ngozi ya mikono yako
ili kurahisisha ushikaji wa vitu
vinavyoteleza ndani ya maji pamoja na
kutembea kwenye utelezi.
6. VIPELE VIPELE VYA BARIDI KWENYE
NGOZI (GOOSEBUMPS)
Kazi kubwa ya vipele hivi ni kupunguza
kiasi cha joto la mwili linalopotea
kupitia matundu ya ngozi. Hivyo kwa
kufanya hivi humfanya binadamu
kutunza joto la mwili hata katika
mazingira ambayo hali yake ya hewa
si rafiki kwa mwili wa mwanadamu au
ni yenye baridi sana.
7. MACHOZI (TEARS)
Zaidi ya kuwa majimaji (MUCOUS
MEMBRANE ) yanayopatikana kwenye
Macho ambayo kazi zake ni kulilinda
jicho dhidi ya kitu chochote kigeni
kinachoingia jichoni (mfano
unapokata vitunguu au mdudu
anapoingia jichoni huwa unatoa
machozi mengi eeeh!! Pia dhidi ya
upepo na moshi) na pia hutumika
kama kilainishi cha jicho pale
linapokuwa linazunguka zunguka
(blink).
Vilevile machozi yana kazi ya
kupunguza HISIA ZA HUDHUNI
zinazozalishwa mwilini. Wanasayansi
wanaamini kuwa mtu anapokua
mwenye msongo wa mawazo (stress)
mwili hutengeneza kitu kipya ili
kwenda kubugudhi na kuharibu
maumivu yote ambayo mtu anajisikia.
Hivyo machozi yanayozalishwa hapa
huwa na kemikali na yanafahamika
kama NATURAL PAINKILLER. Machozi
haya ni tofauti na machozi ya kawaida,
lengo lake hasa la kuzalishwa ni kwa
ajili ya kuondoa kabisa maumivu
yaliyozalishwa mwilini
Hivyo mpaka hapa tumeona kua kuna
machozi ya aina tatu ambayo ni
i. Basal tears (vilainishi)
ii. Reflex tears (mlinzi)
iii. Emotion tears (mtuliza maumivu)
8. KUSHTUKA USINGIZINI
(MYOCLONIC JERKS or HYPNIC JERK).
Je! Ushawahi kutokewa na hali hii?
umelala halafu ghafla unashtuka
usingizini kwa mguvu nyingi kama
umepigwa na shoti ya umeme na akili
inakurudi ghafla huku mapigo ya
moyo yakikuenda mbio? Na hali hii
ikakutokea pasipo hata kuota ndoto
yoyote?
Basi usiogope au kuwasingizia watu
uchawi, hii ni hali ya sayansi ya
mwili.na ni njia moja wapo katika ile
mifumo ya mwili kujilinda.
Je hutokeaje?
Hii ni hali ya ajabu sana isiyofanywa
kwa hiari ambayo huwatokea watu
mara tu wamejinyoosha kitandani na
kupitiwa na usingizi, mwili
hutetemeshwa na kusukumwa kwa
nguvu na mtu hushtuka katika hali
kama vile kapigwa na shoti ya umeme.
Hali hii inaweza kupelekea mtu hata
kuanguka kitandani na humwamsha
mara moja kutoka usingizini.
Wanasayansi wanatuambia kua, pale
tu unapopata usingizi kiwango cha
upumuaji kinashuka ghafla, mapigo ya
moyo nayo taratibu yanapungua,
misuli inatulia kwa ku-relax, Kitu cha
AJABU hapa ubongo unatafsiri hali hii
kama ni DALILI ZA KIFO (brain’s
misinterpretation of muscle
relaxation), hivyo huchukua hatua za
haraka za kuushtua mwili kwa
kuutetemesha au kuuskuma kwa
nguvu, hali ambayo humfanya mtu
kuamka kutoka usingizini kwa KURUKA
kitu ambacho ni hali isiyo ya kawaida.
Hali hii ikimtokea mtu huambatana na
kuongezeka kwa mapigo ya moyo
(rapid heartbeat), kuhema haraka
haraka, na wakati mwingine mtu
hutokwa na jasho jingi.
Wakati mwingine mtu huamka ametoa
macho na kama ukimwangalia, nae
huishia hukuangalia tu huku akikosa
la kukujibu endapo utamuuliza vipi
kuna tatizo gani?
MWILI WAKO NI ZAIDI YA
UNAVYOUJUA. JAMBO LA MSINGI NI
KUONDOA HOFU KWANI MWILI WAKO
UNAJUA NINI UFANYE NA WAKATI
GANI ILI KUKULINDA USIKU NA
MCHANA KATIKA SIKU ZOTE ZA
MAISHA YAKO.
Ukioa mke asiyesoma hata hili unaweza kufanya
KUOA MKE AMBAE HAJASOMA RAHA SANA LEO NIMEMUAMBIA MWEZI HUU HATUTOLIPWA MSHAHARA KWAKUA HAUNA TR 30 KAENDA KUNGALIA KARENDA KARUDI ANANIAMBIA HAMNA SHIDA MME WANGU TUTAVUMILIA TU
🤣🤣🤣
🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂
Maziwa ya unga 2 vikombe
Sukari 3 vikombe
Maji 3 vikombe
Unga wa ngano ½ kikombe
Mafuta ½ kikombe
Iliki kiasi
Paka sinia mafuta kabla ya kupika labania
Katika sufuria chemsha maji na sukari pamoja na iliki mpaka inate vizuri
Kisha mimina mafuta koroga
Halafu mimina unga wa ngano na ukoroge haraka haraka
Kisha tia unga wa maziwa, endelea kukoroga usiwe na madonge mpaka uwe rangi ya browni isiokoleza.
Kisha mimina mchanganyiko kweye sinia uliyoipaka mafuta, iwache ipoe na kata kata upendavo na itakuwa tayari.
Kufanya Masaji kuna faida hizi zifuatazo;
Masaji kushuka kwa homoni inayohusika na kupunguza maambukizi mbalimbali homoni ijulikanayo kama ‘cytokines’ vile vile masaji inashusha homoni inayohusika na matendo ya mashari homoni ijulikanayo kama ‘cortisol’.
Kufanya masaji hakukufanyi ujisikie ni mtulivu peke yake, bali pia kunaweza kukuongezea kinga yako ya mwili.
Masaji ya dakika 45 kwa siku imethibitika kuongeza uwingi wa seli nyeupe za damu (lymphocytes) ambazo ndizo hupigana dhidi ya vijidudu nyemelezi vya magonjwa mbalimbali mwilini.
Tafiti nyingi zinasema masaji inao uwezo wa kuamsha mawimbi ndani ya ubongo yanayohusiana na kutengenezwa kwa usingizi mzito (delta waves) na hii ndiyo sababu kwanini wengine hupitiwa na usingizi mzito mara tu baada ya mazoezi ya masaji.
Tatizo la kukosa usingizi linaweza kutibika kwa kufanya masaji tu kwakuwa masaji husaidia kupunguza uchovu na kuongeza uwezo wa kupata usingizi mtulivu kwa watu wa rika zote yaani watoto wadogo mpaka wazee ikihusisha wale wenye matatizo ya akili, kansa na magonjwa ya moyo, machache kati ya magonjwa mengi yawezayo kutibika kwa masaji tu.
Masaji huondoa hamaki na maumivu huku yakiongeza uwezo wa kupata usingizi mzuri na wa uhakika.
Watafiti wanasema kuwa masaji kuongezeka homoni ijulikanayo kama ‘oxytocin’ na kupungua kwa homoni nyingine iitwayo ‘adrenocorticotropin’.
Oxytocin inahusika na matendo ya huruma, maono, upendo na ushirikiano wa kijamii. Wakati adrenocorticotropin yenyewe huhusika na kupungua kwa mfadhaiko (stress) moja kwa moja.
Masaji hupunguza maumivu hasa ya mgongo na maumivu ya kichwa na maumivu ya kwenye mishipa.
Safisha vyombo vya kulishia na kunyweshea kila siku. Osha, sugua vizuri, kisha suuza kuondoa utando unaobeba bakteria.
Kuku wanahitaji wapewe chakula cha kutosha na chenye virutubisho vyote. Unaweza kuwaongezea majani, makombo, nafaka, mchanga laini, au maganda ya mayai.
Wapatie kuku maji safi muda wote. Wafugaji wengi wameripoti kuwa na matokeo mazuri baada ya kuchanganya dawa ya kuua vimelea kwenye maji ya kunywa.
Nunua chakula kwa wauzaji wazuri na wanaoaminika ili kuepuka minyoo na sumu hatarishi. Usiwape kuku chakula chochote kinachoonekana kuoza au kunuka uvundo.
Hifadhi chakula cha kuku katika sehemu kavu isiyo na joto na isiwe kwa zaidi ya miezi mitatu ili kuepuka kuharibiwa na fangasi.
Juzi nikitoka church nilipanda kihiace na kulikuwa na mrembo mkali hujawahi kuona,kila kijana alikuwa akimtupia macho,so me nilikuwa na wepesi wa kuongea naye kirahisi coz nilikuwa kando yake,,, Sasa kama unavyojuwa wanaume kwa kujikosha Nikaimigine mtto ananiangalia so nikaamuwa kupiga fake phone
“Hello Mr. Supervisor,nitachalewa kidogo coz kuna mahali nitapitia, so nipelekee tu hyo Ferrari yangu nyumbani”
Nikaona mrembo ameniangalia kwa macho ya husda apo nkajua nimeuwa ndege kwa jiwe moja, nkaamua kujikosha mtt wa kiume , “niaje mrembo”, akanikazia macho kisha akaniambia,
“Shika battery yako uliangusha ukitoa simu”
Icho kicheko watu walicheka hujawahi ona jooo adi ikabidi dereva aegeshe gari watu wacheke kwanza 😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Nikaona isiwe tabu nikashukia pale pale🚶🏿🚶🏿🚶🏿
Tujifunze kusema ukweli kwani uongo sio mzuri hata kwa Mungu… 🙏🙏🙏🙏🙏
Mchanganyiko wa chumvi na mafuta ya zeituni (olive oil) ni dawa nyingine inayotibu chunusi. Mafuta ya zeituni yandhibiti bakteria na huondoa sumu vitu ambavyo vinafanya kuwa dawa nzuri kutibu chunusi na matokeo ya chunusi.
Nitaenda mbali Zaidi ya maono yako
Safarini nitajenga hekalu la pendo letu
Nitapuliza filimbi kama ishara ya utambulisho wako
Na mwanzo wa sherehe ya ndoa yetu
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
We Kipepeo,
,.-.-.-._.’ //’_.-.-.-.,
”-.,-.:-)i(:’.-,.-”
‘-..-‘()’-..-‘
Ruka, nenda upesi usichelewe.Tua kwa heshima mbele ya huyu nimpendaye. Sema naye kwa upole, chonde usimsumbue. Mwambie nipo salama ila namuwaza sana. Umwambie nampenda kamwe sitamsahau. Kisha umuage kwa kumwambia nakutak..
Kuwa na harufu mbaya mdomoni ni kitendo kinachoweza kuathiri maisha ya mtu kimahusiano si kwa mpenzi tu bali marafiki na jamii kwa ujumla. Pia kuwa na harufu mbaya mdomoni uondoa haiba ya kupendwa kwani hata unapoongea wengi watakwepa kuongea moja kwa moja na wewe kwa sababu ya harufu mbaya inayotoka mdomoni mwako.
Chakula unachokula kina athiri hewa inayotoka mdomoni au sehemu nyingine za mwili wako. Baadhi ya vyakula vina matokeo mabaya sana kwa hurufu unayotoa mdomoni. Harufu mbaya mdomoni si ugonjwa wa kuambukiza haina haja kuogopa ukikutana na mtu mwenye harufu mbaya mdomoni kwamba atakuambukiza.
Pia tatizo kubwa ni kwamba watu wenye harufu mbaya mdomoni hawajijui kwamba wana harufu mbaya. Asilimia 85 – 90% ya tatizo la harufu mbaya mdomoni asili yake ni kinywa chenyewe. Pia kiwango cha harufu hutofautiana kutokana na muda (mchana, usiku na asubuhi).
Harufu nyingi mbaya mdomoni hutokana na vyakula vyenye asilia ya protein. Kuna zaidi ya aina 600 ya bacteria wanaoishi kwenye kinywa cha Binadamu (sehemu ya juu ya ulimi, fizi na kuzunguka meno).
Kutokuwa makini na usafi wa kinywa kama vile kupiga mswaki vizuri kunakoacha mabaki ya chakula ambayo huoza na kusababisha harufu mbaya mdomoni. (Wengi hupiga mswaki haraka haraka na kuacha mabaki ya chakula). Maambukizi ya magonjwa kama vile fizi kutoka damu, mfumo wa upumuaji na kisukari. Kinywa kuwa kikavu kutokana na madawa (medications) Kuvuta sigara, kunywa kahawa, ulaji wa vyakula vyenye viungo vikali kama vile vitunguu maji au thaumu.
Wanasayansi wamekiri kwamba ni ngumu sana mtu kujijua mwenyewe kama ana harufu mbaya kwa sababu ya mazoea (habituation).
Ni rahisi sana kutambua harufu kutoka kwenye kinywa cha mtu mwingine. Unaweza kutambua kama una harufu mbaya mdomoni kwa kumuuliza mtu unayemuamini.
Pia unaweza kujua harufu mbaya kwa kulamba nyuma ya kiganja na kunusa, wengine hupumua mbele ya kioo na kunusa. Pia unaweza kutumia kijiti cha kuchokonolea meno na kukinusa. Kisayansi unaweza kutumia vifaa kama Halimeter, Gas Chromatography na BANA Test.
Kula vyakula vyenye afya na vyakula ambavyo wakati unakula vinaweza kusafisha kinywa vizuri. Kusafisha meno mara kwa mara au kwa uchache mara mbili kwa siku asubuhi na baada ya mlo wa usiku, hii usaidia kuondoa au kujikinga na harufu mbaya mdomoni. Vilevile unashauriwa kutumia KISAFISHA ULIMI (tongue cleaner) kusafishia ulimi wako. Tumia bazooka (chewing gum) ambazo husaidia kuongeza kiasi cha mate kwenye kimywa kilichokauka. Baadhi ya gums zina viungo vinavyoondoa harufu mbaya mdomoni na zingine husafisha kinywa na bacteria wanaosababisha harufu mbaya. Tumia dawa ya kusukutua mdomoni (mouthwash) kabla ya kulala usiku. Kuwa makini na afya ya kichwa chako kama vile kupiga mswaki vizuri, kuondoa mabaki ya vyakula kwenye meno na kumuona daktari kila unapoona una Matatizo ya meno au kinywa au kila baada ya miezi sita kwa uchache.
Kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku angalau glass mbili za maji.
Mwone daktari wako ukiona una tatizo la harufu mbaya mdomoni.
Watu wengi husumbuliwa na tatizo la kunuka mdomo bila hata kujijua hivyo kuwa kero kwa wenzao na wakati mwingine hujishushia hadhi mbele ya jamii. Mara nyingi ugonjwa wa kunuka mdomo (Halitosis) husababishwa na uchafu wa kinywa na ulaji wa vyakula usiosahihi lakini ni tatizo linalotibika.
Ni rahisi kulizuia na kuliondoa tatizo la kunuka mdomo iwapo utaamua kufuata kanuni za usafi wa kinywa na unywaji wa maji kwa kufuata kwa makini muongozo ufuatao:
Kitu cha kwanza kufanya ni kupiga mswaki kwa ukamilifu kila uamkapo asubuhi. Wakati wa kupiga mswaki, utatakiwa siyo tu kusugua meno, bali pia ulimi, sehemu ya katikati hadi karibu na koromeo kwa kusugua vizuri.
Vile vile kila uamkapo baada ya kulala mchana au jioni, hakikisha unapiga mswaki, kwani bakteria wa kinywani, hutawala kinywa kila ulalapo. Mara baada ya kupiga mswaki na kusugua ulimi sawaswa, hakikisha unasukutua vizuri kwa maji, kwani hapa ndipo baadhi ya watu hukosea kwa kupiga mswaki bila kusukutua kwa maji.
Maji ni muhimu sana karibu kila eneo la mwili wa binadamu. Unywaji wa maji ya kutosha kila siku utakusaidia kudhibiti na hatimaye kuondoa tatizo la kunuka mdomo. Unywaji wa maji mengi ni muhimu, hasa kwa wale watu wenye ugonjwa wa kukauka midomo (xerostomia).
Mara nyingi harufu itokayo mdomoni, hutokea tumboni na siyo kinywaji peke yake kama unavyoweza kudhani. Hivyo, kama tumbo litakuwa chafu, hata kama utasafisha kinywa vizuri bado harufu mbaya inaweza kuendelea kutoka. Harufu mbaya ya tumboni hutokea pale tumbo linapokuwa chafu kutokana na kutopata choo kwa muda mrefu. Miongoni mwa mambo yanayochangia kukosekana kwa choo kwa muda mrefu ni pamoja na tabia ya kutokunywa maji ya kutosha kwa siku, hivyo hakikisha unakunywa maji, kiasi kisichopungua lita moja na nusu hadi mbili au zaidi, kutegemeana na kazi unazozifanya.
Ukiwa na tatizo la kukaukiwa maji mwilini kila mara, mwili hujaribu kutumia njia zake za kiasili kupunguza uzalishaji wa mate ili kuhifadhi maji kwa ajiili ya matumizi mengine, kitendo hicho huchangia kunukisha mdomo kwa sababu ndani ya mate huwa kuna kinga muhimu dhidi ya baktetria wanaonukisha kinywa.
Kwa upande mwingine, ili kuzuia kinywa kunuka pale mdomo unapokuwa umekaukiwa na mate, ni vizuri kutafuna vitu kama bazooka (chewing gum) yoyote ili kuzalisha mate ambayo huhitajika katika kudhibiti bakteria.
Hakikisha unasukutua sawaswa baada ya kula chakula chochote, hata kama ni juisi isipokuwa unapokunywa maji tu ya kawaida. Bila shaka, ukizingatia haya, tatizo ulilonalo la kunuka mdomo litataoweka na kubaki historia.
Ina Imidacloprid 20EC

Dawa hii inaua wadudu Kama vile kimamba, utitiri mweusi, mabaka meusi chini ya Majani, vipepeo weupe na wadudu wanaofyonza maua.
Dawa hii ina nguvu na uwezo wa kufanya kazi Muda mrefu kuulinda mmea/majengo dhidi ya wadudu waharibifu.
—
—
—
Boss;- kwa nini umechelewa kazini
Juma;- kuna mtu njiani alidondosha elfu1
Boss;- ohhoh kwa hiyo ulikuwaunamsaidia kuitafuta
Juma;- hapana nilikuwa nimeikanyaga
😃😃😃😃😃😃😃😂😂😂😂😂😂😂
Mchele wa pishori (basmati) – 4
Nyama ya kuku bila mafupa – 1 Lb
Kamba saizi kubwa – 1Lb
Mchanganyiko wa mboga – njegere, karoti,
mahindi, maharage ya kijani (spring beans) – 2 vikombe
Figili mwitu (Cellery) – 2 mche
Vitunguu vya majani (spring onions) – 4-5 miche
Kebeji – 2 vikombe
Pilipili ya unga nyekundu – 1 kijiko cha chai
Pilipili manga ya unga – 1 kijiko cha chai
Sosi ya soya – 3 vijiko vya supu
Mafuta – 1/4 kikombe
Chumvi – kiasi
Osha na roweka mchele.
Tia kamba chumvi na pilipili nyekundu ya unga. Tia mafuta vijiko viwili katika kikaango (frying pan), kaanga kamba kidogo tu, weka kando.
Katakata kuku vipande vidogo vidogo, tia chumvi na pilipili manga. Kaanga kaTika kikaango (ongeza mafuta kidogo) Weka kando.
Katika karai, tia mafuta kidogo kama vijiko vitatu vya supu, tia kamba na kuku, tia mboga za mchanganyiko, sosi ya soya na chumvi, kaanga kidogo. (Kama mboga sio za barafu) itabidi uchemshe kidogo.
Katakata kebeji, figili mwitu (cellery) na vitunguu vya majani (spring onions) utie katika mchaganyiko. acha kwa muda wa chini ya dakika moja katika moto.
Chemsha mchele, tia mafuta kidogo au siagi, chumvi upikie uive nusu kiini, mwaga maji uchuje.
Changanya vyote na wali rudisha katika sufuria au bakuli la oveni, funika na upike kwa moto wa kiasi kwa muda wa dakika 15-20 takriban.
Epua na upakue katika sahani ukiwa tayari kuliwa.
Mchumba wangu amenialika kwao nikawaone wazazi wake lakini akaniambia nisiende mikono mitupu…
Nikaamua kuvaa gloves…
Sipendagi aibu ndogo ndogo ukweni.😏😏😏
Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: kimya
Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: we nani kwani?
Polisi::: sisi polisi
Jamaa::: mnataka nini?
Polisi::: kuongea na wewe
Jamaa::: kuongea na mimi?!
Polisi::: ndio
Jamaa::: mko wangapi?
Polisi::: tuko watatu
Jamaa::: kama mko watatu si muongee wenyewe…!!!
Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee huku likiwa na ladha tamu isiyomithilika. Licha ya sifa hii, tunda hili linatajwa kuwa na faida lukuki endapo litaliwa na mwanadamu.
Kwanza, linatajwa kuwa na virutubisho kadha wa kadha vyenye kazi mbalimbali mwilini. Baadhi ya virutub
isho hivyo ni pamoja na vitamini za aina mbalimbali, madini, protini, mafuta, uwanga na nyuzinyuzi.
Fenesi pia linatajwa kuwa chanzo kizuri cha nishati kisichokuwa na lehemu. Si hivyo tu, bali pia ni chakula chenye virutubisho vya kuondosha sumu mwilini vinavyoweza kuukinga mwili dhidi ya saratani na magonjwa mengine kadha wa kadha.
Uwepo wa viondosha sumu ndani ya tunda hili kunasaidia pia kuongeza uwezo wa kuona. Tunda hili pia linatajwa kuwa na kiasi kikubwa cha madini ya potassium yanayosaidia kuimarisha mifupa na afya ya ngozi.
Fenesi ni chanzo kizuri cha vitamini C. Uwepo wa kiasi kikubwa cha vitamini hiyo pamoja na viondosha sumu kunaongeza ufanisi wa mfumo wa kinga mwilini. Husaidia kuongeza kinga dhidi ya kifua, mafua na kikohozi.
Ni tunda salama kiafya, halina lehemu licha ya kuwa na kiasi kikubwa cha mafuta. Pia, lina wanga na kalori kwa kiasi kikubwa. Sukari iliyomo ndani yake huchangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha mwili.
Hurekebisha msukumo wa damu na pia husaidia kurahisisha mmeng’enyo wa chakula tumboni pamoja na kuukinga mwili dhidi ya magonjwa ya moyo na kupooza.
Inasadikika pia kuwa tunda hili lina uwezo wa kuukinga mwili dhidi ya ugonjwa wa pumu.
Si hivyo tu, fenesi lina vitamini muhimu katika utengenezaji wa damu mwilini.
Recent Comments