Karibu AckySHINE
Karibu AckySHINE
Chagua Unachotaka Kusoma Hapa
Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.
Upendo na chuki havitangamani
Upendo wa kweli hauambatani na chuki. Huwezi kusema una Upendo wakati kuna watu wengine unawapenda na wengine unawachukia. Ni sawa na kusema kitambaa ni cheupe lakini kina madoa doa, maana yake sio cheupe.
Vyakula vinavyofaa kutumiwa kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza
Vyakula hivyo ni;
- Maharage
- Nyanya
- Samaki
- Mboga za majani zenye rangi ya kijani
- Matunda jamii ya machungwa
- Mafuta ya nazi
- Viazi vitamu
- Vyakula ambavyo havijakobolewa
- Maziwa yasiyo na mafuta ndani yake
- Mbegu za maboga
- Mtindi usio na mafuta ndani yake
Mambo 9 ya kuzingatia kuepuka ugonjwa wa saratani au Kansa
Tafiti nyingi zilizolizofanywa zinaonesha kuwa sababu kuu zinazosababisha saratani ni mtindo wa maisha usiofaa kama ulaji usiofaa na kutofanya mazoezi ya mwili.
Ili kuepukana na ugonjwa wa saratani au kupunguza uwezekano wa kupata saratani ni muhimu kuzingatia yafuatayo:
1. Kula zaidi vyakula vya mimea na nafaka zisizokobolewa
Matokeo ya tafiti yanaonesha kuwa vyakula hivi vinapunguza uwezekano wa kupata saratani, Hakikisha unakula mboga mboga za kijani na rangi nyingine kama njano,zambara. Kula nafaka zisizokobolewa kama unga wa dona, mchele wa brauni,unga wa ngano usiokobolewa,mtama na ulezi.
2. Kuwa na Uzito Uliosahihi
Uzito mkubwa uliopitiliza ni hatari na husababisha saratani. Hakikisha uwiano wa urefu na uzito wako (BMI- Body -to-Mass Index) ni sahihi ambayo ni 18 -25 kwa mtu mzima na mwenye afya nzuri unashauriwa kuwa na uwiano wa 21-23.
Punguza vyakula vinavyonenepesha mwili kama vyenye mafuta na sukari kwa wingi. Vyakula vyenye mafuta kwa wingi kama chipsi na vitumbua mfano ni hatari kwa afya yako.Vyakula vyenye sukari ni kama soda,chokoleti,keki,barafu na iskrimu na juisi bandia.
3. Fanya mazoezi ya mwili
Fanya mazozi ya mwili kila siku. Dakika 15-30 tu zinatosha kufanya mazoezi kwa afya njema. Ukikosa muda fanya anagalau mara 3 kwa wiki kwa muda usiopungua dakika 30.
Kukimbia(jogging) ni njia rahisi ya kufanya mazoezi yanayohusisha mwili mzima. Ukiweza jiunge katika timu ya mpira au klabu za mazoezi ya ndani.
Tembea kwa miguu pale inapobidi. Rafiki yangu mmoja ambaye ana gari ameweka ratiba ya kutotumia gari wakati wa mwisho wa juma. Anapanda dalala na kutembea kwa sehemu kubwa. Unaweza ukafanya hivyo pia.
4. Punguza au Acha kula Nyama nyekundu.
Ukiachia mbali saratani, nyama nyekundu imetambulika kusababisha madhara mengi na makubwa kwa binadamu.
Amua sasa kuachana nayo. Hamia katika samaki na kuku kwa kuanzia na baadae huenda ukaachana na hizo nyingine pia.
Nyama ya nguruwe maarufu kam Kitimoto ni nyama nyekundu na ni hatari kwa afya yako . Heri wale ambao hata dini zao zilikataza nyama hii ya Nguruwe kwani wameepuka hatari.
5. Epukana na Nyama za kusindikwa.
Nyama za makopo na soseji zinasababisha saratani kutokana na kemikali za kutunzia zisioze na pia huwekwa chumvi nyingi sana ambayo ni hatari kwa afya.
6. Punguza Matumizi ya Chumvi
Chumvi ya kupita kiasi inaongeza uwezekano wa kupata saratani hivyo ni hatari. Tumia chumvi kwa kiasi kidogo kwa afya njema. Binadamu anahitaji gramu 5 tu kwa siku sawa na kijoko kidogo cha chai.
Usiongeze chumvi wakati wa kula,chumvi isiyoyeyuka nia hatari zaidi.
7. Acha kula Vyakula vyenye Ukungu
Acha kula nafaka na kundekunde zilizootesha ukungu hasa kwa kutohifadhiwa vyema. Vyakula hivi vinatoa sumu ya aflatoxin
8. Usivute Sigara
Uvutaji wa sigara ni hatari na huenda ukakusababishia saratani ya koo,kinywa na mapafu. Acha kuvuta sigara ili kuepukana na ugonjwa wa saratani. Fikiria kidogo,kwanini ufe kwa sababu ya moshi tu?.
9. Punguza au Acha Pombe Kabisa
Ukiacha pombe utapunguza uwezekano wa kupata saratani na hivyo kuwa salama zaidi.
Achana na pombe, kuna madhara mengi sana ya kunywa pombe ukiachia ya saratani.
Badilisha Mtindo wa Maisha na Uwe Salama na Saratani
Namna ya kuishi kunachangia kwa kiasi kikubwa kupata saratani au la. Chagua mtindo ulio bora na salama kama ilivyoshauriwa katika mada hii juu ya kuepukana na ugonjwa wa saratani.
Afya yako ni jukumu lako mwenyewe na kupanga ni kuchagua. Panga kuishi mtindo wa maisha ulio bora na salama chagua kuishi bila saratani.
Mapishi ya Biskuti Za Mtindi/Yoghurt
MAHITAJI
Chenga za biskuti – 3 gilasi
Mtindi (yogurt) – 1 Kopo (750g)
Maziwa ya unga – 1 gilasi
Siagi – 10 Vijiko vya supu
Sukari – ½ gilasi
Lozi zilizomenywa vipande vipande – ½ gilasi
Nazi iliyokunwa – ½ gilasi
Vanilla – 1 Kijiko cha supu
MAPISHI
Katika mashine ya kusagia (blender), tia mtindi, sukari, siagi na vanilla na usage pamoja hadi ichanganyike.
Mimina katika bakuli la kiasi.
Tia vitu vilivyobakia na uchanganye vizuri.
Mimina kwenye treya ya kuchomea na uvumbike katika oveni moto wa 350° hadi ishikamane na kuwa tayari.
Iaache ipoe kisha katakata vipande na tayari kwa kuliwa.
Baada yakuwa imeshaiva, ukipenda unaweza kupakiza jamu au karameli ya tayari kwa juu, kisha ukarudisha kwenye oveni moto wa juu kidogo kwa ladha nzuri zaidi
Kukosa hela sio tatizo bali ndio kigezo ya kutafuta hela
Ukimonyesha mtu fursa akakwambia hana hela mwambie hiyo ndio sababu ya wewe kumonyesha fursa ili awe na hela tukumbuke kuwa hela haitokani na hela hela inatokana na fursa
Nijukumu la mtu asiye na hela kutafuta njia ya kuwa na hela watu wengi tunachelewa kufanikiwa kwa kutojua majukumu yetu ili kupambana na UMASIKINI mwombe Mwenyezi MUNGU kwa imani yako akufungue akili…
To ur Success!
Mapishi ya Ugali na dagaa
Mahitaji
Dagaa (dried anchovies packet 1)
Unga wa ugali (corn meal flour 1/4 kilo) (unaweza kutumia unga wa choice uipendayo)
Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2)
Kitunguu maji (onion 1)
Limao (lemon 1/4)
Pilipili mbuzi nzima bila kukata (scotch bonnet pepper1, do not chop)
Chumvi (salt 1/4 ya kijiko cha chai)
Mafuta (vegetable oil)
Hoho (green pepper)
Matayarisho
Chambua dagaa kwa kutoa vichwa vyao na utumbo, baada ya hapo waloeke katkika maji ya moto kwa muda wa dakika 5 na uaoshe tena katika maji ya baridi na uwakaushe uwaweke pembeni. Ukishamaliza katakata kitunguu na uandae nyanya tayari kwa upishi. Bandika sufuria ya kupikia dagaa jikoni na utie mafuta, yakishapata moto tia vitunguu pamoja na dagaa. Kaanga mpaka dagaa wawe light brown kisha tia nyanya, chumvi na pilipili. Pika nyanya mpaka ziive (ukitaka kujua kama nyanya zimeiva utaona zinatengana na mafuta) Baada ya hapo kamulia limao kidogo sana na tia pilipili hoho na zipike kama dakika mbili. kisha ipua.
Ukisha maliza kupika dagaa andaa chungu cha ugali. Kwanza unatakiwa kuchemsha maji ya moto, kisha koroga pembeni unga kiasi katika maji ya baridi na utie kwenye maji yanayochemka, Fanya kama unatengeneza uji, uji wa ugali ukishachemka tia unga na uanze kuusonga mpaka ugali uive. Ukisha iva pakua na usevu na mboga tayari kwa kuliwa.
Ndege ya Tanzania
Kuna maprofesa 40 walipanda AIR TANZANIA ili wasafari. Kabla ndege haijaanza kuondoka, Lilipita tangazo kama ifuatavyo:
Ndugu wasafiri wote, ndege unayotarajia kusafiri nayo imetengenezwa na wanafunzi wa Kitanzania.
Baada ya tangazo maprofesa wote waliteremka isipokuwa mmoja alibaki kwenye kiti chake
Walipomuuliza ni kwanini hakuondoka akajibu kwa haraka na furaha kuwa:
Kama ndege hii imetengenezwa na watanzania, hata kuwaka haitawaka!
Huu ndio uchawi unaweza kufanyika siku mpenzi wako akikutambulisha kwao
😂😂😂😂😂
*UCHAWI* ni nini?
`Uchawi ni pale mpenzi wako anapokupeleka kwao kufika tyu ghafla unakutana na dada yake getini ambaye alikuwa ni mpenzi wako wa zamani, ile kuingia ndani unamuona kaka yake ambaye mlipigana baada ya kukufumania na mke wake, hujakaa vizuri unamuona mama yake ambaye ndiye jimama shangingi lako anayekuweka mjini akupaye jeuri ya kutamba ambapo hata gari unalolitumia alikupa yeye na hataki upajue anapoishi, wakati unataka kuondoka unakutana uso kwa uso na baba yake ambaye alikuwaga wakili wako kwenye kesi ya ubakaji`
🤣😂😂😂😂🤣
Tofauti ya mwanamke wa Kizaramo, Kitanga, Kihaya, na wa Kichaga
Mwanamke wakizaramo: Unampa hela ana nunua dela anaenda ana msutia jirani, analivaa dela bila nguo ya ndani mbele yako, unazidiwa anakupa kitu fresh unatoka unatabasamu.🤝🏽🙌🏽
Mwanamke wa kitanga:
Unampa hela anapika vitu mtaa mzima unasikia harufu ya chakula, chenji inayo baki ananunua kinga ukirudi unakula afu unakula..👏🏼👏🏼🤝🏽🙌🏽
Mwanamke wa kihaya:
Unampa hela ukirudi unakuta majirani wote wanataarifa kuwa wew uliacha hela, anakupkia vitu vzuri, usiku anakuhudumia ukimsifia anakuhudumia tena hata mara nne kwa usiku mmoja..we mle sifa tu🙌🏽🙌🏽🤸🏾♀👌🏽.
Mwanamke wa kichaga:
Unampa hela anaenda ananunua dagaa anapika na michuzi mingi mpaka dagaa wanafufuka unakula kwa shida, dagaa wanakula utumbo wako unakufa.. Madaktari wanajitahidi wanakutibu unafufuka. Ukiwa hujapata akili vizuri anakuletea bili ya umeme, anakukumbusha deni la kwa Massawe, anakukumbusha kodi ya nyumba.. *Unashikwa na presha unakufa moja kwa moja*🙌🏽😂🙆🏼♂🏃🏾🤸🏾♀
Mvua zazua kasheshe! Soma hii..
Baba- : Halloo mke wangu.. yaani ni shida sitaweza kurudi nyumban, daraja limevunjika na kutoka morogoro kurudi dar haiwezekani
MAMA:- Mme wangu morogoro ulienda bila kuniaga! ?
BABA:- Ilikuwa ni ghafla sana mke wangu sikuweza kukwambia
MAMA:- kha! Sasa watoto nani atawaangalia
BABA:- Unasemaje! We uko wapi kwan
MAMA:- Niko bagamoyo na daraja limeondolewa na maji sitaweza kurudi.
BABA:- Unasemaje we mwanamke.. nakwambia nikukute nyumban ndani ya dk 15
Baada ya dk 15 Baba kafika nyumban.
MAMA:- Haya umefkaje kutoka morogoro?
BABA:- Nimepewa lift na helkopta ya Mbowe..
Kama umeipenda shea na rfiki zakooo…..
Kila kitu ni mali ya Mungu isipokua hiki
Kila kitu ni mali ya Mungu.
Kuwa na Mungu ni kuwa na kila kitu.
Hata mimi mwenyewe ni mali ya Mungu.
Kitu kimoja tu nina hakika nacho kwamba ni mali yangu binafsi nacho ni dhambi zangu😛.
Ee Mungu naomba niziungame niweze kubaki mali yako bila kuwa na kitu binafsi.
Angalia wanachokifanya Zuzu na msichana chumbani kwenye giza
Zuzu: Mambo Anna!
Anna: Poa!
Zuzu: Kuna kitu nataka nikuonyeshe…
Anna: Kitu gan?
Zuzu: Twende chumbani kwako (wakaenda)
Anna: Haya nionyeshe…
Zuzu: Funga mlango na madirisha kwanza (akafunga)
Anna: Haya nionyeshe sasa!..
Zuzu: Zima taa kwanza (akazima)
Anna: Mhm…nionyeshe sasa!
Zuzu: Haya njoo hapa kitandani…
Anna: Ok, nionyeshe!
Zuzu: Ona nimenunua saa ambayo inawaka yenyewe gizani… Acha mawazo mabaya ww???
Wavuta bangi wa Colombia watoa mpya
Asubuhi ya leo huko nchini Colombia baada ya serikali kuidhinisha matumizi ya bangi kuwa halali +++ Wavutaji bangi wamepanda basi la gorofa wengine juu wengine chini….
Waliopanda chini wanawauliza wa juu huko speed ni ngapi maana huku ni 80.
Wajuu wakajibu huku mpaka sasa hatujui dereva bado hajaja…. 😂😂😂
Amri ya Tisa ya Mungu: Mambo inayokataza na inayoamuru
Katika Amri ya Sita na Tisa Mungu ametuamuru nini?
Mungu ametuamuru kutunza usafi wa moyo na kuwa waaminifu katika ndoa.
Mambo 10 unayofanya kimakosa wakati wa kujipodoa
Kama kote duniani, wanawake wengi Tanzania wanatumia vipodozi kama nyongeza ya urembo wao ya kiasili. Ila, kuna makosa maalum zinazofanyiwa kwenye kutumia vipodozi Tanzania. Kuwasaidia dada zetu, Yafuatayo ni makosa 10 ya kuweka vipodozi na jinsi ya kuzirekebisha.
1. Nyusi
Kuna tabia ya wanawake kunyoa nyusi zao sana, na wengine kuzitoa kabisa. Alafu, wanaishia kuzichora na rangi nyeusi.
Hii inamfanya mwanamke kuonekana kama kikatuni.
Sasa:
- Badala ya kunyoa nywele zote, zipunguze kwa kiasi kidogo
- Usituimie rangi nyeusi kuzijaza. Tumia rangi ya brauni
- Kwa muonekano wa kiasili zaidi, tumia nyusi, poda ya nyusi au gel badala ya penseli.
2. Tumia faundesheni inayofanana na rangi ya ngozi yako
Ingawa kupata faundesheni inayofanana na ngozi yako ni ngumu, hasa kwa wanawake weusi zaidi, wanawake wengi wanapata shida na kukubali rangi ya kiasili na wanajaribu kutumia vipodozi kubadilisa rangi yao.
Suluhisho:
- Kubali rangi yako ya kiasili
- Rangi yetu inaweza ikawa mweusi au mweupe zaidi kutegemea na msimu. Kwa hiyo ni bora kuwa na faundesheni inayoendana na mabadiliko hayo
3. Usitumie poda asana
Wanawake wengi wanfikiri kwamba kutumia poda nying ndio kupendeza zaidi. Matokeo yake, wanaishia kufanana na jinni.
Suluhisho:
- Tumia poda inayofanana na ngozi yako
- Usiweke poda nyingi. Kiasi kidogo kitakutosha
4. Tumia blush kwa usahihi
Kutumia kwa usahihi ni tatizo duniani.
Suluhisho:
- Tumia blush kwenye mifupa ya mashavu, sio kwenye mashavu yenyewe.
- Kama una ngozi yeneye uweusi zaidi, tumia blush ya rangi ya dhahabu au zambarau.
5. Burashi za vipodozi ni muhimu
Badala ya kutumia vidole vyako, utahitaji burashi zifuatayo:
- Burashi ya faundesheni
- Burashi ya poda
- Burashi ya blush
- Burashi ya nyusi
- Burahi ya eyeshadow
6. Tumia kope bandia kwa usahihi
Wanawake wengi wanatumia kope bandia zisizo na ubora. Matokeo yake wanafanana na dolli ya mtoto.
Suluhisho:
- Badala ya kutumia kope bandia, nunua wanja nzuri inayonyoosha na kunenepesha kope zako
- Nunua kope bandia zenye ubora (zilizotengenezwa na nywele za binadamu au yalisanidiwa)
- Jifunze jinsi ya kuweka kope bandia kwa usahihi.
7. Jifunze kuweka jicho la paka kwa usahihi
Jicho la paka ni njia moja ya kuongeza umaridadi kwa sura yako na kuvutia zaidi. Ila, wanawake wengi wanakosea kuiweka.
Suluhisho:
- Ni bora kutumia liner ya maji au mafuta kuliko kutumia penseli kama huna ujuzi wa kutosha
- Jifunze kuchora jicho la paka
8. Matatizo ya nyusi…tena
Wanawake wengi wanatumia konsila kwa nje ya nyusi zao. Tatizo linakuja pale ambapo konsila iliyotumiwa haiendani na ngozi yao. Hii inafanya konsila hiyo kuonekana sana, kwenye picha haswa!
Suluhisho:
- Tumia konsila inayoendana na ngozi yako
- Hakikisha una changanya konsila kwa kutumia burashi, ili ijichangaye vizure na ngozi/faundesheni yako
9. Eyeshadows
Wanawake wanatumia eyeshadow zinazo ng’aa au za rangi kali. Zaidi ya hapo, hawazichanganyi vizuri.
Suluhisho:
- Tumia eyeshadow za rangi ya dhahabu, brauni au zambarau
- Jifunze jinzi ya kuweka eye shadow vizuri, zikiwemo
- Rangi ya highlighter yakuweka chini ya nyusi zako
- Rangi ya msingi ya kuweka
- Rangi ya mpito
- Rangi kuu ya eye shadow
10, Mdomo
Kabla ya kuweka lipstick, hakikisha mdomo yako inaunyevu. Hii ni muhimu sana kwa lipstick yako kuseti vizuri.
Usiweke vipodozi kwa fujo
Kwenye swala la vipodozi, kutumia kidogo ni bora kuliko kutumia nyingi. Unataka urembo wako wa kiasili kuboreshwa, sio kubadalika kabisa.
Kwa kifupi, ukitumia vipodozi lakini unaonekana kama vile hujatumia vipodozi, basi hapo ndio utakuwa umepatia.
Mafundisho Kuhusu Bikira Maria
DOGMA ZA KANISA KATOLIKI KUHUSU BIKIRA MARIA.
kumhusu Bikira Maria ambayo ni lazima
kila Mkatoliki ayasadiki kutokana na
ufunuo wa Mungu: 1. B. Maria
mkingiwa dhambi ya asili 2. B. Maria
Mama wa Mungu 3. B. Maria Bikira
daima 4. B. Maria kupalizwa mbinguni
mwili na roho
MKINGIWA DHAMBI YA ASILI
neema” (Lk 1:28) maana ndiye tunda
bora la ukombozi ulioletwa na Yesu. Ni
imani ya Wakatoliki kwamba kwa stahili
za Mwanae alikingiwa asirithi kwa wazazi
dhambi ya asili na madonda
yanayotokana nayo, wala asitende
dhambi maisha yake yote. Kwa maneno
mengine, Bikira Maria tangu atungwe
mimba Mungu alimkinga na kila doa la
dhambi kwa kutazamia stahili za Yesu
Kristo aliye Mkombozi wa binadamu
wote. Ndiye aliyekombolewa kwa namna
bora kushinda viungo vyote vya Kanisa.
Maisha yake yote hakutenda dhambi
hata moja. Mapokeo ya mashariki
yanamuita “A Panagia” = “Mtakatifu tu”.
Dogma hiyo ilitangazwa na papa Pius IX
mwaka 1854, halafu mwaka 1858 Bikira
Maria alijitambulisha kama Mkingiwa
kwa Bernadeta Soubirous huko Lurdi
( Ufaransa ). Tena mwaka 1917 huko
Fatima ( Ureno ) aliwafunulia Lusia,
Fransisko na Yasinta Marto moyo wake
safi usio na doa.
MAMA WA MUNGU
“Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye
Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno
alikuwa Mungu” (Yoh 1:1). Huyo Mungu
Mwana alitwaa ubinadamu katika Bikira
Maria akazaliwa mtoto, jina lake Yesu,
maana yake Mungu Mwokozi. Huyo ni
binadamu kama sisi katika yote
isipokuwa dhambi. Ubinadamu wa Yesu
unategemea Nafsi yake ya Kimungu:
akisema, ‘Mimi’, ni kwa Nafsi yake hiyo.
Ndiyo maana aliwaambia Wayahudi,
“Kweli nawaambia, kabla Abrahamu
hajazaliwa, nalikuwepo” (Yoh 8:50).
“Kama vile Baba alivyo asili ya uhai,
ndivyo alivyomjalia Mwanae kuwa asili
ya uhai” (Yoh 5:26).
Mtume Paulo akaeleza, “Wakati
maalumu ulipotimia Mungu alimtuma
Mwanae aliyezaliwa na mwanamke” (Gal
4:4). Bikira Maria ni Mama wa Mungu
kwanzia wakati huo: tangu Bikira Maria
alipojaliwa kumchukua mimba, kumzaa,
kumnyonyesha na kumlea mtu ambaye
kwa asili ni Mungu. Cheo hicho
kimemuinua juu kuliko hata malaika.
“Malaika alimwambia, ‘Hicho
kitakachozaliwa kitaitwa Kitakatifu,
Mwana wa Mungu’” (Lk 1:35).
Dogma ilitangazwa mwaka 431 kwenye
Mtaguso wa Efeso uliomuita “Mzazi wa
Mungu”, ukisema Maria anastahili
kuitwa hivyo kwa sababu Mwana wa
milele wa Mungu, ambaye ni Mungu
sawa na Baba, alifanyika mtu toka
kwake. Akiwa mja mzito alishangiliwa:
“Umebarikiwa wewe katika wanawake,
naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Limenitokeaje neno hili, hata mama wa
Bwana wangu anijilie mimi?” (Lk
1:42-43). Ungamo hilo la Elizabeti
likakamilishwa na Mtume Thoma
aliyemuambia Yesu mfufuka: “Bwana
wangu na Mungu wangu!” (Yoh 20:28).
BIKIRA NA MAMA
kuwa Yesu alitungwa bila ya mchango
wa mwanamume. La ajabu zaidi katika
imani hiyo ni kwamba hata uzazi
wenyewe haukuondoa ubikira wake, bali
uliutakasa: ni Bikira daima. Ingawa akili
inasita, ni lazima kukiri na malaika,
“Hakuna lisilowezekana kwa Mungu” (Lk
1:38). Yosefu , ingawa kisheria alikuwa
mume wake, hakutenda naye tendo la
ndoa.
Ni imani ya Wakatoliki na Waorthodoksi
kuwa Mama wa Yesu anastahili kuitwa
“Bikira daima” kwa sababu alimchukua
mimba akiwa bikira, akamzaa bila ya
kupotewa na ubikira, akabaki bikira hadi
mwisho wa maisha yake. Hamu yake ya
kuwa bikira hata kisha kuchumbiwa
inajitokeza katika jibu alilompa malaika
aliyemtabiria mimba: “Litakuwaje neno
hili, maana sijui mume?” (Lk 1:35). Ni
kielelezo cha Wakristo ambao Mtume
Paulo aliwaandikia: “Nawaonea wivu,
wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea
mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira
safi” (2Kor 11:2), “mpate kumhudumia
Bwana pasipo kuvutwa na mambo
mengine” (1Kor 7:35).
Wanaosemwa katika Injili “ndugu zake
Yesu” si watoto wa Bikira Maria, bali
ndugu wa ukoo waliokuwa jirani sana
na familia hiyo takatifu. Kama Bikira
Maria angekuwa na watoto wengine,
Yesu angekuwa amefanya kosa la
kuwanyang’anya Mama yao na
kumfanya awe Mama wa mtume
Yohane alipomkabidhi msalabani,
“‘Mwana, tazama Mama yako’. Na tangu
saa ile huyo mwanafunzi alimchukua
akae nyumbani kwake” (Yoh 19:27).
Katika Agano Jipya yupo Yakobo
anayeitwa na mtume Paulo “ndugu yake
Bwana” (Gal 1:19): Yakobo huyo alikuwa
maarufu katika Kanisa la Yerusalemu
(Mdo 12:7; 15:13-21; 21:18-20; Gal
2:9). Yakobo huyo si mtume Yakobo
kaka yake Yohane (Lk 6:12-16), bali ni
Yakobo ndugu yake Yose na mama yao
kwenye Injili anaitwa “Maria mwingine”,
si Maria Mama wa Yesu. “Walikuwepo
pia wanawake waliotazama kwa mbali.
Miongoni mwao akiwa Maria
Magdalena , Salome na Maria mama wa
akina Yakobo mdogo na Yose” (Mk
15:40). Maria lilikuwa jina la kawaida
kwa Wayahudi: akina Maria wakiwa
wengi hivyo, tujue kuwatofautisha
kwenye Injili, ambazo zinamtaja Bikira
Maria kama “Mama wa Mungu”
KUPALIZWA MBINGUNI MWILI NA ROHO
Maria alipalizwa mbinguni mwili na
roho, ishara ya mwanamke mshindi.
“Ishara kubwa ikaonekana mbinguni,
ambapo mwanamke aliyevikwa jua , pia
na mwezi chini ya miguu yake, na taji la
nyota kumi na mbili juu ya kichwa
chake” (Ufu 12:1). Maneno ya shangilio
lake yametimia: Mungu “amewaangusha
wakuu katika viti vyao vya enzi; na
wanyonge amewakweza” (Lk 1:52).
Imani hiyo ya mapokeo ya kale,
yanavyoshuhudiwa na Mababu wa
Kanisa, ilitangazwa rasmi na Papa Pius
XII kwa niaba ya ma askofu wote mwaka
1950.
Je, Bikira Maria ni Bikira Daima au alizaa watoto wengine?
Tunaweza kuthibitisha kuwa Bikira Maria hakuzaa watoto wengine kwa kunukuu Biblia Kama ifuatavyo;
1. Bikira Maria Alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, 27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. 28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.” 29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini? 30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. 31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu. 32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake. 33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” 34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?” 35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu. (Luka 1:26-35)
2. Biblia Haiwataji ndugu wa Yesu wakati Yosefu na Maria walipokimbilia Misri kumficha Yesu na wakati waliporudi
19 Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri, 20 akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa.” 21 Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli. 22 Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya, 23 akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa Mnazare.” Matayo 2:19-23
3. Biblia haituambii kuwa Yesu alikua na wadogo zake alipokuwa na miaka 12
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka. 42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi. 43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari. 44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki. 45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta. 46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima. 48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.” 49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?” 50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia. 51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake. 52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu. (Luka 2:41-52).
4. Kukosekana kwa neneo “Binamu” kwenye lugha ya Yesu
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?” (Mathayo 13:55-56)
5. Biblia haitumii neno Ndugu, kaka au dada ikimaanisha ndugu wa kuzaliwa mama mmoja na baba mmoja
6. Undugu wa Yakobo, Simoni, Yosefu na Yuda kwa Yesu Sio wa mtu na kaka zake
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?” (Mathayo 13:55-56)
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.” (Marko 10:35)
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56)
19 Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana. (Wagalatia 1:19)
1 Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo. (Yuda 1:1)
25 Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene. (Yohana 19:25)
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56).
7. Yesu alimwacha Mama yake kwa Yohane kwa kuwa hakuwa na Kaka na dada wakumwachia mamaye
26 Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake: “Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao.” 27 Halafu akamwambia yule mwanafunzi: “Tazama, huyo ndiye mama yako.” Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake.
Jifunze kupitia mfano huu Ili uishi kwa amani na watu
Siku moja nilichukua taxi aina ya UBER nikiwa naelekea uwanja wa Ndege Mwl. Nyerere Dereva huku akiendesha kwa ustaarabu sana mara ghafla pasipo kutegemea gari ya taka ikajitokeza mbele yetu kutokea nje ya barabara. Dereva wa taxi kwa umakini na neema ya Mungu akalikwepa gari hilo na ilikuwa kidogo agonge gari zingine mbele yetu.
Pasipo kutegemea dereva wa gari la taka akaanza kufoka na kutoa matusi kwa kelele kubwa!
Katika hali ya kushangaza dereva wa taxi alitabasamu na kuwapungia mkono waliokuwa kwenye gari la taka na ndipo kwa mshangao nilimuuliza; “Inakuwaje ufanye hivyo wakati walitaka kutuua na hata kuharibu mali yako?”
Akajibu kwa upole akinitazama kwa tabasamu akasema. “Katika maisha yetu, kuna watu wako kama gari la taka. Wamejaa misongo, hasira, maumivu, wamechoka kifikra, kiuchumi na kimaisha, na wamejaa masikitiko mengi. Watu hao takataka zao zinazopowazidi hutafuta mahali pa kuzitupa na haijalishi mazingira wanakozitupia.
FUNZO!
Jifunze kutogombana nao. Wapungie mkono, wape tabasamu, songa mbele. Haikupunguzii kitu. Wala usiruhusu takataka zao zikupate.”
Uliumbwa kuyafurahia maisha. Usiyafupishe kwa kuamka asubuhi na kinyongo, na hasira, na ghadhabu kwa sababu ya mtu fulani.
Watafiti wanasema 10% ya maisha ni vile ulivyoyatengeneza lakini 90% ya maisha ni vile unavyochukuliana nayo.
Jifunze kuchukuliana na maisha kuliko vile unavyoyatengeneza huku ukimtegemea Mungu.
ANGALIZO!
Ukiona umeanza kueleweka, kukubalika, kutambulika, kufahamika, kuheshimika na kupata nafasi zaidi kwa kile unachokifanya kumbuka kuendelea kuzingatia misingi, nguzo, miiko na nidhamu iliyokuwezesha kufika hapo ulipo ili uende mbali zaidi.
MUNGU AKUBARIKI SANA.
Mkalimani alivyoharibu ibada ya leo
Leo nikaamua niingie misa ya asubuhi kwenye kanisa moja la kilokole kulikua na ugeni wa mchungaji kutoka Bulgaria, Mahubiri yameanza saa 1 asubuhi hali ikawa kama hivi:
MCHUNGAJI: My name is Pastor Livingstone
MKALIMANi: Kwa jina naitwa mchungaji Jiwe linaloishi
MCHUNGAJI: We thank God for All goals we set by our hands
MKALIMANI: Tunamshukuru Mungu kwa Magoli yote tuliyoweka kwa Mkono
Hivi navyoongea kanisa halina viti waumini wote tumekimbia nje naona Mkalimani amebaki na kiatu cha kushoto tu.
Sunday joke
Kilichompata huyu jamaa akiwa anaangalia mpira mechi kali na mke wake
WIFE: Baibie, yule ni nani? Ni Chris Brown??
HUSBAND: Yule ni Theo Walcott
WIFE: ile Yellow Card ni ya nini?
HUSBAND: ile ni ya Onyo, na Red Card inamaanisha mchezaji awache kucheza na atoke inje ya uwanja.
WIFE: Oooooh! Inakaa kama traffic light! Yellow- Ilani na Red – Simama
HUSBAND: Yeah yeah swity! Ndio hivyo.
WIFE: Na je Green Card??
HUSBAND: Aaaah! Hakuna kitu kama hicho.
WIFE: Nataka Arsenal ishinde world cup.
HUSBAND: [kimya]
WIFE: Ni nani yule mzee anakaa kama Mr. Bean??
HUSBAND: Yeees swity, yule ni kocha wa Arsenal, anaitwa Arsene Wenger.
WIFE: Oooooh! inamaanisha yule kocha mwengine ni Chelsea Wenger??
HUSBAND: [Kabadilisha channel]
Recent Comments