Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Amri ya nne ya Mungu: Kuheshimu Wazazi

Katika Amri ya nne ya Mungu tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tuwaheshimu wazazi wetu na wakubwa wetu wote, tuwapende, tuwatii na tuwaombee. (Kut 20:12, Kol 3:20)


Amri ya Nne ya Mungu tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tuwaheshimu wazazi wetu na wakubwa wote, tuwapende, tuwatii na tuwaombee. (Kut 20:12), Kol 3:20


Kwa sababu gani yatupasa kuwaheshimu Baba na Mama?

Yatupasa kuwaheshimu Baba na Mama kwa sababu;

1. Wameshirikiana na Mungu kutuleta duniani walipotuzaa
2. Wamewekwa na Mungu ili watulee na kutuongoza Mbinguni
3. Mungu ameamuru tuwapende wazazi mara baada ya Yeye. (Ayu 3:1-9)


Wazazi na wakubwa wameamriwa nini?

Wazazi na wakubwa wameamriwa watutunze na kutulea


Tuwaheshimu Baba na Mama kwa matendo gani?

Tuwaheshimu Baba na Mama kwa matendo ya adabu, heshima, utii na mapendo (Ayu 3:12)


Twawakosea Heshima Baba na Mama kwa kufanya nini?

Twawakosea Heshima Baba na Mama kwa;

1. Tukiwakasirisha na kuwatukana
2. Tukiwakaidi na kuwapiga
3. Tukiacha kuwaombea
4. Tukiacha kuwasaidia katika shida na uzee. (Kut 21:15-17)


Wazazi wawaleeje watoto wao katika imani ya Kikristo?

Wawalee hasa kwa mfano wao, kwa sala, kwa katekesi ya kifamilia na kushiriki maisha ya Kanisa


Lini tunakatazwa kuwatii watu?

Tunakatazwa kuwatii watu wanaotuamuru jambo lililokatazwa na Mungu (Mdo 5:29)


Katika Amri ya Nne ya Mungu tumekatazwa nini?

Tumekatazwa haya;

1. Kukaidi wazazi na wakubwa wetu
2. Kuwakasirisha.
3. Kuwadharau.


Wakubwa tunaopaswa kuwaheshimu ni kina nani?

Wakubwa hao ni;

1. Viongozi wa Kanisa
2. Viongozi wa Serikali
3. Walimu na walezi
4. Wakubwa wa kazi (War 13:1)
5. Viongozi wa Jumuiya

Amri za Kanisa: Mambo ya Muhimu kujua na Kuzingatia

Amri za Kanisa ni zipi?

Amri za kanisa ni;
1. Hudhuria Misa Takatifu Dominika na sikukuu zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya Majivu; usile nyama siku ya Ijumaa Kuu
3.Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Pasaka
5. Saidia Kanisa Katoliki kwa zaka
6. Shika sheria Katoliki za ndoa.


Katika Amri ya kwanza ya Kanisa tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tusikilize Misa kila siku ya Mungu na Sikukuu zilizoamriwa.


Sikukuu zilizoamriwa ni zipi?

Ndizo:

1. Kuzaliwa kwa Yesu – Noeli tarehe 25/12
2. Pasaka –
 Ufufuko wa Bwana Yesu
3. Kupaa Yesu —- Siku 40 baada ya Pasaka.
4. Kupalizwa Mbinguni Bikira Maria 15/8
5. Sikukuu ya Watakatifu Wote 1/11


Katika Amri ya Kwanza ya kanisa tumekatazwa nini?

Tumekatazwa;
1. Kukosa Misa
2. Kufanya kazi nzito siku hizo


Kujinyima ni nini?

Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.


Nani ana lazima ya kufunga?

Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula. (Jumatano ya Majivu)


Siku za kufunga ni zipi? Na siku gani tumekatazwa kula nyama?

Siku za kufunga ni Jumatano ya majivu, siku za Kwaresima isipokuwa Dominika zake, na siku iliyokatazwa kula nyama ni siku ya Ijumaa kuu.


Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa kuungama mara kwa mara walau mara moja kila mwaka


Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa tupokee Ekaristi Takatifu walau mara moja kwa mwaka wakati wa pasaka.


Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa kufahamu kuwa gharama za dini na za mapadre zatupasa. Yaanai wakristo walitegemeze Kanisa na wahudumu wake na hasa katika kazi ya kueneza injili.


Zaka ni nini?

Zaka ni asilimia kumi (10%) ya pato la mtu kwa mwaka ambalo anapaswa kulitoa kwa Kanisa.


Asiyelipa Zaka na michango mingine ya Kanisa ya lazima atenda dhambi gani?

Atenda dhambi kubwa: Yampasa kulipa na kuungama.


Amri ya Sita ya Kanisa Inadai nini?

Inadai kushika Sheria Takatifu Za ndoa

Angalia kilichomkuta huyu dada mwenye zarau, mwanae alikufa kwa zarau zake

Dada mmoja akiwa ofisini alipigiwa simu kuwa mwanae amepata ajali wakati anatoka shule, alikuwa ameumia sana. Kwa harakaharaka yule dada aliwasha gari na kuanza safari kuelekea hospitali ili kumuona mwanae.

Akiwa njiani katika mistari ya Zebra huku akiwa na mawazo alitaka kumgonga Kaka mmoja ambaye alikuwa akivuka barabara kwa kukimbia. Katika kumkwepa gari iligonga ukingo wa barabara na kukwaruizika kidogo.

Kwa hasira yule dada alishuka na kuanza kumtukana yule kijana kuwa kamsababishia ajali na kumchelewesha. Alimtukana sana, hali iliyowafanya watu kujaa. Watu walipofika walianza kuuliza nini ndipo yule dada kwa uoga alidanganya kuwa yule kaka alitaka kumuibia.

Watu walianza kumpiga Kaka wa watu kama mwizi, kuona vile yule dada aliingia kwenye gari na kuelekea hospitalini kumuona mwanae. Huku nyuma Polisi walikuja na kumuokoa yule kijana lakini akiwa ameumizwa sana.

Alifika hospitalini na kumkuta binti yake akiwa katika hali mbaya, alikuwa akitakiwa kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kuokoa maisha yake, manesi walishamuandaa mtoto na alikuwa akisubiriwa Daktari ambaye alipigiwa simu na alikuwa njiani.

Wakati wakimsubiri Daktari, Nesi alikuja na kuwamabia kuwa, wampeleke hospitali nyingine kwani Daktari waliyekuwa wakimsubiri asingeweza kumfanyia upasuaji mtoto wao kwani alikuwa amepigwa na wananchi wakati akija hospitalini wakimuita mwizi.

Dada na mumewe walichanganyikiwa, mtoto kutokana na hali yake mbaya alichukuliwa harakaharaka na gari la wagonjwa ili kuhamishwiwa hospitalini nyingine. Wakati wanatoka kuelekea kwenye gari kulikuwa na gari ya Polisi inaingia.

Kijana mmoja akiwa hoi alishushwa, yule Dada alimtambua ni yule kijana ambaye alimuitia mwizi kule barabarani. Kwa hasira yule Dada allimuambia Mume wake.
“Huyu Kaka namfahamu ni kibaka tu alitaka kuniibia, ndiyo amenichelewesha kufika huku hospitalini!”
Nesi ambaye alikuwa akimsaidia kumpandisha mtoto katika gari la wagonjwa alimkatisha na kusema.
“Hapana Dada huyu kaka si kibaka, ni Daktari ambaye alipaswa kumfanyia upasuaji mwanao. Amepigwa wakati akikimbia kuja hospitalini, mimi ndiyo nimempigia simu kuja…”

Dada wawatu nguvu zilimuishia ilibidi anyamaze, walifika hospitali nyingine, mtoto alikuwa katika hali mbaya. Aliandaliwa na kuingizwa katika chumba cha upasuaji lakini kabla hajafanyiwa chochote yule mtoto alifariki.

Baada ya uchunguzi ilionekana damu ilishaingia kwenye ubongo. Wangeweza kuokoa maisha yake kama angefanyiwa upasuaji katika hospitali ya mwanzo, kule kusafirishwa tena na kurushwa rushwa barabarani kulisababisha damu kuendelea kuvuja kwa kasi ndani.

Yule dada alizimia baada ya kupata habari zile, maneno yake yalisababisha kuondoa maisha ya mwanae.

FUNZO

Usimdharau mtu kutokana na hali yake kwani hujui ni kitu gani anaweza kukusaidia.

Tabia za wachepukaji

WACHEPUKAJI WENGI WANATABIA HIZI

1.Hachezi mbali na simu yake kila wakati.
2.Inbox na sending items hufutwa kila
wakati.
3.Ukimuomba simu yake ghafla lazima
akwambie hebu
kwanza…….
4. Kamwe haiiti always vaibration.
5. Namba nyingi ha save.
6. Kuna simu hapokei hata
iweje….anapenda sms zaidi
7.Majina mengi kwenye simu yameseviwa
kwa majina ya
kufikirika.
8.Muda mwingi ni mtu wakujihami.
9.Anapenda password na anabadili mara
kwa mara.
10.Akiazima simu yako, akitumia tu
anafuta dial no
haraka.
11.Always yuko na simu…..hadi bafuni
ikibidi.
12. Anajazba ukimuuliza chochote kuhusu
simu….anajishtukia.
13. Akiwa anachati anakuangalia mara kwa
mara
kiwiziwizi
14. Hana jeuri ya kukuweka profile picture
na akikuweka
humalizi masaa anakudampu huko
Hapa kuna ukweli asilimia millioni moja
kabisa
Share na washikaji zako😜😜😜😜😜

Sababu na tiba ya tatizo la kukoroma usiku: Kukoroma unapolala

Kukoroma ni tatizo linalowapata watu wengi wakati wanapolala ambalo linaweza kuwatokea watu wa kila umri ingawa hutokea mara nyingi kwa wanaume au watu wanene. Kukoroma huzidi kwa kadri umri unavyoongezeka na asilimia 54 ya watu wazima hukoroma baadhi ya wakati huku asilimia 25 ya wengine wakiwa na tabia ya kukoroma kila wakati. Kukoroma baadhi ya wakati kwa kawaida sio tatizo kubwa na mara nyingi huleta tu karaha kwa mtu anayelala karibu na mkoromaji.

Hata hivyo kukoroma huko sio tu kwamba huharibu usingizi wa anayekoroma bali pia huwasumbua na kuwakeresha wanaolala karibu na mkoromaji. Wale wenye tabia ya kukoroma, hukoroma kila wanapolala na mara nyingi huchoka wanapoamka, na watu wa aina hii hushauriwa kumuona daktari na kushauriwa kuhusiana na tatizo hilo. Lakini kabla hatujaendela mbele ni bora tujue kukoroma hasa ni nini au hutokea vipi?

Mtu huwa anakoroma pale kunapokuwa na kitu au sababu yoyote itakayoziba kuingia au kutoka kwa hewa mdomoni na katika pua. Kuta za koo hutikisika wakati wa kupumua na matokeo yake ni sauti inayosikika ya kukoroma. Kuingia au kutoka kwa hewa huweza kuzuiwa na sababu mbalimbali kama vile:

• Kuziba tundu za pua kusiko kamili ambako husababisha nguvu zaidi zitumike katika kupitisha hewa kwenye pua wakati mtu akiwa amelala. Kitendo hicho hupelekea nyama laini za pua na koo zijikusanye na kusababisha mkoromo.

Kuna baadhi ya watu wanakoroma tu kipindi cha allergy (allergy season) au wanapatwa na matatizo ya sinus. Baadhi ya matatizo kama vile kupinda pua (deviated septum) au ukuta unaotenganisha tundu za pua na polyps za pua pia huweza kufanya pua zizibe na kusababisha kukoroma. Watu wengi wanaofanya operesheni za pua pia hupatwa na tatizo la kukoroma.

• Kuwa na misuli dhaifu katika koo na ulimi. Misuli au nyama za koo na ulimi zinapokuwa dhaifu sana hulegea na kuanguka upande wa nyuma wa sehemu inayopita hewa. Suala hilo hutokea pale mtu anapolala fofofo au kuwa na usingizi mzito na kusababisha kukoroma.

• Kuwa na misuli minene ya koo. Hii ni kwa wale watu wanene ambao hata nyama zao za koo pia hunenepa na kupanuka na suala hilo husababisha kukoroma, Pia watoto wenye tonsesi kubwa na adenoids baadhi ya wakati hukoroma.

• Kuwa na kilimi kikubwa ni mojawapo ya sababu zinazosababisha kukoroma. Kilimi kirefu kinaweza kuzuia koo na pale kinapotikisika wakati hewa inapita kwa msukumo husababisha kukoroma.

• Sababu nyinginezo zinazoweza kumsababishia mtu akorome anapolala ni kuwa na umri mkubwa au uzee, imeshuhudiwa kuwa watu wa makamo na wazee hukoroma, kwani misuli na nyama za koo huanza kuzeeka na kulegea kadri umri unayoongezeka. Vilevile wanaume wanakoroma zaidi kuliko wanawake hii ni kutokana na wanaume kuwa na njia nyembamba zaidi ya hewa kuliko wanawake.

Kukoroma pia kunaweza kuwa ni tatizo la kurithi. Pombe, kuvuta sigara na matumizi ya baadhi ya dawa pia husababisha misuli ya koo ilegee na hivyo hupelekea mtu akorome. Kulala vibaya pia husababisha kukoroka kama vile kulala kichalichali, kwani hufanya nyama za koo zilegee na kuziba hewa.

Je, Dawa ya kukoroma ni nini?

Swali hilo limeulizwa sana na mimi katika kulijibu ningependa kusema kuwa, kujua sababu inayosababisha mtu akorome na kuitatua au kuiondoa sababu hiyo ndiko kunakotibu kukoroma.

Sote tunajua adha inayotokana na kukoroma, na sauti hiyo inavyosumbua hasa iwapo anayekoroma ni mtu wako wa karibu kama vile mumeo, mwenzi wako au yoyote yule inayekubidi ulale naye karibu au katika kitanda kimojana hata chumba kimoja. Kukoroma pia huathiri usingizi wa mkoromaji kwani anayekoroma humbidi aamke mara kadhaa usingizini akijua au bila kujua kutokana njia zake za hewa kufunga kwa sekunde kadhaa ambapo usingizi pia hukatika.

Wanaokoroma pia hushindwa kulala vizuri suala linalopelekea asubuhi wawe wamechoka na kutofanya majukumu yao vyema, na pia wale wanaolala nao karibu hupatwa na matatizo kama hayo. Vilevile tunapaswa kujua kuwa kukoroma kuna athari za kiafya za muda mrefu kwa mtu anayekoroma hivyo si jambo la kufanyia mzaha na ni tatizo ambalo linapaswa kushughulikiwa na kutatuliwa.

Wataalamu wanatuambia kuwa ili kujua kukoroma kwako kunasababishwa na nini ni bora ushirikiane na mwenzi wako au yoyote unayelala naye ili akuchunguze pale unapolala na kujua jinsi mwili wako unavyokuwa pale unapokoroma.

Ni bora aandae orodha na kuchunguza yafuatayo:

1. Kufunga mdomo na kukoroma kunaonyesha kuwa kuna matatizo ya ulimi.

2. Kufungua mdomo na kukoroma kunaonyesha unaweza kuwa na tatizo katika misuli au nyama za koo.

3. Kukoroma unapolala kichalichali kunaonyesha kuwa pengine kwa kubadilisha namna unavyolala kukoroma nako kunaweza kwisha.

4. Kukoroma wakati unapolala kwa kila mlalo kunaonyesha kwamba tatizo lako ni kubwa na pengine kunahitajia tiba kubwa zaidi.

Tiba

Iwapo umebadilisha namna unavyolala na haikusaidia, unashauriwa ujaribu yafuatayo:

Punguza uzito

Safisha njia yako ya hewa.

Kuwa na pua iliyoziba hufanya kupumua kuwe kugumu na kusababisha kukoroma. Unaweza kufanya hivyo kwa kutumia dawa za kusaidia kupumua kwa urahisi (nasal decongestants) zinazopatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa.

Wacha kuvuta sigara.

Lala mapema na pata usingizi wa kutosha kila mara huku ukijiepusha na kuchoka sana.

Nyanyua kichwa

Kunyanyua kichwa kwa nchi 4 huweza kupunguza kasi ya kupumua na kusaidia ulimi na taya kwenda mbele hali ambayo hupunguza kukoroma. Fanya hilo kwa tumia mito maalum ya kupunguza kukoroma au lala bila mto.

Kula vyakula hivi

Wataalamu pia wanasema kwamba unaweza kupunguza kukoroma kwa kutokula baadhi ya vyakula au dawa kabla ya kulala ambavyo huongeza kukoroma. Vitu hivyo ni kama vile;

  • Kutokula mlo mkubwa kabla ya kulala.
  • Kutokula vyakula vinavyotokana na maziwa au maziwa ya soya.
  • Kutokunywa pombe kabla ya kulala.
  • Kutotumia dawa aina ya antihistamines.
  • Kutotumia vyakula au vinjwaji venye kafeini.

Vilevile wanaokoroma wanashauriwa kufanya mazoezi ya koo ambayo ni pamoja na kuimba, kusoma kwa kurudia rudia voweli (a,e,i,o,u) kwa nguvu kwa dakika tatu mara kadhaa kwa siku, kuweka ncha ya ulimi chini ya meno ya mbele na kurudisha ulimi nyuma kwa dakika 3 kila siku au huku mdomo ukiwa wazi pelekea taya yako upande wa kulia na wacha ibakie katika hali hiyo kwa sekunde 30.

Huku mdomo ukiwa wazi, kaza misuli ya nyuma ya koo na rudia kitendo hicho kwa sekunde thelathini. Unaweza kutizama kwenye kioo na kuona jinsi kilimi kinavyokwenda juu na chini.
Iwapo kukoroma hakutoisha kwa kutumia njia hizo tofauti zilizoelezwa, usife moyo jaribu kumuona

Daktari na akupe ushauri wa kitiba kuhusiana na tatizo hilo. Madakatari wataalamu wa magonjwa ya pua, masikio na koo au ENT wanaweza kukusaidia zaidi kutatua tatizo hilo. Siku hizi kuna vifaa mbalimbali vinavyotumiwa mahospitalini ili kuondoa kukoroma kama vile kifaa kinachowekwa kwenye meno, CPAP, kidude kinachowekwa mdomoni au hata kufanyiwa operesheni ili kuondoa tatizo hilo.

++ TIBA YA MBADALA YA KUACHA KUKOROMA
Dawa ya kukoroma Fanya hivi: Fungua mdomo wako mpaka mwisho, toa ulimi na usukume nje mpaka mwisho, rudisha ulimi ndani mpaka mwisho-rudia mara 20. Ukimaliza utahisi kuna misuli nyuma

na pembeni ya koo umeifanyisha kazi,sasa misuli hii ikilegea ndio inayosababisha kukoroma. Fanya zoezi hili mara 2 mpaka 3 kwa siku na tatizo hili litaisha baada ya siku 10-20 kutegemea mtu hadi mtu.

Unafahamu kuwa Imani ni Cheti cha Kuweza Kupata Yote?

Utangulizi

Imani ni kuwa na uhakika hata kwa mambo yasiyoonekana na yasiyowezekana. Ni kujua au kutarajia kwa uhakika kwa mambo ambayo bado hayajawa bayana (wazi) kuwa yapo au yatafanyika.

Kwa Imani Kila Kitu Kinawezekana. Kwa Sala na kwa Matendo.

Yesu Kristu anatufundisha tuwe na Imani kupitia Mfano huu;

18Yesu alipokuwa anarudi mjini asubuhi na mapema, aliona njaa. 19Akauona mtini mmoja kando ya njia, akauendea; lakini aliukuta hauma chochote ila majani matupu. Basi akauambia, “Usizae tena matunda milele!” Papo hapo huo mtini ukanyauka.

20Wanafunzi walipouona walishangaa wakisema, “Kwa nini mtini huu umenyauka ghafla?” 21Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani bila kuwa na mashaka, mnaweza si tu kufanya hivyo, bali hata mkiuambia mlima huu: Ng’oka ukajitose baharini, itafanyika hivyo. 22Na mkiwa na imani, chochote mtakachoomba katika sala, mtapata.”
Mathayo 21:18-22

Basi Ili tuweze kuwa na Imani tumuombe Mungu atujalie Imani. Tuombe tujaliwe fadhila ya Imani hasa Tunaposali. Vile vile tumwombe Mungu atujalie Imani katika yale yote tunayoyafanya.

Tuombe hasa Imani isiyokuwa na Mashaka. Mashaka na Kusita sita ndiyo adui mkubwa wa Imani.

Imani ni Cheti cha Kuweza Kupata Yote

Imani ni kuwa na uhakika hata kwa mambo yasiyoonekana na yasiyowezekana. Ni kujua au kutarajia kwa uhakika kwa mambo ambayo bado hayajawa bayana kuwa yapo au yatafanyika. Imani ni msingi wa maisha ya Kikristo, na ni muhimu kuelewa jinsi inavyofanya kazi na jinsi inavyoweza kubadilisha maisha yetu. Katika maisha ya kiroho, imani inaweza kulinganishwa na cheti kinachokupa uwezo wa kupokea baraka na neema zote kutoka kwa Mungu. Kama cheti kinavyokupa sifa na uwezo wa kupata kitu, vivyo hivyo, imani inatupa uwezo wa kupokea kutoka kwa Mungu.

Imani ni Cheti cha Kuweza Kupata Yote

Kama vile cheti kinavyothibitisha sifa zako za kupokea kitu fulani, imani yetu inathibitisha sifa zetu mbele za Mungu na kutupa uwezo wa kupokea baraka zake. Bila imani, ni vigumu kupokea kutoka kwa Mungu kwa sababu imani ndio msingi wa uhusiano wetu naye. Waebrania 11:1 inasema:

“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” (Waebrania 11:1)

Imani inatufanya tuwe na matumaini na kuamini kwamba mambo ambayo tunatarajia yatatimia, hata kama hatuyaoni bado kwa macho yetu ya kawaida.

Imani Inafanya Kila Kitu Kinawezekana

Kwa imani, hakuna lisilowezekana. Imani inafanya miujiza iwe sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Kwa sala na matendo, imani yetu inadhihirika na kuwa na nguvu za kutenda mambo makubwa. Yesu Kristo anatufundisha kuwa na imani kupitia mfano huu kutoka Mathayo 21:18-22:

“Yesu alipokuwa anarudi mjini asubuhi na mapema, aliona njaa. Akauona mtini mmoja kando ya njia, akauendea; lakini aliukuta hauna chochote ila majani matupu. Basi akauambia, ‘Usizae tena matunda milele!’ Papo hapo huo mtini ukanyauka. Wanafunzi walipouona walishangaa wakisema, ‘Kwa nini mtini huu umenyauka ghafla?’ Yesu akawajibu, ‘Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani bila kuwa na mashaka, mnaweza si tu kufanya hivyo, bali hata mkiuambia mlima huu: Ng’oka ukajitose baharini, itafanyika hivyo. Na mkiwa na imani, chochote mtakachoomba katika sala, mtapata.'” (Mathayo 21:18-22)

Yesu anatufundisha kuwa na imani thabiti bila mashaka. Anatushawishi kuelewa kwamba kwa imani, tunaweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu, hata kuhamisha milima.

Kuomba Imani kutoka kwa Mungu

Ili tuweze kuwa na imani, tunapaswa kumwomba Mungu atujalie imani. Imani ni zawadi kutoka kwa Mungu, na tunahitaji kumwomba atupe fadhila hii tunaposali. Kwa kumwomba Mungu, tunapata nguvu na uhakika wa kuamini bila kusita.

Yakobo 1:6-7 inasema:

“Lakini aombe kwa imani, pasipo shaka yoyote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo na kupeperushwa huku na huku. Mtu kama huyo asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.” (Yakobo 1:6-7)

Hii inatukumbusha umuhimu wa kuomba kwa imani isiyokuwa na mashaka. Mashaka na kusita-sita ni adui mkubwa wa imani, na ni lazima tuwe na imani kamili ili tuweze kupokea kutoka kwa Mungu.

Imani Katika Sala na Matendo

Imani yetu inapaswa kudhihirika si tu katika sala zetu bali pia katika matendo yetu ya kila siku. Tunapomwomba Mungu kwa imani, tunapaswa pia kuchukua hatua kwa imani, tukiamini kwamba Mungu atatenda. Yakobo 2:17 inasema:

“Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake.” (Yakobo 2:17)

Imani bila matendo ni imani isiyo na uhai. Tunapomwomba Mungu kwa imani, tunapaswa pia kuwa tayari kuchukua hatua kwa kuamini kwamba Mungu atatenda kupitia juhudi zetu.

Kuomba Imani Thabiti

Tunapomwomba Mungu atujalie imani, ni muhimu tuombe imani thabiti isiyokuwa na mashaka. Yesu alitufundisha kwamba tunaweza kufanya mambo makubwa kama tu tuna imani bila mashaka. Kwa hiyo, tuombe kwa bidii ili tujaliwe na Mungu imani inayoweza kuhamisha milima, imani inayoweza kufanya mambo yasiyowezekana yawezekane.

Mifano Halisi ya Imani katika Biblia

Biblia imejaa mifano ya watu waliojawa na imani na jinsi walivyoweza kupata mambo makubwa kupitia imani yao. Hapa kuna mifano sita ya imani kutoka katika Biblia:

  1. Ibrahimu:
    Ibrahimu alionyesha imani kuu kwa Mungu alipoambiwa kumtoa mwanawe Isaka kama sadaka. Alikuwa tayari kumtii Mungu, akiamini kwamba Mungu anaweza kumfufua Isaka kutoka kwa wafu. Imani yake ilimfanya awe baba wa mataifa mengi. (Waebrania 11:17-19)
  2. Musa:
    Musa alionyesha imani alipowaongoza Waisraeli kutoka utumwani Misri, licha ya changamoto nyingi alizokutana nazo. Aliamini ahadi za Mungu na kuamini kwamba Mungu atawatua kwenye nchi ya ahadi. (Waebrania 11:24-29)
  3. Yoshua na Yeriko:
    Yoshua alionyesha imani alipowaongoza Waisraeli kuzunguka ukuta wa Yeriko kwa siku saba kama alivyoamriwa na Mungu. Siku ya saba, ukuta wa Yeriko ulianguka, na Waisraeli walishinda mji huo. (Yoshua 6:1-20)
  4. Danieli:
    Danieli alionyesha imani kubwa alipoendelea kumwomba Mungu licha ya amri ya mfalme ambayo ilipiga marufuku maombi. Aliwekwa kwenye tundu la simba, lakini Mungu alimlinda na simba hawakumdhuru. (Danieli 6:10-23)
  5. Mwanawake aliotokwa na Damu:
    Mwanamke aliyekuwa akitokwa na damu kwa miaka kumi na miwili alionyesha imani kubwa alipogusa vazi la Yesu akiamini kwamba ataponywa. Imani yake ilimponya mara moja. (Marko 5:25-34)
  6. Petro:
    Petro alionyesha imani alipomwomba Yesu amruhusu kutembea juu ya maji. Alipoanza kutembea juu ya maji kuelekea kwa Yesu, aliona nguvu za Mungu. Ingawa alianza kuzama alipokuwa na mashaka, imani yake ilimfanya aweze kutembea juu ya maji kwa muda. (Mathayo 14:28-31)

Hitimisho

Imani ni cheti cha kuweza kupata yote. Kwa imani, tunaweza kuona mambo makubwa yakitendeka katika maisha yetu. Imani inatufanya tuwe na uhakika wa mambo yasiyoonekana na yasiyowezekana. Tunapaswa kumwomba Mungu atupe imani thabiti, na imani hiyo inapaswa kudhihirika katika sala na matendo yetu ya kila siku. Kwa kumtumaini Mungu bila mashaka, tunaweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu, tukijua kwamba kwa imani, kila kitu kinawezekana.

Kumtafuta Mungu ni Jukumu lako Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Huwezi kumfuata Mungu kwa kufwata njia ya wengine. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine, Kwa maana Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee.

Melkisedeck Leon Shine

Kumtafuta Mungu: Jukumu la Mtu Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Kila mmoja wetu ana safari ya kiroho inayomwita kumtafuta Mungu kwa njia yake mwenyewe. Safari hii ni ya kipekee na haifanani na ya mwingine yeyote. Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee, akitufundisha na kutuongoza kupitia maisha yetu binafsi. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa, bali ni uamuzi wa kibinafsi unaohitaji moyo wa kujitolea na utayari wa kipekee.

“Nitajitokeza kwenu, nanyi mtaniona; nanyi mtakaponiomba, nitasikiliza.” (Yeremia 29:12-13)
“Wakati unapotaka kujua mambo ya Mungu, basi mpe nafasi, naye atakujulisha siri zake.” (Amosi 3:7)
“Ee Mungu, Mungu wangu, nakutafuta asubuhi; roho yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakutamani, katika nchi kame na yenye kuia, isiyo na maji.” (Zaburi 63:1)

Njia ya Kipekee ya Kumtafuta Mungu

Huwezi kumfuata Mungu kwa kufuata njia ya wengine. Ingawa tunaweza kupata mwongozo na msaada kutoka kwa wale walio karibu nasi katika jumuia au kanisa, ni muhimu kutambua kuwa kila mtu ana njia yake ya kumfikia Mungu. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine. Hii ni kwa sababu Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee. Katika ulimwengu huu wa tofauti na utofauti, Mungu anazungumza nasi kwa njia ambazo zinaendana na maisha yetu binafsi na hali zetu za kipekee. Hili ni jambo la kibinafsi na si suala la jumuia au kanisa.

“Kwa maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu, asema Bwana.” (Isaya 55:8)
“Pendo la Mungu limemiminwa mioyoni mwetu na Roho Mtakatifu tuliyekirimiwa.” (Warumi 5:5)
“Mmoja na mmoja wenu, ajaribu sana kutafuta kibali mbele za Bwana, kwa moyo wote, maana hatuwezi kumpendeza Mungu bila imani.” (Waebrania 11:6)

Kutembea Katika Wito Wako

Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee. Kila wito unaambatana na vipawa, changamoto, na fursa ambazo ni za kipekee kwa kila mmoja wetu. Kwa hivyo, ni muhimu kumsikiliza Mungu katika maisha yako na kutembea katika wito wako binafsi. Hii inamaanisha kujifunza kusikiliza sauti ya Mungu katika maombi, kusoma Neno lake, na kutafakari juu ya maisha yako. Kutembea katika wito wako ni hatua ya kibinafsi inayohitaji kujitolea na uwazi wa moyo.

“Bali nyote mtakuja kwa njia ya utulivu na kunyamaza; na mtafakari kwa utulivu wa moyo, ndipo mtakapoona nuru ya Bwana.” (Isaya 30:15)
“Jitoe kwa Bwana, na umetulie mbele zake; nawe atakupatia maombi ya moyo wako.” (Zaburi 37:4)
“Naye atatenda katika njia zako, atakuongoza kwa haki na njia zake zote.” (Mithali 3:6)

Umuhimu wa Maombi na Tafakari

Kumtafuta Mungu kunahitaji muda wa maombi na tafakari. Huu ni wakati wa kuwa kimya mbele za Mungu, kumwambia mahitaji yako, na kumsikiliza. Maombi ni mazungumzo na Mungu, na ni katika mazungumzo haya tunapopata mwongozo wa kiroho. Tafakari juu ya Neno la Mungu na jinsi linavyohusiana na maisha yako binafsi ni muhimu katika safari hii ya kiroho. Hili ni jukumu la kibinafsi, ambalo linaweza kufanyika vyema wakati unapotenga muda maalumu kuwa peke yako na Mungu.

“Basi, kesheni, mkiomba kila wakati, ili mweze kuokoka mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.” (Luka 21:36)
“Kwa maana mkimtafuta kwa bidii mtampata, mkimtafuta kwa moyo wenu wote.” (Yeremia 29:13)
“Jilindeni, ninyi wenyewe, na usiache moyo wako upotee, bali mwombe Mungu kwa bidii, naye atakujulisha mapenzi yake.” (Yakobo 1:5)

Kusikiliza Sauti ya Mungu

Mungu anaweza kuzungumza nasi kwa njia nyingi tofauti. Anaweza kuzungumza kupitia Neno lake, kupitia watu wengine, au kupitia matukio katika maisha yetu. Ni muhimu kuwa na moyo wazi na kusikiliza kwa makini sauti ya Mungu. Unapokuwa na utayari wa kusikiliza na kufuata mwongozo wake, utaona njia zako zikifunguka na kupata mwanga mpya wa kiroho. Hii ni safari ya kibinafsi inayohitaji kujitoa na kuwa na moyo wa kusikiliza.

“Kwa maana Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara mbili, lakini mwanadamu hajali.” (Ayubu 33:14)
“Ee Bwana, unayenifundisha na kuniongoza kwa njia ya haki, unayenipenda kwa upendo wa milele.” (Zaburi 32:8)
“Ee Mungu, unayejua kila kitu, unayejua kwamba nakupenda. Unayejua kwamba nakutafuta kwa moyo wote.” (Yohana 21:17)

Kumtafuta Mungu ni Jukumu la Kibinafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na si suala la jumuia au kanisa. Mwisho wa siku, kila mmoja wetu atahitajika kusimama peke yake mbele za Mungu na kutoa hesabu ya maisha yake. Hatutaweza kutumia njia za wengine kama kigezo cha safari yetu ya kiroho. Ni muhimu kuchukua jukumu la kumtafuta Mungu kwa bidii na moyo wote, kwa kuwa hatimaye, ni uhusiano wetu binafsi na Mungu ndio utakaotupa uzima wa milele.

“Kwa maana kila mmoja wetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12)
“Usiwe na hofu, maana mimi nipo nawe; usishike, maana mimi ndimi Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia; naam, nitakushika kwa mkono wangu wa kuume wa haki.” (Isaya 41:10)
“Lakini wewe, unaposali, ingia katika chumba chako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini atakupa.” (Mathayo 6:6)

Katika safari ya kumtafuta Mungu, kumbuka kwamba ni jukumu lako binafsi na nafsi yako. Usijaribu kufuata njia ya mwingine, bali tembea katika njia yako binafsi ambayo Mungu ameiweka mbele yako. Kwa kufanya hivyo, utaweza kumfikia Mungu kwa undani na kujenga uhusiano wa kipekee na wa kweli naye. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa; ni mwito wa ndani unaohitaji kujitoa na kuwa tayari kusimama peke yako mbele za Mungu.

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia tango

Tango ni tunda na ni mboga pia na ni chanzo kizuri cha potasiamu na vitamini nyingi ambazo zina kazi mhimu katika ngozi yako na huifanya ngozi ngozi ionekane laini na yenye kupendeza.

Tango ni moja kati ya dawa kamili za kutibu chunusi. Ni rahisi kulitumia tango kutibu chunusi.

Kata tango katika silesi ndogo ndogo na uvibandike juu ya ngozi yenye chunusi. Kumbuka kusafisha kwanza ngozi yako kabla ya kubandika hizi silesi za tango.

Namna nyingine na kusaga tango upate juisi yake na uchanganye na sukari kasha jisuguwe kwenye ngozi yenye chunusi kwa dakika 2 au 3 kisha jisafishe na maji safi.

Misemo 10 bora ya kuchekesha itakayokuacha mdomo wazi

1. Mwanaume hata awe bahili vipi, hawezi kumpa mwanamke mimba nusu.

2. Hata uwe na magari mangapi chooni utaenda kwa miguu.

3. Kama ubinadamu kazi mbona hatupewi mishahara?

4. Ukichanganya wali na choroko unapata mseto, lakini hautibu malaria.

5. Hata njiwa nae ana makinda, lakini hawezi kuwa spika wa Bunge.

6. Hata uwe na haraka vipi kwenda Zenj, huwezi kupanda Jahazi ya Yusuph Mzee.

7. Umeme hauna kiuno lakini unaongoza kwa kukatika.

8. Hata uwe kauzu vipi, huwezi kujamba wakati unatongoza.

9. Hata uwe na imani kali vipi, huwezi kusali wakati unafanya mapenzi.

10. Hata kizibo ni mfuniko lakini hauwezi
kufunika sufuria.

Maisha ya Pwani ni Shidaaaaah

😆😆 😂😂😂😂😂😂 Jamaa kagombana na mkewe, akasusa kula🍽🍨 kurudi kazini kamkuta mkewe amevaa kanga imeandikwa ukisusa wenzio wala ilipofika asubuhi mke akavaa kanga imeandikwa ukitoka 🚶🚶mwenzio anaingia💃💃

jamaa akagoma kwenda kazini 😬😬 mke akabadili kanga na kuvaa iloandikwa nimemdhibiti ndo mana hatoki🚷 jamaa akaenda kuomba ushauri kwa rafiki yake akaambiwa twende nyumbsni kwako, walipofika walimkuta mke kavaa kanga imeandikwa ulidhani rafiki yako kumbe adui yako🤔🤔 jamaa akaamua kusafiri siku tano ili kupunguza hasira. Aliporudi akamkuta mke amevaa kanga imeandikwa ni bora nimpe jirani kuliko kiozee ndani
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

hata kama hupendagi ujinga kwa maneno ya kwenye kanga utasanda tu

Maana ya jina Bikira Maria

Jina asili kwa Kiaramu ni מרים, Maryām lenye maana ya “Bibi”; watafsiri wa kwanza wa Biblia ya Kiebrania wanaojulikana kama Septuaginta (LXX) waliliacha kama lilivyo wakiandika kwa Kigiriki Μαρίαμ, Mariam, au walilifupisha wakiandika Μαρία, Maria.
Katika Kurani jina hilo kwa Kiarabu ni مريم, Maryam.
Jina hili limeenea sana duniani kote, hasa kwa heshima ya mama wa Yesu.
Anatajwa kwa kawaida kwa kutanguliza sifa yake mojawapo, hasa Bikira.
Mapokeo ya karne ya 2 (Injili ya Yakobo) kuhusu Bikira Maria yanasema alikuwa binti pekee wa Yohakimu na Ana. Lakini habari muhimu zaidi ni zile zinazopatikana katika Biblia ya Kikristo.

Ishi kama Penseli ili uwe mtu bora

Muumbaji wa penseli alipomaliza kuiumba penseli yake aliiambia mambo muhimu ya kuzingatia ili iweze kuwa penseli bora kabla hajaituma kuingia kazini kwa matumizi.

“Kuna vitu sita unatakiwa uvitambue, “ Aliiambia penseli,

“Kabla sijakutuma kwenda kutumika, unatakiwa uviweke akilini vitu hivyo na usivisahau kamwe. Vitakusaidia siku zote na utakuwa penseli bora maisha yako yote.”

Alisema muumbaji wa penseli.

“Moja,” alianza kuvitaja,”utakuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi, lakini kama utakubali na utaruhusu kuongozwa na mkono wa mtumiaji wako”

“Mbili” aliendelea kutoa nasaha, “utapata maumivu makali kutokana na kuchongwa mara kwa mara. Lakini vumilia kwani itakusaidia kuwa penseli bora na kuandika vizuri.”

“Tatu, utakuwa na uwezo wa kusahihisha makosa utakayo yafanya.”

“Nne, kitu pekee cha muhimu katika maisha yako ni kile kilicho ndani yako kwa sababu ndicho chenye uwezo wa kuandika.”

“Tano” alisisitiza mtengenezaji penseli, “kwenye kila sehemu utakayotumika, utaacha alama yako. Hata ikiwa ni kwenye sehemu ngumu au mbaya kiasi gani, ni lazima alama yako ibaki.

“Na sita”, alimalizia muumbaji yule wa penseli, “ipo siku utaisha na kupotea. Hivyo usiwe na hofu wala woga wala hudhuni uikaribiapo siku hiyo na ukaogopa kutimiza wajibu wako kwa kuhofia kuisha. Ukiogopa kuisha hautotumika na umuhimu wako hautonekana kwani hautatimiza wajibu uliombiwa kuufanya”

Penseli ilielewa na kuahidi kukumbuka na ikaingia sokoni ikiwa na dhamira yake moyoni.

Sasa tutumie mfano huo wa penseli katika maisha yetu halisi. Ukivikumbuka vitu hivyo sita ilivyopewa penseli, utaweza kuwa mtu bora kabisa kwenye maisha yako yote.

Moja, una uwezo wa kufanya mambo mengi na makubwa, kama utajiweka kwenye mikono ya Mungu.

Mbili, utakutana na magumu mengi ya kuumiza, lakini hayo ndiyo yatakufanya uwe mtu imara na bora, usiyakimbie.

Tatu, una uwezo wa kurekebisha makosa yote uliyoyafanya. Usijilaumu.

Nne, sehemu yako ya muhimu ni ile iliyo ndani yako kwani ndiyo inayoandika maisha yako. Ilinde.

Tano, kila sehemu utakayopita, acha alama yako kwa kufanya mazuri yatakayokufanya ukumbukwe daima, bila kujali mazingira. Timiza wajibu wako kwa kiwango cha juu.

Sita, tambua kuwa ipo siku utakufa. Usiwe na hofu yoyote juu ya kifo kwani ukiogopa kifo hutafanya lolote hapa duniani.

Tumia mfano huu wa penseli upate ujasiri wa kutambua kuwa wewe ni mtu muhimu hapa duniani na umeumbwa kwa madhumuni maalumu na umepewa uwezo mkubwa sana na Muumba wako! Ni wewe pekee mwenye uwezo wa kutimiza dhamira uliyotumwa na Muumba.

UBARIKIWE SANA.

Angalia huyu secretary anavyomjibu bosi wake

Boss mmoja aliingia kazini kwake kasahau kufunga zipu ya suruali yake sasa secretary wake akamfuata na mazungumzo yakawa hivi:

SECRETARY: Boss leo umesahau kufunga geti nyumbani kwako…

Boss akabaki anashangaa… Baadae wakati anakwenda chooni kujisaidia ile anataka kufungua zipu akaikuta iko wazi ndio akajua alichokuwa ameambiwa na Secretary wake.

Akarudi mpaka kwa secretary na mazungumzo yakaendelea:

BOSS: Bibie ulivyoona geti wazi je uliona benz langu lime paki au…?

SECRETARY: Hapana Boss niliona kitoroli kidogo kimepaki kina matairi mawili

MAANA YA SALA KWA MKRISTO

Sala ni kuinua mioyo yetu kwa Mungu na kuongea nae. Watu wote wanapaswa kusali, wema na wabaya. Inatupasa kusali kila siku bila kukata tama kwa ibada, kwa matumaini na kwa saburi. Kama mfano Yesu Alitufundisha sala ya Baba yetu.
Yatupasa kuwaombea wengine, watu wote wenye shida wakosefu na hata maadui zetu, vilevile tumtolee Mungu shukrani kila wakati na hasa kwa kuadhimisha Ekaristi Takatifu.
Masifu ni sala au wimbo unaomsifu na kumtambua Mungu kuwa Mungu.
Sababu za kusali
1. Kumuabudu Mungu
2. Kumshukuru Mungu
3. Kuomba Neema na Baraka kwa ajili yetu na wenzetu
4. Kuomba msamaha
Namna za sala
1. Sala ya sauti : Sala asaliyo mtu au kikundi kwa kutumia maneno
2. Sala ya fikra : Sala asaliyo mtu akiwa peke yake au na wengine kimya kimya akimuwaza Mungu.
3. Sala ya Taamuli: Kumtazama tuu Mungu kwa upendo Mkubwa Moyoni.
Nyakati zote zinafaa kwa sala hasa
1. Asubuhi na jioni
2. Kabla na baada ya kula
3. Kila dominika
4. Sikukuu za amri
5. Kabla na baada ya kazi
6. Katika kishawishi
Vyanzo vya sala za Kikristo
1. Neno la Mungu
2. Liturujia ya Kanisa
3. Fadhila za Kimungu
4. Matukio ya kila siku
Aidha Roho Mtakatifu ndiye mlezi wa ndani wa sala ya Kikristo akitufundisha kusali na kusali ndani mwetu.
Sala Muhimu kwa Mkristo
Sala kubwa ya kanisa ni Misa Takatifu na sala Bora kwa Bikira Maria ni Rozari Takatifu.
Sala nyingine Muhimu kwa Mkristu ni:
1. Baraka ya Sakramenti kuu
2. Andamo la Ekaristi
3. Litania Takatifu
4. Njia ya Msalaba
5. Rozari takatifu
6. Novena
Mtu anaweza kusali popote lakini kanisani ndio mahali rasmi pa sala, Aidha familia ni shule ya kwanza ya sala ambapo mtu hujifunza na kujizoesha kusali anapokua katika familia.
Changamoto na majaribu wakati wa kusali
1. Mtawanyiko wa mawazo
2. Ukavu wa Moyo
3. Uvivu na uregevu
Faida ya Sala
1. Zinaleta neema nyingi
2. Zinatuimarisha ili tushinde vishawishi na dhambi
3. Zinatuunganisha na Mungu
4. Zinatudumisha katika kutenda mema
Neno Amina katika sala linamaana ‘Na iwe hivyo’. Na neno Aeluya maana yake ni Msifuni Mungu.

Soma hii, kama wewe ndio mzazi wa huyu msichana ungefanyaje?

Wewe ni mzazi mwanao anasoma kidato cha tatu mkoani umemsafirisha leo kwenda shule baada ya masaa matano ukasikia gari alilo panda mwanao limepata ajali wamekufa watu wote upo ktk harakati za kuandaa msiba,

mwanao anakupigia simu baba/mama mimi mzima sijafa mpenzi wangu ABDUL aliniambia nishuke Chalinze ili niwe nae kwa siku mbili alafu niende shule je, wewe mzazi unge mfanyaje mwanao?

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About