Amri za Kanisa ni zipi?
Amri za kanisa ni;
1. Hudhuria Misa Takatifu Dominika na sikukuu zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya Majivu; usile nyama siku ya Ijumaa Kuu
3.Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Pasaka
5. Saidia Kanisa Katoliki kwa zaka
6. Shika sheria Katoliki za ndoa.
Katika Amri ya kwanza ya Kanisa tumeamriwa nini?
Tumeamriwa tusikilize Misa kila siku ya Mungu na Sikukuu zilizoamriwa.
Sikukuu zilizoamriwa ni zipi?
Ndizo:
1. Kuzaliwa kwa Yesu – Noeli tarehe 25/12 Ufufuko wa Bwana Yesu
2. Pasaka –
3. Kupaa Yesu —- Siku 40 baada ya Pasaka.
4. Kupalizwa Mbinguni Bikira Maria 15/8
5. Sikukuu ya Watakatifu Wote 1/11
Katika Amri ya Kwanza ya kanisa tumekatazwa nini?
Tumekatazwa;
1. Kukosa Misa
2. Kufanya kazi nzito siku hizo
Kujinyima ni nini?
Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.
Nani ana lazima ya kufunga?
Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula. (Jumatano ya Majivu)
Siku za kufunga ni zipi? Na siku gani tumekatazwa kula nyama?
Siku za kufunga ni Jumatano ya majivu, siku za Kwaresima isipokuwa Dominika zake, na siku iliyokatazwa kula nyama ni siku ya Ijumaa kuu.
Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa nini?
Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa kuungama mara kwa mara walau mara moja kila mwaka
Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa nini?
Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa tupokee Ekaristi Takatifu walau mara moja kwa mwaka wakati wa pasaka.
Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa nini?
Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa kufahamu kuwa gharama za dini na za mapadre zatupasa. Yaanai wakristo walitegemeze Kanisa na wahudumu wake na hasa katika kazi ya kueneza injili.
Zaka ni nini?
Zaka ni asilimia kumi (10%) ya pato la mtu kwa mwaka ambalo anapaswa kulitoa kwa Kanisa.
Asiyelipa Zaka na michango mingine ya Kanisa ya lazima atenda dhambi gani?
Atenda dhambi kubwa: Yampasa kulipa na kuungama.
Amri ya Sita ya Kanisa Inadai nini?
Inadai kushika Sheria Takatifu Za ndoa
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Nakuombea 🙏
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Katika imani, yote yanawezekana
Neema ya Mungu inatosha kwako
Rehema hushinda hukumu
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Dumu katika Bwana.
Endelea kuwa na imani!
Tumaini ni nanga ya roho
Mwamini Bwana; anajua njia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Rehema zake hudumu milele
Mwamini katika mpango wake.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Nguvu hutoka kwa Bwana
Sifa kwa Bwana!
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Imani inaweza kusogeza milima
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Neema na amani iwe nawe.
Mungu akubariki!
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni mwema, wakati wote!
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Baraka kwako na familia yako.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia