Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Ujumbe mzuri wa kumtumia mpenzi wako kumtakia usiku mwema

“””””Yule””””” Anipendezae lazima nimkumbuke”” “”nimpe salamu “”moyo”” wangu “”uridhike”” “”Nimuombee kwa MWENYEZI “”MUNGU”” mabaya yamuepuke”” “”na kila lililo la kheri kwake lisiondoke”” “”nakutakia”” “ucku mwema”

Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa

Maujanja ya kumkalisha mwanamme wako nyumbani weekend haya hapa

Siku hizi wa naume licha ya kukimbia nyumba zao kwa kisingizio cha kazi maajabu weekend hasa Jumamosi utasikia wanaaga nafika hapo njiani naja naenda kununua gazeti.

Kumbe wanaenda kunywa supu unasubiri wee mpaka alasiri au jioni

Hivyo wanandoa wengi hili limekuwa tatizo mwanaume kiguu na njia asb mchana na njia kumuacha mama na watoto.

Nini kifanyike hasa weekenda Mwanaume ashinde NYUMBANI akikupumzikia??

Zipo njia nyingi mojawapo SUPU YA WEEKEND NA MAZUNGUMZO NA MKAO

Ni kweli wanawake wengi hamjuagi kuwakalisha waume home.

Anza hivi
Siku uko home wewe amka mapema kabla yake anza makeke jikoni…

Mara blenda priiiii… juice… ama milk shake…. hahahaha..Utaona anasogea jikoni..

Wakati anakunywa juice ama milk shake…Anza kukuna nazi…

Chambua mnafu…

Hapo jikoni kuna kanyama kanachemka… katia kitunguu tupia viazi 2 na ndizi.Hahaha..

ile harufu ikianza kutoka utasikia anafuata maji jikoni… hahahaha kwenye friji… wala hatumi..

Hahaahha… utasikia nini kiko jikoni?Hahahaa.

Mmiminie supu…

Na ndizi mbili na kiazi kimoja kapilipili mbuzi pembeni..

Muulize kuna chapati…Mpe.. hahahahaha..Akimaliza supu nakuapia atasinzia..

.Akishtuka ugali na mnafu na nyama umeiva…Mpe ale..Mshushie na glass ya mtindi…Hahahaha..

analewa full Hata kama kuna mama junior anaambiwa usipige…

Hahahahahaha….Baada ya hapo acha apumzike… aoge…

Kisha funga ka khanga kako kepesi jilaze pembeni.. woiiiiiiiii..

Mkimaliza muombe pesa ya sokoni…

NAKUAPIA HATA KAMA JANA YAKE ALIKUPA ATAKUPA TENA.

Hahahahaha.. jamani…

Hahahahaha… yani kwa raha ya supu… nakuapia utaambiwa hata mama alipiga simu jana… hahahaha.. ama utasikia mamii.. njoo uone njoo… unaitiwa kitu cha kwenye tv.. hahaha.

Hata hujaona mwanzo ila kwa raha yakasupu utaitwa…

Hata kama huna kalio nakuambia utapigwa kibao hata cha mgongo…. hahahahahahahahahaha.

Sasa wewe unaamka chai na mkate kama chuo cha uhazili…
Wali maharage kama jeshi la j

Visababishi, dalili, matibabu na kinga ya presha ya kushuka

Hypotension ndio jina linalotumika kuelezea presha ya kushuka ambayo mpaka sasa chanzo chake hakijawa wazi. Kipimo cha presha huwa na namba mbili. Namba moja huwa juu na nyengine huwa chini. Hivyo basi namba ya juu kikawaida kwa mtu mzima inapaswa kuwa 100 hadi 139 na ya chini inapaswa kuwa 60 hadi 90. Hivyo basi pressure yako ikiwa chini ya 100/60 Ndio inajulikana kama Hyptension yaani pressure iko chini.

Hypotension (haipo juu). Kwa watu wengi presha hii huwatia kizunguzungu na kuwaangusha. Presha hii ikiwa ya muda mrefu husababisha mtu kupata maradhi ya mshtuko.Watu wenye afya nzuri, hasa wakimbiaji, presha ya kushuka huwa ni dalili ya uzima kwao.

Si rahisi kuziona dalili kwa mtu mwenye presha ya kushuka hata kama imedumu kwa muda mrefu. Mara nyingi matatizo ya kiafya huonekana pale mtu presha yake inaposhuka ghafla. Wakati huo wa matatizo ya kiafya, damu kidogo hufika katika ubongo. Hali hii humfanya mtu awe na kizunguzungu au kuumwa na kichwa.

Kushuka ghafla kwa presha mara nyingi humtokezea mtu pale anapofanya jambo la haraka kama mtu aliyekaa na kutaka kusimama mara moja. Kitaalamu presha hii inajulikana kama postural hypotension, orthostatic hypotension, au neurally mediated orthostatic hypotension.

Postural hypotension inachukuliwa ni hali ile ya kushindwa kwa mfumo wa mawasilianao unaojiendesha wenyewe mwilini kufanya kazi yake kikamilifu (autonomic nervous system). Mfumo huu huendesha na kuongoza vitendo visivyo vya hiari (involuntary vital actions), kama vile mapigo ya moyo kubadilika kutokana na jambo lililotokea kwa wakati uleopo.

Kwa kawaida unapoinuka, kiwango fulani cha damu yako kinakuwa kimebaki sehemu ya chini (miguuni). Kukiwa hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa na mwili wako, hali hii itasababisha presha yako kushuka. Katika hali hii mwili wako unafanya nini ?

Mwili wako unapeleka taarifa kwenye moyo na kuamuru uongeze usukumaji wa damu ambao utaizidi mishipa yako na kuifanya kuwa membamba hali itakayopelekea kuifanya presha yako kubakia ileile. Ikiwa jambo hili halikufanyika au limaefanyika polepole sana, presha yako itashuka ghafla. Hapa ndipo mtu unapomuona anaguka ghafla.

Kwa ufupi athari ya maradhi ya presha ya kushuka na ya juu huongezeka kadri mtu anapokuwa na umri mkubwa na pia kubadilikabadilika kadri umri unavyoongezeka. Jambo jingine la kufahamu ni kuwa, ufikaji wa damu kikawaida kwenye ubungo unapungua kadri umri unavyoongezeka. Inakisiwa kiasi cha asilimia 10 mpaka 20 ya watu wenye umri unaozidi miaka 65, wanapata tatizo la presha yao kushuka.

Ni kiwango gani cha presha kinapofika ndio huwa maradhi ?

Hakuna kiwango maalum kinachojulikana ambacho ni sawasawa kwa watu wote kikifika ndio kinaitwa maradhi. Kiwango ambacho kwako ndio uzima, basi huenda kwa mwenzako ikawa ni maradhi. Katika presha ya kushuka, madaktari wengi huchukulia kuwa tayari mtu ana maradhi pale aambapo kiwango chake cha presha kinafuatana na dali za maradhi yenyewe.

Hata hivyo, baadhi ya wataalamu wanachukulia tayari mtu ana maradhi ya presha ya kushika pale vipimo vinapoonyesha kiwango hichi 90/60 mm Hg. Tufahamu kuwa kiwango cha namba inayosomwa chini katika kipimo cha presha (… /60 mm Hg ), hichi huonyesha tayari mtu huyu anapresha ya chini hata kama kile cha juu ( 90/…mm Hg) kina namba iliyozidi 100.

Mfano ikiwa umepimwa presha na ukapata kipimo hichi 115/60 mm Hg, presha yako itakuwa ipo chini. Na kama umepata kipimo hichi 115/50 mm Hg, sio kwamba presha yako itakuwa ipo chini tu, bali presha hii itakuwa si ya kawaida.

Dalili za maradhi

Kama nilivyokwisha tangulia kusema, presha inaweza kuwa sawa kati ya watu wawili lakini ikawa na matokeo tofauti. Presha hiyo inayoweza kuwa sawa na ikawa na matokeo tofauti si yenye kipimo hichi 120/80 mm Hg. Presha yenye kipimo hichi 120/80 mm Hg, ndiyo nzuri na watu wenye presha hii wanakuwa na afya nzuri. Kitu muhimu ni kujua, mabadiliko gani yanaleta tatizo katika presha hata inapelekea kuwa si ya kawaida.

Presha nyingi za watu wanapopimwa huwa zinakuwa kati ya 90/60 mm Hg (presha iliyo chini) mpaka 130/80 mm Hg (presha iliyo juu). Mabadiliko ya kushuka presha upande wa chini, hata kama kidogo kiasi cha 20 mm Hg, hupelekea matatizo kwa baadhi ya watu ( hasa watu wasiofanya mazoezi kila siku).

Mtu mwenye mazoezi ambaye presha yake nzuri (120/80 mm Hg) akapimwa presha na kupata kipimo hichi, 110/60 mm au 120/70 mm Hg, mtu huyu hatakuwa na tatizo lolote la presha
Kuna aina tatu za presha ya kushuka :

Orthostatic sambamba na postprandial orthostatic (Orthostatic hypotension, including postprandial orthostatic hypotension)

Orthostatic, hii ni aina ya kwanza ya presha inayosababishwa na kubadili mazingira uliyonayo kwa ghafla, maranyingi hutokea kwa mtu anayesimama kutoka alipolala. Presha hii haidumu muda mrefu, kiasi cha sekunde chache mpaka dakika moja. Ikiwa presha hii itatokeze. baada ya kula, basi itakuwa ni hatua ya pili (postprandial orthostatic) .

Hatua hii ya pili huwapata zaidi wazee na wenye presha ya juu.

Neurally mediated hypotension (NMH)

NMH kama ilivyo kifupisho cha presha aina ya pili, huwapata zaidi vijana na watoto. Presha hii hutokea pale mtu anaposimama kwa muda mrefu. Maranyingi huwapata sana watoto.

Aina hii ya pili ya presha ya kushuka maranyingi husababishwa na hali zifuatazo :

  1. Utumiaji wa pombe
  2. Utumiaji wa dawa za kutibu presha ya juu.
  3. Utumiaji wa dawa za kumtoa fahamu mtu wakati wa kufanyiwa upasuaji

Mambo mengine yanayosababisha presha kushuka ni pamoja na :

  1. Ugonjwa wa Kusukari
  2. Mtu kula kitu kinachomdhuru
  3. Mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida
  4. Maradhi ya kuharisha
  5. Kuzimia
  6. Maradhi ya moyo
  7. Maradhi ya kustuka

Severe hypotension hii ni aina ya tatu ya presha ya kushuka ambayo hutokana na kupoteza damu
Kwa muhtasari, dalili za presha ya kushuka ni pamoja na :

  1. Kuona kizunguzungu/kuumwa na kichwa kusiko kuwa kukubwa
  2. Kuzimia
  3. Kushindwa kuzingatia
  4. Kushindwa kuona vizuri ghafla
  5. Kuona baridi,
  6. Kujihisi kuchoka sana
  7. Kuvuta pumzi kwa tabu
  8. Kutapika
  9. Kuhisi kiu

Hali zinazosababisha kupata presha ya kushuka.

Kinachosababisha presha ya chini bado hakijatambulika hasa. Chanzo chake hakiko wazi. Hata hivyo mambo yafuatayo yanaweza kuhusiswa nayo :

  1. Kuwa na mimba
  2. Matatizo ya homoni mwilini, maradhi ya kisukari, au upungufu wa sukari mwilini
  3. Utumiaji mkubwa wa dawa
  4. Ulaji wa dawa za presha unaopindukia kiwango (Overdose) kwa mtu mwenye presha ya juu.
  5. Maradhi ya moyo
  6. Maradhi ya figo

Nani anapata presha ya kushuka ghafla ?

Presha ya kushuka ghafla inayompata mtu anapoinuka ghafla, inaweza kumpata mtu yeyote kwa sababu tofauti zikiwemo,

  1. kuharisha sana,
  2. kukosa chakula ( njaa kali) kwa muda mrefu,
  3. kusimama kwa mapigo ya moyo, au
  4. kuchoka kupita kiasi.
  5. Pia inawezekana ikawa ni urithi wa maradhi,
  6. Umri mkubwa,
  7. Matumizi ya dawa,
  8. Utapiamlo na mambo mengine kama kupatwa na madhara ya jambo fulani.

Nini kinaifanya presha inayoshuka iendelee ?

Pia Presha ya kushuka mara nyingi huwapata watu wanaotumia dawa kwa kutibu presha ya juu (hypertension). Pia huwapata wajawazito au wagonjwa wa kisukari. Mara nyingi wazee nao hupata maradhi haya hasa wale walio na presha ya juu wakiwa wanaendelea kutumia dawa zao za presha.

Baadhi ya maradhi ambayo yanasababisha presha kushuka kuendelea ni pamoja na;

  1. Ukosefu wa vitamin mwilini,
  2. Madhara kwenye uti wa mgongo, na
  3. Kansa hasa kansa ya mapafu.

Wakati gani wa kuchukua hatua za matibabu

Matibabu huanza na hatua zako wewe mwenyewe. Wakati utakapojiona presha yako inashuka, kaa chini au lala chali na unyanyue miguu yako juu. Wakati yanafanyika haya, ufanyike utaratibu wa kuonana na daktari haraka.

Pia ufanyike utaratibu wa kuonana na daktari yanapoonekana mambo yafuatayo yamemkuta mtu :

  1. Maumivu ya kifua
  2. Kizunguzungu
  3. Kuzimia
  4. Homa kali sana
  5. Mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida
  6. Kupumua kwa tabu

Pia afuatwe daktari haraka ikiwa baada ya hayo yaliyotokea, kuongezeka na haya yafuatayo :

  1. Mtu anapata matatizo makubwa ya mkojo
  2. Kushinwa kula au kunywa chochote
  3. Kuendelea kuharisha au kutapika kwa muda mrefu

Matibabu na Dawa

Presha ya kushuka ambayo haijulikani chanzo chake wala haileti dalili au inampa mtu kizunguzungu anaposimama, mara chache inaweza kutafutiwa matibabu. Ikiwa zipo dalili, matibabu yataendana na chanzo chenyewe na daktari atashughulikia hicho chanzo. ( kuharisha,maradhi ya moyo, kisukari). Ikiwa presha ya chini imesababishwa na matumizi ya dawa kwa matibabu, basi matibabu yake huwa kubadili dawa nyingine ua kuacha kutumia dawa kabisa.

Ikiwa hakuna uhakika wa sababu za presha ya kushuka au hayapatikani matibabu yaliyo sahihi, matibabu sahihi yatakuwa ni kuifanya presha yako ipande na kuondoa zile dalili zanazokupata inapokujia.

Kwa kutegemea umri wako, hali yako ya kiafya na aina ya presha uliyonayo, mambo haya yanaweza kukusaidia :

Kuongeza matumizi ya chumvi. Matumizi ya chumvi lazima yawe kwa kipimo, kwani chumvi nyingi hupandisha presha. Kabla hujaanza kuongeza matumizi ya chumvi, ni vizuri uwasiliane na daktari ili akupe kiwango cha matumizi.

Kunywa maji mengi. Kunywa maji mengi kunamsaidia kila mtu sio mtu mwenye presha ya chini tu. Tunapozungumzia maji tunalenga zaidi vinywaji na sio maji peke yake, lakini vinywaji vyenyewe viwe ni maji, maji ya matunda maziwa na hata kahawa au chai. Tahadhari ichukuliwe kwa vinywaji vya viwandani kwani huwaletea matatizo baadhi ya watu.

Kuvaa mavazi yenye kubana. Haya ni mavazi ya mpira ambayo yanavaliwa sehemu za miguuni. Mavazi haya yanasaidia kufanya damu yako isikae miguuni na iendelee kwenye mzonguko wake kikawaida.

Matumizi ya dawa. Zipo dawa mbalimbali ambazo zinatumika kufuatana na hali ya presha uliyonayo.

Matibabu hospitalini.

Presha ya kushuka inayomtokezea mtu mwenye afya nzuri ambayo haina dalili zozote na haimletei matatizo yeyote, hatahitajika kutumia dawa. Ikiwa zipo dalili, atahitaji matibabu kutokana na hizo dalili zilizoonekana. Ikiwa presha ulokuwa nayo inatokana na matumizi ya dawa, daktari atakubadilishia dawa nyengine au utaacha matumizi ya dawa. Wale wenye NMH pamoja na matumizi ya dawa, inabidi waache tabia ya kusimama muda mrefu. Kimtazamo presha ya chini inatibika hata kufikia mtu kuwa na presha ya kawaida.

Napenda nichukue nafasi hii kuwafahamisha kuwa, bila kubadili mfumo wa maisha ulionao, hata ukikusanyiwa dawa nzuri za dunia nzima kwa kutibu maradhi yako hutopata uzima wowote. Kubadili mfumo wa maisha si katika kuishughulikia presha tu, bali kwa maradhi yote ndio

Tiba sahihi. Nini dawa zinafanya?. Dawa zinalazimisha kuurudisha mfumo katika hali yake ya kawaida tu. Baada ya dawa kutoa msaada wake huu, kinachotakiwa kwako wewe kuendeleza mfumo huo unaofaa ambao dawa zimekurudishia tena.
Kwa kutegemea sababu za kupata presha uliyonayo, unaweza kuchukua hatua zifuatazo :

Kunywa maji mengi, kuacha kunywa pombe, Kula vyakula kiafya (kula nafaka, matunda, mbogamboga, kula mifupa ya samaki na hata ya ndege[kuku,njiwa nk]) Tupendelee kuku wa kienyeji zaidi. Ikiwa kuongeza chumvi katika chakula, basi usizidishe vijiko viwili vya chai kwa siku na ni vizuri sana upate ushauri kwa daktari.

Kujenga utamaduni wa kuinuka taratibu ulipo kaa ua kulala. kulalia mto, ikiwa unapenda kunalalia ubavu, pendelea kulalia upande wa kulia (kila unapozungumzia presha, basi jambo la kwanza la kukumbuka ni moyo, moyo wako uko upande wa kushoto, kitendo cha kulalia upande wa kushoto kinaweza kuupa tabu moyo katika utendaji wake wa kazi).

Kuwa na tabia ya kula chakula kidogo katika mlo wako. Kufanya hivyo kunasaidia presha yako kutoshuka baada ya kumaliza kula. Jipangie utaratibu wa kula mara kwa mara ili uweze kula chakula cha kutosha. Punguza kula vyakula vyenye uwanga kwa wingi kama vile, mbatata, wali na mikate. Kula chakula pamoja na chai au kahawa. Ni vizuri haya yote utakayoyafanya ukawasiliana na daktari kabla.

Kinga ya presha ya kushuka.

Ikiwa wewe ni mzima au tayari una presha ya kushuka, Daktari atakushauri hatua za kuzuia isitokee au isiendelee au kuipunguza. Hatua hizo ni pamoja na :
1. Kuacha unywaji wa pombe.
2. Kuepuka kusimama muda mrefu ( hasa ikiwa tayari una NMH)
3. Kunywa maji kwa wingi
4. Kuinuka taratibu kutoka ulipokaa ua kulala
5. Kuvaa mavazi ya kubana miguuni (ikiwa tayari unayo)

Vitu (6) sita usivyotakiwa kufanya kabla ya kulala

1. USILALE UKIWA UMEVAA SAA.

Saa ya mkononi ina madhara iwapo
utaivaa kwa muda mrefu,
wanasayansi
wanashauri sio sahihi kulala ukiwa
umevaa saa mkononi.

2. USILALE UMEVAA SIDIRIA

(wanawake
wanayovaa kwenye matiti ).
Wanasayansi wa America
wamegundua kuwa wanaovaa sidilia
zaidi ya masaa 12 Wako kwenye
hatari zaidi ya kupata Kansa ya
matiti.

3. USILALE NA SIMU IKIWA KARIBU.

wanasayansi wanashauri usiweke
simu pembeni kwa sababu mionzi
ya simu sio salama hasa ukiwa
umelala, ni vizuri ukaizima kama ni
lazima ukae nayo karibu.

4. USILALE UKIWA UMEWEKA MAKE

– UP
(usoni). Hii usababisha ngozi
kutopumua vizuri na kutopata
usingizi kwa haraka.
5. USILALE UMEVAA NGUO YA
NDANI – Ili kuwa huru na kulala ni
vyema ukalala bila kubanwa
na kitu chochote, nguo ya ndani
haitakiwi.
KITU CHA MWISHO NA CHA MUHIMU
KULIKO VYOTE NI ….

6. USILALE NA MKE/MUME WA MTU.

wanasayansi wanasema jambo kama
hili linapotokea na ukabainika
linaweza chukua uhai wa mtu hata
kukuacha na maumivu baada ya
kuharibiwa uso kwa makondo yasiyo
na mpangilio, ni vizuri ukawa makini
sana hapa!
Ukibisha yakikukuta shauri yako!

Virutubishi, kazi zake katika mwili na vyanzo vyake

Virutubishi

ni viini vilivyoko kwenye chakula ambavyo vinauwezesha mwili kufanya kazi zake, karibu vyakula vyote huwa na kirutubishi zaidi ya kimoja ila hutofautiana kwa kasi na ubora. Kila kirutubishi kina kazi yake mwilini na mara nyingi hutegemeana ili viweze kufanya kazi yake kwa ufanisi. Hakuna chakula kimoja chenye virutubishi vya aina zote isipokuwa maziwa ya mama kwa miezi sita ya mwanzo ya maisha ya mtoto, ni mhimu kula vyakula vya aina mbalimbali ili kuwezesha mwili kupata virutubishi mchanganyiko vinavyohitajika.

Aina za virutubishi vinavyohitajika mwilini

  1. Kabohaidreti / vyakula vya wanga
  2. Mafuta ya Wanyama na Mimea
  3. Protini
  4. Vitamini na Madini
  5. Maji

Kabohaidreti / vyakula vya wanga

Kabohaidreti / vyakula vya wanga huvipa mwili nguvu inayoihitajika kujiendesha. Vyakula
hivi vyaweza kuwa sahili au changamani. Hii inahusu jinsi ambavyo chakula chaweza
kubadilisha sukari katika mwili. Vyakula vya wanga na sukari huvipa mwili nguvu
inayohitajika kuufanya upumue na kuendelea kuishi, kuwa na mwendo na utoaji joto, na kwa
ukuaji na utengenezaji wa mkusanyiko wa seli (tishu). Baadhi ya wanga na sukari
hubadilishwa kuwa mafuta mwilini.
Ufumwele utokanao na kabohaidreti hufanya kinyesi kiwe laini na kingi na huondoa kemikali
za sumu, na hivyo hufanya matumbo yawe na afya njema. Hupunguza uyeyushaji na
ufyonzaji wa virutubishi katika vyakula, na husaidia kupunguza unene.

Vyanzo vya kabohaidreti

Vyanzo vikuu vya kabohaidreti ni:

• Nafaka

– Mahindi/ugali
– Serena
– Mtama
– Mchele
– Unga wa ngano

• Mizizi ya vyakula vya wanga

– Viazi vitamu
– jimbi
– Viazi mviringo
– Muhogo mbichi
– Unga wa muhogo
– Ndizi

Mahitaji ya kabohaidreti mwilini

– Mahitaji hutofautiana kutegemea na umri, jinsi, jinsia, shughuli, hali ya kiafya
– Kula mara tatu au zaidi kwa siku.

Mafuta ya Wanyama na Mimea

Mafuta ya wanyama na mimea kwenye chakula na tishu ya shahamu kwenye miili yetu huwa
na shughuli nyingi

Kazi za mafuta ya wanyama kwenye mwili

• Virutubishi: mafuta ya wanyama hutoa tindikali za mafuta muhimu, ambazo
huhitajika katika ukuaji wa kawaida kwa watoto wachanga na watoto wengine na
kwa uzalishaj wa michanganyiko ya aina ya kihomoni inayorekebisha upeo mpana
wa shughuli za kimwili na kukufanya uwe mwenye afya njema.
• Usafirishaji: mafuta ya wanyama hubeba mafuta ya miyeyusho ya vitamini (A, D,
E, na K) na kurahisisha ufyonzaji wake.
• Ufahamu: mafuta ya wanyama huchangia kwenye harufu nzuri na ladha ya
chakula.
• Umbile la asili: mafuta ya wanyama hufanya chakula (hususan nyama na vyakula
vya kukaushwa) kuwa nyororo.
• Ukinaishaji: mafuta ya wanyama hukipa chakula ukinaishaji, hivyo hujikuta
umeshiba na kutosheka kwa muda mrefu baada ya chakula.
• Mafuta ya wanyama ni chanzo cha utoaji wa mkusanyiko wa kalori. Hili ni jambo
jema unapokuwa kwenye safari ndefu, itumiayo nguvu nyingi, ukiwa umebeba
chakula chako.

Mafuta ya wanyama mwilini hufanya yafuatayo:

• Mafuta ni muundo mkuu wa mwili wa kuhifadhi nishati (ambazo ni muhimu wakati wa
ugonjwa au kupungua kwa ulaji chakula)
• Mafuta hutoa sehemu kubwa ya nishati inayotumika kwenye kufanyiza kazi misuli.
• Mafuta hukinga viungo vya ndani na kuhami miili yetu dhidi ya hali za joto
zinazopitiliza mipaka.
• Mafuta huunda malighafi kuu ya utando wa seli (hususan seli za ubongo na za
mishipa ya fahamu)
• Mafuta hugeuzwa kuwa aina nyingi za homoni (ikiwemo homoni za mambo yahusuyo
mapenzi)
Mafuta ki kitu kizuri! Isipokuwa tu pale uzuri unapozidi kiwango ndipo kunapokua na tatizo.

Aina za mafuta:

mafuta yaliyokolea dhidi ya yale yasiyokolea
Kama ambavyo kuna aina kuu mbili za kabohaidreti, kuna aina kuu mbili za mafuta
kutegemea na mfumo wake wa kikemia; mafuta yaliyokolea na yale ambayo hayajakolea.
Aina hizi za mafuta zina athali tofauti kabisa kwa afya yako.

1. Mafuta yaliyokolea

• Huwa na kawaida ya kuongeza lehemu “mbaya” kwenye damu na kuongeza
uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo.
• Mafuta yaliyokolea huwa na kawaida ya kuganda kwenye hali ya joto la kawaida.
• Hupatikana kwa wingi kutokana na vyanzo vya mafuta ya wanyama.
Vyanzo vya mafuta yaliyokolea
• Siagi, malai, mafuta ya nyama ya ngómbe, ngozi ya kuku, mafuta ya maziwa yenye
malai, jibini, aisikirimu, siagi, samli, mafuta ya nguruwe/ya kupikia, mafuta
yatokanayo na nyama, mawese mekundu, na nazi.
• Yaliyopo nje ya utaratibu: mafuta ya nchi za joto (ikiwemo ya nazi na mawese) yana
kiwango kikubwa cha mafuta yaliyokolea.

2. Mafuta yasiyokolea

• Mafuta yasiyokolea ni aina ya mafuta ambayo kwa ujumla yanahusishwa na afya bora.
• Yana kwaida ya kushusha viwango vya lehemu na kupunguza hatari za magojwa ya
moyo.
• Mafuta yasiyokolea huwa na kawaida ya kuwa ya mmiminiko katika joto la kawaida.
• Hupatikana kwa wingi kutokana na mimea.
Vyanzo vya mafuta yasiyokolea
• Mafuta yatokanayo na mboga za majani, mizeituni, miparachichi, njugu, mafuta ya
karanga, maharagwe meupe, mbegu za alizeti, mbegu za ufuta na aina nyingine za
mbegu, mafuta ya samaki na soya.
• siagi, samli, mafuta ya nguruwe/ya kupikia, maziwa yenye malai, jibini, mafuta
yatokanayo na nyama, mawese mekundu, na nazi.

Kuna mafuta yatokanayo na kuchujwa kwa mafuta ya mbogamboga na kugandishwa. Mafuta
haya huishia kuwa na tabia za mafuta yaliyokolea. Mafuta haya pia hayapashwi kutumiwa
kwa wingi.

Vyanzo ni:

• majarini, mafuta ya nguruwe, vyakula vya kukaangwa, donati, keki, biskuti, aiskrimu.

Mahitaji ya mafuta mwilini

Mahitaji ya mafuta huelezewa kama ‘ni asilimia ya mahitaji yote ya nishati’. Kiwango chote
cha asilimia ya nishati kinachopashwa kitokane na mafuta katika mlo bora uliokamilika ni
kama ifuatvyo:
• Asilimia 30-40 kwa watoto hadi kufikia miaka miwili kwenye milo ya nyongeza
• Asilimia 15-30 kwa watoto wakubwa na wengi wa watu wazima; kwa watu wazimu
wenye afya – hadi asilimia 35 inakubalika.
• Angalau asilimia 20 hadi 30 kwa akina mama wenye umri wa kuweza kuzaa (15-45).

Protini

Protini ni zana za ujenzi wa misuli yetu, viungo na baadhi ya vitu vingi vinavyotengeneza
miili yetu. Hutoa tindikali muhimu za amino zitumiwazo na mwili kutengeneza misuli ya tishu.
Mwili unahitaji protini na kalori kila siku.
Unapokosa kupata kalori na protini za kutosha kila siku, mwili wako hutumia akiba yake
kufidia pengo la ukosefu wa nishati. Hali hii huinyima mwili wako kalori unazohitaji kuufanya
uwe na afya bora na hivyo kusababisha kupungua kwa uzito.

Vyanzo vya protini

Protini yaweza kupatikana kwenye vyakula vya wanyama na mimea.

1. Vyanzo vitokanavyo na wanyama

• Nyama, kuku/mabata n.k., samaki, mayai, jibini, maziwa na mtindi.
• Vyakula hivi vinachukuliwa kuwa kama ‘kamili’ au ‘vyenye kiwango cha juu’cha
protini kwa kuwa vina aina zote za ‘tindikali muhimu za amino’. ‘Muhimu”inamaanisha
lazima vitumiwe kwenye milo yetu; miili yetu haiwezi kuzitengeneza.

2. Vanyzo vitokanavyo na mimea

• Bidhaa zitokanazo na soya, (tofu, tempeh), maziwa ya soya na mazao mengine
yatengenezwayo na soya), maharagwe, mbegu na njugu.
• Viwango vidogo vya protini vinapatikana vilevile kwenye mikate, mahindi /ngano, na
aina nyinge ya nafaka, na mbogamboga pia.
• Vyanzo hivi vya protini vinachukuliwa kama ‘si kamili’kwa kuwa vinakosa moja au
zaidi ya tindikali muhimu za amino.
• Protini ya maharagwe meupe ndiyo ya kipekee. Haya yanachukuliwa kuwa ni kamili.

Mahitaji ya protini mwilini

Mahitaji hutofautiana kulingana na umri, jinsi, jinsia, na shughuli.

Vitamini na Madini

• Vitamini husaidia mwili kugeuza chakula kuwa nishati na tishu.
• Kuna aina 13 za vitamini kwa ujumla: Vitamini A; vitamini B; vitamini B mchanganyiko
unayojumuisha vitamini B1, Vitamini B2, Viamnini B3 vitamin, B6, Vitamini C, Vitamin
B12 tindikali ya pantotheniki (pantothenic acid), na biotini (biotin); na vitamini C, D, E,
na K.
• Madini yanahitajika katika ukuaji na utunzaji wa miundo ya mwili. Yanahitajika pia
katika kutunza juisi za uyeyushaji chakula na mimiminiko iliyopo ndani na
kandokando mwa seli.
• Madini hayatokani na mimea wala wanyama. Mimea hupata madini kutokana na maji
au udongo, na wanyama hupata madini kwa kula mimea au wanyama wanaokula
mimea.
• Vitamini na madini hujulikana pia kama vyakula vya ujenzi na ulinzi wa mwili.
• Vijirutubishi ambavyo havipatikani kwa wingi na ambavyo husababisha matatizo
mengi yatokanayo na utapiamlo wa ukosefu wa vijirutubish duniani ni kama
vifuatavyo; madini ya joto, zinki, vitamini A, chuma na folate.

Vyanzo vya Vitamini na Madini

• Mboga jamii ya machungwa, kama vile viazi vitamu vya njano na karoti, matunda jamii
ya machungwa kama vile, embe, papai, na mawese mekundu ni vyanzo vizuri sana
vya vitamini A.
• Matunda mengi yatokanayo na jamii ya michungwa na mboga zisizoivishwa sana
huwa na vitamini C.
• Mboga za kijani kibichi hutupatia folate na kiasi cha vitamini A.
• Mbogamboga nyingi (mf. nyanya, vitunguu) hutoa vijirutubishi muhimu vya nyongeza
viwezavyo kukinga mwili dhidi ya magonjwa sugu kama ya mioyo.
• Njia bora ya kuhakikisha tunapata vijirutubishi na ufumwele wa kutosha ni kula aina
mbalimbali za mbogamboga, matunda na nafaka zisizokobolewa kila siku.
• Nyama, viungo vya ndani vya wanyama na maini ya aina zote ni chanzo kizuri sana
cha vitamini A.

Mahitaji ya vitamin na madini mwilini

• Vitamini na madini vinahitajika kwa viwango vidogo vidogo.
• Mahitaji hutegemea umri, jinsi na kiwango cha shughuli, na ulaji wa aina mbalimbali
za matunda, mbogamboga na nafaka zisizokobolewa.

Maji

Maji ni kirutubishi muhimu sana. Hakika, zaidi ya nusu ya mwili ni maji. Unaweza kuishi bila
ya chakula kwa wiki kadhaa, bali hauwezi kuishi zaidi ya wiki moja bila ya maji.
Mwili unahitaji maji ili kufanya kazi.

Umuhimu wa maji mwilini

• Kuhifadhi joto la mwili;
• Kusafirisha virutubishi mwilini;
• Kuvifanya viungo viwe na unyevunyevu;
• Kuyeyusha chakula;
• Kuondoa uchafu mwilini;
• Kupoza mwili.
(Fikiria matumizi ya maji unapojenga nyumba; bila ya maji: saruji, mchanga na zege
havitakuwa na matumizi yeyote).

Vyanzo vya maji mwilini

• Maji yenyewe
• Juisi za matunda
• Supu
• Maziwa
• Uji
• Vinywaji visivyo na kafeini (vinywaji vyenye kafeini na kileo vina madawa ya
kuongeza mkojo (diuretics) inayosababisha upotevu wa maji mwilini)

Mahitaji ya maji mwilini

Lita 1.5 au glasi 8 kwa siku.

Huyu mwanamke ni noma cheki alichomwambia mme wake baada ya kumnunulia nguo za ndani

Mume kaingia duka la nguo na kamnunulia mke wake chupi dazeni moja zote za rangi nyeusi, akaenda kumzawadia. Mpenzi akashukuru lakini alipogundua kuwa zote ni nyeusi si akaropoka.
MY HONEY: Sasa umeninunulia chupi zote nyeusi, sasa watu si watadhani nina chupi moja tu sibadili,

Jamaa alifura akawa kama mbogo na hapo ndipo zogo kuu lilipoanza

MUME:Watu gani hao watakaokuambia unachupi moje, inamaana unawaonyesha kitumbua changu? Leo utanambia’
Ungekuwa wewe ungefanya nini?

Hii kazi kweli kweli, Ungekua wewe ungefanyaje?

UNATOKA SEBULENI UNAENDA ZAKO CHOONI UNAINGIA TU HIVI GHAFLA UNAKUTANA NA MZIGO MKUBWA WA MAVI JUU YA CHOO ALAFU UNAAMUA KURUDI ZAKO ILE UNATOKA TU UNAMUONA DEMU MZURI ULIYEMTONGOZA JANA ANAKUJA KUINGIA CHOO ULICHOTOKA WW NA KINA MZIGO WA MAVI JUU NA AMEKUONA WW NDIO UMETOKA MLE NDANI ..unaamua kurudi ili uka flash bahat mby maji hakuna.!!!

😁😁😁HAPO NDIO UTAJUA KWANINI SIKU HIZI HATUPENDI UJINGA😆😆😆😆

Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)

Kuishi ukiwa na afya na kuishi maisha marefu kunawezekana kwa kubadili hali ya maisha unayoishi inayoharibu afya yako mfano uvutaji wa sigara, unywaji wa pombe kupita kiasi,kutokufanya mazoezi na kutokula matunda na mbogamboga.

Mambo yanayoweza kukusaidia kuishi maisha marefu ni kama yafuatayo

  1. Kuuandaa mwili kwa maisha marefu kwa kufanya mazoezi
  2. Kuwa makini kutambua na kutibu matatizo ya kiafya
  3. Kuepuka mazingira na kufanya kazi kwa namna au kazi zinazoweza kudhuru maisha yako. Mfano kuendesha gari bila kufuata utaratibu, kutokuvaa vifaa vya kujikinga wakati wa kazi
  4. Epuka vitu vyenye sumu vinavyoweza kudhuru afya yako na kukuletea matatizo ya kiafya kama dawa za mimea na mifugo, zitumie kama inavyotakiwa
  5. Usinywe pombe, usivute sigara wala kutumia dawa za kulevya
  6. Kula mlo kamili
  7. Usile vyakula vyenye chumvi na mafuta mengi
  8. Kunywa maji mengi ili kusafisha mwili
  9. Epuka msongo wa mawazo

Jinsi ya kupika Mboga Za Majani Makavu (Aina Yoyote)

Viamba upishi

Mboga za majani makavu ¼ kg
Mafuta vijiko vikubwa 3-4
Karanga zilizosagwa kikombe ½
Maziwa au tui la nazi kikombe 1
Kitunguu 1
Nyanya 2
Chumvi (kama kuna ulazima)
Maji baridi

Hatua

• Loweka mboga za majani makavu na maji kwa dakika 10-15.
• Osha , mboga na katakata nyanya na vitunguu.
• Kangaa, pukusua na saga karanga zilainike.
• Kanga kitunguu, weka nyanya, koroga zilainike.
• Ongeza mboga zilizolowekwa na maji yake kwenye rojo, koroga na funikia mpaka maji yakaukie na ive. Punguza moto.
• Koroga karanga zilizosagwa na maji, ongeza kwenye mboga ukikoroga kwa dakika 5.
• Onja chumvi, pakua kama kitoweo.
Uwezekano
Weka nyanya kidogo.
Tumia tui la nazi au krimu badala ya maziwa.
Weka nyama au dagaa au Mayai badala ya Karanga.

Matumizi ya Mrehani (basil) kutibu presha ya kushuka

Hii ni dawa nzuri ya kutibu shinikizo la chini la damu sababu ya kuwa na kiasi kingi cha vitamini C, magnesiamu na potasiamu, vilevile dawa hii husaidia kuweka sawa akili na kuondoa msongo wa mawazo (stress).

Matumizi

  1. Chukua majani 10 mpaka 15 ya mrehani mbichi
  2. Saga au twanga kupata maji maji yake (juisi).
  3. Weka asali kijiko kidogo kimoja ndani yake.
  4. Kunywa mchanganyiko huu kila siku asubuhi ukiamka tu tumbo likiwa tupu.

Vile vile unaweza kutafuna tu moja kwa moja majani kadhaa ya mrehani kila siku asubuhi.

Je, Chuoni kwako Kukoje?

FACT!
1.Ukiona geto lina feni, sabufa, meza ya plastic na kitanda ch sita kwa sita na Pc UJUE ni jamaa wa UDSM.

2. Ukaona geto lina nguo nyingi za watu tofauti tofauti, unga mwingi, vtunguu vng, nyanya halaf pembeni, Vitabu vya kutosha na lundo la karatasi za betting ujue huyu JAMAA ni wa SAUT.

3. Ukaona geto halina kitu ndani zaidi ya mkate wa bakheresa na kopo la maji UJUE huyu jamaa ni wa UDOM😂☝

4. Ukaona geto lina visamaki vikavu mezani, Notes za kutosha mezani na jaba pembeni UJUE huyu ni MJAMAA WA MWENGE/MWECAU😜👤

5. Ukaona geto lina Mawigi mengi na dressing table pembeni, ngazi ya kuwekea viatu UJUE huyu mjamaa ni wa RUCO IRINGA😘

6. Ukaona geto lina spray za kila aina, Nguo nyingi hasa za mitumba ambazo zimemodolewa mpaka tight UJUE huyu MJAMAA ni wa USHIRIKA MOSHI.

7.Ukiona geto lina Nyanya na mikungu ya ndizi halafu halafu nje kuna jiko la Mkaa UJUE huyu mjamaa ni wa TEKU mbeya😳

8. Ukiona geto lina tranka na nje wamevulia buti, viatu vya matope UJUE huyu Mjamaa ni Wa SMUCO MWIKA.

9. Ukaona geto ndan mashuka ya kimasai kinabao, hapa usipatwe na Mashaka, Jua huyu ni Mjamaa wa MAKUMIRA. 😜😜😜😜

10. Ukaona geto lina vimodo, vimini, miwani za tittled, jiko la mafuta ya taa, kitandani mito zaidi ya Minne,Visarafu kwenye meza, Tshirt nyingi za semina za family planning, Ukimwi n.k halafu chini tv ya chogo na king’amuz cha continental Ujue huyu MJAMAA ni wa TIA DSM 😱😱😱😱😱😱😱

⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⤵⏬🆙🆙🆙🆙
JE, KWAKO KUKOJE? ???
😋😋😋😋😋😋😋😋😋😋😋

Ijue Ishara ya Msalaba

Ishara ya Msalaba ni tendo la mtu kugusa paji la uso, kifua na mabega kwa kutumia mkono wa kulia na kutamka ‘Kwa Jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina’.
Kugusa paji la uso tuna maana kukubali kwa akili, kugusa kifua maana yake ni kupokea na kuupenda msalaba moyoni na kugusa Mabega maana yake ni kuwa tayari kuubeba Msalaba kwa nguvu zetu zote.
Tunafanya njia ya Msalaba kwa nia ya kumkiri Mungu Mmoja katika Nafsi tatu. Pia Msalaba ni Ishara ya Ukombozi wetu.
Ishara ya Msalaba Juu ya Paji la uso, mdomo na kifua kabla ya injili:
Hii ina maana kwamba Niko tayari kulifahamu Neno la Mungu Kwa Akili yangu,
Nitalitangaza kishujaa kwa midomo yangu, na Nitalipenda na kulishika kwa Moyo wangu Wote.

Faida ya kunywa maji yenye limao au ndimu kila siku

Watalam mbalimbali wa afya wanasema ya kwamba kwa kila siku ni vyema unywe maji ya ndimu ili uweze kujitibu magonjwa yafuatayo;

Unachotakiwa kufanya ni;
Weka maji yenye joto kidogo (vuguvugu) katika glasi au kikombe , kata limao au ndimu vipande viwili na kamua kipande kimoja tu ndani ya glasi yenye maji.

Kunywa na uanze siku mpya. Ni vizuri ukafanya hivi dakika 30 kabla ya kula chochote kingine kwa faida zaidi.

Anza leo kwa kunywa maji yenye ndimu kila siku asubuhi na uone mabadiliko ndani ya mwili wako. Mshirikishe mwenzio ili naye afaidike.

1. Huchochea Mmeng’enyo wa Chakula Tumboni

Maji yenye ndimu husaidia chakula kusagika vizuri na haraka katika mfumo wa chakula. Japo limao lina asidi(acid) lakini likiwa tumboni huwa alkali (alkaline) na kufanya mazingira mazuri kwa usagaji wa chakula.

Pia maji ya uvuguvugu husaidia kusawazisha utumbo uliojikunja na kutoa mawimbi tumboni na kufanya chakula kusukumwa vizuri.

2. Huboresha Kinga za Mwili

Vitamini C na potasiumu iliyomo kwa wingi katika limao inasaidia katika utengenezaji wa seli za kinga katika mwili.

3. Husaidia Kinga Dhidi ya Saratani

Vitamini C ni antioksidant (antioxidant) ambayo inasaidia kuondoa free radicalsmwilini ambazo zimetambulika kusababisha saratani (cancer).

Usafishaji wa Mwili na DamuLimao husaidia kusafisha damu kwa kuondoa uchafu. Limao pia husafisha figo ,ini na mfumo wa chakula.

4. Kurekebisha Sukari katika Mwili

Limao husaidia kuweka kiasi cha sukari tumboni na katika mwili kuwa katika kiasi stahili.
Hii inawasaidia sana wagonjwa wa kisukari katika ulaji wao.

5. Dawa ya Kikohozi na Mafua

Limao ikitiwa katika maji ya uvuguvugu na asali husaidia sana katika kutibu mafua na kikohozi kwa njia ya asili.

6. Inasaidia Urekebishaji wa Ngozi na Kupona Makovu

Limao inasaidia kufanya ngozi isizeeke. Kama unataka kubaki kijana basi limao litakusaidia. Tabia za vitamin C za kusafisha uchafu zinasababisha kufanya ngozi kuwa na afya na kutozeeka haraka.

7. Husaidia Kupungua Uzito

Limao hupunguza hamu ya kula. Na inajulikana kuwa sababu kubwa ya watu kuwa na uzito mkubwa ni kula chakula kingi au kula mara kwa mara. Limao litakufanya ujisikie kushiba muda mrefu hivyo kusaidia wale amabao wanataka kupungua uzito.

8. Kuondoa Harufu ya Mdomo

Limao husaidia kuua bakteria wabaya mdomoni ambao husababisha harufu mbaya.


Madhara ya kunywa pombe wakati wa ujauzito

Kuacha Matumizi ya pombe wakati wa ujauzito ni moja ya njia ya kuzuia kupata matatizo ya kuzaliwa nayo na udhaifu kwa mtoto. Pia kuna matatizo kadhaa yanaweza kutokea kwa kichaga kutokana na matumizi ya pombe wakati wa ujauzito.

Madhara haya ya pombe huweza kuwa ya kujitambua tabia na madhara madhara ya mkusanyiko wa dalili na viashiria kwa mtoto vinavyoitwa fetal alcohol syndrome-FAS. Kutokana na shirika madhara ya pombe yanayoambatana na dalili na viashiria fulani yanaongezeka sana. Pombe imekuwa ikituiwa vibaya sana wakati wa ujauzito ukilinganisha na madawa mengine.

Dalili za mtoto ambaye mama alikuwa akitumia pombe kwa kiasi kikubwa;

  1. Kutokuwa vema kabla na baada ya kuzaliwa
  2. Mtindio wa ubongo
  3. Udhaifu wa kuzaliwa wa kichwa na uso
  4. Magonjwa ya moyo
  5. Tabia zisizoeleweka
  6. Matatizo ya mfumo wa fahamu

Kiasi gani cha pombe ni salama kwenye ujauzito?

Hakuna kiwango salama cha matumizi ya pombe kwenye ujauzito kilichotambuliwa. Kwa usalama ni kutofikiri kutumia pombe wakati wa ujauzito.

Je kuna uhusiano wa kiwango cha pombe na matokea mabaya ya ujauzito?

Hakuna. Miongozi mwa wanawake waliokunywa ounce 5 ya pombe kwa kila siku, 1/3 ya watoto walikuwa na FAS, 1/3 walionesha madhara sumu kabla ya kujifungua, na 1/3 waliobaki walikuwa kawaida. Kundi jingine lililotumia ounce 1-2 kila siku asilimia 10 ya watoto walikuwa na dalili za FAS. Hata kiwango kidogo cha pombe kimekuwa kikisababisha FAS!. Matumizi ya pombe kwa kiasi kidogo bado yamekuwa yakihusika kusababisha mtoto kuwa na IQ kidogo na matatizo ya kujifunza kwa watoto wenye anatomia ya kawaida.

Je pombe husafilishwa kwenye kondo la mtoto?

Kemikali ya ethyl iliyo kwenye Pombe hupita kwenye kondo na kuingia kwa kwenye mzunguko wa damu wa mtoto. Kiwango cha pombe kwenye damu ya mama huwa sawa na kile kwenye damu ya kichanga tumboni.

Je mama aliyekuwa teja wa pombe anatakiwa aache kunywa pombe?

Mama aliyekuwa teja wa pombe anatakiwa apewe msaada wa wataalamu ili kusaidiwa kuacha pombe, madhara a kujifungua kabla ya mda huongezeka kwa watumiaji wa pombe

Dalili za kuacha pombe ghafla zinaonekana wakati gani wa ujauzito?

Dalili za kukatisha kutumia pombe huanza kuonekana upesi pale mtu anapoacha kutumia pombe, Mara nyingi ndani ya masaa 4 hadi 12. Hata hivyo inawezekana dalili za kukatika kutumia pombe kuonekana siku chache baadae. Mtu asipopata tiba hufikia kilele cha dalili ndani ya masaa 48 na huweza kuendelea kufikia miezi 3 hadi 6 na huwa na dalili kiasi kuliko awali. Dalili na viashiria ni kutetemeka, wasiwasi, mapigo ya moyo kwenda kasi, shinikizo la damu la juu, kutokwa jasho, kichefuchefu, kukosa usingizi na hutegemea utegemezi wa pombe na hali ya mgonjwa.

Mara ujauzito unapotambuliwa kuacha kutumia ama kupunguza husaidia kuondoa madhara kwa mtoto?

Kemikali ya ethyl na ethanol iliyo kwenye pombe hupitaka kwenye kondo la nyuma na kuingia kwenye damu na ubongo wa mtoto. Inafikilika kwamba madhara hutokana na sumu iliyo kwenye pombe na mazao ya uchakataji wa pombe mwilini. Kuacha au kupunguza kutumia pombe mara ujauzito unapotambuliwa huweza kupunguza matatizo ya kuzaliwa kwa mtoto hata hivyo kuna uwezekano kwamba inaweza hili lisitokee. Hivyo tafiti zaidi zinatakiwa kufanyika ili kuonyesha usahihi wa jambo hili.

SMS nzuri sana ya kutakia usiku mwema

Dah! Safari yetu ilikuwa ngumu kweli ila hatimaye tumefika japo ni usiku sana hebu tupige hodi tusije kabwa na vibaka hapa nje. Hodiiiiii, Hodiiiii, Tunaomba tufungulie Mlango,, sisi tunaitwa FURAHA, AMANI na UPENDO. Tumebeba HEKIMA, BUSARA na MAFANIKIO. Tulikuwa wengi HURUMA na UPOLE wanakuja nyuma. CHUKI na WIVU hawana nauli. TABU ni mahututi. SHIDA yuko jela. MATATIZO amepigwa shoti ya umeme. MIKOSI amefariki njiani. LAANA ameliwa na mamba. UVIVU ameungua na maji ya moto hajiwezi. Tutakuwa nawe daima maana tumefika kwa NEEMA . Mungu akulinde na mabaya yote katika dunia hii. ucku mwema.

Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About