- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utusikie
- Kristo utusikilize
- Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
- Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
- Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
- Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie
- Maria Mtakatifu ………. utuombee
- Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
- Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee
- Mama wa Kristo ……… utuombee
- Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
- Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
- Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
- Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
- Mama usiye na doa ……….. utuombee
- Mama mpendelevu ………. utuombee
- Mama mstajabivu ………. utuombee
- Mama wa Muumba ………. utuombee
- Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
- Mama wa Kanisa……….. utuombee
- Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
- Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
- Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
- Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
- Bikra mweye huruma ………….. utuombee
- Bikra mwaminifu………….. utuombee
- Kioo cha haki ………….. utuombee
- Kikao cha hekima ………….. utuombee
- Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
- Chombo cha neema ………….. utuombee
- Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
- Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
- Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
- Mnara wa Daudi ………….. utuombee
- Mnara wa pembe ………….. utuombee
- Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
- Sanduku la Agano ………….. utuombee
- Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
- Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
- Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
- Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
- Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
- Msaada wa waKristo ………….. utuombee
- Malkia wa Malaika ………….. utuombee
- Malkia wa Mababu ………….. utuombee
- Malkia wa Manabii ………….. utuombee
- Malkia wa Mitume ………….. utuombee
- Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
- Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
- Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
- Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
- Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
- Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
- Malkia wa amani ………….. utuombee
- Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusamehe ee Bwana.
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusikilize ee Bwana
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utuhurumie.
- Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
Neema na amani iwe nawe.
Sifa kwa Bwana!