Upendo wa Mungu hauna mwisho
Upendo wa Mungu hauna mwisho. Mtu anaweza akaacha kukupenda na kukusahau kabisa lakini kamwe Mungu haachi kumpenda Mtu wala hamsahau Mtu.
Upendo wa Mungu hauna mwisho. Mtu anaweza akaacha kukupenda na kukusahau kabisa lakini kamwe Mungu haachi kumpenda Mtu wala hamsahau Mtu.
Uzuri wa Mungu ni kwamba anasamehe na kisha anasahau. Unapotubu dhambi zako na kutaka huruma zake yeye anakufutia uovu wote na kukufanya mpya.
Jifunze na jijengea tabia ya kumsikiliza Mungu rohoni mwako unaposali. Sala ni mazungumzo ya Mungu na mwanadamu. Mazungumzo yanahusisha kuongea na kusikiliza.
Mungu anasubiri sala zako kila siku. Anasubiri sala zako akujibu ili uone utukufu wake. Anasubiri sala zako ili akuze mahusiano yake na wewe. Sali daima kwani Mungu yupo milele kukusikiliza na kukuhudumia.
Basi, nasema hivi: Mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia. Maana tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na Tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamuwezi kufanya yale mnayotaka nyinyi wenyewe.
(Wagalatia 5:16-22)
Basi, nasema hivi: Mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia. Maana tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamuwezi kufanya yale mnayotaka nyinyi wenyewe.
“Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtatimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa maana mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.” (Wagalatia 5:16-17)
Kuongozwa na Roho Mtakatifu maana yake ni kuacha maisha yetu yaongozwe na maadili na kanuni za kiroho zinazotoka kwa Mungu. Roho Mtakatifu hutupa nguvu, hekima, na mwongozo wa kila siku katika safari yetu ya kiroho. Tunapoongozwa na Roho, tunakuwa na uwezo wa kupambana na tamaa za kidunia ambazo zinatufanya tuwe mbali na Mungu.
“Lakini Roho wa kweli atakapokuja, atawaongoza awatie kwenye kweli yote. Kwa maana hatasema kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayasema, naye atawapasha habari za mambo yajayo.” (Yohana 16:13)
“Basi, kama mlivyopokea Kristo Yesu Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye mizizi na kujengwa ndani yake, na kuthibitishwa katika imani, kama mlivyofundishwa, mkizidi kutoa shukrani.” (Wakolosai 2:6-7)
“Basi, enendeni kama watoto wa nuru, kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli.” (Waefeso 5:8-9)
Tamaa za kidunia ni yale mambo yanayotupotosha na kutufanya tuishi kinyume na mapenzi ya Mungu. Ni lazima tujifunze kuzishinda kwa kuimarisha uhusiano wetu na Mungu kupitia maombi, kusoma Neno la Mungu, na kushirikiana na wengine waaminio. Roho Mtakatifu hutusaidia kuona na kutambua uovu na udanganyifu wa tamaa za kidunia na kutupa nguvu ya kuzishinda.
“Basi, ndugu zangu, sisi tuna deni, si kwa mwili, kufuatana na mwili; kwa maana kama mkiishi kufuatana na mwili, mnakufa; bali kama mkiyaangamiza matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.” (Warumi 8:12-13)
“Wala msiifanye miili yenu kuwa silaha za dhambi kwa kutenda uovu, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama watu waliotolewa katika wafu na kupewa uhai, na miili yenu iwe silaha za haki kwa Mungu.” (Warumi 6:13)
“Kwa maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome; tukibomoa mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinue juu ya elimu ya Mungu; tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo.” (2 Wakorintho 10:4-5)
Kutembea katika nuru ya Roho Mtakatifu ni kuishi maisha yaliyojaa matunda ya Roho, kama vile upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu, upole, na kiasi. Tunapojitahidi kuishi kwa njia hii, tunakuwa mashahidi wa kweli wa Kristo na tunavutia wengine kwake. Ni muhimu kufahamu kwamba hatuwezi kutembea katika nuru ya Roho kwa nguvu zetu wenyewe, bali kwa neema na uwezo wa Roho Mtakatifu ndani yetu.
“Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.” (Wagalatia 5:22-23)
“Nanyi mkivumiliana na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo nanyi. (Wakolosai 3:13)
“Tazama ni jinsi gani upendo wa Baba alivyotupa, kwamba tuitwe watoto wa Mungu; na ndivyo tulivyo.” (1 Yohana 3:1)
Kuongozwa na Roho Mtakatifu ni wito wa kila Mkristo. Ni mwaliko wa kuacha maisha yetu yaongozwe na Mungu, na kuishi kulingana na mapenzi yake. Tamaa za kidunia ni kikwazo kikubwa kwa uhusiano wetu na Mungu, lakini kwa nguvu na mwongozo wa Roho Mtakatifu, tunaweza kuzishinda na kuishi maisha yaliyojaa matunda ya Roho. Tuishi maisha ya kuongozwa na Roho, tukijua kwamba Mungu yupo nasi na anatupatia nguvu ya kushinda kila jaribu na changamoto.
Sala za kila siku katika maisha ndiyo hazina kubwa na msaada hasa wakati wa kufa. Adumuye katika sala Mungu hatomwacha saa ya mwisho. Tusali, tusali, tusali daima…
Mungu anaporuhusu ukaingia katika majaribu na mateso hana nia ya kukutesa bali anataka kukuimarisha. Mungu ni mwema kila wakati.
Upendo wa Mungu hauna kikomo. Mama anaweza kumchoka na kumtelekeza mwanae lakini Mungu kamwe hamchoki mtu.
Unapo mwomba Mungu Usisahau Kushukuru. Kushukuru ni kuomba mara ya pili. Utazidishiwa kile ulichokiomba na kupewa hata usichokiomba kwa shukrani yako.
Mungu anamjibu mtu sala zake kutokana na anachonuia.
Uwe na subira Baada ya kuomba kwa Mungu. Sio kila unachoomba kwa Mungu utakipata kwa wakati huo huo au kwa wakati unaofikiri. Mungu ni Mwaminifu Sana Kwenye kujibu maombi lakini vile vile ni mwenye Hekima Kwenye kukujibu, anajua wakati gani ni sahihi kukujibu maombi yako. Anaweza kukujibu saa hiyo hiyo, kesho, keshokutwa au hata mwakani kwa kuangalia wakati ufaao na kwa manufaa yako. Kwa hiyo unapoona hujajibiwa usife moyo, bali uwe na matumaini. Mungu anajua akujibu lini kwa kuwa anajua ni lini wakati ufaao na ni lini kitu kipi kina kufaa.
Sala ni Hazina. Kusali ni muhimu sana. Sala unayosali leo inaweza kukusaidia hata miaka kumi ijayo au ikasaidia watoto wa watoto wako. Mungu ni mwenye fadhila na anakumbuka yote. Mwombe Mungu akulinde ukiwa mzima ili uwapo hatarini akukumbuke hata kabla hujamwomba.
Kutubu ndio njia pekee ya kumrudia Mungu. Toba ya kweli ndiyo iletayo maondoleo ya dhambi. Ukiondolewa dhambi unaimarishwa na kufanywa mya. Tubu usamehewe na kufanywa mpya.
Kwa njia ya sala Binadamu anampa Mungu Utukufu, Mungu anampa Binadamu Wokovu na Neema.
Kukosa hata mara moja inahesabika ni kukosea mbele ya Mungu. Kwa kuwa kwa Mungu hakuna kusema, ‘Kukosea mara moja sio kosa bali kurudia kosa ndio kosa’. Mbele ya Mungu kila kosa lina uzito wake haijalishi ni kosa la mara ya kwanza.
Wakati wazazi waliweza kuaamua kuzaa mtoto tuu, Mungu yeye alikuchagua wewe utungwe mimba na kukulinda ungali tumboni mwa mama yako….Wakati wazazi wanasubiri kwa shauku kuona muonekano wako wewe, Mungu anawaweka wajukuu wa wazazi wako/ watoto wako ndani mwako…. Wakati wazazi wakitafuta chakula kwa ajili yako, Mungu yeye aliwawezesha kukipata…. Wakati wazazi wakingoja kuona unavyoendelea kukua huku wakiwaza hatima ya maisha yako Mungu anakuendeleza na alishapanga maisha yako tangu alipokuchagua uwe mtu ukiwa tumboni mwa mama yako…. Wazazi wanaweza kukuombea kwa Mungu lakini Mungu ndiye anayeamua akufanyie nini maana Wewe ni wa kwake….Wewe na wazazi wako ni watoto wa Baba mmoja ambaye ndiye Mungu.
Ukitaka kupata amani, tumaini katika Ahadi za Mungu. Ahadi ya Mungu ni hii “Hatoacha kutusaidia wala kututupa”.
Vile unavyomsogelea Mungu ndivyo na yeye anavyokusogelea. Vile unavyomkubali Mungu katika Maisha yako ndivyo na yeye anavyotenda kazi kwako.
Mungu ni mwema sana tunapokua wadhambi anapotuadhibu haimaanishi kuwa anatuchukia. Inamaanisha kuwa anatuonya na hapendi turudie makosa.
Sala pasipo Imani thabiti, ya nia ya kweli, upendo wa kweli, unyenyekevu wa ndani na tumaini la kweli katika Amani ya rohoni; Haijakamilika na haifai kitu.
Recent Comments