Mafundisho ya Msingi ya Kanisa Katoliki: Makala za Katoliki

Mambo ya Msingi Unayopaswa kufahamu kuhusu Ekaristi Takatifu: Mwili na Damu Ya Bwana Wetu Yesu Kristu

Ekaristi ni nini?

Ekaristi ni Sakramenti ya Mwili na Damu ya Yesu Kristo, katika
maumbo ya mkate na divai. Sakramenti hii
iliwekwa na Yesu Mwenyewe kwenye karamu ya mwisho, siku ya Alhamisi jioni kabla ya mateso
yake. (Yoh 6:1-71; Mt 26:26-28).

Maana ya jina Ekaristia

Tendo la shukrani na baraka.
Jina Ekaristi limetokana na neno la Kigiriki,
εύχαριστείν, maana yake ni “tendo la shukrani”,
“ kutoa shukrani*”, (Lk 22:19; 1Cor 11:24).
Ni tendo ambalo Yesu analifanya kwa Mungu.
Anamshukuru Mungu kwa kukamilisha kazi ya ukombozi. Tendo la baraka – εύλογείν
Kulingana na utamaduni wa Wayahudi baraka ilkua ikitolewa wakati wa mlo ikitukuza kazi za up mbaki za Mungu (Mt 26:26; Mk 14:22).

Injili zinazoongelea kuwekwa kwa Ekaristi

Injili tatu zinatueleza jinsi Yesu Kristo alivyoweka
Ekaristi Takatifu:
Mt 26:26-28.
Mk 14: 22-24
Lk 22:19-20
Mwinjili Yohane anaeleza Yesu Kristo mkate wa
uzima. Sura ya sita.
4. 1Kor 11:23-25
Mtume Paulo anatueleza jambo hilo katika Waraka wa kwanza kwa Wakorintho. 1Kor
11:23-25.

Tunajifunza kutoka kwa Yesu mambo yafuatayo

Lk 22:1. Saa ya Yesu (Lk 22:14). Hapa hamaanishi
saa ya kula, hapana. Bali saa ile ile ya kutimiliza tendo la wokovu. Yohane anapenda kusema saa ya kumtukuza Mungu, saa ya kupita kutoka ulimwengu huu kwenda kwa Baba. Sisi tunaweza kusema, tuna saa maalum ya kuingia katika ulimwengu wa
roho.Saa ya kukutana na Mungu, kutoka
ulimwengu huu kwenda kwa Mungu. (Sala au kifo).
2. Shukrani na masifu kwa Baba (Lk 22:17).
3. Kugawana sisi kwa sisi kikombe cha kwanza (Lk 22:17).
4. Kumbukumbu ya sadaka yake ya wokovu (Lk 22:19).
5. Uwepo wake (Lk 22:19).
6. Damu yake imemwagika kwa ajili yetu, kikombe cha pili (Lk 22:20).
Ekaristi ni Baraka kuu:
Yesu anabariki –kazi ya wokovu inabarikiwa na Yesu Mwenyewe. Hata vitu tunavyovitumia kila siku ni lazima kuviombea
baraka. Kabla ya mageuzo mkate na divai vinaombewa baraka (Mt 26:26).
Yesu anajitoa mwenyewe kwa watu –Yesu anajitoa kwa kila mshiriki (Mt 26:26).

Matunda ya Ekaristi katika maisha ya mkristo.

1. Muungano na Kristo:
Ekaristi inatuunganisha na Kristo kwa muungano wa ndani kabisa (Yoh 6:56).
2. Uzima wa milele : Ekaristi ni chanzo cha
uzima, maisha yetu yote yanapata uzima kwa kushiriki Mwili na damu ya Kristo, (Yoh 6:57).
3. Umoja: Ekaristi inaleta umoja wa kweli.
Tunafanywa kuwa mwili mmoja (1Kor 10:16-17).
4. Huondoa dhambi: Inatuondolea kwa
kuzifuta dhambi ndogo au inatutenga na dhambi ndogo (Mt 26:28; Yoh 1:29). Sakramenti ya
kitubio ndio hasa huondoa dhambi za mauti
(1Yoh 1:7; Yoh 20:22-23).
5. Dawa ya kutuponya kutoka katika umauti:
Ekaristi ni dawa ya kutokufa (Yoh 6:57-58).
6. Kufufuliwa siku ya mwisho: (Yoh 6:54).

Nguvu ya Ekaristi

–Kuponywa kwa
kuondolewa dhambi zetu.
Nguvu za Mungu zimo katika Ekaristi. Kabla ya kupokea Ekaristi tunasali Ee Bwana siesta hili uingie kwangu lakini sema neno tu na roho yangu
itapona. Bila shaka litakuwa kosa kubwa kwetu sisi kufikiri kwamba uponyaji unahusu masuala ya
mwili tu. Si kila uponyaji ni uponyaji wa mwili.
Mtume Paulo katika Waraka wa kwanza kwa Wathesalonike sura ya 5:23 kuwa sisi wanadamu tu mwili, roho na nafsi . Hivyo tunaweza kuponywa nafsi zetu na roho zetu. Hata kama uponyaji haujanja katika mwili.
Lakini mara nyingi ukitokea uponyaji wa ndani basi matokeo
yake utayaona hata kimwili. (anima sana in
corpore sano) (Roho yenye afya katika mwili
wenye afya)
1. Ekaristi Takatifu inayalinda maisha ya
kimanga ya roho tuliyoyapokea wakati wa Ubatizo
, kwa kupata anayekomunika nguvu za kimungu za kupambana na vishawishi, na
kudhoofisha nguvu za tamaa. Inaimarisha uhuru wa mapenzi ya nafsi zetu wa kuhimili
mashambulizi ya shetani.
2. Ekaristi Takatifu inaongeza maisha ya
neema ambayo tayari tunayo. Hufanya hivyo kwa kuhuisha fadhila na vipaji vya Roho Mtakatifu
tulivyonavyo.
3. Ekaristi Takatifu inayatibu magonjwa ya kiroho ya nafsi kwa kuziondoa dhambi ndogo na kumkinga mtu na adhabu ndogo ndogo za kidunia
zitokanazo na dhambi. Ondoleo la dhambi ndogo na mateso ya muda yasababishwayo na dhambi hizi hufanyika mara moja kwa sababu ya upendo
kamili kwa Mungu ambao huamshwa kwa
kuipokea Ekaristi. Ondoleo la dhambi hizi
hutegemea kiasi cha upendo unaoelekezwa
kwenye Ekaristi (Lk 7:47).
4. Ekaristi Takatifu inatupa furaha ya kiroho tunapomtumikia Kristo, tunapotetea njia yake,
tunapotekeleza majukumu yetu ya maisha, na kufanya sadaka zetu zinazotukabili zile ni katika kuiga maisha ya Mwokozi wetu.
The ListPages module does not work recursively.

Utaratibu wa Mkristo Mkatoliki Kanisani

Ninapoingia kanisani nachovya maji ya baraka na kusema;
“Unitakase Ee Bwana mimi na uovu wangu wote, ili nipate kustahili kushiriki ibada takatifu’ Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu” Amina!
Ninapiga goti huku nikisema
“Mungu wangu na Bwana wangu”
🙋🏽Nikiinuka nasema
“Nitakusifu na kukuabudu katika Ekaristi takatifu”
🙋🏽Naenda mpaka kwenye bench, napiga magoti au nakaa nikiwa mimeinamisha kichwa (kama mabenchi yameisha nabaki nimejisimamia) huku nikitoa nia yangu ya kusali misa siku hiyo, mfano
“Ee Mungu, ninaungana nawe na jeshi lote la mbinguni, pamoja na Mama Bikira Maria, nikiwa na nia ya kumwombea mama yangu ambaye ni mgonjwa, jirani yangu ambaye mpaka sasa hatuelewani na pia familia yetu ambayo haina amani, Mungu kupitia misa hii rejesha hali ya mama yangu, rejesha uelewano na jirani yangu, na pia rejesha amani ya familia yetu pamoja na familia zote ambazo hazina amani”
🙋🏽Ninaendelea na misa na Kushiriki litrujia kikamilifu
🙋🏽Wakati wa komunyo nikikumbuka kuwa nina dhambi kubwa huwa nakominika kwa sala ya tamaa wala siendi mbele, huwa najikalia tu kwenye bench naangalia wenye moyo safi wanaenda mbele kumpokea Yesu (Kweli huwa najisikia wivu sana, itanibidi katikati ya wiki nifanye kitubio ili nisikae tena)”
🙋🏽Mwisho wakati wa kuondoka nachovya maji ya baraka nikisema
“Unilinde Ee Mwenyezi Mungu, nikapate kuwa mfano katika jamii yangu, na nikushuhudie katika matendo yangu”
(Hapo nachovya maji ya baraka na kufanya ishara ya msalaba) “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, amina”
Usiku mwema wapendwa. Malaika awalinde

Tarehe ya Pasaka inavyopatikana

KWANINI TAREHE ZA PASAKA HUBADILIKA KILA MWAKA ??

JIBU:
KALENDA za mwanzo ziliutumia mwezi wa
angani kama kipimo cha muda. Ziliitwa “Lunar
calender” au Kalenda-Mwezi. Tarehe 1 ya
Mwezi ilikuwa ni siku ulipoandama yaani
Mwezi-Mdogo (Crescent Moon).
Mwezi unapofika siku ya 15 unakuwa umefikia
ukubwa wa juu na huitwa Mwezi-Mkubwa (Full
Moon). Hivyo kwa kalenda ile tarehe 15
ilikuwa ni siku ya Mwezi-Mkubwa.
Mwaka 45KK, Julius Caesar alitangaza kalenda
mpya ikaitwa “Julian Calender” iwe na siku
365.

Wakati huo ikijulikana kwamba jua
huzunguka kwa siku 365.25. Hivyo pengo la
kalenda na mzunguko likabaki robo siku.
Robo hiyo ifidiwe kila baada ya miaka minne
mwishoni mwa mwezi Februari ambayo sasa
ulifanywa kuwa wa pili baada ya January.
Inapofanyika hivyo, huo ukaitwa mwaka-mrefu
(Leap year).
Mwaka mrefu ukachaguliwa kuwa ni ule tu
unaogawanywa kwa nne mfano miaka ifuatayo
1700, 1800, 1900, 2100, 2200, 2300.
Baadaye iligundulika kuwa dunia huzunguka kwa
siku 365.24218967 ziitwazo “Tropical year”.
Hizi ni chache kuliko siku 365.25
zilizokadiriwa mwanzoni. Uchache huu
husababisha kuwe na pengo la dakika 11 na
sekunde 14.812512 kwa mwaka.
Pengo hili ni dogo, lakini hupanuka hadi kuwa
siku nzima kila baada ya miaka 128.0355.
Mwaka 1545 lilivuka siku 9.25.
Kuondoa tatizo hili, Papa Gregory XIII aliamuru
iundwe kalenda mpya na akachagua Oktoba
04, 1582 iwe siku ya mwisho kutumika “Julian
Calender”. Kesho yake, kalenda mpya ikaanza
kutumika. Ungetegemea hiyo kesho iwe ni
Oktoba 05, 1582. Lakini ili uzibe pengo lile
lililofikia siku kumi, ilibidi kalenda mpya
kuziruka siku hizo siku kumi. Hivyo hii mpya
iliyoitwa “Gregorean Calender” ikaanza kama
Oktoba 15 badala ya Oktoba 05.
Ndiyo sababu katika historia ya nchi nyingi
Ulaya, hakuna tarehe za Oktoba 05, 1582 hadi
Oktoba 14, 1582. Watu walilala Oktoba 04,
1582 kesho yake wakaamka ikiwa ni Oktoba
15, 1582.

Teresa Alonso huandikwa kwamba alifariki
Oktoba 1582, kwenye usiku wa tarehe NNE
kuamkia tarehe KUMI NA TANO! Alipotangazwa
kuwa Mtakatifu, Kanisa Katoliki likaifanya
Oktoba 15 kuwa siku ya kumkumbuka, yaani
siku ya Mtakatifu Teresa wa Avila.
Usipofahamu kwamba Mtakatifu Teresa alifariki
siku kalenda zinabadilishwa, utadhani
aliyeandika vile tarehe za kifo chake
amekosea!
Waandishi, William Shakespeare wa Uingereza
na Miguel de Cervantes wa Spain huandikwa
kwamba wote walifariki Aprili 23, 1616. Lakini
ukweli ni kwamba hawakufa siku moja bali
walipishana siku kumi kwani England
ilichelewa kwa karibu miaka 200 kuikubali
“Gregorean Calender”!
“Gregorean Calender” haikuundwa ili kuishia
kuliziba lile pengo. Bali pia, kuhakikisha
halitokei tena. Tumeshaona kuwa lile pengo ni
dakika 11 na sekunde 14.812512. Hivyo,
linapanuka na kuwa siku tatu ndani ya miaka
400.

Hivyo kuliziba inatakiwa kupunguza siku tatu
kila baada ya miaka 400. Je, zipunguzweje?
Kipande cha miaka 400 kina miaka mitatu ya
karne inayogawanyika kwa 4 lakini
haigawanyiki kwa 400.
Ikakubalika kwamba unaogawanyika kwa 4,
lakini haugawanyaiki kwa 400, usiendelee
kuwa mrefu. Humo siku moja ichomolewe na
uwe mfupi.
Ndipo miaka 1700, 1800, 1900 haikuwa tena
mirefu. Ndivyo pia miaka 2100, 2200, 2300
nayo haitakuwa mirefu. Kwa sababu ni miaka
ambayo “Gregorean Calender” inachomoa siku
moja ili kutosababisha pengo tena.
Kipande hiki cha miaka 400 kikaleta wastani
mpya wa siku 365.2425 kwa mwaka. Sasa lile
pengo lile la siku moja si rahisi kufikiwa.
Kwenye “Julian Calender” tumeona lilikuwa
miaka 128.0355 lakini sasa limekuwa miaka
3,222.
Sasa tuijadili tarehe ya siku ya Pasaka tukiwa
na ufahamu wa kalenda zile. Je, tarehe ya
Pasaka imetajwa ndani ya Biblia? Kuna kifungu
kinasema hivi:
“..Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya
mwezi, wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA.
Na siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni
sikukuu ya BWANA, ndiyo siku ya mikate
isiyotiwa chachu. (Walawi 23:5)..”. Hivyo
Pasaka ni tarehe 15 ya mwezi wa Kwanza.
Lakini Biblia pia inautaja mwezi wa kwanza
kwa jina la Nisan (Esta 3:7, Nehemia 2:1).
Yesu alisulubiwa mwaka ambao Ijumaa
iliitangulia sikukuu ya Pasaka kwa siku moja
(Yohana 18: 28, Marko 15:42-43). Hivyo
tarehe ya Yesu kusulubiwa ni Ijumaa, Nisan
14. Siku moja kabla ya Nisan 15. Siku moja
kabla ya Mwezi-Mkubwa.
Baada ya Yesu, Wakristo wengi Pasaka
waliiadhimisha Jumapili, lakini utata ulijitokeza
kuhusu tarehe ya kuiweka hiyo Jumapili ya
Pasaka. Ilifika wakati jimbo moja la Wakristo
linaadhimisha siku tofauti na jingine na kwa
njia wanayoijua wao.

Utata huu uliondolewa kule Nicaea mwaka 325
ambapo Kanisa Katoliki lilipoamua kuwa,
tarehe ya Pasaka iwe moja tu duniani kote,
yaani iwe ni Jumapili inayokuja baada ya
Mwezi-Mkubwa (Full Moon) unaotokea baada
ya siku ya Ikweta, yaani baada ya Machi 21
(Equinox).
Baada ya uamuzi huu, wataalamu walipania
kuunda chati maalum zenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa zitazokasaidia kuitambua tarehe ya
Pasaka kwa mwaka wowote.
Mwezi huizunguka dunia kwa siku
29.5305891203704 (Synodic Month), wakati
dunia hulizunguka jua kwa siku 365.24218967
(Tropical year).
Mizunguko hii miwili ikianza safari siku moja,
itapishana kila mwaka, lakini itakutana tena
mwezi unapokamilisha mizunguko 235. Dunia
nayo inakuwa imekamilisha mizunguko 19,
yaani miaka 19.
Wataalamu wakaitumia hii miaka 19
kutengeneza chati yenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa unaotokea March 22 hadi April 18.
Tarehe zile zikaitwa tarehe za Mwezi-Mkubwa
Wa Pasaka au Ecclesiastical Full Moon (EFM).
Ndani ya ile miaka 19, kila mwaka ukapewa
tarakimu iitwayo Golden Number inayosimama
badala ya mwaka ikiwa na tarehe zile
ziliorekodiwa za Mwezi Mkubwa wa Pasaka.
Chati yenyewe ya Golden Number na tarehe
zake (siku/Mwezi) ni hii ifuatayo: {1=5/4,
2=25/3, 3=13/4, 4=2/4, 5=22/3, 6=10/4,
7=30/3, 8=18/4, 9=7/4, 10=27/3, 11=15/4,
12=4/4, 13=24/3, 14=12/4, 15=1/4, 16=21/3,
17=9/4, 18=29/3, 19=17/4}
Golden Number ya mwaka inapatikana kuanza
kuugawa mwaka kwa 19. Tulifundishwa
mashuleni kuwa namba inayosalia baada ya
kugawa huitwa “Baki” . Hii “Baki” ukiijumlisha
na 1 unapata Golden Number (GN).
Mfano unatafuta GN ya 27. Hatua ya kwanza ni
kutafuta “Baki” baada ya kugawa 27 kwa 19.
Hizi ni hesabu za “modulo” , yaani zinahitaji tu
namba inayobaki baada ya kugawa.
Ikiandikwa hivi: (27 mod 19) inatakiwa namba
inayobaki baada ya kuigawa 27 kwa 19. Jibu
ni 8. Hivyo tulipaswa tuandike hivi: (27 mod
19=8). “Baki” 8 tuliyoipata, ndiyo tunaihitaji ili
tuijumlishe na 1 ili tupate GN ambayo hapa ni
9 kwani (8+1=9).

Tungeweza pia kuandika hivi : 27 mod 19 +
1=9. Hivyo kanuni ya kupata GN kwa mwaka
wowote ni hii:
(MWAKA mod 19 + 1). Yaani, ugawe huo
mwaka kwa 19, kisha namba itakayobaki
ijumlishe na moja.
Ukishaipata GN, itafute kwenye ile chati
ambapo utaiona ikiwa na mwezi na tarehe.
Jumapili inayofuata baada ya tarehe hii ndiyo
tarehe ya Pasaka ya mwaka huo.
Tutumie chati ile na kanuni hii kujua tarehe ya
Pasaka ya mwaka 1474. GN ni (1474 mod 19 + 1=12). Hivyo GN ni 12.
Kwenye chati, 12 inaonyesha ni tarehe 4/4.
Hivyo, mwaka 1474 Mwezi-Mkubwa wa
Pasaka ulikuwa tarehe 4/4/1474. Hiyo ilikuwa
ni Jumatatu. Hivyo Pasaka ilikuwa ni Jumapili
iliyofuata yaani tarehe 10/4/1474.
Lakini, Kanisa Katoliki liliikubali kanuni hii
karne ya sita. Hii ndiyo sababu, tarehe za
Pasaka zinazojulikana ni zile tu zinazoanza
mwaka 533.

Ndivyo Pasaka ilivyotafutwa miaka ile. Sasa
tuone Pasaka ya kizazi chetu. Kizazi cha
“Gregorean Calender” iliyoanza mwaka 1582.
Tumelijadili lile pengo la siku lililofikia ambalo
mwaka 1582 lilishafika siku 10. Ukweli ni
kwamba kabla halijazibwa, Pasaka ilikuwa
inawadia lakini uhalisi ni kwamba inakuwa
tayari imepitwa siku 10. Kinyume kabisa na
maamuzi ya Kanisa kule Nicaea!
Ili kulizuia lisitokee tena, tumeona uchomoaji
wa siku moja toka kwenye miaka inayofunga
karne, isiyogawanyika kwa 400. Uchomoaji
huu umewekwa kwenye kanuni (formula)
iitwayo “Solar Equation”.
Kama mwendo wa kuzunguka jua
umezingatiwa na “Gregorean Calender”, vipi
kuhusu mwendo wa mwezi?
Tumeuona kwamba mizunguko ya mwezi na
dunia hukutana kila baada ya miaka 19.
Kadirio la dunia kuzunguka kwa siku 365.25
linafanya ikizunguka kwa miaka 19 zinakuwa
siku 6,939.75. Mwezi utakuwa nao
umezunguka mara 235, huku kila mzunguko
ukitumia siku 29.5305891203704.
Hivyo, kukutana kule ndani ya kila miaka 19,
huleta pengo dogo la saa 1, dakika 28,
sekunde 38.5.
Mapengo madogo haya tunayoyapuuza
mwanzoni, yameshatugharimu vya kutosha.
Pengo hili kwa mwaka ni dogo lakini kwa
miaka 2500 linakuwa hadi kufika siku nane.
Kwenye hesabu za kutafuta Pasaka
urekebishaji wa hili pengo hutokea kwenye
kanuni iitwayo “Lunar Equation”. Lakini kwa
sababu ya tofauti ya uelekeo wa mzunguko wa
mwezi na dunia, “Lunar Equation” hujumlisha
mara nane kila baada ya miaka 2500.
Hivyo, mahesabu yoyote ya kuitafuta tarehe ya
Pasaka hayakosi kanuni hizi mbili “Solar
Equation” na “Lunar Equation” .
Tumeona kwamba kalenda ilianza mwaka
1582. “Solar Equation” inaondoa siku moja
toka kwenye miaka 1700, 1800, 1900. Hivyo,
ni kujidanganya kusema kwamba miaka yote
inayogawanyika kwa nne ni mirefu, jambo
ambalo hata mimi nilifundishwa shuleni. Hapa
tumeona kwamba “Solar Equation” imeondoa
siku moja kwenye mwaka 1900 na hivyo
haukuwa mwaka mrefu ingawa unagawanyika
kwa nne.

“Lunar Equation” huongeza siku moja kwenye
miaka 1800, 2100, 2400. Mwaka 1800
unaguswa na vyote “Solar Equation” na “Lunar
Equation”. Hivyo hauathiriki.
Kanuni zote za kuitafuta Pasaka huzingatia
zaidi ya niliyoyaeleza, lakini cha muhimu zaidi
ni hizi mbili yaani “Solar Equation” na “Lunar
Equation” ambazo sijawahi kuzisikia kwa
kiswahili.
Ni vigumu kuepuka hesabu za “modulo” au
“mod” unapotafuta tarehe ya Pasaka. Lakini
ukiwauliza wanafunzi wa darasa la nne
kwamba machungwa 2011 yakipangwa kwenye
mafungu 19, ni mangapi yatakosa fungu?
Wapo watakaopata jibu sahihi kwamba ni
machungwa 16. Kimahesabu swali hilo
linaandikwa hivi: (2011 mod 19) na jibu lake
ni 16, yaani (2011 mod 19=16).
Ifuatayo ni moja ya kanuni zinazotumika
kuipata tarehe za Pasaka ya mwaka wowote
kuanzia 1700 hadi 2099:
(1) : a=MWAKA mod 19;
(2) : b=MWAKA \ 100;
(3) : c=MWAKA mod 100;
(4) : d=b \ 4;
(5) : e=b mod 4;
(6) : f=c \ 4;
(7) : g=c mod 4;
(8) : h=(b + 8)\25;
(9) : i=(b – h + 1)\3;
(10) : j=(19xa + b – d – i + 15) mod 30;
(11) : k=(32 + 2xe + 2xf – j – g) mod 7;
(12) : m=(a + 11xj + 22xk) \ 451;
(13) : n=j + k – 7xm + 114;
(14) : Tarehe=(n mod 31) + 1
(15) : Mwezi =n\31;

Penye neno MWAKA, andika mwaka unaotafuta
kujua tarehe yake ya Pasaka. Panapotokea
alama (\) ni kugawanya ambako hata kama
jibu litaleta desimali, basi hiyo desimali
unatakiwa kuachana nayo ili jibu libaki namba
nzima. Penye alama (x) hiyo ni ya kuzidisha.
Yafuatayo ni majibu niliyopata kwa hatua zote
baada ya kuuingiza mwaka 2017 ili kujua siku
ya Pasaka ya mwaka huu: (1): 3, (2): 20, (3):
17, (4): 5, (5): 0, (6): 4, (7): 1, (8): 1, (9): 6,
(10): 21, (11): 4, (12): 0, (13): 139, (14): 16,
(15): 4.
Tarehe imepatikana kwenye hatua ya 14
ambako jibu ni “16”. Mwezi umepatikana
kwenye hatua ya 15 ambako jibu ni “4”. Hivyo
Pasaka ya mwaka (2017) huu ni Tarehe 16,
mwezi wa 4.
Hivyo, kwa njia hii, unaweza kujua tarehe za
Pasaka kwa miaka ijayo kama unavyoijua
tarehe ya Krismas. Kama kuna tukio lilifanyika
siku ya Pasaka miaka iliyopita na hukumbuki
tarehe, basi tumia kanuni hii.
Zifuatazo ni siku zinazoitangulia Pasaka kwa
idadi ya siku zilizoandikwa kwenye mabano:
Jumatano Ya Majivu (46), Jumapili ya Matawi
(7), Ijumaa Kuu (2).
Zinazotanguliwa na Pasaka ni hizi zifuatazo:
Kupaa (42), Pentekoste (49), Utatu Mtakatifu
(56), Ekaristi (63).
Mwanzo tuliona kwamba Mwezi-Mkubwa wa
Pasaka au “Ecclesiastical full Moon” ni ule wa
March 22 hadi April 18. Ukitokea March 22
basi kuna uwezekano siku hiyohiyo ikawa
Pasaka na ikawa imevunja rekodi ya kuwahi
mapema.
Ukitokea April 18, kuna uwezekano wa Pasaka
kuwa siku saba zaidi ya hapa yaani April 25,
na hiyo ikawa ni tarehe ya juu mno ya Pasaka.
Hivyo, Pasaka yoyote haiwezi kuwa chini ya
Machi 22, wala haiwezi kuwazaidi ya April 25.
Pasaka tuliyoiona mwaka 2008 ndiyo ya
mwisho kwa kizazi chetu kuiona ikiwahi
mapema kiasi kile, kwani ilitokea Machi 23 na
itairudia tena tarehe hiyo mwaka 2160!

NB: iyo ni moja tu ya kanuni(formula) zitumikazo kupata tarehe na mwezi wa pasaka ya kila mwaka

Nawatakia kwaresma njema…..

Usipite bila kusoma kisa hiki cha kusisimua

Siku moja jioni katika mji flani, kulikuwa na basi likisafiri kutoka mji huo kuelekea mji mwingine. Lilikuwa ni basi kubwa na limejaa abiria. Wakati wakiendelea na safari, ghafla, mvua kubwa iliyoambatana na radi ikaanza kunyesha. Dereva hakuogopa, wala abiria, wakaendelea na safari. Mara wakati wanaenda, radi ikaanza kufuatilia gari. Kila wakienda, radi inapiga karibu na basi kana kwamba inalifuata basi. Likisimama, radi inapiga pembezoni mwa basi.

Dereva kuona hivyo, akasimamisha gari mita 5 kutoka kwenye mti… Akawaambia abiria, “Humu ndani ya basi, kuna mtu ambaye leo ni siku yake ya kufa, tena kufa kwa radi. Ili tusife wote, nataka kila abiria ashuke akaguse mti ili anayepigwa na radi, apigwe wengine wasife kwa ajili yake. “Abiria wakitetemeka, wakaanza kushuka mmoja mmoja. Unaenda unagusa mti , kisha unarudi kwenye basi. Abiria wote pamoja na dereva mmoja mmoja, wakaenda, wakagusa mti na kurudi bila dhara lolote! Akawa kabaki abiria mmoja tu, ambaye alikuwa hajagusa mti. Abiria wote kwa macho ya hasira wakamwambia akaguse mti. Akawa anaogopa kufa. Akagoma. Wakamlazimisha kwa nguvu sana na kumtoa nje……. …….. Yule abiria akiwa amefumba macho, akaenda akagusa mti. Hamadi bin Vuu! Radi kali sana ikalipiga basi, abiria na wote waliokuwamo, wakafa palepale. Kumbe uwepo wake ndio ulikuwa unazuia abiria wengine wasidhurike na radi.

MAFUNZO

1. Unapofanikiwa, huwezi jua uwepo wa nani umefanikisha mafanikio yako, usichukue sifa zote peke yako. Wapatie na wengine bila kumsahau MUNGU.
2. Unaweza kujiona huna thamani sehemu ulipo, iwe kwenye kundi la WhatsApp, darasani, kazini, kwenye basi, barabarani bila kujua kama uwepo wako ni wa muhimu sana kwa ustawi wa wengine.
3. Usimtenge wala kumnyanyasa mtu au jirani yako, huwezi jua uwepo wake ni kwa ajili gani.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu umoja wa Kanisa?

Kanisa Katoliki ni moja ya madhehebu makubwa ya Kikristo duniani. Imani yake kuhusu umoja wa Kanisa ni dhahiri kabisa. Kanisa Katoliki linasimamia umoja wa Kanisa kwa kufuata kanuni za Kikristo na sheria zake. Katika makala hii, tutajadili kwa kina imani ya Kanisa Katoliki kuhusu umoja wa Kanisa.

Kanisa Katoliki linatazama umoja wa Kanisa kama sehemu muhimu ya imani yake. Katika Injili ya Yohana 17:20-21, Yesu alisema, "Nakuomba pia kwa ajili ya wale watakaoniamini kwa sababu ya ujumbe wao, ili wote wawe na umoja. Kama wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi ndani yako, hata hao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma." Hii ina maana kwamba Yesu alitaka wafuasi wake kuwa na umoja, ili ulimwengu upate kuona kwamba wao ni kweli wanafunzi wake.

Kanisa Katoliki linasisitiza umoja wa Kanisa kwa njia nyingi. Mojawapo ya njia hizo ni kwa kuhakikisha kwamba liturujia zake ni moja, kwa kutumia lugha ya Kilatini. Hii ni kwa sababu lugha ya Kilatini ni lugha ambayo ilikuwa inatumiwa katika Kanisa la mapema, na ina maana ya kuunganisha na kudumisha utamaduni wa Kanisa la mapema.

Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, kifungu 820 kinasema, "Kanisa, katika Kristo, ni jumuiya ya waamini ambao wanaunganishwa pamoja na wale walioko mbinguni na wale ambao wako njiani kuelekea mbinguni. Ni jumuiya ya watakatifu. Umoja wa Kanisa ni hali ya uaminifu na upendo, ambao unatokana na Roho Mtakatifu." Hii inaonesha jinsi Kanisa Katoliki linavyoona umoja kama sehemu ya imani yake.

Kanisa Katoliki pia linahimiza umoja wa dini katika dunia. Kanisa linakubali kwamba kuna tofauti za kidini, lakini linasisitiza kwamba umoja wa dini ni muhimu kwa ajili ya amani na utulivu wa dunia. Kifungu cha 821 cha Catechism kinasema, "Katika kipindi cha historia, Kanisa limeishi kwa furaha na kwa heshima na dini zote, kwa sababu lilikuwa linatambua kwamba mambo mengi ya kweli na uzuri yanapatikana kwenye dini nyingine."

Kanisa Katoliki pia linahimiza umoja wa familia katika Kanisa. Hii inamaanisha kwamba Kanisa linataka familia zote zifanye kazi pamoja ili kujenga umoja katika Kanisa. Kanisa linahimiza familia kutumia muda pamoja, kusali pamoja na kushiriki Sakramenti pamoja.

Kwa ufupi, Kanisa Katoliki linasisitiza umoja kama sehemu muhimu ya imani yake. Kanisa linataka waamini wake wawe na umoja kama Yesu alivyotaka, ili ulimwengu uweze kuona kwamba wao ni kweli wanafunzi wake. Kanisa pia linahimiza umoja wa dini katika dunia, umoja wa familia katika Kanisa na umoja wa liturujia za Kanisa. Hii ni kwa sababu Kanisa linatambua kwamba umoja ni muhimu kwa ajili ya amani na utulivu wa dunia. Tufuate imani ya Kanisa Katoliki kuhusu umoja wa Kanisa.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya sala?

Kanisa Katoliki linathamini sana maombi kama sehemu muhimu ya maisha yetu ya kiroho. Imani yetu inatufundisha kuwa kupitia maombi tunawasiliana na Mungu na kuimarisha uhusiano wetu naye. Hii ni kwa sababu tumeumbwa kwa mfano wa Mungu na tunaishi kwa neema yake.

Maombi ni mawasiliano ya moyo na Mungu, ambayo yanatuwezesha kumwomba msamaha kwa dhambi zetu na kupata nguvu za kushinda majaribu. Kwa hivyo, sala ni sehemu muhimu ya maisha ya Kikatoliki na inahitajika kwa maendeleo yetu ya kiroho.

Tunapata mafundisho haya kutoka kwa Yesu mwenyewe, ambaye aliwaambia wanafunzi wake kuwa wasali daima na kutokata tamaa (Luka 18: 1). Katika Yohana 15: 7, Yesu anatuambia kuwa ikiwa tunakaa ndani yake na neno lake linakaa ndani yetu, tunaweza kuomba chochote tunachotaka, na Mungu atatupa.

Kanisa Katoliki pia linatupa mfano wa sala kwa kufundisha kwamba sala ya Bwana ni muhimu sana. Sala hii inatufundisha kumwomba Mungu kwa njia ya kinafiki na kutambua kwamba yeye ndiye muumba wetu. Tunamuomba Mungu kwa mahitaji yetu ya kila siku, pamoja na kupata nguvu za kushinda dhambi.

Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunaambiwa kuwa sala ya Kanisa ni muhimu sana. Sala hii inaundwa na sala za Wakristo wote na inaunganisha Kanisa kama mwili wa Kristo. Sala hii inatupa nguvu za kuishi maisha ya Kikristo kwa kupata nguvu zetu kutoka kwa Roho Mtakatifu.

Kwa hivyo, kama Wakatoliki, tunahimizwa kuomba kwa nguvu zetu zote na kwa moyo wote. Tunatafuta kumjua Mungu vizuri zaidi na kukuza uhusiano wetu naye kupitia sala. Kwa njia hii, tunaweza kuwa na maisha yenye furaha, amani, na raha ya ndani.

Kwa hiyo, tunakuhimiza, mpendwa msomaji, kuanza maisha ya sala na kujitolea kwa Bwana wetu. Kwa kufanya hivyo, utapata furaha ya kweli na utaishi maisha yenye maana. "Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; pigeni hodi, nanyi mtafunguliwa" (Mathayo 7: 7).

MAANA YA SALA KWA MKRISTO

Sala ni kuinua mioyo yetu kwa Mungu na kuongea nae. Watu wote wanapaswa kusali, wema na wabaya. Inatupasa kusali kila siku bila kukata tama kwa ibada, kwa matumaini na kwa saburi. Kama mfano Yesu Alitufundisha sala ya Baba yetu.
Yatupasa kuwaombea wengine, watu wote wenye shida wakosefu na hata maadui zetu, vilevile tumtolee Mungu shukrani kila wakati na hasa kwa kuadhimisha Ekaristi Takatifu.
Masifu ni sala au wimbo unaomsifu na kumtambua Mungu kuwa Mungu.
Sababu za kusali
1. Kumuabudu Mungu
2. Kumshukuru Mungu
3. Kuomba Neema na Baraka kwa ajili yetu na wenzetu
4. Kuomba msamaha
Namna za sala
1. Sala ya sauti : Sala asaliyo mtu au kikundi kwa kutumia maneno
2. Sala ya fikra : Sala asaliyo mtu akiwa peke yake au na wengine kimya kimya akimuwaza Mungu.
3. Sala ya Taamuli: Kumtazama tuu Mungu kwa upendo Mkubwa Moyoni.
Nyakati zote zinafaa kwa sala hasa
1. Asubuhi na jioni
2. Kabla na baada ya kula
3. Kila dominika
4. Sikukuu za amri
5. Kabla na baada ya kazi
6. Katika kishawishi
Vyanzo vya sala za Kikristo
1. Neno la Mungu
2. Liturujia ya Kanisa
3. Fadhila za Kimungu
4. Matukio ya kila siku
Aidha Roho Mtakatifu ndiye mlezi wa ndani wa sala ya Kikristo akitufundisha kusali na kusali ndani mwetu.
Sala Muhimu kwa Mkristo
Sala kubwa ya kanisa ni Misa Takatifu na sala Bora kwa Bikira Maria ni Rozari Takatifu.
Sala nyingine Muhimu kwa Mkristu ni:
1. Baraka ya Sakramenti kuu
2. Andamo la Ekaristi
3. Litania Takatifu
4. Njia ya Msalaba
5. Rozari takatifu
6. Novena
Mtu anaweza kusali popote lakini kanisani ndio mahali rasmi pa sala, Aidha familia ni shule ya kwanza ya sala ambapo mtu hujifunza na kujizoesha kusali anapokua katika familia.
Changamoto na majaribu wakati wa kusali
1. Mtawanyiko wa mawazo
2. Ukavu wa Moyo
3. Uvivu na uregevu
Faida ya Sala
1. Zinaleta neema nyingi
2. Zinatuimarisha ili tushinde vishawishi na dhambi
3. Zinatuunganisha na Mungu
4. Zinatudumisha katika kutenda mema
Neno Amina katika sala linamaana ‘Na iwe hivyo’. Na neno Aeluya maana yake ni Msifuni Mungu.

JE,SHERIA YA MAPADRE KUTOOA NA KUISHI USEJA IMEANDIKWA WAPI KATIKA BIBLIA AU IMETUNGWA TU NA PAPA?

Pengine umewahi kuulizwa swali hili wakati fulani.Na jibu lake ni kama ifuayavyo:
Mtu anapouliza kila kitu kimeandikwa wapi katika Biblia ni kudhihirisha kutokuijua au kuielewa vizuri Biblia Takatifu na historia yake.Mtu anapong’ang’ania “nionyeshe kitu fulani kimeandikwa wapi kwenye Biblia”ni kutaka kujiona ya kwamba yeye anaielewa sana Biblia na ameisoma yote kwa hiyo kila kitu kilichopo kwenye Biblia anakifahamu kumbe haijui Biblia bali anakariri Biblia!
Na hili suala la kushupalia swala la kuoa linadhihirisha jinsi gani tulivyo kizazi cha zinaa,ni kama tunadhani kuwa UZIMA upo katika kujamiiana!La hasha.
Paulo anasema “Kwasababu ya zinaa ni bora kuoa na kuolewa”(1Wakorintho 7:2.9) haya sio maneno ya kufurahia na kuchekelea tu maana “YANAWALENGA WALE WALIOSHINDIKANA KATIKA YALE YAPENDEZAYO”(1Wakorintho 7:1.8)sasa ni lazima tujiulize je tumeshindikana kiasi hicho?,hiyo sio sifa!
1Wakorintho 7:1.8
“Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika,ni heri mwanaume asimguse mwanamke,8.Lakini nawaambia wale wasiooa bado na wajane heri wakae kama mimi nilivyo”
Na Paulo Mtume anasema “Ni bora kuoa au kuolewa” lakini hakusema “Ni LAZIMA kuoa au kuolewa”
Suala la kutooa kwa mapadre kadiri ya historia lilianza tangu zamani kabisa mwanzoni mwa milenia ya pili katika mtagusi wa pili wa Laterani mwaka wa 1139 ili waweze kumtumikia Mungu kwa uhuru na bila mawaa wala pasipo vikwazo(1wakorintho 7:32-35)
1wakorintho 7:32-35
“32Lakini nataka msiwe na masumbufu.Yeye asiyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya Bwana ampendezeje Bwana;33.bali yeye aliyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendeza mkewe.34-Tena iko tofauti kati ya mke na mwanamwali.Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana ili apate kuwa mtakatifu mwili na Roho.Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendezesha mumewe.,35.Nasema hayo niwafaidie ninyi,si kwamba niwategee tanzi,bali kwaajili ya vile vipendezavyo,tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine”
Maandiko hayo hapo juu yanajieleza wala sidhani kama yanahitaji kufafanuliwa zaidi ya yanavyojifafanua yenyewe.
Watu wengine wanafikiri kwamba kutooa ni dhambi,kama ni hivyo basi hata Yesu mwenyewe alikosa maana hata yeye mwenyewe hakuoa.
Yesu mwenyewe anafundisha kuhusu ubikira(Mathayo 19:10-12)
Mathayo 19:10-12,
“Wanafunzi wake wakamwambia,kama mambo ya mme na mke yakiwa hivyo ni afadhali kutuooa kabisa.Lakini Yeye akawaambia ‘SI WOTE WAWEZAO KULIPOKEA NENO HILO,ILA TU WALE WALIOJALIWA,maana wako MATOWASHI waliozaliwa katika hali hiyo toka matumboni mwa mama zao;tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi,tena wako Matowashi WALIOJIFANYA WENYEWE KUWA MATOWASHI KWAAJILI YA UFALME WA MBINGUNI’,awezaye kulipokea neno hili na alipokee”
Yesu mwenyewe analifafanua jambo hili kwa mapana,katika orodha ya matowashi Yesu aliowataja,Mapadre ni Matowashi waliojifanya hivyo kwaajili ya huduma ya kanisa na ufalme wa Mungu.
Tena Yesu anatuambia waziwazi kwamba”sio wote wawezao kulipokea neno hilo”yaani sasa sio wote wawezao kuwa Matowashi(Mapadre)bali ni wale tu waliojaliwa na Mungu neema hiyo.wale wasioweza kuishi upadre huoa na kuwa na familia.Tena Yesu anamalizia kwa kusema “Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee”,kwa maana nyingine ni kusema “Fundisho au Utowashi huu sio wa lazima”anayeweza kuishi maisha hayo basi na ayapokee na yule asiyeweza basi aache!
Vilevile Mitume ili kumfuata Yesu kikamilifu waliyaacha yote waliokuwa nayo ikiwepo familia zao ili wamtumikie Bwana(Mathayo 19:27.29)
Mathayo 19:27.29:
“Ndipo Petro akajibu akamwambia ‘Tazama sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe,tutapata nini basi?29.Amini nawaambia,kila mtu aliyeacha nyumba au ndugu wa kiume au wakike,au baba au mama au watoto au mashamba KWAAJILI YA JINA LANGU,atapokea mara mia zaidi na kuurithi uzima wa milele”
katika injili hiyo,Yesu anadhihirisha kwamba aliyeacha hayo yaliotajwa si kwasababu hawezi kuyapata la hasha,bali ameyaacha hayo yote KWAAJILI YA JINA LA YESU atapokea mengi hapa duniani halafu tena ataurithi ufalme wa mbinguni.
Mapadre wameyaacha hayo yote,wameacha nyumba,familia zao na kila kitu SIO KWASABABU HAWANA UWEZO AU HAWAWEZI KUPATA MAMBO HAYO bali WAMEACHA KWASABABU YA KUMTUMIKIA MUNGU KWA KADIRI YA MAANDIKO MATAKATIFU na kwakutaka kwao kuyaishi kimamilifu MASHAURI YA INJILI ikiwepo USEJA.
Maneno ya Paulo na yale ya Yesu mwenyewe kuhusu kumtumikia Mungu bila kuoa sio ya bahati mbaya bali ndiyo njia bora na inayofaa sana na kukubalika mbele ya Mungu.
Kwahiyo unapowaona mapadre hawaoi ujue sababu yake ni hiyo kwamba “Wamejitoa kwaajili ya kulihudumia kanisa”
(Na pia huwa nawashangaa mno watu wanaowapiga vita Mapadre kwamba kwanini hawaoi,najiuliza je,hao Mapadre wamewakataza wao kwamba wasioe?.)..na kama jibu ni hapana,sasa Je,”Pilipili ya shamba usiyoila inakuwashia nini?”
TUMSIFU YESU KRISTO!

Je, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha Kipaimara kama sakramenti ya neema ya Roho Mtakatifu?

Karibu kwenye makala hii ambayo itakupa ufahamu juu ya sakramenti ya kipaimara kwa mujibu wa imani ya Kanisa Katoliki. Kipaimara ni mojawapo ya sakramenti saba ambazo zinafundishwa na Kanisa Katoliki. Hii ni sakramenti ya neema ambayo inaunganisha mwamini na Roho Mtakatifu, na kufungua milango ya kumpokea Roho Mtakatifu kwa nguvu zake kamili.

Kuna mafundisho mengi ya Kipaimara, lakini moja kuu ni kwamba ni sakramenti inayohusika na kumpokea Roho Mtakatifu. Katika Matendo ya Mitume 8:14-17, tunaona jinsi Petro na Yohane walivyokwenda Samaria kutoa kipaimara kwa waamini ambao tayari walikuwa wamebatizwa. Tendo hilo linaonyesha kwamba kipaimara ni sakramenti inayotolewa baada ya ubatizo, na kwamba kwa kupokea kipaimara, mwamini anapokea Roho Mtakatifu.

Kwa mujibu wa Catechism of the Catholic Church, kipaimara ni "sakramenti ya neema ambayo inatufanya kuwa imara katika imani, na kutupatia nguvu za kuwa mashahidi wa Kristo" (CCC 1285). Hii inaonyesha kwamba kipaimara ni sakramenti inayotufanya tuwe imara katika imani na kutupatia nguvu za kuwa mashahidi wa Kristo. Ni sakramenti inayotufanya tuwe na ujasiri na nguvu za kushuhudia imani yetu kwa wengine.

Katika kipaimara, tunapokea Roho Mtakatifu, ambaye anatufanya tuwe na nguvu za kushinda majaribu na kujaribiwa. Roho Mtakatifu anatupa nguvu za kujitolea kwa ajili ya wengine, na kutupatia uwezo wa kutenda kazi kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Kwa njia hii, tunapata nguvu za kuishi kwa kadiri ya mapenzi ya Mungu, na kuishi kama wanafunzi wa Kristo.

Kwa hiyo, kipaimara ni sakramenti ya neema ambayo inafanya kazi ndani yetu kupitia Roho Mtakatifu. Ni sakramenti inayotufanya tuwe imara katika imani yetu, na kutupatia nguvu za kuwa mashahidi wa Kristo. Tunaalikwa tukumbuke kwamba tunapokea kipaimara kwa neema ya Mungu, na kwamba Roho Mtakatifu anatufanya tuwe watoto wa Mungu, wana wa Kanisa, na mashahidi wa Kristo. Naam, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha kipaimara kama sakramenti ya neema ya Roho Mtakatifu.

Mafundisho na mapokeo Katika Kanisa Katoliki yanapopatikana kwenye Biblia

Wakatoliki wengi huyumbishwa kwa kuambiwa huamini mambo ambayo hayako au ni kinyume na Biblia. Aya zifuatazo zitakusaidia wewe mkatoliki kuelewa au kujua mistari ya Biblia inayofafanua imani katoliki.
1) KUOMBEA MAREHEMU:
2 Mak. 12:38-46
Hek. 3:1
Tob 4:17
2) MATUMIZI YA SANAMU NA VISAKRAMENTI
2Fal 3:20-21
Hes. 21:8-9
Kut. 25:17-22
Kol. 1:20, 2:14
Yn. 12:32
Mt. 19:11-12
3) USAHIHI WA MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI KAMA CHANZO CHA IMANI
2 The 2:15
2 Kor. 10:10-11
Yn 21-25
2 Yoh. 1:12
3 Yoh. 1:13
4) KUABUDU JUMAPILI BADALA YA JUMAMOSI(SABATO)…. Hasa ni kwa sababu Yesu aliitukuza siku ya kwanza ya juma kwa ufufuko wake na kwa kuwatokea wanafunzi wake siku hiyo.
Ufu 1:10
Mdo 20:7
Mt 28:1-8
Lk. 24:1-7
Lk. 24:13ff
1 Kor. 16:1-2
Yn. 20:1-22
5) MAMLAKA YA PAPA KAMA MFUASI AU MRITHI WA MT. PETRO
Yn. 21:15-17
Mt 16:18-19
W 2:1-14
6) MAPADRI KUITWA BABA WAKATI BABA NI MMOJA ALIYEKO MBINGUNI
Mwa 17:4
Yer. 7:7
Hes. 12:14
Yn. 6:49
Mt 23:30
Lk. 1:73
7) JE BIBLIA INATAMBUA MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA?
Efe. 4:11-13
1Tim 5:17-25
1Tim 3:1-7,8-18
8) JE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU TOHARANI.
Isa 35:8, 52:1
Zek 13:1-2
1Kor 3:15
Lk 12:47-48, 58-59
Ufu 21:27
Ebr 12:22-23
Ayu 14:13-17
9) KUHUSU MATUMIZI YA UBANI
Kut 30:34-37
Hes 16:6-7
Law 16:12-13
Lk 1:10
Ufu 8:32
10) ROZARI IKO KATIKA BIBLIA?
Lk 1:28
Lk 1:42
11) JE KUTUMIA MAJI YA BARAKA NI MAPENZI YA MUNGU?
2Fal 2:19-22
Yn 5:1-18
Yn 7:37
Hes 19:1-22
12) KWANINI TUNAOMBA WATAKATIFU WATUOMBEE?
Mit 15:8, 15:29
Ayu 42:8
Yak 5:16
Mt 16:19
13)KWANINI TUNATUMIA MEDALI, MISALABA, SCAPURALI NA MIFUPA YA WATAKATIFU?
2Fal 13:20-21
14) KWANINI TUNAUNGAMA DHAMBI ZETU KWA PADRI
Mt 16:19,1-20
Yak 5:15-16
15) UBATIZO WA WATOTO WACHANGA UKO KATIKA BIBLIA
Mdo 16:15-33
Mdo 18:8
Mt 28:19
Mdo 10:47-48
16) KUSIMIKWA KWA UTUME
Kut 28:4-43
17) RANGI ZA KANISA
Kut 27:9-29
18) MATUMIZI YA MISHUMAA
Kut 25:31-40; 27:20-21
Hes 8:1-4
19) MPAKO WA MAFUTA YA KRISMA
Kut 30:22-32
20) MPAKO WA MAFUTA YA WAGONJWA
Yak 5:14-15

Huruma ya Mungu: Chemchemi ya Upendo Usiokwisha

Huruma ya Mungu: Chemchemi ya Upendo Usiokwisha

  1. Kama Mkristo Katoliki, tunajua kwamba huruma ya Mungu ni jambo muhimu sana katika imani yetu. Huruma hii si tu inatufundisha upendo usiokwisha wa Mungu kwetu, lakini pia inatufundisha jinsi ya kushiriki upendo huu kwa wengine.

  2. Kwa maana hiyo, Huruma ya Mungu ni chemchemi ya upendo usiokwisha. Tunajifunza kupitia huruma hii jinsi ya kuwajali na kuwasaidia wale wanaotuzunguka, kama vile watu maskini, wakimbizi, watoto yatima, na wengineo.

  3. Katika Kitabu cha Zaburi 136:1-3, tunaona maneno haya yaliyoandikwa: "Msifuni Bwana kwa kuwa ni mwema, Maana fadhili zake ni za milele. Msifuni Mungu mkuu wa miungu, Maana fadhili zake ni za milele. Msifuni Bwana wa mabwana, Maana fadhili zake ni za milele." Hili ni kielelezo cha huruma ya Mungu kwetu.

  4. Kwa kuwa sisi ni watoto wa Mungu, tunapaswa pia kuwa na huruma kwa wenzetu. Kwa mfano, katika Injili ya Mathayo 25:35-36, Yesu anasema, "Nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaniandalia kinywaji, nilikuwa mgeni mkanipokea, nilikuwa uchi mkaniwafunika, nilikuwa mgonjwa mkanitembelea, nilikuwa gerezani mkanijia."

  5. Kwa hiyo, tunapokuwa na huruma kwa wengine, tunamfanya Yesu kuwepo katikati yetu. Kama tunavyoona katika Kitabu cha Yohana 13:34-35, Yesu anasema, "Amri mpya nawapa: Pendaneni. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Kwa hili watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, kama mtakavyo kuwa na upendo kati yenu."

  6. Kwa hiyo, upendo na huruma ni sehemu muhimu sana ya kuwa Mkristo. Tunapaswa kuwa watu wa huruma na wema, kama vile Mungu ni mwenye huruma na wema kwetu. Hii inapatikana katika Catechism of the Catholic Church, kifungu 2447: "Kati ya maagizo ya Mungu, ya kwanza ni upendo kwa Mungu na kwa jirani, kwa sababu inatoka kwa upendo unaobubujika kutoka kwa Mungu."

  7. Kwa hiyo, tunapaswa kuishi maisha ya huruma, kama vile Mtakatifu Maria Faustina Kowalska alivyokuwa. Katika kitabu chake, Diary of Saint Maria Faustina Kowalska, anaelezea jinsi Mungu alivyomfunulia huruma yake kwa njia ya Yesu Kristo, na jinsi alivyopaswa kuwa na huruma kwa wengine. Kwa hiyo, kama wakristo tunapaswa kujifunza na kuishi kulingana na mfano huu.

  8. Tunapaswa kuwa watu wa huruma sio tu kwa wale tunaowajua, lakini pia kwa wale ambao hatuwajui. Kama ilivyoelezwa katika Kitabu cha Luka 10:29-37, Yesu anaelezea mfano wa Mtu Mwema, ambaye alimwonea huruma mtu aliyepigwa na kujeruhiwa barabarani. Tunapaswa kuwa kama Mtu huyu mwema, kuwa na huruma kwa kila mtu tunayekutana naye katika maisha yetu.

  9. Kwa hiyo, tunapaswa kuonyesha huruma kwa wengine kwa njia nyingi, kama vile kutoa msaada wa kifedha na kimwili, kutoa ushauri na faraja, na kwa kusali kwa ajili yao. Katika 1 Wakorintho 13:13, tunajifunza jinsi upendo na huruma ni muhimu sana katika maisha yetu ya kikristo: "Basi sasa, imani, tumaini, na upendo, haya matatu; lakini lililo kuu kati ya hayo ni upendo."

  10. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa wakristo wa huruma na upendo, kama vile Mungu mwenyewe alivyo na huruma na upendo kwetu. Tunapaswa kuishi kulingana na mfano wa Kristo, ambaye alikuwa na huruma kwa watu wote, na kuwasaidia kwa njia nyingi. Kwa hiyo, tunapaswa kuwafanyia wengine vile vile, kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee ya kuonesha upendo na huruma ya Mungu kwetu.

Swali: Je, wewe unafikiri unaweza kuishi kulingana na mfano wa Kristo katika maisha yako ya kila siku? Na ikiwa ndivyo, unafikiri utafaidika vipi na huruma na upendo wa Mungu?

Je Bikira Maria Alizaa Watoto Wengine?

Mapokeo kuhusu Bikira Maria yanaonyesha alikuwa binti pekee wa wazee watakatifu Yohakimu na Ana. Vilevile
Mt. Yosefu, ingawa kisheria alikuwa mume wake, hakutenda naye tendo la ndoa hata moja. Ndiyo maana kwenye
litania yake tunamuita mwenye usafi kamili. Yosefu likufa kabla Yesu hajaanza utume kwa kubatizwa kwenye mto
Yordani. Sisi tunasadiki Maria ni “Bikira daima”.
Ndugu wa Yesu wanaosemwa katika Injili ni kina nani?
Wanaosemwa katika Injili “ndugu zake Yesu” si watoto
wa Bikira Maria wala Yosefu mtakatifu, bali ndugu wa kiukoo waliokuwa jirani sana na familia hiyo takatifu. Kama
Bikira Maria angekuwa na watoto wengine, je, Yesu Bwana wetu asingekuwa amefanya kosa la kiudugu
kuwanyang’anya Mama yao na kumfanya awe Mama wa mtume Yohane alipomkabidhi msalabani, “‘Mwana, tazama
Mama yako’. Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake” (Yoh 19:27).
Katika Agano Jipya yupo Yakobo anayeitwa na mtume Paulo “ndugu yake Bwana” (Gal 1:19): Yakobo huyo
alikuwa maarufu katika Kanisa la Yerusalemu (Mdo 12:7; 15:13-21; 21:18-20; Gal 2:9). Yakobo huyo si mtume
Yakobo mwana wa Alfayo, wala mtume Yakobo kaka yake Yohane (Lk 6:12-16), bali ni Yakobo ndugu yake Yose na
mama yao kwenye Injili anaitwa “Maria mwingine”, si Maria Mama wa Yesu. “Walikuwepo pia wanawake
waliotazama kwa mbali. Miongoni mwao akiwa Maria Magdalena, Salome na Maria mama wa akina Yakobo mdogo
na Yose” (Mk 15:40). Maria lilikuwa jina la kawaida kwa Wayahudi: akina Maria wakiwa wengi hivyo, tujue
kuwatofautisha kwenye Injili. Bikira Maria Injili zinamtaja kama “Mama wa Yesu”.

Je, Bikira Maria ni Bikira Daima au alizaa watoto wengine?

Jibu fupi ni kwamba Bikira Maria hakuzaa watoto wengine na hakuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu
Hapo zamani hakuna mkristu au dehebu lolote lililokuwa linapinga kuwa Bikira Maria sio Bikira Daima hata Waprotestanti/walokole waliamini Bikira Maria ni Bikira Hata Baada ya Kumzaa Yesu. Kwenye Miaka ya 1400-1600 Watu wote wakwanza waliopinga Kanisa Katoliki walikubali kuwa Bikira Maria ni Bikira daima wakiwemo Martin Lutha aliyeanzisha kanisa la Lutheran, John Calvin aliyeanzisha Ulokole/Protestanti, Mchungaji Ulrich Zwingli, Heinrich Bullinger, and Thomas Cranmer. Kwa miaka zaidi ya 350 Waprotestant/walokole waliendelea kuamini kuwa Bikira Maria ni Bikira Daima.
Lakini baadae wakristo wengi walianza kupinga kuwa Bikira Maria ni Bikira Daima.

Tunaweza kuthibitisha kuwa Bikira Maria hakuzaa watoto wengine kwa kunukuu Biblia Kama ifuatavyo;

1. Bikira Maria Alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu

Biblia inatuambia wazi kwamba Bikira Maria alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu Kama tunavyosoma katika Luka 1:26-35
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, 27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. 28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.” 29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini? 30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. 31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu. 32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake. 33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” 34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?” 35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu. (Luka 1:26-35)

2. Biblia Haiwataji ndugu wa Yesu wakati Yosefu na Maria walipokimbilia Misri kumficha Yesu na wakati waliporudi

19 Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri, 20 akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa.” 21 Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli. 22 Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya, 23 akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa Mnazare.” Matayo 2:19-23
Kama wangekuwepo wadogo zake Yesu Biblia ingetuambia kwamba walikuwa wapi wakati huo na walikuwa na Yesu au la.

3. Biblia haituambii kuwa Yesu alikua na wadogo zake alipokuwa na miaka 12

Wakati wa Maria, Yoseph na Yesu walipoenda Yerusalemu Yesu akiwa na miaka 12 Biblia haituambii kuwa Yesu alikuwa na wadogo zake na walikuwa wapi. Kumbuka walikuwa na Desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka kwa ajili ya Pasaka familia nzima kama familia. Je hao watoto wengine walikuwa wapi. Kwa nini walikuwa na Yesu Mwenyewe? Maana yake ni kwamba Yesu hakuwa na Wadogo zake.
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka. 42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi. 43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari. 44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki. 45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta. 46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima. 48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.” 49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?” 50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia. 51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake. 52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu. (Luka 2:41-52).
Kwa hiyo Biblia haionyeshi kuwa Yesu alikuwa na kaka na dada wakati akiwa na miaka 12. Kama wangekuwepo wangetajwa hapa kuwa walikuwa pamoja na Wazazi wao kama Yesu au walikuwa na Yesu wakati anapotea. Biblia haituambii chochote kwa hiyo wakati huo hapakuwa na wadogo zake Yesu.

4. Kukosekana kwa neneo “Binamu” kwenye lugha ya Yesu

Wakristu wa kwanza pamoja na Yesu aliongea Kiaramaiki au Kiebrania. Katika lugha zote hizo hakuna neno “Binamu” kwa hiyo mabinamu walijulikana kama dada na kaka wa mtu. Kwenye Agano jipya Neno kaka na Dada lilitumika pia kuwakilisha binamu.
Biblia inapotuambia kuwa Kaka na dada zake Yesu haimaanishi kaka wa kuzaliwa bali ndugu au Binamu
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?” (Mathayo 13:55-56)
Kwa hiyo wanaotajwa hapa ni ndugu wa Yesu kwa maana maneno kama; ndugu, kaka au dada lilitumika badala ya Binamu yaani mtoto wa shangazi au mjomba. Hapa juu Yosefu ametajwa kama kaka yake Yesu lakini tunajua kuwa Yosefu ni Baba yake Yesu. Baba na mwana hawawezi kuwa na jina sawa.

5. Biblia haitumii neno Ndugu, kaka au dada ikimaanisha ndugu wa kuzaliwa mama mmoja na baba mmoja

Sio mara zote Biblia imetumia neno Ndugu kumaanisha ndugu (Dada na Kaka) wa kuzaliwa yaani kaka na dada kwa mfano
Kwa kuangalia lugha ya Kiswahili na Kiingereza 1 Wakorintho 15:6 tunaona tafsiri tofauti.
KISWAHILI 6 Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
ENGLISH 6 After that, he appeared to more than five hundred of the brothers and sisters at the same time, most of whom are still living, though some have fallen asleep.
Kwa hiyo hapa neno kaka dada na ndugu linaonekana wazi halikumaanisha ndugu au kaka wa damu.

6. Undugu wa Yakobo, Simoni, Yosefu na Yuda kwa Yesu Sio wa mtu na kaka zake

Wasemao kuwa Bikira maria alikuwa na wana zaidi ya Yesu wananukuu kifungu hiki;
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?” (Mathayo 13:55-56)
Kumbuka kulikuwa na Yakobo wawili wakati wa Yesu, Vifungu vifuatavyo yunaweza kuona kuwa kulikuwa na yakobo wawili ambao walikuwa ndugu za Yesu lakini sio kaka wa kuzaliwa kwa mama.
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.” (Marko 10:35)
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56)
Tunaweza kuona Undugu huu na Yesu kwa kusoma;
19 Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana. (Wagalatia 1:19)
Lakini Yuda anasema;
1 Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo. (Yuda 1:1)
Kwa hiyo Yakobo na Yohane walikuwa watoto wa Mama mwingine ambao baba yao ni Zebedayo. Na Yakobo na Yosefu walikuwa watoto wa Maria Mwingine. Kwa hiyo ni Yakobo wa wili wa Mama wengine Tofauti na Maria. Yuda alikuwa ni ndugu yake Yakobo. Yakobo vilevile alikuwa ndugu yake Yesu.
Kuthibitisha kuwa Hawa kina Mama ndio waliokuwa Mama zao kina Yakobo wote hao wawili na wengine tunaweza kusoma;
25 Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene. (Yohana 19:25)
Kwa hiyo kwenye (Yohana 19:25) tunaona Kuwa ni kwenye Msalaba wa Yesu alikuwepo Mama yake Yesu (Bikira Maria), Dada yake Bikira Maria, Mke wa Cleopa na Maria Magdalena. Na kwenye (Matayo 27:55-56) wamwtajwa ni Mama za kina nani kama inavyoonekana kwenye kifungu kifuatachi;.
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56).
Kwa hiyo hii ina maanisha kulikua na wanawake watatu wenye majina sawa ya Maria waliokuwa chini ya Msalaba. Yakobo na Yuda walikuwa watoto wa Maria Mke wa Cleofasi, na sio Mama wa Yesu, na hivyo sio kaka za Yesu.

7. Yesu alimwacha Mama yake kwa Yohane kwa kuwa hakuwa na Kaka na dada wakumwachia mamaye

26 Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake: “Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao.” 27 Halafu akamwambia yule mwanafunzi: “Tazama, huyo ndiye mama yako.” Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake.
Ndiyo maana Bikira Maria tangu siku ile alihamia kwa Yohani kwa kuwa hakuwa na watoto wengine.

Huruma ya Mungu: Faraja na Ufariji katika Majaribu

Huruma ya Mungu: Faraja na Ufariji katika Majaribu

Huruma ya Mungu ni zawadi kubwa kutoka kwake kwa sisi wanadamu. Mara nyingi tunapokuwa katika majaribu, tunahitaji faraja na ufariji. Kwa nini unahitaji kumtegemea Mungu katika kila hali? Tunajua kwamba kuna mambo mengi ambayo tunayaweza kwa uwezo wetu, lakini kuna wakati ambapo tunahitaji msaada wa Mungu.

  1. Mungu yuko karibu na sisi katika kila hali

Kama vile mtoto anavyohitaji upendo na msaada wa mzazi, hivyo ndivyo tunavyohitaji upendo na msaada wa Mungu katika hali zetu ngumu. Kama ilivyoelezwa katika kitabu cha Zaburi 46:1, "Mungu ndiye kimbilio letu na nguvu yetu, msaada unaopatikana wakati wa dhiki."

  1. Huruma ya Mungu ni kubwa kuliko dhambi zetu

Mungu hutupenda sana hata kama tunafanya makosa na kukosea. Kama ilivyoelezwa katika Warumi 5:8, "Lakini Mungu huonyesha upendo wake kwetu kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu tulipokuwa tungali wenye dhambi." Kwa hiyo, hatupaswi kuhisi hatia sana tunapofanya makosa, bali tunapaswa kumgeukia Mungu kwa toba na kumwomba msamaha.

  1. Tunapaswa kumtegemea Mungu katika kila hali

Mungu hupenda sana kuwa karibu nasi na kutusaidia katika kila hali. Kama ilivyoelezwa katika Wafilipi 4:6-7, "Msijisumbue kwa lolote; badala yake, katika kila hali, kwa kuomba na kuomba omba, pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yawasilishwe kwa Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawalinde mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu."

  1. Mungu hutusaidia kwa njia zake za ajabu

Mungu hufanya miujiza na hutusaidia kwa njia ambazo hatutarajii. Kama ilivyoelezwa katika Yeremia 32:27, "Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa kila mwili; je, mambo yoyote ni magumu sana kwangu?" Kwa hiyo, tunapaswa kuwa na imani kwamba Mungu atatusaidia katika njia ambazo hatutarajii.

  1. Tunahitaji kumtegemea Mungu kabla ya kila jambo

Mungu anataka tuwe na uhusiano mzuri naye na atusaidie katika kila jambo tunalofanya. Kama ilivyoelezwa katika Methali 3:5-6, "Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zako zote mkiri yeye, naye ataelekeza mapito yako."

  1. Mungu hutuongoza katika njia sahihi

Mungu anataka tuwe na maisha bora na yenye furaha. Kama ilivyoelezwa katika Zaburi 16:11, "Umenijulisha njia ya uzima; furaha kamili iko mbele za uso wako; raha za milele ziko mkononi mwako." Kwa hiyo, tunapaswa kumfuata Mungu na kumwomba atuongoze katika njia sahihi.

  1. Mungu anatupenda hata katika dhiki

Mungu hutupenda hata katika wakati wa dhiki na majaribu. Kama ilivyoelezwa katika Warumi 8:35, "Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?" Kwa hiyo, tunapaswa kumtegemea Mungu hata katika wakati mgumu.

  1. Mungu hutuponya na kutuponyesha

Mungu ni mponyaji wetu na hutusaidia katika afya zetu. Kama ilivyoelezwa katika Zaburi 103:2-3, "Msifie Bwana, nafsi yangu, wala usisahau fadhili zake zote. Yeye ndiye anayesamehe maovu yako yote, naye ndiye anayeponya magonjwa yako yote." Kwa hiyo, tunapaswa kumwomba Mungu atusaidie katika afya zetu na kutuponya.

  1. Mungu anataka tuwe na amani katika mioyo yetu

Mungu anataka tuwe na amani katika mioyo yetu. Kama ilivyoelezwa katika Yohana 14:27, "Amani yangu nawapa; nawaachia amani yangu. Mimi sipi kama ulimwengu upeavyo. Msiwe na wasiwasi wala msifadhaike." Kwa hiyo, tunapaswa kumwomba Mungu atupe amani katika mioyo yetu na kutusaidia kuishi kwa amani na furaha.

  1. Mungu hutupenda sana

Mungu hutupenda sana na anataka tuwe karibu naye. Kama ilivyoelezwa katika Yohana 3:16, "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele." Kwa hiyo, tunapaswa kumwomba Mungu atusaidie kuwa karibu naye na kutusaidia katika kila jambo tunalofanya.

Kwa hiyo, tunapaswa kumtegemea Mungu katika kila hali na kumwomba atusaidie katika majaribu. Kwa kuwa Mungu hutupenda sana, tunaweza kuwa na uhakika kwamba atatusaidia na kutupa amani katika mioyo yetu. Tunapaswa pia kuwa na imani kwamba Mungu atatuponya na kutuponyesha. Kwa hiyo, tunapaswa kumwomba Mungu atutegemeze katika kila jambo tunalofanya. Je, unafikiri nini kuhusu huruma ya Mungu? Jisikie huru kutoa maoni yako.

Ibada ya Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Upendo na Ukarimu

Ibada ya Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Upendo na Ukarimu

Karibu kwa maelezo ya Ibada ya Huruma ya Mungu. Ibada hii ni sehemu muhimu ya maombi katika Kanisa Katoliki kama ilivyofundishwa na Kanisa. Ibada hii inatufundisha jinsi ya kuishi kwa upendo na ukarimu, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha.

  1. Kuanza Ibada ya Huruma ya Mungu kila siku

Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, Ibada ya Huruma ya Mungu ni muhimu kwa ajili ya maisha ya Kikristo. Kwa hivyo, unapaswa kuianza kila siku kwa kusali chaplet ya Huruma ya Mungu. (CCC 1419). Kusali chaplet hii kunaweza kutufungulia mioyo yetu kwa upendo wa Mungu.

  1. Kusamehe na kuwa tayari kusamehe

Hakuna mtu ambaye hajawahi kufanya makosa. Ni kwa kuwasamehe wengine ndipo tunaweza pia kusamehewa (Matthew 6:14-15). Hiyo ni kwa sababu, Bwana wetu Yesu Kristo alitufundisha kwamba kusamehe ni sehemu muhimu ya upendo na ukarimu.

  1. Kutenda wema na kutoa sadaka

Ibada ya Huruma ya Mungu inatufundisha pia jinsi ya kutenda wema na kutoa sadaka kwa wengine. (CCC 2447). Tunaweza kufanya hivyo kwa kufanya kazi za upendo, kutoa msaada na kuwa tayari kutoa mali zetu ili kusaidia wengine katika shida zao.

  1. Kumuomba Mungu kwa unyenyekevu

Tunapomwomba Mungu kwa unyenyekevu, tunafungua mioyo yetu kwa upendo na huruma yake. (CCC 2559). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kuomba huruma na kumwomba Mungu atusaidie kuishi kwa upendo na ukarimu.

  1. Kuwa na imani

Ibada ya Huruma ya Mungu inatufundisha pia jinsi ya kuwa na imani. Tunahitaji kumwamini Mungu na ahadi zake. Kwa kufanya hivyo, tunakuwa na uhakika kwamba Mungu atatupatia kila kitu tunachohitaji ili kuishi kwa upendo na ukarimu. (CCC 156).

  1. Kuwa tayari kuomba msamaha

Tunapojitokeza mbele ya Mungu kwa unyenyekevu na kuomba msamaha kwa mapungufu yetu, tunamruhusu Mungu kuingia ndani ya maisha yetu na kujaza nafasi zetu za udhaifu na upungufu. (CCC 2631). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kuomba msamaha kila wakati tunapojikuta tumeanguka au kutenda makosa.

  1. Kutafakari juu ya huruma ya Mungu

Kutafakari juu ya Huruma ya Mungu kunaweza kutusaidia kukua katika upendo na ukarimu. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kufahamu zaidi jinsi Mungu anatupenda na anatujali. (CCC 2708). Tunaweza kutafakari juu ya Huruma ya Mungu kwa kusoma Injili, kusoma vitabu vya maombezi au hata kusoma Kitabu cha Maisha ya Mtakatifu Faustina Kowalska.

  1. Kujifunza kutoka kwa watakatifu

Watakatifu ni mfano wa kuigwa katika maisha yetu ya Kikristo, na wanaweza kutusaidia kukua katika upendo na ukarimu. (CCC 2683). Kwa hiyo, tunapaswa kujifunza kutoka kwa watakatifu kwa kusoma maisha yao na kufuata mifano yao.

  1. Kuwa na moyo wa shukrani

Kuwa na moyo wa shukrani ni muhimu katika maisha ya Kikristo. Tunapomshukuru Mungu kwa yote anayotufanyia, tunaujaza moyo wetu na upendo na ukarimu. (CCC 2648). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kumshukuru Mungu kwa yote, iwe ni kubwa au ndogo.

  1. Kuishi kwa upendo

Kuishi kwa upendo ni muhimu katika maisha ya Kikristo. Kama ilivyofundishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, upendo ni amri kuu ya Kanisa. (John 13:34-35). Kwa hivyo, tunapaswa kuishi kwa upendo kwa kila mtu, iwe ni mtu wa familia yetu, jirani, au mtu yeyote tunayekutana nae.

Ibada ya Huruma ya Mungu ni sehemu muhimu ya maisha yetu ya Kikristo. Inatufundisha jinsi ya kuishi kwa upendo na ukarimu, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha. Je, umepata nafasi ya kusali Ibada ya Huruma ya Mungu leo? Je, unaishi kwa upendo na ukarimu katika maisha yako ya Kikristo?

Majivuno na Kujikweza Mbele ya Mungu

Rejea Luka 14:7-24 na Luka 18 :9-18
Mungu anakawaida ya kumkweza yoyote ajishushaye na kumshusha yule ajikwezaye. Vile unavyojiona bora mbele ya Mungu na mbele ya watu ndivyo na Mungu anatakavyokuonyesha kuwa wewe sio bora au wewe sio zaidi ya wengine.

Madhara ya Kujikweza au majivuno

1. Sala zako hazitajibiwa kwa kuwa mara zote nia ya sala zako zitakua ni za kujitakia makuu.
2. Kusahau nafasi ya Mungu katika maisha yako na kuhisi unajitosheleza kwa yote.
3.Kusahau nafasi na umuhimu wa wengine kwa kuhisi kuwa hawana thamani kama wewe.

Dalili za Kujikweza au majivuno

1.Kutaka au kupenda kuwa na nafasi ya kwanza kwenye kila kitu.
2. Kukosa uvumilivu
3. Kuwa na hofu ya kushindwa na kufedheheshwa
4.Kukosa upendo na kujali kwa wengine
5. Kupungua imani kwa Mungu. Yani kuhisi kama Mungu anaweza kufanya au hawezi.
6. Kupungua ukaribu wako kwa Mungu.
7.Kutokupenda kusali /kuomba Mungu.

Dawa ya majivuno au jinsi ya kujishusha

1.Kujifunza unyenyekevu.
2.Kujifunza upendo wa kweli kwa Mungu na wengine.
3. Jifunze kuwaombea wengine. Hii itasaidia kujenga unyenyekevu.
4. Kujifunza kuridhika
5. Jifunze kufurahia mafanikio ya wengine.
6. Usiwe muongeaji sana na mchunguzi wa mambo ya watu sana.

JE IMANI AU MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI YANAPATIKANA KATIKA BIBLIA?

Wakatoliki wengi huyumbishwa kwa kuambiwa huamini mambo ambayo hayako au ni kinyume na Biblia. Aya zifuatazo zitakusaidia wewe mkatoliki kuelewa au kujua mistari ya Biblia inayofafanua imani katoliki.
1) KUOMBEA MAREHEMU:
2 Mak. 12:38-46
Hek. 3:1
Tob 4:17
2) MATUMIZI YA SANAMU NA VISAKRAMENTI
2Fal 3:20-21
Hes. 21:8-9
Kut. 25:17-22
Kol. 1:20, 2:14
Yn. 12:32
Mt. 19:11-12
3) USAHIHI WA MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI KAMA CHANZO CHA IMANI
2 The 2:15
2 Kor. 10:10-11
Yn 21-25
2 Yoh. 1:12
3 Yoh. 1:13
4) KUABUDU JUMAPILI BADALA YA JUMAMOSI(SABATO)…. Hasa ni kwa sababu Yesu aliitukuza siku ya kwanza ya juma kwa ufufuko wake na kwa kuwatokea wanafunzi wake siku hiyo.
Ufu 1:10
Mdo 20:7
Mt 28:1-8
Lk. 24:1-7
Lk. 24:13ff
1 Kor. 16:1-2
Yn. 20:1-22
5) MAMLAKA YA PAPA KAMA MFUASI AU MRITHI WA MT. PETRO
Yn. 21:15-17
Mt 16:18-19
W 2:1-14
6) MAPADRI KUITWA BABA WAKATI BABA NI MMOJA ALIYEKO MBINGUNI
Mwa 17:4
Yer. 7:7
Hes. 12:14
Yn. 6:49
Mt 23:30
Lk. 1:73
7) JE BIBLIA INATAMBUA MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA?
Efe. 4:11-13
1Tim 5:17-25
1Tim 3:1-7,8-18
8) JE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU TOHARANI.
Isa 35:8, 52:1
Zek 13:1-2
1Kor 3:15
Lk 12:47-48, 58-59
Ufu 21:27
Ebr 12:22-23
Ayu 14:13-17
9) KUHUSU MATUMIZI YA UBANI
Kut 30:34-37
Hes 16:6-7
Law 16:12-13
Lk 1:10
Ufu 8:32
10) ROZARI IKO KATIKA BIBLIA?
Lk 1:28
Lk 1:42
11) JE KUTUMIA MAJI YA BARAKA NI MAPENZI YA MUNGU?
2Fal 2:19-22
Yn 5:1-18
Yn 7:37
Hes 19:1-22
12) KWANINI TUNAOMBA WATAKATIFU WATUOMBEE?
Mit 15:8, 15:29
Ayu 42:8
Yak 5:16
Mt 16:19
13)KWANINI TUNATUMIA MEDALI, MISALABA, SCAPURALI NA MIFUPA YA WATAKATIFU?
2Fal 13:20-21
14) KWANINI TUNAUNGAMA DHAMBI ZETU KWA PADRI
Mt 16:19,1-20
Yak 5:15-16
15) UBATIZO WA WATOTO WACHANGA UKO KATIKA BIBLIA
Mdo 16:15-33
Mdo 18:8
Mt 28:19
Mdo 10:47-48
16) KUSIMIKWA KWA UTUME
Kut 28:4-43
17) RANGI ZA KANISA
Kut 27:9-29
18) MATUMIZI YA MISHUMAA
Kut 25:31-40; 27:20-21
Hes 8:1-4
19) MPAKO WA MAFUTA YA KRISMA
Kut 30:22-32
20) MPAKO WA MAFUTA YA WAGONJWA
Yak 5:14-15

Kukimbilia Huruma ya Mungu: Nguvu katika Majaribu

Kukimbilia Huruma ya Mungu: Nguvu katika Majaribu

Mara nyingi tunapitia majaribu katika maisha yetu na mara nyingine inaonekana kama hakuna njia ya kuepukana navyo. Hata hivyo, kuna msaada unaopatikana kutoka kwa Mungu ambao unaweza kutusaidia kupita majaribu haya. Kukimbilia huruma ya Mungu ni njia nzuri ya kupata nguvu ya kuvumilia majaribu.

  1. Tafuta Msaada wa Mungu

Kukimbilia Huruma ya Mungu ni njia ya kuomba msaada wa Mungu. Tunahitaji kumwomba Mungu atusaidie kupitia majaribu yetu. Kwa kufanya hivyo, tunafungua mioyo yetu kwa nguvu za Mungu ambazo zinaweza kutusaidia kupambana na majaribu.

“Ndiyo, nimekukimbilia wewe, Ee Bwana; nisiaibike milele.” Zaburi 31:1

  1. Utulivu katika Moyo

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatuletea utulivu wa moyo. Tunapokabiliana na majaribu, tunahitaji kubaki watulivu katika moyo wetu. Mungu anatupa amani ambayo inatulinda na hofu na wasiwasi.

“Pindi ile amani ya Mungu, inayopita akili yote, itakayolinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu” Wafilipi 4:7

  1. Kupata Faraja

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatuletea faraja. Mungu anatupatia faraja ambayo inaweza kuondoa maumivu ya moyo wetu. Faraja hii inatokana na upendo wa Mungu kwetu.

“Naye Mungu wa faraja yote, atawafariji ninyi katika dhiki yenu yote” 2 Wakorintho 1:4

  1. Upendo wa Mungu

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya tuelewe upendo wa Mungu kwetu. Tunapojua upendo wa Mungu kwetu, tunaweza kupata nguvu ya kupitia majaribu yetu.

“Kwa sababu Mungu aliupenda ulimwengu hivi, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” Yohana 3:16

  1. Ujasiri

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya tuwe na ujasiri. Tunapojua kwamba Mungu yuko pamoja nasi, tunapata ujasiri wa kutembea kwa imani hata katikati ya majaribu.

“Je, si mimi ndiye ninayekuamuru? Jitie moyo, na uwe hodari; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe, popote utakapokwenda.” Yoshua 1:9

  1. Kutafakari Neno la Mungu

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya kutafakari neno la Mungu. Tunapojifunza neno la Mungu na kulitafakari, tunapata nguvu ya kupitia majaribu yetu.

“Tena maneno haya ninayowaamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe utayafundisha watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo nyumbani mwako, na utembeapo njiani, ukilala, na kuamka.” Kumbukumbu la Torati 6:6-7

  1. Kuomba

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya kuomba. Kuomba ni njia ya kuwasiliana na Mungu na kumwomba msaada wake. Tunapokuwa na majaribu, tunahitaji kuomba ili tupate nguvu ya kupitia majaribu yetu.

“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.” Mathayo 7:7

  1. Kuwa na Imani

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya tuwe na imani. Imani yetu katika Mungu inatufanya tujue kwamba yeye yuko pamoja nasi wakati wote, hata katika majaribu yetu.

“Kwa maana mimi ni hakika ya kwamba wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye nguvu, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine chochote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.” Warumi 8:38-39

  1. Kupata Msamaha

Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya tupate msamaha wa dhambi zetu. Tunapopitia majaribu, mara nyingi tunakuwa na dhambi. Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya tupate msamaha wa dhambi zetu na kuwa safi mbele za Mungu.

“Mimi, naam, mimi, ndimi nitakayemsamehe dhambi zake, wala sitakumbuka tena maovu yake.” Isaya 43:25

  1. Kupata Maisha ya Milele

Hatimaye, Kukimbilia Huruma ya Mungu inatufanya tupate uzima wa milele. Tunapata nguvu ya kupitia majaribu yetu kwa imani ya kuwa tuna uzima wa milele.

“Maana kila mtu aaminiye katika yeye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” Yohana 3:16

Hitimisho

Kukimbilia Huruma ya Mungu ni njia nzuri ya kupata nguvu ya kupitia majaribu yetu. Tunapokimbilia huruma ya Mungu, tunapata faraja, upendo, na imani ambayo inatufanya tupate nguvu ya kuvumilia. Hivyo basi, tukumbuke kwamba Mungu yuko pamoja nasi wakati wote na anatupatia nguvu ya kupitia majaribu yetu. Kwa hiyo, tuendelee kumwomba Mungu na kumkimbilia huruma yake daima.

Je, unadhani Kukimbilia Huruma ya Mungu ni njia nzuri ya kupata nguvu ya kupitia majaribu yetu? Nipe maoni yako.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu matakwa ya Mungu na mapenzi ya binadamu?

Kanisa Katoliki linatambua kuwa Mungu aliumba ulimwengu na binadamu kwa mapenzi yake, lakini pia Mungu alitupa uhuru wa kuchagua. Ni wajibu wa binadamu kutimiza matakwa ya Mungu na kuishi maisha yanayoambatana na mapenzi yake.

Katika Waraka wa Yohane Paulo II, Fides et Ratio, Kanisa Katoliki linatilia mkazo kwamba binadamu ana jukumu la kutafuta ukweli na kuelewa mapenzi ya Mungu. Kupitia kwa imani na akili, binadamu anaweza kufikia maarifa ya ukweli huu.

Katika Maandiko Matakatifu, tunaona jinsi ambavyo Mungu anatutaka kufuata mapenzi yake. Mtume Paulo aliandika katika Waraka wa Waebrania 10:36, "Kwa hiyo, ninyi mnahitaji subira ili mtimize mapenzi ya Mungu na mpokee ahadi yake." Hii inamaanisha kuwa kwa kumtii Mungu na kufuata mapenzi yake, tunaweza kufikia ahadi zake.

Kanisa Katoliki linamfundisha mtu anapaswa kumtii Mungu na kusubiri mapenzi yake. Hii inamaanisha kuwa tunapaswa kufuata amri za Mungu na kuishi maisha yenye haki na kwa upendo. Katika KKK 2822, inasemekana, "Tunatafuta mapenzi ya Mungu katika maisha yote, hasa katika maamuzi yetu muhimu."

Katika Maandiko Matakatifu, tunajifunza kwamba Mungu anataka tufanye kazi yetu kwa bidii na kwa upendo. Paulo aliandika katika Waraka wa Wakolosai 3:23-24, "Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wenu wote, kama kwa Bwana, si kwa ajili ya wanadamu, kwa maana mnajua ya kuwa mtapokea ujira wa mrithi kutoka kwa Bwana."

Kanisa Katoliki linatilia mkazo kwamba inatupasa kufanya kazi kwa heshima na kwa uaminifu, kwa kuwa kwa kufanya hivyo tunamfurahisha Mungu. Kanuni ya Maadili ya Kikatoliki inatufundisha kuwa tunapaswa kutoa kazi yetu kwa Mungu na kuifanya kwa uangalifu na upendo, ili kuonyesha upendo wetu kwa Mungu.

Kwa hiyo, Kanisa Katoliki linatambua kwamba tunapaswa kutimiza matakwa ya Mungu na kuishi maisha yanayoambatana na mapenzi yake. Tunapaswa kumtii Mungu, kufanya kazi yetu kwa bidii na kwa upendo, na kutafuta ukweli na maarifa ya mapenzi yake. Kwa kufanya hivyo, tunapata baraka za Mungu na kupokea ujira wake wa milele.

Maana ya Zaka, Sababu za Kutoa Zaka na Faida zake kulingana na Mafundisho ya Kikatoliki, Katekisimu, na Biblia

Tumsifu Yesu Kristo…

Nakualika tujifunze pamoja kuhusu maana ya Zaka, Sababu za Kutoa Zaka na Faida zake kulingana na Mafundisho ya Kikatoliki, Katekisimu, na Biblia

Maana ya Zaka

Zaka ni sehemu ya kumi ya mapato au mazao ambayo Mkristo anatoa kwa ajili ya kazi ya Mungu. Katika Biblia, zaka inatajwa kama sehemu ya lazima kwa kila Mwisraeli kutoa kwa ajili ya kuendeleza kazi ya Mungu na kuwasaidia wasiojiweza.

Sababu za Kutoa Zaka

  1. Agizo la Mungu:
  • Katika Kitabu cha Mambo ya Walawi 27:30, Mungu anatoa amri kwa Waisraeli kwamba zaka ni takatifu na ni mali ya Bwana.
  1. Shukrani kwa Baraka za Mungu:
  • Kutoa zaka ni ishara ya kumshukuru Mungu kwa baraka na mafanikio tunayopata (Kumbukumbu la Torati 8:18).
  1. Kutoa kwa moyo wa hiari:
  • Biblia inasisitiza umuhimu wa kutoa kwa hiari na kwa moyo mkunjufu (2 Wakorintho 9:7).
  1. Kuwezesha Huduma za Kanisa:
  • Zaka zinatumika kusaidia kazi za kanisa kama huduma za kiroho na kimwili (Malaki 3:10).
  1. Kuwasaidia Watu Wenye Mahitaji:
  • Zaka hutumika pia kusaidia maskini, yatima, wajane na wale walioko kwenye mahitaji (Kumbukumbu la Torati 14:28-29).

Faida za Kutoa Zaka

  1. Kubarikiwa na Mungu:
  • Mungu anaahidi kumimina baraka nyingi kwa wale wanaotoa zaka kwa uaminifu (Malaki 3:10).
  1. Kukuza Imani na Kumtegemea Mungu:
  • Kutoa zaka ni njia ya kukuza imani yetu na kumtegemea Mungu zaidi kwa mahitaji yetu (Mithali 3:9-10).
  1. Kupata Neema na Fadhila za Mungu:
  • Kutoa zaka kunaleta neema na fadhila za Mungu katika maisha yetu (Luka 6:38).
  1. Kujenga na Kuimarisha Jamii ya Wakristo:
  • Zaka zinasaidia katika kuimarisha huduma na shughuli mbalimbali za jamii ya Wakristo, kuleta umoja na upendo (Matendo ya Mitume 2:44-45).
  1. Kusafisha Nafsi na Kujenga Roho ya Ukristo:
  • Ni njia ya kujisafisha na kujenga roho ya ukarimu, unyenyekevu na upendo (2 Wakorintho 8:12).

Marejeo ya Biblia

  • Mambo ya Walawi 27:30: “Kila zaka ya nchi, ikiwa mbegu za nchi, au matunda ya miti, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.”
  • Kumbukumbu la Torati 14:28-29: “Kila mwisho wa miaka mitatu utatoa zote zaka za maongeo yako katika mwaka ule, nawe utaziweka ndani ya malango yako…”
  • Malaki 3:10: “Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa hayo, asema Bwana wa majeshi…”
  • Luka 6:38: “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwa sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu…”
  • 2 Wakorintho 9:7: “Kila mmoja na atoe kama alivyoamua moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.”

Kwa ujumla, kutoa zaka ni tendo la utii kwa Mungu na njia ya kuonyesha shukrani, upendo na kujitoa kwa ajili ya kuendeleza kazi ya Mungu na kusaidia wengine katika jamii.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu toba na wongofu?

Katika Kanisa Katoliki, toba na wongofu ni sehemu muhimu ya maisha ya Kikristo. Imani yetu inatufundisha kuwa tunapokuwa na dhambi, tunapaswa kurejea kwa Mungu kwa toba na kufanya mabadiliko katika maisha yetu.

Toba ni nini? Toba ni kitendo cha kujutia dhambi zetu na kurejea kwa Mungu. Tunaungama dhambi zetu kwa padri na kupokea msamaha kutoka kwa Mungu. Ni muhimu kwamba tunajuta kwa kweli kwa dhambi zetu na tunajitahidi kuepuka kufanya dhambi tena. Kama inavyosema katika Kitabu cha Mathayo 3:2, "Tubuni, kwa kuwa ufalme wa mbinguni umekaribia."

Wongofu ni nini? Wongofu ni kubadilisha mwelekeo wa maisha yetu kutoka dhambi na kuelekea Mungu. Hii inamaanisha kuwa tunabadilisha maisha yetu kwa kufuata mafundisho ya Kanisa Katoliki na kumtumikia Mungu. Kama inavyosema katika Warumi 12:2, "Msiifuatishe namna hii ya ulimwengu, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na yaliyo kamili."

Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa toba na wongofu ni muhimu sana kwa wokovu wetu. Kama inavyosema katika KKK 1428, "Kanisa linafundisha kwamba kila mmoja wetu anapaswa kutubu dhambi zake, kumrudia Mungu, kujiweka katika neema ya Mungu, na kuwa na dhamiri safi. Toba inatupatia nafasi ya kuanza upya na kumtumikia Mungu kwa moyo safi."

Ni muhimu pia kukumbuka kwamba toba na wongofu ni mchakato wa maisha. Hatupaswi kujuta tu dhambi zetu mara moja na kufikiria kuwa tumeokoka. Badala yake, tunapaswa kujitahidi kwa bidii kumtumikia Mungu kila siku, kujitahidi kufuata mafundisho ya Kanisa Katoliki, na kuomba neema ya Mungu ili kuendelea kufanya mema.

Kwa hivyo, kama wakatoliki tunapaswa kujifunza kuhusu toba na wongofu kwa undani zaidi. Tunapaswa kujua kwamba hata kama tunafanya dhambi, tunaweza kurudi kwa Mungu na kupokea msamaha kupitia toba na kufanya mabadiliko ya maisha. Kama inavyosema katika 1 Yohana 1:9, "Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na uovu wote."

Kwa hiyo, katika maisha yetu ya Kikristo, tunapaswa kuwa na moyo wa toba na wongofu, kutubu dhambi zetu, na kujitahidi kumtumikia Mungu kwa bidii. Kama inavyosema katika KKK 1434, "Toba ni kuanza upya, na wakati huu ni wa neema na rehema ya Mungu. Toba ni zawadi ya Roho Mtakatifu ambayo inatuongoza kwenye maisha mapya katika Kristo."

Shopping Cart
15
    15
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About