Mafundisho ya Msingi ya Kanisa Katoliki: Makala za Katoliki
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya kuwa mtakatifu?
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya kuwa mtakatifu? Hili ni swali muhimu sana kwa wakristo wote. Kuwa mtakatifu ni kielelezo cha maisha ya kujitolea kwa Mungu, kuishi katika mapenzi yake na kufuata maagizo yake yote. Ni kuitikia wito wa Mungu kwetu sisi wote kuishi maisha ya utakatifu.
Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa kila mmoja wetu ameitwa kuwa mtakatifu. Katika barua ya kwanza ya Mtume Petro, anasema "Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu" (1 Petro 1:16). Lakini ni vipi tunaweza kuwa watakatifu? Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa njia pekee ya kuwa mtakatifu ni kwa kufuata maagizo ya Mungu, kuishi maisha ya sala, na kumtumikia Mungu na wenzetu.
Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa kuwa mtakatifu ni jambo linalowezekana kwa kila mmoja wetu. Kwa mfano, tunaweza kuwa watakatifu kwa kuishi maisha ya kuwajali wengine, kwa kusameheana, kuwapenda na kuwatumikia wengine. Kanisa linatufundisha kuwa kuwa mtakatifu ni kumfuata Yesu kwa karibu, kufuata maagizo yake na kuwa na imani thabiti kwa Mungu.
Kanisa Katoliki linatukumbusha kuwa tunapokuwa watakatifu, sisi ni sehemu ya jumuiya ya watakatifu na kwamba utakatifu ni karama inayotolewa na Mungu. Utakatifu unatokana na neema ya Mungu na hakuna mtu anayeweza kuwa mtakatifu kwa nguvu zake mwenyewe. Kwa kufanya hivyo, Kanisa linatufundisha kuwa tunahitaji kudumisha maisha yetu ya kiroho, kwa kuishi maisha ya sala, kuwahi sakramenti na kufanya kazi ya kiroho.
Kanisa Katoliki linatufundisha kwamba kila mtu ana wajibu wa kutafuta utakatifu. Hii ina maana kuwa tunapaswa kutafuta kumjua Mungu zaidi, kumtii na kumtumikia. Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunasomwa kwamba "Mtakatifu ni mtu aliyejisalimisha kikamilifu kwa Mungu. Kwa hiyo, kuishi maisha ya utakatifu ni kuwa na urafiki wa karibu na Mungu" (CCC 2013).
Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa ili kuwa mtakatifu lazima tujifunze kutawala tamaa zetu, kutetea ukweli, kusamehe, kuwa na msamaha na kujitolea kwa kazi ya Mungu. Tunahitaji kuwa jasiri na kuwa na nguvu za kiroho ili kupambana na ulimwengu wa dhambi na uovu.
Katika hitimisho, Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa kila mmoja wetu ana wajibu wa kuitikia wito wa Mungu wa kuwa mtakatifu. Kwa kufanya hivyo, tunahitaji kuwa karibu na Mungu, kuishi maisha ya sala na kutumia maisha yetu kujitolea kwa kazi ya Mungu. Tunahitaji kuwa na imani thabiti katika Mungu na kujitahidi kutimiza mapenzi yake. Kwa kufanya hivyo, tutaweza kufikia utakatifu wa kumjua Mungu na kuishi maisha ya utakatifu.
Maana ya jina Bikira Maria
Siri ya kamba nyekundu
Miaka zaidi ya 3000 iliyopita katika mji wa Yeriko alikuwepo mwanamke mmoja kahaba, jina lake Rahabu. Huyu mwanamke aliwaokoa wapelelezi wa Israel waliotumwa kwenda kufanya uchunguzi ktk nchi yao.
Wakati wana wa Israel wanatoka Misri kuelekea nchi ya Kaanani, Mungu aliwaahidi kuwapa mji wa Yeriko. Kwahiyo walipofika ng’ambo ya mto Yordani, Yoshua akatuma wapelezi wawili kwenda kuipeleleza Yeriko kabla wana wa Israel kuivamia na kuitwaa. Wale wapelelezi walipofika mji wa Yeriko mfalme akapelekewa taarifa kuwa kuna watu wawili wameingia kuipeleleza nchi.
Kwahiyo mfalme akaagiza wakamatwe na wauawe. Wale wapelelezi wakaingia ktk nyumba ya mwanamke kahaba aitwaye Rahabu akawaficha darini. Akawafunika kwa mabua ya kitani. Wale askari walipofika na kumuuliza Rahabu kwamba wako wapi waisrael wawili walioingia humu ndani, Rahabu akajibu kuwa wameondoka.
Akasema ni kweli waliingia ktk nyumba yangu lakini walitoka kabla lango la mji halijafungwa. Akawaambia wafuateni haraka kabla hawajafika mbali. Wale askari wakatoka kuwafuata wale wapelelezi hadi katika vilima vya nje ya mji lakini wasiwaone. Ilipofika usiku Rahabu akawashusha darini wale wapelelezi na kuwaelekeza namna ya kutoroka mji wa Yeriko. Akawaelekeza wapite njia nyingine tofauti na ile waliyoiendea wale askari. Akawashusha kupitia dirishani ili watu wa mji ule wasiwaone.
Kwa ukarimu aliowatendea wale wapelelezi wakaweka agano nae kwamba siku wana wa Israel wakija kuiangamiza Yeriko, BWANA ataiponya nyumba ya Rahabu na ndugu zake wote. Ili kutimiza agano hilo wale wapelezi wakamwambia Rahabu weka kamba nyekundu katika dirisha lako kama alama, ili jeshi la Israel liltakapouteketeza mji nyumba yako isiangamizwe.
Yoshua 2:17 &18 “Wale wapelelezi wakamwambia Rahabu, Sisi tunataka tusiwe na hatia kwa ajili ya kiapo hiki ulichotuapisha. Angalia, tutakapoingia katika nchi hii, funga kamba hii nyekundu katika dirisha hili ulilotuteremshia; nawe uwakusanye nyumbani mwako, baba yako, mama yako, na ndugu zako, na watu wote wa nyumba ya baba yako.”
Rahabu akafanya hivyo, na siku Jeshi la Israel lilipovamia Mji wa Yeriko ili kuuteketeza, Rahabu na ndugu zake walipona.
Yoshua 6:23 &24 “Basi wale vijana wapelelezi wakaingia, wakamtoa Rahabu, na baba yake, na mama yake, na ndugu zake, na vitu vyote walivyokuwa navyo, wakawatoa na jamaa zake wote pia; wakawaweka nje ya matuo ya Israeli. Kisha wakauteketeza mji kwa moto, na vitu vyote vilivyokuwa ndani yakeโฆ”
MORAL OF THE STORY.!
Habari hii ina mengi ya kutufundisha lakini leo nataka nikufundishe kuhusiana na siri ya kamba nyekundu ambayo Rahabu aliiweka katika dirisha lake na jinsi ilivyomuokoa.
Rahabu hakua mtakatifu, hakuwa mteule wa Mungu wala hakuwa kizazi cha Israel. Alikua mwanamke wa mataifa, tena kahaba. Hakuwa mwema sana machoni pa Mungu. Lakini aliokoka kwa sababu ya “kamba nyekundu” dirishani mwake. Pengine wapo maaskofu, wachungaji, mitume au manabii walioangamizwa, lakini kahaba Rahabu akaokolewa yeye na ndugu zake licha ya kwamba alikua kahaba. Siri ni “kamba nyekundu” dirishani mwake.
Jiulize je wewe unayo kamba nyekundu? Kuna watu katika maisha wanaonekana wenye dhambi, wachafu, dhaifu au wasiofaa, lakini Mungu huwanyanyua na kuwabariki na kuwaacha wale tunaodhani ni watakatifu au wenye haki. Mungu anaangalia “kamba nyekundu”. Unaweza kuwa mtakatifu lakini huna “kamba nyekundu” itakayomfanya Mungu akurehemu.
Unaweza kuwa umemaliza masomo yako na umefaulu vizuri, lakini kila unapoomba kazi huitwi hata kwenye usaili, na ukiitwa hupati kazi, miaka inazidi kwenda. Unaamua kwenda kwenye maombi. Kila siku unafanya maombi lakini bado hufanikiwi. Unajiuliza tatizo liko wapi. Unaji-asses na kuona hakuna tatizo mahali. Kumbe huna “kamba nyekundu”
Au unaweza kuwa una biashara yako lakini haifanikiwi. Hupati wateja. Umehitahidi kwa kila hali lakini bado huoni faida. Unadhani tatizo labda Mungu amekuacha. Unaamua kuwa mtu wa maombi. Unazunguka makanisa mbalimbali kuonbewa lakini bado haufanikiwi. Kumbe huna “kamba nyekundu”.
“Kamba nyekundu” imekuwa siri ya mafanikio ya watu wengi bila kujalisha mahusiano yao kiroho na Mungu. Bila kujalisha kama ni wakristo au si wakristo. Kamba nyekundu imewasaidia hata wenye dhambi kubarikiwa. Rahabu alikua kahaba lakini yeye na ndugu zake waliokolewa kwa sababu ya “kamba nyekundu”.
Je kamba nyekundu ni nini? Kamba nyekundu ni mfumo wako wa maisha; jinsi unavyoishi na unayowatendea watu wengine, hasa “wateule” wa Mungu.
Kuna wakati Mungu huamua kukubariki si kwa sababu wewe ni mwema sana, bali kwa sababu kuna watu wema wanaoomba kwa ajili yako. Inawezekana tangu uanze kuomba, maombi yako hayajawahi kufika kwa Mungu lakini unabarikiwa, kwa sababu ya kamba nyekundu.
Kuna watu ambao ni “wateule” wa Mungu, kwahiyo kadri unavyowatendea mema hao watu baraka zinakuja kwako “automatically” hata kama wewe si mkristo. Rahabu aliwatendendea mema wapelelezi wa Israel baraka zikaenda kwake “automatically” bila kujalisha kwamba alikua kahaba.
Yatima, wajane, maskini, wazee, wagonjwa na wengine wenye uhitaji ni wateule wa Mungu. Kwahiyo ukiwatendea mema watu hawa baraka zinakuja kwako hata kama wewe ni mwenye dhambi.
Kwa mfano kama kuna watoto yatima unawasomesha, au kuna wajane unawasaidia mahitaji yao, au wagonjwa unawasaidia matibabu, si rahisi Mungu kuondoa mkono wake wa baraka kwako hata kama wewe ni mwenye dhambi. Mungu akiondoa baraka kwako watu wake watateseka.
Wale yatima, wajane, wagonjwa ambao wewe ni msaada kwao kila wakiomba Mungu huongeza baraka kwako ili uzidi kuwahudumia. Inawezekana maombi yako hayafikagi kwa Mungu lakini unabarikiwa kwa sababu ya maombi ya hao unawaosaidia.
Kuna wakati Mungu anaweza kuamua kuzipiga dhoruba biashara za wenzako, lakini ya kwako ikasimama imara. Si kwa sababu wewe ni mwema sana, bali kwa sababu kuna watu wanamlilia Mungu kwa ajili yako. Kuna wanategemea ada za shule kwenye hiyo biashara yako. Kuna watu wanategemea pesa za matibabu kwenye biashara yako. Kwa hiyo Mungu akiyumbisha biashara yako atakua anawaumiza watu hao. So ili asiwaumize anaamua kukuaacha. Hiyo ni kamba nyekundu.!
Kuna wakati wenzio wakifanya makosa madogo kazini wanafukuzwa kazi, lakini unajishangaa wewe umefanya makosa makubwa na hufukuzwi. Si kwa sababu una bahati sana. Ni kamba nyekundu. Kuna watu walioko nyuma yako ambao ni wateule wa Mungu. Kuna yatima wanategemea kulipiwa ada kwa mshahara wako, kuna wagonjwa wanategemea kusaidiwa hela za matibabu kwenye mshahara wako, kuna wajane wanategemea hela ya kuishi kutoka kwako. Kwahiyo Mungu akikuadhibu anakua amewaadhibu na wao. Kwahiyo ili wapone inabidi akulinde hata kama umefanya kosa kazini. Unashangaa tu kesi imeisha hata kwa namna ambayo hujui. Hiyo ni kamba nyekundu.!
Kuna mtu ambaye ni maskini wa kutupwa hana hata uwezo wa kununua sukari. Lakini anamuomba Mungu kwa imani kuwa ampe sukari aweze kunywa chai kila siku. Kwa kuwa huyo maskini huwa anapata sukari kutoka kwako, Mungu atazidi kukubariki ili uendelee kumhudumia huyo maskini. Hiyo ni Kamba nyekundu.!
Kamba nyekundu ilimuokoa Rahabu na ndugu zake licha ya kwamba alikua kahaba. Jiulize wewe una kamba nyekundu? Je kuna watu wako nyuma yako ambao Mungu akiwaangalia anakubariki, anakuokoa hata kama upo kwenye hatari?
Kama unamsomesha mwanao shule ya “mamilioni” kwa mwaka wakati mtoto wa jirani yako hana hata uniform za kuendea shule, au unatumia “mamilioni” kwa pombe na starehe wakati kuna wagonjwa wanaokufa kwa kukosa panadol, siku Mungu akitaka kukuadhibu hajiulizi mara mbili maana huna “kamba nyekundu” nyuma yako.
Lakini yule anayesaidia wenye uhitaji, kama yatima, wagonjwa, wazee, wajane,walemavu, au maskini atazidi kubarikiwa tu hata kama ni mwenye dhambi, maana anayo kamba nyekundu.
Hii ni kwa sababu Mungu akitaka kumuadhibu, kabla hajamtizama yeye anatizama kwanza yatima walioko nyuma yake anaowasaidia, anatizama wagonjwa wanaomtegemea kwa matibabu, anatizama wajane. Anaona akimuadhibu, atakuwa ameadhibu na hao wanaomtegemea. Kwa hiyo anaamua kumuacha.
Hii ina maana kuwa baraka na utakatifu ni vitu viwili tofauti. Unaweza usiwe mtakatifu lakini Mungu akakubariki na akakulinda. Unaweza kubarikiwa si kwa sababu unastahili, bali kwa sababu kuna “wanaostahili” wapo nyuma yako wakikupigania kwa baba yao (Yehova). Ndio maana kuna watu wengi wasio Wakristo wanabarikiwa kila siku hata kama hawamjui Mungu. Ni kwa sababu wana “kamba nyekundu”.
Malisa G.J
Ni nini maana ya Ekaristi Takatifu katika imani ya Kanisa Katoliki?
Ekaristi Takatifu ni moja ya Sakramenti muhimu katika imani ya Kanisa Katoliki. Sakramenti hii huadhimishwa kwa kutumia mkate na divai, ambavyo vinageuka kuwa mwili na damu ya Yesu Kristo. Ni matukio muhimu sana katika ibada za Kanisa Katoliki, kwa sababu Ekaristi Takatifu ni chakula cha kiroho ambacho kinawapa waumini nguvu na neema ya kumtumikia Mungu.
Kanisa Katoliki linatambua Ekaristi Takatifu kama Sakramenti, ambayo ni ishara ya uwepo wa Yesu Kristo. Kwa njia hii, mtu anayepokea Ekaristi Takatifu anakuwa na umoja na Yesu Kristo, ambaye ni Bwana wa maisha yote. Kwa hiyo, Ekaristi Takatifu ni chanzo cha maisha ya kiroho ya kila Mkristo.
Ekaristi Takatifu pia ina maana ya kumbukumbu ya kifo cha Yesu Kristo msalabani. Kristo alitia damu yake kwa ajili ya wokovu wa wanadamu wote. Kwa hiyo, kila tunapoadhimisha Ekaristi Takatifu, tunakumbuka dhabihu ya Kristo na tunashukuru kwa ajili ya upendo wake kwetu sisi.
Kwa mujibu wa Kitabu cha Matendo ya Mitume 2:42, Kanisa la mwanzo lilikuwa likifanya mkutano kila siku "kwa kula chakula chao pamoja kwa furaha na kwa unyofu wa moyo, wakimsifu Mungu". Kanisa Katoliki linatambua Ekaristi Takatifu kama chanzo cha umoja na mshikamano wa waumini. Katika Ekaristi Takatifu, waumini huwa na uzoefu wa kuwa sehemu ya familia ya Mungu.
Kanisa Katoliki linatambua umuhimu wa kuenenda kwa uungwana wakati wa maadhimisho ya Ekaristi Takatifu. Kwa sababu Ekaristi Takatifu ni Sakramenti ya uwepo wa Kristo, ni muhimu kuheshimu Sakramenti hii kwa kutumia vitu vizuri, kama vile chombo cha kuwekea Ekaristi Takatifu.
Kwa kumalizia, Ekaristi Takatifu ni Sakramenti muhimu katika imani ya Kanisa Katoliki. Ni ishara ya uwepo na upendo wa Yesu Kristo, na inatupa neema ya kuwa sehemu ya familia ya Mungu. Kwa hiyo, tunapaswa kuheshimu na kuenenda kwa uungwana katika maadhimisho ya Ekaristi Takatifu. Kama inavyoelezwa katika KKK 1324, "Ekaristi ni chanzo na kilele cha maisha ya Kikristo".
Huruma ya Mungu: Upendo Usiokuwa na Kifani
Huruma ya Mungu ni upendo usiokuwa na kifani ulioelekezwa kwetu sisi binadamu. Tunapokea huruma hii kwa neema ya Mungu, ambaye daima yuko pamoja nasi katika safari yetu ya kiroho. Kwa njia ya huruma yake, Mungu anatupatia msamaha na uponyaji wa dhambi zetu. Ni muhimu kuelewa maana ya huruma ya Mungu, na jinsi inavyoweza kutusaidia katika maisha yetu ya kila siku.
-
Huruma ya Mungu inamaanisha kusamehe dhambi zetu. Mungu anatualika kumwomba msamaha kwa makosa yetu, na kwa neema yake atatusamehe. โLakini Mungu, kwa sababu ya rehema yake kuu aliyo nayo, alituokoa, kwa kuoshwa kwa maji, na kufanywa upya kwa Roho Mtakatifuโ (Tito 3:5).
-
Huruma ya Mungu inatupatia nguvu za kushinda majaribu na dhambi. Tunapata neema ya Mungu kwa njia ya Sakramenti ya Kitubio, ambapo tunamkiri Mungu dhambi zetu na kupokea msamaha wake. โMungu ni mwaminifu, naye hatawaacha mjaribiwe kuliko mwezavyo, lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kuvumiliaโ (1 Wakorintho 10:13).
-
Huruma ya Mungu inatufariji katika mateso yetu. Tunajua kwamba Mungu yuko pamoja nasi katika kila hali, na tunaweza kumwomba aondoe mateso yetu au atupatie nguvu ya kuvumilia. โMungu ni wetu wa faraja yote, atufariji katika taabu yetu, ili sisi tuweze kuwafariji wale wamo katika taabu yoyote, kwa faraja hiyo ile ile ambayo sisi tunafarijiwa na Munguโ (2 Wakorintho 1:3-4).
-
Huruma ya Mungu inatupatia upendo usio na kifani. Tunajua kwamba Mungu anatupenda bila kikomo, na kwamba upendo wake ni wa kudumu. โKwa kuwa Mungu aliupenda ulimwengu hivi, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa mileleโ (Yohana 3:16).
-
Huruma ya Mungu inatupatia tumaini la uzima wa milele. Tunajua kwamba mwisho wa maisha yetu sio kifo, bali uzima wa milele pamoja na Mungu. โKwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, lakini karama ya bure ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetuโ (Warumi 6:23).
-
Huruma ya Mungu inatufundisha kusamehe wengine. Tunapokea huruma ya Mungu kwa sababu ya neema yake, na tunapaswa kuwa na huruma kwa wengine pia. โBasi, kama Mungu alivyowasamehe ninyi katika Kristo, vivyo hivyo ninyi mnapaswa kusameheanaโ (Wakolosai 3:13).
-
Huruma ya Mungu inatufundisha kutoa msamaha bila kikomo. Tunapaswa kusamehe wengine mara kwa mara, bila kujali makosa yao. โBasi, ikiwa ndugu yako akakosa dhidi yako mara saba katika siku moja, na akaja kwako akisema, Naungama, usamehe, utamsameheโ (Mathayo 18:21-22).
-
Huruma ya Mungu inatufundisha kumpenda jirani yetu. Tunapaswa kuwa na huruma kwa wengine kama vile Mungu anavyotupa huruma. โKwa maana huu ndio upendo wa Mungu, kwamba tuzishike amri zake, na amri zake si nzitoโ (1 Yohana 5:3).
-
Huruma ya Mungu inatufundisha kuishi kwa uadilifu na upendo. Tunapaswa kuishi kwa uadilifu na upendo, kama vile Mungu anavyotuonyesha huruma. โBasi, iweni wafuatao wa Mungu kama watoto wake wapendwa, na enendeni katika upendo, kama vile Kristo naye alivyowapenda sisi, akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukatoโ (Waefeso 5:1-2).
-
Huruma ya Mungu inatupatia neema ya kufikia utakatifu. Tunapokea huruma ya Mungu kwa neema yake, na tunapaswa kutumia neema hiyo kufikia utakatifu. โLakini kama alivyo mtakatifu yeye aliyewaita ninyi, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifuโ (1 Petro 1:15-16).
Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunajifunza kwamba huruma ya Mungu ni โupendo wa Mungu unaotenda katika maisha yetu kadiri ya hali yetu ya dhambi na uhitaji wetuโ (CCC 1846). Tunapokea huruma hii kwa njia ya Sakramenti ya Kitubio, ambapo tunamkiri Mungu dhambi zetu na kupokea msamaha wake. Katika Diary ya Mtakatifu Maria Faustina Kowalska, tunajifunza kwamba huruma ya Mungu ni kubwa zaidi ya dhambi zetu, na kwamba tunapaswa kuomba huruma yake kila siku.
Je, unajisikiaje kuhusu huruma ya Mungu? Je, unajua kwamba Mungu anatakia mema yako na anataka kukupa upendo na neema yake? Tunaweza kumwomba Mungu kwa moyo wote na kumwomba aonyeshe huruma yake kwetu sisi, na kwa wale wote tunaowapenda. Tumaini katika huruma ya Mungu na utaona mabadiliko makubwa katika maisha yako!
Mafundisho makubwa ya Yesu Kristo
Heri
Basi Yesu alipoona makutano, alipanda
mlimani akaketi chini, nao wanafunzi
wake wakamjia. 2Ndipo akaanza kuwafundisha,
akisema:
3 โWana heri walio masikini wa roho,
maana hao Ufalme wa Mbinguni ni wao.
4Wana heri wale wanaohuzunika,
maana hao watafarijiwa.
5Wana heri walio wapole,
maana hao watairithi nchi.
6Wana heri wenye njaa na kiu ya haki,
maana hao watatoshelezwa.
7Wana heri wenye huruma,
maana hao watapata rehema.
8Wana heri walio na moyo safi,
maana hao watamwona Mungu.
9Wana heri walio wapatanishi,
maana hao wataitwa wana wa Mungu.
10Wana heri wanaoteswa kwa sababu ya haki,
maana hao Ufalme wa Mbinguni ni wao.
11Mna heri ninyi watu watakapowashutumu
na kuwatesa na kunena dhidi yenu mabaya ya
aina zote kwa uongo kwa ajili yangu. 12Furahini
na kushangilia kwa maana thawabu yenu ni
kuu.
Chumvi na Nuru
13โโNinyi ni chumvi ya ulimwengu. Lakini
chumvi ikipoteza ladha yake, yawezaje
kurudishiwa ladha yake tena ? Haifai tena kwa
kitu cho chote, ila kutupwa nje ikanyagwe na
watu.
14โโNinyi ni nuru ya ulimwengu. Mji
uliojengwa kilimani hauwezi kufichika. 15Wala
watu hawawashi taa na kuifunika kwa bakuli.
Badala yake, huiweka kwenye kinara chake,
nayo hutoa mwanga kwa kila mtu aliyemo ndani
ya ile nyumba. 16Vivyo hivyo, nuru yenu iangaze
mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu
mema wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Kutimiza Sheria
17โMsidhani kwamba nimekuja kuondoa
Torati au Manabii, sikuja kuondoa bali kutimiza.
18Kwa maana,amin, nawaambia, mpaka mbingu
na dunia zitakapopita, hakuna hata herufi moja
ndogo wala nukta itakayopotea kwa namna yo
yote kutoka kwenye Torati mpaka kila kitu kiwe
kimetimia. 19Kwa hiyo, ye yote atakayevunja
mojawapo ya amri ndogo kuliko zote ya amri
hizi, naye akawafundisha wengine kufanya
hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika Ufalme wa
Mbinguni, lakini ye yote azitendaye na
kuzifundisha hizi amri ataitwa mkuu katika
Ufalme ya Mbinguni. 20Kwa maana nawaambia,
haki yenu isipozidi haki ya waandishi wa sheria
na Mafarisayo, kamwe hamtaingia katika
Ufalme wa Mbinguni.
Mafundisho ya Yesu Kuhusu Hasira
21โMmesikia walivyoambiwa watu wa
zamani kwamba, โUsiue, ye yote atakayeua
atapasiwa hukumu.โ 22Lakini mimi nawaambia
kwamba, ye yote atakayemkasirikia ndugu yake
wa kiume au wa kike, atapasiwa hukumu. Tena,
ye yote atakayemwambia ndugu yake wa kiume
au wa kike, โRacaโa, yaani kumdharau na
kumdhihaki, atapasiwa kufanyiwa baraza. Lakini
ye yote atakayesema โWe mpumbavu ulaaniwe!โ
Atapasiwa hukumu ya moto wa jehanam.
23โKwa hiyo, kama unatoa sadaka yako
madhabahuni, ukakumbuka kuwa ndugu yako
ana kitu dhidi yako, 24iache sadaka yako hapo
hapo, mbele ya madhabahu, uende kwanza
ukapatane na ndugu yako wa kiume au wa kike,
kisha urudi na ukatoe sadaka yako.
25โPatana na mshtaki wako upesi wakati
uwapo njiani pamoja naye kwenda
mahakamani, ili mshtaki wako asije akakutia
mikononi mwa hakimu, naye hakimu akakutia
mikononi mwa walinzi, nawe ukatupwa
gerezani. 26Amin, nakuambia, hutatoka humo
mpaka umelipa hadi senti ya mwishoโ
Mafundisho ya Yesu Kuhusu Uzinzi
27โMmesikia kwamba ilinenwa, โUsizini’.
28Lakini mimi nawaambia: kwamba ye yote
amtazamaye mwanamke kwa kumtamani,
amekwisha kuzini naye moyoni mwake. 29Jicho
lako la kuume likikufanya utende dhambi, ling’oe
ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza
kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako
mzima utupwe jehanam. 30Kama mkono wako
wa kuume ukikufanya utende dhambi, ukate
uutupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza
kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako
mzima utupwe jehanam.
Mafundisho ya Yesu Kuhusu Talaka
31โโPia ilinenwa kwamba, โMtu ye yote
amwachaye mkewe na ampe hati ya talaka.โ
32Lakini mimi nawaambia, ye yote amwachaye
mkewe isipokuwa kwa kosa la uasherati,
amfanya mkewe kuwa mzinzi. Na ye yote
amwoaye yule mwanamke aliyeachwa azini.โโ
Mafundisho ya Yesu Kuhusu Kuapa
33โTena mmesikia walivyoambiwa watu wa
zamani kwamba, โUsiape kwa uongo, bali
timizeni, nadhiri zile ulizofanya kwa Bwanaโ
34Lakini mimi nawaambia,โโMsiape kabisa, ama
kwa mbingu, kwa kuwa ni kiti cha enzi cha
Mungu, 35au kwa nchi, kwa kuwa ndipo mahali
pake pa kuwekea miguu, au kwa Yerusalemu,
kwa kuwa ndio mji wa Mfalme Mkuu. 36Nanyi
msiape kwa vichwa vyenu kwa kuwa hamwezi
kuufanya hata unywele mmoja kuwa mweupe
au mweusi. 37โNdiyo,โ yenu iwe โNdiyoโ na
โHapanaโ, yenu iwe โHapana.โ Lo lote zaidi ya hili
latoka kwa yule mwovu.โโ
Mafundisho ya Yesu Kuhusu Kulipiza Kisasi
38โMmesikia kwamba ilinenwa, โJicho kwa
jicho na jino kwa jino.โ 39Lakini mimi nawaambia,
msishindane na mtu mwovu. Lakini kama mtu
akikupiga kwenye shavu la kuume, mgeuzie na
la pili pia, 40Kama mtu akitaka kukushtaki na
kuchukua shati lako, mwachie achukue na koti
pia. 41Kama mtu akikulazimisha kwenda
kilometa moja, nenda naye kilometa mbili.
42Mpe yeye akuombaye, wala usimgeuzie
kisogo yeye atakaye kukukopa.โโ
Mafundisho ya Yesu kuhusu Upendo Kwa Adui
43โโMmesikia kwamba ilinenwa, โMpende
jirani yako na umchukie adui yako.โ 44Lakini
mimi ninawaambia : Wapendeni adui zenu na
waombeeni wanaowatesa ninyi, 45ili mpate
kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa
maana Yeye huwaangazia jua lake watu waovu
na watu wema, naye huwanyeshea mvua
wenye haki na wasio haki. 46Kama mkiwapenda
wale wanaowapenda tu, mtapata thawabu gani?
Je, hata watoza ushuru hawafanyi hivyo?
47Nanyi kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je,
mnafanya nini zaidi ya wengine? Je, hata watu
wasiomjua Mungu, hawafanyi hivyo? 48Kwa hiyo
iweni wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni
alivyo mkamilifu.โโ
Mafundisho ya Yesu kuhusu Kuwapa Wahitaji
โโAngalieni msitende wema wenu mbele ya
watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya
hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu
aliye mbinguni.
2โโHivyo mnapowapa wahitaji, msipige
panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki
katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na
watu. Amin, amin nawaambia wao wamekwisha
kupokea thawabu yao. 3Lakini ninyi mtoapo
sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa
kushoto usijue mkono wako wa kuume
unachofanya, 4ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo
Baba yako wa mbinguni, Yeye aonaye sirini
atakupa thawabu kwa wazi.
Mafundisho ya Yesu Kuhusu kusali
5โNanyi msalipo, msiwe kama wanafiki,
maana wao hupenda kusali wakiwa
wamesimama katika masinagogi na kando ya
barabara ili waonekane na watu. Amin, amin
nawaambieni, wao wamekwisha kupata
thawabu yao. 6Lakini wewe unaposali, ingia
chumbani mwako, funga mlango na umwombe
Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye
sirini atakupa thawabu yako. 7โNanyi mnaposali
msiseme maneno kama wafanyavyo watu
wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani
kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa
maneno yao. 8Msiwe kama wao, kwa sababu
Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla
hamjamwomba.โโ
9โโHivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba :
โBaba yetu uliye mbinguni,
Jina lako litukuzwe.
10Ufalme wako uje.
Mapenzi yako yafanyike hapa duniani
kama huko mbinguni.
11Utupatie leo riziki zetu za kila siku.
12Utusamehe deni zetu,
kama sisi nasi tulivyokwisha
kuwasamehe wadeni wetu.
13 Usitutie majaribuni,
bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu,
kwa kuwa Ufalme ni Wako na nguvu
na utukufu hata milele. Amen.โ
14Kwa kuwa kama mkiwasamehe watu wengine
wanapowakosea, Baba yenu wa mbinguni
atawasamehe pia na ninyi. 15Lakini
msipowasamehe watu wengine makosa yao,
wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa
yenu.
Mafundisho ya Yesu Kuhusu Kufunga
16โMnapofunga, msiwe wenye huzuni kama
wafanyavyo wanafiki. Maana wao hukunja
nyuso zao ili kuwaonyesha wengine kwamba
wamefunga. Amin, amin nawaambia wao
wamekwisha kupata thawabu yao kamilifu.
17Lakini mnapofunga, jipakeni mafuta kichwani
na kunawa nyuso zenu 18ili kufunga kwenu
kusionekane na watu wengine ila Baba yenu
aliye sirini, naye Baba yenu aonaye sirini
atawapa thawabu yenu kwa wazi.โ
Akiba Ya Mbinguni
19โMsijiwekee hazina duniani, mahali
ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi
huvunja na kuiba. 20Lakini jiwekeeni hazina
mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu
haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba.
21Kwa sababu mahali akiba yako ilipo, hapo
ndipo pia moyo wako utakapokuwa.โโ
Jicho Ni Taa Ya Mwili
22โโJicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni
nyofu, mwili wako wote utakuwa na nuru.
23Lakini kama jicho lako ni ovu, mwili wako wote
utajawa na giza. Kwa hiyo basi, kama nuru
iliyomo ndani yako ikiwa giza, hilo ni giza kuu
namna gani ! โ
Mungu Na Mali
24โโHakuna mtu ye yote awezaye
kuwatumikia mabwana wawili, kwa kuwa ama
atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine,
au atashikamana sana na huyu na kumdharau
huyu mwingine. Ninyi hamwezi kumtumikia
Mungu na malia.โโ
Msiwe Na Wasiwasi
25โโKwa hiyo nawaambia, msiwe na
wasiwasi kuhusu maisha yenu: mtakula nini au
mtakunywa nini, au kuhusu miili yenu, mtavaa
nini. Je, maisha si zaidi ya chakula na mwili
zaidi ya mavazi? 26Waangalieni ndege wa
angani, wao hawapandi wala hawavuni au
kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni
huwalisha hao. Je, ninyi si wa thamani zaidi
kuliko hao ndege? 27Ni nani miongoni mwenu
ambaye kwa kujitaabisha kwake aweza
kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha
yake au kuongeza dhiraa mojab kwenye kimo
chake ?
28โโNanyi kwa nini kujitaabisha kwa ajili ya
mavazi? Fikirini maua ya shambani yameavyo.
Hayafanyi kazi wala hayafumi. 29Lakini
nawaambia, hata mfalme Solomoni katika fahari
yake yote hakuvikwa kama mojawapo ya hayo
maua. 30Lakini ikiwa Mungu anayavika hivi
majani ya shambani, ambayo leo yapo na kesho
yanatupwa motoni, je, hatawavika ninyi vizuri
zaidi, enyi wa imani haba? 31Kwa hiyo msiwe na
wasiwasi, mkisema, โTutakula nini?โ Au
โTutakunywa nini?โ Au โTutavaa nini?โ 32Kwa
maana watu wasiomjua Mungu ndio
wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa
mbinguni anafahamu kwamba mnahitaji hayo
yote. 33Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa
Mungu na haki yake na haya yote
mtaongezewa. 34Kwa hiyo msiwe na wasi wasi
kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia
yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.โโ
Mafundisho ya Yesu kuhusu Kuwahukumu Wengine
โUsihukumu ili usije ukahukumiwa. 2Kwa
maana kwa jinsi ile unavyowahukumu
wengine, ndivyo utakavyohukumiwa na kwa
kipimo kile utakachotoa ndicho utakachopokea.
3โโKwa nini unatazama kibanzi kidogo
kilichomo kwenye jicho la ndugu yako na wala
huoni boriti iliyoko kwenye jicho lako? 4Au
unawezaje kumwambia ndugu yako, โAcha nitoe
kibanzi kwenye jicho lako wakati kuna boriti
kwenye jicho lako mwenyewe ?โ 5Ewe mnafiki,
toa kwanza boriti kwenye jicho lako mwenyewe,
nawe ndipo utakapoona wazi ili kuondoa kibanzi
kilichoko kwenye jicho la ndugu yako.
6โโMsiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu, wala
msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya
hivyo, watazikanyaga kanyaga na kisha
watawageukia na kuwararua vipande vipande. โ
Omba, Tafuta, Bisha
7โOmbeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi
mtapata, bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
8Kwa maana kila aombaye hupewa, naye
atafutaye huona, naye abishaye hufunguliwa
mlango.
9โโAu ni nani miongoni mwenu ambaye
mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
10Au mwanawe akimwomba samaki atampa
nyoka? 11Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua
jinsi ya kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi
sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu
vizuri wale wamwombao ? 12Kwa hiyo cho chote
ambacho mngetaka mtendewe na watu, ninyi
nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii
ndiyo Torati na Manabii.โโ
Njia Nyembamba Na Njia Pana
13โโIngieni kwa kupitia mlango mwembamba,
kwa maana lango ni pana na njia ni pana
ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa
kupitia lango hilo. 14Lakini mlango ni
mwembamba na njia ni finyo ielekayo kwenye
uzima, nao ni wachache tu waionao.โโ
Mti na Tunda lake
15โJihadharini na manabii wa uongo,
wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya
kondoo, lakini ndani wao ni mbwa mwitu
wakali.16Mtawatambua kwa matunda yao. Je,
watu huchuma zabibu kwenye miiba au tini
kwenye michongoma? 17Vivyo hivyo, mti
mwema huzaa matunda mazuri na mti mbaya
huzaa matunda mabaya. 18Mti mwema hauwezi
kuzaa matunda mabaya wala mti mbaya
hauwezi kuzaa matunda mazuri. 19Kila mti
usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa
motoni. 20Hivyo, kwa matunda yao,
mtawatambua.โ
Mwanafunzi Wa Kweli
21โSi kila mtu aniambiaye, โBwana, Bwana,โ
atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni bali ni
yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye
mbinguni. 22Wengi wataniambia siku ile,
โBwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako
na kwa jina lako kutoa pepo na kufanya miujiza
mingi? 23Ndipo nitakapowaambia wazi,
`โSikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi
watenda maovu!โ
Msikiaji Na Mtendaji
24โโKwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya
maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu
mwenye busara aliyejenga nyumba yake
kwenye mwamba. 25Mvua ikanyesha, mafuriko
yakaja na upepo ukavuma ukaipiga hiyo
nyumba, lakini haikuanguka kwa sababu msingi
wake ulikuwa kwenye mwamba. 26Naye kila
anayesikia haya maneno yangu wala
asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga
nyumba yake kwenye mchanga. 27Mvua
ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo
ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo
ikaanguka kwa kishindo kikubwa.โโ
28Yesu alipomaliza kusema maneno haya,
makutano ya watu wakashangazwa sana na
mafundisho yake, 29kwa sababu alifundisha
kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama
walimu wao wa sheria.
Ibada ya Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Upendo na Ukarimu
Ibada ya Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Upendo na Ukarimu
Karibu kwa maelezo ya Ibada ya Huruma ya Mungu. Ibada hii ni sehemu muhimu ya maombi katika Kanisa Katoliki kama ilivyofundishwa na Kanisa. Ibada hii inatufundisha jinsi ya kuishi kwa upendo na ukarimu, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha.
- Kuanza Ibada ya Huruma ya Mungu kila siku
Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, Ibada ya Huruma ya Mungu ni muhimu kwa ajili ya maisha ya Kikristo. Kwa hivyo, unapaswa kuianza kila siku kwa kusali chaplet ya Huruma ya Mungu. (CCC 1419). Kusali chaplet hii kunaweza kutufungulia mioyo yetu kwa upendo wa Mungu.
- Kusamehe na kuwa tayari kusamehe
Hakuna mtu ambaye hajawahi kufanya makosa. Ni kwa kuwasamehe wengine ndipo tunaweza pia kusamehewa (Matthew 6:14-15). Hiyo ni kwa sababu, Bwana wetu Yesu Kristo alitufundisha kwamba kusamehe ni sehemu muhimu ya upendo na ukarimu.
- Kutenda wema na kutoa sadaka
Ibada ya Huruma ya Mungu inatufundisha pia jinsi ya kutenda wema na kutoa sadaka kwa wengine. (CCC 2447). Tunaweza kufanya hivyo kwa kufanya kazi za upendo, kutoa msaada na kuwa tayari kutoa mali zetu ili kusaidia wengine katika shida zao.
- Kumuomba Mungu kwa unyenyekevu
Tunapomwomba Mungu kwa unyenyekevu, tunafungua mioyo yetu kwa upendo na huruma yake. (CCC 2559). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kuomba huruma na kumwomba Mungu atusaidie kuishi kwa upendo na ukarimu.
- Kuwa na imani
Ibada ya Huruma ya Mungu inatufundisha pia jinsi ya kuwa na imani. Tunahitaji kumwamini Mungu na ahadi zake. Kwa kufanya hivyo, tunakuwa na uhakika kwamba Mungu atatupatia kila kitu tunachohitaji ili kuishi kwa upendo na ukarimu. (CCC 156).
- Kuwa tayari kuomba msamaha
Tunapojitokeza mbele ya Mungu kwa unyenyekevu na kuomba msamaha kwa mapungufu yetu, tunamruhusu Mungu kuingia ndani ya maisha yetu na kujaza nafasi zetu za udhaifu na upungufu. (CCC 2631). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kuomba msamaha kila wakati tunapojikuta tumeanguka au kutenda makosa.
- Kutafakari juu ya huruma ya Mungu
Kutafakari juu ya Huruma ya Mungu kunaweza kutusaidia kukua katika upendo na ukarimu. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kufahamu zaidi jinsi Mungu anatupenda na anatujali. (CCC 2708). Tunaweza kutafakari juu ya Huruma ya Mungu kwa kusoma Injili, kusoma vitabu vya maombezi au hata kusoma Kitabu cha Maisha ya Mtakatifu Faustina Kowalska.
- Kujifunza kutoka kwa watakatifu
Watakatifu ni mfano wa kuigwa katika maisha yetu ya Kikristo, na wanaweza kutusaidia kukua katika upendo na ukarimu. (CCC 2683). Kwa hiyo, tunapaswa kujifunza kutoka kwa watakatifu kwa kusoma maisha yao na kufuata mifano yao.
- Kuwa na moyo wa shukrani
Kuwa na moyo wa shukrani ni muhimu katika maisha ya Kikristo. Tunapomshukuru Mungu kwa yote anayotufanyia, tunaujaza moyo wetu na upendo na ukarimu. (CCC 2648). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kumshukuru Mungu kwa yote, iwe ni kubwa au ndogo.
- Kuishi kwa upendo
Kuishi kwa upendo ni muhimu katika maisha ya Kikristo. Kama ilivyofundishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, upendo ni amri kuu ya Kanisa. (John 13:34-35). Kwa hivyo, tunapaswa kuishi kwa upendo kwa kila mtu, iwe ni mtu wa familia yetu, jirani, au mtu yeyote tunayekutana nae.
Ibada ya Huruma ya Mungu ni sehemu muhimu ya maisha yetu ya Kikristo. Inatufundisha jinsi ya kuishi kwa upendo na ukarimu, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha. Je, umepata nafasi ya kusali Ibada ya Huruma ya Mungu leo? Je, unaishi kwa upendo na ukarimu katika maisha yako ya Kikristo?
Usipite bila kusoma kisa hiki cha kusisimua
Siku moja jioni katika mji flani, kulikuwa na basi likisafiri kutoka mji huo kuelekea mji mwingine. Lilikuwa ni basi kubwa na limejaa abiria. Wakati wakiendelea na safari, ghafla, mvua kubwa iliyoambatana na radi ikaanza kunyesha. Dereva hakuogopa, wala abiria, wakaendelea na safari. Mara wakati wanaenda, radi ikaanza kufuatilia gari. Kila wakienda, radi inapiga karibu na basi kana kwamba inalifuata basi. Likisimama, radi inapiga pembezoni mwa basi.
Dereva kuona hivyo, akasimamisha gari mita 5 kutoka kwenye mtiโฆ Akawaambia abiria, “Humu ndani ya basi, kuna mtu ambaye leo ni siku yake ya kufa, tena kufa kwa radi. Ili tusife wote, nataka kila abiria ashuke akaguse mti ili anayepigwa na radi, apigwe wengine wasife kwa ajili yake. “Abiria wakitetemeka, wakaanza kushuka mmoja mmoja. Unaenda unagusa mti , kisha unarudi kwenye basi. Abiria wote pamoja na dereva mmoja mmoja, wakaenda, wakagusa mti na kurudi bila dhara lolote! Akawa kabaki abiria mmoja tu, ambaye alikuwa hajagusa mti. Abiria wote kwa macho ya hasira wakamwambia akaguse mti. Akawa anaogopa kufa. Akagoma. Wakamlazimisha kwa nguvu sana na kumtoa njeโฆโฆ. โฆโฆ.. Yule abiria akiwa amefumba macho, akaenda akagusa mti. Hamadi bin Vuu! Radi kali sana ikalipiga basi, abiria na wote waliokuwamo, wakafa palepale. Kumbe uwepo wake ndio ulikuwa unazuia abiria wengine wasidhurike na radi.
MAFUNZO
1. Unapofanikiwa, huwezi jua uwepo wa nani umefanikisha mafanikio yako, usichukue sifa zote peke yako. Wapatie na wengine bila kumsahau MUNGU.
2. Unaweza kujiona huna thamani sehemu ulipo, iwe kwenye kundi la WhatsApp, darasani, kazini, kwenye basi, barabarani bila kujua kama uwepo wako ni wa muhimu sana kwa ustawi wa wengine.
3. Usimtenge wala kumnyanyasa mtu au jirani yako, huwezi jua uwepo wake ni kwa ajili gani.
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu toba na wongofu?
Katika Kanisa Katoliki, toba na wongofu ni sehemu muhimu ya maisha ya Kikristo. Imani yetu inatufundisha kuwa tunapokuwa na dhambi, tunapaswa kurejea kwa Mungu kwa toba na kufanya mabadiliko katika maisha yetu.
Toba ni nini? Toba ni kitendo cha kujutia dhambi zetu na kurejea kwa Mungu. Tunaungama dhambi zetu kwa padri na kupokea msamaha kutoka kwa Mungu. Ni muhimu kwamba tunajuta kwa kweli kwa dhambi zetu na tunajitahidi kuepuka kufanya dhambi tena. Kama inavyosema katika Kitabu cha Mathayo 3:2, "Tubuni, kwa kuwa ufalme wa mbinguni umekaribia."
Wongofu ni nini? Wongofu ni kubadilisha mwelekeo wa maisha yetu kutoka dhambi na kuelekea Mungu. Hii inamaanisha kuwa tunabadilisha maisha yetu kwa kufuata mafundisho ya Kanisa Katoliki na kumtumikia Mungu. Kama inavyosema katika Warumi 12:2, "Msiifuatishe namna hii ya ulimwengu, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na yaliyo kamili."
Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa toba na wongofu ni muhimu sana kwa wokovu wetu. Kama inavyosema katika KKK 1428, "Kanisa linafundisha kwamba kila mmoja wetu anapaswa kutubu dhambi zake, kumrudia Mungu, kujiweka katika neema ya Mungu, na kuwa na dhamiri safi. Toba inatupatia nafasi ya kuanza upya na kumtumikia Mungu kwa moyo safi."
Ni muhimu pia kukumbuka kwamba toba na wongofu ni mchakato wa maisha. Hatupaswi kujuta tu dhambi zetu mara moja na kufikiria kuwa tumeokoka. Badala yake, tunapaswa kujitahidi kwa bidii kumtumikia Mungu kila siku, kujitahidi kufuata mafundisho ya Kanisa Katoliki, na kuomba neema ya Mungu ili kuendelea kufanya mema.
Kwa hivyo, kama wakatoliki tunapaswa kujifunza kuhusu toba na wongofu kwa undani zaidi. Tunapaswa kujua kwamba hata kama tunafanya dhambi, tunaweza kurudi kwa Mungu na kupokea msamaha kupitia toba na kufanya mabadiliko ya maisha. Kama inavyosema katika 1 Yohana 1:9, "Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na uovu wote."
Kwa hiyo, katika maisha yetu ya Kikristo, tunapaswa kuwa na moyo wa toba na wongofu, kutubu dhambi zetu, na kujitahidi kumtumikia Mungu kwa bidii. Kama inavyosema katika KKK 1434, "Toba ni kuanza upya, na wakati huu ni wa neema na rehema ya Mungu. Toba ni zawadi ya Roho Mtakatifu ambayo inatuongoza kwenye maisha mapya katika Kristo."
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Roho Mtakatifu?
Katika Kanisa Katoliki, Roho Mtakatifu ni Mungu mmoja katika Utatu Mtakatifu (Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu). Ni kwa njia ya Roho Mtakatifu tu ndipo tunapata uwezo wa kuelewa na kukubali mambo ya Mungu. Katika Biblia, Roho Mtakatifu anaelezwa kama "Mlinzi", "Msaidizi", "Mwalimu", na "Mwongozi".
Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama mtakatifu na mmoja wa wanaume wa Mungu watatu. Roho Mtakatifu anahusika katika kazi ya Mungu ya wokovu wa mwanadamu. Katika Luka 11:13, Yesu anasema, "Baba yenu wa mbinguni atawapa Roho Mtakatifu wale wanaomwomba." Hii inaonyesha wazi kuwa Roho Mtakatifu ni zawadi ya Mungu kwa watu wake.
Katika Kanisa Katoliki, Roho Mtakatifu anachukua jukumu muhimu katika sakramenti nyingi za Kanisa. Kwa mfano, wakati wa Ubatizo, Roho Mtakatifu anamdhihirisha mwanadamu kama mwana wa Mungu. Wakati wa Kipaimara, Roho Mtakatifu anaimarisha neema ya ubatizo na kuwawezesha Wakristo kushiriki kikamilifu katika maisha ya Kanisa.
Katika Waraka kwa Wagalatia 5:22-23, Paulo anaelezea matunda ya Roho Mtakatifu: "Upendo, furaha, amani, uvumilivu, urafiki mwema, fadhili, uaminifu, upole na kiasi." Kanisa Katoliki linakubali kuwa Roho Mtakatifu ndiye anayewezesha watu kuzalisha matunda haya maishani mwao.
Kwa hivyo, imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Roho Mtakatifu ni kwamba ni mmoja wa wanaume wa Mungu watatu, na anachukua jukumu muhimu katika maisha ya Wakristo na katika sakramenti za Kanisa. Roho Mtakatifu anatupa uwezo wa kuelewa na kukubali mambo ya Mungu, na anatupa matunda ya upendo, furaha, amani, na zaidi. Kwa hivyo, ni muhimu kwetu kumwomba Roho Mtakatifu katika maisha yetu ya kila siku, ili aweze kutuongoza na kutusaidia kuishi maisha ya Kikristo.
Maana ya siku ya Jumatano ya Majivu
Utangulizi
Nini maana ya Jumatano ya majivu?
Kwaresma ni nini?
Mama kanisa anatupatia kipindi hiki ili tuweze kutafakari njia na mienendo yetu na kubadilika kama haimpendezi Mungu
Kwa nini ikaitwa Jumatano ya majivu?
Nini maana ya majivu tunayopaka?
Angalia; Isaya 61:3, Ester 4:1-3, Yeremia 6:26, Ezekieli 27:30, Mathayo 11:21 na Luka 10:13.
Kwa nini majivu yanapakwa kwenye paji la uso na si vinginevyo?
Hali kadhalika hutukumbusha ishara ya msalaba tuliyochorwa na mafuta matakatifu siku ya ubatizo wetu, hutukumbusha ahadi tuliyoiweka siku hiyo ya ubatizo na kutuita tuishi maisha ya utakatifu
Padri hutamka maneno gani wakati anapaka majivu?
Tunapopakwa majivu Padre husema; Mwanadamu kumbuka u mavumbi na mavumbini utarudi AU Tubuni na kuiamini Injili.
Maneno anayosema padre yana maana gani?
Hivyo maandalizi tunayoalikwa kuyafanaya si maandalizi ya kuelekea mavumbini bali maandalizi ya kuelekeza roho zetu mbinguni. Ndio maana pia twaambiwa tubuni na kuiamini Injili.
Majivu tunayopakwa yanatoka wapi?
Kwa nini unatumia matawi ya Jumapili ya Matawi?
Kanisa limekataza nini siku ya Jumatano ya majivu?
Nani analazima kufunga siku ya Jumatano ya majivu na Kwaresma?
Tunaposema kujinyima wakati wa Kwaresma tunamaana gani?
Mwisho
Je, Kuangalia Picha za Ngono ni dhambi?
Zaburi 101:3
โSitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.โ
Watu wengi wameanguka katika mtego huu wa Ibilisi na kujikuta wakifanya mambo ya “AIBU” wanapokuwa sehemu zao za Siri iwe ni chumbani au bafuni.
1. MAANA YA PICHA ZA NGONO
Neno PICHA ni kivuli cha mtu, watu, kitu n.k. PICHA si kitu halisi bali ni kivuli chake. Unaweza ukapewa PICHA ya mtu lakini usifahamu urefu wake au ni mfupi kiasi gani lakini sura yake ukawa umeiweka katika kumbukumbu yako. NGONO ni kitendo cha mtu, watu kufanya kitendo cha kujamiana (Tendo la Ndoa) na pia ni ile hali ya kuwa uchi wa mnyama. Kuangalia picha za ngono ni kitendo cha kuangalia watu wakifanya Matendo ya kujamiana iwe kwa njia ya asili, kinyume na maumbile au kufanya na wanayama. Kitendo hicho huleta kuchochea tamaa ya miili kiasi ambacho watu wengine hufanya mambo ya “AIBU” katika nyumba zao (Warumi 1:24-28). PICHA za NGONO zimeenea kila mahali kwa sasa, kwenye simu yako unaweza ukakutana na “uchafu” wa namna hiyo. Wahindi wao picha za ngono huziita “kachumbali” na unaweza ukamkuta Mhindi amekaa na familia yake anaangalia “kachumbali” wanadai inanogesha utamu wanapofika kitandani. Huko ni kujidanganya Mungu hakumletea Adamu PICHA ya NGONO bali alimletea mke ambaye watashirikiana naye kwenye Tendo Takatifu (Mwanzo 2:18, 21-25). Wakati mmoja Mfalme Daudi wakati watu wake wa vita wamekwenda vitani yeye akawa yuko ghorofani anaangalia “PICHA LIVE” ya NGONO mwanamke alikuwa akioga matokeo yake yakawa ni kufanya kitendo chenyewe na kuamua kumuua mume wa Bathsheba (2Samweli 11:2-27).
โIkawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?โโฆโฆโฆ..
Kile kitendo cha Daudi “kuona” lilikuwa kosa kubwa la kiufundi katika akili yake likamchanganya. Ndivyo ilivyo kwa PICHA ZA NGONO lazima ukiangalia upate “UKICHAA” wa muda ukajikuta umeng’ang’ania sabuni au ndizi ukiwa unapiga punyeto. Ni aibu sana sana mtu mwenye heshima zako kama wewe labda wewe ni meneja, mkurugenzi, mtu mwenye Elimu yako ya maana unakutwa unaangaika sabuni, godoro au toy la jinsia ya kiume.
2. JE! KUANGALIA PICHA ZA NGONO NI DHAMBI?
Kuangalia picha za ngono “NI DHAMBI” kwa herufi kubwa. Katika Sheria ya Musa ilikuwa mtu anahesabika kuwa ametenda dhambi pale ambapo atakutwa akifanya kitendo hicho au kukiwa na mashahidi wawili au watatu atatakiwa kuhukumiwa sawasawa na Sheria husika. Kwenye dhambi ya uzinzi mtu alitakiwa apigwe mawe hadi afe sivyo kwa Sheria ya Kristo yenyewe inazungumzia juu ya kitendo cha “kutamani” tu unahesabika kuwa umefanyika DHAMBI (Mathayo 6:27-29, Waebrania 10:28). Tamaa mbaya ni dhambi kama dhambi nyinginezo. Kwa kawaida tamaa huja na ile tamaa huchukua mimba na baadaye huzaa dhambi (Yakobo 1:13-16). Kitendo cha kuangalia picha za ngono hupofusha “FIKRA” nzuri za mtu alizonazo. Mawazo machafu uanza kutawala katika ubongo wako hadi “USHUSHE” huo mzigo ulioko kwenye viungo vyako vya uzazi. Ahaaa ni hatari aiseeee. Wewe unayengalia picha za ngono Kama ndiyo starehe yako unaiharibi nafsi yako “unakuwa zezeta wa akili” Biblia inasema “taa ya Mwili jicho na jicho lako likiwa safi mwili wako wote utakuwa na nuru. Lakini jicho lako likiwa bovu mwili wako wote utakuwa na giza..”(Mathayo 6:22-23). Kwa wale wanandoa ni “MWIKO” kutumia picha za ngono ili kunogesha kufanya Tendo la Ndoa. Wewe mume unaye hapo “chombo” unakiona “live” na kimethibitishwa na Mungu mwenyewe sasa hiyo mipicha ya nini? Kila kiungo Mungu alikiweka kwa ajili ya kusudi maalum kama ni mdomo kwa ajili ya kuongea na kupitisha chakula na si kunyonya sehemu za Siri za mwenzi wako. Mungu ameweka sehemu ya “haja kubwa” kwa ajili ya kutolea uchafu uliotengenezwa na tumbo na si kiungo kingine kiende kukoroga “zege” hilo huo ni uchafu(Ufunuo 22:10-15).
Warumi 1:26:27
โHivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.โ
3. JINSI YA KUSHINDA DHAMBI YA KUANGALIA PICHA ZA NGONO
PICHA ZA NGONO zinavutia sana kuziangalia ila zina maangamizo makubwa sana katika maisha yako. Lazima ufikie mahali kukata shauri ndani ya Moyo wako kuambatana na Mungu. Kusudi kubwa la shetani kuachilia mambo yake ya NGONO kwenye mitandao ili apate wafuasi wengi zaidi. Hakuna kitu unachoweza kukifanya katika simu za Android wengine wasikitambue. Kila unalolipitia na kuliangalia kwa Siri siku ya siku litaletwa hukumuni na Mungu mwenyewe (Warumi 2:16, Mhubiri 12:14)
USHAURI WAKIVITENDO:
I) Yatie Nuru macho yako – Zaburi 13:3, 19:8 – Yaruhusu macho yako yaingiziwe nuru na Yesu. Chukua muda wa kutosha kuingiza PICHA zinazomhusu Mungu zaidi. Angalia wahubiri mbalimbali.
II) Tazama mambo ya Adili(mema) – Zaburi 17:2-3 – Kuna nguvu kubwa sana tunapokuwa tunaangalia mambo mema. Vipindi vizuri vya neno la Mungu. PICHA zinazojenga siyo zinazoharibu fikra zetu.
III) Kumuomba Mungu afumbue macho yako – Zaburi 119:18, 146:8- Maombi ni muhimu ili kufanya macho yako kuona kusudi la Mungu na Kutambua uwepo wa shetani katika PICHA ZA NGONO.
IV) Weka maneno ya Mungu Mbele za macho yako – Mithali 4:20-21
Wakati wote soma neno la Mungu kupitia kifaa chochote cha ki-electronic ili uweze kumjua Mungu zaidi.
V) Macho yako yatazame Mbele – Mithali 4:25-27
Kutazama Mbele maana yake uwe na maono. Maono ni PICHA au TASWIRA ya Mbele ya maisha yako. Yeremia aliulizwa unaona nini naye akasema “anaona ufito wa mlozi” anaona kitu kizuri (Yeremia 1:11-12).
VI) Pendezwa na njia za Mungu – Mithali 23:26
Kuanzia sasa anza kupendezwa na njia za Mungu katika maisha yako. Acha kuzifuata njia zako katika kuufurahisha mwili wako wa PICHA zisizofaa.
VII) Tafuta watumishi wa Mungu ili wakufundishe – Isaya 48:17, 30:20-21
Kuna mambo ambayo yanatupa shida katika maisha yetu ni vizuri kuwaona waalimu ili watusaidie jinsi ya kutoka katika mtego huo.
VIII) Omba rehema na neema ya Yesu – Waebrania 4:16
Tunahitaji neema ya Mungu ili kushinda Hali hiyo ya kupenda KUANGALIA PICHA ZA NGONO na pia kufunguliwa kutoka katika vifungo hivyo vya pepo wa tamaa na mahaba.
Mungu atakubariki ukipeleka ujumbe huu kwa wengine
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Kipaimara?
Sakramenti ya Kipaimara ni sakramenti ya tatu katika Kanisa Katoliki baada ya Sakramenti ya Ubatizo na Ekaristi. Ni sakramenti muhimu sana katika maisha ya Mkristo, kwa sababu inaweka muhuri wa Roho Mtakatifu na inapeana nguvu ya kushuhudia imani yetu kwa Yesu Kristo. Kwa hivyo, ni muhimu kujua imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti hii.
Kanisa Katoliki linaamini kwamba sakramenti ya Kipaimara inaweka muhuri wa Roho Mtakatifu kwa Mkristo na inawapa nguvu kushuhudia imani yao kwa Kristo. Inafuatilia mfano wa Yesu mwenyewe aliyehitimu huduma yake kwa ubatizo wa Roho Mtakatifu (Mathayo 3:16, Marko 1:10, Luka 3:22).
Kupitia sakramenti ya Kipaimara, Mkristo anapokea nguvu ya kushuhudia imani yake kwa Kristo. Roho Mtakatifu anamwongoza, kumtia nguvu na kumwimarisha katika imani yake. Hii inampa Mkristo uwezo wa kuwa shahidi wa Kristo katika maisha yake na miongoni mwa watu wake.
Kufuatia mfano wa Yesu, Kanisa Katoliki linatambua sakramenti ya Kipaimara kama sehemu muhimu ya kujiunga na Kanisa. Ni kielelezo cha uhusiano wa kina wa Mkristo na Kristo, na pia ni kielelezo cha uhusiano wake na Kanisa.
Sakramenti ya Kipaimara pia inaunganishwa na Sakramenti ya Ubatizo kwa sababu inaendeleza kazi ya Roho Mtakatifu ambayo ilianza katika ubatizo. Kwa hivyo, Kanisa Katoliki linahimiza watu kukamilisha ubatizo wao kwa kupokea sakramenti ya Kipaimara.
Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunaona kwamba sakramenti ya Kipaimara inathibitisha imani ya Mkristo na inaimarisha uhusiano wake na Kanisa. (CCC 1285). Ni sakramenti ya kudumu ambayo inatukumbusha jukumu letu la kushuhudia imani yetu kwa Kristo na kuhudumia Kanisa.
Kanisa Katoliki pia linatambua kuwa sakramenti ya Kipaimara inaunganisha Mkristo na washiriki wengine wa Kanisa. Ni kielelezo cha umoja wa kanisa na inawawezesha Wakristo kushiriki katika huduma ya Kanisa la Kristo.
Kwa kumalizia, Kanisa Katoliki linathamini sana sakramenti ya Kipaimara kama sehemu muhimu ya maisha ya Mkristo. Ni sakramenti ambayo inaweka muhuri wa Roho Mtakatifu na inawapa nguvu kushuhudia imani yao kwa Kristo. Kama Mkristo, ni muhimu kushiriki katika sakramenti hii na kuzingatia yale inayofundisha ili kuimarisha imani yetu.
Zifahamu dhambi ambazo huondolewa na PAPA pekee au Padre kwa ruhusa maalumu kutoka kwa Baba Mtakatifu
Padre kuzini na muumini hiyo inabaki kuwa ni dhambi Kati ya Padre na muumini wake.Kwa dhambi hiyo Padre anaweza akatafuta Padre mwenzake akaungama kadhalika na kwa muumini huyo.
Shida ni pale tu endapo,Padre anataka KUMUUNGAMISHA mwanamke (muumini) aliyetoka KUZINI naye au yule ANAYEZINI naye hiyo dhambi na kosa hilo hata Askofu wako hana mamlaka ya kukuungamisha wala kukusamehe ni kiti cha Baba Mtakatifu pekee chini ya Congregatio inayoshughulikia mambo matakatifu iitwayo kwa kifupi CDF yaani Congregation for Doctrine of Faith.
Ambayo inashughulikia na mambo mawili hasa makuu yaani;
1.Protection of Sanctity of Sacraments
2.Dealing with Grave Disorders and bad conducts in the Church.
Kwa ufupi ndio hivyo ninaweza kukwambia.
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Ndoa?
Sakramenti ya Ndoa ni muhimu sana katika Kanisa Katoliki. Kwa mujibu wa imani ya Kanisa, ndoa ni sakramenti inayofungamanisha mume na mke kwa maisha yote. Kupitia sakramenti hii, wawili hao wanakuwa kitu kimoja mbele ya Mungu na Kanisa. Kwa hiyo, kuna taratibu nyingi na sheria zinazohusiana na sakramenti hii ambazo zinapaswa kufuatwa kwa umakini.
Kanisa Katoliki linazingatia ndoa kuwa ni muhimu sana katika kuleta upendo, umoja na amani katika familia. Kwa mujibu wa imani ya Kanisa, ndoa inapaswa kufungwa kwa upendo, heshima, uaminifu na uwazi. Mume na mke wanapaswa kuwa wawazi kuhusu mambo yote yanayohusiana na ndoa yao, na wanapaswa kuelewana kwa kila hali ili ndoa yao iwe na baraka za Mungu.
Kuna taratibu nyingi ambazo wanandoa wanapaswa kufuata kabla ya kufunga ndoa. Wanandoa wanapaswa kuhudhuria kikao cha maandalizi ya ndoa kinachoendeshwa na padri wao. Kikao hiki ni muhimu sana kwani kinawapa wanandoa mafunzo juu ya imani ya Kanisa kuhusu ndoa na jinsi ya kuishi kama mume na mke.
Kanisa Katoliki linaamini kwamba ndoa ni sakramenti inayofungamanisha mume na mke kwa maisha yote. Kwa hiyo, ndoa haiwezi kuvunjwa isipokuwa kwa sababu za kikatili kama vile ndoa ya kulazimishwa, ndoa iliyopigwa marufuku na Kanisa au ndoa iliyofungwa kinyume cha sheria za Kanisa. Kwa mujibu wa Katekisimu ya Kanisa Katoliki (CCC), ndoa ni ahadi ambayo imefungwa kwa upendo na inapaswa kudumu hadi kifo. (CCC, 1660)
Kanisa Katoliki linahimiza wanandoa kuishi kwa upendo na heshima kwa kila mmoja. Wanaume wanapaswa kumpenda na kumheshimu mke wao kama Kristo alivyompenda Kanisa lake. (Waefeso 5:25) Wanawake wanapaswa kuwatii waume zao kama vile Kanisa linavyomtii Kristo. (Waefeso 5:22) Kupitia upendo na heshima hizi, wanandoa wanaweza kuwa mfano bora wa maisha ya Kikristo kwa watoto wao na kwa watu wengine.
Kwa hiyo, ni muhimu sana kuheshimu ndoa na kuzingatia taratibu zote zinazohusiana na sakramenti hii. Ndoa ni baraka kubwa kutoka kwa Mungu, na ni jukumu letu kuitunza na kuilinda. Kwa kufuata mafundisho ya Kanisa Katoliki na kuishi kwa upendo na heshima, tunaweza kujenga ndoa yenye baraka za Mungu na yenye furaha katika maisha yetu.
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema?
Leo tutajadili kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema. Kwa Wakatoliki, msamaha na rehema ni mada muhimu sana katika imani yetu. Tunakubali kwamba sisi sote ni wenye dhambi na tunahitaji kusamehewa dhambi zetu kwa ajili ya kufikia wokovu.
Tunamwamini Mungu kama mwenye rehema, ambaye anatupenda sana hata kama tumeanguka katika dhambi zetu. Kwa sababu ya upendo wake, Mungu ametoa njia ya msamaha na rehema kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu.
Kanisa Katoliki linahimiza Wakatoliki kutubu dhambi zao na kupata Sakramenti ya Upatanisho kama njia ya kupata msamaha wa dhambi. Sakramenti hii inaruhusu Wakatoliki kusema dhambi zao kwa padri na kufanya toba kwa ajili ya dhambi hizo. Padri kisha anawapa Wakatoliki msamaha wa dhambi zao kwa jina la Yesu Kristo.
Kanisa Katoliki linapenda kutumia Biblia kama mbinu ya kuwasilisha ujumbe wake. Katika wosia wa Yohana, tunasoma kwamba "ukiungama dhambi zako, yeye ni mwaminifu na wa haki hata akusamehe dhambi zako, na kukusafisha na uovu wote" (1 Yohana 1:9). Yesu mwenyewe pia alitoa uwezo wa kupata msamaha wa dhambi kwa wanafunzi wake katika Yohana 20:23.
Kanisa Katoliki pia linazingatia Catechism ya Kanisa Katoliki, ambayo inasema kwamba "Sakramenti ya Upatanisho inatupatia msamaha wa dhambi na kutufungulia njia ya kuwa na uhusiano mzuri na Mungu na Kanisa" (CCC 1422).
Kwa hiyo, msamaha na rehema ni muhimu sana katika imani ya Kanisa Katoliki. Tunamwamini Mungu kuwa mwenye rehema na tunajua kuwa kupata msamaha wa dhambi zetu ni njia ya kufikia wokovu. Kwa hiyo, tunahimiza Wakatoliki kuja kwa Sakramenti ya Upatanisho mara kwa mara ili kufurahia msamaha wa dhambi zao na kuwa na uhusiano mzuri na Mungu na Kanisa.
Tofauti kati ya Ibada, Sadaka na Sala/maombi
Ibada
Ibada mara nyingi huusisha matendo ya kipekee. Ibada inaweza kuwa ya kuabudu, kusifu, kuomba toba na kushukuru
Mfano wa ibada ni, Ibada ya Ijumaa kuu, Ibada ya kuabudu sakramenti kuu
Sadaka
Ni majitoleo kwa Mungu kwa nia ya kuomba, kushukuru, zawadi au kutakasa.
Sadaka ninayoiongelea hapa ni sadaka tofauti na hela/pesa ambayo inapotolewa hupewa binadamu mwingine na sio Moja kwa moja kwa mlengwa (Mungu). Sadaka ninayoiongelea mimi ni sadaka mfano wa ile ya Kaini na Abeli, Mfano wa ile ya Ibrahimu, Mfano wa sadaka alizotoa Musa Jangwani. Naongelea sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya damu ya kuchinjwa.
Sadaka hii inatolewa knisani kwenye adhimisho la ibada ya misa takatifu pale padri anapotolea mkate na divai na kuigeuza kuwa mwili na damu ya kristu.
Kinachofanyika hapa ni matoleo ya sadaka ya mwili na damu ya Yesu aliyoitoa pale msalabani, Pale Mkate na divai vinapogeuzwa mwili na damu ya Yesu basi ni ishara ya Sadaka ya mwili na damu aliyoitoa Yesu.
Mfano wa sadaka ni inapofanyika mageuzi ya Ekaristi pekee bila kwenda na mtiririko wa Misa
Sala
Sala ni kuongea kwa sauti au kimya, kwa nia ya kuomba, kushukuru, kusifu au kutafakari.
Sala inaweza ikawa sala za maombi, shukrani, sifa au tafakari
Mfano wa sala ni, jumuiya za kikatoliki zinapokutana, Sala za kawaida za kila siku mfano Asubuhi, mchana, Jioni
Kumbuka: Sala sio maombi. Sala ni zaidi ya maombi. Sala inaweza ikawa tafakari, maombi, sifa au shukrani
Umuhimu wa Ibada ya misa ya kikatoliki
Ibada ya misa ya kikatoliki imechukua nafasi ya vyote hivi vitatu, sala/maombi, sadaka na ibada. Ukishiriki misa ya Katoliki ni sawa na umeshiriki Ibada, Sawa na umeshiriki maombi na ni Sawa na umeshiriki Sadaka.
Tofauti kati ya misa ya kikatoliki na ibada za madhehebu mengine
Madhehebu menginehayachukui yote mfano inaweza ikawa imefanyika ibada tuu, na maombi bila sadaka.
Kwa hiyo unapohudhuria na kushiriki ibada ambayo sio ya kikatoliki, unakua hujakamilisha misa bali ni ibada na maombi tuu. Unakua umekosa sadaka yani sadaka ya mwili na damu ya Kristu.
Ndiyo maana unatakiwa uudhurie Ibada ya Misa Takatifu ya Kikatoliki.
Ushauri wangu kwa leo, ni Heri kuchagua kunyamaza
MITHALI 11:12 Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
MITHALI 17:28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.
Changamoto kubwa tuliyonayo ni kwamba tunataka kuongea kila wakati, tunataka kujibu kila tunachokisikia, kila tunachokiona tunataka kukisemea kitu.
Kuna wakati tunasikia na kukutana na mambo ambayo kiuhalisia moyo unagoma kabisa kunyamaza, unatamani ujibu, unatamani uwaambie watu yale umefanyiwa, unatamani uelezee vile umeumizwa lakini kumbe si kila jambo linatakiwa kuongelewa.
Si kila ukionacho unatakiwa kukisemea kitu. Si kila usikiacho/uambiwacho ni lazima ujibu.
Si kila ufanyiwacho ni lazima umwambie kila mtu.
MUHUBIRI 3:1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
Ipo nguvu katika kunyamaza
Yapo mambo ambayo tunapaswa kuongea, kusema, lakini yapo mambo ambayo tunapaswa kunyamaza kwa ajili ya usalama wa Roho zetu.
Ni kweli kuna wakati unasemwa sana vibaya, unasingiziwa, unatukanwa nk nk, lakini ni lazima ukumbuke kwamba kuna mazingira ambayo hupaswi kujibizana hata kama umeumia kiasi gani.
Unajua ni kwanini?
Ukisemwa vibaya, ukitukanwa, ukidharauliwa lazima moyo utaghafilika, moyo ukighafilika lazima utakuwa na hasira na ghadhabu.
Ukiwa na hasira katu usitegemee kuwa utajadiliana na mtu kwa hekima.
Ukiongea utaongea katika uwepo wa hasira, ukijibu utajibu kulingana na kiwango cha hasira ulichonacho.
Sasa jiulize majibu yanayotoka kutokana na msukumo wa hasira huwa yanakuwaje?
Mazuri? Ya upole? Ya hekima? Ya unyenyekevu? I am sure jibu ni hapana.
Kama jibu ni hapana that means utaongea vitu vibaya ambavyo ni chukizo kwa MUNGU kwa sababu amesema maneno yetu na yakolee munyu (chumvi).
Sasa badala ya kuongea upumbavu na ukamkosea MUNGU kwanini usichague kunyamaza?
AMOSI 5:3 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya.
Nimekuwa inspired sana na mwanamke Abigaili, ni kweli mumewe alikuwa na makosa, ni kweli alikuwa mlevi, lakini mwanamke huyu alijua ni wakati gani, na mazingira gani alipaswa kuongea na mumewe na alijua aongee nini. Alipomkuta mumewe yupo katika hali ya ulevi, ALINYAMAZA, alijua kuwa huu sio wakati wa kusema jambo lolote.
1 SAMWELI 25:1
Ni vyema sisi pia tukajifunza kusoma mazingira na nyakati na hali za watu zilivyo ili tujue ni wakati gani tujibu, tuongee nini na ni wakati gani tunyamaze
Kilinde kinywa, hakikisha haukiachi kinene mabaya โ ZABURI 50:19.
Usipoteze marafiki na kuharibu mahusiano kwa ajili ya kinywa kibovu โ MITHALI 11:9.
Ni vyema tukajifunza kujua ni neno gani tukitamka kwa wakati/hali/mazingira gani litakubaliwa โMITHALI 10:32.
ZABURI 19:14 โ Bwana na akafanye maneno yetu yakapate kibali mbele zake MUNGU na mbele za wanadamu pia.
1SAMWELI 25:36
Umeumizwa, umekwazwa, umetukanwa, umedharauliwa, KATIKA MAZINGIRA YA HASIRA NA GHADHABU JITAHIDI KUNYAMAZA.
Ni kweli moyo na akili na hisia vinakusukuma kujibu, kubisha nk nk, lakini elewa impact za kujibizana ukiwa na hasira na hizo ni bora ukae kimya.
*”AKUSHINDAE KUONGEA, MSHINDE KUNYAMAZA
“Uwe na siku njema!
Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo?
Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo?
Ndio! Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo. Kutubu ni kutambua makosa yetu, kujuta na kuahidi kubadili tabia zetu kwa kufuata kanuni za Mungu. Kimsingi, toba ni kuanza upya kwa njia ya Mungu.
Kanisa Katoliki linasisitiza kuhusu umuhimu wa toba kwa sababu inampendeza Mungu na inaleta amani na furaha kwa wanaotubu. Biblia inatuambia katika Luka 15:10 kwamba mbinguni kuna furaha kubwa miongoni mwa malaika wa Mungu wanapompokea mwenye dhambi anayetubu.
Kanisa linatueleza kuwa toba inahitaji kujutia dhambi zetu na kujitakasa. Inasema kwamba kutubu ni kujikana, kujinyenyekeza na kumwomba Mungu msamaha kwa unyenyekevu. Kuna haja ya kutambua kuwa dhambi zetu zinamuumiza Mungu na kuanza kutafuta njia ya kumpendeza.
Kanisa Katoliki linatufundisha pia juu ya umuhimu wa sakramenti ya toba. Sakramenti hii inasaidia katika wongofu wa moyo kwa kupata msamaha wa Mungu na kijito cha uzima katika Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, sakramenti hii ni muhimu katika kujenga uhusiano wetu na Mungu.
Kwa mujibu wa Catechism of the Catholic Church, toba ni muhimu kwa sababu inaponya na kurejesha uhusiano wetu na Mungu. Inaelezea kuwa kutubu kunatufanya kuwa wapya kwa sababu inatutoa katika hali ya dhambi na kutufanya watakatifu. Catechism pia inasisitiza umuhimu wa toba kama njia ya kuungana na Mungu na kufikia utakatifu.
Kwa hiyo, tunaweza kusikia kwa ufasaha kwamba Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa toba na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo. Tunatakiwa kujifunza kwa kina juu ya toba na kujitahidi kutenda kulingana na kanuni za Mungu. Mwisho wa siku, toba inatuleta karibu na Mungu na inatuwezesha kuishi kwa furaha kama wana wa Mungu.













































































I’m so happy you’re here! ๐ฅณ

Recent Comments