Vituko Vya Jumanne
Kilichotokea baada ya polisi wa kibongo kukutana na mwizi mzungu
POLISI KAKAMATA MZUNGU ‘yestaday I saw u at ze maize shop..(jana nilikuona dukani kwa muhindi) when u saw me u started 2 six six.(uliponiona ulianza ku-sitasita) u ran n decided 2 plant a car.(ulikimbia na ukaamua kupanda gari) zen u pot-cry me through ze window.(kisha ukanichungulia dirishani) now sleep down n snake well b4 I cut u a millet.(sasa lala chini kisha nyooka vizuri kabla sijakukata mtama) Chezea lugha wewe..!!!
Cheki huyu mtoto anachomjibu mwalimu wake, kufundisha watoto ni kazi kweli kweli
Mwanafunzi wa darasa la 2 kaulizwa na mwalimu wake
Hivi:je ukipewa maandazi 5 ukiambiwa kula 3 tu yatabaki mangapi?
Akamjibu hivi:nikipewa na chai hakibaki kitu mwalimu.
Tatizo la kukuta nywele kwenye chakula
Hapa ni shida
KUKUTA NYWELE KWENYE CHAKULA SIO TATIZO,TATIZO NI KUWAZA ITAKUWA IMETOKA SEHEMU GANI
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Cheki hiki kibabu kulivyowaacha watu hoi wakati mchungaji anafungisha ndoa
Mchungaji Kauliza: Yeyote mwenye pingamizi la haki kwa ndoa hii asimame na aje mbele.
Mara kasimama kibabu na kwenda mbele, bibi harusi alipomuona tu yule babu akazimia.
Mchungaji akauliza: tueleze pingamizi lako
Kibabu kikajibu: Nimeamua kuja mbele kwasababu kule nyuma sisikii!!!.
kanisa zima hoi,
Upendo wa kweli ni nini?
*Upendo wa kweli ni nini?*
*👉Upendo wa kweli ni pale mwanaume anapomfumania mwanamke wake na kisha kumwambia baby vaa nguo twende nyumbani*
*Kifo ni nini?*
*👉Kifo ni pale mwanamke anapokubali kwenda nyumbani na mwanaume yule.*
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Madogo wa sikuizi ni kiboko, cheki huyu alichokifanya akiwa darasani na mwalimu wake
Muda wa kwenda nyumbani ulikuwa umefika, mwalimu
akasema: yeyote atakaye jibu swali langu lolote kwa usahìhi ataondoka asiye jibu atabaki.
Dogo mmoja akatupa begi nje ya dirisha.
Mwalimu akauliza nani katupa ilo begi nje?
Dogo akajibu fasta mimi. Akafungua mlango akaenda kwao.
neno moja kwa dogo
Huyu Jamaa ubahili umezidi kwa hiki anachomwambia huyu dada
Kama ni ubahili hapa umezidi
mdada Bby naomba hela nimpeleke mdogo wangu hospital kang’atwa na nyoka
JAmaa embu mpe huyo nyoka cm niongee nae.. maisha yanakaba..😂😂
Maswali ya kijinga yakijibiwa vizuri
Haya ndiyo majibu mazuri😁😁👇👇👇👇👇👇👇👇
Q: Umenyoa nywele?
A: *Hapana, nimebadilisha kichwa.*
Q: Hiyo simu umenunua?
A: *Hapana nimeitengeneza mwenyewe.*
Q: Utakula mboga na nini?
A: *Mdomo*
(Simu inaita usiku,then aliyepiga anauliza) Q: Nimekuamsha?
A: *Hapana nilikuwa naota jua hapa nje.*
Q: Gazeti la leo linasemaje?
A: *Sijaongea nalo.*
Q: Gari limejaa, nitakaa wapi?
A: *Usijali dereva anashuka kituo kinachofata utapata kiti.*
Q: Hiyo ni ajali?
A: *Hapana ni driver ameamua kupark gari upside down* .
Q: Umepause movie?
A: *Hapana wamechoka kuact wanarest.*
😂😂😂😂😂😂
🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂🏃♂
Angalia kilichonikuta nilipoenda kwa mganga
Usije ukaenda kwa mganga, mwenzako yamenikuta, yani masharti niliyopewa, acha tu,
yalikua hivi:-
1.Jasho la nyoka.
2.Manyoya ya mende.
3.Sisimizi Shoga.
4.Mbwa mjane.
5.Kuku aliye single.
6.Samaki mwenye miaka miwili bila kuoga
7.Mti wenye ujauzito.
8.Mbavu za Nzi.
9.Nywele za Kiroboto.
10.Mwanya wa Mbu.
Duuh..!! mwanangu kwa hali hii mbona itakula kwako.
Wengine wanasemaga
IGA UFE! Rizik anagawa Mungu tu shetan simuelew!
Cheki hawa washikaji wanachokifanya baada ya kuvuta bangi, Bangi si mchezo
Kuna washikaji walikuwa wakivuta bangi… kiberiti kikawaishia… wakamtuma mwenzao akatafute kingine… bangi lilikuwa limemkolea… akazungukazunguka hatimaye akarudi palepale kijiweni…
MSHIKAJI: oyaaa wanangu eeeh… niazimeni kiberiti mwanangu mwenyewe …..
WENZAKE: baharia ee subiria kimtindo kuna mwana tumemtuma akatafute kiberiti.
Sio kwa wivu huu
Wanawake nilianza kuwachukia tokea shule ya msingi.
Ni pale mwanamke wangu aliponiacha na kwenda kwa jamaa mwenye kichongeo kipya …inauma sanaa…
WANAWAKE SIO WATU WA MCHEZO MCHEZO ASEEE Bac tuu
Angalia huyu jamaa alivyomuweza huyu binti wa chuo
😁😁😁😁 .. TABU KUDATE NA MADEMU WA CHUO
Demu ; Baby Safari Hii Nataka Pale Hostel Niwafunike Mashoga Zangu Wote.
Jamaa ; Poa Sweetie Ondoa Shaka Nitakununulia #Turubai Utawafunika Wote…!!!
Demu: Mxiuuuuuuuu Lione Sura Kama Goti La mbuzi Na Namba yangu futa Nakublock Mpaka Sanduku la posta…!!!
😂😂😂😂nmecheka adi nmelazwa
Jinsi Mapenzi yanavyoweza kukupa stress
Mapenzi ni balaa
Mapenzi ujue yanawez kukupa stress adi mama ako akikuuliz what’s wrong🤔-—unawez kumjib MAMA WE BADO MDOGO UWEZ ELEW🤣🤣🤣
Wanaume ni noma, Angalia huyu alivyomdanganya huyu 👧 girlfriend wake
Jamaa kamdanganya girlfriend wake kuwa anasomea HOTEL MANAGEMENT. Siku huyo girlfriend akamkuta jamaa anaosha vyombo kwa MAMA NTILIE.
Girlfriend akamuuliza jamaa “beby vipi mbona uko hapa?” Jamaa bila woga akajibu “NIPO FIELD.
Wanaume hatupendi ujinga sisi 😠😠😠
Kali za leo: Misemo ya kuchekesha na kuvunja mbavu
1. Ati wee ni m-black mpaka ukiingia kwa dinga(gari), dirisha zinakuwa tinted!
2. Kwenu kuchafu mpaka mende zinatema mate.
3. Vile wewe mfupi, ukipiga picha ya passport inatokea full.
4. Ati(house) yenu ina gate lakini hakuna fence.
5. Baba alienda ku buy ngombe akaona ikikojoa akasema sitaki hiyo imetoboka.
6.Wee mblack mpaka ukikutana na mzungu afternoon anakusalimia: Good evening.
7. Mko wengi kwa house mpaka kuna rush hours na kukinyesha kunakuwa na jam.
8. Paka yenu noma mpaka ikishika panya inaomba chumvi, fork na pilipili.
9. We ni mrefu mpaka ukikunywa maziwa inafika kwa tumbo ikiwa mgando.
10.Wewe ni mweusi ukikanyanga makaa unawacha footprint nyeusi.
11. Kwenyu mkikunywa maji mnaitisha toothpick
12. We ni mbishi hadi ulikataa kuzaliwa uchi
13. Kwenu kuna insecurity ikifika usiku hadi geti mnaingiza ndani
14. Kwenu ni wengi sana hadi mmeweka round about ndani.
15. Wewe ni mlafi hadi maji uliyochemshia mayai unayafanya supu.
16. We ni mjinga sana hadi blood test ulifeli.
17. Una chogo refu hadi ukigeuka haraka unaweza kuliona.
18. Una kichwa kikubwa hadi ukiingia kwenye daladala konda anakwambia “abiria usiingie na mizigo, tunaweka juu kwenye carrier
Misemo 10 bora ya kuchekesha itakayokuacha mdomo wazi
1. Mwanaume hata awe bahili vipi, hawezi kumpa mwanamke mimba nusu.
2. Hata uwe na magari mangapi chooni utaenda kwa miguu.
3. Kama ubinadamu kazi mbona hatupewi mishahara?
4. Ukichanganya wali na choroko unapata mseto, lakini hautibu malaria.
5. Hata njiwa nae ana makinda, lakini hawezi kuwa spika wa Bunge.
6. Hata uwe na haraka vipi kwenda Zenj, huwezi kupanda Jahazi ya Yusuph Mzee.
7. Umeme hauna kiuno lakini unaongoza kwa kukatika.
8. Hata uwe kauzu vipi, huwezi kujamba wakati unatongoza.
9. Hata uwe na imani kali vipi, huwezi kusali wakati unafanya mapenzi.
10. Hata kizibo ni mfuniko lakini hauwezi
kufunika sufuria.
Hii ndiyo sababu ya kumfanya huyu jamaa kujiita fara
MZEE:”sasa huyu mgeni sijui alale wap?”
MKE:”saa hizi ni usiku akalale na Bebi.”
jamaa akaona huyo Bebi pengne mtoto anakojoa kitandani au akalia asije msumbua usiku
JAMAA:”msipate tabu mi ntalala hapa kwenye kochi” akalala
asubh wanakunywa chai akaibuka mrembo,jamaa akapigwa bumbuwazi almanusra ajimwagie chai.
BINTI:”Naitwa BEBI,we unaitwa nani?”
Jamaa akasema mimi naitwa Fara…..!
Dunia ina mambo! Angalia kilichotokea baada ya mgonjwa kuwekewa macho ya paka
Kuna jamaa alipata ajali akapofuka macho👀, akaenda hospital akawekewa macho ya paka🐈🐱,
dokta akamuuliza: vipi saizi unaona?
jamaa: naona ila naona panya tu
👀🐀🐁🐀👀
Recent Comments