Vihoja Vya Kimjin Mjini
Angalia alichokifanya huyu mkaka alipoenda benki 🏦
At the bank..
Teller: Hii pesa ni fake
Mkaka: Shida iko wapi..pesa ni yangu..account pia ni yangu..weka tu!!!😂😂😂
🏃🏃🏃🏃
Kilichompata sista duu bishoo wakati akijidai kununua pete
Mwanamke mmoja aliingia duka la vito vya thamani, akaona pete moja ya dhahabu nzuri sana amabayo ilikuwa kwenye shelf ya chini, wakati anainama apate kuitazama vizuri kwa bahati mbaya (au nzuri!), shuzi likamtoka- druuuuuu, soni ikamuingia huku akigeuka haraka kuangalia kama kuna yeyote dukani pale ameliskia shuzi lake, macho yakagongana na mwenye duka ambaye alikuwa karibu huku uso ukiwa umejaa tabasamu zito, mwana mama hakuwa na uhakika kama amesikika au hakusikika, akaona atumie nafasi ile kuyeyusha…Akauliza “Hii pete bei gani?” . Jamaa mwenye duka, huku akiangua kicheko, akajibu “Umeiona tu umejamba, je nikikuambia bei yake si utakunya kabisa?”
Duh! Angalia alichokula huyu mwizi! Wizi mwingine bwana!
Baada ya mwizi kuvunja mlango huko Tarime, akaingia kwenye stoo akaona vinyama kwenye bakuli vikiwa vimekauka. Akaonja 1 akaona kitamu na kina chumvi! Akavila vyote. Alipomaliza akaangalia juu ya mlango akaona pameandikwa; “chumba cha UKEKETAJI WANAWAKE”. Unafikiri atakuwa amekula nini?
Huyu mama mkwe kazidi sasa
Eti kuna mkaka alitembelewa na mama yake mzazi. Wakiwa sebuleni yeye, mama na mke wake, mke wake akaanza kuonekana tofauti kama vile anajiskia vibaya. Akaenda chumbani. Baada ya muda mfupi yule mkaka akamfuata. Wakakaa sana huko kisha mkaka akarudi sebuleni kuendelea kuongea na mama yake. Lakini zipu ya suruali yake ilikuwa wazi. Mama akamuuliza, mkeo anaendeleaje? Akamuambia, anajisikia vzr sasa. Nimempa panadol. Mama akatabasamu na kumwambia mwanaye, sawa. Lakini siku nyingine ukishatoa panadol ukumbuke kufunga pharmacy😂😂
Madenge hakosi visa. Soma hii
MADENGE
HAKOSI
VISA
baada ya kumaliza form four baba akamwambia achague zawadi yoyote aipendayo
MADENGE: naomba pesa nikamuoe bibi maana siku nyingi amekuwa akiniita mchumba wake.
BABA: Shenzi, yule ni mama yangu mzazi huwezi kumuoa.
MADENGE: Mbona wewe umemuoa mama yangu mzazi sijasema kitu ww inakuuma? lazima nilipize kisasi ikikuuma muache mama yangu kila mtu akae na mamayake. 😂😂😂
Kali za leo: Misemo ya kuchekesha na kuvunja mbavu
1. Ati wee ni m-black mpaka ukiingia kwa dinga(gari), dirisha zinakuwa tinted!
2. Kwenu kuchafu mpaka mende zinatema mate.
3. Vile wewe mfupi, ukipiga picha ya passport inatokea full.
4. Ati(house) yenu ina gate lakini hakuna fence.
5. Baba alienda ku buy ngombe akaona ikikojoa akasema sitaki hiyo imetoboka.
6.Wee mblack mpaka ukikutana na mzungu afternoon anakusalimia: Good evening.
7. Mko wengi kwa house mpaka kuna rush hours na kukinyesha kunakuwa na jam.
8. Paka yenu noma mpaka ikishika panya inaomba chumvi, fork na pilipili.
9. We ni mrefu mpaka ukikunywa maziwa inafika kwa tumbo ikiwa mgando.
10.Wewe ni mweusi ukikanyanga makaa unawacha footprint nyeusi.
11. Kwenyu mkikunywa maji mnaitisha toothpick
12. We ni mbishi hadi ulikataa kuzaliwa uchi
13. Kwenu kuna insecurity ikifika usiku hadi geti mnaingiza ndani
14. Kwenu ni wengi sana hadi mmeweka round about ndani.
15. Wewe ni mlafi hadi maji uliyochemshia mayai unayafanya supu.
16. We ni mjinga sana hadi blood test ulifeli.
17. Una chogo refu hadi ukigeuka haraka unaweza kuliona.
18. Una kichwa kikubwa hadi ukiingia kwenye daladala konda anakwambia “abiria usiingie na mizigo, tunaweka juu kwenye carrier
Angalia kile kitabia cha kufuta namba kwenye simu kilivyomponza huyu jamaa
Jana nilijipa kazi ya kufuta vitu visivyo na umuhimu kwenye sm yangu. Katika futa futa si nimefuta namba ya bosi wangu. Halafu boss mwenyew wa kike. Mida ya Saa mbili usiku nikawa chumbani kwangu. Mara simu ýäñgù ikawa inaita. Kucheki namba ngeni. Nikapokea baada ya salamu. Me→nani mwenzangu?? Boss→we hunijui me ?? Me→usinijbu swali kwa swali Nita kublacklist sasa hiv. Sipendagi ujinga.. Kwa sasa nazurura tu mtaani na roba langu La machupa
Huyu kashauzwa!! Angalia kilichomkuta sasa
Jamaa alionekana Mnyooooonge sana ikabidi mpita njia amuulize…
Kaka, mbona u mnyonge hivyo?”
Jamaa : ‘aaaaah we niache tu, kuna rafiki yangu nimemkopesha laki tano akafanye PLASTIC SURGERY ya uso, Mwanaharamu sasa nashindwa kumtambua!!!
😂😂😂😂😂😂
Mipango ya mke na mume ya pasaka
Mke: Unampango gani na pasaka hii mmewangu..
Mume: Nitafanya kama yesu..
Mke: Unamaanisha Nini?
Mume: Nitaondoka ijumaa na Kurudi j3..
Mke: Unanishangaza, kama utafanya hivi nami nitafanya kama Maria..
Mume: Unamaanisha Nini?
Mke: Nitapata mimba bila ya kuingingiliwa na wewe mume wangu..
Mume: 😳😳😳
😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Cheki nilichomfanyia boss wangu
Bosi wangu karudi safari yake kutoka serengeti..! Si akanitumia picha, lakini ilikuwa network yenyewe tabu.. kwahio picha haikufunguka na kwa vile niliona itachelewa kufunguka na ataona sikumjibu basi nami..
Nikampelekea msg nikamuandikia umependeza saana bosi mashaallah…!!
sasa baada tu ya kumfika msg.. na huku picha ikafunguka kumbe picha ya Sokwe..!!
Basi Kaniambia kesho niende ofsini kwake kuna barua yangu..
Nahisi hyo barua ina pesa, hapa cjalala, nmekosa usingizi kabisa,nawaza ninunulie nn hyo pesa.Na kesho asubuhi sa 12 asubuhi atanikuta ofisini kwake naisubiri barua, sipendagi ujinga mimi.
Omba omba sio barabarani tuu
Boy:- baby ivi nikifa utakuja msibani?
Girl:-ntakuja ukinitumia nauli.
Hapo ndo unagundua kuwa sio kila omba omba yuko barabarani.
🤒🤒🤒🤒🤒🤔
Soma hii, Nani haelewi kati ya hawa?
Dogo: Bro naomba nitumie hela.
Bro: Tumia tu mpaka uchoke.
Dogo: Hujanielewa,nitumie hela.
Bro: We ndo hunielewi, nimesema tumia tu…!!!
Haya ndiyo madhara ya kulala kanisani
Tukiwa kanisani mdada alikuwa amelala , akaamka akasikia Pastor anasema
” SIMAMA”
Yule dada akasimama akashangaaa kanisa zima linamtizima kwa mshangao akiwemo mumewe, akaangalia kanisa zima akashtuka kujiona yeye peke yake ndiye aliesimama
Pastor akaendelea vizur endelea kusimama, tumepata mmoja hadi sasa aliyesimama narudia kwa mara ya mwisho kama hujasikia vizuri
” kama wew umewahi kumsaliti au bado unasaliti ndoa yako SIMAMA”
Binti akazimia
Hizi swaga za huyu jamaa ni shida, Google!
Jamaa alikuwa kwenye daladala pembeni kuna
dada mrembo kakaa. Kamlia timing kwa muda
kisha halafu akamuuliza “Samahani dada
unaitwa Google?”.
Dada: “hapana, kwanini umedhani naitwa
hivyo?”. Jamaa: “Una kila kitu nnachokitafuta
“😅😃😃😃😃😃😃😃😃😃
Jee wajua! Maajabu ya whatsapp..
JE WAJUA?
Je wajua kwamba kuku wa kwenye Whatsapp anamzidi tembo ukubwa? 🐓👉🏽🐘.
😂😂😂Maajabu!
Mke alichomfanyia mme wake kabla ya kwenda safari, Chezea mawaifu walokole wewe!
JAMAA alimuaga mke wake mlokole kuwa anaenda semina ya siku tatu, kumbe anakwenda kwa bi mdogo.
Mke akamwambia mumewe; “Tupige magoti tusali”,
Wakapiga magoti…:
MKE: Eee baba msaidie mume wangu afike salama safari yake.
MUME: Emen…
MKE: Mpe nguvu katika yote atakayoyafanya huko.
MUME: Emen…
MKE: Akitaka kufanya uasherati ashindwe.
MUME: Kimya…
MKE: Akifanya uasherati apatwe na janga baya kwa uwezo wako bwana.
MUME: …….!!
MKE: Yaani akifanya uasherati afie hukohuko kwa mateso makali.
MUME: Maombi gani sasa hayo!!?. Haya basi siendi semina ufurahi wewe.
Chezea mawaifu walokole wewe!
Huyu dogo nimsaidieje? Cheki alivyojichanganya
Nimekutana na dogo mmoja hivi hapa analia,namuliza analia nin??ananambia ”ALIPEWA MIA TANO ZIPO MBILI,MIA TANO MOJA YA NYANYA na MIA TANO NYINGINE YA VITUNGUU sasa KAKOSEA KAZICHANGANYA HAJUI TENA IPI NI YA NYANYA na IPI NI YA VITUNGUU!!!
.
.
NA PESA ZOTE ANAZO KAZISHIKA MKONONI,
Duh! Hii sababu ya huyu mwanaume kulewa ni shida
👧: “Mpenzi, nakuomba uache kulewa”
👨: “poa, na wewe acha kutumia make up”
👧: “Mimi napaka make up ili unione mzuri”
👨: “Na mimi nalewa ili nikuone mzuri”
Vodka hatareee😂😂
Maisha ya Pwani ni Shidaaaaah
😆😆 😂😂😂😂😂😂 Jamaa kagombana na mkewe, akasusa kula🍽🍨 kurudi kazini kamkuta mkewe amevaa kanga imeandikwa ukisusa wenzio wala ilipofika asubuhi mke akavaa kanga imeandikwa ukitoka 🚶🚶mwenzio anaingia💃💃
jamaa akagoma kwenda kazini 😬😬 mke akabadili kanga na kuvaa iloandikwa nimemdhibiti ndo mana hatoki🚷 jamaa akaenda kuomba ushauri kwa rafiki yake akaambiwa twende nyumbsni kwako, walipofika walimkuta mke kavaa kanga imeandikwa ulidhani rafiki yako kumbe adui yako🤔🤔 jamaa akaamua kusafiri siku tano ili kupunguza hasira. Aliporudi akamkuta mke amevaa kanga imeandikwa ni bora nimpe jirani kuliko kiozee ndani
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
hata kama hupendagi ujinga kwa maneno ya kwenye kanga utasanda tu
Recent Comments