SMS Nzuri: Meseji za Vihoja Vya Katikati Ya Juma
Ziara za kushtukiza zinachekesha sana
Mimi Nimecheka sana
ππππππππππ
ZIARA ZA KUSHTUKIZAππ
Mimi ni msomaji mzuri wa magazeti, na msikilizaji mzuri wa redio, huwa naangalia luninga mara chache sana kama nikibahatika kupita mahala kuna luninga. Sasa wiki hii nimesikia mengi kuhusu hizi ziara za kushtukiza za viongozi wetu, nikaona hili ni jambo zuri tena linafaa kuigwa na sisi wananchi wapenda maendeleo. Nikaona nijipange na mimi nifanye ziara kadhaa za kushtukiza katika sehemu mbalimbali zinazonihusu.
Nikaona nianze na ziara ya kushtukiza pale shuleni kwa huyu mwanangu, maana kila siku anakunywa chai na kuondoka na daftari zake na mie sijawahi kwenda shuleni kwao toka nilipomuandikisha shule mwezi Januari. Nilifika shuleni na kumuona mwalimu mkuu, ambae alianza kutetemeka nilipomuambia kuwa nimekuja pale kwa ziara ya kustukiza, sijui alidhani mi ni mmoja wa Mawaziri wapya, maana nilimuona jasho linamtiririka ghafla. Akanikaribisha ofisi yake iliyokuwa na vitabu kila kona, na kuita waalimu wote na kunitambulisha kuwa ni kiongozi nimekuja kwenye ziara ya kustukiza.
Nilipojitambulisha kuwa ni mzazi, waalimu wote nikawaona waanza kupumua kwa raha. Nikawaambia kuwa mimi nina mwanafunzi pale na nilikuja ziara ya kustukiza kujua maendeleo yake. Baada ya mwalimu mkuu kusaka jina la mwanangu nae akanambia, βMzee huyu mtoto hajaja shule mwezi wa tatu sasa, tulijaribu kukutafuta ikashindikana, hatujui yu wapiβ Jasho likaanza kunitoka mimi, yule mtoto kila asubuhi nampa nauli anaenda shule, na mara nyingi ananiomba michango kumbe hata shule haji. Niliondoka bila kuaga presha ikiwa juu.
Nikaona niende kwenye genge la mke wangu nae nikamfanyie ziara ya ghafla nimhadithie mambo ya mwanae, nilipofika pale nikakuta kuna mdada mwingine anauza genge. Nikamsalimu, na kumuuliza mwenye genge ntampataje, jibu lake lingeniua kama ningekuwa si mkakamavu, βMume wake kaja kumchukua na gari wameenda kununua shamba Bagamoyoβ. Nikaondoka nimechanganyikiwa, nikajuwa hapa dawa yangu moja tu, nayo ni Sabrina, mtoto wa Kinyaturu pale ambapo nikipata maudhi huwa naenda kubembelezwa.
Nikatwanga mguu kwa Sabrina nae nikamfanyie ziara ya ghafla ili anipoze moyo. Nilipogonga mlango wa chumba chake akatoka mbaba wa miraba minne, akanisalimia kwa upole, βSalama kaka unasemaje?β Jibu likanitoka βSamahani mie nilimkopesha huyu dada wa chumba hiki vitenge, nilikuja kuuliza kama ameshapata hela yanguβ Ziara za kushtukiza zinataka moyo wa chuma jamani
Hiki ndicho kifo mbele ya Mwanamke
Hiki ndiyo kifo.
KIFO NI NINI..
Kifo ni pale girlfriend wako anapofanya fujo Club akiwatukana MABAUSAΒ Huku akisema
“BABY WANGU HATA HAWAOGOPI”
ππππ
Watu wana vimaneno
Eti linalo jamba ni tumbo makalio ni spika tu
Dah!!
Nimecheka hadi basi leo
πΈπΈπΉπΉ
Cheki huyu jamaa anachomfanyia huyu mrembo kanisani
Jamaa kaenda kanisani akakaa karibu na mrembo.
Wakati mahubiri yakiendlea jamaa akaanza kuingiza vocal:
Jamaa: dada mi nakupenda saana
Dem: Kaka naomba umsikilize mchungaji
Jamaa: nipe nafasi uwe msimamizi wa serikali ya moyo wanguβ¦
Dem: niacheβ¦
Jamaa: kweli nakupenda mpnz
Dem: (kwa sauti kubwa) nmesema NIACHEEEE!!
Watu wote kanisani wakageuka⦠Jamaa kaona noma na ili atulize msala
Jamaa: sikuachi hadi ukiri YESU kuwa Bwana na mwokozi wa Maisha yako.
Angalia huyu baba alichowafanya mtoto wake wa kike na boyfriend wake
BABA OYEEEEEEπͺπͺ
Soma hiiβ¦
Msichana alikuwa amekaa na baba yake kibarazani, mara akamuona MVULANA friend wake akija, yule mvulana alipokaribia tu, yule msichana akamwambia hivi:-
MSICHANA: Umekuja kuchukua kile kitabu chako, kinachoitwa “DADDY IS AT HOME?” by Ngozi Okafor
MVULANA: Hapana!, Nimekuja kuazima kitabu cha maombi kama kinaitwa “WHERE SHOULD I WAIT FOR YOU?” by NgΕ©gΔ© wa Thiong’o
MSICHANA: Aaah! Hicho sina ila ninacho kimoja kinaitwa “UNDER THE MANGO TREE” by Chimamanda Adichie
MVULANA: Ooh! Vizuri, Basi usisahau kuja nacho kesho kitabu cha Okot p’Bitek kile kinachoitwa “CALL ME IN 5 MINUTES BEFORE” Utakapokuja shule.
MSICHANA: Usijali, tena nina kitabu kipya kinaitwa “I WON’T LET YOU DOWN” by Chinua Achebe
Baba mtu akawatazama kisha akasema
BABA: Vitabu vyote hivyo, mbona vingi sana, atavisoma vyote kweli
MSICHANA: Ndio Daddy, huyu mvulana yupo smart sana na ana akili atavisoma vyote hivyo!
BABA: Sawa! Usisahau kumpatia na kile ambacho nimekiweka pale juu ya meza, kinaitwa “I AM NOT STUPID, I UNDERSTOOD EVERYTHING YOU’VE BEEN SAYING” by Shakespeare!
Na kuna kingine nimekiweka juu ya kabati la vyombo, kinaitwa “IF YOU GET PREGNANT PREPARE TO GET MARRIED” by Wole Soyinka.
Cheka kidogo: Majibu ya mhindi kwenye mtihani wa Kiswahili alipoambiwa ajibu methali
Mhindi kwenye mtihani wa kiswahili anaambiwa amalizie methali:
(a)Nyani haoniβ¦..valisa miwani!
(B)Debe tupuβ¦.weka dengu!
(c)Masikini akipataβ¦.iko acha iba!
(d)Penye kuku wengiβ¦chinja bili,tatu!
(e)Asiyesikia la mkuuuβ¦.peleka yeye polisi!
(f)Penye wengiβ¦β¦iko kutano ya chadema!
Bangi si mchezo, Angalia kilichowakuta hawa
Bangi si mchezo!
Jamaa kaikoleza si ikamtuma avue nguo!
Akavua nguo zote akaenda kwenye kioo, kujitazama akaona kama kavaa suti!
then akaenda kama alivyo zaliwa kwa masela wenzake akawauliza vp suti imenikaa? Mvuta bangi mwenzie akamwambia “imekutoa kinyama ila tai umeifunga chini sana”.
Angalia huyu mgonjwa
Mngojwa: daktari Nina tatizo la kusahausahau kila dakika.
Daktari: hilo tatizo lilianza lini?
Mngojwa:tatizo lipi?
πππππππ
Ujinga wa ndoto ndio huu
πUjinga wa ndoto ndiyo huu
β’β’Utaota umeokota dolla ukiamka emptyβ¦
β’β’Utaota umeokota dhahabu ukiamka kitandani patupu daadeeki OTA Sasa UMEKOJOAβ¦..
ππππππ
Angalia ndoto nyingine zilivyo na Majanga
Ndoto zingine bwana usiombe zikupate
Mimi usiku wa kuamkia Leo nikiwa nimelala nimeota naendesha gari Yangu aina ya BMW mpya Mara gafla ikakwama kwenye tope .hivyo ikabidi nishuke ili kuisukuma loh! Yani kudadeki ile kuamka nikakuta nimesukuma kitanda hadi sebleni Daaa ilinisikitisha sana jiangalie sana sese hivi ndio narudisha kitanda chumbani .angalizo angalia ndoto unazo ota unaweza kuota upo baharini ukaamka unajikukuta unaogelea kwenye Jaba la Maji shauri yako.
Duh, hii sasa kazi
Wakati unafikiria dingi yako afe ili urithi nyumba, dingi nae anafikiria uanze kufa ili apangishe chumba unacholala.. hiyo inaitwa kufa kufaana.. πππππππππ #Hatutaki ujinga
Duh, huyu mama alichokifanya
Mke:Β Naelekea london, nikuletee zawadi gani?
Mume:Β kitu gani unaweza niletea wewe?
Mke:Β we omba Alafu utaona.
Mume:Β Niletee msichana wa kizungu.
Mke:Β (mke akaendaLondon na kurudi)
Mume:Β zawadi yangu iko wapi?
Mke: Subiri ndani ya miezi 9!!!! ππππππππ
Pia Wamama hawapendi ujinga
Misemo ya kina dada
Misemo ya kina dada
walianza na halohalooo!
Wakaja unalo babu weee!
Ikafuata utajijuuu!
Ikafupishwa utajiJJ!
Mara ghafla kantangazeee!
Haikukaa sana kansajiriii!
Ikatoka nyingine nishiiiiida!
Unaijua iliyotoka Leo?
Heh! Heh! Heeeh! MB zenyewe 8 nikudownload unanini?
Angalia kilichonikuta nilipoenda kwa mganga
Usije ukaenda kwa mganga, mwenzako yamenikuta, yani masharti niliyopewa, acha tu,
yalikua hivi:-
1.Jasho la nyoka.
2.Manyoya ya mende.
3.Sisimizi Shoga.
4.Mbwa mjane.
5.Kuku aliye single.
6.Samaki mwenye miaka miwili bila kuoga
7.Mti wenye ujauzito.
8.Mbavu za Nzi.
9.Nywele za Kiroboto.
10.Mwanya wa Mbu.
Duuh..!! mwanangu kwa hali hii mbona itakula kwako.
Wengine wanasemaga
IGA UFE! Rizik anagawa Mungu tu shetan simuelew!
Ulevi noma! Angalia huyu mlevi alichomfanyia huyu jamaa usiku! Ungekua wewe ungefanyaje?
Jamaa alikuwa amelaa na mkewe saa tisa ya usiku akastuka baada ya kusikia mtu anabisha hodi kwenda kufungua mlango
Akamkuta jamaa kalewa sana mlangoni kwao
JAMAA: Nini tena mheshimiwa kuamshana saa hizi?
MLEVI: Naomba uje unisukume.
Jamaa akiamini kuwa pengine kuna gari la huyu mlevi limezima jirani akamwambia subiri nikavae viatu. Baada ya kuvaa viatu akatoka na wakaanza kusindikizana na mlevi. Mlevi akaongoza njia
mpaka kwenye mabembea ya jirani akakaa kwenye bembea moja na kumgeukia jamaa na kumwambia.. Okay nisukume basi.
Nani Mkali Hapa kati ya DEMU na MSHIKAJI?
“MAENEO FLANI ya KISHUA”
-Mshikaji kamwona demu mkali
anakatiza kitaa akamkubali akaamua
amfuate amtemee cheche
MSHIKAJI- mambo dada?
DEMU- pouwa
MSHIKAJI-
umependezaa!!!
DEMU- asante.
MSHIKAJI- unaweza ukanisaidia
namba
yako ya simuβ¦β¦..
maana duh
nmekukubali
kinyama.
Demu baada ya kuambiwa vile
akazama kwenye pochi lake akatoa
noti ya
sh.10000 akaandika namba yake
kwenye
noti akampa mshikaji.
Mshikaji kapokea ile noti kachana
sehem
iliyoandikwa namba halafu
kamrudishia
Demu noti yake..!!!
NANI ANA DHARAU
NA NANI JEURI..
DEMU AU MSHIKAJI??!
Majibu ya mkato ya kuchekesha Kutoka Kenya
Njeri:Β Roysambu ni ngapi?
Makanga:Β Roysambu ni moja tu. Pengine kama Chinese wamejenga ingine.
Odhis:Β Hii gari haina watu bana.
Makanga:Β Kwani hao wawili wenye wamekaa hapo ndani ni ngβombe?
Man:Β Wekeni nyimbo za Yesu tafadhali.
Makanga:Β Yesu bado hajatoa album. Akitoa tutaeka.
Mwikali:Β Excuse me condaβ¦gari za Mwingi zinapandiwa wapi?
Makanga:Β Ziliacha kupandwa juu hazimei.
Man:Β Kwani mwisho wa gari ni wapi?
Makanga:Β Mwisho ni hapo penye number plate iko.
Karis:Β Ruaka ni how much?
Makanga:Β Sijaskia Ruaka ikiuzwa. But nikiskia nitakwambia.
Passenger:Β Shukisha dere.
Makanga:Β Tukishukisha dere utaendesha gari?
Johnny:Β Maze, hii gari iko na joto sana.
Makanga:Β Basi shuka upande fridge
Angalia wanachokifanya Zuzu na msichana chumbani kwenye giza
Zuzu: Mambo Anna!
Anna: Poa!
Zuzu: Kuna kitu nataka nikuonyesheβ¦
Anna: Kitu gan?
Zuzu: Twende chumbani kwako (wakaenda)
Anna: Haya nionyesheβ¦
Zuzu: Funga mlango na madirisha kwanza (akafunga)
Anna: Haya nionyeshe sasa!..
Zuzu: Zima taa kwanza (akazima)
Anna: Mhmβ¦nionyeshe sasa!
Zuzu: Haya njoo hapa kitandaniβ¦
Anna: Ok, nionyeshe!
Zuzu: Ona nimenunua saa ambayo inawaka yenyewe gizani⦠Acha mawazo mabaya ww???
Recent Comments