SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Ujumbe kwako wewe mwajiriwa au uliyejiari

Kama umeajiriwa au pia umejiajiri ni mojawapo ya njia zinazokuingizia kipato maana wengi wanaanzia hapo mpaka kuja kufikia kule wanakohitaji.
Ila kuna maswali machache ya kukupa changamoto ambayo nataka ujiulize:-

Kwako muajiriwa

👉🏿Umeshawahi kujiuliza huo mshahara unaolipwa unakutosha kukutimizia Yale yote unayohitaji maishani mwako??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza ukifukuzwa au ukipunguzwa kazini utafanya nini?

👉🏿Umeshawahi kujiuliza ofisi au kampuni unayofanyia ikifilisika wewe utafanya nini?

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unataka kuhama au kuacha kazi hapo unapofanyia uende ofisi nyingine??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwanini hupapendi hapo unapoishi lakini bado unaendelea kuishi hapo?

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini huo usafiri unaoutumia huupendi lakini kila siku unautumia huo huo??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza ni kwa nini wanao au watoto wako hawapendi shule wanayosoma lakini wewe uwezo wako ndipo ulipoishia??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini hupendi mikopo lakini bado unaendelea tu kukopa??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza unaipenda kwa dhati tena kutoka moyoni kazi unayoifanya??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unaomba kila Mara kuongezewa mshahara kama sio kuandamana??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unatamani ukasome uongeze elimu??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini mkubwa wako kazini hataki uache kazi au ukasome au uhamie ofisi nyingine??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini kila siku uko “busy” kazini au ofisini mpaka unakosa muda wa kufurahia na ndugu,jamaa,na marafiki na familia na mifuko yako au akaunti yako benki haiko “busy”??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unataka kufungua kibiashara chako au unataka ufanye kilimo Fulani kwa sababu umesikia kinawatoa watu???

👉🏿Umeshawahi kujiuliza usipokwenda kazini kwa muda Wa wiki au mwezi au mwaka je kipato hicho hicho unachokipata utaendelea kukipata??

Hebu jiulize hayo maswali na mengine mengi yanayofanania na haya ujaribu kuona kama majibu yake unayo na kama majibu yapo ni njia gani unatumia au unategemea kutumia ili kuondokana na hayo??

Kwako wewe uliyejiajiri

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini biashara yako haikui kwa muda wote huo uko pale pale??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unataka uachane na hiyo biashara ufanye nyingine??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini kila kitu unafanya wewe mwenyewe haumruhusu msaidizi kuwepo??

👉🏿Kwa nini huthubutu kumuachia mtu biashara yako kwa muda tu ukiondoka unafunga??

👉🏿Kwa nini unawaumiza wengine au wengine wanaumia ndipo wewe utengeneze faida yako??

👉🏿Kwa nini huwezi kuwasaidia wengine waweze kutengeneza kipato kama chako??

👉🏿Kwa nini akija mwenzako pembeni yako kufungua biashara kama yako unachukia???

👉🏿Kwa nini unachukia kulipa kodi ya pango lakini inakubidi tu ufanye hivyo??

👉🏿Ni watu wangapi wanaichukia au kuipenda biashara yako??

👉🏿Wangapi wanakuongea vizuri au vibaya kutokana na Huduma yako unayotoa??

👉🏿Kwa nini unatamani usiwe unalipa kodi??

👉🏿Kwa nini hupendi kuwaonyesha wengine njia unazotumia katika kuijenga biashara yako??ikiwa ni pamoja na upatikanaji Wa mizigo,unavyouza na unavyopata Wateja??kwa nini?

👉🏿Kwa nini hupendi kuona aliyeanza nyuma yako akifanikiwa kabla yako??

Hayo ni baadhi ya maswali ya kujiuliza wewe kama mjasiriamali au uliyejiajiri ingawa yapo na mengine unaweza kujiuliza tu uone kama utapata majibu yake na yawe ya kueleweka

Angalia kilichompata huyu mwanafunzi kilaza anayejiamini

Teacher: Who is a pharmacist?

Shemdoe raised up his hand.

Teacher: So it’s only Shemdoe that can tell who a pharmacist is in this class? So there is no body else to answer the question except Shemdoe? (There was no reply from the students)

Teacher: Ok now Shemdoe, chukua hii fimbo, charaza vilaza hawa wote kila mmoja viboko kumi…. Shemdoe akiwa amevimba kichwa, akawatwanga viboko kumi kumi vya kushiba darasa nzima

Teacher: Now, my dear Shemdoe tell this dumb students who a pharmacist is…

Shemdoe: Yes, sir. A Pharmacist is a farmer who assists people. Shemdoe saiv amelazwa MOI kwa wataalam wa mifupa 🏃

Stori za simu za wavulana na wasichana

STORY ZA WASICHANA KTK SIM

Mary… Hallow mpenzii
Lily…. Niambie my dear
Mary..Pouwaa za siku jamani
Lily…Nzuri rafiki Yangu wa damu
Mary…Jioni nakuja kwako tule Na
kunywa japo wine wanguu
Lily…Nakusubiri kwa hamuu
mpenziiii

BAADA YA KUKATA SIMU…KILA
MMOJA ANAWAZA

Lily…Huyu mchawi wa kike Leo
anataka kuja kwangu wala hanikuti.
Mary..Hahahahaaaa Uwiiiiiiiiii huyu
kahaba eti nakusubir Kwa hamuu
nani aende!!!

STORY ZA WAVULANA KATIKA SIMU

John…Niaje we mbwaa
Sam…Pouwa kichaa wanguu
John..Upo wap mpumbavu wewe
Sam…Niko hom, we fala Uko wap?
John..Baadae nakuibukia jambaz
langu tukale bata
Sawa… Pouwaa we ms**nge
nakusubiri

BAADA YA KUKATA SIMU…KILA
MMOJA ANAWAZA

John…Dah baadae nikakae na
mwanangu Sam sijamuona long
time
Sam…John bwana akiwa Na pesa
lazima anitafute mwanaeee.

FUNZO..

Baadhi ya Wasichana
hujifanya wanapendana Kwa
maneno lkn ni Kwa nje tu!! lkn
WANACHUKIANA
WAVULANA unaweza Kudhani
hawapendani Kwa Maneno lkn
WANAPENDANA..

Mpe TANO mchizi wako kudumisha upendo wetu wavulana…
High 👊👊👊👊👊 boys

hiyo apo

Vitu ambavyo mama mjamzito hapaswi kutumia

Vipo vitu mbalimbali ambavyo mama mjamzito hapaswi kuvitumia wakati wa ujauzito kwani vina athari kubwa sana kwake yeye mwenyewe pamoja na mwanaye aliye tumboni.

Miongoni mwa vitu hivyo ni pamoja na;

1. Matumizi ya Pombe wakati wa ujauzito huathiri mtoto hivyo hairuhusiwi kabisa kutumia kwa kipindi hicho.

2. Uvutaji Sigara.

3. Kupunguza unywaji wa kahawa au vinywaji vyenye caffeine nyingi.

4. Samaki aina ya papa, swordfish, tilefish na king mackerel kwani wana mekuryi kwa wingi amabayo ni mbaya kwa afya.

Madhara ya Kujichubua

Katika baadhi ya sehemu duniani watu wanaamini kuwa ngozi angavu huashiria uzuri, utajiri na uwezo(kifedha) alionao mtu.Katika baadhi ya sehemu watu wenye ngozi nyeusi huchukuliwa kuwa wapo chini ya kiwango, hii hupelekea watu hawa kutumia ving´arisha ngozi kama krimu, vidonge au nyenzo zingine kubadilisha ngozi zao.

Tafiti zinaonyesha kwamba wavulana na wasichana hupendelea kutumia bidhaa zinazong´arisha ngozi ili waweze kupata hadhi nzuri katika kundi la familia zao, na jamii. Kwa kweli,hata matangazo yanayoonyeshwa kwenye televisheni mbalimbali huonyesha kitu hiki. Mambo hayo yote huwa na athari kubwa juu ya mawazo ya vijana wa kiume na wakike ambayo hupelekea kuwafanya wachague chochote wanachomudu kati ya krimu au vidonge.

Madhara ya kujichubua ni yapi?
Mtu anaeyejichubua anaweza kupata kansa ya ngozi, chunusi, uvimbe katika ngozi, ngozi kuwa nyembamba,Kuongezeka kwa hamu ya kula na uzito,kutokwa na mabaka, pumu, kupata watoto wenye kasoro, kupata matatizo ya akili, kuharibika kwa ini, kuharibika kwa mishipa ya fahamu pamoja na figo kutokana na kiwango kikubwa cha zebaki(mercury) kilichomo katika krimu,Osteoporosis(kupungua kwa uzito wa mifupa ambapo huongeza hatari ya kuvunjika kwa mifupa)

Baadhi ya madhara haya huonekaa mara moja na mengine hujitokeza kadri mtu anavyotumia ving´arisha ngozi.

Jinsi ya kumlisha n’gombe anayekamuliwa atoe maziwa mengi

Ng’ombe wa maziwa wanahitaji virutubisho zaidi ili kuweza kuzalisha maziwa kwa wingi hasa katika kipindi cha miezi 3-4 ya mwanzo baada ya kuzaa, wakati ambao uzalishaji wa maziwa unakuwa juu.

Malisho ya ng’ombe wa maziwa ni lazima yawe na uwiano sahihi wa viungo. Mifugo inahitaji chakula kitakachowapa nguvu, protini, madini, na vitamin ili kujenga miili yao, kuzalisha maziwa, na kuzaliana.

Kulisha ng’ombe wa maziwa kwa kutumia aina yoyote ya malisho haitoshi kukuhakikishia ng’ombe anakuwa na afya nzuri na kutoa maziwa ya kutosha. Kama ilivyo kwa mifugo mingine kama kuku na hata binadamu, ng’ombe anahitaji
mlo bora yaani kamili.

Vyakula vinavyohitajika kwa ng’ombe wa maziwa

Malisho ya kijani (Majani)

Huu ni mlo mkuu kwa ng’ombe wa maziwa. Mlo ni muhimu na wenye virutubisho. Lakini malisho bora ya kijani ni yale yanayoweza kumpatia ng’ombe wa maziwa virutubisho muhimu vinavyohitajika.

Malisho ya kijani yanatakiwa yawe ya kijani kibichi na machanga, hii ina maana kuwa, majani ya malisho ni lazima yakatwe na kuhifadhiwa yakiwa bado machanga na kabla ya kuchanua. Hii ina maana kuwa mimea ambayo imepoteza rangi yake halisi ya kijani inaweza tu kuwasaidia mifugo kuishi lakini haina virutubisho muhimu vya kuwapa mifugo nguvu, madini, protini na haiwezi kusaidia katika uzalishaji wa maziwa.

Malisho yenye viwango vya chini vya virutubisho yanatakiwa yaongezewe kwa chakula cha ziada chenye virutubisho vya kutosha kitakachoziba pengo la virutubisho vilivyokosekana.

Vyakula vya kutia nguvu

Kwa kawaida aina zote za majani ni chanzo kizuri cha vyakula vya kutia nguvu kwa mifugo, kama tuu tu yatalishwa yakiwa bado machanga.

Mfano wa Majani yaliyo maarufu kwa malisho ni matete, ukoka, majani ya tembo, seteria na Guatemala. Majani ya mahindi au mtama ni chakula kizuri sana kwa kuwapa nguvu mifugo.

Vyakula vingine vinaweza kutokana na aina zote za nafaka, punje za ngano, au molasesi.

Vyakula hivi vya kutia nguvu vinatakiwa vilishwe kwa kiasi kidogo.

Vyakula vya Protini

Mimea michanga ina kiasi kikubwa cha protini kuliko mimea iliyokomaa. Mahindi machanga pamoja na majani ya viazi vitamu ni mahususi kwa protini.

Mikunde ina protini nyingi zaidi kuliko nyasi. Mfano, mabaki ya majani ya maharage, njegere, desmodium na lusina. Majani yanayotokana na mimea kama lusina, calliandra au sesbania ina kiwango kikubwa cha protini pia.

Aina nyingine ya vyakula vyenye protini ni mashudu ya pamba, mashudu yaalizeti na soya.

Ng’ombe wa maziwa wasilishwe kwa kutumia aina zote za jamii ya mikunde kwa zaidi ya asilimia 30 ya uwiano wa mchanganyiko wa malisho ili kuepuka matatizo ya kiafya.

Madini

Ng’ombe wa maziwa wanahitaji madini ya ziada. Madini Ni lazima yapatikane muda wote, mfano kama jiwe la chumvi au kama chumvi ya unga ya kuweka kwenye (chakula) pumba.

Wanyama wanaokuwa, wenye mimba, na ng’ombe anaenyonyesha wanahitaji kiasi kikubwa cha madini, mfano calcium na phosphorous kwa kuwa madini mengi yanatoka kwenye maziwa.

Madini yanaweza kupatikana katika Mimea ya jamii ya mikunde na mengineyo isipokuwa nyasi. Mimea hii inatoa kiasi kikubwa cha calcium na madini mengineyo.

Chakula cha ziada (mf. Pumba)

Ng’ombe wa maziwa anapewa cha kula cha ziada mfano pumba. Pumba inahitajika kwa ng’ombe lakini kwa kiasi kidogo. Pumba aina ya Dairy meal ina kiwango kikubwa sana cha madini. Lakini ina madhara kwa mifugo endapo wanyama watalishwa kwa kiwango kikubwa.

Malisho yanayotokana na majani au nyasi kavu ni lazima yabakie kuwa chakula kikuu kwa mifugo. Haishauriwi kulisha zaidi ya kilo 6 za pumba kwa siku kwa ng’ombe mwenye kilo 450.

Ni lazima wapewe kwa kiwango kidogo sana, ambacho si zaidi ya Kilo 2 kwa mara moja na kichanganywe na majani. Kuongeza kiwango cha pumba kabla na wakati wa kunyonyesha/kukamuliwa, kisizidi kiasi cha kilo 2 kwa wiki ili tumbo la mnyama lizoee.

Faida za mnyonyo na mazao yake

Nyonyo Mbarika (Castor)
Mnyony(KiSwahili) Erand (KiHindi) Kastorka(KiRusi) ni mmea wa jamii ya Mbono Kaburi, kwa
jina la kitaalamu Japtropha

Baadhi ya faida za mnyonyo na mazao yake

Mbali na kuweza kutumia mnyonyo kama uzio hai,njia hii inaweza
kutumika kwa wale wasio na eneo kubwa la shamba ndipo sasa wakapata faida zake kama
ifuatavyo:🔽

Majani ya mnyonyo yanaweza kutumika kama tiba ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB), kukanda
(massage) ili kuondoa maumivu na majani haya
yakifungwa kwenye mguu unaouma huleta nafuu hasa kwa maumiviu yanayokuja baada ya kuteguka, pia hutumika kutibu uvimbe kwa wanyama.

Mizizi ya mnyonyo huweza kutumiwa kama dawa
ya mafundo fundo, uvimbe, kuungua, macho ya
manjano, kuumwa koo na magonjwa ya
kuambukiza ya kisonono na kaswende. Ukijaza
maji baridi kwenye kikonyo cha mnyonyo na
kumpa mtu mwenye kwikwi kila baada ya dakika
mbili au tatu hivi, mara nyingi huondoa
usumbufu unaoletwa na kwikwi. Mbegu/Punje/Tunda/Njugu za mnyonyo zikimezwa na maji bilauri moja kila siku kwa muda wa siku tano huweza kutibu maumivu yaliyosababishwa na kuungua. Vile vile, mbegu hizi huweza kusagwa na kisha kuenguliwa mafuta
kwa ajili ya kulainisha mashine na mitambo viwandani. mbegu za mnyonyo kabla ya kukomaa
Mafuta
yatokanayo na
mbegu za nyonyo mfano
Ricinoleic Acid,
Oleic Acid,
Linoleic Acid
nk hutumika
kutibu ugonjwa
wa wa jongo
(rheumatism)unaowakumba watu wengi wanaoishi maeneo ya miinuko na
baridi, pia hutibu ugonjwa wa mifupa ujulikanao kwa jina la kitaalamu kama arthritis na gauti. Mafuta ya mnyonyo pia yanaweza kutumika
kama njia ya kupanga uzazi kwani yana kiasi
fulani cha sumu ya protini ijulikanayo kitaalamu kama ricin ambayo ikitumiwa kwa kiasi kidogo huharibu utungo,huweza pia kutumiwa kama
mafuta ya kupaka ama losheni katika sehemu za
siri ili kuua mbegu za uzazi za kiume wakati wa tendo la kujamiiana. uzazi wa mpango.

Tahadhari:

Mnyonyo ni mti wenye sumu
inayoweza kuua binadamu au
wanyama endapo itatumika kuzidi
kipimo. Mazao yoyote yatokanayo na mnyonyo huhatarisha au/na
kuharibu mimba na hata kuweza
kusababisha kifo cha mjamzito,
hivyo, matumizi yake lazima yawe
ya uangalifu mkubwa. Mafuta ya Ricinoleic acid
yanayopatikana kutokana na mnyonyo vile vile yanaweza kutumika kurekebisha hedhi
(mzunguko wa damu ya mwezi kwa wanawake) ikiwa mzunguko
umechelewa ama kusimama katika
umri usiotarajiwa. Huweza pia
kupunguza maumivu makali
yanayotokea wakati wa hedhi.

Mafuta ya mnyonyo yanayojulikana
kitaalamu kama Undecylenic Acid
huweza kutumika kutibu magonjwa
mbalimbali ya ngozi na vidonda
vinavyosababishwa na bakteria ama ukungu(fungus). mbegu za mnyonyo baada ya kukomaa

Akina mama wanaonyonyesha pia wanaweza kutumia mafuta
baridi ya mnyonyo (kiasi kidogo ili kuepuka madhara ya mafuta hayo kwa mtotokumbuka
hapo awali nimeandika kuwa mafuta haya
yakitumiwa kwa kiwango kikubwa ni sumu ) kuongeza wingi na mtiririko rahisi wa maziwa.

Nywele nzuri, safi, nadhifu na zisizokatika pia
ngozi imara inapatikana kutokana na matumizi ya mafuta ya mnyonyo.Mafuta ya mnyonyo pia ni
dawa nzuri ya kufungua tumbo la uyabisi(kuvimbiwa).

Mnyonyo unaweza pia kuwafaa watu wanaoishi na VVU (Virusi Vya UKIMWI) kwani mafuta yake ni sumu ya kuua vimelea vya
magonjwa kama vile bakteria na ukungu(fungus).

Njia:

Kupakaza: Chukua kipande cha nguo ama
kitambaa, kisha kiloweke kwenye mafuta ya
mnyonyo ndipo ufunge katika kiwiko ama
eneo lenye maumivu ama kidonda.Vinginevyo
chukua kiasi cha mafuta na kupaka eneo linalohusika mfano, penye kidonda, kuugua
ama pakaza kichwani au juu ya tumbo wakati
wa maumivu ya hedhi nk. Unaweza kuacha kwa muda wa saa moja kabla ya kunawa ili uipe ngozi muda wa kunyonya kiasi cha
mafuta. Unaweza kujifunga kitambaa hicho
tumboni ama mgongoni kama kibwebwe na kuendelea na shughuli za kawaida.

Kunywa: Chemsha mbegu chache za mnyonyo
pamoja na maji na maziwa kisha unywe kiasi kidogo kadiri ya nusu hadi bilauri moja ya ujazo wa mili lita mia mbili na arobaini.

Kusafisha utumbo: Kunywa mafuta ya mnyonyo vijiko viwili vikubwa vya chakula asubuhi, kisha pumzika kwa saa mbili ndipo unywe maji glasi mbili na endelea kunywa maji glasi moja kila baada ya saa moja.

Kali za leo: Misemo ya kuchekesha na kuvunja mbavu

1. Ati wee ni m-black mpaka ukiingia kwa dinga(gari), dirisha zinakuwa tinted!

2. Kwenu kuchafu mpaka mende zinatema mate.

3. Vile wewe mfupi, ukipiga picha ya passport inatokea full.

4. Ati(house) yenu ina gate lakini hakuna fence.

5. Baba alienda ku buy ngombe akaona ikikojoa akasema sitaki hiyo imetoboka.

6.Wee mblack mpaka ukikutana na mzungu afternoon anakusalimia: Good evening.

7. Mko wengi kwa house mpaka kuna rush hours na kukinyesha kunakuwa na jam.

8. Paka yenu noma mpaka ikishika panya inaomba chumvi, fork na pilipili.

9. We ni mrefu mpaka ukikunywa maziwa inafika kwa tumbo ikiwa mgando.

10.Wewe ni mweusi ukikanyanga makaa unawacha footprint nyeusi.

11. Kwenyu mkikunywa maji mnaitisha toothpick

12. We ni mbishi hadi ulikataa kuzaliwa uchi

13. Kwenu kuna insecurity ikifika usiku hadi geti mnaingiza ndani

14. Kwenu ni wengi sana hadi mmeweka round about ndani.

15. Wewe ni mlafi hadi maji uliyochemshia mayai unayafanya supu.

16. We ni mjinga sana hadi blood test ulifeli.

17. Una chogo refu hadi ukigeuka haraka unaweza kuliona.

18. Una kichwa kikubwa hadi ukiingia kwenye daladala konda anakwambia “abiria usiingie na mizigo, tunaweka juu kwenye carrier

Mambo 6 muhimu ya kuzingatia kupata udongo bora mzuri shambani

1. Usiuchoshe sana udongo

Udongo ni kiungo muhimu sana katika uzalishaji wa mazao. Ni mfumo wa uhai kwa mimea. Kwa hiyo, mkulima ni lazima alenge katika kutunza uhai wa udongo na kuepuka usumbufu kwa uhai wa udongo.
Sababu muhimu za kulima/kutifua udongo ni:
• Hulainisha udongo ili kuruhusu mizizi ya mimea kupenya kwa urahisi.
• Kutifua kunaboresha uwezekano wa kupenya kwa nitrogen na oxygen kutoka kwenye hewa.

• Kunawawezesha viumbe hai waliopo kwenye udongo kufanya kazi zao ipasavyo.
• Kunasaidia Kuandaa sehemu ya kuwekea mbegu.
• Kutifua kunauongeza uwezekano wa maji kupenya kwenye udongo na kupunguza uyeyukaji wa maji.
• Kuchanganya mabaki ya mimea na samadi kwenye udongo

2. Acha udongo upumue

Kama ilivyo kwa binadamu, viumbe hai wanahitajika kwa udongo wenye rutuba, pia mimea inahitajika kwa ajili ya binadamu kupata hewa safi ya oxygen. Kuchanganya matandazo,na mboji kwenye udongo ni muhimu sana ili kuboresha mzunguko wa hewa. Viumbe hai wadogo wadogo, wadudu, minyoo, na wanyama wengineo wanapenyeza hewa kwenye udongo.

3. Weka Matandazo kwenye udongo

Huu ni utaratibu wa kufunika udongo kwa kutumia mabaki ya mimea, kwa mfano, matawi madogo madogo ya miti, majani, mabaki ya mimea ya mazao, magugu na kadhalika. Hata hivyo inahitajika nguvu kazi kwa ajili ya kutawanya matandazo.

Matandazo yanazuia mmomonyoko wa ardhi unaotokana na maji na upepo, yanasaidia ardhi kunyonya maji ya mvua, kutunza unyevu unyevu kwenye udongo kwa kuzuia myeyuko wa maji ardhini.

Matandazo yanapo oza hutoa virutubisho vinavyoboresha na kuongeza rutuba kwenye udongo, mbali na hilo pia hubadilika kuwa udongo mweusi wenye rutuba zaidi. Kama kuna uhitaji wa kuharakisha kuoza kwa matandazo ili kuongeza rutuba kwenye ardhi kwa haraka, kinyesi cha ng’ombe kinaweza kuwekwa na kutandazwa juu ya matandazo, hii husaidia kuongeza virutubisho vya nitrogen.

Matandazo yana faida nyingi sana kwenye ardhi, lakini pia yanaweza kusababisha madhara. Mabaki ya mboga za majani yasitumike kama matandazo kwani yanaweza kusababisha wadudu na magonjwa kwa mimea. Viumbe hatari kama bangu (stem borers) wa shina wanaweza kuishi kwenye mabaki ya mimea.

Mabaki ya mimea iliyokuwa imeathiriwa na magonjwa ya virusi au fangasi yasitumike kama matandazo kuepuka uwezekano wa magonjwa hayo kuambukizwa kwa mazao yatakayopandwa msimu utakaofuata. Kilimo cha mzunguko ni njia bora kuepuka athari hiyo.

4. Panda mazao kwa mzunguko

Kupanda mazao kwa mzunguko ina maana ya kuwa na aina mbalimbali ya mazao katika eneo moja kwa msimu.

Kwa mfano, kama shamba lako umepanda mahindi na maharagwe kwa kipindi cha mwaka mmoja, mkulima anaweza kubadili mzunguko kwa kupanda aina nyingine ya mazao katika eneo hilo kwa mwaka unaofuata.

Mimea iliyo mizuri zaidi katika kilimo cha mzunguko ni pamoja na jamii ya kunde, au malisho kama sesbania ambayo husaidia kuongeza rutuba kwenye udongo.

5. Lisha udongo

Udongo unatakiwa ulishwe ili uwe na virutubisho. Hii ni kazi muhimu sana kwa kila mkulima. Mkulima anaweza Kuulisha udongo kwa kutumia samadi na mboji. Kumbuka udongo uliotumika sana bila virutubisho, umekufa, hauwezi kuzalisha.

6. Kuwa makini na maji

Maji ni mazuri shambani, lakini maji yakizidi ni hatari. Maji yakizidi shambani yanaweza kusababisha mmomonyoko wa udongo. Mmomonyoko wa udongo ni tishio na baa hatarishi kwa rutuba kwenye udongo. Mmomonyoko unaondoa tabaka la juu la udongo, sehemu ambayo ndiyo yenye rutuba zaidi.

Kupanda mimea kwa matuta (kontua) hupunguza kasi ya maji. Baada ya miaka kadhaa, nyasi zinazopandwa zinazopandwa kwenye matuta ya kontua husaidia kuunganisha na kusawazisha sehemu iliyotengwa, kwa kuwa udongo unaomomonyolewa hukusanyika katika sehemu iliyozuiwa na kuunganishwa kwa matuta.

Kwenye mwinuko mkali, kuta au mashimo, ndiyo njia pekee inayoweza kuzuia mmomonyoko wa udongo. Changanya na mimea kama matete, inasaidia kuzuia mmomonyoko na pia kutoa malisho kwa mifugo.

Mbali na matandazo (tazama hatua ya 3) mimea inayotambaa ni mbinu nyingine nzuri zaidi inayoweza kuzuia mmomonyoko wa ardhi. Matone ya maji hufikia ardhi yakiwa na nguvu kidogo sana hivyo kuepuka kumomonyoa ardhi, kwa kuwa yanakuwa tayari hayana nguvu ya kutiririka kwa kasi. Pia mimea inayotambaa hutumika kama kivuli kwa udongo. Mmea wowote unaofunika udongo na kuongeza rutuba unaweza kutumika.

Mfano maharage na mimea mingine ya jamii ya kunde, ambayo ina virutubisho vya nitrogen kwa wingi. Mimea inayopendekezwa ni ile ya jamii ya kunde. Inastahimili ukame, inatoa virutubisho vya naitrojeni, inatoa chakula, na pia inaweza kutumika kama chakula cha mifugo kilicho na protini nyingi. Kwa kuongezea inaweza pia kukabiliana na wadudu waharibifu.

Jinsi ya Kujaza nywele kwa njia za Asili

Zingatia mambo haya yafuatayo;

  1. Chukua parachichi kubwa moja, asali vijiko vitatu na kiini cha yai.
  2. Osha nywele zako kwa shampoo na uzikaushe.
  3. Ponda ponda parachichi mpaka lilainike kabisa. Chukua vijiko vitatu vya asali na kiini cha yai kisha changanya yote kwa pamoja.
  4. Paka mchanganyiko huo kaa nao kwa muda wa dakika 15 kisha osha.
  5. Fanya hivyo kwa muda wa wiki moja hadi mbili na utaweza kuona matokeo mazuri katika nywele yako
Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About