SOMO 1
Kut. 19 :2-6
Waisraeli walipokuwa wameondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, wakatua katika lile jangwa; wakapiga kambi huko wakiukabili mlima. Musa akapanda kwa Mungu, na Bwana akamwita toka mlima ule, akisema, Utawaambia nyumba ya Yakobo, na kuwaarifu wana wa Israeli, maneno haya: Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi. Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu, nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 100 :2-3, 5 (K) 3
(K) Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.
Mtumikieni Bwana kwa furaha;
Njoni mbele zake kwa kuimba. (K)
Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)
Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)
SOMO 2
Rum. 5 : 6-11
Wapendwa, hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu. Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema. Bali Mungu aonyesha pendo lake veye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake, zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake. Wala si hivyo tu, ila pia twajifurahisha katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, am have kwa yeye sasa tumeupokea huo upatanisho.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANG1LIO
Yn. 15 :15
Aleluya, aleluya, Ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
Aleluya.
INJILI
Mt. 9:36-10:8
Yesu alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake. Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza
magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Na majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya; Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa Zebedayo, na Yohane nduguye; Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo wa Alfayo, na Thadayo; Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote, naye ndiye mwenye kumsaliti. Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mwamini katika mpango wake.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Neema na amani iwe nawe.
Sifa kwa Bwana!
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuwa na imani!
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Katika imani, yote yanawezekana
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu akubariki!
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mwamini Bwana; anajua njia
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Baraka kwako na familia yako.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema zake hudumu milele
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Nakuombea 🙏
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Tumaini ni nanga ya roho
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Dumu katika Bwana.
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Rehema hushinda hukumu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Neema ya Mungu inatosha kwako