SOMO I
Isa. 56:1, 6-7
Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatenda haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.
Neno la Bwana…Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 67:1-2, 4-5, 7 (K) 5
(K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu,
Watu wote na wakushukuru.
Mungu na atufadhili na kutubariki,
na kutuangazia uso wake.
Njia yake ijulikane duniani,
wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K)
mataifa na washangilia,
naam, waimbe kwa furaha.
Maana kwa haki utawahukumu watu,
na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K)
watu na wakushukuru, Ee Mungu,
watu wote na wakushukuru.
Mungu atatubariki sisi;
miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K)
SOMO 2
Rum. 11:13-15, 29-32
Nasema na ninyi, mlio watu wa Mataifa. Basi, kwa kadiri nilivyo mtume wa watu wa Mataifa. Basi, naitukuza huduma iliyo yangu? Huenda nikapata kuwapatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao. Maana ikiwa kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa ulimwengu, je! Kukubaliwa kwao kutakuwa nini kama si uhai baada ya kufa. Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake. Kwa maana kama ninyi zamani mlivyomwasi Mungu, lakini sasa mmepata rehema kwa kuasi kwao; kadhalika na hao wameasi sasa, ili kwa kupata rehema kwenu wao nao wapate rehema. Maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kuasi ili awarehemu wote.
Neno la Bwana…Tumshukuru Mungu
SHANGILIO
Mdo. 16:14
Aleluya, aleluya,
Fungua mioyo yetu, Ee Bwana,
Ili tuyatuze maneno ya Mwanao.
Aleluya
INJILI
Mt. 15:21-28
Yesu aliondoka huko, akaenda kando pande za tiro na Sidoni. Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Naye akaja akamsujudia, akisema, Bwana unisaidie. Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.
Neno la Bwana…Sifa kwako, ee Kristo
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika imani, yote yanawezekana
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ni mwema, wakati wote!
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Dumu katika Bwana.
Rehema zake hudumu milele
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Baraka kwako na familia yako.
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema hushinda hukumu
Nguvu hutoka kwa Bwana
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Neema na amani iwe nawe.
Mwamini Bwana; anajua njia
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Nakuombea 🙏
Tumaini ni nanga ya roho
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Imani inaweza kusogeza milima
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mungu akubariki!
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mwamini katika mpango wake.
Sifa kwa Bwana!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Endelea kuwa na imani!
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe