SOMO I
Isa. 22:19-23
Bwana, Bwana wa majeshi, asema hivi: Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo. Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia; nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nvumba ya Yuda. Na ufunguo wa nvumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga. Nami nitamkaza kanta msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.
Neno la Bwana…Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 138: 1-3, 6, 9 (K) 9
(K) Ee Bwana, fadhili zako ni za milele,
Usiziache kazi za mikono yako.
Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,
Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu. (K)
Nitalishukuru jina lako,
Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwa maana umeikuza ahadi yako,
Kuliko jina lako lote.
Siku ile niliyokuita ulinitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. (K)
Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu,
Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.
Ee Bwana, fadhili zako ni za milele;
Usiziache kazi za mikono yako. (K)
SOMO 2
Rum 11: 33-36
Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake? Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena? Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.
Neno la Bwana…Tumshukuru Mungu
SHANGILIO
Mt 11: 25
Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi,
kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye
hekima na akili. ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya
INJILI
Ml 16:13-20
Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipo, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena Yohane Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaa- mbia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia. Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikufunulia hili, bali Baba vangu aliye mbinguni. Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. Ndipo alipowakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.
Neno la Bwana…Sifa kwako, ee Kristo
Neema na amani iwe nawe.
Nakuombea 🙏
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema zake hudumu milele
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Nguvu hutoka kwa Bwana
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Tumaini ni nanga ya roho
Katika imani, yote yanawezekana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Dumu katika Bwana.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Endelea kuwa na imani!
Mwamini Bwana; anajua njia
Sifa kwa Bwana!
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Imani inaweza kusogeza milima
Baraka kwako na familia yako.
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu akubariki!
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rehema hushinda hukumu
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mwamini katika mpango wake.