Anachokiangalia Mungu
Mungu haangalii matemdo ya mtu ya nje tuu, bali anaangalia ndani kabisa mawazo ya mtu na nia yake. Nia ya mtu ndiyo inayoonyesha mtu alivyo.
Mungu haangalii matemdo ya mtu ya nje tuu, bali anaangalia ndani kabisa mawazo ya mtu na nia yake. Nia ya mtu ndiyo inayoonyesha mtu alivyo.
Kukosa hata mara moja inahesabika ni kukosea mbele ya Mungu. Kwa kuwa kwa Mungu hakuna kusema, ‘Kukosea mara moja sio kosa bali kurudia kosa ndio kosa’. Mbele ya Mungu kila kosa lina uzito wake haijalishi ni kosa la mara ya kwanza.
Kama mtu anasali kila siku katika maisha yake hakuna kitu kitakachokuwa kigumu. Sala ni njia ya kujipatia neema za kuendesha maisha yetu. Usiache kusali kila siku hata kama upo katika hali gani.
Usiogope wala usisite kutubu na kuomba msamaha kwa Mungu. Uwe na Amani na Matumaini katika Huruma ya Mungu itokayo katika Upendo wake wa Mfano wa baba awapendavyo wanawe. Mungu anasubiri kukupokea kwenye mikono yake Ili akutunze kama mtoto wake kama utatubu na kumrudia yeye. Amua kumwendea leo! Anakungoja ni wewe tuuโฆ
Sala sio kitu cha muhimu kufanya wakati wa shida tuu. Sala ni kitu cha muhimu zaidi kila siku katika Maisha kuwe na shida au kusiwe na shida.
Mungu anasubiri sala zako kila siku. Anasubiri sala zako akujibu ili uone utukufu wake. Anasubiri sala zako ili akuze mahusiano yake na wewe. Sali daima kwani Mungu yupo milele kukusikiliza na kukuhudumia.
Mawazo ya Mungu ni makuu. Mungu anatuwazia mema daima. Hata unapopitia shida na matatizo katika maisha nia ya Mungu inabaki kuwa njema ya Kukuonyesha ukuu wake na kukuwezesha kumjua yeye. Pengine usingejua matendo ya Mungu bila kupitia shida na changamoto katika maisha. Mungu hapendi upate shida bali anaruhusu hayo ili upate faida ya kumjua na kujua uwezo wake. Hata Yesu ilibidi apitie mateso na kifo ili uwezo wa Mungu udhihirike baada ya kufufuliwa. Amini kuwa kuna mema mbele yako baada ya mateso haya ya sasa.
Hakuna Binadamu anayemchukia Mungu kama hajichukii yeye mwenyewe na wale wanaomzunguka. Huwezi kusema humtaki Mungu kama hujichukii mwenyewe na wale waliokuzunguka vivyo hivyo huwezi kusema Unampenda Mungu kama hupendi wengine waliokuzunguka.
Uzuri wa Mungu ni kwamba anasamehe na kisha anasahau. Unapotubu dhambi zako na kutaka huruma zake yeye anakufutia uovu wote na kukufanya mpya.
Mungu ni rahisi sana kupatikana. Ugumu ni njia ya Kumtafuta Mungu na namna ya kumuishi Mungu. Hapa ndipo watu wengi wanashindwa.
Kama yalivyo maisha ya kimwili, maisha ya kiroho pia yanahitaji mipango. Kila siku panga utafanya nini kiroho, mfano unaweza kupanga sala, kusaidia masikini, kuwa mpole au mwema. Vivyo hivyo kila wiki, kila mwezi na kila mwaka mpya panga cha kufanya kiroho naye Mungu atakubariki na kukupangia zaidi. Huwezi kufanikiwa kiroho kama hujui unafanya nini kiroho.
Unapo mwomba Mungu Usisahau Kushukuru. Kushukuru ni kuomba mara ya pili. Utazidishiwa kile ulichokiomba na kupewa hata usichokiomba kwa shukrani yako.
Hakuna Maisha ya Kikristo bila Kusali. Kama kuna Mkristo anaishi bila kusali huyo siyo Mkristo bali Mkristo mfu. Sala ndiyo uhai wa Mkristo. Hakuna Njia nyingine yoyote ya kumfikia Mungu isipokua sala.
Uhuru Na Amani Ya Moyoni hupatikana kwa kusali wala sio kwa kusoma vitabu na kujua sana Mambo mengi.
Kutubu ndio njia pekee ya kumrudia Mungu. Toba ya kweli ndiyo iletayo maondoleo ya dhambi. Ukiondolewa dhambi unaimarishwa na kufanywa mya. Tubu usamehewe na kufanywa mpya.
Njia pekee ya Kumrudia Mungu tunapoanguka dhambini ni Njia ya Toba ya kweli ikiambatana na kukiri makosa na kusamehewa. Mara nyingi tunapotubu tunasahau dhambi za mawazo na kukumbuka za matendo tuu. Dhambi ya Mawazo pia ni dhambi yapaswa toba na maondoleo.
Usifadhaike moyoni pale unapokuwa katika matatizo au unapopitia changamoto katika maisha. Kumbuka kuwa Mungu yupo, anayaona hayo na anataka kukusaidia, ni wewe tuu kumpa nafasi ya kukusaidia. Hatumpi Mungu nafasi pale tunapozani tunaweza wenyewe.
Mungu ni mwenye Hekima, anajibu Sala zetu kwa kutupa kile tunachohitaji na chenye kutufaa na Sio kutupa kile tunachokitaka na kukitamani kwa kuwa anatupenda na kututakia mema.
Basi, nasema hivi: Mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia. Maana tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na Tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamuwezi kufanya yale mnayotaka nyinyi wenyewe.
(Wagalatia 5:16-22)
Basi, nasema hivi: Mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia. Maana tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamuwezi kufanya yale mnayotaka nyinyi wenyewe.
“Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtatimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa maana mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.” (Wagalatia 5:16-17)
Kuongozwa na Roho Mtakatifu maana yake ni kuacha maisha yetu yaongozwe na maadili na kanuni za kiroho zinazotoka kwa Mungu. Roho Mtakatifu hutupa nguvu, hekima, na mwongozo wa kila siku katika safari yetu ya kiroho. Tunapoongozwa na Roho, tunakuwa na uwezo wa kupambana na tamaa za kidunia ambazo zinatufanya tuwe mbali na Mungu.
“Lakini Roho wa kweli atakapokuja, atawaongoza awatie kwenye kweli yote. Kwa maana hatasema kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayasema, naye atawapasha habari za mambo yajayo.” (Yohana 16:13)
“Basi, kama mlivyopokea Kristo Yesu Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye mizizi na kujengwa ndani yake, na kuthibitishwa katika imani, kama mlivyofundishwa, mkizidi kutoa shukrani.” (Wakolosai 2:6-7)
“Basi, enendeni kama watoto wa nuru, kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli.” (Waefeso 5:8-9)
Tamaa za kidunia ni yale mambo yanayotupotosha na kutufanya tuishi kinyume na mapenzi ya Mungu. Ni lazima tujifunze kuzishinda kwa kuimarisha uhusiano wetu na Mungu kupitia maombi, kusoma Neno la Mungu, na kushirikiana na wengine waaminio. Roho Mtakatifu hutusaidia kuona na kutambua uovu na udanganyifu wa tamaa za kidunia na kutupa nguvu ya kuzishinda.
“Basi, ndugu zangu, sisi tuna deni, si kwa mwili, kufuatana na mwili; kwa maana kama mkiishi kufuatana na mwili, mnakufa; bali kama mkiyaangamiza matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.” (Warumi 8:12-13)
“Wala msiifanye miili yenu kuwa silaha za dhambi kwa kutenda uovu, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama watu waliotolewa katika wafu na kupewa uhai, na miili yenu iwe silaha za haki kwa Mungu.” (Warumi 6:13)
“Kwa maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome; tukibomoa mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinue juu ya elimu ya Mungu; tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo.” (2 Wakorintho 10:4-5)
Kutembea katika nuru ya Roho Mtakatifu ni kuishi maisha yaliyojaa matunda ya Roho, kama vile upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu, upole, na kiasi. Tunapojitahidi kuishi kwa njia hii, tunakuwa mashahidi wa kweli wa Kristo na tunavutia wengine kwake. Ni muhimu kufahamu kwamba hatuwezi kutembea katika nuru ya Roho kwa nguvu zetu wenyewe, bali kwa neema na uwezo wa Roho Mtakatifu ndani yetu.
“Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.” (Wagalatia 5:22-23)
“Nanyi mkivumiliana na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo nanyi. (Wakolosai 3:13)
“Tazama ni jinsi gani upendo wa Baba alivyotupa, kwamba tuitwe watoto wa Mungu; na ndivyo tulivyo.” (1 Yohana 3:1)
Kuongozwa na Roho Mtakatifu ni wito wa kila Mkristo. Ni mwaliko wa kuacha maisha yetu yaongozwe na Mungu, na kuishi kulingana na mapenzi yake. Tamaa za kidunia ni kikwazo kikubwa kwa uhusiano wetu na Mungu, lakini kwa nguvu na mwongozo wa Roho Mtakatifu, tunaweza kuzishinda na kuishi maisha yaliyojaa matunda ya Roho. Tuishi maisha ya kuongozwa na Roho, tukijua kwamba Mungu yupo nasi na anatupatia nguvu ya kushinda kila jaribu na changamoto.
Sala ni ufunguo wa kufungulia mema na kufungia Mabaya. Tusali ili tufungue mema katika maisha yetu na tufunge mabaya katika maisha yetu.
Recent Comments