Vichekesho Vya Kukuparaha
Kilichotokea baada ya bibi na babu kukumbukia mahaba ya ujanani
Mzee wa miaka 60 alimwambia mkewe, leo nataka tukumbukie enzi zetu kutongozana, mke akajibu sawa, inabidi unisubiri mwembeni saa 1 usiku nitapita, mzee akafika saa 1 alikaa hadi saa 5 usiku, aliporudi nyumbani akamuuliza mkewe kwa hasira; sasa tumepanga nin halafu haujatokea ?
Mke; leo mama alinikataza nictoke nyumbani usiku nijisomee ! Babu hoiiโฆ
Mkalimani alivyoharibu ibada ya leo
Leo nikaamua niingie misa ya asubuhi kwenye kanisa moja la kilokole kulikua na ugeni wa mchungaji kutoka Bulgaria, Mahubiri yameanza saa 1 asubuhi hali ikawa kama hivi:
MCHUNGAJI: My name is Pastor Livingstone
MKALIMANi: Kwa jina naitwa mchungaji Jiwe linaloishi
MCHUNGAJI: We thank God for All goals we set by our hands
MKALIMANI: Tunamshukuru Mungu kwa Magoli yote tuliyoweka kwa Mkono
Hivi navyoongea kanisa halina viti waumini wote tumekimbia nje naona Mkalimani amebaki na kiatu cha kushoto tu.
Sunday joke
Je hili ni kweli kuhusu mpenzi maskini na Tajiri?
Siku hizi kudekezwa na kupetiwa petiwa tunawaachia matajiri
Hakuna mwanamke yupo tayar kulalia kifua cha maskini ambacho moyo unadunda
Deni,, Deni,Deni, Deni .
๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐ถ๐ฝโโ
Sitasahau mwaka huu
Sitasahau mwaka ule ambapo nilipeleka barua ya maombi yangu ya kazi kwenye kampuni moja maarufu. Wakati nasubiri majibu siku moja nikaenda kwa mama ntilie kununua maandazi akanifungia vizuri, kufika nyumbani hamu yote ya maandazi iliniishia pale nilipogundua karatasi iliyofungiwa maandazi ni barua yangu ya kuombea kazi๐๐
Makonda wana mambo, Kila mtu ni ndugu yao
Hakuna m2 mwenye ndugu wengi kama konda wa daladala.
Utasikia,
“HAYA, DADA HAPO MBELE, MJOMBA KULE MWISHO.
MA-MDOGO UNAENDA?,
NGOJA ASHUKE BIBI.
HAYA SHEMEJI UMEIKUTA YA KUWAH.
Babu njoo ukae!
Baba angu hapo tusogee kidogo,
Shangazi maliza ngazi,
Swaiba geukia mbele,
Kaka hapo shika upande wa pili,
Mdogo wangu mpishe Ma Mkwe akae.
Subiri Shemeji yako apandeโฆ
Duhโฆ makonda nomaโฆ!!
Hyuyu daktari ni noma, cheki anachokisema
Kuna Daktari wa Moyo alifariki wakamchongeaa jeneza lenye umbo la Moyo. Ghafla Daktari mwingine akaanza kucheka, watu wakamuuliza “kwanini unacheka unafurahia mwenzako kufariki?” Daktari yule akajibu “hapana mimi ni Daktari wa kutahiri nafikilia nikifa mtanichongea jeneza lenye umbo la โฆ.”
Utani wa wahindi, cheka kidogo
Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili
(1) Mfa maji ?โฆโฆโฆโฆโฆโฆ.. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?โฆโฆโฆโฆ Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?โฆโฆโฆ.. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?โฆโฆโฆโฆโฆโฆ Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?โฆโฆ. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?โฆโฆโฆ Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?โฆโฆ.. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?โฆโฆ Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?โฆโฆโฆ Takosa guo ya sikukuuโฆ
(10) Kila ndege ?โฆโฆโฆโฆ.. โฆHutua Airport
(11) Bandu bandu ?โฆ.. โฆโฆ.Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?โฆ Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?โฆ.Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?โฆโฆโฆ. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?โฆโฆ.. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?โฆ. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? โฆโฆ.. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? โฆโฆโฆโฆ..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?โฆโฆ.. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?โฆ.Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?โฆโฆ.. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? โฆโฆโฆ.Taenda Chadema
(23) Bendera ?โฆโฆโฆโฆโฆ. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?โฆโฆ. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?โฆโฆโฆ. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? โฆโฆ.. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.
Huu ndio uhondo na raha ya kupanda daladala wajameni
Wasiopanda dalaladala wanakosa uhondo wa kauli hizi
1. nitakupa
2. Atapewa mbele
3. Hujapewa mbele?
4. Utapewa nyuma
5. Nitakupa nikikaa vizuri
6. Ngoja isimame nikupe
7. subiri asimamishe nikupe
8. hivi nlivyo kaa ntakupaje?
9. Utapewa tulia
10. Nikupe mara ngapi?
Angalia huyu jamaa alivyowafanyia watu uhuni bar
Jamaa kaingia Bar;
Jamaa: Muhudumu, nipe kinywaji na mpe kila mtu humu ndani kinywaji, maana wakati napata kinywaji lazima kila mtu apate kinywaji. Haraka sana muhudumu akagawa vinywaji,
Jamaa: Muhudumu nipe supu na kila mtu humu ndani mpe supu maana ninapokunywa supu kila mtu lazima anywe supu. Watu wakapewa supu tena safari hii wakapiga makofi.
Jamaa: Muhudumu nipe bili, na kila mtu humu ndani mpe bili maana wakati nalipa bili yangu kila mtu lazima alipe yake. Zogo lilianzia hapoโฆโฆ.
Tofauti ya mwanamke wa Kizaramo, Kitanga, Kihaya, na wa Kichaga
Mwanamke wakizaramo: Unampa hela ana nunua dela anaenda ana msutia jirani, analivaa dela bila nguo ya ndani mbele yako, unazidiwa anakupa kitu fresh unatoka unatabasamu.๐ค๐ฝ๐๐ฝ
Mwanamke wa kitanga:
Unampa hela anapika vitu mtaa mzima unasikia harufu ya chakula, chenji inayo baki ananunua kinga ukirudi unakula afu unakula..๐๐ผ๐๐ผ๐ค๐ฝ๐๐ฝ
Mwanamke wa kihaya:
Unampa hela ukirudi unakuta majirani wote wanataarifa kuwa wew uliacha hela, anakupkia vitu vzuri, usiku anakuhudumia ukimsifia anakuhudumia tena hata mara nne kwa usiku mmoja..we mle sifa tu๐๐ฝ๐๐ฝ๐คธ๐พโโ๐๐ฝ.
Mwanamke wa kichaga:
Unampa hela anaenda ananunua dagaa anapika na michuzi mingi mpaka dagaa wanafufuka unakula kwa shida, dagaa wanakula utumbo wako unakufa.. Madaktari wanajitahidi wanakutibu unafufuka. Ukiwa hujapata akili vizuri anakuletea bili ya umeme, anakukumbusha deni la kwa Massawe, anakukumbusha kodi ya nyumba.. *Unashikwa na presha unakufa moja kwa moja*๐๐ฝ๐๐๐ผโโ๐๐พ๐คธ๐พโโ
Sio kwa wivu huu
Wanawake nilianza kuwachukia tokea shule ya msingi.
Ni pale mwanamke wangu aliponiacha na kwenda kwa jamaa mwenye kichongeo kipya โฆinauma sanaaโฆ
WANAWAKE SIO WATU WA MCHEZO MCHEZO ASEEE Bac tuu
Mambo ya mke na mume haya, chezea mchepuko!?
Mume akamwambia mke wake:
“Funga macho yako tufanye maombi”
Akaanza kwa Kimombo:-
“โฆ Lord I pray for Grace, I pray for Mercy, I pray 4 Joy, I pray 4 Love, I pray 4 Hope, I pray 4 GLORY, I pray 4 Faith, I pray 4โฆ.”
Mke akadakia, “Unadhani mimi sina ee” akaanza:-
I pray 4 Felix, I pray 4 Temu, I pray 4 Rweyemamu, I pray 4 Masawe, I pray 4 Benson, I pray 4 Onyango, I pray 4 Swai, I pray kwa wote niliowasahau!!
Chezea mchepukoโฆ!!
Baada ya kunitumia SMS usiku ikawa hiviโฆ.
Jana usiku kuna Jirani yangu..kanitumia text “mambo vipi?”โฆhalafu tunakaa nae mtaa mmoja nikaona nikimjibu ni uharibifu wa hela nikaenda kumgongea mlango saa 7 usiku. Alipofungua nikamjibu “shwari”halafu nikarudi nyumbani kulala zangu..
Sipendagi kuchezea salio..
๐๐๐๐๐
Tofauti kati ya mwanamke na mwanamme
UTOFAUTI KATI YA MWANAMKE NA MWANAUME
1. Kwenye mshituko; mwanaume hushituka halafu huangalia nini kimemshitua, mwanamke hushituka halafu huzimia hivyo ataambiwa na mwanaume kilichomshitua๐๐
2. Kwenye kupenda; mwanaume huanza kutamani alafu hupenda, mwanamke huanza kupenda moja kwa moja bila kumjua vizuri huyo ampendae๐๐๐
3.Kwenye kusaidia; mwanaume hutoa msaada alafu uhuzunika, mwanamke huuzunika badae ndo anakumbuka km msaada unahitajika๐๐๐
4.Kwenye maamuzi; mwanaume hufikiri ndipo hutenda, mwanamke hutenda halafu hufikiri๐๐๐
5.Kwenye kudanganya; Mwanaume hudanganya ili kumlinda mwanamke, mwanamke hudanganya ili kumkomoa mwanaume๐๐๐
6.Kwenye ugomvi; wanaume hupigana halafu hueshimiana, wanawake hupiga mikelele alafu kila mmoja hurud kwake, kexho tena๐๐๐
7.Kwenye ndoa; mwanaume hutafuta maixha ndipo huoa, mwanamke huolewa ndipo atafute maisha๐๐๐
8.Kwenye kukata tamaa; mwanaume hukata tamaa mapema ili jambo lisimsumbue, mwanamke hajui kukata tamaa hadi aumizwe๐๐๐
9.Kwenye kula;Mwanaume hushiba alafu huanza madoido, mwanamke huanza na madoido alafu badae hujilaumu hakushiba๐๐
10.Kwenye siri; Mwanaume hutunza siri hasa za aibu, mwanamke humueleza shoga yake badae hugombana nae baada ya kumrudia mwenyewe kwa siku 2 tu๐๐๐
Hizi ni baadhi tu ya sifa tofauti kati ya mwanaume na mwanamkeโฆ.. VIVA GENTLEMEN๐๐ฝ๐
Tabia za Kimama kwa wanaume
1, mwanaume kuoga haraka haraka ili uwahi kuangalia igizo, huo ni UMAMA..๐
2, mwanaume kupiga picha umeng’ata Lips na Unapiga na Camera Beauty Plus huo ni UMAMA..๐
3, Mwanaume kuangalia tamthilia na Jamai Raja na Maigizo kwenye chanel ya sinema zetu wakati mechi za kombe la dunia zinaendelea, pia nawe ni MMAMAAโฆ๐๐
4, Mwanaume kuandika ‘Jomon’ badala ya Jamani, kuandika ‘Pw’ badala ya Poa, kuandika ‘Thatha’ badala ya Sasa, kumwandikia mwanaume mwenzio ‘Mambo my’ Huu ni UDADA, tena UDADA wa CHUO..๐
.
5, Mwanaume kunywa soda au Juice na kubakisha, kununua chakula halafu unakibakisha, kubagua bagua chakula na kujamba hovyo hovyo baada ya kushiba, huo nao ni UMAMAA..๐
.
6, Mwanaume kumuuliza mwanaume mwenzio anapata faida gani kuangalia Mpira, pia nawe ni MMAMAโฆ
.
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Bangi si mchezo, Angalia kilichowakuta hawa
Bangi si mchezo!
Jamaa kaikoleza si ikamtuma avue nguo!
Akavua nguo zote akaenda kwenye kioo, kujitazama akaona kama kavaa suti!
then akaenda kama alivyo zaliwa kwa masela wenzake akawauliza vp suti imenikaa? Mvuta bangi mwenzie akamwambia “imekutoa kinyama ila tai umeifunga chini sana”.
Kuwa na mahusiano na msichana kama huyu ni changamoto, Mabinti bwana!
Binti: Hallow mpenzi, Mambo
Jamaa: Poa baby
Binti:Uko wapi?
Jamaa: Niko town napata lunch
Binti: Wow unarudi saa ngap? Nina njaa dear naomba uniletee msosi
Jamaa: Narudi baada ya nusu saa nikuletee nini?
Binti: Niletee chipsi kuku, soseji, mayai manne ya kukaangwa pembeni, baga, piza, coke take away baridi, mkate wa moto kwenye ile bekari ya wapemba na maji ya kunywa ya kiimanjaro.
Jamaa:Umesahau viti, meza, masufuria, sahani na beseni na vijiko.
Binti: Kwanini dear?
Jamaa: Naona hutaki kula unataka kufungua hoteli!
Mke anamwambia mme wake kuwa angetamani mme wake awe tajiri cheki alichojibiwa
Mke; mme wangu ungekuwa tajiri ningefurahi
Mimi; kwa nini?
Mke; ungekuta na sisi tuna gari nzuri hatutembeu kwa mguu
Mimi; ah wap,unadhani ningekuwa tajiri ningekuwa na wewe?ungekuta natoka na kina wema,zariโฆ
๐๐๐
naona anakusanya nguo zake itakuwa anaenda kufua
Angalia nilivyomkomoa huyu dogo
Kuna mtoto wa jirani ananibore sana kila nkimtuma kitu dukani lazima aonje,
Jana nlimtuma sukari akala yote..ย
Sahii nmemtuma superglue haongeiย Sipendi ujinga mimiย
๐ก๐ก๐ก๐ก๐ก๐ก


I’m so happy you’re here! ๐ฅณ











































































Recent Comments