SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Duh! Tamaa mbaya, cheki kilichompata Huyu

HAHAHAHAHAAAAAA DUH TAMAA MBAYA

Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna ki2, alipoifungua likatoka jitu la ajabu. Huku akitetemeka lile jitu likamwambia kijana asante sana kwa kuniokoa omba vi2 viwili sasa hivi. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko la hela na pete ya bahati vikadondoka. Akaambiwa ombi la pili,akasema nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada Hapohapo akageuzwa akawa chipsi yai.!!😂🤣🤣🤣

Jinsi ya kulima vizuri zao la kabichi

Kichwa cha kabichi kinapofunga vizuri, hutumika kama chakula na huvunwa baada ya kufunga na kukomaa vizuri. Kwa kawaida kabichi hupandwa kwa msimu mmoja, lakini iwapo itakuzwa kwa ajili ya kutoa mbegu hukuzwa zaidi ya msimu mmoja. Endapo inalimwa sehemu yenye maji ya kutosha, inaweza kulimwa msimu wote wa mwaka. Soko lake ni la uhakika katika kipindi chote na ni muhimu kwa afya. Pia, linaweza kutumika kama malisho ya mifugo
Mizizi: Mizizi ya kabichi hutawanyika ardhini vizuri. Kwa kawaida, huenda chini kiasi cha sentimita ishirini (20 sm), na hujitawanya kwa kiasi cha sentimita sabini na tano (75sm).
Shina: Shina la mmea wa kabichi huwa na rangi ya kijani au zambarau. Hii hutegemeana na aina ya kabichi, na kwa kawaida ni fupi.

Aina za kabichi

Kuna aina nyingi za kabichi na zifuatazo ni miongoni mwa aina hizo:
1. Prize drumhead

Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3.5
2. F1-High Breed

Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 2-4
3. Duncan

Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3
4. Early Jersey wakefield

Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3.5
5. Sugar loaf

Aina hii hukomaa mapema sana, kiasi cha miezi 2.5
6. Glory of enkhuizen

Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3.5

Jinsi ya kulima kabichi

Hali ya hewa

Kabichi hustawi vyema katika sehemu yenye hali ya baridi, hali ya joto jingi haifai kwa kabichi kwa kuwa huathiri uotaji na ukuaji wake. Joto jingi pia husababisha kulegea kwa vichwa vilivyofunga. Zao hili hustawi vema katika maeneo yenye mwinuko wa zaidi ya mita 100 toka usawa wa bahari.

Udongo

Zao hili linaweza kustawishwa kwenye udongo wa aina yoyote mradi tu udongo huo usiwe na chumvichumvi nyingi na usiotuhamisha maji. Udongo wa kichanga na ule usio na rutuba ya kutosha husababisha kabichi kukomaa upesi na kuzaa kabichi hafifu zenye vichwa vidogo.

Kitalu cha kabichi

Kitalu ni muhimu katika uzalishji wa zao hili. Ni vema kutengeneza matuta yenye upana wa mita moja, na urefu wowote kulingana na matakwa ya mkulima. Mbolea za samadi na zenye asili ya chokaa zichanganywe vizuri kwenye udongo. Kiasi cha gramu 500 za mbegu huhitajika kwa hekta moja. Katika upandaji kwenye kitalu ni vizuri kutengeneza mistari katika tuta, umbali toka mstari hadi mstari uwe sentimita ishirini (20). Udongo kiasi kidogo utumike katika kufunika mbegu.
Baada ya mbegu kuota ni vizuri kupunguza baadhi ya miche na uwe katika kipimo cha sentimita 2-3 toka mche hadi mche. Hii itasaidia kuwa na miche mifupi na yenye nguvu. Inafaa kunyeshea kitalu mara moja au mbili kwa siku na katika sehemu za joto ni vizuri kuweka kivuli katika matuta. Katika wiki ya tatu, hadi wiki ya nne, ni vyema kuondoa kivuli kidogo kidogo huku ukipunguza unyeshaji. Hali hii itasaidia miche isipate mshtuko wa uhamishaji shambani.

Kuhamisha na kupanda

Hamisha na kupandikiza miche shambani ikiwa na umri wa wiki nne, wakati huo miche ikiwa na majani manne ya mwanzoni na urefu wa kiasi cha sentimita kumi na mbili (12). Wakati wa upandaji, ni vizuri udongo ukashindiliwa kwenye kila mche. Inafaa upandaji ufanyike mara moja, na ni vizuri ukafanyika nyakati za jioni au asubuhi sana, na udongo uwe na unyevu wakati wote.

Nafasi kati ya mmea

Katika mstari hadi mstari inatakiwa iwe sentimita 60-75. Kutoka mmea hadi mmea ni sentimita 30-60. Pia sentimita 75-90 inaweza kutumika kati ya mstari na mstari.

Mbolea

Ni vizuri kuweka kiasi cha viganja 2-3 vya mbolea ya samadi iliyooza vizuri katika kila shimo.

Palizi

Wakati wa palizi ni vizuri mkulima akawa mwangalifu ili asiharibu mizizi. Wakati kabichi inapoanza kufunga hufunika ardhi, hivyo, husaidia kuzuia magugu yasiote, kwa wakati huu hakuna haja ya kupalilia.

Kuvuna:

Kabichi hukomaa katika kipindi cha siku 60-100 tangu kupandwa. Kwa ajili ya kuuza ni vizuri kuvuna wakati vichwa vinapofunga vizuri na huwa na uzito wa kutosha kabichi iangaliwe na kutunzwa baada ya kuvunwa ili isikwaruzwe na kuoza kabla ya kutumiwa. Kwa kawaida hekta moja hutoa mavuno kiasi cha tani 50-80.

Yafahamu Mambo Mbalimbali ya muhimu kuhusu kilimo cha Mazao ya Mboga Mboga kwa Ku-Download Kitabu cha MBINU ZA KILIMO BORA CHA MBOGA

Ni kitabu kinachotoa elimu ya Kilimo Cha Mboga. Kipo katika Mfumo wa PDF (Soft copy).

Kina kurasa 100 na utaalamu wa mazao zaidi ya 10, ambayo ni nyanya, kabichi, bamia, vitunguu maji, vitunguu twaumu, hoho, matikiti, karoti, uyoga na matango. Bila kusahau kilimo cha mboga kama chainizi na mchicha.

Pia utaweza kufahamu mbinu mbalimbali za kilimo cha mboga kama vile kuandaa shamba na kitalu, udhibiti wa wadudu na magonjwa katika mboga, kuvuna na kuhifadhi mboga, vilevile utajifunza kuhusu kilimo cha matone.

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Utani wa wahindi, cheka kidogo

Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili

(1) Mfa maji ?……………….. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?………… Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?……….. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?……………… Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?……. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?……… Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?…….. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?…… Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?……… Takosa guo ya sikukuu…
(10) Kila ndege ?………….. …Hutua Airport
(11) Bandu bandu ?….. …….Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?… Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?….Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?………. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?…….. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?…. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? …….. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? …………..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?…….. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?….Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?…….. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? ……….Taenda Chadema
(23) Bendera ?……………. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?……. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?………. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? …….. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.

Angalia nilichokifanya Jana kumkomoa x-wangu

Mwenzenu nilikatiwa umeme jana basi leo si nikaamua kwenda kununua luku ya 10,000. Kufika njiani nikatamani fursana nikaingia kijisupermarket mara sindo nakutana na ex wangu! Mshenzi yule kaniona mimi sijui alikua na mpango wa kununua vocha ya jero eti kabadili kanunua vocha ya buku tano ilimradi nione maisha yake safi tangu tuachane. Mambo ya kijinga spendi kudadeky nimetoa buku kumi nikanunua mipampers nami nijifanye nimeowa nina mtoto halafu huyoo nikashika njia yangu.

Sasa washkaji zangu tafadhalini mwenye mtoto au shida ya pampers naomba anunue kwangu maana leo nalala tena kiza 🙆‍♂

Jinsi ya kuepuka kunuka mdomo

Kuwa na harufu mbaya mdomoni ni kitendo kinachoweza kuathiri maisha ya mtu kimahusiano si kwa mpenzi tu bali marafiki na jamii kwa ujumla. Pia kuwa na harufu mbaya mdomoni uondoa haiba ya kupendwa kwani hata unapoongea wengi watakwepa kuongea moja kwa moja na wewe kwa sababu ya harufu mbaya inayotoka mdomoni mwako.

Chakula unachokula kina athiri hewa inayotoka mdomoni au sehemu nyingine za mwili wako. Baadhi ya vyakula vina matokeo mabaya sana kwa hurufu unayotoa mdomoni. Harufu mbaya mdomoni si ugonjwa wa kuambukiza haina haja kuogopa ukikutana na mtu mwenye harufu mbaya mdomoni kwamba atakuambukiza.

Pia tatizo kubwa ni kwamba watu wenye harufu mbaya mdomoni hawajijui kwamba wana harufu mbaya. Asilimia 85 – 90% ya tatizo la harufu mbaya mdomoni asili yake ni kinywa chenyewe. Pia kiwango cha harufu hutofautiana kutokana na muda (mchana, usiku na asubuhi).

Harufu nyingi mbaya mdomoni hutokana na vyakula vyenye asilia ya protein. Kuna zaidi ya aina 600 ya bacteria wanaoishi kwenye kinywa cha Binadamu (sehemu ya juu ya ulimi, fizi na kuzunguka meno).

 

KINACHO SABABISHA HARUFU MBAYA MDOMONI

 

Kutokuwa makini na usafi wa kinywa kama vile kupiga mswaki vizuri kunakoacha mabaki ya chakula ambayo huoza na kusababisha harufu mbaya mdomoni. (Wengi hupiga mswaki haraka haraka na kuacha mabaki ya chakula). Maambukizi ya magonjwa kama vile fizi kutoka damu, mfumo wa upumuaji na kisukari. Kinywa kuwa kikavu kutokana na madawa (medications) Kuvuta sigara, kunywa kahawa, ulaji wa vyakula vyenye viungo vikali kama vile vitunguu maji au thaumu.

 

NAMNA YA KUJUA KAMA UNA HARUFU MBAYA MDOMONI

 

Wanasayansi wamekiri kwamba ni ngumu sana mtu kujijua mwenyewe kama ana harufu mbaya kwa sababu ya mazoea (habituation).
Ni rahisi sana kutambua harufu kutoka kwenye kinywa cha mtu mwingine. Unaweza kutambua kama una harufu mbaya mdomoni kwa kumuuliza mtu unayemuamini.
Pia unaweza kujua harufu mbaya kwa kulamba nyuma ya kiganja na kunusa, wengine hupumua mbele ya kioo na kunusa. Pia unaweza kutumia kijiti cha kuchokonolea meno na kukinusa. Kisayansi unaweza kutumia vifaa kama Halimeter, Gas Chromatography na BANA Test.

NAMNA YA KUJILINDA NA HARUFU MBAYA MDOMONI (TIBA) 

 

Kula vyakula vyenye afya na vyakula ambavyo wakati unakula vinaweza kusafisha kinywa vizuri. Kusafisha meno mara kwa mara au kwa uchache mara mbili kwa siku asubuhi na baada ya mlo wa usiku, hii usaidia kuondoa au kujikinga na harufu mbaya mdomoni. Vilevile unashauriwa kutumia KISAFISHA ULIMI (tongue cleaner) kusafishia ulimi wako. Tumia bazooka (chewing gum) ambazo husaidia kuongeza kiasi cha mate kwenye kimywa kilichokauka. Baadhi ya gums zina viungo vinavyoondoa harufu mbaya mdomoni na zingine husafisha kinywa na bacteria wanaosababisha harufu mbaya. Tumia dawa ya kusukutua mdomoni (mouthwash) kabla ya kulala usiku. Kuwa makini na afya ya kichwa chako kama vile kupiga mswaki vizuri, kuondoa mabaki ya vyakula kwenye meno na kumuona daktari kila unapoona una Matatizo ya meno au kinywa au kila baada ya miezi sita kwa uchache.
Kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku angalau glass mbili za maji.
Mwone daktari wako ukiona una tatizo la harufu mbaya mdomoni.

NAMNA YA KUJIKINGA NA KUONDOA HARUFU MBAYA MDOMONI!

Watu wengi husumbuliwa na tatizo la kunuka mdomo bila hata kujijua hivyo kuwa kero kwa wenzao na wakati mwingine hujishushia hadhi mbele ya jamii. Mara nyingi ugonjwa wa kunuka mdomo (Halitosis) husababishwa na uchafu wa kinywa na ulaji wa vyakula usiosahihi lakini ni tatizo linalotibika.

Ni rahisi kulizuia na kuliondoa tatizo la kunuka mdomo iwapo utaamua kufuata kanuni za usafi wa kinywa na unywaji wa maji kwa kufuata kwa makini muongozo ufuatao:

KUPIGA MSWAKI

Kitu cha kwanza kufanya ni kupiga mswaki kwa ukamilifu kila uamkapo asubuhi. Wakati wa kupiga mswaki, utatakiwa siyo tu kusugua meno, bali pia ulimi, sehemu ya katikati hadi karibu na koromeo kwa kusugua vizuri.
Vile vile kila uamkapo baada ya kulala mchana au jioni, hakikisha unapiga mswaki, kwani bakteria wa kinywani, hutawala kinywa kila ulalapo. Mara baada ya kupiga mswaki na kusugua ulimi sawaswa, hakikisha unasukutua vizuri kwa maji, kwani hapa ndipo baadhi ya watu hukosea kwa kupiga mswaki bila kusukutua kwa maji.

KUNYWA MAJI MENGI

Maji ni muhimu sana karibu kila eneo la mwili wa binadamu. Unywaji wa maji ya kutosha kila siku utakusaidia kudhibiti na hatimaye kuondoa tatizo la kunuka mdomo. Unywaji wa maji mengi ni muhimu, hasa kwa wale watu wenye ugonjwa wa kukauka midomo (xerostomia).

Mara nyingi harufu itokayo mdomoni, hutokea tumboni na siyo kinywaji peke yake kama unavyoweza kudhani. Hivyo, kama tumbo litakuwa chafu, hata kama utasafisha kinywa vizuri bado harufu mbaya inaweza kuendelea kutoka. Harufu mbaya ya tumboni hutokea pale tumbo linapokuwa chafu kutokana na kutopata choo kwa muda mrefu. Miongoni mwa mambo yanayochangia kukosekana kwa choo kwa muda mrefu ni pamoja na tabia ya kutokunywa maji ya kutosha kwa siku, hivyo hakikisha unakunywa maji, kiasi kisichopungua lita moja na nusu hadi mbili au zaidi, kutegemeana na kazi unazozifanya.

Ukiwa na tatizo la kukaukiwa maji mwilini kila mara, mwili hujaribu kutumia njia zake za kiasili kupunguza uzalishaji wa mate ili kuhifadhi maji kwa ajiili ya matumizi mengine, kitendo hicho huchangia kunukisha mdomo kwa sababu ndani ya mate huwa kuna kinga muhimu dhidi ya baktetria wanaonukisha kinywa.

Kwa upande mwingine, ili kuzuia kinywa kunuka pale mdomo unapokuwa umekaukiwa na mate, ni vizuri kutafuna vitu kama bazooka (chewing gum) yoyote ili kuzalisha mate ambayo huhitajika katika kudhibiti bakteria.

MWISHO:

Hakikisha unasukutua sawaswa baada ya kula chakula chochote, hata kama ni juisi isipokuwa unapokunywa maji tu ya kawaida. Bila shaka, ukizingatia haya, tatizo ulilonalo la kunuka mdomo litataoweka na kubaki historia.

Faida za kufanya Masaji kiafya

Masaji uongeza kinga ya mwili

Masaji kushuka kwa homoni inayohusika na kupunguza maambukizi mbalimbali homoni ijulikanayo kama ‘cytokines’ vile vile masaji inashusha homoni inayohusika na matendo ya mashari homoni ijulikanayo kama ‘cortisol’.

Kufanya masaji hakukufanyi ujisikie ni mtulivu peke yake, bali pia kunaweza kukuongezea kinga yako ya mwili.

Masaji ya dakika 45 kwa siku imethibitika kuongeza uwingi wa seli nyeupe za damu (lymphocytes) ambazo ndizo hupigana dhidi ya vijidudu nyemelezi vya magonjwa mbalimbali mwilini.

Kufanya masaji huondoa tatizo la kukosa usingizi

Tafiti nyingi zinasema masaji inao uwezo wa kuamsha mawimbi ndani ya ubongo yanayohusiana na kutengenezwa kwa usingizi mzito (delta waves) na hii ndiyo sababu kwanini wengine hupitiwa na usingizi mzito mara tu baada ya mazoezi ya masaji.

Tatizo la kukosa usingizi linaweza kutibika kwa kufanya masaji tu kwakuwa masaji husaidia kupunguza uchovu na kuongeza uwezo wa kupata usingizi mtulivu kwa watu wa rika zote yaani watoto wadogo mpaka wazee ikihusisha wale wenye matatizo ya akili, kansa na magonjwa ya moyo, machache kati ya magonjwa mengi yawezayo kutibika kwa masaji tu.

Kuondoa mfadhaiko wa akili au Stress

Masaji huondoa hamaki na maumivu huku yakiongeza uwezo wa kupata usingizi mzuri na wa uhakika.

Masaji huondoa huzuni

Watafiti wanasema kuwa masaji kuongezeka homoni ijulikanayo kama ‘oxytocin’ na kupungua kwa homoni nyingine iitwayo ‘adrenocorticotropin’.

Oxytocin inahusika na matendo ya huruma, maono, upendo na ushirikiano wa kijamii. Wakati adrenocorticotropin yenyewe huhusika na kupungua kwa mfadhaiko (stress) moja kwa moja.

Kuondoa maumivu mbalimbali mwilini

Masaji hupunguza maumivu hasa ya mgongo na maumivu ya kichwa na maumivu ya kwenye mishipa.

Masaji huongeza uwezo wa kujiamini

Masaji hutuliza mwili na kuongeza concentration

Cheki hawa wachungaji

CHEKA KIDOGO

Wachungaji watatu walikutana kwa siri na kuelezana matatizo yao ili waweze kuombeana.

MCHUNGAJI WA KWANZA: mimi tatizo langu ni wizi, kila nikimaliza ibada lazima niibe pesa za sadaka.

WA PILI: Mimi tatizo langu ni wanawake yani nimeshalala na wana kwaya wote pamoja na mke wa ASKOF.

WA TATU akaanza kulia badala ya kuongea.WENZAKE:

We vp unatatizo gani mbona unalia???

AKAJIBU: jamani mimi tatizo langu ni “umbea” haya yote tuliyoongea lazima nikaseme!

😂😂😂😂😂👆🏻😂😂

Magonjwa hatari 10 yanayotibika kwa kutumia mbegu za Maboga

Mbegu za maboga zina protini na madini ya kutosha na ya mhimu zaidi mwilini kama madini ya zinki, kopa, maginizia, manganizi na chuma, mbegu za maboga ni tamu na zinaweza kutafunwa nyakati zozote na mahali popote hasa kwa wapenda kutafuna-tafuna kama mimi. Tafiti mbalimbali zimethibitisha pasipo na shaka kuwa mbegu za maboga zina faida nyingi kiafya na zina uwezo wa kukuepusha na magonjwa hatari zaidi ya 10 yafuatayo:

1. UGONJWA WA MOYO:

Kiasi kingi cha madini ya magnesium katika mbegu za maboga yanazifanya mbegu hizi kuwa mhimu sana kwa watu wenye magonjwa mbalimabli ya moyo. Madini ya magnesium ni mhimu kwa ajili ya kuimarisha msukumo wa damu kwenye moyo na kuimarisha afya ya mishipa ya damu hatimaye kutibu na kuzuia magonjwa ya moyo. Mbegu hizi pia zina mafuta mengine mhimu zaidi kwa watu wenye ugonjwa wa moyo yenye OMEGA 3.

2. HUIMARISHA KINGA YA MWILI:

Mbegu za maboga zimebarikiwa kuwa na kiasi cha kutosha cha madini ya zinki (zinc). Kazi kubwa ya madini ya zink ni kuimarisha kinga ya mwili. Upungufu wa madini ya zink unaweza kupelekea matatizo kadhaa mwilini ikiwemo kuzaa watoto njiti, kuishiwa nguvu za kiume, matatizo ya homoni, chunusi nyingi mwilini, watoto kuwa na uwezo mdogo shuleni kimasomo na matatizo mengine kadhaa ya kimwili na kiakili.

3. HUONGEZA UWEZO WA MACHO KUONA

Mbegu za maboga zina Vitamini E, vitamini A, lutein, beta-carotene na zeaxanthin, vitu hivi vinavyopatikana katika mbegu za maboga ni mhimu kwa ajili ya nuru ya macho. Vitamini A na madini ya zinki ni mhimu kwa ajili ya uzalishaji wa ‘melanin’ kimeng’enya mhimu ambacho hutengenezwa kwa asili na miili yetu kwa ajili ya ulinzi wa afya ya macho.

4. KINGA YA KISUKARI

Kisukari ni moja ya ugonjwa unaoendelea kwa kasi kuwasumbua watu wengi kila pembe ya dunia. Mbegu za maboga zina vitu vitatu mhimu zaidi ambavyo ni ‘Nicotinic acid’, ‘Trigonelline’ na ‘D-chiro-inositol’ ambavyo husaidia kushusha damu sukari mwilini na kudhibiti kazi za insulini hivyo kuwa kinga na kuleta ahueni kubwa kwa watu wenye kisukari.

Kama unasumbuliwa na kisukari fanya mazoea ya kutafuna mbegu za maboga kila siku na unipe mrejesho hapa.

5. DAWA BORA YA USINGIZI

Mbegu hizi zimegundulika pia kuwa na kirutubisho kinachozalisha homoni za usingizi. Kwenye mbegu za maboga kuna vimeng’enya viwili mhimu zaidi ambavyo huhusika na usingizi na afya ya akili moja kwa moja navyo ni ‘L-tryptophan’ na ‘tryptophan’. Gramu 100 tu za mbegu za maboga zina kiasi cha kutosha cha ‘tryptophan’ mpaka mg 576. Tryptophan ndiyo inahusika kuleta usingizi wenye utulivu pia huondoa msongo wa mawazo au stress mwilini. Kwa kuongezea mbegu za maboga zina kiasi kingi cha vitamini za kundi B. Muda mchache kabla ya kwenda kulala tafuna mbegu za maboga na utapata usingizi mtulivu kabisa mpaka asubuhi.

Kwahiyo kama una tatizo la kukosa usingizi jaribu kutumia mbegu za maboga na uniletee majibu hapa. Kumbuka kukosa usingizi mara nyingi huwa ni matokeo ya msongo wa mawazo na kama ulivyoona mbegu hizi zinaondoa pia stress! Kazi ni kwako ndugu.

6. DAWA BORA YA UVIMBE

Mbegu za maboga zinao uwezo mkubwa wa kuondoa sumu mwilini sambamba na uvimbe (inflammation). Kama ujuavyo sehemu kubwa ya vivimbe mwilini ni matokeo ya sumu kadhaa mwilini. Mbegu za maboga zitakuondolea uvimbe mwilini bila kukuachia madhara yoyote mabaya hapo baadaye. Kama unasumbuliwa na uvimbe popote jaribu kutumia mbegu za maboga na utuletee majibu. Mbegu za maboga pia ni dawa nzuri kwa aina nyingi za kansa mwilini.

7. HUONGEZA MAZIWA KWA MAMA ANAYENYONYESHA

Mbegu za maboga zina protini nyingi bora itokanayo na mimea isiyo na madhara kama ile ya kwenye wanyama. Pia zina OMEGA 3. Mama mjamzito hata unayenyonyesha tumia mbegu za maboga na utakuwa na uhakika wa kutoa maziwa ya kutosha kwa ajili ya mtoto.

8. DAWA NZURI KWA MATATIZO YA TEZI DUME

Wataalamu wengi wa lishe wanapendekeza mbegu za maboga zitumike kwa wanaume wa rika zote yaani vijana hadi wazee kwani zimethibitika kuwa msaada mkubwa kwa afya ya tezi dume. Tafiti nyingi zinasema mbegu za maboga zina kiasi kingi cha madini ya Zinki madini ambayo ni mhimu SANA kwa afya ya tezi dume na husaidia uponyaji wa tatizo la tezi dume moja kuwa kubwa kuliko nyingine tatizo lijukanalo kwa kitaalamu kama ‘benign prostatic hyperplasia’. Wanaume kazi ni kwenu.

9. ZINAONGEZA NGUVU ZA KIUME

Maajabu mengine ya mbegu za maboga ambayo ulikuwa huyajuwi bado.

Utaniuliza kivipi zinaondoa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume? Kwanza kabisa zinaondoa msongo wa mawazo/stress kitu ambacho ni namba 1 katika kusababisha upungufu wa nguvu za kiume, lakini pia zinashusha lehemu (cholesterol), zinatibu kisukari, zinatibu tezi dume (matatizo kama ya ngiri nk), zinashusha kisukari, zina protini nyingi ya kutosha na yenye ubora na mbaya zaidi ni kuwa zina madini ya ZINKI madini mhimu kuliko kitu kingine chochote kwenye upande wa nguvu za kiume na kinga ya mwili. Bado huelewi? Zina madini ya chuma pia

Uzuri ni kuwa mbegu hizi hazina uchungu wowote, ni tamu kuzitafuna wakati wowote na mahali popote hata ukiwa ofisini unaweza kuwa nazo pembeni unatafuna huku unaendelea na kazi zako. Sambamba na hilo kama tulivyoona pale juu kwamba zinaongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha kwa upande wa wanaume zinaongeza pia uwingi wa mbegu za kiume (sperm count) ukitafuna mbegu za maboga siku mbili tu utaona ukimwaga bao linatoka la kutosha na zito kweli kweli basi ujuwe ni mbegu za maboga hizo.

10. ZINAONDOA PIA MSONGO WA MAWAZO (STRESS)

Msongo wa mawazo au stress kama mlivyozoea wengi ni tatizo linaloendelea kuwasumbua watu wengi miaka ya sasa. Mbaya zaidi wengi huwa hawaelewi nini madhara ya hizo stress wanazojipa. Yaani stress au msongo wa mawazo unaweza kukuletea magonjwa mengine mwilini zaidi ya 50, hivyo utaona ni jinsi gani ilivyo mhimu kwako kuweka chini stress zako na uendelee na maisha kwani kuendelea kuwa na stress ni hatari zaidi kwa afya yako.

Moja ya sababu kuu ya watu wengi kuwa na stress ni usawa usio sawa wa homoni zao (hormonal imbalance). Hivyo kama una tatizo la homoni kwenye mwili hebu weka mazoea ya kutafuna mbegu za maboga kila siku na hutakawia kuona tofauti. Mbegu za maboga zina kimeng’enya mhimu sana kwa kutuliza mawazo kiitwacho ‘tryptophan’ na asidi amino zingine mhimu zinazohusika kutengenezwa kwa homoni nyingine ijulikanayo kama ‘serotonin’. Kama ulikuwa hujuwi ni kuwa serotonin ni homoni inayohusika na kazi mhimu sana ya kurekebisha matendo ya kitabia na kutoa matokeo chanya kwa mambo yanayohusu usingizi, hali ya mawazo kwa ujumla na mambo yanayohusu njaa.

Mbegu za maboga ni msaada mkubwa kwa kina mama waliofikia ukomo wa siku zao na huondoa matatizo ya kiafya yatokanayo na kukoma kwa hedhi. Ni msaada kwa watu wenye saratani mbalimbali, huimarisha ukuaji na ustawi wa mifupa na meno, huondoa harufu mbaya ya kinywa na husaidia pia wenye tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu kila mara.

NAMNA NZURI YA KULA MBEGU ZA MABOGA:

Unaweza kula zikiwa kavu na ndiyo utapata faida nyingi zaidi ingawa mimi napenda kuzikaanga kidogo kama dakika 15 hivi na huwa nazichanganya na maji ya chumvi ya mawe ya baharini kidogo kwa mbali ili kupata radha.

Unahitaji ujazo wa kiganja kimoja cha mkono wako cha mbegu za maboga kwa siku ujazo wa kama nusu kikombe cha chai hivi kwa siku.

Eti wanadamu walikuja vipi duniani

Mtoto wa miaka sita alimuuliza babake:
MTOTO: Baa, eti sisi wanadamu tulikuja vipi
duniani?
BABA: Mungu alimuumba Nabii Adam na Hawa.
Kisha wao wakaanza kuzaa watoto na watoto
wakazaa mpaka tukazaliwa sisi. (Mtoto hakuridhika
akamfuta mamake)
MTOTO: Mma, eti sisi wanadamu tulikuja vipi
duniani?
MAMA: Wanasayansi wamesema sisi tulitokana na
manyani baadae tukawa binadamu. (Mtoto akarudi
kwa baba)
MTOTO: Baa mbona mama ansema sisi tulikuwa
manyani mwanzo?Au wanidanganya?
BABA: Mwanangu, mimi nimekuelezea kuhusu ukoo
wetu. Mamako amekuelezea kuhusu ukoo wao😂😂🚶🏼🚶🏼🚶🏼

Madhara ya Kuvaa viatu virefu wakati wa Ujauzito

Wakati wa ujauzito ni kipindi cha kubadili mambo mengi katika mfumo wa maisha wa mjamzito. Mjamzito anapaswa kubadili mambo mbalimbali ili kuhakikisha anakua na afya nzuri katika kipindi chote cha ujauzito na ili kuhakikisha kwamba atajifungua mtoto mwenye afya nzuri. Moja ya mambo makubwa ni pamoja na tabia ya kuvaa viatu vyenye visigino virefu. Mjamzito hashauriwi kuvaa viatu vyenye visigino virefu kutokana na athari zinazoweza kutokana na aina hizi za viatu.

Zifuatazo ni athari za kuvaa viatu vyenye visigino virefu wakati wa ujauzito:

Mimba kutoka.

Mjamzito akivaa viatu vyenye visigino virefu anakua katika hatari kubwa ya kuanguka. Hii huweza kusababisha majeraha makubwa kwa mtoto aliyeko tumboni hali inayoweza kusababisha mimba kutoka.

Maumivu ya misuli ya mapaja.

Wadada hupenda kuvaa “high heels” husababisha misuli ya mapaja kukaza na kuwa na muonekano mzuri. Katika ujauzito, mabadiliko ya homoni huweza kupelekea misuli hii kuwa na maumivu tofauti na ilivyokua kabla ya ujauzito.

Hatari ya kuanguka.

Ni wazi kuwa uzito huongezeka wakati wa ujauzito na mabadiliko ya vichocheo vya mwili huweza kupelekea kizunguzungu cha hapa na pale. Hii huongeza hatari ya kuanguka iwapo utavaa “high heels” na kupelekea majeraha kwako na kwa mtoto aliyeko tumboni.
Uvimbe miguuni.
Ni jambo la kawaida miguu kuvimba wakati wa ujauzito. Kuvaa viatu vyenye visigino virefu na vyenye kubana huweza kuongeza tatizo hilo na kupelekea maumivu.

Maumivu ya mgongo.

Wakati wa ujauzito, uzito mkubwa huhamia mbele na misuli ya nyonga hulegea. Mabadiliko haya ya kimsawazo huweza kusababisha maumivu ya sehemu ya chini ya mgongo na kiuno.

Mambo ya Kuzingatia kama ni lazima kuvaa

Iwapo kuna ulazima sana wa kuvaa viatu hivyo, unapaswa kuzingatia yafuatayo:

  1. Epuka visigino vyembamba sana.
  2. Usivae siku nzima. Vitoe mara kwa mara kupumzisha miguu.
  3. Epuka kutembea au kusimama muda mrefu ukiwa umevivaa.
  4. Ukihisi maumivu kwenye misuli ya mapaja jaribu kufanya mazoezi ya kujinyoosha na kujikanda.
  5. Ni salama kuvaa viatu hivi katika muhula wa kwanza wa ujauzito (Miezi mitatu ya mwanzo).
  6. Viatu visiwe virefu sana na visigino viwe imara.
  7. Vaa viatu visivyo na bugdha na usivikaze sana.

BADILIKA: Anza kupiga hatua ya maendeleo sasa

Ili kutoka hapo ULIPO uweze kwenda HATUA inayofuata kuna SWALI muhimu sana unahitaji kujiuliza.
Watu ambao huwa wanashindwa kupiga hatua katika maisha yao ni kwa sababu huwa wanajiuliza kinyume cha swali hili.
Swali hili ndilo wanalojiuliza watu wote waliofanikiwa:

Swali: “Hivi kwa sasa nina nini ambacho naweza kuanza kukitumia kama mtaji wa kwanza kuanza kufanya ninachotaka”?

Siku moja wakati nasoma biblia niliona Mungu alipotaka kumtumia Mussa kuokoa wana wa Israel akamuuliza-

“Una nini mkononi mwako”-

Mussa akajibu
kwa kudharau alichonacho kuwa “Nina fimbo kavu tu ya kuchungia mifugo”.

Ndipo Mungu alianza kumuonyesha miujiza kutumia fimbo ambayo siku zote
alikuwa nayo na kujidharau ndiyo ambayo ikatumika kwenda kuokoa wana wa Israel.

Watu wengi sana wanashindwa kuanza kwa sababu huwa wanajiuliza-

“Hivi ninakosa nini ili niweze kuanza”
badala ya ‘Hivi nina nini cha kuanzia’.

Cha kuanzia sio lazima iwe pesa-Inawezekana ni uwezo wa kufanya jambo fulani la kipekee,inawezekana ni
mahusiano mazuri uliyonayo na watu fulani(mtandao wako),inawezekana ni uzoefu ulionao,inawezekana ni kipaji n.k
Leo unapoanza siku yako naomba ijiulize-

“Nina nini mkononi mwangu ambacho naweza kutumia katika
hatua ya kwanza”?.

Kumbuka hakuna mtu ambaye hana
kitu kabisa-KITAFUTE HADI UKIPATE NA ANZA KUKITUMIA KUCHUKUA HATUA.

Share ili wengine wajifunze…..uwe na Jumatatu njema……..

Njia 8 za kupata mtaji kwa ajili ya Biashara yako

Njia hizo ni kama ifuatayo!!

1. Mtaji mbadala
Mtaji mbadala unarejelea rasilimali au mbinu ambazo zinaweza kutumika badala ya fedha katika kuendeleza biashara au mradi fulani. Ni muhimu kuelewa kwamba si kila hatua inahitaji matumizi ya fedha taslimu. Kuna nyakati ambapo unaweza kutumia rasilimali zingine ulizonazo ambazo zinaweza kuchukua nafasi ya fedha. Kwa mfano, mtu anaweza kutumia nguvu zake mwenyewe katika kutengeneza kitu kama bidhaa au katika kutoa huduma, hivyo kuokoa gharama ambayo angehitaji kulipa mtu mwingine kufanya kazi hiyo.

Ujasiriamali unahusisha pia kutumia maarifa na uzoefu ambao mtu amepata katika fani au sekta fulani. Maarifa haya yaliyotokana na mafunzo au uzoefu yanaweza kugeuzwa kuwa bidhaa au huduma bila ya gharama za ziada. Halikadhalika, mtaji mbadala unaweza kujumuisha kutumia umaarufu au jina lako kuvutia wateja au wabia bila haja ya matangazo ya gharama.

Kukopa au kuazima ni njia nyingine ya mtaji mbadala. Badala ya kutumia akiba yako ya fedha au kuchukua mkopo wa riba kubwa, unaweza kuazima vifaa au pata mikopo isiyo na riba kutoka kwa marafiki, familia, au taasisi zinazotoa mikopo midogo midogo.

Ubunifu ni sehemu muhimu ya mtaji mbadala. Kwa kutumia ubunifu, mtu anaweza kubuni njia mpya na tofauti za kutekeleza miradi ambazo hazihitaji fedha nyingi. Hii inaweza kujumuisha kufanya biashara kwa njia ya kubadilishana bidhaa na huduma (barter trade) au kuanzisha njia mpya ambazo zinapunguza gharama za uendeshaji.

Kipaji ni rasilimali nyingine ambayo inaweza kutumika kama mtaji mbadala. Kwa mtu mwenye kipaji kikubwa katika sanaa, muziki, riadha, au tasnia nyingine, kipaji hicho kinaweza kuwa njia ya kujipatia kipato bila haja ya kuwekeza fedha nyingi. Uwezo binafsi uliojengwa kama vile uongozi, mawasiliano na uwezo wa kushawishi watu, pia ni mali ambazo zinaweza kutumika kama mtaji mbadala.

Kwa ujumla, dhana ya mtaji mbadala inasisitiza umuhimu wa kuchangamkia rasilimali na vipawa tulivyonavyo, na kutafuta njia mbadala za kufanikisha malengo bila kutegemea fedha taslimu pekee.

2. Kupata mtaji kwa ndugu, jamaa na marafiki

Watu wengi wanakuwa kwenye umaskini wakati wamezungukwa na ndugu matajiri kisa wanaona aibu kuomba msaada, lakini amini usiamini watu wengi wametajirika kupitia ndugu, jamaa na marafiki, mfano mtu tajiri kuliko wote barani Afrika kutoka Nigeria ndugu Dangote yeye alivyotaka kuanza ujasiriamali aliomba msaada toka kwa mjomba wake ambaye alimuazima kama milioni 3 hiv , kwa kuwa aliona fursa kwenye mambo ya ujenzi (cement) yeye akaanza kununua cement na kuuza leo hii ndugu Dangote amekuwa bilionea ambaye amewekeza sana barani Afrika anauza cement, unga , mchele, mafuta, sukari na saa hivi anauza mafuta kule Africa Magharibi hata hapa Tanzania tuna kiwanda chake kule Mtwara,

Kuomba msaada sio ishara ua udhaifu bali ni ishara ya nguvu kwamba unajiamini ndio maana unaomba msaada. kumbuka kwenye neno UJASIRIAMALI kuna neno Jasiri pia, huwezi kuwa na mali bila kuwa jasiri.Umezungukwa na watu waliobarikiwa usisite kuwaambia wakusaidie ,.

3. Kwa kujiwekea akiba.

Watu wengi sana hapa kwetu Tanzania ukiwaambia weka akiba wanakwambia mimi siwezi kuweka akiba, sina utamaduni wa kuweka akiba, hivyo mi nakushauri anza leo kujifunza kuweka akiba, ni ngumu sana kufika juu bila kuweka akiba kwa mfano kama umeajiriwa na unajua biashara fulani inataka milioni 2 ili kuifanya na wewe mshahara wako ni laki 4, kwa nini basi kila mwezi usiweke laki 1 pembeni, ndan ya miaka miwili utakuwa na milioni 2.4 huo ni mtaji wako wewe mwenyewe.

Usisite kuanza kidogo kwa kuweka akiba polepole mpaka ufike huko unakoenda.

4. Pata kazi ya ziada
Kama kipato unachopata hakitoshi unaweza kujitafutia kazi ya ziada kwa muda wako wa jioni au weekend ili uweze kupata ziada ya akiba kwa ajili ya mtaji.

Watu wengi wanatumia muda vibaya, Je baada ya kazi yako unafanya nini? ile saa 10 hadi saa 4 usiku unatumiaje muda wako? Jinsi unavyotumia muda huu itakupelekea kuwa tajiri au maskini

5. Pata Mtaji kwa njia ya kudunduliza
Hii njia ya kudunduliza ndio njia ambayo ni nyepesi kabisa ambayo watu wengi hawaioni, ukiamua kutumia njia hii kamwe huwezi kukosa mtaji, hii ina maana unaanza katika hali ya chini kabisa ya kufanya kitu chochote halafu ile faida unayoipata hauitumii bali unaiwekeza kwenye biashara yako.Tuone mfano wa dada Christine ambaye ni mfano mzuri wa mtaji wa kudunduliza

Christine Momburi alikuwa amejifungua na mume wake walikuwa wamemuachisha kazi kwa hivyo maisha hayakuwa mazuri sana,

Sasa siku moja walitembelewa na mgeni nyumbani kwao yule mgeni alipotaka kuondoka alimpa Christina shilingi 700 ili anunue maziwa ya mtoto, baada ya yule mgeni kuondoka Christina alijiuliza Je aitumie ile sh 700 kununua maziwa au afanyie nini hasa ili iweze kubadili maisha yake? kwa hiyo alijiuliza sana baadae akaamua kuichukua ile hela aende sehemu akanunue nyanya chungu na mboga mboga kwa bei ya jumla. Akazinunua akaenda kuuza, kwa siku ya kwanza ikatoka sh 700 kwenda 1500 akaongeza mtaji wake, ilikufupisha stori baada ya wiki moja Christina akawa na mtaji wa sh 25000/=.

Siku moja akasikia kuna mahali wanajenga wanataka mama lishe wa kuwapelekea chakula akachukua ile tenda akawa anawapelekea chakula, baadae akasikia kuna sehemu wanataka mtu wa kuwapelekea sare za shule. akawa anazidi kukua na kukua na hivi sasa Christina amekuwa ni mjasiriamali mkubwa pale Moshi ana maduka makubwa sana na amehojiwa na vyombo vya habari mbalimbali na yeye amekiri kwamba kudunduliza ndio kuliko mtoa.

Sasa swali la msingi nalotaka nikuulize ni swali lifuatalo:

Swali, Ni je ni Sh 700 ngapi zimepita mikononi mwako? Je ni Sh 7000 ngapi zimepita mikononi mwako? Je ni Sh 70000 zimepita mikononi mwako? vipi kuhusu laki 7 au milioni 7 ngap zimepita mikononi mwako? mara nyingi tumeidharau fedha na kuona ni ndogo lakini kumbuka nilishasema siku za nyuma kuwa kila shilingi inayopita mikononi mwako ni itazame kwa jicho la kimilionea.

Nikukumbushe kuwa tajiri kuna maumivu ambayo utayapitia, watu wengi hawataki kupitia maumivu ndio maana watu wachache sana wanakuwa matajiri., watu wengi wanapenda utukufu lakini hawataki kubeba msalaba.

Hivyo usidharau pesa bali fikiria kwa ubunifu jinsi ya kuizalisha fedha hiyo.

6. Pata Mtaji mdogo kupitia wawekezaji

Wakati mwingine kutokana na mazingira uliyonayo unaweza ukagundua kwamba una wazo zuri sana la biashara lakini hauna mtaji, hapa jambo la msingi ni kuangalia unaweza kumpata vipi muwekezaji ambaye atataka faida, ni afadhali ukawa na wazo ukawashirikisha wengine wakakupa mtaji halafu mkagawana faida kuliko kufa na wazo lako zuri,.

Sisi watanzania tupo nyuma sana katika suala la kufanya biashara pamoja ( Partinership) tofauti na wakenya.
mfano mzuri ni rafiki yangu anaitwa Elisha Edson yuko Iringa, yeye aliwaza kuanzisha kiwanda cha mbao hizi nguzo za umeme, bahati mbaya hakuwa na mtaji wa kutosha akaamua kuongea na marafiki zake zaidi ya 10 akamshawishi kila rafiki yake awekeze kiasi kadhaa cha fedha na kumpatia hisa kwenye kile kiwanda chake, rafiki zake walikusanyika waktoa fedha na sasa kiwanda kimeanzishwa na kinakaribia kutoa nguzo wakati wowote kuanzia sasa.

Je wewe una weza ukatumia njia hii? je una wazo ambalo unajua kabisa hili wazo nikipata wawekezaji wa nanmna hii? masharti yake yanaweza kuwa magumu sababu unaweza kuambiwa uandike mchanganuo wa biashara unao eleweka, na wazo lako la biashara lionekane limetulia kabisa.

Lakini ni afadhali ukapitia mchakato huu kuliko kuwa na wazo zuri halafu wewe huna fedha. na kumbe ungeweza kutoa ajira na kulipa kodi kwa nchi hii na kufanya wenzako wakanufaika na wazo ulilonalo.

7. Mtaji kwa njia ya Mgavi ( Supplier Financing)

Hii ni njia ya uhakika ya kupata mtaji wako. Naomba nitoe stori halisi , Miaka mingi iliyopita kijana mmoja anayeitwa Reginald alikuwa anatafuta kalamu za kuandikia mtaani kwake, lakin bahati mbaya baada ya kutafuta sana kwa muda mrefu alikosa kalamu pale mtaani kwake, jambo hilo lilimfanya aweze kushangaa sana na kujiuliza hivi kweli inawezekana vipi hakuna kalamu hapa mtaani? kwa hyo hilo likamfanya aanze kutafuta mbinu na maarifa ya yeye kuwa mtu ambaye analeta kalamu Tanzania. baada kufanya uchunguzi kwa marafiki mbalimbali wakati huo yeye alikuwa muhasibu tu, akaambiwa Mombasa kuna mtu ana kiwanda cha kalamu na baada ya kufanya mazungumzo na yule ndugu ikaonekana bwana Reginald angeweza kuwa anaingiza kalamu hapa Tanzania lakini hakuwa na mtaji, ndipo hapo ilibidi atumie mali kauli yaani awshawishi wale watu wampatie zile kalamu azilete hapa, aziuze halafu aweze kurejesha fedha na kuchukua faida yake.

Hivyo akaanza hiyo biashara kwenye chumba chake kidogo sebuleni akisaidiwa na familia yake baadae wahamia nje wakatengeneza banda la mabati tayari ikawa ndio kiwanda kwa ajili ya kupaki zile kalamu kwa pamoja. mwaka huo huo wa kwanza bwana Reginald alipata faida kubwa sana takriban bilion ya shilingi

8.Kupitia Taasisi za kifedha
Mada hii ni ndefu sana lakini tutajifunza huko mbele mada inayoitwa Jinsi ya kuishawishi benki ikukopeshe hata kama hukopesheki. hii mada tutaiongelea zaidi huko mbele , lakini nataka tu ujue ili benki ikukope inahitaji uwe na biashara ambayo imeshakuwepo kwa takribani miezi 6 au zaidi, pia watahitaji uwe na mzunguko mzuri wa fedha unaoeleweka, uwe na dhamana ambayo unaiweka ili kama unashindwa kulipa waweze kuichukua ile dhamana, watahitaji uwe umefanya usajili rasmi wa biashara yako., uwe na account ya benk n.k

Sasa basi kwa kuwa watu wanaogopa kwenda benki kutokana na yote haya ndipo unaweza kujaribu kutumia microfinances, hizi ni taasis za kifedha ambazo hutoa mikopo midogo midogo, kwa hiyo angalia kama huko ndiko unapoweza ukaponea. Zaidi ya hayo, taasisi hizi za kifedha zinajulikana kwa kutoa huduma zilizobinafsishwa zaidi, ambazo zinaweza kuwa na manufaa hasa kwa wajasiriamali wadogo na wa kati, watu binafsi, na biashara ndogo ndogo ambazo zinatafuta fursa za kukuza mitaji.

Microfinance institutions (MFI) zina sifa ya kuwa na mifumo inayoweza kufikiwa kwa urahisi, kwani mara nyingi hawana vikwazo vikali vya kielimu au kiuchumi kama vile benki kubwa. Wanaweza kutoa mikopo kwa riba nafuu na wakati huo huo kutoa mafunzo na ushauri wa kibiashara, ambayo yanaweza kuwa na manufaa makubwa kwa wakopaji.

Pia ni muhimu kufahamu kwamba MFI zinaweza kuwa na mitandao mikubwa inayowezesha huduma kufika hata vijijini ambako benki kubwa haziwezi kufika. Hii ina maana kwamba watu wanaoishi maeneo ya vijijini wanaweza kupata huduma za kifedha bila ya kuwa na ulazima wa kusafiri masafa marefu kwenda kwenye miji mikubwa.

Kwa kutumia huduma za microfinance, unaweza kupata fursa ya kuongeza mtaji, kuboresha biashara yako, na hata kupata elimu ya kifedha ambayo inaweza kusaidia katika kufanya maamuzi bora ya kibiashara na kifedha. Ni muhimu kuchunguza chaguzi zilizopo, kulinganisha tofauti za riba na masharti ya mkopo kabla ya kuchukua uamuzi wa kutumia taasisi fulani ya microfinance.

Madhara ya kubana mkojo muda mrefu

Utakubaliana na mimi kwamba, kitendo cha mtu kubanwa na haja ndogo siyo kitu cha hiyari kwamba sasa mtu anaamua ngoja nibanwe na mkojo, hili ni jambo la asili na ni matokeo ya vyakula, matunda au vinywaji tunavyotumia. Kwa lugha nyingine tumekuwa tukiita kuwa ni wito wa asili au nature’s call.

Yawezekana mtu akawa katika mkutano, safarini, akawa katika mitandao ya kijamii anachati au popote pale akiwa anafanya jambo fulani na kutokana na jambo hilo, mtu akaendelea kujibana na kutokwenda kuyapunguza maji haya kutoka katika kibofu cha mkojo kwa kutoa kipaumbele kwa shughuli anayoifanya kuliko kusikiliza kwanza wito huu wa asili. Mambo haya tunayafanya sana, utasikia, mkojo umenibana kweli, ila ngoja nimalizie hii kazi halafu niende kujisaidia, hivi ndivyo watu wengi wanafanya.

Kutokana na vyakula na vinywaji tunavyotumia, kibofu cha mkojo huanza kujaa mkojo, mkojo unapofikia karibu mililita 50 mpaka 500 mtu huanza kuhisi hitaji la kwenda kukojoa. Kibofu cha mkojo kimezungukwa na vigunduzi asili (Receptors) vinavyopeleka taarifa katika Ubongo kuonyesha kuwa kibofu cha mkojo kimekaribia au kimejaa, baada ya taarifa hizi kufika katika ubongo, ubongo unatoa taarifa katika kibofu cha mkojo ili kiweze kushikilia mkojo huo kwa kuikaza misuli maalumu (Sphincters) mpaka hapo muda wa wewe kwenda kukojoa utakapofika.

Kibofu cha mkojo hufanya kazi kwa mfumo wa kujiendesha wenyewe yaani, automatic, kitendo cha mtu kupuuzia kwenda kukojoa husababisha Ubongo upate usumbufu wa taarifa za kujaa kwa kibofu cha mkojo na kwa kuwa Ubongo nao hutuma taarifa katika kibofu cha mkojo kusema kuwa mkojo uendelee kushikiliwa mpaka muda muafaka utakapofika, itafika kipindi uwezo wa ubongo kutoa taarifa hizi na pia uwezo wa vigunduzi asili (Receptors) vilivyoko katika kibofu cha mkojo kupoteza uwezo wake tena wa kufanya kazi hizo au uwezo kuwa mdogo. Matokeo yake ni mtu siku kweli anahitajika kuvumilia kidogo ili afike sehemu inayostahihi kujisaidia, lakini hawezi tena na kujikuta muda mdogo tu….mtu tayari kaloanisha nguo yake.

Mpenzi msomaji, mtu kujibana na kupuuzia kwenda kukojoa husababisha uwezo wa kibofu cha mkojo kujitawala (control) upotee. Pia kama uwezo wa neva zinazopeleka taarifa kwenye ubongo kuhusu mabadiliko/ujazo wa kibofu cha mkojo zitaharibika, basi misuli maalumu ya kubana mkojo (sphincter) itashindwa kuachia na matokeo yake mtu ataendelea kukaa na mkojo katika kibofu chake kwa muda mwingi zaidi kitu ambacho ni hatari kwa afya yake. Endapo mkojo huu utashindwa kutoka, utatengeneza mazalia ya bakteria na kukusababishia magonjwa ya kibofu (bladder infection). Magonjwa ya kibofu cha mkojo ni pamoja na U.T.I (Urinary Tract Infections), pia huweza kusababisha magonjwa ya figo na mchafuko wa damu, bacteremia.

Kuna hali huwa inajitokeza kwa baadhi ya watu, yawezekana alikuwa kabanwa na mkojo au alikuwa hajahisi kwenda kukojoa, ila akinywa maji au akisikia sauti ya maji yanachuluzika mfano maji yakitoka bombani, basi atahisi kwenda kukojoa.

Mpenzi msomaji, ni vyema tukawa wasikivu pale mtu unapobanwa na mkojo, hii ni kwa ajili ya afya ya kibofu chako cha mkojo lakini pia ni kwa ajili ya afya yako kwa ujumla. Kama unalo tatizo, usisite kuonana na wataalamu wa afya.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About