Tenda Wema Uende Zako
Nimekuta panya ana struggle kuingia chini ya mlango wa jirani yangu…
Nikagonga mlango Jirani kafungua panya akapenya mi nkaenda zangu…..
Tenda Wema Uende Zako!!! Sipendi Ujinga mimi kwanini panya wa watu apate shida
Nimekuta panya ana struggle kuingia chini ya mlango wa jirani yangu…
Nikagonga mlango Jirani kafungua panya akapenya mi nkaenda zangu…..
Tenda Wema Uende Zako!!! Sipendi Ujinga mimi kwanini panya wa watu apate shida
Jamaa kaenda kanisani akakaa karibu na mrembo.
Wakati mahubiri yakiendlea jamaa akaanza kuingiza vocal:
Jamaa: dada mi nakupenda saana
Dem: Kaka naomba umsikilize mchungaji
Jamaa: nipe nafasi uwe msimamizi wa serikali ya moyo wangu…
Dem: niache…
Jamaa: kweli nakupenda mpnz
Dem: (kwa sauti kubwa) nmesema NIACHEEEE!!
Watu wote kanisani wakageuka… Jamaa kaona noma na ili atulize msala
Jamaa: sikuachi hadi ukiri YESU kuwa Bwana na mwokozi wa Maisha yako.
moyo wangu saafi kama upole wa tausi wingi wa baridi kama maji ya mtungi ,yote ni kutokana na mapenzi unayonipatia. ASANTE KWA KUNIPENDA MPENZI
Ngozi nyeusi katika magoti na nyuma ya mikono hutokana na mkusanyiko wa cells zilizokufa, na hata unavyoweka pressure kwenye magoti na vipepsi vya mikono yako. Kama ukiwa unaweka mikono kwenye meza ukiwa kazini, ule msuguano unafanya ngozi iwe nyeusi.
Kama una magoti myeusi na nyuma ya mikono pia ni peiusi, tumia hizi njia asili kuweza kuondoa weusi huo:
Juice ya Aloe Vera inasaidia kuondoa weusi, all you have to do ni kupaka juice hiyo kwenye sehemu yenye weusi na uache kwa nusu saa kisha nawa na upake moisturizer. Rudia kufanya hivi mara mbili kila siku.
Changanya vyote hivi utapata mchanganiko mzito, paka kwenye magoti na kwenye mikono yako palipo na weusi. Kaa nayo kwa dakika 30, nawa na paka moisturizer. Rudia hii kila siku kwa wiki 3-4, utapata matokeo mazuri.
Chukua pamba na uitumie kupaka juice ya ndimu katika sehemu zenye weusi. Au unaweza kuikata tu ndimu na kuipaka directly kwenye sehemu zenye weusi. Kaa nayo kwa lisaa 1 kisha nawa. Rudia hivi kila siku hadi weusi utakapopotea.
Changanya vizuri, hii itakuwa kama exfoliation/scrub kwa ajili ya magoti na mikono. Paka katika hizo sehemu zenye weusi kisha kuwa kama una-massage polepole. nawa kwa maji ya uvuguvugu kisha paka moisturizer.
Wakati unafikiria dingi yako afe ili urithi nyumba, dingi nae anafikiria uanze kufa ili apangishe chumba unacholala.. hiyo inaitwa kufa kufaana.. 😂😂😀😀😀😀😀😀😀 #Hatutaki ujinga
Kila unachokifanya natamani niwepo, nikitumainia kila
ndoto yako itimie kila muda na sehemu, niwepo nikikutakia
mafanikio mema kwasababu nakujali.
Simu huboa wakati mwingine, kwani ni lazima ufungue meseji
na kuzisoma, kuichaji simu kila mara, lakini usichoke
kwani ndiyo inayotuwezesha tuwasiliane
Moja ya sababu za kutokea chunusi katika ngozi yako ni kuwepo kwa takataka au uchafu juu ya ngozi yako na njia rahisi ya kusafisha taka hizo ni kwa kutumia baking soda hivyo kuifanya ngozi ipumuwe vizuri.
Kwahiyo ukiwa na chunusi hebu fikiri kuhusu baking soda. Baking Soda husaidia kubandua seli za ngozi zilizokufa na kufanya mafuta yaliyozidi kuondoka.
Ni rahisi zaidi kutumia baking soda kutibu chunusi. Chukua baking soda na uchanganye kidogo na vijiko vinne vidogo vya maji au vya maji maji ya limau na upake uji huo moja kwa moja kwenye chunusi. Subiri kwa dakika 10 na ujisafishe na maji ya moto.
Wanaume wengi hupenda kujua wao ni wangapi kuwa na mwanamke Fulani. Lakini mwanamke kamwe hawezi akakwambia wewe ni wa ngapi. Kumuuliza jambo hili kunamkera sana mwanamke na ndio maana mara nyingi hawezi akakwambia ukweli.
Mwanamke mara nyingi anakulinganisha na mpenzi wake wa zamani japokuwa hawezi kukwambia waziwazi. Wakati mwingine tabia hii huwafanya wanawake kuwatamani wapenzi wa zamani na hata kurudiana nao endapo watakosa mtu aliye bora kuliko mpenzi wake wa zamani.
Mwanamke kamwe hawezi kukwambia kasoro zako. Wanawake wanajua kumfichiaa mpenzi wao mambo wasiyotaka yajulikane kwa wengine na kwa mpenzi wake. Wanajua njia za kiujanja za kutumia ili kufichua siri zako zote. Mwanamke hawezi kukwambia kasoro zako kwa kuogopa kukuumiza.
Mwanamke hawezi kukwambia mapungufu yake labda kwa kuhofia kusheshwa thamani. Wanawake ni wasiri sana kwa mapungufu yao. Wanajua vyema hofu zinazomuandamana, vitu vinavyowakosesha usingizi na mambo yanayowalemea maishani japo sio rahisi kuonyesha. Kwa nje anaweza akaonekana yuko vizuri na hana tatizo kumbe ndani ana matatizo au mapungufu. Anaweza kufanya yote kufunika upungufu wake!
Hili halisemi kabisa mwanawake kwa sababu anaona haya kutumia maneno ya wazi kueleza raha unayompa. Maneno ya kuzuzua ni himaya ya wanaume, lakini wakati mwingine wapo wasioweza kuficha.
Wanawake wengi hawapendi kusema kama hawaridhiki Kwenye tendo la ndoa. Wanawake wanahitaji kuandaliwa vilivyo kwa dakika 10, 20 ama nusu saa. Mara nyingine wanaume huwahi kabla mwanamke hajawa tayari na hivyo kushindwa kuridhika lakini hawezi kusema.
Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.
Kasuku alisimama mlango wa kuingia supermarket wakapita wanawake watatu akasema nyeupe, nyekundu, kijani. Wale wanawake wakatatizika baada ya mda wakajua ni chupi walizovaa. Wakasema basi kesho tubadilisheni. Siku ya pili wakapita tena kasuku akasema nyeusi, manjano, zambarau. Loh! Wanawake wakastaajabu sana. Wakasema lazima wamshinde yule kasuku kwa hekima. Wakaambiana basi kesho tusivae chupi tuone kama ni kweli anaona mpaka ndani. Siku ilipowadia wakapita mbele ya kasuku akasema- kipilipili, kipara, rasta…
Mahindi ni miongon mwa mazao makuu ya chakula hapa nchin Tanzania na ulimwa karibu kila mkoa. Ulimwa zaidi nyanda za juu kusini katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Ruvuma, Njimbe na Katavi. Pia mikoa ya Morogoro Mwanza Dodoma Shinyanga Arusha Tanga na mikoa mingine. Kwakua ni zao la biashara hivyo karibu kila mkoa unalima zao hili.
★Chakula (stample food)
★Chakula kwa mifugo
★Nishati (biofuel)
☆Dawa za asiri(mbelewele zake)
☆kutengenezea mapambo.
☆mabaki utumika kama mbolea n.k.
Pia wapo wakulima waliojikita katika kulima zao hili kibiashara ambao uuza katika soko la ndani ya mkoa nje ya mkoa na nje ya nchi. Hapa itategemea uwekezaji wa mkulima husika.
Mahindi uota vizuri katika jotoridi lenye wastani wa 20-30 nyuzi joto za centigradi. Pia linaitaji mvua hasa wakati wa uotaji na uotaji wa mbelewele.
Kuna aina nyingi za mbegu. Zipo za Asili na pia zipo mbegu chotara (Hybrid F1 & F2) kutoka makampuni mbalimbali, za mda mfupi na za mda mrefu kulingana na kipindi/vipindi vya mvua kwa mwaka kwa mkoa usika.
Kwakua Tanzania ina kanda tofauti za hali ta hewa ikiwemo nyanda za juu kusini, nyanda za juu kaskazini, nyanda za kati na maeneo mengine ya pwani na pia ndani ya mkoa mmoja panaweza pakawa na matabaka tofauti yakijografia (geographical/ecological zone).
Hivyo mbegu za mahindi zinazofanya vizuri mikoa ya Pwani Morogoro Arusha Mwanza haziwezi kufanya viruzi katika mikoa ya Njombe Iringa n.k kwakua utofautiana katika ukanda.
Mbegu zinazofanya vizuri Njombe mjini ama wanging’ombe zinaweza zisifanye vizuri Ludewa ama Makete wilaya tofauti lakini mkoa mmoja.
Hivyo ni vema kujua kua mbegu upandao inafaa kwa ukanda upi?? Wa mvua za mda mrefu! Mda mfupi! Ama sehemu zenye ukame!!.
Hii itategemea aina ya mbegu na pia namna ya utunzaji ambao utegemea sana kusudi la ulimaji (chakula ama biashara).
Mche hadi mche ni sm 30-40. Mstar hadi mstari ni sm 70-75.
Yaani sm 75X30, pia waweza tumia sm 80X25 punje moja moja za mbegu chotara ya mahindi.
Ni vema ukapanda siku moja ambayo utaweka na mbolea. Anza na mbolea 5g kwa shimo fukia kidogo kisha weka mbegu ( mbegu moja kama ni Hybrid).
Mbolea nzuri zaidi yenye maboresho na lishe linganifu kwa mmea (balanced nutrition) ni YaraMila Cereal, Yara Vera Amidas na YaraBela Sulfan kutoka kampuni ya Yara Tanzania ltd. Mfuko mmoja mmoja, utapandia, utakuzia mkuzio wa kwanza na utamalizia mkuzio wa pili kama zilivyo orodheshwa hapo.
Hili lina gharama zaidi na linachukua mda mwingi na pia SIO SAHIHI kwakua halireti majibu mazuri katika kuzuia magugu.
Hapa utumika matandazo kama majana makavu, majani ya mgomba, pumba za mpunga n.k ( Mulching). Huitaji kujipanga zaidi na piaupatikanaji wa matandizo wakati wakilimo unaweza ukawa ni shida.
Hapa ndio upatikana suluhisho sahihi kwa mkulima ingawa changamoto zipo katika ubora wa dawa wingi wa madawa uwepo wa dawa feki na gharama.
Ni vema ukatumia dawa zinazotumika kuzuia magugu mara baada yakupanda kabla ya magugu kuota (somo la magugu litafuata sio mda).
Tumia PRIMAGRAM GOLD kutoka Syngenta Tanzania Ltd epuka palizi la mkono okoa mda pata faida pata mda wakupumzika na kujishughurisha na mambo mengine na uongeze kipato.
Maize aphids, African armyworms, Bollworm, Stalk borer, leaf hoppers.
Dawa nzuri kuzuai hili ni Match 050EC na Karate 5EC/Karate 5CS(Originali kutoka Syngenta epuka dawa feki ilikopiwa nembo/lebo)
Magonjwa ya ardhini (soil born disease), kutu ya majani n.k.
Magonjwa ya kuvu sio tatizo sana ktk kilimo hiki ingawa maeneo ya nyanda za juu kaskazini yameoneka.
Tumia Artea na Amistar Kutoka kampuni ya Syngenta.
Mda ambao mahindi uchukua kukaa shamban hadi kuvunwa inategemea na ukanda na pia na mbegu, mahindi ukaa wastan wa miezi mitano toka kupandwa shambani. Lakini ni tamaduni za wakulima wengi kuacha mahindi shambani kwa mda mrefu zaidi ili yakauke kwa matumizi ya biashara. Mahindi kwa ajiri ya gobo ukaa mda mfupi (sio kila mbegu ni ya gobo/mahind yakuchoma) zaidi uvunwa kabla yakukomaa.
→ utaratibu uliofuatwa wakitaalum (Agronomic practices)
→ aina ya mbegu
→mazingira (ukanda)-mvua ama umwagiliaji.
→mapambano dhidi ya wadudu magonjwa na magugu.
→ usimamizi/mbolea/rutuba ya udongo wako.
Kila mbegu hasa chotara zinakua na kiasi tajwa cha mavuno kwa ekari.
Mf. Gunia 30, 25-30, ama 40 n.k. (gunia tafsiri yake kitaalum ni 100kg.
Soko utegemea sana wastani ama ungezeko la walimaji na uzalishaji. Soko lake utegemea sana watumiaji wa ndani.
Pia utokea soko katika mkampuni kama wanunuzi wadogo wadogo, kampuni ndogondogo za usagaji mahindi, taasis mbalimbali,Mohamed enterprise, Hifadhi ya taifa ya chakula, n.k na pia soko la nje ya nchi eg Kenya Uganda Sudani Ethiopia n.k
Ni kitabu kinachotoa elimu ya Kilimo Cha Mboga. Kipo katika Mfumo wa PDF (Soft copy).
Kina kurasa 100 na utaalamu wa mazao zaidi ya 10, ambayo ni nyanya, kabichi, bamia, vitunguu maji, vitunguu twaumu, hoho, matikiti, karoti, uyoga na matango. Bila kusahau kilimo cha mboga kama chainizi na mchicha.
Pia utaweza kufahamu mbinu mbalimbali za kilimo cha mboga kama vile kuandaa shamba na kitalu, udhibiti wa wadudu na magonjwa katika mboga, kuvuna na kuhifadhi mboga, vilevile utajifunza kuhusu kilimo cha matone.
Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.
Mwanafunz alikuwa kila siku anachelewa shule, na kila siku alikuwa anachapwa, basi siku moja mwalimu akaona ngoja amuulize.
Mwalimu: Mbona unachelewa kila siku?
Mwanafunzi: Nakaa mbali mwalimu
Mwalimu: (huku ana hasira akauliza)Mbali mbinguni?
Mwanafunzi: Mbinguni kwa mbele😂😂😂😂😂
Nafsi yangu inafurahia ya kwamba
wewe ndio chaguo langu, ubavu wangu
tabasamu usoni mwangu ndio siri ya
pendo lako kwangu
MTOTO: Hivi Baba wewe umezaliwa wapi?????
BABA: Mbeya
MTOTO: Mama nae kazaliwa wapi????
BABA: Tanga
MTOTO: Mimi jee?????
BABA: Dar
MTOTO: Sasa tulikutanaje????
😂😂 hapo wee kama baba ungemjibuje mwanao😳😳😳
Ujasiriamali ni mojawapo ya nguzo muhimu zinazochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika jamii. Ni mchakato wa kuthubutu au kujaribu kufanya shughuli zozote halali, zenye lengo la kuzalisha bidhaa au kutoa huduma zinazoweza kutatua matatizo au kutosheleza mahitaji ya watu katika soko. Ujasiriamali unahusisha ubunifu na uvumbuzi, na mara nyingi unakuwa ni matokeo ya mtu binafsi au kikundi cha watu kuchukua hatua kusonga mbele na wazo au suluhisho la kipekee ambalo linaweza kutekelezwa kibiashara.
Vyema, ujasiriamali si tu juu ya ukuaji binafsi na faida; unajumuisha pia uwezo na nia ya kuchangia kijamii na kuinua maisha ya wengine. Kwa kufanya hivyo, wajasiriamali huweza kuchangia kwenye soko la ajira kwa kutoa nafasi mpya za kazi, hivyo kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira. Kupitia shughuli za kijasiriamali, mtu au watu wanaweza kujenga mustakabali mzuri zaidi si tu kwao binafsi lakini pia kwa jamii zao na uchumi wa nchi kwa ujumla.
Ni muhimu pia kutambua kwamba ujasiriamali unaweza kuwa wa aina mbalimbali, kuanzia biashara ndogo na za kati (SMEs), hadi biashara kubwa na za kimataifa. Haijalishi ukubwa, kila biashara ilianza na hatua ya ujasiriamali; kuona fursa katika soko, kutathmini na kuwa tayari kuchukua hatari ili kugeuza fursa hiyo kuwa uhalisia. Katika hili, wajasiriamali hawahitaji kuwa na raslimali nyingi awali, bali wanahitaji kuwa na mtazamo chanya, uwezo wa kufanya kazi kwa bidii, na, zaidi ya yote, subira na ujasiri wa kukabiliana na changamoto zitakazoibuka katika safari yao ya kijasiriamali.
Mjasiriamali mara nyingi huchukuliwa kama nguzo muhimu katika ukuaji wa uchumi katika jamii yoyote ile. Watu hawa, ambao wanachukua hatari na kufanya uvumbuzi, wanaweza kuleta mageuzi na kuhamasisha maendeleo katika viwango mbalimbali. Kwa mfano, mjasiriamali anaweza kuanza biashara inayojikita katika uzalishaji wa bidhaa ambazo zinakidhi mahitaji ya eneo lake, hii basi si tu inaongeza fursa za ajira bali pia inachangia kwenye uchumi kwa kuongeza uzalishaji.
Shughuli za kijasiriamali zinaweza kuwa tofauti tofauti – zingine zinaanza na mtaji mdogo na zingine zinahitaji uwekezaji mkubwa. Lakini, katika hali zote, kipengele kinachokita umuhimu ni ubunifu na uwezo wa mjasiriamali kuona fursa katika changamoto. Kwa kujitosa katika biashara ya uzalishaji mali au bidhaa, mjasiriamali anaweza kujenga thamani sio tu kwa wateja bali pia kwa jamii yake.
Ni muhimu kutambua kwamba ujasiriamali sio tu kuhusu kuanzisha biashara; ni mtazamo, ni uwezo wa kuchukua hatari kinagaubaga na kujituma kutafuta na kutumia fursa zilizopo au hata kutengeneza fursa mpya. Mjasiriamali mwenye mafanikio huwa na uwezo wa kubadilika, kujifunza kutokana na makosa na kujikita katika maono yake hata wakati wa changamoto.
Mwishowe, ujasiriamali unaweza kuchukua sura nyingi – kuwa mwanzilishi wa teknolojia mpya, mmiliki wa duka la rejareja, au mkulima anayetumia njia za kisasa. Kila mmoja kwa nafasi yake, anaweza kutoa mchango katika kujenga jamii inayojitegemea na yenye uchumi imara.
1»Kujenga mtazamo wa kijiasiriamali
pamoja na kuona na kutumia fursa
mbalimbali za kibiashara zilizopo
.Mjasiriamali lazima ajenge uwezo wa
kutumia nyenzo mbalimbali zilizopo katika
kutekeleza majukumu yake kwa kutumia
fursa mbalimbali za kibiashara.
2»>Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa
mipango na mikakati ya kibiashara.
Mjasiriamali anahitaji kuwa mbunifu,kuweka
mipango na mikakati ya biashara zake
3»>Kuweka kumbukumbu muhimu na
kuandaa mahesabu ya biashara
4»>Kutumia mbinu rahisi kupata wateja wa
bidhaa au biashara inayofanywa.
5»>Kupata mitaji na kutumia vizuri fedha
na bidhaa za biashara.kuwajengea uwezo wa
nidhamu ya matumizi ya mapato hasa fedha
au bidhaa za biashara
6»>Kutafuta ,kuongoza na kusimamia
wafanyakazi.kuimarisha muundo wa uongozi
katika biashara na usimamizi bora wa
shughuli yenyewe
7»>kutumia wataalamu na washauri kwa
manufaa ya biashara
1-Mradi wako utapunguza gharama za
maisha
2-Mradi wako utakufanya uwe kiongozi
[watu watakuiga na kufanikiwa].
3-Mradi wako utakufanya upate heshima
katika jamii.Mfano utaweza kujitosheleza
katika mahitaji yako yote -nyumba yako
,usafiri,n.k.
4-Mradi wako utakuletea afya na uhakika
wa maisha .Mfano:ukipatwa na tatizo
utaweza kujitegemeya kwa sehemu kubwa
badala ya kuitegemea jamii.
5—-Mradi wako utaimarisha upendo kati
yako na wazazi wako kwani hutakuwa
tegemezi na pia utakuwezesha kuwasaidia.
NAMNA AU JINSI YA KUPATA MTAJI
i»Kujiwekea akiba wewe mwenyewe kwa
kujinyima,kula kuvaa na kutoa michango kwa
kujionyesha.
ii»Kucheza mchezo wa kukopeshana na
ndugu?rafiki hasa wale mnaoaminiana
(waaminifu).
iii»Kuomba mkopo kwa ndugu/rafiki
iv»Kuomba mkopo Benki-Unapokopa benki
uwe makini na mradi wako kwani ukishindwa
kurudisha utafilisiwa mali zako.
AINA ZA MIRADI
a»>KILIMO
Kinaweza kuwa kilimo cha Masika
kwa kulima mazao kama
vile:Maharage,Alizeti,Ufuta,Mahindi,Mbaazi
n.k
unashauriwa kulima mazao kama
vile:Uyoga,matunda,Mboga(kabichi,pilipili
hoho,Bilinganya,bamia na Nyanya n.k
b»>UFUGAJI
asili,Nguruwe,Bata mzinga,kuku wa kisasa
(mayai na nyama),Samaki,nyuki n.k
c»>BIASHARA
zinazoweza kufanywa mafano;Kununua
mazao wakati wa mavuno na kuuza
yanapopanda bei,Biashara ya kitaalam
mfano Kliniki,Shule,Biashara ya kuagiza na
kupeleka bidhaa nje.
i»Ukishapata mtaji tulia na omba ushauri
kwa wazoefu juu ya mradi wako-uwe makini
na watu utakaowaomba ushauri.
ii»Fanya utafiti wa kutosha kuhusu mradi
wako,mfano utafiti wa masoko,usifanye
mradi kwa kuiga (kufuata mkumbo)
iii»Fanya mradi ambao unaupenda
iv»Fanya mradi ambao una ujuzi nao kama
hauna ujuzi nao unaweza kuanza kwa kiasi
kidogo
v»Hudhuria semina za kimaendeleo au
soma vitabu vya kukufanya uelewe namna ya
kuendeleza mradi huo.
vi»Fanya biashara halali na kama kubwa
kidogo inahitaji leseni basi itafute leseni
husika.
1»Tafuta ushauri wa kitaalamu kabla ya
kuanza mradi wako
2»Usikate tamaa kwa changamoto/
misukosuko unayoweza kukutana nayo
njiani.
3»Ufanye mradi wako na mambo yote kwa
bidii kubwa
4»Jiwekee malengo ya wiki,mwezi na
mwaka
5»Uwe mbunifu na unayekubali kujifunza
mambo mapya na kukubali kubadilika
KUMBUKA-Soko ni kitu cha muhimu katika
mradi wako kwa sababu mwishoni
ukishapata mavuno yako kwa shughuli za
itahitaji uziuze hivyo kuwa makini na mradi
unaochagua kwa sasa miradi ambayo soko
lake ni rahisi kulipata ni Kuku wa kienyeji,
kuku wa mayai/nyama
matunda,mbaazi,ufuta n,k
Jamaa alimfumania mtu anazini na mkewe,
Akamtoza Faini ya sh 5000 tu,yule mtu akatoa 10000.
Jamaa akasema lala nae tena sina chenji!😀😀😀😀😀😀😀
Asilimia kubwa tunapenda kutumia karoti katika kuunga katika mboga ya nyama na si kuila karoti kama karoti. wataalamu wanashauri ili uwe na afya bora unatakiwa ule karoti sita kwa wiki au moja kwa siku. Unaweza kula karoti ya kuchemshaa,juisi au mbichi.
1. Karoti husaidia kuimarisha macho kuona vizuri, mfano tatizo la kutoona vizuri usiku, pia inasaidia kuondoa matatizo ya allergy kwenye macho mfano macho kuwasha sababu ya vumbi.
Karoti inarutubisha cells mwilini na kuzifanya zisizeeke haraka. Hii inatokana na uwepo wa Vitamin A ambayo ni muhimu katika kuimarisha uwezo wa macho kuona.
2. Huifanya ngozi iwe nzui na yenye afya, kama utatumia kurutubisha ngozi yako, ikwangue kwa kutumia grater kiasi unachotaka tia asali mbichi kijiko 1 kikubwa (cha kulia chakula) mafuta ya nzai au olive kijiko kimoja kikubwa na limao kijiko 1 kikubwa changanya vizuri, kisha itumie kusugua mwilini sehemu yoyote unayotaka, ukimaliza acha kama dakika 15 na zaidi kisha oga, itasaidia kuondoa taka katika vinyweleo, kuifanya ngozi iwe laini na kuondoa mikunjo katika ngozi, Kumbuka inatakiwa asali mbichi na siyo asali yoyote.
Karoti husaidia kuondoa sumu na taka mwilini, inaondoa mafuta yasiyotakiwa katika ini (cholesterol) na kuliwezesha lifanye kazi vizui, Kusafisha njia ya haja kubwa na kusaidia kupata choo vizuri (kuzuia constipation).
3. Karoti zinasaidia kufanya fizi na meno kuwa imara na kuchochea uzalishwaji wa mate.
Pia inasaidia kuzuia stroke (kiharusi, baadhi ya watafiti kutoka vyuo vikuu duniani wanasema ulaji wa karoti sita kwa wiki husaidia kutopata stroke.
Pia wamegundua kaoti zinatibu tatizo la kupoteza kumbukumbu kwa wazee.
4. Karoti hupunguza hatari ya kupata Shinikizo la Damu (blood pressure) kwani ulaji wa karoti husaidia mwili kupata madini muhimu ya Potassium ambayo husaidia kutanua mirija ya damu (bllod vessels na kufanya damu kufika katika maeneo husika ya mwili (organs).
5. Karoti pia husasidia kuzuia magonjwa mengine kama vile kisukari (Diabetes), Kiharusi (Stroke), Kansa pamoja na magonjwa ya moyo.
6. Karoti husaidia kuongeza kinga mwilini (immune booster). Kwasababu tabaia asilia ya karoti kuwa na antibacteia pamoja na antiseptic ambazo husaidia kuzuia kinga za mwili. Pia Karoti ina Vitamin C muhimu kwa kusisimua seli nyeupe za damu (white blood cells) ambazo ni sehemu muhimu katika kinga ya mwili.
Unapotokwa na damu puani fanya yafuatayo;
1. Simama wima na inamisha kichwa kwa mbele, kusimama itakusaidi kupunguza kasi na presha katika mishipa ya damu puani wakati unapoinamisha kichwa kwa mbele huzuia kumeza damu ambayo italeta shida tumboni.
2. Weka pamba au kitambaa chenye uwezo wa kufyonza damu nje ya pua na bana pua kwa muda wa dakika 15 huku ukitumia mdomo kupumua, kubana pua hurudisha damu katika mishipa ya pua na kuzuia kuvuja.
3. Kuzuia damu isitoke tena usichokonoe pua wala kuinamisha kichwa mbele kwa nguvu na kwa muda mrefu.
4. Kama damu inaendelea kutoka bana pua kwa kutumia kitambaa chenye ubaridi au barafu itasaidia kusinyaa kwa mishipa ya damu na kuzuia damu.
5. Nenda hosipitali kama damu puani inatoka na kuumia kichwani, haijakata kwa muda wa dakika 20 na kama pua imeumia au kuvunjika
KUMBUKA: Kutokwa na damu puani ni jambo la kawaida sana kwa kila mtu na mara nyingi huwa sio hatari sana isipokuwa kama linaambatana na dalili nyingine hatari. Tatizo ili huweza kusababishwa na kuumia ndani au nje ya pua, kuchokonoa pua mara kwa mara, shinikizo la damu, matumizi dawa za aspirini, ukosefu wa vitamini K, pombe kupita kiasi, na mabadiliko ya hormoni kwa wajawazito
Recent Comments