SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

UKWELI KUHUSU MSHAHARA

1. Epuka kugeuza mshahara wako kuwa mali ya ukoo. Kamwe mshahara wako siyo mali ya ukoo. Siku utakapoacha kuufanya mshahara wako mali ya ukoo ndipo siku mshahara huo utakuwa mkubwa! Hapo ndipo mshahara utatosha.

2. Siku utakapokuwa na vyanzo vya mapato zaidi ya mshahara wako ndipo mshahara wako utakapotosha mahitaji yako ya kila mwezi.

3. Usiombe mwajiri wako akulipe overtime allowance, mwombe akupe muda wa kufanya kazi zako za ziada(perform your own overtime duties)

4. Epuka kuwasambazia pesa za mshahara wako watu wa ukoo wako ili uwaokoe na hali ngumu ya ukosefu wa fedha waliyonayo. Badala yake Wasaidie kuona fursa za kuwapatia Pesa!

5. Usiombe mwajiri wako akuongezee mshahara bali omba Mungu akuwezeshe Kupata kipato endelevu nje ya mshahara wako.

6. Mtu anayeishi kwa kutegemea mshahara wake tu ni sawa na mtu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga na mafuriko yalipokuja anguko la nyumba hiyo lilikuwa na mshindo mkubwa sana.

7. Mto Kagera au Maragalasi haijawahi kukauka maji yake. Kwa nini? Ni kwa sababu inapokea maji yake kutoka kwenye vyanzo vingi vya maji au vijito vingi! Mtu mwenye vyanzo vingi vya mapato zaidi ya mshahara atafanishwa na mto Kagera au Maragalasi isiyokauka maji yake.

8. Usisubiri kustaafu kazi ndipo ulipwe mamilioni ya pesa za kiinua mgongo bali tafuta kumiliki vyanzo sahihi vya pesa, na ndipo malipo ya kiinua mgongo utalipwa kila wiki mamilioni ya pesa.

9. Watu wenye busara hutafuta vyanzo vya pesa vinavyoweza kuwalipa mshahara au pensheni ya Tshs 150 milioni kwa mwezi badala ya kusubiri kulipwa kiinua mgongo cha Shs 150milioni baada ya kufanya kazi kwa miaka 30 au zaidi.

10. Waajiriwa wenye hekima na busara hutumia mishahara yao kutengeneza au kutandaza mabomba ya fedha au mtandao wa fedha endelevu ili hata kama hawatakuwepo tena duniani watoto wao na watoto wa watoto wao waendelee kupata mshahara kila mwezi!

Faida za kiafya za Kula Matunda

Matunda yote yana faida mwilini kiafya lakini matunda yanatofautiana kifaida. Zifuatazo ni faida za kula matunda ya aina Mbalimbali;

FAIDA ZA TANGO

1. Kuzuia kisukari, kuboresha mfumo wa damu na kuondoa kolesteroli mwilini.
2. Chanzo kikubwa cha Vitamin B.
3. Kusaidia kutunza ngozi.
4. Kuongeza maji mwilini.
5. Kukata hangover.
6. Kuimarisha mmeng’enyo wa chakula mwilini.
7. Kuzuia saratani mwilini.
8. Kusaidia kupungua uzito.
9. Kuondoa maumivu na kuboresha viungo vya mwili.
10. Kuondoa harufu mbaya ya kinywa.

FAIDA ZA PAPAI

1. Kuua na kuondoa mazalia ya minyoo mwilini.
2. Kusaidia kutibu vidonda vya tumbo.
3. Kuboresha mmeng’enyo wa chakula.
4. Majani yake huleta ahueni kwa wagonjwa wa saratani.
5. Kupunguza uvimbe (anti-inflammatory).
6. Kuboresha misuli na neva mwilini.
7. Kusaidia kumeng’enya protini.
8. Kuboresha kinga ya mwili.
9. Kuboresha macho.
10. Kuboresha mfumo wa hewa

FAIDA ZA UBUYU

1. Kuzuia uhalibifu na mikunjo ya ngozi.
2. Kusaidia katika kupunguza uzito wa mwili.
3. Kuimarisha moyo.
4. Kusafisha ini na kuondoa sumu.
5. Kiwango kikubwa cha vitamin C.
6. Chanzo cha madini ya Calcium.
7. Kuimarisha kinga ya mwili.
8. Kuimarisha figo.
9. Kuimarisha mifupa na meno.
10. Kuimarisha mfumo wa fahamu

FAIDA ZA EMBE

1. Kupunguza kiwango cha asidi mwilini.
2. Kuboresha mmeng’enyo wa chakula.
3. Kurekebisha kiwango cha insulin.
4. Kuboresha macho.
5. Kusafisha damu.
6. Kuboresha ngozi.
7. Kuzuia saratani.
8. Kuimarisha kinga mwilini.
9. Kutibu joto kiharusi (heat stroke).
10. Kupunguza kiwango cha kolesteroli.

FAIDA ZA NANASI

1. Chanzo kikubwa cha vitamin A.
2. Kusaidia kumeng’enya chakula.
3. Inarekebisha mapigo ya moyo.
4. Kuimarisha mifupa ya mwili.
5. Ina kiwango kidogo cha kalori.
6. Inasaidia kuzuia mafua na homa.
7. Kuimarisha mfumo wa kinga.
8. Chanzo cha vitamin C.
9. Inapunguza uvimbe.
10. Kupunguza spidi ya kuzeeka kwa seli mwilini

FAIDA ZA NJEGERE

1. Kuzuia saratani ya tumbo.
2. Kurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu.
3. Chanzo kizuri cha protini.
4. Kuboresha ufanyaji kazi wa ini.
5. Ina kiwango kidogo cha kalori.
6. Kuboresha kinga ya mwili.
7. Inaleta nguvu mwilini.
8. Ina virutubisho vya nyuzi nyuzi.
9. Inazuia kuzeeka haraka.
10. Imejaa virutubishi vingi muhimu mwilini.

FAIDA ZA PILIPILI HOHO

1. Husaidia kupunguza uzito.
2. Kuboresha mzunguko wa damu.
3. Inapunguza kolesteroli mwilini
4. Kuzuia shinikizo la damu.
5. Ina kiwango kidogo cha kalori.
6. Nzuri kwa kuboresha macho.
7. Kuimarisha mfumo wa kinga.
8. Inatibu anemia.
9. Inazua saratani.
10. Kuboresha moyo.

Jinsi ya kujua kama mwanamke anakupenda kweli kwa dhati

Yafuatayo ni maswali ya kujiuliza ili kujua kama mwanamke anakupenda kweli.

Anajitoa kwa ajili yako?

Mwanamke anayekupenda atakuwa tayari kujitoa muhanga kwa ajili yako. Mwanamke anayekupenda atakua tayari kufanya chochote kile kwa ajili yako kitu ambacho hawezi kufanya kwa ajili ya mtu mwingine yoyote.

 

Atakupa kipaumbele?

Mwanamke anayekupenda atakupa kipaumbele katika vitu na mambo yake yote. Mbele ya Marafiki zake wewe utakuwa ni bora zaidi.

Anakuchukulia tofauti na wanaume wengine?

Mwanamke anayekupenda atakufanyia mambo ambayo hawezi kuwafanyia wanaume wengine.

Anakupa nafasi na muda wake?

Mwanamke anayekupenda anakupa nafasi na muda wake. Anauwezo wa kuacha mabo mengine ili aweze kuwa na wewe.

 

Anakuhangaikia?

Mwanamke anayekupenda atahangaika juu yako, Kawaida mwanamke anayekupenda atahangaika juu ya usalama wako, raha yako, heshima yako na maendeleo yako. Hii ni moja kati ya ishara kubwa kuwa mwanamke uliyemlenga anakupenda kweli.

Ana wivu juu yako?

Mwanamke anayekupenda atakuonea wivu mara kadhaa. Anaogopa usije ukamtoa moyoni mwako na nafasi yake ikachukuliwa. Wivu ni ishara kuwa anakupenda wewe na anataka akulinde usiibiwe au asije akakupoteza, anaogopa usije ukatoka katika maisha yake.

 

Anakushirikisha furaha yake?

Mwanamke anayekupenda atakapokuwa mbele ya marafiki zake au watu wengine atacheka nao lakini atakugeuzia wewe macho namaanisha uso wake haraka sana. Kufanya hivi ni kuonyesha kuwa anakuhesabia wewe kuwa utaweza kumletea furaha katika maisha yake, zaidi ya hilo ni kwamba anatumaini kuwa utamuona kuwa yeye ni mtu aliye rahisi kufurahishwa kwa kuwa yeye ni mtu wa furaha.

Anakuangalia sana?

Mwanamke anayekupenda ataendelea kukuangalia usoni kwa muda mrefu kuliko ilivyo kawaida ya wanawake wengine, atakuangalia na kutabasamu vizuri. Hii ni ishara moja muhimu sana ya kukuambia kuwa anakuhitaji katika maisha yake.

 

Anavaa vizuri mkutanapo?

Mwanamke anayekupenda atajitahidi apendekeze kwa kuvaa vizuri pale anapojua kuwa atakutana na wewe, atajali sana juu ya nywele zake, nguo zake na hata anavyonukia. Hii ni ili kukuvutia wewe na kuonyesha uwepo wake kwako.

Anapenda kuwa karibu na wewe?

Mwanamke anayekupenda ataonyesha dalili za kupenda kuwa karibu yako katika mazungumzo au maeneo mengine, atapenda mara nyingi kuwepo katika maeneo unayopendelea na pia sauti yake itabadilika kuashiria hali ya kukupenda na kutaka kukuvuta kwa sauti yake.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Mlevi kazua tafrani, angalia alichokifanya hapa

MLEVI mmoja aliingia baa akavuta kiti na kukaa mhudumu akatokea kumsikiliza.
MHUDUMU: Nikusaidie nini?
MLEVI: Eeh! nipe bia ya baridi kisaha wasikilize wote waliokaa hapa, wape bia na wao maana sipendi kunywa pombe wengine wananiangalia
Akaja mhudumu wa jikoni “nikusaidie nini?”

MLEVI: Niletee supu kisha wasikilize wote waliokaa hapa na wao wape supu sipendi kunywa supu watu wananiangalia
Safari hii watu wakapiga makofi
Baadae akamuita mhudumu
MLEVI: Niandikie bili zangu kisha waandikie wote bili zao sipendi kulipa huku watu wananiangalia

Wale wateja wakamvaa na kumshushia kichapo… teh teh teh teh teh hii kali hakuna cha bure mjini hahahaha na jasho la mtu haliliwi wandugu

Huyu bibi kweli kiboko, cheki alichofanya akiwa na babu

Bibi na Babu walisafiri wakielekea kwa mtoto wao ambae hawajamuona zamani.

Walipofika njiani wakawa wamechoka Sanaa. Wakaamua kutafuta hotel ili walale.

Wakakubaliana walale kwa masaa 4. Wakalala, Walipoamka, mfanyakazi wa Hotel akawatoza Tsh. 500,000/=

Wale wazee wakashangaa hata kama ni hotel ya kisasa lakini sio laki tano kwa masaa 4.

Babu akagoma kulipa akasema aitiwe meneja.

Meneja akaja kuwasikiliza

Babu: ” Kwanini bili ni kubwa hata kama ni hotel ya kisasa?”

Manager;“kuna maswiming puli, ya kisasa “

Babu; “Lakini hatukuyatumia”

Manager; “Ah ah ah. Lakini mungeweza kama mngetaka”

Babu: “Hata hivo bado haithamini kuwa laki 5”

meneja: “Pia Kuna waimbaji kutoka sauzi, Uganda , Congo”

Babu: “Lakini sisi hatukuwasikiliza”

Meneja: “Ndiooo. Lakini mngeweza kama mngetaka”

Babu; aka give up na kumwambia mkewe andika cheki uwape,,

Bibi akaandika akampa meneja.

Meneja anaangalia anaona sh. 50,000

Akashangaa na kusema. “VP mbona hamsini'”

Bibi akajibu “450,000 ya kulala na mimi”

Meneja akajibu; “Lakini sijalala”

Bibi :“ungeweza kama ungetaka”

Kukataliwa ni mtaji

Hakuna mtu duniani ambaye hajawahi kukutana na hali ya kukataliwa. Yaani kukataliwa katika hali yoyote ile. Waweza kuwa umekataliwa katika kupata ajira, umekataliwa katika mahusiano, umekataliwa kupata nafasi ya kusoma, umekataliwa kupata mtaji wa biashara, umekataliwa tuu..umekataliwa.

—-= Unaweza kuwa umekataliwa katika ajira moja kumbe kuna ajira nyingine tena yenye maslahi zaidi inakusubiri.

—-= Umekataliwa na mteja mmoja na kumbe kuna wateja wengi wanakusubiri.

—-= Umekataliwa katika chuo kimoja mwaka huu kumbe mwakani kuna nafasi yako inakusubiri.

——= Umekataliwa na mpenzi ulioamini kabisa atakua wako wa maisha kumbe aliye wako haswaa anakusubiri ufike.

Watu wengi kinachowarudisha nyuma, “ni kuacha kuboresha fikra zao ili kuwa watatuzi wa matatizo_(problem solvers)_ ila wameamua kuwa walalamikaji tu kila siku, ili tuendelee ni lazima tujikite katika kutafuta majibu ya matatizo yanayotuzunguka.” Yaani, mara zote jiulize ” *sasa nifanye nini? Na sio kwa nini mimi?”*

Mtaalamu mmoja aliwahi kusema ” _Life is 10% of what happens to you and 90% of how you respond to it_”. Yaani _yale yanayokutokea maishani yanachangia asilimia kumi tu kuboresha au kuharibu maisha yako na asilimia 90 ya maisha yako ni jinsi wewe unavyoyachukulia maisha hayo_. Kwa nini ukate tamaa baada ya kukataliwa. Yape maisha yako maana sana thamani ya juu kabisa ili kukataliwa kwako iwe ni kukupa nguvu ya kufanya vizuri zaidi. Tambua utakacho na unachoweza kukifanya. Jifunze vizuri na ubobee ili kuuhakikishia ulimwengu kwamba wewe sio mzigo ila ni sehemu ya wenye majibu ya matatizo yanayotuzunguka.

Kukataliwa, ni mtaji. Kila jambo lina wakati wake.

Mambo 6 ambayo ni siri ya mwanamke na sio rahisi kukwambia

1. Idadi ya wapenzi wake wa zamani

Wanaume wengi hupenda kujua wao ni wangapi kuwa na mwanamke Fulani. Lakini mwanamke kamwe hawezi akakwambia wewe ni wa ngapi. Kumuuliza jambo hili kunamkera sana mwanamke na ndio maana mara nyingi hawezi akakwambia ukweli.

2. Anakulinganisha na mpenzi wa zamani

Mwanamke mara nyingi anakulinganisha na mpenzi wake wa zamani japokuwa hawezi kukwambia waziwazi. Wakati mwingine tabia hii huwafanya wanawake kuwatamani wapenzi wa zamani na hata kurudiana nao endapo watakosa mtu aliye bora kuliko mpenzi wake wa zamani.

 

3. Kasoro zako

Mwanamke kamwe hawezi kukwambia kasoro zako. Wanawake wanajua kumfichiaa mpenzi wao mambo wasiyotaka yajulikane kwa wengine na kwa mpenzi wake. Wanajua njia za kiujanja za kutumia ili kufichua siri zako zote. Mwanamke hawezi kukwambia kasoro zako kwa kuogopa kukuumiza.

4. Mapungufu yake

Mwanamke hawezi kukwambia mapungufu yake labda kwa kuhofia kusheshwa thamani. Wanawake ni wasiri sana kwa mapungufu yao. Wanajua vyema hofu zinazomuandamana, vitu vinavyowakosesha usingizi na mambo yanayowalemea maishani japo sio rahisi kuonyesha. Kwa nje anaweza akaonekana yuko vizuri na hana tatizo kumbe ndani ana matatizo au mapungufu. Anaweza kufanya yote kufunika upungufu wake!

 

5. Huwa unampagawisha mpaka anakosa la kusema

Hili halisemi kabisa mwanawake kwa sababu anaona haya kutumia maneno ya wazi kueleza raha unayompa. Maneno ya kuzuzua ni himaya ya wanaume, lakini wakati mwingine wapo wasioweza kuficha.

6. Haumridhishi katika tendo la ndoa

Wanawake wengi hawapendi kusema kama hawaridhiki Kwenye tendo la ndoa. Wanawake wanahitaji kuandaliwa vilivyo kwa dakika 10, 20 ama nusu saa. Mara nyingine wanaume huwahi kabla mwanamke hajawa tayari na hivyo kushindwa kuridhika lakini hawezi kusema.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Huyu mchungaji ni noma, cheki alichomwambia pedeshe

Mchungaji kamfuata pedeshe moja maarufu kwa
kumwaga pesa kwenye kumbi za muziki;
MCHUNGAJI: Kijana, tuko katika harakati za
kujenga kanisa, jitafutie nafasi katika ufalme wa
mbingu kwa kuchangia ujenzi huu. Na Mungu
atakubariki zaidi

PEDESHE: Samahani Mchungaji haitakuwa vizuri
mimi kuchangia kanisa, fedha zangu ni haramu,
huwa nazipata kwa utapeli na kuuza madawa ya
kulevya.
MCHUNGAJI: Yote ni heri, pesa yako tutatumia
kwa kujenga eneo la choo we toa tu!!!

Kuwa na mahusiano na msichana kama huyu ni changamoto, Mabinti bwana!

Binti: Hallow mpenzi, Mambo

Jamaa: Poa baby

Binti:Uko wapi?

Jamaa: Niko town napata lunch

Binti: Wow unarudi saa ngap? Nina njaa dear naomba uniletee msosi

Jamaa: Narudi baada ya nusu saa nikuletee nini?

Binti: Niletee chipsi kuku, soseji, mayai manne ya kukaangwa pembeni, baga, piza, coke take away baridi, mkate wa moto kwenye ile bekari ya wapemba na maji ya kunywa ya kiimanjaro.

Jamaa:Umesahau viti, meza, masufuria, sahani na beseni na vijiko.

Binti: Kwanini dear?

Jamaa: Naona hutaki kula unataka kufungua hoteli!

Dalili za mahusiano feki, mahusiano ya kichina

Ukitaka kujua Simu ya Kichina utajua tu jinsi ilivyo na makelele mengiiiii sana wakati wa kuita….

Sasa ukitaka kujua relationship feki ya kichina utaona tu makelele yalivyo mengi kama ile simu…

Watu hawatulii kwenye wall,mara I miss my baby,mara baby come back,mara baby this,ooh my man/Girl is special,mara picha…

Mi and my baby,full kujishaua..ukiona wall zenye hayo makelele asilimia 90 ni penzi la kichina na lazima lina double line.

Relationship serious na Original hazina makeke wala mikelele mingi kama hiyo yako na milio mikubwa ya ajabu na vibration ambazo zinaweza kufyeka hata majani.

TULIA, hatuhitaji kujua who is ur baby au umemmiss, ukimmiss mpigie simu hukooo! Ebooo!!!

Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kauli 10 mbaya za walimu darasani, unakumbuka ipi hapa?

1:Mkimaliza kuongea niambieni niendelee kufundisha

2:Baba yako kauza ng’ombe ili alete ng’ombe mwingine shule

3:Kama unajua kuliko mimi njoo ufundishe wewe

4:Ulikuja peke yako na utaondoka peke yako

5:Hata msiponisikiliza mshahara wangu uko pale pale

6:Baba yako anahangaika kulipa ada wewe unafanya utumbo tu

7:Hata nikeshe nafundisha wengine ni mizigo hawatoki na lolote

8:Tunavisaidia tu kwan vikifanikiwa mbelen hata salam vinatoa?

9:Bichwa kubwa ubongo nukta

10:Wengine hapa wamekuja kukua tu

SHARE NA MARAFIKI ZAKO WAKUMBUKE ENZI ZA SHULE KIDOGO

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About