Karibu AckySHINE

Karibu AckySHINE

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

UJASIRIAMALI NA CHANZO CHA MTAJI

UJASIRIAMALI

Ujasiriamali ni mojawapo ya nguzo muhimu zinazochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika jamii. Ni mchakato wa kuthubutu au kujaribu kufanya shughuli zozote halali, zenye lengo la kuzalisha bidhaa au kutoa huduma zinazoweza kutatua matatizo au kutosheleza mahitaji ya watu katika soko. Ujasiriamali unahusisha ubunifu na uvumbuzi, na mara nyingi unakuwa ni matokeo ya mtu binafsi au kikundi cha watu kuchukua hatua kusonga mbele na wazo au suluhisho la kipekee ambalo linaweza kutekelezwa kibiashara.

Vyema, ujasiriamali si tu juu ya ukuaji binafsi na faida; unajumuisha pia uwezo na nia ya kuchangia kijamii na kuinua maisha ya wengine. Kwa kufanya hivyo, wajasiriamali huweza kuchangia kwenye soko la ajira kwa kutoa nafasi mpya za kazi, hivyo kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira. Kupitia shughuli za kijasiriamali, mtu au watu wanaweza kujenga mustakabali mzuri zaidi si tu kwao binafsi lakini pia kwa jamii zao na uchumi wa nchi kwa ujumla.

Ni muhimu pia kutambua kwamba ujasiriamali unaweza kuwa wa aina mbalimbali, kuanzia biashara ndogo na za kati (SMEs), hadi biashara kubwa na za kimataifa. Haijalishi ukubwa, kila biashara ilianza na hatua ya ujasiriamali; kuona fursa katika soko, kutathmini na kuwa tayari kuchukua hatari ili kugeuza fursa hiyo kuwa uhalisia. Katika hili, wajasiriamali hawahitaji kuwa na raslimali nyingi awali, bali wanahitaji kuwa na mtazamo chanya, uwezo wa kufanya kazi kwa bidii, na, zaidi ya yote, subira na ujasiri wa kukabiliana na changamoto zitakazoibuka katika safari yao ya kijasiriamali.

MJASIRIAMALI

Mjasiriamali mara nyingi huchukuliwa kama nguzo muhimu katika ukuaji wa uchumi katika jamii yoyote ile. Watu hawa, ambao wanachukua hatari na kufanya uvumbuzi, wanaweza kuleta mageuzi na kuhamasisha maendeleo katika viwango mbalimbali. Kwa mfano, mjasiriamali anaweza kuanza biashara inayojikita katika uzalishaji wa bidhaa ambazo zinakidhi mahitaji ya eneo lake, hii basi si tu inaongeza fursa za ajira bali pia inachangia kwenye uchumi kwa kuongeza uzalishaji.

Shughuli za kijasiriamali zinaweza kuwa tofauti tofauti – zingine zinaanza na mtaji mdogo na zingine zinahitaji uwekezaji mkubwa. Lakini, katika hali zote, kipengele kinachokita umuhimu ni ubunifu na uwezo wa mjasiriamali kuona fursa katika changamoto. Kwa kujitosa katika biashara ya uzalishaji mali au bidhaa, mjasiriamali anaweza kujenga thamani sio tu kwa wateja bali pia kwa jamii yake.

Ni muhimu kutambua kwamba ujasiriamali sio tu kuhusu kuanzisha biashara; ni mtazamo, ni uwezo wa kuchukua hatari kinagaubaga na kujituma kutafuta na kutumia fursa zilizopo au hata kutengeneza fursa mpya. Mjasiriamali mwenye mafanikio huwa na uwezo wa kubadilika, kujifunza kutokana na makosa na kujikita katika maono yake hata wakati wa changamoto.

Mwishowe, ujasiriamali unaweza kuchukua sura nyingi โ€“ kuwa mwanzilishi wa teknolojia mpya, mmiliki wa duka la rejareja, au mkulima anayetumia njia za kisasa. Kila mmoja kwa nafasi yake, anaweza kutoa mchango katika kujenga jamii inayojitegemea na yenye uchumi imara.

UMUHIMU WA KUJIFUNZA UJASIRIAMALI

1ยปKujenga mtazamo wa kijiasiriamali
pamoja na kuona na kutumia fursa
mbalimbali za kibiashara zilizopo
.Mjasiriamali lazima ajenge uwezo wa
kutumia nyenzo mbalimbali zilizopo katika
kutekeleza majukumu yake kwa kutumia
fursa mbalimbali za kibiashara.
2ยป>Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa
mipango na mikakati ya kibiashara.
Mjasiriamali anahitaji kuwa mbunifu,kuweka
mipango na mikakati ya biashara zake
3ยป>Kuweka kumbukumbu muhimu na
kuandaa mahesabu ya biashara
4ยป>Kutumia mbinu rahisi kupata wateja wa
bidhaa au biashara inayofanywa.
5ยป>Kupata mitaji na kutumia vizuri fedha
na bidhaa za biashara.kuwajengea uwezo wa
nidhamu ya matumizi ya mapato hasa fedha
au bidhaa za biashara
6ยป>Kutafuta ,kuongoza na kusimamia
wafanyakazi.kuimarisha muundo wa uongozi
katika biashara na usimamizi bora wa
shughuli yenyewe
7ยป>kutumia wataalamu na washauri kwa
manufaa ya biashara

SABABU ZA KUWA MJASIRIAMALI NA KUANZISHA MRADI/MIRADI

1-Mradi wako utapunguza gharama za
maisha
2-Mradi wako utakufanya uwe kiongozi
[watu watakuiga na kufanikiwa].
3-Mradi wako utakufanya upate heshima
katika jamii.Mfano utaweza kujitosheleza
katika mahitaji yako yote -nyumba yako
,usafiri,n.k.
4-Mradi wako utakuletea afya na uhakika
wa maisha .Mfano:ukipatwa na tatizo
utaweza kujitegemeya kwa sehemu kubwa
badala ya kuitegemea jamii.
5โ€”-Mradi wako utaimarisha upendo kati
yako na wazazi wako kwani hutakuwa
tegemezi na pia utakuwezesha kuwasaidia.
NAMNA AU JINSI YA KUPATA MTAJI
iยปKujiwekea akiba wewe mwenyewe kwa
kujinyima,kula kuvaa na kutoa michango kwa
kujionyesha.
iiยปKucheza mchezo wa kukopeshana na
ndugu?rafiki hasa wale mnaoaminiana
(waaminifu).
iiiยปKuomba mkopo kwa ndugu/rafiki
ivยปKuomba mkopo Benki-Unapokopa benki
uwe makini na mradi wako kwani ukishindwa
kurudisha utafilisiwa mali zako.
AINA ZA MIRADI
aยป>KILIMO

Kinaweza kuwa kilimo cha Masika

kwa kulima mazao kama
vile:Maharage,Alizeti,Ufuta,Mahindi,Mbaazi
n.k

unashauriwa kulima mazao kama
vile:Uyoga,matunda,Mboga(kabichi,pilipili
hoho,Bilinganya,bamia na Nyanya n.k
bยป>UFUGAJI

asili,Nguruwe,Bata mzinga,kuku wa kisasa
(mayai na nyama),Samaki,nyuki n.k
cยป>BIASHARA

zinazoweza kufanywa mafano;Kununua
mazao wakati wa mavuno na kuuza
yanapopanda bei,Biashara ya kitaalam
mfano Kliniki,Shule,Biashara ya kuagiza na
kupeleka bidhaa nje.

NAMNA YA KUANZISHA MRADI

iยปUkishapata mtaji tulia na omba ushauri
kwa wazoefu juu ya mradi wako-uwe makini
na watu utakaowaomba ushauri.
iiยปFanya utafiti wa kutosha kuhusu mradi
wako,mfano utafiti wa masoko,usifanye
mradi kwa kuiga (kufuata mkumbo)
iiiยปFanya mradi ambao unaupenda
ivยปFanya mradi ambao una ujuzi nao kama
hauna ujuzi nao unaweza kuanza kwa kiasi
kidogo
vยปHudhuria semina za kimaendeleo au
soma vitabu vya kukufanya uelewe namna ya
kuendeleza mradi huo.
viยปFanya biashara halali na kama kubwa
kidogo inahitaji leseni basi itafute leseni
husika.

MAMBO YA KUZINGATIA ILI KUBORESHA MRADI WAKO

1ยปTafuta ushauri wa kitaalamu kabla ya
kuanza mradi wako
2ยปUsikate tamaa kwa changamoto/
misukosuko unayoweza kukutana nayo
njiani.
3ยปUfanye mradi wako na mambo yote kwa
bidii kubwa
4ยปJiwekee malengo ya wiki,mwezi na
mwaka
5ยปUwe mbunifu na unayekubali kujifunza
mambo mapya na kukubali kubadilika
KUMBUKA-Soko ni kitu cha muhimu katika
mradi wako kwa sababu mwishoni
ukishapata mavuno yako kwa shughuli za
itahitaji uziuze hivyo kuwa makini na mradi
unaochagua kwa sasa miradi ambayo soko
lake ni rahisi kulipata ni Kuku wa kienyeji,
kuku wa mayai/nyama
matunda,mbaazi,ufuta n,k

Matumizi ya mbaazi kama dawa

Mbaazi ni zao la chakula ambalo linalimwa sehemu nyingi sana hapa nchini, zao hili pia linaweza kutumika kama dawa kwa kutumia majani, mizizi na maua

MAANDALIZI

Chukua majani, maua au mizizi kiasi cha nusu kilo (ni vizuri kama utachanganya vyote) pondaponda na uloweke kwenye maji safi kiasi cha lita 2 kwa muda wa masaa 24.

Chuja na uweke dawa hii mbali na jua/joto, ni vizuri kama ataweka kwenye friji, kunywa kikombe kimoja kutwa mara 3 kwa siku 3

TIBA

Dawa hii inaweza kutibu magonjwa yafuatayo

1-Inauwezo mkubwa wa kushusha homa

2-Husaidia kuponesha vidonda.

3-Husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi kwa wanawake.

4-Husaidia kupunguza uvimbe

5-Huponyesha kifua na kukohoa.

6-Husafisha kibofu/njia ya mkojo.

7- Huongeza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbali mbali

FUNZO: Maisha ni kuchagua

Siku hizi kuna tangazo moja la kampuni ya simu za mikononi, Tigo, likimuonesha mama akiwa _busy_ na pembeni yupo mwanae mdogo apo akijisemesha na akatamka maneno ambapo mama akaona ni kama ameanza kuongea. Kwa furaha anampigia simu mumewe akimtaka amsikilize mwanae akiongea. Hapo mama anamtaka mwanae aseme “mama” na baba naye anavutia kwake akimtaka aseme “baba”. Kwa maajabu kabisa mtoto anawapotezea wote na kutamka “ni Tigo peesa”. Wazazi wakashikwa na butwaa lakini huku wakitabasamu.

Ukiitazama vizuri kazi ya ubunifu iliyotumika katika tangazo hili unaweza kupata funzo, pamoja na mengine, kwamba mtoto alikua na chaguzi lake ambalo ni tofauti na yale ambayo wazazi walikua wamempa. Lakini zaidi, pamoja na kuwa amekuwa na chaguzi lake binafsi, pasipo kufuata alichoagizwa na baba au mama, bado wazazi wanatabasamu kwani wanaona mwanao kafanya jambo jema.

๐Ÿ‘‰Unaona unavyofanya kazi bila furaha kwa kua ulifanya chaguo la kazi hiyo kwa kusikiliza ndugu au marafiki.

๐Ÿ‘‰Unaona unavyo _struggle_ katika biashara kwani halikua chaguo lako bali ni la ndugu au marafiki

๐Ÿ‘‰Unakumbuka ulivyoshindwa kusomea kile unachopenda kwa kusikiliza ndugu au marafiki
9
๐Ÿ‘‰Unakumbuka ulivyoshindwa kuishi na yule mwenzi uliyempenda na mkapendana naye kwa kusikiliza ndugu na marafiki

Unaweza kushauriwa, na ushauri ukawa ni mzuri kabisaa na ukaona ni vyema uufuate kwa kua hata wewe umeambiwa na ukachanganya na akili yako ukaona inafaa.

Jana nilitoa semina kwa wanafunzi wote wa Shule ya Sekondari Chang’ombe, pamoja na mambo mengine nikawataka kupima sana marafiki walio nao na kuona kama ni washauri wazuri na kama sivyo waachane nao na kuwa na marafiki wapya wenye mawazo chanya ya kuwasaidia kutimiza ndoto zao.

Kuna hii daladala imeandikwa nyuma *_Marafiki wengi mjini hasara_*. ๐Ÿ˜ƒ. Mie nakuambia sio marafiki tu, hata ndugu pia. Kikubwa ni kuwapima wale ulio nao karibu na kuona kama bado ni wa msaada kwako. Wapime na chukua hatua. Kumbuka Mheshimiwa JK aliwahi kutuasa ” _Akili za kuambiwa, changanya na za kwako_ “.

Mtoto ni wa baba au wa mama? Angalia hoja za baba na mama kila mmoja anadai ni wake

Mtoto ni wa baba au wa mama?

Mume alimpa mkewe talaka wakaenda mahakamani ili hakimu aamue nani akae na mtoto.

MME: Akasimama akauliza hivi: Mheshimiwa hakimu hivi nikichukua ATM card nikaingiza kwenye mashine ikatoa pesa, sasa pesa zitakuwa ni za ATM au zakwangu?

MKE: Akasimama na kusema: Mheshimiwa hakimu hivi ukimwaga mbegu ktk shamba la mtu mti ukiota utakuwa wa kwako au wa mwenye shamba?.

Hebu tumsaidie hakimu aamue kesi hiiโ€ฆ

Matumizi ya Papai Katika Urembo

Tunda la kitropiki la papai lina vitamini C na E likiwa na siri kubwa ya urembo na hutumika kutengeneza facial za aina mbalimbali.
Papai limekuwa likitumiwa kama njoia boya ya kutunza uso wako na kumfanya mtu kuwa na ngozi ya asili.

Bidhaa ambazo zimekuwa zikitengenezwa kwa kutumia tunda la papai ni pamoja na sabuni, lotion, tona, moisturiza, facial peels na nyingine nyingi.

Ukitumia facial mask ya papai utakuwa na sura nzuri ya asili na kukupa uonekanaji mzuri wa uso wako. Facial mask hii huweza hutumika kwa watu wa umri na aina yoyote ya ngozi.

Facial mask ya papai ina nguvu ya kungโ€™arisha uso wako.
Pia inasaidia ngozi ambayo imeshaanza kupatwa na makunyanzi kutokana na umri kuonekana ya kuvutia kwani pia imekuwa ikiondoa chunusi na makunyanzi pia.

Ni rahisi kutengeneza facial mask ya papai na ukitumia itakusaidia katika kukabiliana na ngozi iliyoanza kuchoka, kungโ€™arisha ngozi.

Kuna na njia nzuri za kuhakikisha kuwa, tunakuwa na nyuso nzuri zenye kupendeza na kuvutia ikiwemo kutumia vitu vya asili pamoja na matunda ya aina mbalim ambayo husaidia zaidi katika kuimarisha ngozi.

Mask ya mchanganyiko wa papai yai na yai ni nzuri katika kuhakikisha kuwa unakuwa na ngozi nzuri na nyororo.

Njia hii pia husaidia hata wale wenye nyuso za mafuta ambao wamekuwa wakisumbuliwa na chunusi mara kwa mara kwa kufanya ngozi kuwa kavu.

Unaweza kutengeneza aina hii ya mask kwa kufanya yafuatayo:-
Chukua papai likate kasha toa mbegu na kasha lisage kwa kutumia blenda ya kuondaponda kwenye kibakuli kwa kutumia kitukama mchi mdogo wa kinu.

Kisha weka mchanganyiko huo kwenye chombo ulichokichagua kama kikombe au bakuli.
Vunja yai na koroga kuhakikisha kuwa mchanganyiko huo umechanganyika vizuri.
Safisha uso wako kwa kutumia cleanser au maji ya vuguvugu na uondoeuchafu wote ulioganda usoni.

  • Kisha paka mask kuzunguka uso wako, na unapopaka hakikisha kuwa,
  • mchanganyiko huo haugusi macho yako.
  • Osha uso wako baada ya dakika 15 kwa kutumia maji ya vuguvugu.
  • Jifute kwa kutumia taulo safi
  • Unaweza kupaka losheni, tona au moisturiza.

Husaidia kutunza ngozi na kuondoa vipele na uchafu ulioganda usoni.
Hii ni njia rahisi ya kutengeneza uso isiyo na gharama.

Jifunze kupitia mfano huu Ili uishi kwa amani na watu

Siku moja nilichukua taxi aina ya UBER nikiwa naelekea uwanja wa Ndege Mwl. Nyerere Dereva huku akiendesha kwa ustaarabu sana mara ghafla pasipo kutegemea gari ya taka ikajitokeza mbele yetu kutokea nje ya barabara. Dereva wa taxi kwa umakini na neema ya Mungu akalikwepa gari hilo na ilikuwa kidogo agonge gari zingine mbele yetu.

Pasipo kutegemea dereva wa gari la taka akaanza kufoka na kutoa matusi kwa kelele kubwa!

Katika hali ya kushangaza dereva wa taxi alitabasamu na kuwapungia mkono waliokuwa kwenye gari la taka na ndipo kwa mshangao nilimuuliza; “Inakuwaje ufanye hivyo wakati walitaka kutuua na hata kuharibu mali yako?”

Akajibu kwa upole akinitazama kwa tabasamu akasema. โ€œKatika maisha yetu, kuna watu wako kama gari la taka. Wamejaa misongo, hasira, maumivu, wamechoka kifikra, kiuchumi na kimaisha, na wamejaa masikitiko mengi. Watu hao takataka zao zinazopowazidi hutafuta mahali pa kuzitupa na haijalishi mazingira wanakozitupia.

FUNZO!
Jifunze kutogombana nao. Wapungie mkono, wape tabasamu, songa mbele. Haikupunguzii kitu. Wala usiruhusu takataka zao zikupate.”

Uliumbwa kuyafurahia maisha. Usiyafupishe kwa kuamka asubuhi na kinyongo, na hasira, na ghadhabu kwa sababu ya mtu fulani.

Watafiti wanasema 10% ya maisha ni vile ulivyoyatengeneza lakini 90% ya maisha ni vile unavyochukuliana nayo.

Jifunze kuchukuliana na maisha kuliko vile unavyoyatengeneza huku ukimtegemea Mungu.

ANGALIZO!
Ukiona umeanza kueleweka, kukubalika, kutambulika, kufahamika, kuheshimika na kupata nafasi zaidi kwa kile unachokifanya kumbuka kuendelea kuzingatia misingi, nguzo, miiko na nidhamu iliyokuwezesha kufika hapo ulipo ili uende mbali zaidi.

MUNGU AKUBARIKI SANA.

Ushauri kuhusu mwanamke wa kufaa kuoa

Nawaandikia ninyi vijana wa kiume na wanaume wote, maana mna nguvu na mmejaliwa na mwenyezi Mungu utashi, hekima na busara. Yote hayo ni ili muweze kutawala kila kitu tokea kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu huu. Wekeni wivu pembeni na Yafuateni haya;

1. Oa mwanamke ambae unaweza KUSALI nae na sio kwa sababu anajua KUFANYA MAPENZI vema.

2. Mwanaume bora KAMWE hapimwi kwa idadi ya wanawake alionao au aliotembea nao BALI kwa idadi ya wanawake aliowaambia “Mimi ni mume wa mtu” au ninae mtu tayari.

3. Kuna aina ya wanawake unatakiwa kuwaepuka kabisa kwa gharama yoyote ile, “wanawake wamaodhani uzuri wao ndio bora zaidi kuliko tabia zao”

4. Kila mwanamke anavutia akivaa nguo fupi inayoonesha maungo yake wazi, ila kama utakuta mwanamke amevaa nguo ndefu au za kusitiri mwili wake na bado anavutia, huyu ni dhahabu! Anathamini mali za mumewe!

5. Kamwe usimpe mwanamke mimba ya mtoto kabla hujampa mimba ya malengo na ukayatimiza.

6. Tafuta mwanamke ambae atakupa challenge ya maisha na kuongeza uwezo wako wa kufikiri na sio mwanamke wa kila kitu Ndio mzee!

7. Wanawake wakamilifu hawapatikani popote duniani, ila wanawake bora wapo kila mahali.

8. Mwanamke anaweza kukusaliti, ila Mungu hawezi kukusaliti, hivyo basi kabla hujapata mwanamke Mpate Mungu kwanza. Kuna raha sana kuwa ndani ya Mungu asikwambie mtu!

9. Kama unajijua umefikisha miaka 25 na kuendelea epuka mambo ya kivulana, kuvaa suruali katikati ya makalio, kuvaa hereni, kubadili badili wanawake kama unachambua mitumba ya karume etc

10. Usitumie kichwa chako kunyoa kiduku, tumia kichwa chako kuwaza mambo yenye tija ikiwemo kutafuta pesa na kuongeza hazina ya maarifa.
MBARIKIWE SANA WANAUME WOTE WENYE BUSARA..

Kama Mwanamme Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE ili uweze kuwafahamu zaidi wanawake

Aina ya vyakula vinavyotakiwa kwa wajawazito

Kwa ajili afya ya mama na mtoto ni muhimu sana, mwanamke anatakiwa apate chakula bora kilicho na madini yote kama vitamini na protini. Mama mjamzito anatakiwa apate gramu 100 za protini kila siku. Ifuatayo ni mlo kamili anaotakiwa apate mama mjamzito kila siku ya ujauzito wake kwa afya bora.

Hivi ndivyo vyakula bora ambavyo mama mjamzito na mtoto wake wanastahili kula;

1. Jamii Kunde

Mbegu za kunde ni sehemu muhimu ya chakula kwa mama mjamzito kwa sababu huwa na kiwango kikubwa cha protini. Kwa watu wasiokula nyama au wana uwezo mdogo tu kujipatia nyama mbegu za jamii kunde zinatosheleza mahitaji ya protini. Hivi ni vyakula vya mimea kama Soya,Peas,Karanga, Alfa alfa,Mikunde, maharage.

2.Mayai

Mayai mawili kwa siku husaidia kuupa mwili protini, vitamini A na madini ambayo itasaidia kuzuia kupatwa na maradhi ya magonjwa mbali mbali.

3. Maziwa na vyakula vya jamii ya maziwa

Glasi nne au zaidi ya maziwa ya aina yoyote pamoja na/au vyakula vyenye jamii ya maziwa kama jibini, mtindi na siagi. Maziwa ni muhimu kwa protini, calcium, vitamini na virutubisho vingi. Vitasaidia ukuaji wa mifupa na misuli, Ni muhimu kwa damu yenye afya, kusaidia usingizi na kusawazisha mdundo wa moyo.

4. Viazi tamu

Viazi vitamu vina vitamini A ambayo husaidia ukuaji wa macho ya mtoto,ngozi na mifupa

5. Nyama

Nyama ya kuku au ngombe huwa na protini nyingi sana na husaidia katika ukuaji wa mwili wa mtoto hasa kwa mama mjamzito wa miezi minne

6. Nafaka na vyakula vya Wanga

Vyakula hivi huipa mwili nguvu ya kufanya kazi na pia ukuaji wa mtoto tumboni.Vyakula hivi ni kama mahindi,mtama ,mihogo,vyakula vya ngano kama mkate n.k.

7. Avocado

Ni matunda ambayo yana mafuta mengi maarufu kama fatty acid. Avocado inasaidia katika ukuaji wa ubongo,ngozi nyororo na ukuaji wa misuli ya mtoto tumboni.

8 .Mboga za majani

Mboga za majani kama spinach, kabeji, mchicha na matembele. Mboga hizi zinafaa ziwe zenye rangi ya kijani iliyokolea kwa sababu hizi ndizo zenye virutubisho vya kutosha. Mboga hizi zitampa mama na mtoto wake Vitamin A na B, pia virutubisho vitakavyosaidia mwili kupata protini ya kutosha, ukuaji wa mwili, na utengenezaji wa damu. Kutopata mboga za kutosha kunaweza sababisha mama kupata ugonjwa wa Anemia.

9. Mafuta ya samaki

Mafuta ya maini ya samaki huwa na Omega fatty acids ambayo inasaidia ukuaji wa ubongo na macho ya mtoto.

10.Maji

Maji ni muhimu kwa mwili kwa sababu inasaidia kwenye mmenyenyo na unyonywaji chakula na pia husaidia kuzia choo ngumu Maji pia huzuia uvimbe wa mwili na maambukizi ya mfumo wa mkojo(UTI)

Ushauri wa ukweli Ili Uwe mwanaume wa Ukweli

1. Ukija kijiweni au pub au kwenye nyama choma acha zile stori za sijui umesoma wapi hadi wapi, sijui una madigirii mangapi. Piga stori nyingine, mbona ziko nyingi tu. Kujielezea sana shule yako ni ushamba fulani hivi, dizaini kama hujiamini so lazima ujivishe nyota. Unaboa.

2. Tembea na keshi mfukoni kama vipi, stori za kadi yangu ya benki imegoma sio ishu.

3. Punguza mambo yako ya kuvaa sana kipapaa. Sometimes ibuka na pensi na jinsi tu mwana.

4. Punguza kukesha nje mfululizo, iwe umeoa, una mpenzi au upo upo. Kikanuni kabisa usikae nje hadi usiku wa manane siku tatu mfululizo labda uwepo mchongo wa maana sana. I mean wa maana sana.

5. Epuka sana mchezo wa kujipiga tattoos. Kuna watu wamekosa wake au michongo hevi in life kisa hizo mambo.

6. Nasisitiza sana epuka kumtaka mpenzi wa zamani wa mshikaji wako. Pigia mstari hii pointi. Kwani lazima upite palepale? Tusiishi kikondoo bro.

7. Jiunge walau na mtandao mmoja wa kijamii. Keep in touch na washikaji. Kuna wana toka mmemaliza primary hamjachekiana, utawakuta mitandaoni. Unaweza kupata mchongo au kujifunza ishu mbili tatu, au kuwa fala zaidi ukiamua.

8. Maisha mafupi sana, jitahidi kupunguza kukunja ndita. Jiachie mara moja moja.

9. Ukifika baa uwe tayari unajua unakunywa nini. Sio Mhudumu anakuja kukusikiliza unawaaaaaza. Inaonyesha hujisomi na huna mipango. Samahani lakini.

10. Kama hujaalikwa kwenye ishu, usiende mwanangu. Sometimes hata ukialikwa usiende pia. Unaweza kualikwa ili useme no, kiushahidi tu.

11. Halafu tumechoka wewe kuwa kituko ukilewa. Kama pombe huziwezi ziache, piga juisi tu au maji wakati wana tunapiga monde, sio kesi, ni uwezo tu wa kuhimili.

12. Toa tip bila kuomba namba ya baamedi basi mwanangu. Jifanye kama umetoa tu msaada. Hata simba sio swala wote huwa anawala porini, wengine anawacheki anapita zake.

13. Punguza kutumia simu sana, tena wakati mwingine kwa ishu ambazo hazina mpango.
Ukumbuke juzi juzi hapa wataalamu wamesema simu zinaleta ugumba.

14. Nunua tumiwani twa jua twa bei bei hivi, inakupa mwonekano wa kijentlomani sometimes.

15. Piga push-ups walau 50, sit ups na dips kabla ya kuoga asubuhi, hii afya tumeazimwa tu, jiweke fit.

16. Toka out na washikaji zako at least mara moja kwa mwezi mpige msosi na kinywaji. Wife au demu wako na wanao waache home! Sio kila kona kila siku uko nao kama mkoba, kichwa kitatia kutu.

17. Julikana walau hata baa mbili tatu au sehemu mbili tatu. Baa, basketball ground, soccer ground, acha kujikunyata home. Wewe mtoto wa kiume man.

18. Jifanye mjuaji sometimes, then jifunze baadaye. Sio kila kitu wewe ni โ€œI donโ€™t knowโ€.

19. Beer moja au glass moja ya wine baada ya mlo haiwezi kukuvurga, kama hutaki, kunywa majuisi yako basi ulete inzi, au misoda ujijazie magonjwa.

20. MTOTO WA KIUME HAPIGI SELFIE OVYO OVYO NA KUBINUA MIDOMO na KULAMBA LIPSI. PIGA SELFIE KWENYE ISHU MUHIMU. FAMILIA HIVI, DEMU MKALI, etc. Umenisoma?

21. Ukiweza miliki hata panga ghetto, maana bastola najua ngumu. Sio nyumba nzima huna hata kasilaha kadogo.

22. Ridhika. Hamna hata siku moja utakuwa na kila kitu. Jifunze kushukuru kwa ulicho nacho.

23. Sometimes agiza matunda badala ya chipsi.

24. Ukikutana na demu mzuri kiwanja yuko peke yake, muongeleshe.

25. Miliki walau suti moja kabla hujapitisha miaka 30 bro. Please. Na tupafyumu.

26. Kuwa na mpenzi moja
kwa wakati mmoja. Anatosha sana. Trust me.

27. Ukitaka kujilinganisha, jilinganishe wewe wa jana na wewe wa leo. Utafika mbali. Ukijilinganisha na wana utapasuka kichwa.

28. Piga picha nyingi kwa camera (again, sio selfies) tunza kumbukumbu.

29. Ukialikwa kwenye party usiende mikono mitupu. Nenda walau na kachupa kamoja ka mvinyo.

30. Date demu nje ya wale unaokutana nao club au baa mara wa mara. Utakuja kuniambia faida zake.

31. Huwezi kuwa mpenzi wa pombe au sigara kwa sababu hivyo vitu havitakaa vikupende.

32. Hata siku moja usirudiane na demu aliyekuacha kisa huna mkwanja. Kaenda kutafuta kakosa ndio maana kakurudia labda baada ya kuona umepata. Siku akikutana na mwenye chambi kukuzidi? Jibu kaa nalo.

33. Sometimes jitoe out mwenyewe, kaa mahali piga msosi wako na kinywaji chako, tafakari ishu zako. Alone.

34. Jisomee ukiwa na time. Inakupa chance kuazima ubongo wa mtu mwingine lakini pia inakupa matirio kwenye maongezi, ila stori za kuja kwenye joint na washikaji na kuanza kusema oh nimesoma kitabu hiki na kile kausha!

35. Puuza wanaozomea. Huwa wamekaa viti vile vya bei rahisi.

36. Hata siku moja usiseme โ€œNdo hivyo bwana, hamna namna tenaโ€. Ipo namna bro.

37. Usi-bet kama ukipoteza buku 5 we ni mtu wa kulia lia kindezi.

38. Muombe na Mshukuru Mungu wako. Kama huna Mungu jishukuru mwenyewe, kiazi wewe.

39. Kumbuka, sheria hufuatwa na wajinga lakini huwaongoza wenye busara.

Kama Mwanamme Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Faida za kunywa juisi ya ubuyu

Mungu ameumba miti na mimea kwa ajili ya binadamu. Kila mti au mmea una makusudio yake. Mbuyu ni miongoni mwa miti yenye faida nyingi na maajabu mengi. Vitu vyote vilivyomo kwenye mbuyu vinatumika kama chakula au dawa kwa faida ya binadamu.

Faida za kunywa juisi ya Ubuyu

Unga wa ubuyu unaelezwa kuwa na vitamini na madini mengi kuliko matunda mengine yoyote unayoyajuwa.

  1. Inaelezwa kuwa unga wa ubuyu una vitamini C nyingi mara 6 zaidi ya ile inayopatikana katika machungwa.
  2. Ubuyu una kiwango kingi cha madini ya Kashiamu (Calcium) mara 2 zaidi ya maziwa ya ngโ€™ombe, pia madini mengine yapatikanayo katika ubuyu ni pamoja na madini ya Chuma, Magnesiamu na Potasiamu ambayo ni mara 6 zaidi ya ile potasiamu ipatikanayo katika ndizi!
  3. Husaidia kujenga neva za fahamu mwilini
  4. Ina virutubisho vya kulinda mwili
  5. Ubuyu una vitamini B3 na B2 ambayo ni mhimu katika kuondoa sumu mwilini na umengโ€™enyaji wa madini ya chuma, kimsingi vyakula vyenye afya zaidi kwa ajili ya mwili ya binadamu huwa pia huwa na vitamin B2.
  6. Unaongeza kinga ya mwili sababu ya kuwa na kiasi kingi cha vitamini C
  7. Huongeza nuru ya macho
  8. Husaidia kuzuia kuharisha na kutapika
  9. Ina magnesiam ambayo husaidia kujenga mifupa na meno
  10. 10Husaidia wenye presha ya kushuka na wenye matatizo ya figo

Unywe kiasi gani? Jipatie kikombe kimoja cha juisi ya ubuyu kila siku hasa usiku na baada ya wiki kadhaa utaona matokeo yake mwilini.

Ili upate faida za juisi ya ubuyu, zinazoelezwa hapa, lazima upate ule ubuyu halisi (mweupe) usiochanganywa na kitu kingine cha kuongeza ladha au rangi.

Uwe na subira Baada ya kuomba

Uwe na subira Baada ya kuomba kwa Mungu. Sio kila unachoomba kwa Mungu utakipata kwa wakati huo huo au kwa wakati unaofikiri. Mungu ni Mwaminifu Sana Kwenye kujibu maombi lakini vile vile ni mwenye Hekima Kwenye kukujibu, anajua wakati gani ni sahihi kukujibu maombi yako. Anaweza kukujibu saa hiyo hiyo, kesho, keshokutwa au hata mwakani kwa kuangalia wakati ufaao na kwa manufaa yako. Kwa hiyo unapoona hujajibiwa usife moyo, bali uwe na matumaini. Mungu anajua akujibu lini kwa kuwa anajua ni lini wakati ufaao na ni lini kitu kipi kina kufaa.

Mapishi ya Ndizi na samaki

Mahitaji

Ndizi laini (Matoke 6)
Viazi mbatata (potato 3)
Samaki wabichi wa wastani ( Fresh tilapia 2)
Kitunguu swaum (garlic 6 cloves)
Tangawizi (fresh ground ginger vijiko 2 vya chai)
Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 kopo)
Vitunguu (onion 1)
Pilipili (chilli 1 nzima)
Chumvi (salt to your taste)
Mafuta (vegetable oil)
Limao (lemon 1/2)
Curry powder (1/2 kijiko cha chai)

Matayarisho

Safisha samaki kisha wakate vipande vitatu. Wakaushe maji kisha wamarinate na kitunguu swaum,tangawizi, chumvi, na limao kwa muda wa masaa 2. baada ya hapo waoke kwenye oven kwa muda wa dakika 30. baada ya hapo andaa ndizi na viazi kwa kuzimenya na kuziosha kisha ziweke pembeni. Kisha katakata vitunguu maji, Tangawizi, vitunguu swaum na nyanya kisha vitie kwenye blenda na usage mpaka mchanganyiko usagike vizuri. Baada ya hapo tia mchanganyiko katika sufuria na ubandike jikoni, acha uchemke mpaka maji yote yakauke. Maji yakisha kauka punguza moto na utie mafuta, curry powder, pilipili na chumvi. Kaangiza mpaka mchanganyiko uive na baada ya hapo tia viazi na maji kiasi na uache viazi vichemke mpaka vikaribie kuiva kisha tia ndizi na samaki na ufunike. Pika mpaka ndizi na viazi viive. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuseviwa.

Dondoo muhimu kwa Afya yako unapostuka usiku

Kumekuwepo na tatizo la vifo vya ghafla sana tena kwa watu ambao wana afya njema na hii inatokana na kuamka ghafla usiku ambapo ubongo hukisa damu ya kutosha.

Unapoamka katikati ya usiku kwenda kujisaidia haja ndogo mfumo wa damu unakuwa umebadilika. Kwa sababu kuamka ghafla,kinakuwa hakuna mzunguko wa kutisha wa damu kwenye ubongo unaosababisha moyo kushindwa kufanya kazi kutokana na ukosefu wa damu.

Ushauri:tumia dakika 3 na nusu kufanya yafuatayo”:

1. Unapoamka usingizini lala kitandani kwa nusu dakika ;
2. Kaa kitandani kwa takribani nusu dakika;
3. Shusha miguu,kaa pembeni ya kitanda takribani nusu dakika.

Baada ya dakika 3 na nusu hutakuwa na tatizo la ukosedu wa damu kwenye ubongo na moyo kushindwa kufanya kazi inapunguza uwezekano wa vifo vya ghafla na kuanguka ghafla.

Shirikisha marafiki na jamaa.

Inatokea bila kujali umri.

Kushare ni kujali.Kama tayari ulikuwa unajua hili lichukulie kama kumbukumbu.

Jinsi ya Kupika skonzi

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Sukari (sugar 1/2 kijiko cha chakula)
Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai)
Hamira (yeast 1/2 kijiko cha chakula)
Baking powder 1/2 kijiko cha chai
Siagi (butter 1/4 ya kikombe cha chai)
Maziwa (fresh milk 3/4 ya kikombe cha chai)(unaweza kutumia maji badala ya maziwa)

Matayarisho

Pasha maziwa yawe ya uvuguvugu kisha weka pembeni, pia yeyusha siagi na uweke pembeni.Baada ya hapo tia kila kitu kwenye bakuli la kukandia kasoro maziwa, na uchanganye vizuri kisha tia maziwa kidogo kidogo katika mchanganyiko huo kisha ukande. Ukimaliza uweke kwenye sehemu ya joto na uache uumuke. Ukisha umuka utawanyishe katika madonge saba Kisha .pakaza mafuta au siagi katika chombo cha kuokea kisha yapange hayo madonge katika hicho chombo na uyaache yaumuke tena (kwa mara ya pili). Baada ya hapo pakaza mafuta juu ya hayo madonge na uyaoke (bake) katika oven (moto 200ยฐC ) kwa muda wa dakika 25 na hapo scones au maskonzi yatakuwa tayari

Jinsi ya kupika Biriani Ya Nyama Mbuzi Ya Mtindi Na Zaafaraan

Vipimo – Nyama

Nyama mbuzi – 1 kilo

Kitunguu menya katakata – 1

Nyanya/tungule – 2

Thomu (kitunguu saumu/garlic) saga – 5 chembe

Tangawizi mbichi โ€“ kuna/grate au saga – 1 kipande

Pilipili mbichi saga – 2

Bizari ya pilau nzima (cumin seeds) – ยฝ kikombe cha kahawa

Mdalasini – 1 kijiti

Karafuu nzima – 5 chembe

Gilgilani/dania (coriander seeds) – ยฝ kikombe cha kahawa

Bizari ya mchuzi – 1 Kijiko cha supi

Chumvi – Kiasi

Mtindi – 1 glass

Hiliki ilopondwa – 2 vijiko vya chai

Vitunguu โ€“ menya katakata slices kwa ajili ya kukaanga- 7- 9

Mafuta – Kiasi ya kukaangai vitunguu

Vipimo – Wali

Mchele wa pishori/basmati – 4 glass

Zaafarani roweka katika kikombe cha kahawa – Kiasi

Mafuta – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Katika sufuria, changanya nyama pamoja, kitunguu kimoja, tangawizi, thomu, nyanya, na viungo vyake isipokuwa mtindi, hiliki na vitunguu vilobakia.

Tia maji kisha funika ichemke mpaka iwive nyama na ikauke supu.

Tia mtindi na hiliki changanya pamoja.

Weka mafuta katika karai, kaanga vitunguu mpaka viwe rangi ya hudhurungi. Toa uchuje mafuta. Kisha viponde ponde kwa mkono uchanganye na nyama.

Chemsha mchele uive nusu kiini, mwaga maji.

Mimina katika nyama utie zaafarani, funika upike wali hadi uwive.

Epua ukiwa tayari.

Huyu bibi kweli kiboko, cheki alichofanya akiwa na babu

Bibi na Babu walisafiri wakielekea kwa mtoto wao ambae hawajamuona zamani.

Walipofika njiani wakawa wamechoka Sanaa. Wakaamua kutafuta hotel ili walale.

Wakakubaliana walale kwa masaa 4. Wakalala, Walipoamka, mfanyakazi wa Hotel akawatoza Tsh. 500,000/=

Wale wazee wakashangaa hata kama ni hotel ya kisasa lakini sio laki tano kwa masaa 4.

Babu akagoma kulipa akasema aitiwe meneja.

Meneja akaja kuwasikiliza

Babu: ” Kwanini bili ni kubwa hata kama ni hotel ya kisasa?”

Manager;“kuna maswiming puli, ya kisasa “

Babu; “Lakini hatukuyatumia”

Manager; “Ah ah ah. Lakini mungeweza kama mngetaka”

Babu: “Hata hivo bado haithamini kuwa laki 5”

meneja: “Pia Kuna waimbaji kutoka sauzi, Uganda , Congo”

Babu: “Lakini sisi hatukuwasikiliza”

Meneja: “Ndiooo. Lakini mngeweza kama mngetaka”

Babu; aka give up na kumwambia mkewe andika cheki uwape,,

Bibi akaandika akampa meneja.

Meneja anaangalia anaona sh. 50,000

Akashangaa na kusema. “VP mbona hamsini'”

Bibi akajibu “450,000 ya kulala na mimi”

Meneja akajibu; “Lakini sijalala”

Bibi :“ungeweza kama ungetaka”

Maswali na Majibu kuhusu dhamira

Dhamiri adilifu ni nini?
Dhamiri adilifu, iliyo ndani kabisa mwa mtu, ni uamuzi wa akili ambao kwa wakati wake unamuagiza mtu atende mema na kukwepa maovu


Katika hukumu zake dhamira ifuate nini?
Katika hukumu zake dhamira ifuate daima Injili, Amri za Mungu na za Kanisa na wajibu zetu.


Twajenga na kutunza dhamira zetu namna gani?
Twajenga na kutunza dhamira zetu kwa;-
1. Kufuata sauti ya Roho Mtakatifu
2. Kuzingatia mafundisho ya dini
3. Kuzingatia mila na desturi njema tulizopata katika malezi.
4 Kufuata mifano na tabia njema ya wenzetu na ya Watakatifu


Hadhi ya nafsi ya mtu inadai nini kuhusu dhamiri adilifu?
Hadhi ya nafsi ya mtu inadai unyofu wa dhamiri adilifu, yaani upande wa akili na sheria ya Mungu


Dhamiri adilifu inaundwa namna gani iwe nyofu na ya kweli?
Dhamiri nyofu inayosema kweli inaundwa kwa;
1. Malezi
2. Upokeaji wa neno la Mungu
3. Upokeaji wa Mafundisho ya Kanisa
4. Sala
5. Utafiti wa dhamiri


Dhamiri adilifu inatengenezwa na kusaidiwa na nini?
Dhamiri adilifu inatengenezwa na vipaji vya Roho Mtakatifu na kusaidiwa na mashauri ya watu wenye busara.


Dhamiri inatakiwa kufuata daima masharti gani?
Dhamira inatakiwa kufuata daima masharti yafuatayo
1. Hairuhusiwi kutenda maovu kusudi yapatikane mema
2. Yoyote muyatakayo mtendewe na watu, ninyi watendeeni vivyo hivyo. (Mt 7:12)
3. Upendo hufuata daima nia na heshima kwa jirani na kwa dhamira yake

Hizi hapa, Aina 10 za ndoa usizozijua

Karibuni tuangalie aina hizi 10 za ndoa.

1. NDOA YA MKEKA

Inatokana na kufumaniwa na Binti wa watu.
Ndoa hii huwa Haina mahari. Hii huvunjika
mwaka mmoja tu,baada ya wanandoa kugundua
hawakuwa wakipendana!

2. NDOA YA MIHEMKO (NYEGE)

Hufungwa na vijana wenye umri wa miaka kati
mume18 mke 16.Huvunjika baada ya miaka 3 au
4 ya ndoa.

4. NDOA YA MAONYESHO

Wenye ndoa Hii hupenda kujionyesha
barabarani.Ila ndani hazina utii.Hupigana kila
wanaporudi kutoka kwenye mizunguko. Cha
kushangaza huwa hazivunjiki lakini ndiyo ndoa
zinazoongoza kwa kuchepuka!

5. NDOA YA UHAMISHO.

Hufungwa na watumishi wa vijijini na mjini. Ili wa
kijijini ahamie mjini.Mahari utoa anaetaka
kuhamia mjini. Hata kama mahari atatoa mume
lakini hii ndiyo ndoa yenye ukakasi
zaidi.Huvunjika mara tu wanapoanza kuishi wote
mjini. Salama ya hii ndoa ni kuhama kutoka mjini
kwenda kijijini.

6. NDOA YA MIMBA.

Hufungwa kwa sababu wanaoowana hawataki
kuonekana makwao kuwa wamezaa nje. Au
muolewaji alikuwa hampendi muoaji kwa
dhati.Muoaji hutumia mimba kama mtego wa
kuingia ndoani. Hii huvunjika mtoto akizaliwa na
kufikisha mwaka 1.

7. NDOA YA MALI (UTAJIRI)

Muolewaji miaka 18 au 28 Muoaji 65 au 70.Ndoa
hii pia huitwa ndoa ya babu na mjuukuu. Ndoa ya
aina hii hudumu, kwasababu mwenye kauli ni
mwenye mali. Asilimia kubwa ya waume wa ndoa
hizi hulea watoto wasio wao.

8. NDOA YA KWASABABU.

Hufungwa ili mradi muoaji au muolewaji
aonekane tu kwa jamii kuwa naye kaoa au
kaolewa.Huwa hazina utii wala upendo dhati.
Ndoa ya aina hii ikifikisha miaka 4 huwa
hazivunjiki wahusika huishi kwa mazoea.

9. NDOA YA UPENDO.

Ndoa hizi ziliishia mwaka 1978 kabla ya vita vya
kagera.Muoaji na muolewaji hawakuangalia vitu
ila utu tu ambao uliwaunganisha na kutengeneza
upendo wa kudumu. Hii ilidumu miaka yote.

10. NDOA KUCHUMA

Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji
akapate kitu au vitu fulani kutoka kwa upande
mmoja wapo. Hii hudumu miaka kadhaa
kutegemea na malengo ya mhusika. Wengine
husubiri mpaka mhusika afe,lkn hujikuta
wanakufa wao kwanza.
Kuwa mwangalifu!

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About