Somo la Kwanza
1Fal 19:9, 11-13
Eliya alifika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia. Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunjavunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi: na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.
Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi vake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango.
NENO LA BWANA…….
Wimbo wa Katikati
Zab 85:8-13
Nisikie atakavyosema Mungu Bwana,
Maana atawambia watu wake amani.
Hakika wokovu wake u karibu na wamchao,
Utukufu ukae katika nchi yetu.
(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.
Fadhili na kweli zimekutana,
Haki na amani zimebusiana.
Kweli imechipuka katika nchi,
Haki imechungulia kutoka mbinguni.
(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.
Naam, Bwana atatoa kilicho chema,
Na nchi yetu itatoa mazao yake.
Haki itakwenda mbelc zake,
Nayo itazifanya hatua zake kuwa njia.
(K) Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.
Somo la Pili
Rum 9:1-5
Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu, ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.
Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili; ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake; ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili.
Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.
NENO LA BWANA…..
Shangilio
Lk 19:38
Aleluya, aleluya,
Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana;
Aleluya.
Somo la Injili
Mt 14:22-33
Yesu aliwalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambe. wakati yeye alipokuwa akiwaaga makutano. Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.
Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho. Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea. akienda kwa miguu juu ya bahari.
Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli, wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu akanena, akawaambia, Jipeni movo; ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji. Akasema, Njoo.
Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe akisema, Bwana, niokoe.
Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? Nao walipopanda chomboni, upepo ulikoma. Nao waliokuwamo ndani ya chombo wakamsujudia wakisema, Hakika wewe ni Mwana wa Mungu.
NENO LA BWANA……….
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Nakuombea 🙏
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Dumu katika Bwana.
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Neema na amani iwe nawe.
Katika imani, yote yanawezekana
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mungu akubariki!
Baraka kwako na familia yako.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Endelea kuwa na imani!
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Sifa kwa Bwana!
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema zake hudumu milele
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tumaini ni nanga ya roho
Rehema hushinda hukumu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia