SOMO 1
Hes. 21:4-9
Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu; ili kuizunguka nchi ya Edomu watu wakafa moyo kwa sababu ya ile njia. Watu wakamnung’unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.
Bwana akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa. Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung’unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa Bwana, atuondolee nyoka hawa. Basi, Musa akawaombea watu. Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo, ataishi. Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 102:1-2, 15-20 (K) 1
(K) Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, kilio changu kikufikie.
Ee Bwana, usikie kuomba kwangu,
Kilio change kikufikie,
Usinifiche uso wako siku ya shida yangu,
Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi. (K)
Kisha mataifa wataliogopa jina la Bwana,
Na wafalme wote wa dunia utukufu wako;
Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni,
Atakapoonekana katika utukufu wake,
Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa,
Asiyadharau maombi yao. (K)
Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo,
Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.
Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu,
Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,
Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa,
Na kuwafungua walioandikiwa kufa. (K)
SHANGILIO
Yn. 8:12
Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema Bwana, yeye anifuataye, atakuwa na nuru ya uzima.
INJILI
Yn. 8:21-30
Yesu aliwaambia Mafarisayo: Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi mtakufa katika dhambi yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja.
Basi, Wayahudi wakasema, Je! Atajiua! Kwa kuwa asema, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja?
Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu. Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.
Basi wakamwambia, U nani wewe? Yesu akawaambia, Hasa neno lilo hilo ninalowaambia. Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu; lakini yeye aliyenipeleka ni kweli, nami niliyoyasikia kwake ndiyo ninenayo katika ulimwengu.
Wala hawakutambua ya kuwa anawatajia Baba. Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo. Naye aliyenipeleka yu pamoja nami; hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.
Naye alipokuwa akisema hayo, wengi walimwamwini.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Imani inaweza kusogeza milima
Neema na amani iwe nawe.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu akubariki!
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tumaini ni nanga ya roho
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Rehema hushinda hukumu
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Dumu katika Bwana.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Endelea kuwa na imani!
Sifa kwa Bwana!
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Katika imani, yote yanawezekana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Neema ya Mungu inatosha kwako
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Mwamini katika mpango wake.
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Nakuombea 🙏
Baraka kwako na familia yako.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Rehema zake hudumu milele
Mwamini Bwana; anajua njia
Mungu ni mwema, wakati wote!