SOMO 1
Hek. 2:1, 12-22
Wasiomsadikia Mungu walisema hivi, huku wakimfikiri yasiyo kweli, Zaidi ya hayo na tumwotee mtu wa haki, maana hatuna haja naye, naye yu kinyume cha matendo yetu; atukaripia ya kama tumeiasi torati, na kutushitaki ya kama tumekosa adabu. Asema ya kwamba anamjua Mungu, na kujiita mtumishi wa Bwana. Ametuwia magombezi ya fikira zetu. Hata kumtazama twaona ni kugumu; maan amaisha yake si sawasawa na masiha ya wengine, na mwenendo wake ni wa kigeni. Tuanhesabiwa naye kuwa kama madini hafifu; anajitenga na njia zetu kama na uchafu. Wenye haki asema kuwa mwisho wao ni heri; hujivuna ya kwamba Mungu ndiye baba yake.
Haya na tuone kama maneno yake ni kweli; tufanye kujaribu yatakayompata wakati wa mwisho wake; mradi mwenye haki akiwa ni mwana wa Mungu, Yeye atamtegemeza na kumwokoa mikononi mwa adui zake. Na tumhakikishe kwa jeuri na maumivu, ili tujifunze upole wake na kuithibitisha saburi yake akidhulumiwa. Hata tumhukumu auawe mauti ya aibu, maana ataangaliwa sawasawa na maneno yake.
Ndivyo walivyosemezana, wakakosea kabisa. Kwa maana uovu wao uliwapofusha; hawakuzijua siri za Mungu; wala hawakuutarajia mshahara wa utakatifu, wala kudhani ya kwamba iko thawabu kwao wenye roho zisizo na hatia.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 34:16-20, 22 (K) 18
(K) Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo.
Uso wa Bwan ani juu ya watenda mabaya,
Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Walilia, naye Bwan akasikia,
Akawaponya na taabu zao zoe. (K)
Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,
Na waliopondeka roho huwaokoa.
Mateso ya mwenye haki ni mengi,
Lakini Bwana humponya nayo yote. (K)
Huihifadhi mifupa yake yote,
Haukuvunjika hata mmoja.
Bwana huzikombo a nafsi za watumishi wake,
Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao. (K)
SHANGILIO
Lk. 8:15
Heri wale walishikao neno la Mungu katika moyo wao mwema na mnyofu, na wazaao matunda katika uvumilivu.
INJILI
Yn. 7:1-2, 25-30
Baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuw awakitafuta kumwua.
Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu. Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye laipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.
Basi baadhi ya watu wa yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue? Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu tuna jua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo? Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.
Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi. Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.
Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mwamini Bwana; anajua njia
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Imani inaweza kusogeza milima
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Dumu katika Bwana.
Neema na amani iwe nawe.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Neema ya Mungu inatosha kwako
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Nakuombea 🙏
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rehema zake hudumu milele
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Endelea kuwa na imani!
Baraka kwako na familia yako.
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Sifa kwa Bwana!
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mungu akubariki!
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mwamini katika mpango wake.
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Nguvu hutoka kwa Bwana
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Tumaini ni nanga ya roho
Katika imani, yote yanawezekana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema hushinda hukumu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Kwa Mungu, yote yanawezekana