SOMO 1
Eze. 47:1-9, 12
Malaika alinileta mpaka lango la nyumba; na tazama, maji yalitoka chini ya kizingiti cha nyumba, kwa njia ya mashariki, maana upande wa mbele wa nyumba ulielekea upande wa mashariki; nayo maji yakashuka toka chini ya upande wa kuume wa nyumba, upande wa kusini wa madhabahu. Ndipo akanileta nje kwa njia ya lango upande wa kaskazini, akanizungusha kwa njia ya nje mpaka lango la nje, kwa njia yake iliyoelekea mashariki; na tazama, maji yalitoka upande wa kuume. Na alipotoka mtu yule, mwenye uzi wa kupimia mkononi mwake, kwenda masharikini, akapima dhiraa elfu, akanivusha maji yale; maji yakafika mpka viweko vya miguu.
Kisha akapima dhiraa elfu, akanivusha maji yale, maji yakafika mpaka magoti. Kisha akapima dhiraa elfu, akanivusha, maji yakafika mpaka viuno. Kisha akapima dhiraa elfu, yakawa mto nisioweza kuuvuka; maana maji yamezidi, maji ya kuogelea, mto usiovukika. Akaniambia, Mwanadamu, je! Umeona haya? Kisha akanichukua, akanirudisha mpaka ukingo wa mto.
Basi nikiisha kurudi, tazama, kando ya ukingo wa mto ilikuwapo miti mingi sana, upande huu na upande huu. Ndipo akaniambia, Maji haya yanatoka kwenda pande za nchi ya mashariki, nayo yanashuka mpaka Araba, na kuingia katika bahari; maji yatokezwayo yataingia baharini, na maji yake yataponyeka. Tena itakuwa, kila kiumbe hai kisonganamacho, kila mahali itakapofika mito hiyo, kitaishi; kutakuwapo wingi mkubwa wa samaki, kwa sababu maji haya yamefika huko; maana maji yale yataponyeka, na kila kitu kitaishi popote utakapofikilia mto huo.
Na karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayatatindika kamwe; utatoa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu maji yake yanatoka mahali patakatifu; na matunda yake yatakuwa ni chakula; na majani yake yatakuwa ni dawa.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 46:1-2, 4-5, 7-8 (K) 7
(K) Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,
Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi,
Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari. (K)
Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu,
Patakatifu pa maskani zake Aliye juu.
Mungu yu katikati yake hautatetemeshwa;
Mungu atausaidia asubuhi na mapema. (K)
Bwana wa majeshi yu pamoja nasi,
Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Njoni myatazame matendo ya Bwana,
Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. (K)
SHANGILIO
Amo. 5:14
Tafuteni mema, wala si mabaya, mpate kuishi, hivyo Bwana, atakuwa pamoja nanyi.
INJILI
Yn. 5:1-3, 5-16
Baada ya hayo palikuwa na sikukuu ya Wayahudi; naye Yesu akakwea kwenda Yerusalemu. Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Betzatha, nayo ina matao matano. Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu, viwete, nao waliopooza.
Na hapa palikuwa na mtu, ambaye amekuwa hawezi muda wa miaka thelathini na minane. Yesu alipomwona huyu amelala, naye akijua ya kuwa amekuwa hali hiyo siku nyingi, alimwambia, Wataka kuwa mzima? Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu. Yesu akamwambia, Simama, jitwike godoro lako, uende. Mara yule mtu akawa mzima, akajitwika godoro lake, akaenda.
Nayo ilikuwa ni sabato siku hiyo. Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwambia yule aliyeponywa, Leo ni sabato, wala si halali kwako kujitwika godoro. Akawajibu, Yeye aliyenifanya kuwa mzima ndiye aliyeniambia, Jitwike godoro lako, uende. Basi wakamwuliza, Yule aliyekuambia, Jitwike uende, ni nani? Lakini yule mtu aliyeponywa hakumjua ni nani; maan aYesu alikuwa amejitenga, kwa sababu palikuwa na watu wengi mahali pale.
Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi. Yule akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima. Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Tumaini ni nanga ya roho
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mungu ni mwema, wakati wote!
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Sifa kwa Bwana!
Endelea kuwa na imani!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mungu akubariki!
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Rehema zake hudumu milele
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Imani inaweza kusogeza milima
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Nakuombea 🙏
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Neema ya Mungu inatosha kwako
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mwamini Bwana; anajua njia
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema hushinda hukumu
Mwamini katika mpango wake.
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Dumu katika Bwana.
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Neema na amani iwe nawe.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Baraka kwako na familia yako.
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida