SOMO 1
Yer. 11:18-20
Bwana akanijulisha haya, nami nikayajua; ndipo uliponionyesha matendo yao. Lakini mimi nalikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.
Lakini, Ee Bwana wa majeshi, uhukumuye haki ujaribuye viuno na moyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Bwana.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 7:1-2, 8-12 (K) 1
(K) Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe.
Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe,
Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye.
Asije akaipapura nafsi yangu kama samba,
Akiivunja-vunja pasipokuwa na wa kuponya. (K)
Bwana, unihukumu mimi,
Kwa kadiri ya haki yangu,
Sawasawa na unyofu nilio nao.
Ubaya wao wasio haki na ukome,
Lakini umthibitishe mwenye haki. (K)
Ngao yangu ina Mungu,
Awaokoaye wanyofu wa moyo.
Mungu ni mwamuzi mwenye haki,
Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku. (K)
SHANGILIO
Lk. 15:18
Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.
INJILI
Yn. 7:40-52
Wengine katika mkutano walipoyasikia maneno ya Yesu, walisema, Hakika huyu ndiye nabii yule. Wengine walisema, Huyu ndiye Kristo. Wengine wakasema, Je! Kristo atoka Galilaya? Andiko halikusema ya kwamba Kristo atoka katika uzao wa Daudi, na kutoka Bethlehemu, mji ule alioukaa Daudi? Basi kukaingia matengano katika mkutano kwa ajili yake. Baadhi yao wakataka kumkamata, alkini hakuna mtu aliyenyosha mikono yake ili kumshika.
Basi wale watumishi wakawaendea wakuu wa makuhani na Mafarisayo. Nao wakawaambia, Mbona hamkumleta? Wale watumishi wakajibu, Hajanena kamwe mtu yeyote kama huyu anavyonena. Basi Mafarisayo wakawajibu, Je! Ninyi nanyi mmedanganyika? Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo? Lakini makutano hawa wasioifahamu torati wamelaaniwa.
Akawaambia Nikodemo, (naye ni yule aliyemwendea zamani, maana ni mmoja wao), Je! Torati yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza, na kujua atendavyo? Wakajibu, wakamwambia, Je! Wewe nawe umetoka Galilaya! Tafuta, ukaone ya kuwa kutoka Galilaya hakutokea nabii.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Neema ya Mungu inatosha kwako
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Imani inaweza kusogeza milima
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Neema na amani iwe nawe.
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Dumu katika Bwana.
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tumaini ni nanga ya roho
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mungu ni mwema, wakati wote!
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mwamini katika mpango wake.
Mwamini Bwana; anajua njia
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Nakuombea 🙏
Endelea kuwa na imani!
Rehema zake hudumu milele
Katika imani, yote yanawezekana
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Sifa kwa Bwana!
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Baraka kwako na familia yako.
Mungu akubariki!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Rehema hushinda hukumu