1000+ Vichekesho vipya: Vichekesho vya AckySHINE
Padri Akimbia wakati wa kuungamisha, chanzo ni hiki
Padri alikuwa amekaa katika confession booth kanisani
peke yake.
Mara kukaingia jamaa mmoja akapiga magoti upande wa
pili, akafanya ishara ya msalaba kisha akaanza kuungama
{confess}
“Padri nimekuja kuungama dhambi zangu, leo nimefanya
dhambi kubwa sana.”
Padri, “Endelea⦔
“Bosi wangu aliniita nyumbani kwake, akaniambia
amegundua nimeiba shilingi millioni 100 kazini. Akasema
nisipozitoa atanipeleka polisi, sa kwa ukweli mi naogopa
kufungwa.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu,nikatoa bastola nikamuuaβ¦.. Yesu atanisamehe?”
Padri: “Utasamehewa.”
“Basi wakati nataka kuondoka nikasikia mlango
unafunguliwa kutazama, Loh! Mke wa bosi, alipoona
kilichotokea akasema anapiga polisi simu.
Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu, nikamuua na yeye piaβ¦ Yesu atanisamehe hilo?”
Padri: “Utasamehewa.”
Nikatoka nje, nikawasha gari niondoke, lakini mlinzi
akakataa kunifungulia, ati amesikia mlio wa
bastola. Nikaona ataniletea kizuizi huyu.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu, nikamuuaβ¦.. Yesu atanisamehe?”
Padri:”Utasamehewa.”
“Nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda
nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto wa bosi
akabisha hodi, nikawaza mambo gani tena, akasema alirudi
nyumbani na kukuta yaliyotokea akanionesha diary ya
babake, inayoonesha nilikuwa na appointment naye
wakati nilipomuua. Nikamuuliza nani mwingine anayejua?
Akasema ameanzia kwangu kisha anaenda polisi.
Nikatazama huku na huku nikakuta tuko wawili peke
yetu, nikamuuaβ¦.. Yesu atanisamehe na hilo?”
Kimyaaβ¦.
“Padri yesu atanisamehe?”
kimyaβ¦.
Jamaa akatazama kwenye confession booth padri
hayupo, lakini kwenye kona moja akaona kabati la nguo
za mapadri linatikisika. Kufungua akaona padri kajificha ndani anatetemeka huku akitokwa na jasho.
Jamaa, “Sasa baba mbona umekimbia?”
Padri kwa taabu akajibu, “Nilitazama huku na huku
nikagundua tuko wawili peke yetuβ¦β¦.”
Angalia wanachokifanya Zuzu na msichana chumbani kwenye giza
Zuzu: Mambo Anna!
Anna: Poa!
Zuzu: Kuna kitu nataka nikuonyesheβ¦
Anna: Kitu gan?
Zuzu: Twende chumbani kwako (wakaenda)
Anna: Haya nionyesheβ¦
Zuzu: Funga mlango na madirisha kwanza (akafunga)
Anna: Haya nionyeshe sasa!..
Zuzu: Zima taa kwanza (akazima)
Anna: Mhmβ¦nionyeshe sasa!
Zuzu: Haya njoo hapa kitandaniβ¦
Anna: Ok, nionyeshe!
Zuzu: Ona nimenunua saa ambayo inawaka yenyewe gizani⦠Acha mawazo mabaya ww???
Mzee wa kichaga na hela zake. Angalia anachofanya
Mzee moja alikuwa kila usiku anapita mbele ya bank anasimama,kisha anapiga honi,akitoka askari mlinzi,anaondoka.Hilo jambo likamkera sana askari mlinzi, askari akawa na mvizia yule mzee wa kichaga ,siku alipokuja tena akamkamata, akamuuliza kwa nini unakuja unapiga honi kisha unakimbia? Mzee akasema: Haki ya mungu babaangu , Nina pesa zangu ktk account hapa bank naogopa usilale usingizi ndo maana kila siku usiku napita kukuangalia kama umelala!!
ππππππ
Maujanja ya kumkalisha mwanamme wako nyumbani weekend haya hapa
Siku hizi wa naume licha ya kukimbia nyumba zao kwa kisingizio cha kazi maajabu weekend hasa Jumamosi utasikia wanaaga nafika hapo njiani naja naenda kununua gazeti.
Kumbe wanaenda kunywa supu unasubiri wee mpaka alasiri au jioni
Hivyo wanandoa wengi hili limekuwa tatizo mwanaume kiguu na njia asb mchana na njia kumuacha mama na watoto.
Nini kifanyike hasa weekenda Mwanaume ashinde NYUMBANI akikupumzikia??
Zipo njia nyingi mojawapo SUPU YA WEEKEND NA MAZUNGUMZO NA MKAO
Ni kweli wanawake wengi hamjuagi kuwakalisha waume home.
Anza hivi
Siku uko home wewe amka mapema kabla yake anza makeke jikoniβ¦
Mara blenda priiiiiβ¦ juiceβ¦ ama milk shakeβ¦. hahahaha..Utaona anasogea jikoni..
Wakati anakunywa juice ama milk shakeβ¦Anza kukuna naziβ¦
Chambua mnafuβ¦
Hapo jikoni kuna kanyama kanachemka⦠katia kitunguu tupia viazi 2 na ndizi.Hahaha..
ile harufu ikianza kutoka utasikia anafuata maji jikoni⦠hahahaha kwenye friji⦠wala hatumi..
Hahaahha⦠utasikia nini kiko jikoni?Hahahaa.
Mmiminie supuβ¦
Na ndizi mbili na kiazi kimoja kapilipili mbuzi pembeni..
Muulize kuna chapatiβ¦Mpe.. hahahahaha..Akimaliza supu nakuapia atasinzia..
.Akishtuka ugali na mnafu na nyama umeivaβ¦Mpe ale..Mshushie na glass ya mtindiβ¦Hahahaha..
analewa full Hata kama kuna mama junior anaambiwa usipigeβ¦
Hahahahahahaβ¦.Baada ya hapo acha apumzikeβ¦ aogeβ¦
Kisha funga ka khanga kako kepesi jilaze pembeni.. woiiiiiiiii..
Mkimaliza muombe pesa ya sokoniβ¦
NAKUAPIA HATA KAMA JANA YAKE ALIKUPA ATAKUPA TENA.
Hahahahaha.. jamaniβ¦
Hahahahaha⦠yani kwa raha ya supu⦠nakuapia utaambiwa hata mama alipiga simu jana⦠hahahaha.. ama utasikia mamii.. njoo uone njoo⦠unaitiwa kitu cha kwenye tv.. hahaha.
Hata hujaona mwanzo ila kwa raha yakasupu utaitwaβ¦
Hata kama huna kalio nakuambia utapigwa kibao hata cha mgongoβ¦. hahahahahahahahahaha.
Sasa wewe unaamka chai na mkate kama chuo cha uhaziliβ¦
Wali maharage kama jeshi la j
Ndoa zina mambo, cheki haya mambo ya mtu na mke wake
Mke: mume wangu leo 2badilishe stail kwani nimechoka kla siku hiyo hiyo tu
Mme: kwel mke wang hata mimi nilikuwa nataka nikuambie hivyo hivyo
Mke: sasa stail ya leo wewe utaosha vyombo mimo nitaangalia tv
Mme: huna haya wala hujui bayaβ¦!!!
we unadhani ni xtail gani mume aldhani???
Angalia huyu Jamaa alichomfanyia mke wake jana
Jana niligombana na mke wng, Akaniambia nibebe kila kitu changu niondoke, Bas kiustaarabu tu nikachukua nguo zangu,mwishoni nikambeba na yeye nikamuweka begani nikaanza kuondoka nae
hua sipendagi ujinga, amesahau na yeye pia ni wangu
Baada ya kuumizwa kimapenzi haya ndiyo maneno
Mkishaumizwa ndo utasikia, Moyo sukuma damu sio mengine. wakati mnapenda mlizani moyo ulikuwa unasukuma kinyesi!!!!!??????ππππ
Kilichotokea baada ya kumdanganya mchungaji wangu
Jumapili baada ya kutoka KANISANI, Pastor akaona simu yangu niliyonunua LAKI 5,akaniuliza hiyo simu umenunua Bei gani?
Kwakuwa natoaga sadaka kidogo,na ZAKA ndo sijawahi kutoa,Nikamjibu nimenunua JANA,ELFU 50, akanipa LAKI MOJA,nikanunue mbili,yake na ya mke wake. Sa najaribu kumuuliza Mungu,kwanini kaamua kuniadhibu mbele ya mchungaji bila hata kunionya!
Muda mzuri wa kulipa mahari
Amini Nawaambieni
Hakuna Muda Mzuri wa Kulipa Mahari Kama Mwezi January. Baba Mkwe Anapokea Hata Buku Kumiβ¦. ππππππ
Sababu ya girlfriend π§ kuniblock
Nimeblockiwa bila kosa X Girlfriend From no where kanitext eti Hi; Vp na huko kwenu mvua inanyesha β¦Nimemjibu kwani nimekutumia text ina matope?
sipendangi ujinga mimi
Angalia mchezo wa kutuma message mara zikubali mara zikatae.. Lilishakukuta hili???
GARLFREND»»hellow sweetheart
BOYFREND»»hellow darling(SENDING FAILED)
GARLFREND»»kwanin hutaki kujibu sms yangu,au huna mda»??
BOYFRENDΒ»>najitahid kukujibu lakin mtandao unasumbua,imefika??(SENDING FAILED)
GARLFREND»»kama hunipend bhas usinijbu,kama unanipenda kwel bhas nijibu
BOYFREND»»i love you (SENDING FAILED)
GALFREND»»do you lov me????
BOYFREND»»i lov you baby(SENDING FAILED)
GARLFREND»»usiongee na mimi tenaaaaa
BOYFREND»»i love you sweetieeee(SENDING FAILED)
GARLFREND»»unataka mim na wew tuachaneee????
BOYFREND»»nshachoka mie na huu upUmbavu,shenz (MESSAGE SENT)
πππππππππππππππππππππππππππ
Misemo 10 bora ya kuchekesha itakayokuacha mdomo wazi
1. Mwanaume hata awe bahili vipi, hawezi kumpa mwanamke mimba nusu.
2. Hata uwe na magari mangapi chooni utaenda kwa miguu.
3. Kama ubinadamu kazi mbona hatupewi mishahara?
4. Ukichanganya wali na choroko unapata mseto, lakini hautibu malaria.
5. Hata njiwa nae ana makinda, lakini hawezi kuwa spika wa Bunge.
6. Hata uwe na haraka vipi kwenda Zenj, huwezi kupanda Jahazi ya Yusuph Mzee.
7. Umeme hauna kiuno lakini unaongoza kwa kukatika.
8. Hata uwe kauzu vipi, huwezi kujamba wakati unatongoza.
9. Hata uwe na imani kali vipi, huwezi kusali wakati unafanya mapenzi.
10. Hata kizibo ni mfuniko lakini hauwezi
kufunika sufuria.
Huyu Jamaa bwana! Cheki anavyojibu sasa
*Mdukuzi:* _halloo massai unasemaj_
*Massai:* _safi rafiki_
*Mdukuzi:* _nikikuuliza swali unaakili ya kujibu?_
*Massai:* _ulisa acha maneno yako._
*Mdukuzi:* _nitajie wanyama kumi wa porini_
*Massai:* _swala watatu na tembo saba_ππππππππΏ
Sipendi ujinga. Cheki nilichokifanya
Nimeingia chumban nikakuta panya wamekula dawa yangu ya minyoo,
Na mimi nimechukua yakwao nikanywa.
Sipendagi ujinga mm!!
πππ
Angalia kilichompata huyu mwanafunzi kilaza anayejiamini
Teacher: Who is a pharmacist?
Shemdoe raised up his hand.
Teacher: So itβs only Shemdoe that can tell who a pharmacist is in this class? So there is no body else to answer the question except Shemdoe? (There was no reply from the students)
Teacher: Ok now Shemdoe, chukua hii fimbo, charaza vilaza hawa wote kila mmoja viboko kumiβ¦. Shemdoe akiwa amevimba kichwa, akawatwanga viboko kumi kumi vya kushiba darasa nzima
Teacher: Now, my dear Shemdoe tell this dumb students who a pharmacist isβ¦
Shemdoe: Yes, sir. A Pharmacist is a farmer who assists people. Shemdoe saiv amelazwa MOI kwa wataalam wa mifupa π
Duh, huyu mama alichokifanya
Mke:Β Naelekea london, nikuletee zawadi gani?
Mume:Β kitu gani unaweza niletea wewe?
Mke:Β we omba Alafu utaona.
Mume:Β Niletee msichana wa kizungu.
Mke:Β (mke akaendaLondon na kurudi)
Mume:Β zawadi yangu iko wapi?
Mke: Subiri ndani ya miezi 9!!!! ππππππππ
Pia Wamama hawapendi ujinga
Hizi sifa zimezidi sasa
MADEM KWA SIFA..
kuumwa aumwe yeye lakn kujifanya anajali sana bas utamsikiaΒ BABY KARIBU TUMEZE DAWAΒ πππ
Ni wazo tuu!
Siyo watu wote wanaokuuliza kwamba watoto hawajambo,wanakuuliza kwa nia nzuri,wengine wanaulizia watoto wao waliozaa na mkeo.duh!! tutafika kwel
πππππππ
Mjini shule. Soma hii
Kuna mdada nilimkopesha pesa kwa ahadi kuwa baada ya wiki moja atanirejeshea pesa zangu.
Baada ya wiki moja nampigia simu hapokei simu zangu, nimempigia zaidi ya mara kumi (10) bila ya mafanikio!
Kila nikimpigia simu hajibu simu zangu, nikahamua kumwandikia message kwa WhatsAppβ¦!
_Hello Mamu, Nakupigia simu sio kukudai pesa zangu, ila nataka kukwambia kuwa hapa Ubungo Plaza kuna wadada wawili walikuwa wanapigana kumgombea Mumeo (Baba Nang’oto). Ilikuwa vuta nikuvute na mumeo alikuwa kasimama tu anawaangalia akitabasamu. Baada ugomvi kwisha akaondoka na mmoja wao na kumwacha yule mwingine akitukana matusi kama ana akili nzuri._
β
_*Kisha nikaituma ile message*_
Baada ya dakika kama mbili hivi, akanipigia simu nami wala sikupokea simu yake⦠Akapiga tena na tena kama mara ishirini hivi wala sikupokea.
*Akatuma message akiniulizaβ¦*
_Hao wanawake unawajuwa, β¦mume wangu na huyo mwanamke wameelekea wapi, wewe unawajuwa hao wanawake waliopigana, yaani hapa nimechanganyikiwa kwa kweliβ¦!_
Nikaisoma message yake wala sikuijibu, nikamchunia kimyaaaβ¦!
Akanipigia tena simu mara tano, sikupokea simu zake, kimyaaaβ¦! Akaniandikia message nyingineβ¦.
*β¦Nakupigia jamani pokea simu basi nina pesa zako nataka nikupeβ¦ Naomba basi tukutane mjini unihadithie vizuriβ¦!*
Nami nikamjibuβ¦
_Nitumie hizo pesa kwenye Namba yangu ya Mpesa, ili nipitie sheli kujaza mafuta nije mjini kukupitia nikupeleke mahala walipoβ¦!_
Baada ya dakika 2 message ikaingia, kuangalia balance yangu ya Mpesa, nikakuta kaingiza pesa zangu zote ninazo mdaiβ¦!
Nikazima simu nikajilalia zangu kimyaaaβ¦. Kama sio mie!









I’m so happy you’re here! π₯³




































































Recent Comments