Vituko Vya Wasichana Na Wavulana
Huyu jamaa kawaweza wapenda vya bure
Jamaa kaingia mgahawani kwa fujo
JAMAA :ย Nipe soda moja na kila mtu mpe yake maana ninapokunywa soda napenda kila mtu anywe
WATU :ย Ha! Ha! Ha! Haaaa!
JAMAA :ย Nipe mchemsho na kila mtu mpe wa kwake maana ninapokula mchemsho napenda kila mtu ale wake
WATU:ย Watu weweeee! Tena safari hii Na makofi juu..
JAMAA :ย Mhudumu, nipe bili na kila mtu mpe yake maana ninapolipa bili napenda kuona kila mtu analipa yake
๐๐๐๐๐๐๐
Angalia kilichompata huyu mwanafunzi kilaza anayejiamini
Teacher: Who is a pharmacist?
Shemdoe raised up his hand.
Teacher: So itโs only Shemdoe that can tell who a pharmacist is in this class? So there is no body else to answer the question except Shemdoe? (There was no reply from the students)
Teacher: Ok now Shemdoe, chukua hii fimbo, charaza vilaza hawa wote kila mmoja viboko kumiโฆ. Shemdoe akiwa amevimba kichwa, akawatwanga viboko kumi kumi vya kushiba darasa nzima
Teacher: Now, my dear Shemdoe tell this dumb students who a pharmacist isโฆ
Shemdoe: Yes, sir. A Pharmacist is a farmer who assists people. Shemdoe saiv amelazwa MOI kwa wataalam wa mifupa ๐
Walevi wana Mambo! Angalia wanachokisema
WALEVI WAWILI KATIKA MAZUNGUMZO YAO
MLEVI 1ย hivi rafiki yangu china ni mbali kweli
MLEVI 2ย sidhani mbona pale kazin kuna mchina anakuja na baiskeli
๐๐๐๐๐
Mwizi kawezwa ki kwelii
Et jana usiku mwiz kavunja mlango kwangu akaanza kutafuta kitu kila kona ikabid na mie niamke namuuliza unatafuta nini ananijibu hela ndipo nilipoanza na mie kutafuta nae maana hta hela ya kula Jana sikua nayo alichoka zaid nilipomuliza una uhakika uliweka humu? sipendagi ujinga๐ถ๐ป na kitu hela mm!
Mvua zazua kasheshe! Soma hii..
Baba- : Halloo mke wangu.. yaani ni shida sitaweza kurudi nyumban, daraja limevunjika na kutoka morogoro kurudi dar haiwezekani
MAMA:- Mme wangu morogoro ulienda bila kuniaga! ?
BABA:- Ilikuwa ni ghafla sana mke wangu sikuweza kukwambia
MAMA:- kha! Sasa watoto nani atawaangalia
BABA:- Unasemaje! We uko wapi kwan
MAMA:- Niko bagamoyo na daraja limeondolewa na maji sitaweza kurudi.
BABA:- Unasemaje we mwanamke.. nakwambia nikukute nyumban ndani ya dk 15
Baada ya dk 15 Baba kafika nyumban.
MAMA:- Haya umefkaje kutoka morogoro?
BABA:- Nimepewa lift na helkopta ya Mbowe..
Kama umeipenda shea na rfiki zakoooโฆ..
Wanawake wa leo mbele ya hela. Hii ni hatari
MDADA: Baby nikwambie kitu
MKAKA: Yeah Baby Uko huru nambie
MDADA: nilikua naomba hela babyโบ
MKAKA: WW nae kwa kupenda hela jana tu nmekupa hela Leo unaomba ya nn ๐
MDADA: hapana๐ Bby sio hivyo nlikua nataka nikashuhudie tetemeko la ardhi BUKOBA nasikia huko linaonekana vizur .
๐๐๐๐๐๐๐๐
Wanawake kumbukeni sio vizuri
Ndege ya Tanzania
Kuna maprofesa 40 walipanda AIR TANZANIA ili wasafari. Kabla ndege haijaanza kuondoka, Lilipita tangazo kama ifuatavyo:
Ndugu wasafiri wote, ndege unayotarajia kusafiri nayo imetengenezwa na wanafunzi wa Kitanzania.
Baada ya tangazo maprofesa wote waliteremka isipokuwa mmoja alibaki kwenye kiti chake
Walipomuuliza ni kwanini hakuondoka akajibu kwa haraka na furaha kuwa:
Kama ndege hii imetengenezwa na watanzania, hata kuwaka haitawaka!
Utoto raha..! Angalia hawa watoto wanachokifanya sasa
Leo nimepulizia Air Fresh yenye Harufu ya Pilau nyumbani kwangu sasa watoto wa Jirani wamehamia Mlangoni kwangu ndio wanacheza hapo. Kila nikitoka wananisalimia. Mama yao ndio kanimaliza kabisa nimetoka akaniambia
“Kumbe wewe ni Mpishi mzuri, Hongera”
Imebidi nisirudi nyumbani maana wale watoto wanaweza kuingia ndani kabisa na pilau hakuna.
#UTOTO RAHA ๐
๐๐๐๐๐๐ป๐๐ป๐๐ป
Staili nyingine za michepuko ni shida
Mtu na mkewe walikuwa bado wamelala asubuhi, mtu akapiga hodi mke akaenda kufungua mlango, si akakuta mchepuko wake,
MKE: Unataka nini we mpumbavu?
MUME: Nani huyo unamtukana?
MKE: Kuna mtu hapa anakichwa kama nenda urudi badae
MCHEPUKO:Nawewe pua kama poa
MKE:Miguu kama masaa mawili
MCHEPUKO:Masikio kama sichelewi
MKE: Ondoka hapa mjinga we. โฆโฆ Akafunga mlango
MUME: mwambie ana macho kama sitoki leo ng’oo
SIPENDI UJINGA MM nikiwa na my love pr
Kichekesho cha mtalii na mbongo
Duh! Sikubali bora mbavu zituume wote!
Watalii wana dharau sana bana, Mtalii alikodi boti akazunguka nayo kwenye mto Rufiji kuangalia mandhari, akamuuliza kijana anayeongoza boti, “Do you know Biology, Psychology and Anthropology?” Kijana akajibu “NO,” Mtalii akamwambia “nothing you know under the sun? You are useless, and u’ll die with your illiteracy!” baada ya muda boti ikaanza kuzama, kijana akamwambia mtalii “Do you know kuogelealogy and kusepalogy from mambalogy? Mtalii akajibu huku ametoa macho “No” kijana akamwambia “You will kufalogy and mambalogy wil eat your matakology because of your bad-mdomology..๐๐๐๐๐๐
Cheki hawa washikaji wanachokifanya baada ya kuvuta bangi, Bangi si mchezo
Kuna washikaji walikuwa wakivuta bangiโฆ kiberiti kikawaishiaโฆ wakamtuma mwenzao akatafute kingineโฆ bangi lilikuwa limemkoleaโฆ akazungukazunguka hatimaye akarudi palepale kijiweniโฆ
MSHIKAJI:ย oyaaa wanangu eeehโฆ niazimeni kiberiti mwanangu mwenyewe โฆ..
WENZAKE:ย baharia ee subiria kimtindo kuna mwana tumemtuma akatafute kiberiti.
Duh! Tamaa mbaya, cheki kilichompata Huyu
HAHAHAHAHAAAAAA DUH TAMAA MBAYA
Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna ki2, alipoifungua likatoka jitu la ajabu. Huku akitetemeka lile jitu likamwambia kijana asante sana kwa kuniokoa omba vi2 viwili sasa hivi. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko la hela na pete ya bahati vikadondoka. Akaambiwa ombi la pili,akasema nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada Hapohapo akageuzwa akawa chipsi yai.!!๐๐คฃ๐คฃ๐คฃ
Hizi sifa zimezidi sasa
MADEM KWA SIFA..
kuumwa aumwe yeye lakn kujifanya anajali sana bas utamsikiaย BABY KARIBU TUMEZE DAWAย ๐๐๐
Angalia hawa kina mama, ni shida..!
Mama mdaku alishangaa kila siku mchungaji anaingia nyumba ya jirani yake ambaye hana mume, akawa anajiuliza anakwenda kufanya nini? Uzalendo ukamshinda akamuuliza “Mwenzangu, mbona kila siku mchungaji anakuja kwako, vipi anakuja kukuombea?” Akajibiwa “Nyoo, umbea tu! Mbona kwako kila siku anakuja mwanajeshi kuna vita! chefuuuu ๐ณ๐ณ๐ณ๐ณ๐ณ
๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Safari ni safari
FUNDISHO : SAFARI NI SAFARI
Maisha ni ya ajabu sana, wakati mwingine maisha ni mazuri na mwingine ni mabaya, katika maisha yetu tumeshapitia safari nyingi sana na za aina mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Lakin kiukweli kila safari ni safari tuu.
Japokua kila safari ina changamoto zake lakini mwisho wake ni ule ule , kila safari ina uzuri na upekee wake.
Vile vile kila safari ina ubaya wake, kwa mfano kila safari ina gharama yake kulingana na upekee wake.
Usiwe na wasiwasi na mashaka na aina ya safari ulionayo, jipe moyo utaimaliza na kupata ulichokitarajia. Haya ndio maisha na wote tunatakiwa tuyafurahie.
Ingawa kila mtu ana safari yake bado wote tunatakiwa tufurahie pamoja kwa safari tuliyo nayo. Hata Uwe Na safar ya aina gani wewe furahi tuu. Hii ni kwa sababu safari mwisho wake ni mmoja kwa wote burudani ni ile ile
Safari๐บ ni safari ๐บhata kama ni ya chupa au ya kopo mwisho wake ๐ค๐ค
๐๐๐๐๐๐
Ulijua ni nn??
Huyu mtoto kaongea point kweli, angalia anachomwambia baba yake
Mtoto alimwuuliza baba yake,
Mtoto: Baba unaweza kumwachia hilo gari lako house boy/girl akaliendesha?
Baba: siwezi kumwachia gari langu hili aliendeshe ni ghali sana.
Mtoto: je mnaweza kumwachia chumba chenu house boy/girl kikiwa wazi na mkaenda kazini?
Baba: haiwezekani kamwe kuna vitu vya gharama na pia heshima haitakuwepo.
Mtoto: unaweza ukampa house boy/girl ATM CARD yako na namba ya siri ukakuchulie pesa?
Baba: mtoto unatafuta balaa sasa, unataka siku akiiba hii card akachukue pesa zote tuwe maskini, sithubutu.
Mtoto: aahaaaaaa, kumbe hauwezi kumkabidhi chochote chenye thamani house boy/ girl, sasa kwa nini mnanikabidhi mimi kwa house boy/girl na nyie mnaenda kazini mpaka mnarudi kumbe mimi sina thamani kwenu eeeeh!
Mjini shule. Soma hii
Kuna mdada nilimkopesha pesa kwa ahadi kuwa baada ya wiki moja atanirejeshea pesa zangu.
Baada ya wiki moja nampigia simu hapokei simu zangu, nimempigia zaidi ya mara kumi (10) bila ya mafanikio!
Kila nikimpigia simu hajibu simu zangu, nikahamua kumwandikia message kwa WhatsAppโฆ!
_Hello Mamu, Nakupigia simu sio kukudai pesa zangu, ila nataka kukwambia kuwa hapa Ubungo Plaza kuna wadada wawili walikuwa wanapigana kumgombea Mumeo (Baba Nang’oto). Ilikuwa vuta nikuvute na mumeo alikuwa kasimama tu anawaangalia akitabasamu. Baada ugomvi kwisha akaondoka na mmoja wao na kumwacha yule mwingine akitukana matusi kama ana akili nzuri._
โ
_*Kisha nikaituma ile message*_
Baada ya dakika kama mbili hivi, akanipigia simu nami wala sikupokea simu yakeโฆ Akapiga tena na tena kama mara ishirini hivi wala sikupokea.
*Akatuma message akiniulizaโฆ*
_Hao wanawake unawajuwa, โฆmume wangu na huyo mwanamke wameelekea wapi, wewe unawajuwa hao wanawake waliopigana, yaani hapa nimechanganyikiwa kwa kweliโฆ!_
Nikaisoma message yake wala sikuijibu, nikamchunia kimyaaaโฆ!
Akanipigia tena simu mara tano, sikupokea simu zake, kimyaaaโฆ! Akaniandikia message nyingineโฆ.
*โฆNakupigia jamani pokea simu basi nina pesa zako nataka nikupeโฆ Naomba basi tukutane mjini unihadithie vizuriโฆ!*
Nami nikamjibuโฆ
_Nitumie hizo pesa kwenye Namba yangu ya Mpesa, ili nipitie sheli kujaza mafuta nije mjini kukupitia nikupeleke mahala walipoโฆ!_
Baada ya dakika 2 message ikaingia, kuangalia balance yangu ya Mpesa, nikakuta kaingiza pesa zangu zote ninazo mdaiโฆ!
Nikazima simu nikajilalia zangu kimyaaaโฆ. Kama sio mie!
Njia 3 rahisi za kuondoa kitambi
JE, una KITAMBI na unataka kukiondoa?
FANYA HAYA;
1. Kopa mkopo mkubwa benki
2. Nunua gari bovu la biashara
3.Oana na mke mwenye kelele.
Ukiona miezi mitatu hakijaisha basi ujue umevimba BANDAMA sio kitambi..
Mambo makuu matatu waafrika tusiyoyajua
NIMEKAA NIKAWAZA ๐๐ผ KUWA KUNA MAMBO KAMA MATATU HIVI๐๐ป WAAFRIKA HATUYAJUI ๐
KAMA TUNGEKUWA TUNAYAJUA HATA HAWA WAMAREKANI,๐บ๐ธWACHINA๐ฏ๐ต NA HATA WATU WA ULAYA TUNGEKUWA๐ฝ๐ช TUNAWAPITA KIMAENDELEO
MAMBO YENYEWE,,
HATA MIMI SIYAJUI MAANA NA MIMI NI MWAFRIKA ๐๐๐๐
Recent Comments