Vituko Vya Jumamosi
Maajabu ya wananchi wa Tanzania, Je, wajua hili?
JE WAJUA TANZANIA NI NCHI PEKEE AMBAYO WATU WANAPOANZA KUCHAT huanza kwa kiingereza ‘morning’ na hupiga stor zote kwa kiswahil mwishon humalizia tena kwa kiingereza ‘ g9t
Wasichana wafupi wanafurahisha
Wasichana wafupi wananifurahisha sana…. Yaan siku ya Valentine, wakivaa magauni mekundu huwa wanakuwa kama Fire extinguishers au mitungi ya Oryx 😁😁😁😁😀
Hii dunia kweli haina haki, soma hii
Unapiga kilimo chako unamsomesha girlfriend anafika chuo anakutana na msomi mwenzake anarudi anakwambia unanidai shilingi ngapi..,,?
Hapo ndo utatambua kwann kinyesi hakina mwiba ila ukikanyaga lazima uchechemee..😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂💤
Tofauti ya mchaga na mhaya wakipata kazi
Mchaga hata apate kazi bank bado atasema yupo kibaruani.
Acha sasa mhaya apate kazi katka mashine ya kusaga na kukoboa; utaskia i work as a crucial engineer in a monocotyledon finalizing company
😂😂😂
Ukata wa January
Boss;- kwa nini umechelewa kazini
Juma;- kuna mtu njiani alidondosha elfu1
Boss;- ohhoh kwa hiyo ulikuwaunamsaidia kuitafuta
Juma;- hapana nilikuwa nimeikanyaga
😃😃😃😃😃😃😃😂😂😂😂😂😂😂
Kilichotokea baada ya bibi na babu kukumbukia mahaba ya ujanani
Mzee wa miaka 60 alimwambia mkewe, leo nataka tukumbukie enzi zetu kutongozana, mke akajibu sawa, inabidi unisubiri mwembeni saa 1 usiku nitapita, mzee akafika saa 1 alikaa hadi saa 5 usiku, aliporudi nyumbani akamuuliza mkewe kwa hasira; sasa tumepanga nin halafu haujatokea ?
Mke; leo mama alinikataza nictoke nyumbani usiku nijisomee ! Babu hoii…
Ukimuona mbwa kwenye harusi hii ndiyo maana yake
Hili nalo neneo.
Ukimuona mbwa🐶 harusini usimpige mawe wala kumfukuza inawezekana kilichomleta pale ndicho kilichokupeleka na wewe hapo
Cheka kidogo na wewe hapa
*Kama mtaani kwenu mambo yamekuwa tait , usikimbilie mtaani kwetu kwani huku yamekuwa dera kabisa*😂😂😂😂😂
Jana nilipeleka viatu kwa fundi sasa hivi nimekutana nae amevivaa namuuliza ananiambia eti ni ROAD TEST” 😂😂😁
Cheki hiki kibabu kulivyowaacha watu hoi wakati mchungaji anafungisha ndoa
Mchungaji Kauliza: Yeyote mwenye pingamizi la haki kwa ndoa hii asimame na aje mbele.
Mara kasimama kibabu na kwenda mbele, bibi harusi alipomuona tu yule babu akazimia.
Mchungaji akauliza: tueleze pingamizi lako
Kibabu kikajibu: Nimeamua kuja mbele kwasababu kule nyuma sisikii!!!.
kanisa zima hoi,
Cheki kilichompata huyu dada!!
NDOA inafungwa KANISANI Mchungaji akauliza-Yeyote mwenye Pingamizi La Ndoa hii kufungwa aje Mbele, +++ KIBABU kikasimama na kwenda Mbele,
Bi harusi akaanguka na akazimia ghafla!😭😭😭
Mchungaji- Tuambie Babu Pingamizi Lako!
Babu-Nimeamua kuja mbele,kule nyuma sisikii vizuri! watu hoiiii!!
hata mimi hoi…😃😃😃😃😃😃😃
Ameniomba nimfungulie akaunt facebook cheki nilichomjibu
Leo nimechoka zangu alafu shangazi amekuja anataka nimuunganishe facebook. Imebidi nimwambie
lazima awe na picha passport size 4 kwaajili ya kuweka profile picture, barua kutoka kwa afisa mtendaji na Atm card ya nmb bank. Alafu awe na marefa wanne ambao wamekuwa facebook for more than 3 years. Amesema
hataki tena kujiunga fb!
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Saa ivi niko zangu nimelala naendelea kupunguza uchovu
Eti kwa nini Watu hawapostigi hii? Hata selfie sijaonaga
Vijana mkiwa mnaendesha magari mna post mukiwa mpo beach mna post mkiwa kwenye masherehe mna post Lakin mkiwa mmeenda kwa mganga siwaoni kupost mitunguli na vibuyu vya mganga unakuwa je wa zee tena. 😀😀😀😀
Analia kilichompata huyu jamaa baada ya kubadili jinsia yake kichawi
Jamaa alimpa ujauzito mwanafunzi akashtakiwa kumbe yule jamaa ana bibi yake mtaalam wamambo yetu ya Jadi…
Jamaa akaongea na bibi yake amuwekee jinsia ya kike ili akashinde Mahakamani na akitoka arudishiwe mambo yake kama kawaida.
Bibi akampachika jamaa jinsia ya kike alipofika mahakamani kuhojiwa akasema mi sijampa ujauzito kwasababu minina jinsia ya kike pia…!
Kwa kuthibitisha akajifunua nguo, basi jamaa akashinda kesi.
Jamaa akawa anarudi Home, lakini wakati anakaribia kufika akaona watu wengi wamejaa home wanalia akauliza kulikoni akaambiwa “Bibi amefariki”!
Vuta picha hapo…!!!
Dongo kwako kama una degree moja Halafu unachagua kazi
Mtu una degree 1 unachagua kazi! Wakati thermometer ina degree 100, inafanya kazi kwenye kwapa.
😃😄😆😆😆
Ni Utani tuuuuu!
Kilichowakuta boss, mke wake na mfanyakazi wao
Bakari ni house boy mara nyingi huiba wine ya boss wake na kisha kuongeza maji kwenye chupa ili boss asigundue.
Mara kadhaa boss alihisi ladha tofauti anapokunywa wine hivyo kuhisi kuna mchezo mchafu alihisi tu Bakari anahusika.
Ilikua ni bahati tu alimvizia na
kumbamba Bakari akichakachua wine, kwa kuwa mkewe alikua
anamtetea Bakari, ili kumthibitishia mkewe kuwa Bakari ndo culprit, boss alianza kwa kumuuliza Bakari maswali.
Siku hiyo Bakari alikua jikoni, boss na mkewe walikua sebuleni.
Boss: Bakariiii!
Bakari: Naam baba!
Boss: nani anakunywa wine yangu?
Bakari kimyaaaa hajibu kitu!
Boss: Bakariiiii !
Bakari: naam baba!
Boss: nauliza nani anakunywa wine yangu halafu anajazia majiii!
Bakari kimyaaaaa!
Boss akaamua amfuate hukohuko jikoni.
Boss: Kwanini nikikuita unaitikia, nikikuuliza unanyamaza?
Bakari: baba huku jikoni ndo kulivyo, unasikia jina tu likiitwa lakini maneno menginehusikii, na kama huamini baki jikoni mi niende sebuleni.
Bakari akaenda sebuleni akaanza kuita.
Bakari:Babaa!
Boss: naam Bakari!
Bakari: Saa sita usiku huwa unaenda kufanya nini chumba cha house girl?
Boss kimyaaaa!
Bakari: Baba babaa!
Boss:ndio Bakari!
Bakari: Nauliza hivii, chumbani kwa house girl saa sita za usiku huwa wafuata nini?
Boss kimyaaaaaaa!
Boss akatoka nje: Bakari huku jikoni ni kweli husikii kitu zaidi ya jina!
Mke wa Boss akaingilia kati
Mama: nyie msinitanie kabisa mnasemaje?
Bakari: kweli mama ukiwa jikoni husikii kitu nenda uone
Mama akaenda na Bakari akaanza
Bakari: mamaaaa!
Mama: abeee!
Bakari: hebu niambie hiyo mimba ni ya baba au yangu?
Mama kimya
Bakari: mamaaaa!
Mama: abeeee!
Bakari: hebu niambie ukweli hiyo mimba ni ya baba au yangu??
Mama kimya
Mama akatoka nje: kweli humu jikoni kuna tatizo nilikuwa nasikia jina tu
Mshahara usiobadilika
PAMOJA NA HALI NGUMU YA UCHUMI NCHINI HUWEZI AMINI MSHAHARA WA DHAMBI HAUJABADILIKA HATA KIDOGO…BADO NI MAUTI VILEVILE
😊😊😊😊
Kichekesho cha mwalimu na wanafunzi
Mtoto: Mwalimu mimi nataka nisome darasa la nne kwani hili la3 halinifai.
Mwalimu: Kwa nini unasema hivyo?
Mtoto: Nina akili…
Basi mwalimu akamueleza mkuu wa shule na mkuu kaitisha interview kwa dogo. Maswali ni haya….
Mwalimu: Kwenye ndege kuna matofali 20 tukitoa moja tukalidondosha chini yatabaki mangapi?
Dogo: Yatabaki 19.
Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka tembo kwenye friji.
Dogo: Unafungua friji unamuweka tembo kisha unafunga.
Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka nyani kwenye friji.
Dogo: Unafungua friji unamtoa tembo ulemuweka..unamueka nyani kisha unafunga friji.
Mwalimu: Kuna sherehe ya siku ya kuzaliwa kwa simba, wanyama wote wameenda kasoro mmoja. Ni nani na kwa nini?
Dogo: Ni nyani kwa sababu tumemuweka kwenye friji.
Mwalimu: Bibi kizee amevuka mto unaokuwaga na mamba na viboko wakali, aliwezaje?
Dogo: Aliweza kwani mamba na viboko nao walienda kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa simba.
Mwalimu: Ingawa bibi kizee alivuka mto, baadae alikufa. Unadhani ni kwanini alikufa?
Dogo: Alidondokewa na lile tofali tulotoa kwenye ndege na kutupa chini.
Mwalimu mkuu: Huyu dogo akasome chuo kikuu….
😆😆😆😆😆😆😆😆
Angalia kilichonikuta nilipoenda kwa mganga
Usije ukaenda kwa mganga, mwenzako yamenikuta, yani masharti niliyopewa, acha tu,
yalikua hivi:-
1.Jasho la nyoka.
2.Manyoya ya mende.
3.Sisimizi Shoga.
4.Mbwa mjane.
5.Kuku aliye single.
6.Samaki mwenye miaka miwili bila kuoga
7.Mti wenye ujauzito.
8.Mbavu za Nzi.
9.Nywele za Kiroboto.
10.Mwanya wa Mbu.
Duuh..!! mwanangu kwa hali hii mbona itakula kwako.
Wengine wanasemaga
IGA UFE! Rizik anagawa Mungu tu shetan simuelew!
Recent Comments