Vihoja Vya Juma Hili
Kilichotokea baada ya kichaa kumfumania mke wake na mwanamme mwingine
Jay akaruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospital ya Vichaa, akapakiwa ktk ambulance hadi karibu na nyumbani kwake, akaulizwa unapakumbuka? akajibu ndio nyumba yangu ileee, mara wakatoka watoto wawili wamevaa uniform akasema watoto wangu walee wanakwenda shule.. akatoka mwanamke akasema na mke wangu yulee, ghafla akatoka mwanaume Jay akasema na mimi yule naenda kazini. hivi Jay kweli kapona?
Tabia za Kimama kwa wanaume
1, mwanaume kuoga haraka haraka ili uwahi kuangalia igizo, huo ni UMAMA..😂
2, mwanaume kupiga picha umeng’ata Lips na Unapiga na Camera Beauty Plus huo ni UMAMA..😂
3, Mwanaume kuangalia tamthilia na Jamai Raja na Maigizo kwenye chanel ya sinema zetu wakati mechi za kombe la dunia zinaendelea, pia nawe ni MMAMAA…😂😂
4, Mwanaume kuandika ‘Jomon’ badala ya Jamani, kuandika ‘Pw’ badala ya Poa, kuandika ‘Thatha’ badala ya Sasa, kumwandikia mwanaume mwenzio ‘Mambo my’ Huu ni UDADA, tena UDADA wa CHUO..😂
.
5, Mwanaume kunywa soda au Juice na kubakisha, kununua chakula halafu unakibakisha, kubagua bagua chakula na kujamba hovyo hovyo baada ya kushiba, huo nao ni UMAMAA..😂
.
6, Mwanaume kumuuliza mwanaume mwenzio anapata faida gani kuangalia Mpira, pia nawe ni MMAMA…
.
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Watu wana vimaneno
Eti linalo jamba ni tumbo makalio ni spika tu
Dah!!
Nimecheka hadi basi leo
😸😸😹😹
Kuwa na mahusiano na msichana kama huyu ni changamoto, Mabinti bwana!
Binti: Hallow mpenzi, Mambo
Jamaa: Poa baby
Binti:Uko wapi?
Jamaa: Niko town napata lunch
Binti: Wow unarudi saa ngap? Nina njaa dear naomba uniletee msosi
Jamaa: Narudi baada ya nusu saa nikuletee nini?
Binti: Niletee chipsi kuku, soseji, mayai manne ya kukaangwa pembeni, baga, piza, coke take away baridi, mkate wa moto kwenye ile bekari ya wapemba na maji ya kunywa ya kiimanjaro.
Jamaa:Umesahau viti, meza, masufuria, sahani na beseni na vijiko.
Binti: Kwanini dear?
Jamaa: Naona hutaki kula unataka kufungua hoteli!
Breaking news
Breaking news 💥
Watu wasiojulikana wamevamia jengo lisilojulikana na
Kufanya tukio lisilo julikana na kukimbilia🏃🏿 kusiko julikana na mpaka sasa hakuna kinachojulikana na mimi sijui ninachosema 😕😕
Google, Facebook, WhatsApp, Internet na Umeme nani zaidi?
Google alisema : mimi nina kila kitu
Facebook ikasema : mimi najua watu wote
Whatsapp akasema : mimi napendwa zaidi kuliko nyinyi
Internet akasema : hahahaha nyinyi nyote bila mimi si kitu !
umeme ukatamka : mutabadilisha topic au niwaonyeshe😂😂😂😂😂
Wanaume wote ni waaminifu
Hii ni kwa wanaume ila mwanamke anaweza kusoma na kujifunza kuwa wanaume wote ni waaminifu.
Mwanaume mmoja alienda kukata miti kwa ajili ya mkaa, bahati mbaya panga likadondokea mtoni, akaanza kulia sana. Malaika akatokea na kumuuliza kwanini analia. Jamaa akajibu; “Panga langu limedondokea mtoni na ndilo ninalotegemea kuendeshea maisha yangu”.
Malaika akazama mtoni na kuibika na panga la DHAHABU na kumuuliza, ndio hili?
Jamaa: Hapana.
Malaika akazama tena na kuibuka na panga la SHABA na kuuliza, ndio hili?
Jamaa: Hapana.
Malaika akazama tena mara hii akaibuka na panga la CHUMA na kuuliza ndio hili?
Jamaa: NDIYO.
Malaika akafurahishwa sana na uaminifu wake hivyo akampa mapanga yote matatu. Jamaa akafurahi sana.
Siku nyingine jamaa alikuwa anatembea na mkewe njiani ghafla mke akadondokea mtoni, jamaa akaanza kulia. Malaika akatokea na kumuuliza: Kwanini unalia?
Jamaa: Mke wangu kadondokea mtoni na nampenda sana.
Malaika akazama mtoni akaibuka na WEMA SEPETU na kuuliza; “huyu ndiye mkeo?”
Jamaa: NDIYO.
Malaika akakasirika sana na kumuuliza: kwa nini umenidanganya?
Jamaa: Nimesema ndiyo kwa sababu ningesema hapana ungezama tena na kuibuka na AUNT EZEKIEL na ningesema hapana tena ungezama na kuibuka na MKE wangu alafu ningesema ndiyo ungenipa wote watatu!
Sasa mimi maskini sina uwezo wa kuhudumia wote hao, ndio maana nikasema NDIYO kwa Wema Sepetu.
*FUNDISHO*
Wanaume huwa hatusemi uongo bila sababu na inakuwa sababu maalumu kwa faida ya wote.
WANAUME WOTE NI WAAMINIFU. Hii ndiyo kauli mbiu yetu.
😀😀😀😀
Askari na yeye kumbe muoga, cheki anachomjibu afande
Askari wametumwa nyumba iliyokuwa kuna ugomvi wakafika wakatakiwa kuripoti kwa njia ya simu juu ya walichokikuta
ASKARI: Mkuu tumekuta mama mwenye nyumba kampiga mumewe chuma cha kichwa na kumuumiza vibaya sanaa
AFANDE: Kha! kisa mkasa mpk akafanya hivyo
ASKARI: Mama mwenye nyumba alikua anapiga deki mumewe akaingia ndani viatu kabla sakafu haijakauka
AFANDE: Sasa mmesha mkamata huyo mwanamke
ASKARI: Bado mkuu
AFANDE: Kha! sasa mnangoja nini
ASKARI: Si tunangoja sakafu ikauke
Hii bahati mbaya hii haifai kusema Samahani
(KIFO NI NIN)
KIFO ni pale unapokosea text na kumtumia
BABA yako kipindi mnakula
“hello Mrembo”😁😁
Kama utazubutu kusema Samahani 😁
Kilichotokea baada ya jambazi kuvamia kanisa
Jambazi mmoja aliingia kanisani na bunduki akapiga risasi juu ya bati akasema “asiyempenda YESU atoke nje” wakatoka wote ispokuwa Mchungaji na Wazee wawili.
Jambazi likamwambia Mchungaji “unaweza kuendelea na ibada, nilikuwa nakuondolea wanafiki”, Mchungaji akasema “ungewaacha kwanza nichukue sadaka…!
Tofauti ya mchaga na mhaya wakipata kazi
Mchaga hata apate kazi bank bado atasema yupo kibaruani.
Acha sasa mhaya apate kazi katka mashine ya kusaga na kukoboa; utaskia i work as a crucial engineer in a monocotyledon finalizing company
😂😂😂
Angalia kilichonikuta nilipoenda kwa mganga
Usije ukaenda kwa mganga, mwenzako yamenikuta, yani masharti niliyopewa, acha tu,
yalikua hivi:-
1.Jasho la nyoka.
2.Manyoya ya mende.
3.Sisimizi Shoga.
4.Mbwa mjane.
5.Kuku aliye single.
6.Samaki mwenye miaka miwili bila kuoga
7.Mti wenye ujauzito.
8.Mbavu za Nzi.
9.Nywele za Kiroboto.
10.Mwanya wa Mbu.
Duuh..!! mwanangu kwa hali hii mbona itakula kwako.
Wengine wanasemaga
IGA UFE! Rizik anagawa Mungu tu shetan simuelew!
Amri za chuo
Ndio hizi sasa
1.Hicho ndicho chuo chako usiwe na chuo kingine ila hicho.
2.Usilitaje bure jna la chuo chako mana utawaumiza wengine.
3.Ikumbuke cku uliyochaguliwa na kuiheshimu.
4.Waheshimu tcu, bodi ya mkopo na uongoz wa chuo ili upate kuendelea kuwepo chuon.
5.Usisapu
6.Usidisko
7.Usitumie mkopo ovyo.
8.Usitaman chuo cha mwenzio
9.Usitamani fakat ya mwenzio
10. Usitaman bumu lake wala chochote alichonacho. hahaha chezea chuo weye!
BREAKING NEWS!!! Nyoka wa ajabu agundulika
HABARI MPASUKO..
jana katika taasisi ya wanyama pori ya Nat Geo ilitangazwa kuwa ametokea Nyoka hatar san Ambaye hajawah kutokea duniania.. wanadai kwamba nyoka huyo anaongezeka ulrefu wa 0.5sm kila akila chakula na huwa anakula chakula kuanzia sekunde 30 kurudi nyuma.. mpaka sasa hakuna siraha ya kuweza kumuua nyoka huyo isipokuwa akiji uma mwenye ndo anaweza kufa, wanasayansi hao walieleza japo uchunguz zaid bado unaendelea… huyu ni nyoka anayeua kuliko nyoka wote waliowah kutokea katika historia ya maisha ya mwanadam..
nyoka huyu hupatikana katika simu pekee za nokia toch katika sehem ya game inaitwa snake xenzia..
asanteni kwa kufurah na umakin mkubwa katika usomaji wa matini hii…
haya ni mambo ya wikiend jaman na iwe njema kwenu wote
Nilichojibu kwenye interview walipoulizia status
Nimetoka kufanya interview wakaniuliza status yangu nikaawabia status yangu ni Hey there! Iam using watsApp, wameniambia nitoke nje I think wanajadiliana namna ya kunipangia kituo cha kazi
Cha kufanya msichana akikukimbia halafu atake kukurudia
……… Kama msichana atakutupa kwa sababu huna pesa, na baadaye unapopata pesa akarudi tena kuomba msamaha… Ndugu yangu….. Msamehe…. Mpe ahadi ya ndoa, mwambie utamuoa…. iambie familia yake unataka kufanya ukarabati wa nyumba yao…… Ondoa paa lote la nyumba yao halafu TOWEKA…..
😂……… 😂…….. 😂
Kilichotokea baada ya kuzamia sherehe
Pale unapozamia kwenye Dinner Party ya Jumuiya Fulani, sasa Lengo la Jumuiya hiyo ni kupata Fedha za kutunisha Mfuko wa Jumuiya…sasa unakakaa mbele kabisa ili Muda wa Msosi usichelewe na kukuta kwenye Buffee yamebaki maharage!
MC : “Papai zuri kabisa kutoka Newala, Papai Mwendokasi, hili ni Shilingi laki 1..jamani Papai,nipeni ofa!”
MOSHA : “Laki 3 hapaaa!”
“Jamani laki 3 pale kwa Mosha, Papai linaondoka jamani, papai hili ni self contained kabisa….papai jamani”
KIBOLIBO: “Milioni 1 hapaaa”
“Jamani Mambo yanazidi kunoga hapa!…Benedict Kibolibo anataka papai kwa milioni 1 jamani, linaondoka papai!”
RWEYEMAMU : “nitanunua Papai hilo kwa Milioni 5”
Haya sasa jamani Rweyemamu ametoa ofa ya Milioni 5 Jamani, nani mweingineee?”
Kimyaaa…
Haya jamani Papai kama hakuna Ofa basi Papai linakwenda kwa Rweyemamu!……..haya sasa Kuna Kuku hapa Jogoo kabisa, bei yake ni laki 6 jamani Jogoo twitter huyu!”
WEWE “Milioni Mojaaa!”( hapa umejiwahi wa kwanza na wewe uonekane upo huku ukijua kabisa Wakina Mosha na Rweyemamu lazima watampandia Dau Jogoo, tena dau kubwa”
MC: ee sasa Kumekucha Jamani, Kabasele anamtaka Jogoo kwa Milioni 1 jamani!….ofa nyingineeee!”
Kimyaaa…
Jamani Jogoo anakwenda kwa Kabasele jamani!…ofa nyinginee!
Kimyaaa….
Kimyaaa….
😝😝😝…hapa sasa ndio mfukoni kuna Buku jero,..huko kwengineko NMB nill balance…sasa unageuza mimacho kumtazama Mosha kama atapanda dau kwa jogoo👀(mama wee Mosha anachezea Simu!)…..unamtazama Rweyemamu (teh anatafuna Kuku)…..mama weee😝
MC: Haya jamani kama hakuna Mwingine basi zoezi letu liishie hapa na limekwenda kwa Mafanikio, Mpatieni Kabasele Jogoo wake!
Hapa sasa unapokea jogoo wako wa MILIONI kwa Tabasamu la Maiti….kule nyumbani Jogoo wako Mkubwa unauza elfu 20 lakini sasa haka kajogoo kapya Mkononi kanakuwa kazito utadhani umembeba John Cena👀…Mama weee hapa sasa vidari ulivyotafuna unaviona kama vimerudi kwenye Ulimi….Chicken wings zinataka kutokea Masikioni…..Uuuuwiiiii,😝😝😝
Na hapa sasa kabla Dinner haijaisha ndipo unapojikuta Umebuni Cocktail ya Sparetta na Tomato😂😝😝😝😂.
chiel wie okee
Cheki jamaa alivyoumbuka baada ya kuhudhuria semina isiyomuhusu
Jamaa kavamia semina ya wasomi iliyokua inafanyika maeneo ya ubungo plaza bas wakaanza kujitambulisha
1. Naitwa Anna niko SUA mwaka3 nasoma agriculture
2. Naitwa Stella niko UDSM mwaka2 nasoma public relation
3. Naitwa Emmanuel niko UDOM mwaka3 nasoma computer science
bas jamaa nae akainuka kwa kusuasua huku akijishtukia akasema”Naitwa Elisha niko Tanesco mwaka wa 7 nasoma mita”
Recent Comments