Vichekesho Vya Tanzania

BREAKING NEWS!!! Nyoka wa ajabu agundulika

HABARI MPASUKO..

jana katika taasisi ya wanyama pori ya Nat Geo ilitangazwa kuwa ametokea Nyoka hatar san Ambaye hajawah kutokea duniania.. wanadai kwamba nyoka huyo anaongezeka ulrefu wa 0.5sm kila akila chakula na huwa anakula chakula kuanzia sekunde 30 kurudi nyuma.. mpaka sasa hakuna siraha ya kuweza kumuua nyoka huyo isipokuwa akiji uma mwenye ndo anaweza kufa, wanasayansi hao walieleza japo uchunguz zaid bado unaendeleaโ€ฆ huyu ni nyoka anayeua kuliko nyoka wote waliowah kutokea katika historia ya maisha ya mwanadam..

nyoka huyu hupatikana katika simu pekee za nokia toch katika sehem ya game inaitwa snake xenzia..

asanteni kwa kufurah na umakin mkubwa katika usomaji wa matini hiiโ€ฆ

haya ni mambo ya wikiend jaman na iwe njema kwenu wote

Cha kufanya msichana akikukimbia halafu atake kukurudia

โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Kama msichana atakutupa kwa sababu huna pesa, na baadaye unapopata pesa akarudi tena kuomba msamahaโ€ฆ Ndugu yanguโ€ฆ.. Msameheโ€ฆ. Mpe ahadi ya ndoa, mwambie utamuoaโ€ฆ. iambie familia yake unataka kufanya ukarabati wa nyumba yaoโ€ฆโ€ฆ Ondoa paa lote la nyumba yao halafu TOWEKAโ€ฆ..

๐Ÿ˜‚โ€ฆโ€ฆโ€ฆ ๐Ÿ˜‚โ€ฆโ€ฆ.. ๐Ÿ˜‚

Utani wa wahindi, cheka kidogo

Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili

(1) Mfa maji ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?โ€ฆโ€ฆ. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?โ€ฆโ€ฆ.. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?โ€ฆโ€ฆ Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ Takosa guo ya sikukuuโ€ฆ
(10) Kila ndege ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.. โ€ฆHutua Airport
(11) Bandu bandu ?โ€ฆ.. โ€ฆโ€ฆ.Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?โ€ฆ Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?โ€ฆ.Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?โ€ฆโ€ฆ.. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?โ€ฆ. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? โ€ฆโ€ฆ.. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?โ€ฆโ€ฆ.. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?โ€ฆ.Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?โ€ฆโ€ฆ.. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? โ€ฆโ€ฆโ€ฆ.Taenda Chadema
(23) Bendera ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?โ€ฆโ€ฆ. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?โ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? โ€ฆโ€ฆ.. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.

Tabia za Kimama kwa wanaume

1, mwanaume kuoga haraka haraka ili uwahi kuangalia igizo, huo ni UMAMA..๐Ÿ˜‚

2, mwanaume kupiga picha umeng’ata Lips na Unapiga na Camera Beauty Plus huo ni UMAMA..๐Ÿ˜‚

3, Mwanaume kuangalia tamthilia na Jamai Raja na Maigizo kwenye chanel ya sinema zetu wakati mechi za kombe la dunia zinaendelea, pia nawe ni MMAMAAโ€ฆ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

4, Mwanaume kuandika ‘Jomon’ badala ya Jamani, kuandika ‘Pw’ badala ya Poa, kuandika ‘Thatha’ badala ya Sasa, kumwandikia mwanaume mwenzio ‘Mambo my’ Huu ni UDADA, tena UDADA wa CHUO..๐Ÿ˜‚
.
5, Mwanaume kunywa soda au Juice na kubakisha, kununua chakula halafu unakibakisha, kubagua bagua chakula na kujamba hovyo hovyo baada ya kushiba, huo nao ni UMAMAA..๐Ÿ˜‚
.
6, Mwanaume kumuuliza mwanaume mwenzio anapata faida gani kuangalia Mpira, pia nawe ni MMAMAโ€ฆ
.
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Tofauti ya ukopaji wa mzungu na mswahili

MZUNGU: Hi, I need $100, will pay back on Monday

MSWAHILI: Kaka vipi, shwari? Dah.. hatuonani mzee, mishe vipi, mnatunyima nini? Juzi nimekuona kwa mbaaaliโ€ฆ mzee shavu dodo, full kipupwe! Sie tupo bwana, shida tu, afu misiba mingi tu, wife nae kajifungua ghafla. Sasa, kuna cheque naisubiri haijatoka hadi leo, wanasema itatoka next week, hapa nimekwama kweli. Naweza pata ‘Laki Moja’ ya karibu hapo nitarudisha mwisho wa mweziโ€ฆ?๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Angalia kilichojiri katika semina ya wanandoa kuhusu upendo

Kulikuwa na semina ya wanawake kuhusu namna ya kuishi kwa upendo katika ndoa.
Mwalimu aliwauliza ni wangapi wanawapenda waume zao? Wote wakanyoosha mikono kama ishara ya kuwa wanawapenda waume zao.
Mwalimu akauliza tena, โ€œNi lini mara ya mwisho umemwambia mumeo โ€œNakupenda Mpenziโ€?

Majibu yalikuwa kama ifuatavyo:
Wengine wakisema Asubuhi ya leo,
Wengine jana,
Wengine wiki iliyopita
Wengine mwezi uliopita
Na wengine wakasema hawakumbuki!
Mwalimu aliwapa kazi kila mwanasemina achukue simu yake na kumtumia mume wake meseji yenye neno โ€œNAKUPENDA MPENZIโ€
Baada ya meseji kwenda aliwaamuru kubadilishana simu kila mtu na jirani yake.
Kila mwanasemina aliambiwa kusoma meseji za majibu kwenye simu aliyoshika

Simu ya 1 โ€“ โ€œSamahani, nani mwenzanguโ€!
Simu ya 2 โ€“ โ€œSamahani, wrong numberโ€!
Simu ya 3 โ€“ โ€œSi nimekuambia usinitumie messages kwenye namba hiiโ€!
Simu ya 4 โ€“ โ€œMh! leo mvua itanyeshaโ€!
Simu ya 5 โ€“ โ€œNikija tutaongea zaidiโ€!
Simu ya 6 โ€“ โ€œโ€ฆโ€ฆImedhibitishwa umepokea Tsh300,000 kutoka kwa โ€ฆโ€ฆโ€!
Simu ya 7 โ€“ โ€œMe tooโ€!
Simu ya 6 โ€“ โ€œHuu ujumbe ndio ulikuwa unamtumia huyo hawara yako ee, leo utanikomaโ€!

Alichofanya mke baada ya mme wake kupenda kumchunga sana

Alifanya hivi;
Siku ya kwanza

MUME: Halooo vipi mke wangu salama weye?.
MKE: Salama tu
MUME: Uko wapi?
MKE: Jamani si niko nyumbani
MUME: Mhh kama kweli uko nyumbani washa blender nisikieโ€ฆ..mkeยญ akawasha blender
MKE: Umesikia?
MUME: Okay haya mi natoka kazini naja

Siku ya pili
MUME: Vipi mko salama huko?
MKE: Tupo kama ulivyotuacha
MUME: kwani uko wapi?
MKE: Niko nyumbani napika
MUME: Washa brender kama kweli uko nyumbani
Mke akawasha blender
MKE: Umesikia?
MUME: Poa ntarudi baada ya masaa mawili

Siku sita baadaeย mume akaamua kurudi bila kumtaarifu mkewe alipofika home kamkuta mdada wa kazi yuko peke yake.
MUME: We mama yako yuko wapi?
MDADA: Sijui ameondoka na blender toka asubuhi

Wanaume wote ni waaminifu

Hii ni kwa wanaume ila mwanamke anaweza kusoma na kujifunza kuwa wanaume wote ni waaminifu.

Mwanaume mmoja alienda kukata miti kwa ajili ya mkaa, bahati mbaya panga likadondokea mtoni, akaanza kulia sana. Malaika akatokea na kumuuliza kwanini analia. Jamaa akajibu; “Panga langu limedondokea mtoni na ndilo ninalotegemea kuendeshea maisha yangu”.

Malaika akazama mtoni na kuibika na panga la DHAHABU na kumuuliza, ndio hili?

Jamaa: Hapana.

Malaika akazama tena na kuibuka na panga la SHABA na kuuliza, ndio hili?

Jamaa: Hapana.

Malaika akazama tena mara hii akaibuka na panga la CHUMA na kuuliza ndio hili?

Jamaa: NDIYO.

Malaika akafurahishwa sana na uaminifu wake hivyo akampa mapanga yote matatu. Jamaa akafurahi sana.

Siku nyingine jamaa alikuwa anatembea na mkewe njiani ghafla mke akadondokea mtoni, jamaa akaanza kulia. Malaika akatokea na kumuuliza: Kwanini unalia?

Jamaa: Mke wangu kadondokea mtoni na nampenda sana.

Malaika akazama mtoni akaibuka na WEMA SEPETU na kuuliza; “huyu ndiye mkeo?”

Jamaa: NDIYO.

Malaika akakasirika sana na kumuuliza: kwa nini umenidanganya?

Jamaa: Nimesema ndiyo kwa sababu ningesema hapana ungezama tena na kuibuka na AUNT EZEKIEL na ningesema hapana tena ungezama na kuibuka na MKE wangu alafu ningesema ndiyo ungenipa wote watatu!

Sasa mimi maskini sina uwezo wa kuhudumia wote hao, ndio maana nikasema NDIYO kwa Wema Sepetu.

*FUNDISHO*
Wanaume huwa hatusemi uongo bila sababu na inakuwa sababu maalumu kwa faida ya wote.

WANAUME WOTE NI WAAMINIFU. Hii ndiyo kauli mbiu yetu.
๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€

Cheki kilichotokea stesheni ya treni, mambo mengine ukipaniki inakula kwako kama huyu jamaa

Jamaa Wawili Walifika Stesheni, wakakuta Treni ndo kwanza inaondoka. Wakaanza Kuikimbiza. Mmoja akafanikiwa kupanda akaondokaโ€ฆ

Yule aliyebaki akaanza kucheka sanaa mpaka machozi yakamtoka. Watu wakamuullza, unacheka nini sasa wakati umeachwa? Akawajibu: “kinachonichekesha, yule aliyepanda alikuwa ananisindikiza.

Shopping Cart
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About