SMS Nzuri: Meseji za Visa Vya Kukubadilisha Mood
Angalia huyu mgeni anachokifanya, wageni wengine ni hatari
Hata kama ni Mgeni this is too much.
Mwenyeji: Karibu mgeni karibu ukae,utapenda chai au soda?
Mgeni: Nipe nianze na soda wakati chai inachemka.
Mwenyeji: Utakunywa fanta au sprite?
Mgeni: Nipe fanta wakati sprite inapoa.
Mwenyeji: Utakunywa na keki au mkate?
Mgeni: Nipe keki mkate nitanywea chai ikishachemka.
Mwenyeji: Utapendelea ndiz au machungwa,
Mgeni: Nipe machungwa ndizi ntakula na wali
mchana.
Chezea mgeni ww.!!!
Mwizi kawezwa ki kwelii
Et jana usiku mwiz kavunja mlango kwangu akaanza kutafuta kitu kila kona ikabid na mie niamke namuuliza unatafuta nini ananijibu hela ndipo nilipoanza na mie kutafuta nae maana hta hela ya kula Jana sikua nayo alichoka zaid nilipomuliza una uhakika uliweka humu? sipendagi ujingaπΆπ» na kitu hela mm!
Angalia huyu mtoto anachomjibu baba yake baada ya kutoka kwenye mtihani
BABA: mwanangu kwenye huu mtihani uliofanya natumaini utafanya vizuri.
DOGO: ndio baba nitapata mia kwa mia.
BABA: kwanini unasema hivyo?.
DOGO: kwasababu jana kanisani tulifundishwa “Yesu ni jibu” kwahiyo kote nimejaza Yesu.
BABA: kwel kazi ipo
JE UNGEKUWA WEWE HUYO NDO MWANAO UNGEMFANYAJE?
Kwa nini vitu vunavyoanza na “K” ni vitamu sana?
Zuzu kaniuliza, “Anko, unajua vitu vinavyoanzia na K ni vitamu sana.”
Nikashtuka, “Astaghafilulah we mtoto! Niondolee wehu wako hapa!”
Zuzu akatabasamu. Akaendelea kuongea kabla sijafanikiwa kumzuia. “Kweli kabisa anko. Vitu vinavyoanza na K ni vitamu sana kwa mfano kuku, kalimati, keki, kabab, katleti, kashata, kisheti na karoti.”
Nikashusha pumzi. “Ahaa! Kumbe ndo hivyo, ni kweli!”
Zuzu akanitupia swali. “Kwani we anko ulidhani nini?”
Angalia walichofanyiana hawa wanadoa, Kati ya huyu mme na mke nani zaidi?
MUME wakati anakata roho huku mkewe akiwa amemshikilia alisema mke wangu, mi natubu kwako, kwani nilifanya mapenzi na dada yako, mdogo wako, rafiki yako na mama yako
MKE akamnong’oneza mume wake na kumwambia mbona mimi nayafahamu yote, ndio maana nimekupa sumu ili na wewe ujue uchungu wake. JE NANI ZAIDI?
Utani wa wahindi, cheka kidogo
Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili
(1) Mfa maji ?β¦β¦β¦β¦β¦β¦.. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?β¦β¦β¦β¦ Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?β¦β¦β¦.. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?β¦β¦β¦β¦β¦β¦ Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?β¦β¦. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?β¦β¦β¦ Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?β¦β¦.. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?β¦β¦ Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?β¦β¦β¦ Takosa guo ya sikukuuβ¦
(10) Kila ndege ?β¦β¦β¦β¦.. β¦Hutua Airport
(11) Bandu bandu ?β¦.. β¦β¦.Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?β¦ Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?β¦.Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?β¦β¦β¦. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?β¦β¦.. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?β¦. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? β¦β¦.. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? β¦β¦β¦β¦..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?β¦β¦.. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?β¦.Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?β¦β¦.. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? β¦β¦β¦.Taenda Chadema
(23) Bendera ?β¦β¦β¦β¦β¦. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?β¦β¦. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?β¦β¦β¦. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? β¦β¦.. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.
Huu mchezo hautaki makeup
Mama mwenye nyumba anajipodoa anashinda saloon kujipodoa lakini house girl hata mafuta usoni hapaki lakini akipita na khanga yake moja tuu nyumba inatetemekaππππππππππππππ huu mchezo hautaki mekapu
Eti hili nalo ni kweli kwa dada yako?
Oya people hv kwa mfano Dada yako akisomea sheria ndo anaitwa sister in law? au
πππππππππππ
Angalia sababu ya mwanamme kubadili jina na Kuitwa jina la kike, hii dunia ina mambo kweli
Rashidi alimpa ujauzito mwanafunzi, akashtakiwa.
Kumbe Rashidi ana bibi yake mtaalamu wa yale mambo yao ya Sumbawanga, akampachika Rashidi i jinsia ya kike.
Alipofika mahakamani kuhojiwa Rashidi akasema sijampa ujauzito kwa sababu mimi pia nina jinsia ya kike.
Kwa kuthibitisha Rashid wakaenda kumkagua basi akashinda kesi, kufika nyumbani Rashid akawakuta watu wamejaa wanalia, akauliza kulikoni?
Akaambiwa bibi yako amefariki. πππππππ°π°π°ππππππ
Kwa sasa Rashid anaitwa Leilaπππ
Wachaga kweli kiboko: Mcheki huyu mchaga na mbuzi!!!
Mchaga alinunua mbuzi akamwambia mpishi Nyama nusu ipike pilau na ingine itie kwenye friza. Kichwa fanya supu, miguu fanya mchuzi chukuchuku. Ngozi usitupe tutafanya mswala, utumbo pikia ndizi na mifupa tutawauzia wenye mbwa. Kinyesi kihifadhi kwa mbolea ya bustani.
Mpishi akamuuliza Hutaki na sauti ya mbuzi tufanye ring tone kwenye simu yako? Mchaga akajibu Yesuu! hivi inawezekana? bac fanya hivyo tuwauzie na wengine hiyo ringtone. ππ
Eti hii ni kweli kwa mwanaume anayempa simu mkewe
Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana
..unaenda kuoga, unakumbuka kuwa umesahau sabuniβ¦unaenda kuchukua sabuni kurudi bafuni, unakuta ng’ombe amekunywa maji yote..unaamua kufuata mengne,unarudi unakuta mbuzi kala sabuniβ¦ππππ
Utoto raha..! Angalia hawa watoto wanachokifanya sasa
Leo nimepulizia Air Fresh yenye Harufu ya Pilau nyumbani kwangu sasa watoto wa Jirani wamehamia Mlangoni kwangu ndio wanacheza hapo. Kila nikitoka wananisalimia. Mama yao ndio kanimaliza kabisa nimetoka akaniambia
“Kumbe wewe ni Mpishi mzuri, Hongera”
Imebidi nisirudi nyumbani maana wale watoto wanaweza kuingia ndani kabisa na pilau hakuna.
#UTOTO RAHA π
ππππππ»ππ»ππ»
Baada ya kunitumia SMS usiku ikawa hiviβ¦.
Jana usiku kuna Jirani yangu..kanitumia text “mambo vipi?”β¦halafu tunakaa nae mtaa mmoja nikaona nikimjibu ni uharibifu wa hela nikaenda kumgongea mlango saa 7 usiku. Alipofungua nikamjibu “shwari”halafu nikarudi nyumbani kulala zangu..
Sipendagi kuchezea salio..
πππππ
Kama mpezi wako akikuita MAMITO Unatakiwa umjibu hivi
Akina dada mpenzi wako akikuita MAMITO usikubali
na yeye mwite MAFORONYA kama mbwai na iwe mbwaiπ€ͺπ€ͺπ€ͺπ€ͺπ€ͺπ€ͺ
Cha kufanya mpenzi wako akikuacha
Kumkomoaβ¦
MPENZI WAKO AKIKUACHA BILA SABABU CHUKUA SIMU MPIGIE MAMA AKE MWAMBIE MWANAO AMEKUFA UWEZIβ¦. KULIA PEKE YAKOπ€
Dongo kwako kama una degree moja Halafu unachagua kazi
Mtu una degree 1 unachagua kazi! Wakati thermometer ina degree 100, inafanya kazi kwenye kwapa.
πππππ
Ni Utani tuuuuu!
Mapenzi Stress tupu
Stress Tupu
Unapokea Sms kwa mpenzi wako anakuambia
“Kuanzia Leo Mimi Na wewe Basi! ????”
Unashtuka ??β¦. Una muuliza kulikoni? ????
Anakujibu: “Sorry Sio Sms yako?”
Hapo Ndo utajua Kwanini Hakuna Mmasai Albino??????
Angalia nilichomfanyia huyu dereva sasa
Tulikua kwa basi tunaelekea arusha,ile namcheki dereva kumbe ni best yangu na basi ilikua kwenye spidi hatari, nikaenda kumziba macho nkamuulizaΒ otea mi ni nani, kabla hajanijibu nikasikia kishindo kikubwa sana
NA SASA HIVI NIMEZINDUKA NIMEONA ABIRIA WOTE TUPO WODI NAMBA 3 HAPA KCMC MOSHI. π€π€π€π€
SODA ZA WAGONJWA PLIIIZ!!! πππππ
Kuna watu makauzu ila huyu kazidi.. Soma hii!
Kakubaliana vizuri na msichana fulani hivi kuwa aibuke gheto, mchizi kajipanga vizuri kabisaβ¦. mara saa nne hivi mdada kasema hana nauli.
Mshkaji kajikunja kamtumia Elfu tano maana mwenye shida alikuwa ni yeyeβ¦β¦
Baada ya nusu saa yule dada akamtumia meseji.
“Jamani mpenzi, kumbe baba hatoki nilijua atatokaβ¦ sorry bae sitaweza kuja kwa leoβ¦ sooo sorry!”
Mshkaji jiii! hajajibu kituβ¦..
Baada ya muda kidogo meseji ikaingia katika simu ya binti, akajua mchizi kajibu. Mh! kutazama ni meseji kutoka Mpesa.
“CA90F0511 IMETHIBITISHWA Tshs 5000 ILIYOTUMWA KIMAKOSA KATIKA ACCOUNT YAKO IMETOLEWA SALIO LAKO NI Tshs 5”
Halafu ndo ikaingia meseji ya mshkaji.
“BASI POA SIKU NYINGINE KAMA VIPI”
#dada wa watu mashavu yakamshukaβ¦ hakuamini kilichotokeaβ¦. yaani jamaa keshawapigia Voda na pesa fasta imezuiliwaβ¦β¦














































































I’m so happy you’re here! π₯³
Recent Comments