SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Misemo 17 ya kuchekesha

1) gari la kuvutwa halina overtake
2) kisigino hakikakai mbele
3) wimbo wa taifa haupgwi disko
4) feni haiwashwi beach
5) mshkaki hauchomwi kwa jiko la ges
6) mganga haagiz tembele
7) hata bibi alikuwa bint
8) mke wa mtu sumu,mume wamtu maziwa
9) kipara bila pesa ni kovu
10) mbwa hanenepi migiuu
11) picha ya rais haina bodyguard
12) mjini shule kijiji tuition
13) saa ya ukutani haivaliwi mkonon
14) heshima pesa shkamoo makelele
15) ulinz pesa bastora mzgo
16) kuku ni kuku jogoo mbwembwe
17) kusoma kuelewa kukesha mbwembwe

UKWELI KUHUSU MSHAHARA

1. Epuka kugeuza mshahara wako kuwa mali ya ukoo. Kamwe mshahara wako siyo mali ya ukoo. Siku utakapoacha kuufanya mshahara wako mali ya ukoo ndipo siku mshahara huo utakuwa mkubwa! Hapo ndipo mshahara utatosha.

2. Siku utakapokuwa na vyanzo vya mapato zaidi ya mshahara wako ndipo mshahara wako utakapotosha mahitaji yako ya kila mwezi.

3. Usiombe mwajiri wako akulipe overtime allowance, mwombe akupe muda wa kufanya kazi zako za ziada(perform your own overtime duties)

4. Epuka kuwasambazia pesa za mshahara wako watu wa ukoo wako ili uwaokoe na hali ngumu ya ukosefu wa fedha waliyonayo. Badala yake Wasaidie kuona fursa za kuwapatia Pesa!

5. Usiombe mwajiri wako akuongezee mshahara bali omba Mungu akuwezeshe Kupata kipato endelevu nje ya mshahara wako.

6. Mtu anayeishi kwa kutegemea mshahara wake tu ni sawa na mtu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga na mafuriko yalipokuja anguko la nyumba hiyo lilikuwa na mshindo mkubwa sana.

7. Mto Kagera au Maragalasi haijawahi kukauka maji yake. Kwa nini? Ni kwa sababu inapokea maji yake kutoka kwenye vyanzo vingi vya maji au vijito vingi! Mtu mwenye vyanzo vingi vya mapato zaidi ya mshahara atafanishwa na mto Kagera au Maragalasi isiyokauka maji yake.

8. Usisubiri kustaafu kazi ndipo ulipwe mamilioni ya pesa za kiinua mgongo bali tafuta kumiliki vyanzo sahihi vya pesa, na ndipo malipo ya kiinua mgongo utalipwa kila wiki mamilioni ya pesa.

9. Watu wenye busara hutafuta vyanzo vya pesa vinavyoweza kuwalipa mshahara au pensheni ya Tshs 150 milioni kwa mwezi badala ya kusubiri kulipwa kiinua mgongo cha Shs 150milioni baada ya kufanya kazi kwa miaka 30 au zaidi.

10. Waajiriwa wenye hekima na busara hutumia mishahara yao kutengeneza au kutandaza mabomba ya fedha au mtandao wa fedha endelevu ili hata kama hawatakuwepo tena duniani watoto wao na watoto wa watoto wao waendelee kupata mshahara kila mwezi!

Cheki huyu jamaa anavyoungama kwa padri sasa

JAMAA: Baba Padri nimekuja kuungama
PADRI: Haya
JAMAA: Niliiba kamba
PADRI: Kamba?
JAMAA: Ndio, kamba lakini kule mwisho kulikuwa kumefungwa ng’ombe
PADRI: Kwa hiyo uliiba ng’ombe?
JAMAA: Kiukweli nilikuwa nina lengo la kuiba kamba, kwa bahati mbaya mwisho kulikuwa na ng’ombe
PADRI: Mi naona mueleze Mungu direct, mi sikuelewi kabisaaa

🙈😃😃😃😀😀😀😂🙊

Angalia sababu ya mke Mtarajiwa kuzimia kabla ya harusi

*Jihadharini* na wachapaji wa kadi za harusi. Hakikisha unasoma maandishi yaliyochapwa kabla ya kadi kuchapwa na kusambazwa!

Mchapaji aliombwa aweke 1 Yohana 4:18 katika kadi ya harusi lakini mchapaji kwa makosa aliweka Yohana 4:18.

1 Yohana 4:18 panasema, “Katika pendo hakuna hofu, lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu…”

Lakini Yohana 4:18 tunasoma, “Kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako.”

🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃😂😂😂😂_MKE MTARAJIWA AKAZIMIA HAPA, TUNAMPEPEA_

SOMA HII: Kama wewe ndo baba au mama hapa ungefanyaje!???

Bakari ni house boy mara nyingi huiba wine ya boss wake na kisha kuongeza maji kwenye chupa ili boss asigundue. Mara kadhaa boss alihisi ladha tofauti anapokunywa wine hivyo kuhisi kuna mchezo mchafu alihisi tu Bakari anahusika. Ilikua ni bahati tu alimvizia na kumbamba Bakari akichakachua wine, kwa kuwa mkewe alikua anamtetea Bakari, ili kumthibitishia mkewe kuwa Bakari ndo culprit,
boss alianza kwa kumuuliza Bakari maswali. Siku hiyo Bakari alikua jikoni,boss na mkewe walikua sebuleni.

Boss:- Bakariiii!
Bakari:- Naam baba!
Boss:- Nani anakunywa wine yangu?

Bakari:- Kimyaaaa hajibu kitu! Boss:- Bakariiiii !
Bakari:- naam baba! Boss:- nauliza nani anakunywa wine yangu halafu anajazia majiii!
Bakari:- kimyaaaaa!

Boss akaamua amfuate hukohuko jikoni.
Boss: Kwanini nikikuita unaitikia, nikikuuliza unanyamaza?
Bakari: Baba huku jikoni ndo kulivyo, unasikia jina tu likiitwa lakini maneno menginehusikii, na kama huamini baki jikoni mi niende sebuleni.

Bakari akaenda sebuleni akaanza kuita.
Bakari:Babaa!
Boss: Naam Bakari!
Bakari: Saa sita usiku huwa unaenda kufanya nini chumba cha house girl?
Boss:- kimyaaaa!
Bakari:- Baba babaa!
Boss:- Ndio Bakari!
Bakari:- Nauliza hivii, chumbani kwa house girl saa sita za usiku huwa wafuata nini?
Boss:- kimyaaaaaaa!

Boss akatoka nje: Bakari huku jikoni ni kweli husikii kitu zaidi ya jina!.
Mama akasema msinizingue nyie…Mbona siwaelewi..
Bakar: mama kama uamini na ww nenda uone.

Mama akaenda jikoni..
Bakari: akaita mamaa
Mama : bee bakari
Bakari: eti hiyo mimba niya baba au yangu.?
Mama kimya
Bakari; mama nakauliza tena hiyo mimba niyababa au yangu.

Mama akatoka aisee kweli humu unasikia jina tu…..😄😄😄😄😄

Huyu jamaa bonge la bwege, ungekua wewe ndiyo rafiki ake ungemwambiaje?

RAFIKI: Vipi mbona leo huna uchangamfu
JAMAA: Wanawake bwana, mwanamke hata umpendeje atakugeuka tu
RAFIKI: Nini tena ndugu yangu? Mbona shemeji mtu fresh sana
JAMAA: Hata mimi nilikuwa najua hivyo, leo nimegundua kumbe ana siri kubwa sana
ananificha, mi naita huu ni usaliti wa ndoa.
RAFIKI: Nini tena?

JAMAA:Nimegundua mke wangu kumbe anafanya biashara ya kitimoto na hajawahi hata kuniambia
RAFIKI: Kitimoto? We umejuaje?
JAMAA: Leo asubuhi nilichelewa kuamka niliamua nijipumzishe kidogo kabla ya kwenda kazini, simu ya mke wangu ikalia, nikaamua kuipokea, kabla hata sijafungua mdomo, nikasikia sauti ya mwanaume mmoja akauliza, “Huyo nguruwe umeshamuondoa?’ Hebu we fikiria nilivyoshtuka, yaani mpaka sasa nashindwa kuamini kuwa mke wangu ananizunguka anafanya biashara ya nguruwe hajaniambia hata siku moja

Aina ya mazoezi na umuhimu wa mazoezi kwa wamama wajawazito

Leo tutaongelea mazoezi gani ya kawaida ambayo mama mjamzito anaweza kuendelea kuyafanya kila siku ya ujauzito wake na umuhimu wake.

Mazoezi wakati wa ujauzito yanasaidia:

1. Kupata usingizi mzuri usiku.

2. Kuondoa stress.

3. Kulegeza na kunyoosha misuli ya uzazi na kuitayarisha kwa kazi ya kujifungua.

4. Kupunguza kichefu chefu(morning sickness) na kiungulia(heartburn)

KUMBUKA:

Wakati unafanya mazoezi hakikisha kuwa husikii maumivi yoyote na ukipatwa na maumivu hakikisha unaonana na daktari haraka iwezekanavyo. Kumbuka usilalie mgongo wakati wa kufanya mazoezi au usifanye mazoezi aina ya jogging (kukimbia) au kuruka ruka (bouncing) na hakikisha mdundo wa moyo (pulse) na temperature yako ya mwili ziko sawa. Kunwya maji mengi kuzuia dehydration na angalia balance yako iko sawa ili kuzuia kuanguka.

Kama ulikuwa unafanya mazoezi kabla ya ujauzito unaweza kuendelea na mazoezi yafuatayo:

Kuogelea

Uzuri wa zoezi hili ni kwamba halihitaji nguvu nyingi linasaidia kurelax na misuli yote ya mwili inafanya kazi. Unaweza kuogelea kwa dakika 20 hadi 35 lakini uchukue break pale utakapoona umechoka au kuishiwa na nguvu au pumzi. Kuogelea pia kunasaidia kupunguza maumivu yatokanayo na miguu kuvimba.

Kutembea

Ni zoezi zuri sana kwa mwanamke mjamzito. Zoezi hili linaweza kufanywa dakika 20 had 35 kwa siku. Zoezi hili linapunguza stress, linasaidia chakula kushuka vizuri na digestion. Pia linasaidia katika kuweka sawa uti wa mgongo. Tatizo la uti wa mgongo kutokunyooka linasababishwa na tumbo kuongezeka na kukosekana kwa balance kwenye mwili. Hiki ni chanzo cha maumivu ya mgongo. Kumbuka kuchuka break na kupumzika pale utakaposikia uchovu.

Kucheza Muziki

Mama mjamzito anaweza kucheza mziki kama zoezi hasa hasa mziki wa belly dancing wa kunyonga kiuno na miziki aina ya salsa. Hii inasaidia katika kulainisha misuli ya uzazi tayari kwa kujifungua, kusaidia kujifungua kwa urahisi na kupona kwa haraka zaidi baada ya kujifungua, kupunguza michirizi ya tumbo(stretch marks) inayojitokeza kwa ajili ya ngozi ya tumbo kuvutwa, pia inasaidia confidence ya mwanamke kujiona bado ana mvuto, kuondoa stress, kusaidia na balance, kupunguza maumivu ya mgongo na kusaidia kunyoosha uti wa mgongo.

Kuendesha baiskeli.

Pia unaweza kuendesha baiskeli ila uangalie balance usianguke na usiendeshe sehemu zenye msongamano wa watu au traffic ikiwezekana tumia baiskeli special za mazoezi ndani ya gym(stationary bikes).

SMS nzuri ya mapenzi ya kutakia usiku mwema

Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka.
Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika.
Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka.
Kitale katikati yake ukila utaridhika.
Matamu na maji yake hukata kiu haraka.
Weupe watui lake lina ladha ukipika.
Kupaka mafuta yake mwili hulainika.
Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika.
Hata na upepo wake uvumapo utacheka.
Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema

Ujumbe kwa leo

Kuna baadhi ya LEVEL huwezi kufika…Kuna MAFANIKIO huwezi kuyafikia…Kuna HELA huwezi kuzipata…Kama umezungukwa na watu BASIC…
Kuanzia asubuhi mpaka jioni wanaongelea WATU TU..Fulani kamegwa na yule..halafu yule naniliu saivi anatembea na yule ex wa nanii…Asubuhi mpaka jioni DISCUSSING PEOPLE…Hawa ndio watu BASIC…Hata siku 1 hawatakupa Ushauri kuhusu HOW TO REACH SOMEWHERE…NEVER

Na ukionekana unaanza kufanya vitu EPIC watakugeuka kwamba UNARINGA.. UNAJISIKIA.. UMEWATENGA…UNAJIDAI UNA HELA…and lots of bullshit…
Pengine ulipaswa kuwa mbaaalii kibiashara lakini HUWEZI coz umezungukwa n Mbaazi tupu…BASIC PEOPLE…Ukiwaambia umesikia Kiwanja kinauzwa Kigamboni wanakwambia Kigamboni watu wanatapeliwa kuna mradi wa Joji Bushi…Ukiwambia unataka kujiunga Forever Living wanakwambia UNALIWA HELA…Ukiwaambia kuna SACCOSS wanatoa mikopo unataka uchukue ujenge wanakwambia INTEREST ZAKE UTASHINDWA na kujenga sio mchezo shosti..Unaamini unaacha!…Nataka kufanya Kitu flani WANAKUKATISHA TAMAA
Unahitaji kuzungukwa na watu wenye POSITIVE ENERGY ambao ukiwambia unataka kwenda Mbinguni kwa kupitia Mkuranga wanakuchangia Nauli…Niliposema naacha kazi watu ohh utakula nini..utaishije…Mji Mgumu huu..Wenzio wanatafuta kazi we unaacha utalosti…WHO SAID??Nadunda kama kawa..NEGATIVE PEOPLE WILL BRING U DOWN….Ukitaka Kupaa kaa karibu na ndege…We unataka kupaa unakuwa rafiki wa Nyangumi…UNAZAMISHWA SASA HIVI!!
Tangu nianze kukaa na watu Positive I have changed a lot…Nikiwaza jambo wanauliza HOW DO WE ACHIEVE THIS na sio FULANI ALIWAHIFANYA HII AKAFELI..
Ikikusaidia Chukua..
KILL ALL NEGATIVE PEOPLE AROUND YOU kama unataka kufikia Malengo Makubwa, I will be ur Lawyer at the Court na mwambie Hakimu nilikutuma mimi!
TIME TO DELETE ALL BASIC PEOPLE who wait of option😜😜😉😉

Shopping Cart
2
    2
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About