SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

JE UNAFAHAMU NINI KUHUSU KUJAMBA?

Kwanini tunajamba? kwanini “ushuzi” unanuka?
Kujamba inaweza kuwa kitendo cha aibu kwa wengi wetu,lakini
inaweza kukufanya ujisikie vizuri kujua kwamba ni tendo
la kawaida sana kwa mwili wa binadamu kutenda.Kila
mtu anajamba,hata Halle Berry nae hujamba.

1.Kujamba ni nini hasa?
Kujamba kunasababishwa na kubanwa kwa hewa,ambayo
inaweza kutoka mwilini kwa njia nyingi.Baadhi ni hewa
tuliyoimeza wakati wa kula au kunywa.Hewa ingine
husababishwa na gesi kuingia kwenye utumbo wetu
kutoka kwenye damu,na baadhi ya gesi huzalishwa na
kemikali katika utumbo au bakteria.Kwa kawaida
“ushuzi” unakua na asilimia 59 ya gesi ya
nitrogen,asilimia 21 ni hydrogen,asilimia 9 ni carbon
dioxide,asilimia 7 methane na asilimia 4 ni oygen.
Asilimia moja tu ya “ushuzi” inaweza kuwa hydrogen
sulfide na mercaptans,ambayo ndio ina sulfur ndani
yake,sulfur ndo hufanya “ushuzi” utoe harufu mbaya
Kujamba huambatana na sauti,hii ni kutokana na
“vibration” katika njia ya haja kubwa.Ukubwa wa mlio wa
kujamba hutegemea “presha” inayosukuma gesi itoke nje
na pia ugumu wa misuli ya njia ya haja kubwa.

2.Kwa nini Ushuzi hutoa Harufu mbaya?
Harufu mbaya ya ushuzi hutegemea na ulaji wa
mtu,vyakula vyenye sulfur kwa wingi ndio husababisha
hili.Vyakula vyenye sulfur kwa wingi ni kama
maharage,kabichi,soda na mayai.

3.Watu hujamba hadi mara 14 kwa siku
Mtu wa kawaida hutoa hata nusu lita ya ushuzi kwa
siku.Inasemekana mtu akijamba mfululizo kwa kipindi
cha miaka 6,anaweza kuzalisha nishati ya kutosha
kutengeneza bomu la atomiki.

4.Ushuzi husafiri kwa mwendo wa futi 10 kwa sekunde.
Harufu ya ushuzi huanza kusikika sekunde 10-15 baada
ya mtu kujamba,hiyo ni kwa sababu inachukua muda
mrefu kwa harufu kufikia pua.

5.Kujizuia Kujamba Inaweza Kuhatarisha Afya Yako
Madaktari hawajakubaliana moja kwa moja kama kujizuia
kujamba ni hatari kiafya.Baadhi ya wataalam wanafikiri
kujamba ni sehemu muhimu katika mfumo wa
mmeng’enyo wa chakula,hivyo kujizuia kujamba
haitakuletea madhara.Wengine wanadhani kwamba
kujizuia kujamba kunaweza kusababisha tumbo kujaa
gesi,na pia inaweza sababisha bawasili (hemorrhoids).

6.Kwa Baadhi ya Tamaduni,Kujamba Sio Ishu
Wakati tamaduni nyingi zikichukulia tendo la kujamba
lifanywe kistaarabu,kuna baadhi ya tamaduni hawaoni
haya kujamba hadharani,na pia hufurahia tendo
hilo.Mfano kabila la Yanomami huko America ya
Kusini,kwao husalimiana kwa kujamba,na China
unaweza kupata kazi ya kunusa ushuzi! Katika Roma ya
zamani,Mfalme Claudius akihofia kwamba kujizuia
kujamba inaweza kuwa hatari kiafya,alipitisha sheria
kwamba ni ruhusa kujamba kwenye “banquets”.

7.Ushuzi Unawasha Moto
Kama ilivyoandikwa hapo juu,methane na hydrogen
inayozalishwa na ushuzi inaweza sababisha moto.

8.Mchwa Hujamba Kuliko Wanyama Aina Zote
Ni ngumu kuamini kuwa mchwa ndo anawajibika na
matatizo yetu ya “Global Warming”.Mchwa huongoza kwa
kujamba kwa wanyama,na hiyo huzalisha gesi ya
methane.

9.Ukiubana Ushuzi,Utakutoka Usingizini
Hata ujitahidi kuubana vipi,ushuzi utatoka mara
utapokua umepumzika,hasa ukiwa umelala.

10. Watu Hujamba Hata Baada ya Mauti Kuwafika
Maiti huendelea kutoa gesi hadi masaa matatu baada ya
mtu kufariki dunia,hii huambatana na milio ya
kujamba.Hali hii husababishwa na misuli kusinyaa.

UKIPATA NAFASI JAMBA MWANANGU

JITAMBUE: Kipi hauna kati ya pesa na muda?

Soma kidogo hapa.. Kuna watu wa aina NNE tunapoongelea pesa na muda.

1. WANA MUDA MWINGI ILA HAWANA PESA

Watu ambao hawana pesa ila wana muda wa bwerere. Hawajui thamani ya muda. Hawa ndo wale ambao hawajui cha kufanya. Anaamka mpaka analala usiku hana specific timetable. Unaweza kumkuta anaenda dukani ukamwambia nisindikize saluni na akakubali. Yupo yupo tu. Unaweza kuta ameingia Facebook hajui hata kwa mini. Basi tu kwa sababu ana bando. Akiperuzi akaona mahali wanaongelea mpira yumo. Akiscroll post za chini akakuta kuna mtu kapost kuhusu UKAWA yumo. Akikuta kuna mtu kapost mtu ana uvimbe mkuuubwa watu wameambiwa wacomment AMEN na yeye huyo anacomment AMEN. Akikuta watu wanaongelea TRUMP na yeye anaingia kucomment. Kundi hili ni kundi lenye watu wengi mno. Watu wa aina hii kufanikiwa ni bahati nasibu. Labda kwa bahati tu akutane na post nzuri kama hii na post zingine nzuri huenda ikamsaidia. Otherwise hawa ndo hawaelewi maisha yanaenda wapi maana hawana kitu fulani specific wanachofanya. Wakisikia tu kuna kitu kiko kama dili hivi wanaenda. Wakikuta kumbe kinahitaji bidii na kujituma wanaondoka. Wanataka maisha mazuri yaje tu yenyewe.

2. WANA PESA ILA HAWANA MUDA

Hili ni kundi la watu wenye shughuli fulani ya kiuchumi. Labda ameajiriwa au amejiajiri. Wako busy kweli kweli. Na ukweli pesa inaonekana. Hawa huwezi kumwambia njoo tuonane akaja hapo hapo. Huyu lazima apange kwanza ratiba zake. Maana yupo busy. Au lazima aombe ruhusa kazini maana hana uhuru na muda wake. Muda wake kamuuzia mtu (mwajiri). Au labda atoroke ndo anaweza kupata muda wa kufanya mambo yake binafsi. Au asubiri weekend ambapo kila ratiba itategemea siku hizo mbili, kama ni ibada, usafi, kutembelea wagonjwa au ndugu kwenda mahali kuona labda kiwanja kinauzwa au kuona ujenzi au mradi wake unaendeleaje nk. Mara nyingi watu wa kundi hili hushindwa kufanya vitu vingi vinavyohusu maendeleo yako binafsi mfano kujisomea, kuhudhuria semina zinazofundisha mambo yanayoweza kuwa na manufaa kwake nk. Sababu ana ratiba iliyobana. Ukiwa na sherehe ukamwomba mchango hashindwi kukuchangia angalau chochote kile lakini muda wa kuja kujumuika na wewe ni vigumu akaupata.
Hili ni kundi ambalo kuna watu wanaitwa MIDDLE CLASS people. Watu wa maisha ya kati. Mambo yako si mabaya sana lakini si kwamba ni mazuri. Wasomi wengi na watafutaji wengi wapo hapa. Afu ndo wanahisi wanajua kila kitu. Na wengi wao huishia kupata changamoto za kifedha na kiafya ukubwani au uzeeni kama stress na maradhi mbali mbali nk. Sababu ya kutokuwa na muda hata wa kuangalia wa kuinvest na kujifunza biashara au ujasiriamali mapema wala kujishughulisha na afya zao, mazoezi, kupumzika vizuri nk kwa kuwa walikuwa busy siku zote. Maisha ya watu hawa middle class mwishoni huja kuwa magumu kwa kuwa hata kuwa na muda na majirani tu ilikuwa ishu. Kwa kuwa wengi wana magari (mengi ni mkopo. Wengine gari la kazini) na kwa kuwa wanaweza kulipa kodi ya nyumba au hata kupata kakiwanja na kuanza kujenga huko Malamba Mawili basi wanaridhika. Hawawezi kuota kumiliki nyumba Masaki au kununua kiwanja Upanga. Kama upo kundi hili lazima uanze kutafuta mbinu mbali mbali za kuyakabili maisha vizuri siku za usoni. Waangalie wastaafu ambao walikuwa busy zamani. Saivi utasikia mgongo, miguu, macho nk vinasumbua. Hawa middle class people ndo ukimkuta social media wengi wao wako critical kwa kila kitu. Maana haoni kama ana shida yoyote.

3. HAWANA MUDA WALA HAWANA PESA

Ulishasikia mtu anaambiwa “busy for nothing”? Ni kitu kama hicho. Yani mtu unakuta labda ni kibarua tu mahali anatumwa kazi asubuhi mpaka jioni. Labda ameajiriwa kazi ya ulinzi, au gereji, au kwenye mradi wa ujenzi anabeba zege au kupaka rangi. Hashindi njaa ni kweli lakini ukweli hana hela. Wala hatamani kuendelea kuwa hivyo. Kuamka alfajiri kulala saa tano usiku. Hela anayopata inatosha kula kwa mama ntilie tu na nauli. Basi. Hawezi kuota hata gari. Hata ya mkopo. Maana hata hakopesheki. Huyu hata muda wa Facebook ni nadra akiingia ni kupitisha macho afu anatoka. Au hata simu ya Facebook hana.

4. WANA MUDA NA WANA PESA

Hapa ndo utakuta wale ambao hana tena shida ya pesa. Pesa iko. Hana tena shida ya muda. Akihitaji kwenda mahali haombi ruhusa wala kuaga mtu labda kumuaga mwenza wake tu. Anaweza kusikia kuna shamba linauzwa mahali na hahitaji kutafuta hela tena ili akalinunue bali anaanza michakato ya kisheria pale pale kununua kama amelipenda. Kuna siku nilienda Morocco Square hapo Kinondoni jirani na Airtel kuna Apartments zinajengwa nikaonana na watu wa NHC waliokuwa wanakagua ujenzi unaendeleaje. Nikawauliza hizo apartments zinauzwaje wakasema kuna za milioni 600 na za milioni 800. Na unatakiwa kulipa cash 10% (yaani aidha milioni 60 au 80 cash) halafu inayobakia unaweza kuimalizia ndani ya miezi 12. Na kuna watanzania kadhaa wamenunua tena kwa hela halali. Hawa wako kundi hili hapa. Hela ipo. Muda upo. Kuna watu walienda kutembea Marekani kibiashara walipokuwa njiani kurudi wakapita mahalinchi nyingine wakakuta kuna mnada wa nyumba kwenye nchi hiyo. Hawakujiuliza mara mbili wakanunua. Kuna wazee fulani wana mtoto wao alikuwa akisoma Canada. Alipograduate wakamuuliza unataka kuishi wapi akasema huku huku Canada wakamnunulia nyumba Canada. Ukisikia hivyo unaanza kuwaza ni mafisadi. Mawazo yako ninkuwa bila ufisadi watu hawanunui nyumba Canada. Kwa taarifa yako Hawa siyo waajiriwa serikalini wala popote ni wafanya biashara.. Kundi la watu kwenye pesa. Na muda. Wanaweza kuamua kesho wakaenda kutembea visiwa vya Comoros. Watu wanaoishi kundi hili wana discipline kubwa ya maisha. Na watu wengi wanatamani kufika kundi hili. Lakini HAWANA discipline ya kujifunza tabia zinazoweza kukufikisha huko.

Swali muhimu tu la kujiuliza tu ni kuwa je, wewe upo kundi lipi.

Una muda mwingi lakini huna hela? = FUKARA

Una hela nyingi lakini huna muda? = MIDDLE CLASS

Huna muda wala huna hela.. Vijisenti unavyopata vinaishia nauli kula kodi ya nyumba nk? = MASKINI

Au una muda mwingi na hela siyo shida tena? = TAJIRI

Kizungu nacho ni sheeeedeer

Mtalii: Do you have vegetables here.
Mtafsiri: Mnavyo vijimeza hapa.
Waiter: Vijimeza vidogo hatuna.
Mtafsiri: No sir, they don’t have.
Mtalii: OK, fine, do you have hot dogs.
Mtafsiri: Sawa, je mnao mbwa wa moto.
Waiter: Loh! Bwana we, hatupiki mbwa hapa.
Mtafsiri: They don’t cook here
Mtalii: What type of snacks do you have here.
Mtafsiri: Aina ngapi ya nyoka mnao hapa,
Waiter: We bwana we hapa hatupiki aina yeyote
ya nyoka, mwache akale nyumbani kwao.
Mtafsiri: They don’t cook any type of snacks
here,
maybe you can go back and eat at home.
Mtalii: OK, at least give us a cocktail juice.
Mtafsiri: OK, tupatie hata juisi ya mkia wa jogoo.
Waiter: Hebu tokeni na bangi zenu hapa, tena
sasa hivi kabla sijakasirika.
Mtafsiri: Lets get out of here
😝😝😝😂😂😂
Usicheke pekeyako

Jaribu kufikiria haya

1. Uelekeo ni muhimu kuliko kasi. Ni heri kwenda taratibu katika Uelekeo sahihi, kuliko kwenda kwa kasi katika Uelekeo usio sahihi.

2. Kulalamika mambo hayaendi wakati wewe mwenyewe hujui unakokwenda ni kuwa na matatizo ya akili.

3. Kasi yako inaamuliwa sana na umbali unaoweza kuona. Kama huoni chochote mbele ya maisha yako, basi huna chochote.

4. Sayansi inadai kuwa kazi ni nguvu inayotumika kusukuma kitu kwa umbali fulani kwenye Uelekeo maalumu. Kwa hiyo kama unatumia nguvu kusukuma mambo, lakini hayana Uelekeo maalumu jua kwamba hufanyi kazi yoyote, unapoteza nguvu tu.

5. Masaa yanaenda, siku zinapita, miaka inaongezeka, umri wako ndio unaenda hivyo, unafanya nini katika maisha?

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia baking soda

Moja ya sababu za kutokea chunusi katika ngozi yako ni kuwepo kwa takataka au uchafu juu ya ngozi yako na njia rahisi ya kusafisha taka hizo ni kwa kutumia baking soda hivyo kuifanya ngozi ipumuwe vizuri.

Kwahiyo ukiwa na chunusi hebu fikiri kuhusu baking soda. Baking Soda husaidia kubandua seli za ngozi zilizokufa na kufanya mafuta yaliyozidi kuondoka.

Ni rahisi zaidi kutumia baking soda kutibu chunusi. Chukua baking soda na uchanganye kidogo na vijiko vinne vidogo vya maji au vya maji maji ya limau na upake uji huo moja kwa moja kwenye chunusi. Subiri kwa dakika 10 na ujisafishe na maji ya moto.

Tabia za Kimama kwa wanaume

1, mwanaume kuoga haraka haraka ili uwahi kuangalia igizo, huo ni UMAMA..😂

2, mwanaume kupiga picha umeng’ata Lips na Unapiga na Camera Beauty Plus huo ni UMAMA..😂

3, Mwanaume kuangalia tamthilia na Jamai Raja na Maigizo kwenye chanel ya sinema zetu wakati mechi za kombe la dunia zinaendelea, pia nawe ni MMAMAA…😂😂

4, Mwanaume kuandika ‘Jomon’ badala ya Jamani, kuandika ‘Pw’ badala ya Poa, kuandika ‘Thatha’ badala ya Sasa, kumwandikia mwanaume mwenzio ‘Mambo my’ Huu ni UDADA, tena UDADA wa CHUO..😂
.
5, Mwanaume kunywa soda au Juice na kubakisha, kununua chakula halafu unakibakisha, kubagua bagua chakula na kujamba hovyo hovyo baada ya kushiba, huo nao ni UMAMAA..😂
.
6, Mwanaume kumuuliza mwanaume mwenzio anapata faida gani kuangalia Mpira, pia nawe ni MMAMA…
.
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Jamaa alikuwa na tabia ya kutembea na binamu yake cheki kilichomkuta

Jamaa alikuwa na tabia ya kutembea na binamu yake….

Alikuwa anasubiri mjomba na mkewe walale tu halafu ananyata mdogo mdogo mpaka chumbani kwa binamu yake.

Siku moja umeme ulikuwa umekatika ikabidi aamue kuvua nguo kabisachumbani kwake….

Akanyata taratibua akafungua mlango akazama chumbani kwa mjomba ake bila kujua, ghafla umeme ukarudi…

MJOMBA; we mshenzi umefata nini chumbani kwangu tena uko uchi

JAMAA; nimekuja kukuaga kesho naondoka

MJOMBA; ndo uje uchi?

JAMAA; ndio kwasababu nimeshapaki kila kitu kwenye begi

😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

FUNZO: Maisha ni kuchagua

Siku hizi kuna tangazo moja la kampuni ya simu za mikononi, Tigo, likimuonesha mama akiwa _busy_ na pembeni yupo mwanae mdogo apo akijisemesha na akatamka maneno ambapo mama akaona ni kama ameanza kuongea. Kwa furaha anampigia simu mumewe akimtaka amsikilize mwanae akiongea. Hapo mama anamtaka mwanae aseme “mama” na baba naye anavutia kwake akimtaka aseme “baba”. Kwa maajabu kabisa mtoto anawapotezea wote na kutamka “ni Tigo peesa”. Wazazi wakashikwa na butwaa lakini huku wakitabasamu.

Ukiitazama vizuri kazi ya ubunifu iliyotumika katika tangazo hili unaweza kupata funzo, pamoja na mengine, kwamba mtoto alikua na chaguzi lake ambalo ni tofauti na yale ambayo wazazi walikua wamempa. Lakini zaidi, pamoja na kuwa amekuwa na chaguzi lake binafsi, pasipo kufuata alichoagizwa na baba au mama, bado wazazi wanatabasamu kwani wanaona mwanao kafanya jambo jema.

👉Unaona unavyofanya kazi bila furaha kwa kua ulifanya chaguo la kazi hiyo kwa kusikiliza ndugu au marafiki.

👉Unaona unavyo _struggle_ katika biashara kwani halikua chaguo lako bali ni la ndugu au marafiki

👉Unakumbuka ulivyoshindwa kusomea kile unachopenda kwa kusikiliza ndugu au marafiki
9
👉Unakumbuka ulivyoshindwa kuishi na yule mwenzi uliyempenda na mkapendana naye kwa kusikiliza ndugu na marafiki

Unaweza kushauriwa, na ushauri ukawa ni mzuri kabisaa na ukaona ni vyema uufuate kwa kua hata wewe umeambiwa na ukachanganya na akili yako ukaona inafaa.

Jana nilitoa semina kwa wanafunzi wote wa Shule ya Sekondari Chang’ombe, pamoja na mambo mengine nikawataka kupima sana marafiki walio nao na kuona kama ni washauri wazuri na kama sivyo waachane nao na kuwa na marafiki wapya wenye mawazo chanya ya kuwasaidia kutimiza ndoto zao.

Kuna hii daladala imeandikwa nyuma *_Marafiki wengi mjini hasara_*. 😃. Mie nakuambia sio marafiki tu, hata ndugu pia. Kikubwa ni kuwapima wale ulio nao karibu na kuona kama bado ni wa msaada kwako. Wapime na chukua hatua. Kumbuka Mheshimiwa JK aliwahi kutuasa ” _Akili za kuambiwa, changanya na za kwako_ “.

Wosia mzuri wa baba kwa mwanae

Mwanangu, mimi baba yako nimeishi miaka mingi kuliko wewe ndio maana unaniita baba. Ni kweli sijasoma kama wewe ulivyosoma Ila mambo niliyokutana nayo tangu nimezaliwa ni elimu tosha ambayo wewe huna. Sasa nataka nikupe Elimu hiyo ili ukijumlisha na elimu yako ya darasani ujue namna nzuri ya kuishi katika dunia hii iliyojaa mishangazo mingi.

Maisha ni jumla ya mambo yote unayoyatenda kila siku. Namaanisha kila unalolifanya Leo linaathiri maisha yako ya kesho kwa hali chanya au hali hasi. Na kama ni hali hasi ni kwa ukubwa gani halikadharika kama ni hali chanya ni kwa kiwango gani. Mwanangu kila jambo unalolifanya Leo huamua ni mlango gani Unaweza ingia Kesho lakini pia mlango upi huwezi ingia Kesho. Ndio maana ni muhimu kuijua Kesho yako ukiwa Leo.

Mwanangu ili ufanikiwe ni lazima ujue kuishi na watu vizuri. Na mimi sikushauri kabisa kwamba uwe na marafiki wengi. Kuwa na marafiki wengi ni moja ya eneo unaweza jitengenezea mtego mbaya wa kukuangamiza kesho yako. Mwenye hekima mmoja aliwahi kusema ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe. Mwanangu kwa kusema hivyo simaanishi uwe na maadui,hapana. Ila marafiki zako watakusaidia mlango unaotaka kuingia Kesho uingie kwa urahisi au kwa ugumu au usiingie kabisa na wakati mwingine Unaweza kuingia na wakahusika kukutoa kwa aibu kubwa. Ndio maana ni muhimu Kuwa na marafiki ila Kuwa nao wachache chagua kwa makini mno. Sio lazima kila akufaaye kwa dhiki ndiye awe rafiki. Kuna watu wanakufaa kwa dhiki Leo ila Kesho wakutumikishe Kuwa makini sana.

Mwanangu, kuwa makini sana na mahusiano yako ya kimapenzi maana yanagusa hisia zako na mtu unayehusiana naye moja kwa moja. Hivyo basi kuwa makini maana mahusiano hayo yanaweza kukufanya Kesho ukamkosesha raha utakayekuwa naye kama sio huyo uliyenaye leo ndie ukajaaliwa Kuwa naye Kesho. Mwanangu, Unaweza kuniona mshamba sababu ulimwengu wenu unaonekana kama haujali sana haya mambo ila tafadhari zingatia utakapofika Kesho utaelewa sana hiki ninachokuambia.

Mwanangu, jichunge sana na mambo unayoyafanya Leo na uwe muungwana na kupenda haki. Tamaa isikupeleke ukafanya mambo mabaya ambayo yatakulazimisha kutunza siri moyoni mwako hata kama utafika ile Kesho yako. Jiepushe kabisa na mambo mabaya ya siri ya nafsi. Hakuna utumwa mbaya kama utumwa ndani ya nafsi yako mwenyewe maana kila ukikumbuka nafsi itakusuta na kukukosesha raha ya kweli. Hivyo kubali na kuridhika na ulivyo kama huwezi kujiongeza kwa njia halali na za haki. Ni heri uwe masikini mwenye uhuru ndani kuliko uwe tajiri na maarufu mwenye siri mbaya ndani ya Moyo wako. Mwanangu tafadhari uwe makini sana.

Mwanangu, siwezi sahau kukwambia kuhusu Mungu. Maisha ya uchaji wa Mungu yatakuepusha na mengi. Hapa naomba unielewe kwamba usijifanye unamcha Mungu bali mche Mungu. Sio kwasababu unashida ya kufanikiwa ndio umche Mungu, hapana! Bali umche Mungu sababu ni Mungu na yeye ndiye anaijua Kesho yako vizuri kuliko wewe mwenyewe. Ukimshirikisha mambo yako na ukawa mwaminifu kwake hakika hatakuacha kamwe.

Mwanangu, usiku umeenda nenda kalale sasa ila usije ukapenda na kutamani waovu kwa uovu wao na wakakushawishi ujiunge nao. Tafadhari usikubali.

#Kizazi Ganzi#

JIFUNZE KUJIFUNZA

Mwl Makwaya
Kuwa Ni Kufanya.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Huyu jamaa bonge la bwege, ungekua wewe ndiyo rafiki ake ungemwambiaje?

RAFIKI: Vipi mbona leo huna uchangamfu
JAMAA: Wanawake bwana, mwanamke hata umpendeje atakugeuka tu
RAFIKI: Nini tena ndugu yangu? Mbona shemeji mtu fresh sana
JAMAA: Hata mimi nilikuwa najua hivyo, leo nimegundua kumbe ana siri kubwa sana
ananificha, mi naita huu ni usaliti wa ndoa.
RAFIKI: Nini tena?

JAMAA:Nimegundua mke wangu kumbe anafanya biashara ya kitimoto na hajawahi hata kuniambia
RAFIKI: Kitimoto? We umejuaje?
JAMAA: Leo asubuhi nilichelewa kuamka niliamua nijipumzishe kidogo kabla ya kwenda kazini, simu ya mke wangu ikalia, nikaamua kuipokea, kabla hata sijafungua mdomo, nikasikia sauti ya mwanaume mmoja akauliza, “Huyo nguruwe umeshamuondoa?’ Hebu we fikiria nilivyoshtuka, yaani mpaka sasa nashindwa kuamini kuwa mke wangu ananizunguka anafanya biashara ya nguruwe hajaniambia hata siku moja

Angalia sababu ya mwanamme kubadili jina na Kuitwa jina la kike, hii dunia ina mambo kweli

Rashidi alimpa ujauzito mwanafunzi, akashtakiwa.
Kumbe Rashidi ana bibi yake mtaalamu wa yale mambo yao ya Sumbawanga, akampachika Rashidi i jinsia ya kike.

Alipofika mahakamani kuhojiwa Rashidi akasema sijampa ujauzito kwa sababu mimi pia nina jinsia ya kike.
Kwa kuthibitisha Rashid wakaenda kumkagua basi akashinda kesi, kufika nyumbani Rashid akawakuta watu wamejaa wanalia, akauliza kulikoni?
Akaambiwa bibi yako amefariki. 😭😭😭😭😭😭😰😰😰😆😆😆😆😆😆
Kwa sasa Rashid anaitwa Leila😀😀😀

Mambo usiyoyajua kuhusu ugonjwa wa Pumu

Asthma /pumu ni ugonjwa sugu ambao huathiri njia ya hewa ambazo huingiza na kutoa hewa katika mapafu, pia hufanya kuta za ndani ya njia ya hewa kuvimba na hivyo hupunguza kiasi cha hewa kinachoingia na kutoka ktk mapafu, Hali hii husababisha mgonjwa kutoa mlio kama wa filimbi/mluzi wakati wa kupumua, kifua kubana, kushindwa kupumua vizuri na kukohoa sana, watu wa pumu huwa na dalil hizo nyakat za usiku na asubuhi sana pia ugonjwa huu huwaathiri watu wa Rika zote ingawaje Mara nying huwaathiri watoto kwa sababu huanza utoton na hivyo takriban MILION 6 ya watoto wanaumwa pumu na watu takriban 255,000 hufa kila mwaka kwa ugonjwa huu.

KUNA AINA NYINGI ZA PUMU

1 ~PUMU YA UTOTONI (CHILD_ONSET ASTHMA)

Hii ni aina ya pumu inayotokea baada ya mtoto kuzaliwa na kupata mzio (aleji) ambayo hupatkana katika vumbi la wadudu kama mende, pia manyoya ya wanyama kama paka, mbwa pia kutumia baby wipe zenye harufu na sabun zenye harufu kwa watoto huwa ni hatari.
Pumu hii hutokea kwa kuwa mwil wa mtoto hutengeneza Kinga ya mwil (ANTIBODIES) za IgE zinazosababisha pumu.
Ugonjwa wa pumu ni sugu sana kwa watoto wanaozaliwa na uzito mdogo wenye asili ya kiafrka pia pumu ya utotoni huwaathiri Zaidi watoto wa kiume.

2 ~PUMU YA UKUBWANI (ADULT_ONSET ASTHMA)

Pumu hii huanza baada ya kufika miaka 20, PUMU hii huathiri Zaid wanawake kuliko wanaume na pia haitokei sana kama pumu ya utotoni, Vizio pia husababisha aina hii ya pumu kwa asilmia kubwa sana

3~PUMU ITOKANAYO NA MAZOEZ (EXERCISE INDUCED ASTHMA).

Ikiwa utatokewa na Hali ya kukosa pumzi wakati wa mazoez au baada ya mazoezi inawezekana una pumu inayosababishwa na mazoezi pia hata kama sio mwanamichezo kukimbia kwa Kasi angalau dk 10 kunaweza kusababisha kukosa pumzi kwa muda mrefu.

4~PUMU ITOKANAYO NA KUKOHOA (COUGH INDUCED ASTHMA).

Hii ni aina ya pumu iliyo ngumu kwa baadhi ya madaktari kuigundua kwa sababu katika pumu hii inawezekana isitokee hata dalil zingine Zaidi ya kukohoa tu hvyo madaktari wanalazimka kuchunguza Zaidi sababu zingne za kukohoa sana na kuhakiksha sio zinazosababishwa na kukohoa huko.

5~PUMU ITOKANAYO NA KAZI (OCCUPATIONAL ASTHMA)

Aina hii ya pumu humtokea mtu akiwa mahali anapofanya Kazi pia huwatokea sana watumish wa viwandani ambapo kuna Moshi na gesi ya nitrogen oxide.

6~PUMU YA USIKU (NOCTURNAL ASTHMA)

Pumu hii hutokea Kati ya saa sita usiku na saa 2 asubuhi, pumu hii huamshwa na vumbi, harufu za pafyum, harufu za rangi za nyumba na vinyes vya wanyama pia Mara nying wagonjwa wa pumu hii hushtuka usingizini wakat wa usiku wa manane baada ya kukosa pumzi.

7~PUMU KALI ISIYOKUBALI STEROID(SEVERE ASTHMA /STEROIDAL RESISTANT ASTHMA).

Wakat wagonjwa wengi wakipata nafuu baada ya kupata steroid wachache hawapati unafuu na hvyo kuhitaj matibabu makubwa Zaidi.

JE UNAJUA CHANZO CHA PUMU??

Visababishi vya pumu havijulikani waziwazi ila vitu vinavyochangia pumu ni VIZIO mfano MOSHI WA SIGARA, BANGI, GESI, GARI NA KEMIKALI pia kila mgonjwa wa pumu ana mzio, Zaid ya 25%hupatwa na mafua yanayosababishwa na mzio (HIGH FEVER /ALLERGIC RHINITIS) na kuwashwa macho (ALLERGIC CONJUCTIVITY) pia wanaweza kupata pumu.

Pia mzio unaweza kusababishwa na antibodies zilizo ndani ya damu zinazopelekea njia ya hewa kuvimba na kusababisha pumu, pia Moshi wa SIGARA, MARASHI, NK husababisha pumu pia watu wazima wenye uzito unaozid vimo vyao yaani BMI Kat ya 25 na 30 na wanaopata pumu ukilinganisha na wenye mwili mkubwa pia watoto waliozaliwa kwa njia ya upasuaj na Zaidi watu walio katika stress na pia tatizo la ngozi linalosababishwa na mzio /allergc (ECZEMA /ATOPIC DERMATITIS au pumu ya ngozi ni hatar ktk jamii yetu.

DALILI ZA PUMU

Sio watu wote wenye pumu Wana Dalili HIZI na pia sio watu wote wenye Dalili hizi wana pumu.

~KUKOHOA SANA
~KUTOA SAUTI KAMA YA MLUZI /FILIMBI WAKAT WA KUPUMUA
~KUBANWA NA KIFUA
~KUPUNGUKIWA PUMZI

JINSI YA KUTIBU NA KUJIKINGA NA PUMU

~kuna aina mbil za matibabu ya pumu moja ni ya dawa ambayo husaidia kutanua njia za hewa ambazo zimesinyaa (BRONCHOPDILATORS) pia na matibabu mengine ni kutumia dawa za kotikosteroid za kuvuta (INHALED CORTICOSTEROIDS) ila kwa kawaida matibabu haya huwa chanzo cha magonjwa mbalmbal kutokana na dawa za kemikal hivyo si nzur sana.

NJIA YA KUJIKINGA NA PUMU

NI KUJIKINGA NA Vitu vyenye mzio Kama vile PERFUME, DAWA ZA KEMIKAL, RANGI ZA NYUMBA, KUVUTA SIGARA, PIA EPUKA KUNYWA POMBE NA KUCHEZA NA WANYAMA KAMA PAKA NA MBWA PIA WAZAZI MUACHE KUTUMIA BABY WIPES ZENYE HARUFU KWA WATOTO WENU.

Shopping Cart
2
    2
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About