SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Mambo 7 ambayo mwanamme hapaswi kumfanyia mke wake

Mambo 7 ambayo mwanaume apaswi kumfanyia mke wake..
1. Usimpige.
2. Usimtukane na kumshushia heshima.

3. Usimfanye ajihisi hapendwi na anamkosi.
4. Usimbake.
5. Usimsaliti na kujionyesha kabisa kwamba una saliti.
6. Msikilize pale anapokua na stress, mpe muda wako, mkumbatie na mpe maneno ya faraja.
7. Mpe zawadi, hata kama ni ndogo kiasi gani kwake ni alama tosha.

Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE ili kuwafahamu zaidi Wanawake

Mume alichomjibu mchepuko wa mke wake

😎 Jamaa kamuaga mkewe anaenda semina Songea kwa wiki nzima kumbe kahamia kwa demu nyumba ya pili toka kwake. Siku ya 1 kalala asubuhi alipoamka kachungulia kwake kukoje,

Si kamuona jamaa yuko nje ya nyumba yake kavaa taulo lake anapiga mswaki. Akapiga kelele, ‘We nani?’, Jamaa akajibu, ‘Mshikaji mambo ya mjini, mume wa huyu demu kasafiri kaenda Songea mi ndo najivinjari hapa’. Mume kajibu kwa uchungu, Shenzi mkubwa, ngoja nirudi toka Songea nakuua.😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆

*Mniache mimi sipendi Ujinga Ujinga 🏃�🏃�🏃�🏃

Ujumbe mzuri wa kuamsha mapenzi kwa mtu

Kulikuwa na vipepeo wawili waliokuwa wanapendana sana, siku 1 waliamua kucheza mchezo wa mahaba. Waliweka ua na walipanga kesho ambaye atakuja mapema na kukaa juu ya UA, atakuwa anampenda mwenzake zaidi. Asubuhi kipepeo dume alienda mapema sana na kukaa juu ya UA. Masikini kumbe jike alifika tangu jana kumwonesha mpenzi wake ni jinsi gani anavyompenda…!! Jee…!! wewe, utamuonesha nini umpendaye ili aone ni kiac gani …………………….

Athari za Moshi wa sigara kwa mtoto

Utafiti uliofanyika nchini Marekani umebaini kwamba watu wazima wasiovuta sigara lakini walipokuwa watoto wazazi wao walivuta sigara mbele yao,wana hatari kubwa zaidi ya kufa kutokana na maradhi ya mapafu.

Watafiti wanasema kati ya watu laki moja ,watu saba hufa kila mwaka kutokana na madhara ya sigara waliyoyapata wakiwa watoto.

Watalamu wanasema kinga bora zaidi ya kuzuia watoto kutoathirika na sigara ni wazazi kuacha kuvutaji sigara kabisa.

Aidha utafiti huo umebainisha kwamba sio watoto peke yake ndio wanaweza kuathiriwa na sigara bali hata mtu mzima ambaye havuti sigara lakini anaishi au anakuwa karibu na mtu anayevuta sigara.

Moshi wa sigara wa saa 10 au zaidi kwa kila wiki unaongeza hatari ya vifo vya ugonjwa wa moyo kwa asilimia 27,kupooza kwa asilimia 23 na madhara katika mapafu kwa asilimia 42 ukilinganisha na wale ambao wanaishi na watu wasiovuta sigara.

Utafitit huu ambao umechapishwa kwenye jarida la ‘ Preventive Medicine’ uliwauliza watu kuhusu uvutaji sigara katika maisha yao na wanayaangaliaje maisha yao baada ya miaka 22.

Kumekuwa na kampeni ya kuwazuia watu kuvuta sigara katika maeneo ya ndani ili watoto au watu wasiovuta wasiathirike lakini maeneo maalum ya kuvuta sigara yanaonekana kuwa ni machace bado na njia pekee inayoweza kusaidia madhara yasiwepo ni watu kuacha kabisa uvutwaji sigara.

Dr Nick Hopkinson ambaye ni mshauri wa masuala ya afya kutoka taasisi ya mapafu nchini Uingereza ‘the British Lung Foundation, agreed, saying’ anasema kuwa kuna madhara makubwa ambayo mtoto anaweza kuyapata anapovuta moshi wa sigara.

Ni vyema kwa wazazi ambao wana watoto wadogo au wanawake wajawazito kupata msaada wa kuacha kuvuta sigara.

Sigara ina madhara yanayohatarisha Maisha
Watoto ambao wazazi wao wanavuta sigara wapo katika hatari kubwa zaidi ya kupata mangojwa kama ya pumu na athari katika mapafu. Utafiti unaonesha kuwa madhara ya uvutaji wa sigara kwa watoto uonekana pale anapokuwa mtu mzima.

Vilevile madhara ya sigara yanaweza kusababisha ongezeko la magonjwa sugu na maisha ya utegemezi hapo badae.

Sababu ya meno kubadilika rangi

Wapo baadhi ya watu wanashindwa hata kuachia kicheko chenye bashasha hii ni kwa sababu meno yao yamekuwa na rangi, hivyo kuwafanya watu hao kuona aiabu. Pia watu wengi wakiona meno yana rangi ya njano hudhani ni machafu, meusi yanahitaji kusafishwa ili yawe meupe.

Meno kubadilika rangi huweza kuwa ni sababu moja au muunganiko wa sababu mbalimbali kama ifuatavyo;

Matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye kaboni, sigara na mvinyo (wine) kwa muda mrefu husababisha kubadilika kwa rangi ya meno kwa juu (extrinsic staining).

Utumiaji wa maji yenye madini mengi ya fluoride katika kipindi cha utoto (dental fluorosis).

Matumizi ya dawa aina ya tetracycline kwa mama mjamzito ambaye tayari meno ya mtoto aliye tumboni yameanza kuumbwa lakini hayapata madini ya kutosha.

Maumbile yasiyo sahihi ya sehemu ya juu ya jino (amelogenesis imperfecta). Iwapo sehemu hii imeumbwa ikiwa laini kuliko inavyotakiwa huwa rahisi kufyonza rangi na jino huota likiwa limebadilika rangi au hubadilika baada ya muda.

Kufa kwa sehemu hai ya jino hasa kutokana na kuumia kwa jino au ajali (pulp necrosis), hali hii huweza huchukua miaka mingi mpaka kutokea kubalika rangi ya jino..

Jino liliozibwa kwa kutumia material aina ya amalgam huweza kubadilika rangi na kuwa nyeusi.

Mara nyingne jino lililotibiwa kwenye mzizi wa jino (root canal treatment ) huweza kubadilika rangi baada ya miaka mingi.

Kuna njia mbalimbali ambazo hutumika kuyafanya meno yaliyo na rangi isiyo ya kawaida kuwa meupe.

Njia hizi hutofautiana kati ya mtu na mtu kutokana na jinsi alivyoathirika. Kuna njia nyingi ambazo huweza kuyang’arisha kwa ndani (internal bleaching) au kuyangarisha kwa nje (external bleaching).

Endapo una tatizo la meno yaliyobadilika rangi, muone daktari wa kinywa na meno kwaajili ya ushauri na matibabu kwani kinywa kizuri na chenye afya huongeza kujiamini.

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia Mtindi na asali

Kutumia mtindi na asali ni moja ya dawa rahisi zaidi za kutibu chunusi.

Unahitaji:

a)Kijiko kimoja cha asali
b)Kijiko kimoja cha mtindi

Hatua kwa hatua namna ya kutumia:

a)Changanya hayo mahitaji yako mawili vizuri
b)Pakaa ple pole mchanganyiko huu kwenye uso wako
c)Ikikauka unapaka tena, hivyo hivyo mpaka umepaka mchanganyiko wote
d)Acha dakika 10 mpaka 15 hivi
e)Mwishoni jisafishe na maji ya uvuguvugu

Ujumbe kwa mabinti kuhusu uvaaji

Familia Kwanza: Wasichana wawili waliwasili kwenye Kikao huku wamevaa nguo ambazo zilikuwa zikionyesha miili yao.

Hiki ndo kitu ambacho Mwenyekiti wa kikao alichowaambia, aliwatazama kwa muonekano mzuri kisha akawataka wakae, kisha akawaambia jambo ambalo hawatoweza kusahau katika Maisha yao.

Aliwaangalia moja kwa moja katika macho yao, kisha akasema;

“Wasichana, kila kitu ambacho MUNGU amekiumba chenye thamani katika Dunia hii kimesitiriwa, na ni vigumu kukiona au kukipata.

1.Wapi unapoipata Almasi?
Ni chini kabisa ndani zaidi katika ardhi, na yamefunikwa na kuhifadhiwa humo

2. Wapi mnapoweza kuipata Lulu? Pia ni ndani zaidi kwenye kina kirefu zaidi katika Bahari, na yamehifadhiwa humo na kujificha ndani ya Sanamu zuri la Baharini

3. Wapi mnapoweza kuipata Dhahabu? napo pia ni ndani zaidi katika Migodi, na yamefunikwa juu na Ardhi za Miamba na ndio uyapate hapo. Yatupasa tufanye kazi ya ziada zaidi na tulime kwa undani zaidi ndipo tuyapate.

Kisha Mwenyekiti akawaangalia wale Mabinti kwa Jicho kali zaidi na kisha akawaambia;
“Miili yenu ni ya kuogopwa na ina thamani sana, na inazidi sana hata thamani ya Dhahabu, Almasi au Lulu. Na yawapasa muihifadhi zaidii.

Kama mtatunza Madini yenu kama ilivyotunzwa Almasi, Dhahabu na Lulu basi Makampuni yenye sifa nzur katika Jamii, Makampuni ya uhakika, Makampuni ya kuaminika yenye Mitambo mizuri yatatenga Muda wa miaka kadhaa katika kufanikisha kuyapata Madini hayo.

Kwanza itawapasa wawasiliane na Serikali (ambayo ndio familia yako) pia kusahihisha Mikatabata muhimu (ndoa) na mwisho ni Mgodi wenye dhana kubwa (ambayo ndiyo ndoa) lakini kama ukiacha madini yako yenye thamani nje hayajahifadhiwa katika uso wa Dunia basi utamvutia kila Mmoja (Mwanaume) na hasa wale ambao ni Wachimbaji haramu watakuja na kuchimba kiharamu (Zinaa), kwa hiyo kila mmoja atachukua kwa vifaa vilivyo na Makali na hivyo ndio watakavyokulima kirahisi.

Hivyo basi nawashauri hifadhini Miili yenu vizuri ili iwavutie wachimbaji wa halali (Waoaji) ndio wakukaribie upate kuheshimika

FUNZO: Maisha ni kuchagua

Siku hizi kuna tangazo moja la kampuni ya simu za mikononi, Tigo, likimuonesha mama akiwa _busy_ na pembeni yupo mwanae mdogo apo akijisemesha na akatamka maneno ambapo mama akaona ni kama ameanza kuongea. Kwa furaha anampigia simu mumewe akimtaka amsikilize mwanae akiongea. Hapo mama anamtaka mwanae aseme “mama” na baba naye anavutia kwake akimtaka aseme “baba”. Kwa maajabu kabisa mtoto anawapotezea wote na kutamka “ni Tigo peesa”. Wazazi wakashikwa na butwaa lakini huku wakitabasamu.

Ukiitazama vizuri kazi ya ubunifu iliyotumika katika tangazo hili unaweza kupata funzo, pamoja na mengine, kwamba mtoto alikua na chaguzi lake ambalo ni tofauti na yale ambayo wazazi walikua wamempa. Lakini zaidi, pamoja na kuwa amekuwa na chaguzi lake binafsi, pasipo kufuata alichoagizwa na baba au mama, bado wazazi wanatabasamu kwani wanaona mwanao kafanya jambo jema.

👉Unaona unavyofanya kazi bila furaha kwa kua ulifanya chaguo la kazi hiyo kwa kusikiliza ndugu au marafiki.

👉Unaona unavyo _struggle_ katika biashara kwani halikua chaguo lako bali ni la ndugu au marafiki

👉Unakumbuka ulivyoshindwa kusomea kile unachopenda kwa kusikiliza ndugu au marafiki
9
👉Unakumbuka ulivyoshindwa kuishi na yule mwenzi uliyempenda na mkapendana naye kwa kusikiliza ndugu na marafiki

Unaweza kushauriwa, na ushauri ukawa ni mzuri kabisaa na ukaona ni vyema uufuate kwa kua hata wewe umeambiwa na ukachanganya na akili yako ukaona inafaa.

Jana nilitoa semina kwa wanafunzi wote wa Shule ya Sekondari Chang’ombe, pamoja na mambo mengine nikawataka kupima sana marafiki walio nao na kuona kama ni washauri wazuri na kama sivyo waachane nao na kuwa na marafiki wapya wenye mawazo chanya ya kuwasaidia kutimiza ndoto zao.

Kuna hii daladala imeandikwa nyuma *_Marafiki wengi mjini hasara_*. 😃. Mie nakuambia sio marafiki tu, hata ndugu pia. Kikubwa ni kuwapima wale ulio nao karibu na kuona kama bado ni wa msaada kwako. Wapime na chukua hatua. Kumbuka Mheshimiwa JK aliwahi kutuasa ” _Akili za kuambiwa, changanya na za kwako_ “.

Jinsi ya Kulima Mgagani: Kilimo bora cha Mgagani

Utangulizi

Migagani, migange, mikabili au miangani ni mimea ya jenasi Cleome katika familia na oda Brassicales (kabichi). Mgagani (Cleome gynandra) au Spider plant kwa kingereza, ni mmea wa asili ya Afrika unaostawi vizuri kwa kumwagiliwa hapa afrika ya mashariki wakati wa joto. Pia huchumwa mashambani ikiwa imeota yenyewe zao hili hushambiliwa na magonjwa na wadudu mara chache. Majani na Matawi machanga yana virutubisho kuliko Sukuma wiki na kabichi. Mahitaji yake yanaongezeka kwenye miji midogo na mikubwa kila siku.

Mgagani wa kawaida, huliwa takriban kila mahali pa Afrika na katika mabara mengine pia. Wanawake wengi wenye mimba au waliozaa hula mmea huu, kwa sababu una chuma nyingi kiasi na husaidia kuongeza damu. Mboga ya mgagani huitwa magagani.

Aina Za Mgagani

Kwa Afrika kuna aina 50 za mgagani , lakini ni aina nne tu zinazoliwa. Aina bora zinazalishwa na kituo cha AVRDC-THE WORLD VEGETABLE CENTER zina majani mapana, uchungu kidogo na ina majani mengi Zaidi na huvunwa kwa muda mrefu. Aina hizi ni pamoja na PS ambayo ina shina na matawi ya zambarau na GS I yenye shina na matawi ya kijani, mbegu za aina bora zina weza kupatikana toka kwenye kituo cha the world Vegetable Center, Arusha Tanzania. Ikumbukwe kuwa wakilima wengi wa nchi za Tanzania na kenya wanalima na kuuza mbegu za aina hizi na pia baadhi ya makampuni ya mbegu yameanza kuuza.

Mazingira Mgagani Unapoota

Kwa asili mgagani unastawi vizuri sehemu zenye joto na udongo wa aina mbalimbali kama tifutifu. Zao hili halikui vizuri katika udongo unaotuamisha maji, au katika maeneo ya baridi au kivuli. Katika eneo la mita za mraba 1-2, familia inaweza kupata mgagani wa kula kwa muda wa miezi minne.

 


Kutayarisha Shamba La Kuotesha Mgagani

Anza kwa kutifua ardhi vizuri na changanya na mbolea ya samadi kwa kiwango cha kilo moja hadi mbili kwa mita mraba. Mgagani waweza kuoteshwa peke yake au kwa kuchanganywa na mazao mengine kama mnavu au mchicha.

Uoteshaji Wa Mgagani

Baada ya kuandaa shamba lako sia mbegu kwa kutawanya au katika mstari ya umbali wa sm 30-50, majira ya mvua au kwa kumwagilia, kina cha mstari kisizidi sm1, funika kwa udongo kidogo na mwagilia kama hakuna mvua. Punguza miche iliyosongamana inapokuwa na majani manne hadi matano na iwe katika nafasi ya sm 15-20 toka mche hadi mche kwa upandaji wa kutawanya.

Palizi Ya Mgagani

Hakikisha shamba ni Safi hasa mwezi wa kwanza baadae magugu yanaweza kuzuliwa Na kivuli cha mgagani umeota vizuri.

Umwagiliaji Wa Mgagani

Unyevu wa kutosha ni muhimu kwa zao hili na inashauriwa kumwagilia ni majira ya kiangazi angalau mara mbili kwa wiki. Mgagani hustahimili ukame kuliko nyanya au mchicha lakini mimea isiachwe ikanyauka.

Uvunaji Wa Mgagani

Kwa uvunaji wa moja kwa moja mimea inaweza kung’olewa baada ya wiki nne hadi sita, kwa kuvuna majani, uchumaji unaweza kufanyika kila mara hadi miezi minne, Mimea iliyo na umri wa Zaidi ya miezi minne, inaweza kukatwa shina na kuchipua na kuendelea kuvunwa baada ya wiki nne hadi miezi minne kulingana na hali ya hewa na matunzo.

 

Uzalishaji Wa Mbegu Za Mgagani

Kwa kawaida mgagani hutoa mbegu kwenye shina au matawi vifuko vya mbegu vikikauka huwa mbegu imekomaa. Mimea ikatwe usawa wa ardhi na kutungiwa kwenye sakafu. Safi na ngumu, kuondoa mbegu toka kwenye maganda. Ondoa maganda, mashina na majani yaliyochanganyika na mbegu. Uchafu mwingine mbegu zihifadhiwe katika mifuko ya plastiki au ya karatasi au makopo na kuweka sehemu iliyo kavu. Kwa kuwa mbegu zina mafuta ya asili ya dawa za kuua wadudu ni vigumu sana kushambuliwa na wadudu waharibifu.

Mauzo Ya Mbegu Za Mgagani

Makundi ya wakulima yaliyopata mafunzo ya uzalishaji wa mbegu sasa yanazalisha kwa ajili ya wakulima wengine. Katika nchi ya kenya ambapo mgagani unaliwa sana, uzalishaji wa mbegu hupatia wakulima mapato Zaidi kuliko kuzalisha mboga mbegu za mgagani zinaptikana madukani.

Mauzo Ya Mgagani

Matawi malaini na machanga yenye majani yanaweza kuvunwa na kuwekwa kwenye mafungu ya uzito wa gramu 100-200. Majani yaliyo kaushwa kwa jua na kuwekwa kwenye vyombo mbalimbali huuzwa.

Dondoo Muhimu kuhusu ugonjwa wa kisukari

Wapendwa, napenda kushirikiana na nyinyi kujuzana hili nililolisikia kupitia channel ten leo asubuhi kuhusu ugonjwa wa kisukari.
Wataalam waliokua wakitoa mada walikua Prof Endrew Swai na Dr Mohamed Juma.
Kwa ufupi wamesisitiza sana kufanya mazoezi kwa takriban nusu saa kwa siku na ambayo mtu anatoa jasho na moyo kumwenda mbio. Hiyo ni kwa ajili ya kusaidia misuli ya miguu,tumbo kifua, mgongo na mikono kutumia kiasi cha sukari kinachozalishwa mwilini.

Kadhalika wamesisitiza sana kula vyakula visivyokobolewa,ikiwamo kula dona badala ya sembe,ulezi,mtama na matunda.
Watu wapunguze na ikiwezekana kuacha kunywa vimiminika vyenye sukari,ikiwamo juice,soda pombe na vinginevyo. Na hiyo nikwasababu vinywaji hivyo havikai tumboni na badala yake huenda moja kwa moja kwenye utumbo mwembamba na kulazimisha kongosho linalozalisha kemikali ya insulin kufanya kazi kwa kiwango cha juu kuliko ilivyo kawaida.
Vyakula visivyokobolewa vinafaida sana kwani vinachukua muda wa kutosha kutoka kwenye tumbo na kwenda kwenye utumbo mwembamba na hatimaye kuvunjwavunjwa kwa ajili ya kutumika mwilini. Kadhalika makapi yatokanayo na hivyo vyakula hutuzuia kupata kansa ya utumbo. La ajabu wametoa takwimu za kutisha kwani ulaya kwasababu wanakula vyakula vilivyokobolewa wanapata kansa ya utumbo kuliko nchi au bara la afrika,
na kansa hiyo ni ya nne kwa kusababisha vifo barani ulaya na amerika.
Tafadhalini tujihadharini kwani mada ilikua ndefu na nzuri sana kwa mustakabali wetu na afya zetu.
1.Mazoezi ni muhimu
2.Vyakula viwe na uasilia wake
3.Mtu aliye na mwenza wake afanye tendo la ndoa kwa kadiri inavyowezekana kwani ni sehemu ya mazoezi
4. Tubadili mifumo ya maisha yetu,kukaa tu bila kuishughulisha miili yetu.
Atakayeona anataka kupata elimu zaidi hao madaktari niliowataja wapo hospitali ya muhimbili kitengo cha tiba ya kisukari.
Ufahamu juu ya afya yako binafsi …nimeikuta sehemu 👆👆👆👆👆👆

Hii ndiyo bongo sasa!!

Hii ndio Bongo

Ilikuwa Ijumaa mida ya saa 10 jioni, mzee mmoja aliingia na kibinti kizuri kwenye yard ya magari mapya.

MZEE: Chagua gari unalotaka mpenzi….kabinti akazunguka yard yote mwisho akachagua Verrosa metallic .

BINTI: Mi naitaka hii

MZEE: Hakuna tatizo kabisaaa, mtoto mzuri kama wewe lazima upate gari uloichagua mwenyewe. Mzee akatoa kitabu cha cheki na kuandika palepale na kumpa mwenye yard

MUUZAJI: Sasa Mzee kwa kuwa umetoa cheki, gari utakuja chukua Jumatatu tukishahakikisha kuwa Account yako ina pesa benki. Naomba namba yako ya simu Mzee

MZEE: Hakuna tatizo (akampa namba). Haya twende zetu sweetie Jumatatu tunakuja wote kuchukua gari lako…

Siku ya Jumatatu mwenye yard kampigia simu Mzee.

MUUZAJI: We Mzee kavu sana, akaunti yako haina hata senti tano.

MZEE: Hilo nilijua, lakini wiki endi yangu ilikuwa tamu sana.

💦😆💦

Alichofanya maasai baada ya kupanda Tax

Baada ya kupanda daladala aina ya DSM kutoka Mbagala chalambe mpaka Mwenge na kulipa sh 500.Masai akachukua tax wakati wa kurudi.walipofika sasa shughuli ilikuwa hivi.

Masai: we dureva? Naulisa Ng’ombe na mbusi ipi ngali?
Dereva: Ni ng’ombe ghali Masai.
Masai: kwanini Ng’ombe ngali?
Dereva: kwa sababu ni mkubwa zaidi ya mbuzi
Masai: umepata..na mbusi na kuku ipi ngali
Dereva: ni mbuzi kwa sababu nae ni mkubwa kuliko kuku.
Masai: Umepata..
Masai: sasa me nimekwenda kule mwenge kwa ngali kubwa nikalitoa sh. 500 hii yko ndogo unasema nikupe 40,000 wewe acha wizi.. Nitakupa 250 Tu..wee acha lbia morani…!!!

Dunia haijali mazuri yako ila ubaya wako, jiamini songa mbele

Siku moja mwalimu wa shule aliandika ubaoni kama ifuatavyo:
9×1=7
9×2=18
9×3=27
9×4=36
9×5=45
9×6=54
9×7=63
9×8=72
9×9=81
9×10=90
Alipo maliza kuandika tu, akaona wanafunzi wote walikua wanamcheka, kwasababu alikua amekosea swali la kwanza.

Mwalimu aliwatazama wanafunzi, kisha akawaambia yafuatayo:
`”Nimejikosesha lile swali la kwanza makusudi, kwasababu nilihitaji mjifunze kitu kimoja muhimu sana. Mnapaswa kujua namna ambavyo dunia inaweza kuwachukulia. Unaona hapo, nimeandika kwa usahihi mswali tisa (9), lakini hakuna kati yenu aliyenipongeza kwa hilo; wote mmecheka na kunilaumu kwasababu ya kosa moja tu nililofanya.”`
Hivyo, hili ni somo kwenu:
`”Dunia haijali mazuri unayofanya hata ukiyafanya mara milioni, lakini fanya baya moja uone jinsi watakavyo kulaumu…”`
“`Hata hivyo usikatetamaa, MARA ZOTE SIMAMA IMARA NA USHINDE VIKWAZO VYOTE.” `
JIAMINI

Kushindwa au vikwazo sio sababu ya kutofanikiwa

“Nilibakwa nikiwa na miaka 9 lakini leo mimi ni mmoja wa wanawake wenye ushawishi mkubwa duniani”- OPRAH WINFREY!

“Sikumaliza elimu yangu ya Chuo Kikuu lakini mimi ndiye binadamu tajiri kuliko wote duniani” – BILL GATES!

“Nilikuwa napata matokeo mabaya sana darasani wakati nilipokuwa shule ya msingi lakini bado mimi ni Daktari Bingwa wa Upasuaji duniani” – DR. BEN CARSON!

“Nilimwambia baba yangu tutakuwa na mali na utajiri mkubwa lakini hakuamini, leo hiyo ndiyo hali halisi”
– CHRISTIANO RONALDO!

“Nilikuwa mhudumu kwenye mgawahawa wa chai ili kulipia ada za mafunzo yangu ya mpira lakini leo mimi ni mchezaji bora wa dunia” – LIONEL MESSI!

“Nilikuwa nalala chini kwenye vyumba vya marafiki zangu, natafuta chupa tupu za soda nipate chakula, pesa na mlo wa bure wa kila wiki lakini bado mimi ndiye mwanzilishi wa APPLE” – STEVE JOBS!

“Walimu wangu waliniita mwanafunzi mjinga na asiyejiweza lakini bado nimekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza” – TONY BLAIR!

“Niliendesha TAKSI ili kulipia ada yangu Chuo Kikuu lakini leo mimi ni Bilionea” – MIKE ADENUGA!

#NOTE: Kushindwa au Vikwazo vya nyuma ni mambo yasiyo na nafasi kwa UWEZO mkubwa uliomo ndani yako. Kwa mtu anayeamini, kila kitu kinawezekana. Ni tunu ulizonazo na talent ulizopewa ndizo ufunguo wa maisha yako. Usiende kukopa shaba kwa jirani wakati umeacha dhahabu nyumbani kwako, tumia dhahabu zako

Cheki masifa yalivyomponza huyu, Sifa nyingine ni mbaya jamani

Mbongo, Mganda, na Mkenya walikamatwa na makosa Uchina.

Wakaambiwa adhabu ni ama kifo cha moja kwa moja au adhabu nyingine ambayo atakayeifaulu atakuwa huru, atakayeshindwa atauawa.

Basi wao wakaomba wapewe hiyo adhabu nyingine wajaribu bahati yao.

Wakapelekwa msituni wakaambiwa kila mmoja aende kwa njia yake halafu arudi na matunda kumi ya kufanana.

Wakaingia msituni kila mtu njia yake.

… Mganda akarudi wa kwanza na machungwa kumi. Akaambiwa adhabu yake ni kumeza moja moja likiwa zima bila kufumba macho bila kulia wala kucheka wala kujitikisa mpaka yote kumi yaishe. Akameza la kwanza. Safi. Kumeza la pili, akashindwa kuvumilia akafumba macho. Akapigiwa risasi akafa.

Mkenya akaja. Ana vitunda vidogo vidogo kama pili vilaini. Akasomewa masharti. Akaanza kumeza bila kufumba macho wala kulia, wala nini… alipofika cha tisa akashindwa kuvumilia akaangua kicheko! Akapigwa risasi pia akafa.

Wakiwa kuzimu Mganda akamwuliza Mkenya, “Vipi, mbona ulishindwa kuvumilia wakati kilibaki kitunda kimoja tu?”

Mkenya akamjibu: “Mkuu, nilishindwa kuzuia kicheko maana nilimwona Mbongo anakuja na matikiti maji!”

Hii ndio ndoto ya harusi ya kila msichana anayotamani

GIRL: Baby, hebu niambie harusi yetu itakuwaje?
BOY: Yaani hii haijawahi kushuhudiwa, ngoja nikupe kionjo kidogo tu
GIRL: Enhee…
BOY: Kwanza siku ya kupeleka mahari nitaswaga zizi zima la ng’ombe napeleka kwa babu yako
GIRL: Ooh baby u care..
BOY: Siyo hivyo tu, baba yako ntamnunulia Range Rover Sport na mama mkwe ntampa Range Rover Evoque
GIRL: Baby u are awesome…
BOY: Halagu mdogo wako wa kiume ntampa Prado Tx, na hapo nimesukutua tu mdomo sijaanza kula….
GIRL: Enhee…na sisi??

BOY: Sisi tutachukua mtaa mzima Oysterbay, kila wiki tutaishi nyumba tofauti
Halafu siku ya harusi yetu tutakodi zile meli zinabeba makontena ndiyo iwe ukumbi wetu, itatupeleka hadi Maldives
GIRL: Baby I love you
BOY: Tukitoka hapo tunaenda honeymoon Bahamas….halafu tunaenda Taiwan shopping ya fenicha, kisha Japan shopping ua electronics, halafu tunaenda Dubai nikununulie vito vya thamani
GIRL: Ooh my sweetheart…halafu tukitoka huko??
BOY: Tukitoka huko nachukua ndoo ya maji nakumwagia uzinduke usingizini na ndoto yako imeishia hapo

Shopping Cart
2
    2
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About