SOMO 1
Mdo. 2:1-11
Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? Waparthi na Wamedi na Waelani, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATI KATI
Zab. 104:1, 24, 29-31, 34, (K) 30
(K) Waipeleka roho yako, Ee Bwana, Nawe waufanya upya uso wa nchi. au: Aleluya.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
Wewe, Bwana, Mungu wangu,
Umejifanya mkuu sana;
Ee Bwana, jinsi yalivyo mengi matendo yako!
Dunia imejaa mali zako. (K)
Waiondoa pumzi yao, wanakufa,
Na kuyarudia mavumbi yao,
Waipeleka roho yako, wanaumbwa,
Nawe waufanya upya uso wa nchi. (K)
Utukufu wa Bwana na udumu milele;
Bwana na ayafurahie matendo yake.
Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake;
Mimi nitamfurahia Bwana. (K)
SOMO 2
1 Kor. 12 :3b-7, 12-13
Hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu
SHANGILIO
Aleluya, aleluya,
Uje Roho Mtakatifu, uzienee nyoyo za waamini wako uwatie mapendo yako.
Aleluya.
INJILI
Yn. 20 :19-23
Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu. Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana.
Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Rehema zake hudumu milele
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu akubariki!
Rehema hushinda hukumu
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Nakuombea 🙏
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Nguvu hutoka kwa Bwana
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Sifa kwa Bwana!
Mungu ni mwema, wakati wote!
Baraka kwako na familia yako.
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Neema na amani iwe nawe.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mwamini Bwana; anajua njia
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Dumu katika Bwana.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Imani inaweza kusogeza milima
Endelea kuwa na imani!
Katika imani, yote yanawezekana
Tumaini ni nanga ya roho
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mwamini katika mpango wake.
Neema ya Mungu inatosha kwako
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu