SOMO 1
Kum. 8:2-3;14-16
Musa aliwaambia makutano: Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu, kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa; aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 147:12-15,19-20 (K) 12
(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.
Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)
Ndiye afanyaye amani mipakani mwako,
Akushibishaye kwa unono wa ngano.
Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana. (K)
Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua.
aleluya. (K)
SOMO 2
1Kor. 10:16-17
Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANG1LIO
Yn. 6:51
Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; asema Bwana; mtu akila chakula hiki, ataishi milele.
Aleluya.
INJILI
Yn. 6:51-58
Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule? Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuwa na imani!
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Tumaini ni nanga ya roho
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mungu akubariki!
Nguvu hutoka kwa Bwana
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Nakuombea 🙏
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Sifa kwa Bwana!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Dumu katika Bwana.
Mwamini Bwana; anajua njia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Baraka kwako na familia yako.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema zake hudumu milele
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Imani inaweza kusogeza milima
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Neema na amani iwe nawe.
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema hushinda hukumu
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Mungu ni mwema, wakati wote!
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mwamini katika mpango wake.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia