MWANZO:
Mdo. 1:11
Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Atakuja vivyo hivyo mlivyomwona akienda zake mbinguni, Aleluya.
SOMO 1
Mdo. 1:1-11
Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua; wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu. Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohane alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.
Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 47 : 1-2, 5-6, 7-8, (K) 5
(K) Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu. au: Aleluya
Enyi watu wote, pigeni makofi,
Mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe,
Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya,
Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote. (K)
Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
Bwana kwa sauti ya baragumu.
Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;
Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni. (K)
Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,
Imbeni kwa akili.
Mungu awamiliki mataifa,
Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu. (K)
SOMO 2
Efe 1 : 17-23
Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Mt. 28:19-20
Aleluya, aleluya,
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote.
Aleluya.
INJILI
Mt. 28:16-20
Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka. Yesu akaja kwao, akasema nao, akawambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Rehema zake hudumu milele
Rehema hushinda hukumu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mwamini Bwana; anajua njia
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Tumaini ni nanga ya roho
Dumu katika Bwana.
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Nakuombea 🙏
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Neema na amani iwe nawe.
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu ni mwema, wakati wote!
Sifa kwa Bwana!
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu akubariki!
Katika imani, yote yanawezekana
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Endelea kuwa na imani!
Mwamini katika mpango wake.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Imani inaweza kusogeza milima
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Baraka kwako na familia yako.
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia