SOMO 1
Eze. 37:21 – 28
Bwana Mungu asema hivi: Tazama, nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe; nami nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo, juu ya milima ya Israeli; na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote; wala hawatakuwa tena mataifa mawili, wala hawatagawanyikana kuwa falme mbili tena, hata milele. Wala hawatajitia uchafu tena kwa vinyago vyao, wala kwa vitu vyao vichukizavyo, wala kwa makosa yao mmojawapo; lakini nitawaokoa, na kuwatoa katika makao yao yote, ambayo wamefanya dhambi ndani yake, nami nitawatakasa; basi watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao. Na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja; nao wataenenda katika hukumu zangu, na kuzishika amri zangu, na kuzitenda. Nao watakaa katika nchi niliyompa Yakobo, mtumishi wangu, walimokaa baba zenu; nao watakaa humo, wao na watoto wao, na watoto wa watoto wao, milele; na Daudi, mtumishi wangu, atakuwa mkuu wao milele. Tena nitafanya agano la Amani pamoja nao; litakuwa agano la milele pamoja nao; naami nitaweka na kuwazidisha, na patakatifu pangu nitapaweka katikati yao milele. Tena maskani yangu itakuwa pamoja nao; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Na mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, mimi niwatakasaye Israeli, patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao milele.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Yer. 31:10 – 13 (K) 10
(K) Bwana anatulinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.
Lisikieni neno la Bwana, enyi mataifa,
Litangazeni visiwani mbali;
Mkaseme: Aliyemtawanya Israeli atamkusanya,
Na kumlinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.
Kwa maana Bwana amemweka huru Yakobo,
Amemkomboa mkononi mwake aliyekuwa hodari kuliko yeye. (K)
Watakuja na kuimba katika mlima Sayuni.
Wataukimbilia wema wa Bwana,
Nafaka, na divai, na mafuta,
Na wachanga wa kondoo na wa ng’ombe. (K)
Ndipo bikira atafurahi katika kucheza,
Na vijana na wazee pamoja;
Maana nitageuza masikitiko yao kuwa furaha,
Nami nitawafariji, na kuwafurahisha waache huzuni zao. (K)
SHANGILIO
Zab. 95:8 , 9
Leo msifanye migumu mioyo yenu, lakini msikie sauti yake Bwana.
INJILI
Yn. 11:45 – 57
Wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Maria, na kuyaona yale aliyoyafanya Yesu, wakamwamini. Lakini wengine wakaenda zao kwa Mafarisayo, wakawaambia aliyoyafanya.
Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi. Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja watamuondolea mahali petu na taifa letu. Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lolote; wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima. Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo, wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili waawe wamoja. Basi tangu siku ile walifanya shauri la kumwua.
Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; na wengi wakakwea toka mashambani kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka, ili wajitakase. Basi wao wakamtafuta Yesu, wakasemezana hali wamesimama hekaluni, Mwaonaje? Haji kabisa sikukuu hii? Na wakuu wa makuhani wa Mafarisayo walikuwa wametoa amri ya kwamba mtu akijua alipo, alete habari, ili wapate kumkamata.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Mungu ni mwema, wakati wote!
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Tumaini ni nanga ya roho
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Endelea kuwa na imani!
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Katika imani, yote yanawezekana
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Neema na amani iwe nawe.
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mwamini Bwana; anajua njia
Nakuombea 🙏
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu akubariki!
Rehema hushinda hukumu
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Dumu katika Bwana.
Sifa kwa Bwana!
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Baraka kwako na familia yako.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Nguvu hutoka kwa Bwana
Imani inaweza kusogeza milima
Rehema zake hudumu milele