SOMO 1
Hos. 5:15-6:6
Bwana asema: Katika taabu yao watanitafuta kwa bidii:
Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tuataishi mbele zake. Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyeshayo nchi.
Ee Efraimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni kama wingu la asubuhi na kama umande utowekao mapema. Kwa sababu hiyo nimewakata-kata kwa vinya vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa change na hukumu yangu itatokea kama mwanga. Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 51:1-2, 16-19 (K) Hos. 6:6
(K) Ninavyotaka ni fadhili, si sadaka.
Ee Mungu, unirehemu,
Sawasawa na fadhili zako.
Kiasi cha wingi wa rehema zako,
Uyafute makosa yangu.
Unioshe kabisa na uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu. (K)
Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,
Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
Dhabihu za MUngu ni roho iliyovunjika;
Moyo uliovunjika na kupondeka,
Ee Mungu, hutaudharau. (K)
Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,
Uzijenge kuta za Yerusalemu.
Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,
Na sadaka za kuteketezwa, na kafara. (K)
SHANGILIO
Eze. 18:3
Tupilieni mbali nanyi makosa yenu yote mliyoyakosa yote, asema Bwana, jifanyieni moy mpya na roho mpya.
INJILI
Lk. 18:9-14
Yesu aliwaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mpato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Dumu katika Bwana.
Endelea kuwa na imani!
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Nakuombea 🙏
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema zake hudumu milele
Baraka kwako na familia yako.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu akubariki!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Neema na amani iwe nawe.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Sifa kwa Bwana!
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Neema ya Mungu inatosha kwako
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Mungu ni mwema, wakati wote!
Tumaini ni nanga ya roho
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Rehema hushinda hukumu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mwamini Bwana; anajua njia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mwamini katika mpango wake.
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako