Hapo Mwanzo Mungu aliumba Malaika katika hali ya njema na Heri kubwa. Kisha aliumba mbingu na nchi, na viumbe vyote vinavyoonekana na visivyoonekena. (Kol, 1;16, Mwa, 1;31)
Malaika ni viumbe vilivyo Roho tuu vyenye akili na utashi. (Zab 91:11, Ebr 1:7, Uf, 12:7-9).
Malaika wengine walikosa kwa kumkaidi Mungu, wakatupwa motoni na ndio Mashetani ambao Mkubwa wao ni Lusiferi. (Yn, 8:44: Uf 12:7-9,).
Mungu aliumba Malaika ili Wamtukuze, Wafurahi nae Mbinguni na wawe Matarishi/wajumbe wake kwa Wanadamu. (Tob 12:12, Lk. 16:22).
Malaika wema kazi yao ni kutuombea, kutumwa na Mungu kwetu, na wanatulinda kama Malaika walinzi. (Ebr, 13:2). Ambapo kila Mwanadamu ana Malaika wake wa kumlinda na kumuongoza Roho na Mwili, ndie Malaika wake mlinzi, (Zab, 91:11, Mt. 18:10).
Malaika wote sio sawa, wapo Malaika Wakuu, Malaika wanaomtumikia Mungu Mbinguni kwa mfano Makerubi na Maserafi, na pia wapo Malaika walinzi.
Malaika wakuu ni Mikaeli, Gabrieli na Raphaeli (Dn, 10:13, Tobiti 12:15, Lk 1:26).
Mashetani kazi yao ni kuteswa Motoni na hutaka kudhuru Roho na Miili ya wanadamuna kutupoteza milele. (1 Petro, 5:8, Yoh, 8:44).
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Uzinzi na Uasherati ndio mtego wa kizazi hiki
Ibada ya Novena ya Huruma ya Mungu: Kupokea Neema na Baraka
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Kipaimara?
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu utunzaji wa mazingira?
Ibada ya Jumapili ya Huruma ya Mungu: Kupata Upendo Usiokuwa na Kifani
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maombi ya watakatifu?
Huruma ya Mungu: Ulinzi na Uongozi katika Maisha
Ibada ya Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Upendo na Ukarimu