Katika Amri ya Sita na Tisa Mungu ametuamuru nini?
Mungu ametuamuru kutunza usafi wa moyo na kuwa waaminifu katika ndoa.
Usafi wa Moyo ndio nini?
Usafi wa Moyo ni fadhila ya kiutu, zawadi ya Mungu, neema na tunda la Roho Mtakatifu.
Kwa sababu gani yatupasa kuwa na usafi wa moyo?
Yatupasa kuwa na usafi wa moyo kwa sababu:
1. Mungu awapenda hasa wenye usafi wa moyo. (Mt 5:8)
2. Sisi Wakristo ni Hekalu la Roho Mtakatifu. (1Kor 3:16-17)
Tumekatazwa nini ili tulinde usafi wa moyo?
Tumekatazwa haya;
1. Kutazama mwili kwa Tamaa mbaya na kuvaa vibaya
2. Kusema na kuimba, ngoma zisizo na adabu.
3. Kusikiliza machafu, kucheza michezo mixhafu.
4. Kutenda machafu peke yetu au pamoja na wenzetu. (Efe 5:3)
5. Kusoma vitabu na magazeti machafu na kuangalia picha chafu.
Katika Amri ya Tisa ya Mungu tumekatazwa nini?
Tumekatazwa haya;
1. Kutomtamani mke au mume wa mwingine
2. Kutamani mambo ya zinaa
Dhambi za uchafu huleta hasara gani?
Huleta hasara hizi;
1. Kuharibu usafi wa Moyo na Hekalu la Mungu
2. Huleta Magonjwa duniani na hasara ya baadae. mf UKIMWI. (Efe 5:5)
3. Huvunja amani ya familia
4. Kujijengea mazoea ya uchafu
Tulinde usafi wa Moyo namna gani?
1. Kusali mara dhidi ya kishawishi.
2. Kupokea sakramenti hasa Kitubio na Ekaristi mara nyingi
3. Kuepuka uvivu, ulevi na madawa ya kulevya.
4. Kukimbia nafasi dha dhambi.
5. Kutunza haya au soni
6. Kuwa na mazoea ya kufunga na kujinyima.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE
Neema na amani iwe nawe.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Good teachings are here. Keep the spirit
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia